Friday, July 1, 2011

JELA ZA Z;BAR KUSHUGHULIKIWA.RAI WA Z;BAR HAMUWEZI KUWASHUGHULIKIYA MTAA SHUGHULIKIA WAFUNGWA..?


MAGEREZA KUSHUGHULIKIWA
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imeahidi kuyashughulikia malalamiko yaliotolewa na wawakilishi ya kuimarisha magereza, watuhumiwa na wafungwa ambao wanakosa haki zao za msingi kwa muda mrefu.
Waziri wa Nchi Afisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Mwinyihaji Makame Mwadini alisema hayo wakati akifanya majumuisho ya hoja mbali mbali za wajumbe wa baraza la wawakilishi waliotoa wakati wa kuchangia hutuba ya majeti ya makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya rais na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi kwa mwaka wa fedha 2-11-2012.
Waziri huyo alisema serikali itaimarisha magereza yake yaliopo Unguja na Pemba yanaimarishwa na kutengenezwa pamoja na watuhumiwa kuwekwa katika mazingira mazuri ikiwa pamoja na kupatiwa haki zote za msingi za kibinaadamu. Kama ilivopendekezwa na wajumbe hao.
Aliwaambia wajumbe hao kwamba katika kulishughulikia suala hilo timu ya wataalamu kutoka wizara ya afya inakusudia kufanya ziara katika magereza ya Unguja na Pemba kwa ajili ya kuangalia hali za afya za wafungwa na magereza kwa ujumla.
“Mheshimiwa naibu spika tumesikia kauli za wajumbe wa baraza lako tukufu waliokuwa wakichangia bajeti ya wizara hii wamesema hali za magereza ni mbaya na wafungwa bado hali zao haziridhishi timu ya wataalamu kutoka wizara ya afya itatembelea katika magereza yetu yote kuhakikisha tunawaangalia afya zao wafungwa na wale watuhumiwa ili kwenda sambamba na azimio la kuheshimu haki za binaadamu” alisema waziri huyo.
Alisema hivi sasa hakuna tena utaratibu wa kutumia ndoo za kwa kwenda haja ‘mtondoo’ katika magereza kwani ni hatari na zinaweza kusababisha hali mbaya ya kiafya kwa wafungwa kwa ujumla kuata maradhi hasa yale ya mripuko na kuharisha.
“Waheshimiwa tumeondowa mtondoo kuweka katika chumba cha wafungwa safi na chenye mazingira mazuri kiafya hili tumeliondowa kwa kuzingatia suala la afya kwa waliopo ndani” alisema Mwinyihaji ambapo Mtondoo ni ndoo zinazotumiwa kujisaidia kwa haja ndogo na kubwa kwa wafungwa ambapo huweka ndani ya chumba chao na kwa anayetaka kujisaidia hujisaidia humo humo chumbani na utaratibu wao ni atakayejisaidia mwisho ndiye hubeba ndoo hiyo na kwenda kuimwaga nje, utaratibu huo umepigiwa kelele kwa muda mrefu wanaharakati wakielezwa ni kwenda kinyume na misingi ya haki za binaadamu

moja ktk jela za wanawake

moja ktk jela zilizokuweko america oneni hapa

au hivi chumba mtu moja tu na kila kitu chake

No comments:

Post a Comment