Monday, July 25, 2011

NAPE SIJUWI NEPI ASEAMA Z;BAR INANUFAIKA NA GUS NA WAPEMBA WANYE MADUKA KARIAKO NA WAZENJI WENYE ASILI YA MKULANGA WANAUTAKA MUUNGANO.

NAPE SIJUWI NEPII NAE AFUNGUWA MDOMO
WAKE KAMA CHOOO

Katika Meza ya Duwara ya redio Germani mdahalo wa Ismail Jussa, wahadhiri 2 wa chuuo kikuu na Nape Nnauye katibu wa itikadi na uenezi wa habari wa CCM,anasema sikweli kuwa zanzibar hawafaidiki na mineral za Tanganyika.Hii imekuja baada ya Mh Ismail Jusa kuulizwa suala la mafuta kutolewa ktk Muungano, Mh Jussa alisema suala hili limeingizwa kinyemela na nihaki kutolewa na kuwa sio la Muungano kama vile mineral za Tanganyika, Mh Jussa alisema kama mafuta na Gus asilia nisuala la Muungano mbona wenzetu  miaka mingi hivi sasa wanavuna gus bila Zanzibar kufaidika?.Nape anakataa kuwa Zanzibar haifaidiki na gus anasema umeme utumikao Zanzibar kutokea Tenesco una tumia gus na Zanzibar inafaidika na umeme huo na ina madeni ya mamilion inayo daiwa.mimi namuliza nepi ahaa  nape miezi mitatu umeme ulikuwa hakuna zenji watu wakika na kizaa je mutawalipa...?na ni umeme gani tunao faidika nao wakukatwakatwa kila saa mpaka munatunguzia vitu ndio umeme wa kujinatia kuwa munatupa umeme..? Katika suala la Muungano Nepe anasema wasio taka Muungano ni viongozi wasiasa lakini Wzanzibar wenye asili ya Mkulanga na Wapemba wenye Maduka Kariakoo wanautaka Muungano.mimi namjibu na wengine watafuatia kama wapemba wenye maduka wanataka muungano basi nyinyi ndio pakuwapa uraia wa kitanganyika ila z;bar mutake musitake tutauvunja muungano.na ni kwa nini  Wzanzibar tusulubiwe na Jindamizi la Muungano fake eti tu kuna wa Pemba watano wenye Maduka Kariakoo..?tumeshajibu swali hili zamani sana kama wanataka watabaki tanganyika kama hawataki watarudi kwao pemba kuko bado. na ni kwa nini  kusumbuliwa kwa umeme wa mgao wa Tenesco..?wakati kuna umeme wa juwa na waupepo na wa mawimbi ya bahari na nchi za nje zote sasa wanabadilisha kuwa na umeme wa aina hiyo sasa sisi tushindwe kwa nini..?Mimi nasema nilazima tujitahidi kuepukana na vitu vyenye kutuletea tharau na usumbufu wa kusumbuliwa kwa makusudi.kwanza wenzetu wamezowea kutusimanga, ukitaja maswala ya Muungano na kasoro zake utambiwa wale Wapemba wenye maduka vipi kule Tanganyika,au utaskia Zanzibar tunawadai mamillion ya umeme wa Tenesco.Sasa hii ni kufanya vitisho na usumbuliaji kwa kuwa tu ili tufumbe midomo ili tuendelee kukubali Muungano hata kama umepoteza uhalali wake na kuhitaji marekebisho.Hili wenzetu hawalitaki kwa kuwa mfumo huu wa Muungano wa sasa unawanufaisha zaidi wao na kuzidi kuizofisha na kuididimiza na kuikatili na kuifisidisha Zanzibar nchi yetu tuipendayo kwa moyo wetu wote.Hivi sasa Mzanzibar au kiongozi wa Zanzibar akizungumzia kero za Muungano au Muungano wenyewe huonekana Aduwi kwa Watanganyika na nithambi kubwa kwa Wzanzibar kuzungumzia suala hilo je hii ni DIMOKRASI AU UDIKTETEA HUU SASA..?na umeanza miaka ya nyerere mpaka leo ila sasa z;bar imesha amkaa kama hawataki wanataka sisi tuko tayari kwa lolote.
Na pia wakizungumza wao sio thambi? nimara ngapi?ZIMWI MIZENGWE PINDA KASEMA ZANZIBAR SIO NCHI,JE HIYO SIO THAMBI..?au KUSEMA SMZ NA BARAZA LA WAWAKILISHI LIFEE HIO SIO THAMBI AU KOSA KUBWA KTK SEREKALI..?au ndio ule msemo wa waswahili wasemao kuwa WALIE WAO TU,NDEGE WAZURI AKINA ZUWARDE LAKINI AKILIA BUNDI NI UCHURO....?

1 comment:

  1. Kama zanzibar kwa kweli wana nufaika kutoka muungano Mtasikia Wazanzibari wanasema wana nufaika si Watanganyika. Wale madai kuwa baadhi ya Wazanzibari wana ardhi kule Tanganyika na umeme unaotoka Bara kwa bei ya juu si la msingi

    ReplyDelete