Wednesday, February 1, 2012

HAWA NDIO MAZIMWI YANAYO WALA WATU WA ZANZIBAR NA ZANZIBAR YENYEWE

Capture
HAWA NDIO MADALALI NA MAZIMWI WAKU WA KUIFANYA ZANZIBAR IMEZWE NA DOMO LA JINI TANGANYIKA NA HAWAHESHIMU HATA MAMUZI YA BARAZA LA WAWAKILISHI MBELE YAKUJIPENDEKEZA KWA MABWANA ZAO KUZITOWA RASILIMALI ZA WATU WA ZANZIBAR.
Namnukuu huyu Dalali wa Zanzibar aliokuwa tayari anapingana na mamuzi ya Baraza la Wawakilishi,aliokosekana hapa Giningi ni Spika wa Zanzibar Pandu Ameri Kificho huyu ndie hujifanya Stakafiri Mungu mtu katika Baraza.Lakini asisahau tu kuwa upeyao ndio uvumawo yeye ameshakuwa shaib tayari yuko kati ya dunia na Akhera hivi sasa ana vijukuu na asome sana kuhusu uadilifu na kuhusu makemeo ya M/mungu kuhusu zulma na mali za mayatima.pili akaye akijuwa walikuwepo kama yeye hapo zanzibar na kibri kuliko yeye na kutaka kudidimiza zanzibar kwa kujinufaisha wao na familia zao na sasa wote wamo makaburini wanakula joto ya jiwe.
a). Katika majadiliano hayo Mwenyekiti wa kikao hicho Dr Mohd Gharib Bilal aliagiza mamlaka zinazo husika kutowa maelezo ndani ya kipindi cha miezi mine utafutaji na uchimbaji mafuta na gesi asilia.
b.) Kuzibiti uharamia wa utekaji meli katika Bahari kuu, hii mana yake katika ufahamu nikuwa Gharibu Bilali anataka kutumia Ujanja wa kigezo hichi ili kuletewa Cost guard Jesh ili liseme linalinda Uharamia wa Wategaji meli kumbe ni kulinda Wachimbaji mafuta ya Zanzibar wasiwe na Bugza.
Hawa ndio eti Wazalendo wa Zanzibar.MAWEEEEEEE
NASHINDWA kuelewa ni kwa nini wahusika wamekuwa wakiilazimisha Zanzibar iendelee kubakia katika Muungano uliozaa Tanzania wakati wenyewe wameonyesha kuwa hawaridhiki na jinsi Muungano huo ulivyo.
Kwa wahusika hapa namaanisha Serikali ya Muungano pamoja na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Kwa upande mmoja, serikali ya Muungano ndio mlezi mkuu wa Muungano huu na CCM ndicho chama pekee ambacho kimeonyesha kuutaka Muungano kwa sura yake ya sasa ya serikali mbili, ambayo nayo imekuwa ni chanzo cha malalamiko kutoka Zanzibar.
Zanzibar wanazo sababu nyingi tu za kuonyesha kutoridhishwa na Muungano jinsi ulivyo ambazo wao wanaamini kuwa ni za msingi. Wahusika wanaweza wasizione sababu hizo kuwa za msingi lakini hilo nalo halizuii Zanzibar kujiondoa katika Muungano.Kimsingi, Zanzibar in mbia katika Muungano huo na kwa maana hiyo ina haki ya kuamua kuendelea kuwapo ndani ya Muungano au kujitoa.Hata kama sababu za kutaka kujitoa hazitaonekana kuwa za msingi sana kwa upande wa pili, lakini hiyo haiondoi haki yao ya kutaka kujitoa kwenye Muungano pale wanapoamini kuwa Muungano huo hauwanufaishi tena.
Inashangaza kuwa kwa miaka sasa Zanzibar imekuwa ikipaza sauti kuwa hairidhiki na jinsi Muungano unavyoendeshwa. Lakini, wahusika walichokifanya, na ambacho wamekuwa wakiendelea kusisitiza kukifanya, ni kiini macho walichokipa jina la kutatua kero za Muungano.na hii yote nikuwa wamezoe hawa kuwadanganya wananchi kwa ubale wa kanga na mapanga na jazi za mpira lakini wao wanavimba kama vyura wenye mimba kisha wanasema nchi masikini sasa hatutaki tena sisi ndio rai na sisi ndio tutakao endesha nchi mukitaka musitake au nyote tutawafanya kama gaddafi musitulete upumbavu.na sisi sasa tunawao na munaonekana kuwa ni majuha ni kuwa kwa miaka kadhaa sasa wamekuwa wakiendelea na kiini macho hicho cha kutatua kero za Muungano lakini badala ya kwisha, kero zimekuwa zikiongezeka.
Ajabu ni kuwa wanaonekana kuwa hawaoni kuwa kero zinaongezeka badala ya kupungua licha ya juhudi zao za kushughulikia kero za Muungano.Kwangu mimi, ilichokifanya Zanzibar mpaka hivi sasa ni njia za kuonyesha kistaarabu kuwa hairidhishwi na Muungano kwa sababu Wazanzibari wanaamini kuwa hauzingatii masilahi ya Zanzibar. Na walichokifanya wahusika ni kutumia nguvu kuwanyima Wazanzibari haki yao ya kujiamulia mambo yao.Walianza kudai kwa maneno tu, wakaonekana hawana hoja, wakakataliwa. Kwa kuwa walidhamiria kuendelea kudai kile wanachoamini kuwa ni haki yao, wakaanza kufanya baadhi ya vitu kwa vitendo.Wakabadilisha sheria kadhaa ambazo kimsingi zinakiuka kabisa makubaliano ya Muungano kama ilivyopo sasa. Walipoona upande wa pili haujashtuka, wakaamua kubadili na Katiba kabisa. Lakini, inaonekana bado wahusika hawaelewi hawa jamaa wanataka nini.Kitakachotokea sasa, sidhani kama ni kosa la Wazanzibari kwa sababu kama ni onyo walishalitoa na wakadharauliwa.Upo msemo kuwa paka akibanwa kwenye kona, anaweza kugeuka kuwa chui. Hilo ndilo litakalotokea kwa Zanzibar. Kwa sababu imebanwa sana katika azima yake ya kutaka Muungano ambao una masilahi kwake, sasa itageuka kuwa mbogo kweli kweli. Na dalalili zimeanza kuonekana.Zipo chockochoko za chini kwa chini ambazo zinawahusisha watu wa kawaida tu hivi sasa. Wapo watu wenye asili ya Tanganyika huko Zanzibar ambao wameanza kunyanyaswa na watu wa kawaida tu wa Zanzibar.Kwa maelezo yanayotolewa, inaonyesha kuwa hilo ni suala la uhalifu wa kawaida tu ambao hata Tanzania bara upo, ingawa haulekezwi kwa Wazanzibari.
Lakini kwa wanaotaka kukiita kitu kwa jina lake halisi wanaelewa fika kuwa chokochoko hizi zina uhusiano ya kutoridhishwa kwa Zanzibari katika masuala ya Muungano. Wahusika hawataki kulikubali hilo lakini hiyo haibadilishi ukweli wa suala hilo.Kwa kuwa tumeamua kuficha maradhi, tusubiri kifo kituumbue. Naamini kuwa Zanzibar haitachoka wala kuacha kudai haki zake ndani ya Muungano. Na kwa jinsi mambo yalivyo,viongozi wezi,majambazi,walafi,watapia mloo miroho ya mali isiyo tosheka kwa walivyo iba tayari wataendelea kukataa kutekeleza matakwa hayo.Kwa kuwa suala hili limeshafika kwenye ngazi ya wananchi, ambao wameamka baada ya kuona kuna viongozi wao wengi tu ambao wana mawazo kama yao, tusitarajie kuwa litakwisha hivi hivi.Nadhani viongozi walafii wana hofu ya kuvunjika kwa muungano. Lakini wafahamu kuwa kuvunjika huko kwa Muungano kunaweza kuwa ndio suluhisho la kujenga Muungano mwingine utakaokuwa imara kwa sababu uta jengwa chini ya maridhiano ya pande mbili zikikubaliana kuungana.Lakini, ni kweli kuwa  Zanzibar inabanwa sana kiuchumi ndani ya muungano na hivyo kuvunjika kwa Muungano kunaweza kuisaidia ikajitanua. Itaisaidia pia Tanganyika iwapo itakuwa na jirani tajiri.na ikiwa mutaileta zanzibar kuwa huru bila ya kusababisha machafuko kwanza kisha ndio muilete kuwa huru wazanzibar hawatakuwa na imani na nyinyi tena kwa hiyo hata wakiwa matajiri vipi hawata watiza nyinyi tena na Kuendelea kulazimisha Muungano huu kutatuletea maafa hapo baadaye. Imeshajidhihirisha kuwa Wazanzibari hawataacha kudai haki zao mpaka wazipate.Na itafika wakati Watanganyika nao watakapochoka na chokochoko hizo na wao kuamua kuanza kudai haki zao kwa hila na kwa nguvu. Sijui kama viongozi walafii miroho isiyotosheka kuwa walivyo iba tayari kama watakuwa na nguvu za kutosha kukabiliana na Watanganyika na Wazanzibari watakapoamua kudai haki zao kila mmoja kivyake.
Kuna nafasi adhimu ambayo viongozi wetu wanataka kutukosesha bila sababu za msingi. Kwa mtu anayepima upepo, atagundua kuwa watu wengi hawaridhishwi na aina ya Muungano uliopo. Na kwa hakika kabisa, miongoni mwa watu hao ni viongozi wetu wengi tu.Tatizo ni kuwa waliopo madarakani hawataki kuingia kwenye vitabu vya historia kuwa ndio walioshiriki kuua Muungano. Wana hofu kuwa Zanzibar ikiruhusiwa kutoka basi Muungano utakuwa umekufa. Ile fursa kuwa kuondoka kwa Zanzibar ni mwanzo mzuri wa kuunda Muungano imara wala hawajaiona.Wamejawa hofu ya kihistoria iliyopatia upofu wa masuala dhahiri kuwa kwa kulazimisha Muungano, eti tu kwa sababu ulianzishwa na waasisi wa taifa nao sio wa asisi wa taifa maana sio walio zitowa nchi ktk mikono ya wakolo ni wengine kisha wao wakawau viongozi wengine na kujiweka wao kuwa ndio wasisi kisha wakaunganisha ili wasipinduliwe kwa hiyo ilikuwa sio muungano wa nchi mbili bali ni kujihami kwa nchi mbili na hawa viongozi wa sasa majizi malafii wanaungangania na kudhani watakuwa wanadumisha utaifa. Lakini kama wakiamua kufungua macho, watabaini kuwa wanachokifanya kinaua utaifa.Kama nilivyoeleza awali, Zanzibar haiwezi kuendelea kuvumilia kulazimishwa kuwepo ndani ya Muungano. Itafika mahali itageuka mbogo na kulazimisha kile inachokitaka. Itakuwa vigumu sana kuzuia na kudhibiti hali ya mambo wakati huo.na mifano tushaiyona ktk nchi tafauti duniani.Kama tunataka salama, ni heri tukaiacha Zanzibar iondoke kwenye Muungano sasa hivi kwa amani na utulivu, nasi tutabaki salama huku tukiwa na uwezekano wa kuunda muungano mwingine wenye nguvu zaidi.Lakini iwapo tutasubiri mpaka Zanzibar, au hata Tanganyika, ikaamua kujiondoa kwa nguvu, hatutabaki salama na wala hakutakuwa na uaminifu uliobakia wa kuwa msingi wa kuunda muungano mwingine wenye nguvu.

No comments:

Post a Comment