Thursday, May 3, 2012

UAMSHO HAKUNA TENA KURUDI NYUMA MPAKA KIELEWEKE


Jana kupitia vyombo vingi vya habari, waziri kutoka ofisi ya makamo wa pili wa rais alidai kuwa sasa wataanza kuzuia mihadhara inayofanywa na jumuia ya uamsho na jumuia nyengine za kiislamu.
Hivyo basi kutokana na kauli ile wanataka kutumia NENO SHERIA ZA NCHI kuzuia harakati za kuwaelimisha wazanzibar kutokana na ukweli kuwa mihadhara hiyo imekuwa ikivuta hisia za watu wengi na tisho kubwa kwa wanaodai kuulinda muungano mbovu uliopo.Sasa ushauri wangu kwa UAMSHO ni kwamba wasije wakatishwa na vitisho vilivyopitwa na wakati kwa sababu tayari smz na smt wameshatikishwa na wametikisika na wamejaa hofu kutokana na kukubalika kwa UAMSHO.
Mimi kwa upande wangu sina wasiwasi na USHUJAA wa viongozi 4, Sheikh Mselem, Sh Azan na Sh Farid. Sheikh Mussa Hawa ni viongozi ambao wamekuwa na msimamo usioyumba kwa yale wanayoyaamini.
MWISHO: NAOMBA NIWAKUMBUSHE MASHEIKH WETU NILIOWATAJA HAPO JUU, MUJUE KUWA WATU WENGI WAMEUNGA MKONO HARAKATI HIZI ZA KUIKOMBOA ZANZIBAR SIO KWAMBA WALIKUWA WANAPENDA KUJIINGIZA KATIKA VUGUVUGU HILI, BALI NI KUTOKANA NA UADILIFU, UAMINIFU NA UJASIRI MUNAOUONESHA KATIKA MASUALA MBALI MBALI HUSUSAN KWENYE DINI.
WAMEAMUA KUWAUNGA MKONO WAKIJUA KUWA MUWAAMINIFU KWA HIYO MSIJE KUTISHWA NA VITISHO VYA WATU WALIOKWISHA KATA TAMAA NA KUONGOZA KIFALME NA KIDIKTETA.
NA PIA NATAKA KUWATAHADHARISHA HAO WANAOJIITA UVCCM ZANZIBAR, KAMA WANADHANI WALIFANYA UOVU NA DHULMA HUKO TULIKOTOKA NA WATU WAKAACHIA KWA HIVYO WANADHANI, WANAWEZA KUENDELEZA KAMA ZAMANI. WAJUE ZANZIBAR YA LEO SIO ILE YA 1995-2005. SASA HIVI KILA MTU ANAWEZA KULIPA KISASI KADRI ANAVYOFANYIA BILA KUJALI NAFASI YAKO KATIKA SERIKALI.
KWA HIYO UAMSHO MAPAMBANO YAENDELEE HADI KIELEWEKE, INSHAALLAH MAFANIKIO YANAANZA KUONEKANA.

No comments:

Post a Comment