Thursday, June 28, 2012

AHADI ALIYOWEKA YA NYUMBA ZA MAYATIMA KAIFUTA ILA YA KUFANYA MUUNGANO UDUMU BADO ANAISHIKILIA NA ATAULINDA ASEMA


shein alipokuwa akila kiapo cha kuwa raisi muadilifu aliweka ahadi akiwa raisi wa zanzibar atajenga nyumba za mayatima pemba kwa bahati mbaya hajajenga je ilikuwa ni moja ya ujanja ili apewe madaraka...?
SERIKALI ya Zanzibar imo katika matayarisho ya kujenga nyumba ya mayatima ili kuwaondolea usumbufu watoto ambao wamepoteza wazazi wao. Hayo yameelezwa na waziri wa ustawi wa jamii, maendeleo ya vijana, wanawake na watoto, Zainab Omar Mohamamed wakati akijibu suali la Mwakilishi wa nafasi za wanawake (CCM) Viwe Khamis Abdallah.
Mwakilishi huyo alitaka kujua juhudi za serikali za kujenga nyumba za watoto mayatima kisiwani Pemba baada ya rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein kuahidi kufanya hivyo wakati akiomba ridhaa ya kuingia madarakani.
“Mheshimiwa waziri tokea kutolewa kwa ahadi hiyo na rais ya kujengwa nyumba ya watoto mayatima hatua gani zilizochukuliwa hadi hivi sasa?” aliuliza Viwe. Akijibu suali hilo Waziri Zainab alisema kwamba katiak kutekeleza ahadi hiyo wizara yake tayari imeanza kulifanyia kazi jambo hilo.
“Hatua za ujenzi zitaanza wakati wowote uwezo wa fedha utakapopatikana” aliahidi waziri huyo ambaye alionesha kubabaika wakati akijibu suali hilo. Alipotakiwa kutaja kiasi cha fedha zitakazogharimu ujenzi wa nyumba hiyo na  wapi zitapatikana waziri alisema “Kwa kweli katika bajeti hii hakuna fedha zilizotengwa kwa ajili ya jengo la nyumba hiyo lakini napenda kuahidi kuwa zitapatikana tu”.
Aidha waziri huyo alisema wizara yake imefanya mazungumzo na shirika la SOS ambalo limeonesha nia ya kuanzisha nyumba ya kuwalelea watoto kisiwani Pemba. Mradi huo alisema pia itasaidia kuwaondolea usumbufu watoto wanaoishi katika mazingira magumu katika kisiwa cha Pemba.
Nyumba za kulelea watoto iliyopo Forodhani Unguja ilianzishwa na rais wa kwanza wa Zanzibar, marehemu Abeid Amani Karume ikiwa na lengo la kuwasaidia watoto waliofiwa na wazazi wao.
Watoto mahabusu
Watoto mahabusu wameanza kutenganishwa na watu wazima katika jela za Zanzibar ikiwa ni juhudi za serikali za kuheshimu haki za watoto. Kauli hiyo imetolewa na waziri wa nchi ofisi ya rais, Dk Mwinyihaji Makame Mwadini alipokuwa akijibu suali la Mwakilishi wa Jimbo la Muyuni (CCM) Jaku Hashim Ayoub aliyetaka kujua kwa nini watoto wenye umri chini ya miaka 18 wanaendelea kuhifadhiwa katika mahabusu kwa kuchanganywa na watu wazima.
Mwakilishi huyo ambaye kujitokeza kuwa ni muulizaji wa masuala mengi zaidi katika baraza hilo alisema kuwa hali hiyo inaifanya Zanzibar kwenda kinyume na haki za binaadamu na kupuuza haki za watoto ambapo Tanzania imetia saini mkataba wa azimio la kuheshimu haki za binaadamu ambapo Zanzibar ni sehemu ya Tanzania.
Akijibu suali hilo Dk Mwadini alisema serikali imeipa umuhimu mkubwa suala la haki za watoto kama inavyojionesha katiak sheria mbali mbali zilizotungwa. “Hivi sasa utaratibu umewekwa katiak vituo vya mafunzo kuwatenganisha watoto na watu wazima” alisema waziri huyo.
Aidha Dk Mwadini alisema hivi sasa serikali imeanza ujenzi wa chuo kipya cha mafunzo (jela) katika eneo la hanyegwa mchana wilaya ya kati unguja, watoto watakuwa na sehemu yao maalumu na kupatiwa huduma zote wanazostahiki.
Alisema sio kweli kuwa serikali haijachukua hatua na inawapuuza watoto wanaohukumiwa kwa makosa mbali mbali na kupelekwa jela. Wajumbe mbali mbali wa baraza la wawakilishi wamekuwa wakilalamikia watoto kuchanganywa na watu wazima katika jela za Zanzibar hali ambayo inawaweka watoto katika hatari ya kunyanyaswa pamoja na kubakwa.

No comments:

Post a Comment