Tuesday, July 10, 2012

MAALIM SEIF ANAVUNJA MIFUPA HUKU AKIPEPETA


Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetakiwa kuangalia matumizi makubwa ya kodi ya nyumba anayoishi makamo wa kwanza wa rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad inayofikia shilingi milioni 10 kwa mwezi.Akichangia hotuba ya bajeti ya wizara ya nchi ofisi ya makamu wa kwanza wa rais kwa mwaka wa fedha 2012/2013 mwakilishi wa jimbo la Mji Mkongwe Ismail Jussa Ladhu amesema fedha hizo ni nyingi ikilingnishwa na uchumi wa Zanzibar.Aidha Jussa amesema makamo huyo pia anatumia fedha nyingi za serikali yeye na ujumbe wake anapolala hoteli wakati akiwa katika ziara zake mjini Dar es Salaam.       Hivyo mwakilishi huyo ameishauri serikali kuangalia uwezekano wa kujenga nyumba za viongozi mjini humo ili kuepusha matumizi makubwa ya fedha za serikali kwa kulala mahotelini.

No comments:

Post a Comment