Saturday, August 11, 2012

SHAMTE ASAMA WANAOLILIA MUUNGANO HUU AU SEREKALI MBILI NI VIBARAKA WA WATANGANYIKA



NA FREE ZANZIBAR PEOPLE FROM MKOLONI MWEUSI
12th August 2012                                                                                                                             Vigogo wachache wa Chama Cha Mapinduzi Zanzibar wanaolilia Muungano wa mkataba kati ya Tanganyika na Zanzibar ni viongozi haswa wanaojuwa nini Zanzibar na inawauma sana ndio maana wakaipigania kwa nguvu zote kama ilivyo kuwa na Chama cha Afro Shraz Party.      Kada maarufu wa CCM Zanzibar, Baraka Mohamed Shamte, alitoa matamshi hayo katika mahojiano maalum na mwandishi wetu wa siri wa FREE ZANZIBAR PEOPLE FROM MKOLONI MWEUSI nyumbani kwake Mkunazini mjini Unguja jana.
Shamte alisema kundi linalojaribu kuzuia mabadiliko yasije hapa Zanzibar ni la vibaraka na wasaliti wapya waliolipwa ujira na fedha nyingi toka ndani  ya Jamhuri ya Muungano wa (Tanzania.)Tanganyika.
Shamte alisema Waraabu toka Oman walijenga zanzibar na kuifanya nchi maarufu duniani na kuikuza kiuchumi na kuifanya kutambulika ulimwengu mzima Zanzibar inajulika kwa uchumi na biashara na wasomi walio bobea kuanzia miaka 132 tokea mwaka 1832 hadi 1964 hadi pale chama cha ASP kilipofanyiwa shawishiwa na Watanganyika na kupandikizwa sumu kali ya Wazanzibari kuwachukia dungu zao kutoka Oman nakuamuwa kufanya mapinduzi yaliyo sababisha vifo vya watu wasio kuwa na hatia na kunajisiwa wanawake na kulazimishwa kuolewa kwa nguvu wanawake wa kizanzibar na kuolewa na mwatana ya kibara ambayo kwa wakati huo yalikuwa hata kutahiriwa hayajatahiriwa.wabara wakiwandanganya Wazanzibari kuwa huu ni  ukombozi wa haki kupitia njia ya Mapinduzi ya damu Januari 12, 1964.kumbe ilikuwa Wazanzibari wanapinduliwa wao na mwatwana ya bara mpaka leo wazanzibari tunatawaliwa na wabara nusu karne sasa.
Alisema jumla ya wafalme 11 waliishi hapa Zanzibar kwa zamu na Wazanzibari walifurahi sana na kuishi kwa amani na utulivu isipokuwa wale wanaojita wafrika kutoka Tanganyika na nchi nyengine walikuwa wakija hapa kwa kitambulisho maalum na kuchuma karafu msimu ukisha lazima warudi kwao Tanganyika hilo liliwachoma sana Watwana hao wa kiaafrika waliokuwa wakiona kama wanakandamizwa kwa karne nyingi, wakionewa na wakibaguliwa katika nchi hii ya Zanzibar kwa sababu hawakuweza kufanya mambo yao machafu kama wanavyofanya sasa pia waliona kama wamenyimwa haki za msingi bila ya kuruhusiwa kuishi hapa au kaka hapa bila ya kibali maalum.
“Utawala wa kifalme uliotawala Zanzibar uliitisha kura na kufunga mkataba na wanyeji wa Kizanzibari,maana Wazanzibari walishawahi kuvamiwa na Mreno na ikabidi wawaite watu wa Oman kuja kumuondoa kwa nguvu mtawala wa Kireno maana mtawala wa kienyeji enzi hizo aliyeitwa Mwinyimkuu hakuweza kupigana na Mreno.na mara zote Mreno alitaka kuitawala Zanzibar bila ya ridhaa,“ alieleza Shamte.
Alisema wanaojitokeza sasa kutaka Tanganyika na Zanzibar ziwe na Muungano wa mkataba, aliwaita hao ndio Wazanzibari na ndio majabari wanaopigania kuurudisha Zanzibar yetu tunayo itamani kwa miaka mingi sana. ukoloni huo kwa sasa basi lazima Zanzibar ijitawale yenyewe.
“ Julius Kambarage Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume walifunga mkataba uliokuwa na ridhaa kupitia ndani ya nyoyo zao vyama vyao havikujuwa lolote,wala hawakuwauliza wananchi wa Tanganyika wala wa Zanzibar pamoja na  Baraza la Mapinduzi Zanzibar halikujuwa lilijuwa baadaye na Bunge la Tanganyika halkathalika halikujuwa hii ilikuwa ni mipango ya chini kwa chini baina ya nyerere na waliomtuma huku akimhada mzee karuma,” alisema Shamte.
‘Namtaka Hassan Nassor Moyo na wenzake wadai Zanzibar kwa nguvu zote mkataba mkataba hakuna cha mkataba hii ni nchi yetu kwisha habari yake”. Alisema Shamte.
Kada huyo wa CCM alieleza kuwa Waoman walikuja hapa Zanzibar kabla ya mabeberu wa nchi za Ulaya kuigawa Afrika katika mkutano uliofanyika mjini Berlin huko Ujerumani mwaka 1884/1885 kinyume na hiari ya waafrika wenyewe isipokuwa Wazanzibari mabeberu hao wa nchi za Ulaya hawakufanikiwa walipofika Zanzibr.
Shamte ambaye ni mtoto wa Waziri Mkuu wa kwanza wa Zanzibar Mohamed Shamte Hamad, alisema Waoman walipokuja Zanzibar waliunganisha utawala wa kienyeji ulioongozwa na Mwinyimkuu ambaye alikuwa na Makao Makuu yake huko Dunga Mkoa Kusini Unguja baina ya utawala wa Zanzibar na wakiomani na ndio maana makao makuu ya Omani pia yalihamishiwa hapa Zanzibar.
Mwanasiasa huyo machachari alisema chama cha ASP kiliwachukulia waaarabu toka Oman ni dungu zao  walio changanyika na wazanzibar kwa nguvu zote na mashirikiano na kuishi nao kwa pamoja hapa Zanzibar kwa miaka mingi kwa hishima na adabu na utu na kusaidiana kwa kila hali yao yoyote.
Alisema Uhuru kamili wa Wazanzibari ni ule wa mwaka 1963 na siyo wa 1964 kama inavyoaminiwa na vibaraka walioosalia Zanzibar wakienddelea kumuunga mkono Mkoloni mweusi tanganyika kama unavyosema wewe  hahahahaha akacheka kidogo aliyepinduliwa Zanzibar Januari 12,1964 Jamshed bin Abdullah.
Alitoboa siri na kutaja kuwa hata baba yake alijuwa kama kuna plani ya kupinduliwa ila hakujuwa afanye nini maana wakati ule wazanzibari waligawiwa kama hivi sasa tunavyo sabaratishwa hatimaye tukapinduliwa na kufikiri tumepinduwa.
Alisema kitendo hicho peke yake kilionyesha ni jinsi gani hila na hadaa zilivyoandaliwa baaina ya Nyerere na walio mtuma Nyerere kuimaliza Zanzibar kati ya vyama vya ZNP , ZPPP,na ASP  mfalme wa Waingereza alianzisha kwa makusudi maana alijuwa watu hapa watabaguwana na kuchukiana na hiyo ndio ilikuwa njia yao ya kututia ndani ya tumbo la Tanganyika na kuwalaghai Wazanzibari.
Shamte ambaye amewahi kuwa Katibu Mkuu wa kwanza wa ASP Youth League, alisema ili kuthibitisha ZNP na ZPPP na ASP ni vyama vya wananchi wa Zanzibar,isipkuwa vililetwa na Mgereza ili awagawe tuchukiane kama ilivyo sasa ooh wewe CCM ooh wewe CUF ooh wewe UAMSHO matokeo yake vilishindwa kupeperusha bendera yao na kujikuta tunapinduliwa na Watanganyika na wakajikuta wakipeperusha bendera aliyo kuja nayo JOHN OKELLO ya Kitanganyika chini ya utawala wa Kitanganyika.
Alisema chama cha ASP baada ya Mapinduzi, mara moja kilipeperusha bendera ya Kitanganyika iliokuwa na rangi nyeusi, buluu ya maji bahari na kijani ili kuionyesha dunia kuwa chama cha waafrika wa Zanzibar kimeleta ukombozi wa haki na kuunda dola mpya hivyo ndivyo ilivyo thaniwa kumbe ndio ukoloni wa Kitanganyika umetuvaa mpaka leo nusu karne bado tunatawaliwa na wafanyaji kazi maana hawa wakati wa Zanzibar Zanzibar Zanzibar alirudi Zanzibar Zanzibar hawa Watanganyika walikuwa ni wafanyaji kazi wa ndani kama unavyo ona sasa na kuchuma karafu tu hawa leo hii wanatutawala na kutupeleka kipunda punda hapa lazima Zanzibar itoke katika tumbo lao.alisema Shamte.

No comments:

Post a Comment