Wednesday, August 15, 2012

TUMSAIDIYE DUNGU YETU HUYU ANAUMA SANA HAPA NCHINI ZANZIBAR

juma kitwana
Napenda kuleta ombi langu hili la kutaka msaada wenu ili tuweze kumsaidia mwenzetu huyu anayeitwa Juma Kitwana anayeishi Kikwajuni nadhani kwa watu ambao wameishi Kikwajuni watakuwa wanamjua vizuri alikuwa ni mpigaji picha maarufu lakini muda mrefu sasa yupo ndani zaidi ya miaka miwili na alipata ugonjwa wa kiharusi na baadae akawa anafanya mazoezi kidogo kidogo baada ya kupata nafuu lakini baadae akaanguka na kuvunjika mguu na sasa yupo ndani anaumwa na hali yake kama mnavyoiona ni dhaifu sana na bahati mbaya hana mtoto wala mke wa kumsaidia isipokuwa dada zake wawili ambao uwezo wao nao ni mdogo. Kwa hivyo kwa wale ambao watahitaji kumsaidia tunawaomba watoe mchango wao kwa kututumia sisi.

Salma Said,
P. O. Box 1442,
Tel: +255 (024) 223 5219
Mobile: +255 777 477 101
E-mail: muftiiy@yahoo.com

Hassan Mussa Khamis
Mobile: +44 7588550153
email: hassan.mussa@gmail.com
United Kingdom

No comments:

Post a Comment