Friday, October 26, 2012

WATETEZI NA WAKOMBOZI WA NCHI YA ZANZIBAR WANYOLEWA NDEVU ZOTE


SIMBA HILO NA PEACE PIA BADO KAWAPA JAPOKUWA WAMENYOWA DEVU YEYE NDIO KWANZA ANAWAPA PEACE. hawa ndio watetezi wa nchi yetu ya zanzibar wakishikiliwa na makaburu weusi wakitanganyika kwa sababu ya maraisi watatu wanaojita dimokrasi kumbe wote ni MADIKTETA SI SEHIN WALA SI MAALIM WOTE MADIKTETA WAKUBWA.

huyu ni sheikh azzan akitoka nje ya mahakama akisindikizwa na washenzi wa shein na maalim seif washenzi wa kitanganyika ambao wamewanyowa devu zote kama unavyo ona katika pic hii.

haya yote mandela na gaddi walifanyiwa lakini mwish nchi walipata sasa kwa shein na maalim seif kuwafanyia mamiri wetu mambo kama haya haitakuwa jambo jipya maana ndivyo ilivyo siku zote ukisimama kwenye haki basi umo mashakani hongera seif sharrif huu ndio umakamo wako unavyo wafaa wazanzibari hongera kishein ulivyo mfupi na mkimya kumbe unavitimbi kuliko firauni.

washenzi wa shein na maalim seif wakijaribu kuwavunja wakombozi wa nchi yetu ya zanzibar

VIONGOZI wanane wa watetezi wa wazanzibari na wenye kutowa Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) walifikishwa mahakamani huku wakiwa wamenyolewa ndevu wameshitakiwa mahakamani kwa madai ati ya kuhatarisha amani Zanzibar.
Wakitarajiwa kufikishwa mahakamani jana kuendelea na kesi yao ya awali kwenye Mahakama ya Wilaya ya Mwanakwereke,hawakupelekwa tena bali viongozi hao walipelekwa Mahakama Kuu Vuga mjini hapa na kufunguliwa mashitaka mapya mbayo hayana miguu wala kichwa utaelewa zaidi msomaji kuwa hakuna serekali bali kuna UDIKTETA.
Wakati wanafikishwa mahakamani kwa siku ya kwanza Jumatatu iliyopita washtakiwa wote walikuwa na ndevu ZAO videvuni mwao lakini jana walikuwa wamenyolewa devu zote na kuwachwa na sharubu tu huu ni mtindo wa viongozi wanao chukia dini ya kislamu siku zote wanachukia devu na kupenda sharubu. Na jambo hilo kuzua gumzo kubwa miongoni mwa jamii.
Mkurugenzi wa Mashitaka Zanzibar (DPP), Ibrahim Mzee Ibrahim ameeleza kwa mamlaka aliyopewa na sheria ya Usalama wa Taifa kifungu cha 10 anawafungulia mashitaka viongozi na wakombozi wa zanzibar akiwemo Sheikh Farid Hadi Ahmed ambaye kutoweka kwake hivi karibuni kulizua ghasia kubwa Zanzibar.
Wengine waliofikishwa mahakamani ni sheikh Msellem Ali Msellem, Mussa Juma Issa, Azzan Khalid Hamdan, Suleiman Juma Suleiman, Khamis Ali Suleiman, Hassan Bakar Suleiman na Ghalib Ahmada Omar.
Walisomewa mashitaka na Wakili wa Serikali, Raya Msellem liyekuwa akisaidiwa na Rashidi Fadhili na Ramadhan Nasibu mbele ya Mrajisi wa Mahakama Kuu Zanzibar, George Kazi. Hati ya mashitaka inasema kuwa kuanzia Oktoba 17 hadi Oktoba 18 mwaka huu katika barabara kadhaa za Mkoa wa Mjini Magharibi washitakiwa hao wanadaiwa kuwachochochea wafuasi wao kuharibu barabara, kuvunja majumba, kuharibu vyombo vya moto na kuleta hasara ya sh. 500 milioni.upuuzi mtupu
Shitaka lingine wanadaiwa kuwa kati ya Mei 26 hadi Oktoba 19 mwaka huu katika mandamano yaliyofanyika Lumumba, Msumbiji, Fuoni Meli sita na Mbuyni Unguja waliwshawishi watu wengine ambao hawapo kortini kufanya ghasia na kuhatarisha amani.upuuzi mtupuu
Jumatatu iliyopita watu 7 bila kuwemo Ghalib Ahmada Omar walifikishwa katika Mahakama ya Mwanakwerekwe kwa madai ya kufanya uchochezi katika mhadhara walioufanya Agosti 17 mwaka huu.
Waliporudishwa tena Mahakama ya Mwanakwereke kwa kesi yao ya awali haikuweza kusikilizwa kwa vile halimu hakuwepo. Washitakiwa hao wamerudishwa rumande hadi Novemba 7 kesi yao ya Mwanakwerekwe itakposikilizwa na Novemba 8 siku ya kesi ya Mahakama Kuu.
Watuhumiwa hao walifikishwa mahakamani bila ya kuwa na mawakili baada ya mawakili wao, Salim Tawfik na Abdallah Juma kujitoa katika kesi hiyo kwa madai ya kuwa wateja wao wanadhalilishwa.
Wakizungumza na waandishi wa habari nje ya Mahakama Kuu Vuga, mawakili hao walisema kitendo cha serikali kuwashikilia wateja wao na kushindwa kuwaleta mahakamani ni dalili tosha ya kuonesha haki haiwezi kutendeka kwani ni kitendo kinachokwenda kinyume na sheria za kimataifa na sheria za nchi hasa kwa kuzingatia kupewa dhamana ni haki ya kila raia.hapa ndio unajuwa kuwa hakuna serekali kuna majambazi watupu si shein wala si maalim seif wote majambazi wauwaji madhalim na MADIKTETA WAKUBWA.
“Inaonesha hapa haki haiwezi kutendeka dalili zimeanza kuonesha mapema kwa sababu kwanza wamezuiliwa kupewa dhamana wakati pande zote mbili hazikuwa na pingamizi ya kutoa dhamana lakini mahakama ndio inakataa kutoa dhamana, lakini jambo jengine na la kushangaza walitakiwa kuletwa hapa mahakamani lakini sisi tumekuja hapa mahakama ya Mwanakwerekwe tunasubiri wateja wetu hawajaletwa mpaka saa 5:30 asubuhi tunaulizia tunaambiwa twende Vuga na tunafika hapa Vuga hakuna mtu kwa hivyo tunajitoa katika hii kesi kwa leo (jana) ili kufikisha ujumbe wa serikali kwamba hawawatendei haki wateja wetu,” alisema Tawfik

MADARAKA MATAMU YAMEWALEVYA SHEIN NA MAALIM SEIF MPAKA WAO SASA NDIO WANAO WATHALILISHA WAISLAMU WENZAO NA WAZANZIBARI ATI NCHI YA KISLAMU MAWE ATI ASILIMIA MOJA WOTE NI WAISLAMU MAWE ATI VIONGOZI WOTE WA NCHI HII NI WAISLAMU MAWE HATA MAKAFIRI BASI WANGELIWAPA THAMANA LAKINI HAWA WANAO JITA WAISLAMU WAMEWANYIMA THAMANA KABISA HAYA MUBAROUK NA GADDAFI NA BEN ALI NA SALEH WAKO WAPI NA WAO WALIKUWA NA MAJESHI YA KWELI NA KWELI ITAKUWA WEWE KISHENZI NA MAALIM SEIF MUNA NINI ZAIDI YA ULUWA MULIOPEWA NA WATANAGNYIKA KUWAKANDAMIZA WAZANZIBARI KILA LENYE MWANZO LINA MWISHO.

No comments:

Post a Comment