Saturday, June 30, 2012

VIDEO-WALIOFANYA JESHI LA KIKURIA NCHINI ZANZIBAR - TRH-26/5/2012

KIJANA AKIMUONYESHA DR SHEIN KAMA WEWE UNAJESHI LA TANGANYIKA
BASI SISI PIA TUNAWEZAKUWA JESHI NA KARATI NA UCHEPE PIA
PART 1

VIDEO-WALIOFANYA JESHI LA KIKURIA NCHINI ZANZIBAR -TRH- 26/5/2012

KISHEINI CHAJIVUNIA KIJISHE CHAKE CHA TANGANYIKA KINACHO
MLINDA NDIO MAANA AKAWA NA MDOMO WA KUSEMA
HAOGOPI MTU
PART 2

VIDEO-WALIOFANYA JESHI LA KIKURI NCHINI ZANZIBAR -TRH- 26/5/2012

KISHEIN HAKIOGOPI WAZANZIBAR KWASABABU KINA KIJISHI CHAKE CHA KUTOKA TANGANYIKA KINAMLINDA NA KITAPIGA MABOMO WAZANZIBAR WOWOTE AMBAO WANATAKA KUVUNJA MUUNGANO NA MACHOGO WENZAKE
PART 3

VIDEO-YALIYO FANYWA NA JESHI LA KIKURIA NCHINI ZANZIBAR -TRH- 26/5/2012

KISHEIN HAKIOGOPI WAZANZIBAR KWA SABABU ANAKIJISHI CHAKE CHA KITANGANYIKA KINAMLINDA
PART 4

Friday, June 29, 2012

VIDEO-MUHADHARA KUELEKEYA UKOMBOZI WA NCHI YETU ZANZIBAR - BUMBWINI

WATUACHEEE TUPUMUWEEEE
PART 1

VIDEO-MUHADHARA KUELEKEYA UKOMBOZI WA NCHI YETU ZANZIBAR - BUMBWINI

WATUWACHEEE TUPUMUWEEE
PART 2

VIDEO-MUHADHARA KUELEKEYA UKOMBOZI WA NCHI YETU ZANZIBAR - BUMBWINI

WATUWACHEEEE TUPUMUWEEEE
PART 3

VIDEO-JESHI LA SHEIN LIKIWAPINGA MABOMU WAZANZIBARI

MWANZO WA MAJESHI YA SHEIN YAKIWAPINGA MABO WAZANZIBARI
PART 1

VIDEO-JESHI LA SHEIN LIKIWATASE WAZANZIBAR

WAZANZIBARI WAKEPEANA MAWAIDHA MAWILI MA TATU NA SUBIRA
JE SUBIRA HII ITAKWENDA MPAKA LINI IKIWA RAISI ASHASEMA
ATAULINDA MUUNGANO AMBAO RAIA WA NCHI HAWAUTAKI..?
PART 2

VIDEO-JESHI LA SHEIN LIKIWATESA WAZANZIBAR

JESHI LA SHEIN LA KUTOKA MRIMA LIKIWATESA WAZANZIBAR
YANAYOTOKEA SYRIA SASA YAJA ZANZIBAR
SHEIN ASEMA ATAULINDA MUUNGANO
PART 3

VIDEO-JESHI LA SHEIN LAWATESA WAZANZIBARI


JESHI LA SHEIN LA KIKURIA KUTOKA MRIMA LIKIWAPIGA MABOWA WAZANZIBAR
WANAOTAKA NCHI YAO KUWA HURU
PART 4


KISHEIN HAKIOGOPI WAZANZIBAR ANAOGOPA!!!!!

KAMA wapo Watanganyika waliobisha ushiriki kamili wa Jeshi la Polisi la kikuria kutoka mrima katika kufanya uhalifu dhidi ya raia wa Zanzibar , kwa matukio ya 26-27 Mei, basi watafakari matukio mapya ya 17 Juni. Katika matukio yale, askari wa kikuria walipewa silaha na kusukumiza risasi za mipira na mabomu ya kutoa machozi. Wakashambulia ofisi za mawakili, gari za wananchi na nyumba za viongozi wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu (JUMIKI).
Ni matukio ambayo hadi leo, polisi wa kikuria haijayatolea taarifa licha ya kupokea malalamiko mbalimbali ya wananchi.
Wananchi walipoteza mali zao: gari zilizoharibiwa kwa mabomu; na Chama cha Wanasheria wa Zanzibar (ZLS) wanaolalamikia kitendo cha polisi wa kikuria kuteketeza kwa mabomu ofisi za wanachama wao zilizoko Amani.
Bado Polisi hawa wa kikuria hawajaeleza chochote kuhusu vitendo vyao hivyo vilivyoonyesha dhahiri kuwageuka wananchi ambao kwa mujibu wa sheria na utendaji wa jeshi hilo , wanapaswa kuwalinda wao kama wananchi pamoja na mali zao.
Mpaka hapo, picha iliyojengwa kuhusu matukio hayo, ni kwamba Uamsho ndio walihusika kuhujumu mali za wananchi ni kichekesho tena kikubwa. Ni Uamsho pia wanaotajwa kuchoma makanisa, lile la Assemblies of God (TAG) la Kariakoo na jingine la Mwanakwerekwe hawakusema kuhusu msikiti walio upiga mabumo na kuvunja vioo vya madirisha.
Ni aibu kuwa Polisi hawa wa kikuria walichosema katika kadhia yote ile, ni hicho tu. Kwa bahati mbaya wanaoelewa dhamira mbaya za jeshi hili wanajua upi mchele wa kuchukua, na zipi pumba za kupuuza.
Kwa kuwa ni wao waliolikoroga, wataendelea kulinywa wao wenyewe. Wanasubiriwa wakatoe ushahidi wa tuhuma zao dhidi ya Uamsho.
Lakini, kama vile matukio hayo ni madogo na ya kuzua na ambayo wanaamini hayathibitishi vitendo vya uhalifu dhidi ya wazanzibari, Jeshi la Polisi  la kikuria likaingia tena katika utendaji wa ovyo wiki tatu tu baadaye – tarehe 17 Juni.
Polisi wa kikuria wenye silaha walikatiza msafara mrefu wa gari, pikipiki na vespa wa wafuasi wa Uamsho waliokuwa wakienda kijiji cha Donge ambako taasisi hiyo iliandaa mhadhara wa kutoa elimu kwa umma kuhusu Muungano.
Mhadhara huo uliokuwa umeruhusiwa kwa mujibu wa sheria zote, ulisimamishwa eneo la Mahonda, Msikiti wa Ijumaa, mita 100 hivi kutoka kilipo kituo cha Polisi Mahonda.
Mpaka wanafanikiwa kutawanya wafuasi wa Uamsho kwa mabomu ya machozi, risasi za mipira na marungu, watu kadhaa waliachwa wameumia na mali nyingi kuharibiwa.
Polisi wa kikuria, wakijua kuwa Uamsho wana vibali vyote vya kufanya mhadhara msikitini Donge Pwani, walijipanga baina ya msikiti wa Ijumaa na kituo cha polisi, wakataka rai wa zanzibar ndani ya nchi yao na  wana Uamsho warudi mjini je huu sio ukaburu.?
Mhadhara umekusudiwa kufanyika Donge, Polisi wanazuia msafara Mahonda, mwanzo wa jimbo la Donge, ambalo wanasiasa wanaojifanya wafalme, wanataka jimbo hilo liwe bikira kisiasa pamoja na mfumo wa vyama vingi kuishi kwa mwaka wa 20 sasa.
Polisi wa kikuria wanajua Uamsho hawajavunja sheria, wana umma mkubwa wa watu unawafuata nyuma na kila waendako kuhadhiri, kuwazuia katikati ya safari yao ni kuwachochea wakasirike.
Wana Uamsho wakasita. Wakashuka kwenye gari zao na vyombo vyao vingine. Wakabaki hapo kusubiri viongozi wao waje kutoa uamuzi. Kwa kuwa pale waliposimamishwa na polisi, pembeni kuna msikiti mkubwa, wakaamua baadhi yao kuingia msikitini kwa ajili ya sala na dua.
Viongozi walipofika Mahonda, na kupata taarifa ya kilichotokea na kinachoendelea, nao wakaamua kushuka. Wakawafuata viongozi wa polisi ili kujadiliana nao. Ndipo wanapewa taarifa ya amri ya mkuu wa mkoa kuzuia mhadhara Donge ati mkuu wa mkoa ila huu ni ufunguwo kwa watu wa Donge m/mungu anawaonyesha kuwa huyu si kiongozi mwema wa kuwaongoza kwa hiyo changuzi zijazo hata asimame vipi wasimchanguwe.
Lahaula, kufa hakuna breki. Pale pale milio ya risasi za mipira na mabomu ya machozi ikaanza kurindima. Askari  wa kikuria wakaingia msikitini bila ya kuvua viatu – hatua ya kunajisi msikiti. Wakapiga watu na kuwatupia matusi.
Mtu mmoja waliyemkuta chooni akijisaidia, alitukanwa kwa matusi ya nguoni. Akalazimishwa kutoka na kupita katikati ya msikiti bila ya kunawa au kusafisha miguu yake; huku akisindikizwa na askari wa kikuria ambaye naye hakuvua viatu vyake ambavyo wakati huu vilikuwa vimenasa uchafu wa chooni aliko mkamatu huyu mtu.
Polisi wa kikuria wakaingia upande wa wanawake na kuwapiga huku wakiwavua nguo na kuwatusi na kuwadhalilisha. Ni matendo yaliyoonyesha uchokozi wa dhahiri dhidi ya dini ya kislamu bayaa zaidi maraisi watatu nchini humu zanzibar tena wanaume ati wanaume imenyamaza kimya je ni waume au MAJIBWA KOKO HAYA MARAISI MATATU TULIYO NAYO NI MAKOKO YAMEUFYATA MKIA.polisi wa kikuria wanafanya wanavyo taka na Kuthibitisha kuwa polisi wa kikuria walishapanga ubaya, walisasambua mitaa ya Mahonda wanamokaa raia na kupita wakipiga wanaume huku wakiwavua nguo wanawake.
Hawakuchoka. Polisi wa kikuria wengine walitumwa kwenda hadi Donge ambako mhadhara ungefanyika na kupiga watu hata wale ambao walikutwa wakizungumza barazani kwao. Watu wazima nao hawakusalimika. Walipigwa na kutukanwa matusi mabaya mabaya.
Polisi wa kikuria hawakuchoka. Walizunguka miji ya Mkokotoni, Kivunge, Mkwajuni, Gamba na Chaani. Mote humo wakipiga risasi za mipira na mabomu ya machozi. Wakitukana watu wazima wanaume na wanawake.
Sasa mhadhara ulikuwa umepangwa kufanyika Donge, vyereje polisi wa wakikuria washambulie wananchi hata vijiji vingine hivyo...? Ndio kule kupanga ubaya na uhalifu dhidi ya wazanzibar kisha jana raisi anakuja na kibri chake cha kusema hamuogopi mtu hii nikuonyesha wazi kuwa yeye ndie anae watuma.
Leo, idadi ya watu wapatao 40 wanatajwa kuwa wanauguza majeraha ya risasi, mabomu na marungu. Wengi wengine wameumizwa kwa mateke.
Haji Khatib Ali wa Mahonda amechakazwa mguu kwa risasi na mzee Thabit Shaka wa Fukuchani amechakazwa kwa sababu ya bomu.
Askari wa kikuria walimpiga mtu mwingine lakini risasi ikaduru ilipokutana na simu iliyokuwa kwenye mfuko wa suruali na kunusuru kumchakaza paja. Simu hiyo ilipasuka na kusambaratika.
Huu ni uhalifu dhidi ya wazanzibar na maraisi watuta kimya ikulu wanakula kuku na raia wanateswa na jeshi la wakaburu weusi wa kitanganyika. Ni uchokozi na uchochezi dhidi ya wananchi wema wanaoipenda amani, wanaotii viongozi wa serikali yao ya umoja wa kitaifa ila inaonyesha viongozi hawa hawajali wananchi wao maana kama wanawajali wangeliwachukulia hatuwa za kinithamu askari hawa wa kikuria waote waliohusika kufanya haya ila hilo halipo inatuthirihikia kuwa maraisi wote watatu wako pamoja na wanajeshi wa kikuria kututia adabu ya kudai nchi yetu na kuendelea kukandamizwa na wakoloni weusi tanganyika.
Vitendo vya polisi wa kikuria vinasikitisha. Na athari zake ni kupandikiza uhasama kati ya askari hawa wa kikuria na raia wema wa zanzibar wanao dai nchi yao kuwa huru sio kutawaliwa na tanganyika. Kuna baadhi ya  askari wa kikuria hawajarudi makwao tangu hapo kwa kuhofia kushughulikiwa na wananchi kwa kuwa wameonekana wakipiga watu na kuripua kwa mabomu vespa na pikipiki zao.
Pia walipondaponda baiskeli za wananchi wanaoishi Mahonda waliokuwa wakisubiri nao kuondoka na msafara kutoka Mahonda kwenda Donge. Huko ni kuzikufuru neema za Mwenyezi Mungu. Hawi radhi kwa mambo haya.
Tatizo kubwa la Jeshi la Polisi la kikuria sasa ni kujichukulia sheria mkononi na kushambulia raia na kuharibu mali zao. Tatizo jingine ni kule kufanya yote hayo, halafu wakaeneza uongo kwa ulimwengu kuwa wanadhibiti wakorofi.na hii sio binu ngeni kwa polisi hata siria na misri askari wansema hivyo hivyo wanathibiti wakorofi kumbe wao ndio wakorofi na wezi maana wanaiba kila watakachoweza kukichukuwa.
Katika matendo hayo, ni nani hasa mkorofi..? Polisi wa kikuria wameamua kuasi raia.
Sasa watu wa Donge wanauliza: Wao ni nchi gani..? Inatumia sheria zilizo tofauti na sehemu nyingine ya nchi yao au wao wana taifa jingine..?
Wanayauliza maswali haya kwa viongozi wao – mwakilishi Ali Juma Shamhuna, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wale wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na haswa HAYA MARAISI MATATU LAKINI SIO MARAISI KUMBE NI VIBARAKA WA TANGANYIKA NA JANA KISHENI KIMETHAHIRISHA KWA KUJIKAZA SIMUOGOPI NTU MIYEEE NA MAALIM NAYE NJONI MMTOE MAONIIIII NA BALOZI IDDI WAZANZIBARI MUSISEMEWA SEMANI WENYEWE INALILAHI WAINA ILEHI RAJIUNI WATU WANAMARAISI SISI TUNA MAJIBWA KOKO.
Polisi wanalia sasa maana shutuma zote zimewaelekea.

Thursday, June 28, 2012

AHADI ALIYOWEKA YA NYUMBA ZA MAYATIMA KAIFUTA ILA YA KUFANYA MUUNGANO UDUMU BADO ANAISHIKILIA NA ATAULINDA ASEMA


shein alipokuwa akila kiapo cha kuwa raisi muadilifu aliweka ahadi akiwa raisi wa zanzibar atajenga nyumba za mayatima pemba kwa bahati mbaya hajajenga je ilikuwa ni moja ya ujanja ili apewe madaraka...?
SERIKALI ya Zanzibar imo katika matayarisho ya kujenga nyumba ya mayatima ili kuwaondolea usumbufu watoto ambao wamepoteza wazazi wao. Hayo yameelezwa na waziri wa ustawi wa jamii, maendeleo ya vijana, wanawake na watoto, Zainab Omar Mohamamed wakati akijibu suali la Mwakilishi wa nafasi za wanawake (CCM) Viwe Khamis Abdallah.
Mwakilishi huyo alitaka kujua juhudi za serikali za kujenga nyumba za watoto mayatima kisiwani Pemba baada ya rais wa Zanzibar Dk Ali Mohammed Shein kuahidi kufanya hivyo wakati akiomba ridhaa ya kuingia madarakani.
“Mheshimiwa waziri tokea kutolewa kwa ahadi hiyo na rais ya kujengwa nyumba ya watoto mayatima hatua gani zilizochukuliwa hadi hivi sasa?” aliuliza Viwe. Akijibu suali hilo Waziri Zainab alisema kwamba katiak kutekeleza ahadi hiyo wizara yake tayari imeanza kulifanyia kazi jambo hilo.
“Hatua za ujenzi zitaanza wakati wowote uwezo wa fedha utakapopatikana” aliahidi waziri huyo ambaye alionesha kubabaika wakati akijibu suali hilo. Alipotakiwa kutaja kiasi cha fedha zitakazogharimu ujenzi wa nyumba hiyo na  wapi zitapatikana waziri alisema “Kwa kweli katika bajeti hii hakuna fedha zilizotengwa kwa ajili ya jengo la nyumba hiyo lakini napenda kuahidi kuwa zitapatikana tu”.
Aidha waziri huyo alisema wizara yake imefanya mazungumzo na shirika la SOS ambalo limeonesha nia ya kuanzisha nyumba ya kuwalelea watoto kisiwani Pemba. Mradi huo alisema pia itasaidia kuwaondolea usumbufu watoto wanaoishi katika mazingira magumu katika kisiwa cha Pemba.
Nyumba za kulelea watoto iliyopo Forodhani Unguja ilianzishwa na rais wa kwanza wa Zanzibar, marehemu Abeid Amani Karume ikiwa na lengo la kuwasaidia watoto waliofiwa na wazazi wao.
Watoto mahabusu
Watoto mahabusu wameanza kutenganishwa na watu wazima katika jela za Zanzibar ikiwa ni juhudi za serikali za kuheshimu haki za watoto. Kauli hiyo imetolewa na waziri wa nchi ofisi ya rais, Dk Mwinyihaji Makame Mwadini alipokuwa akijibu suali la Mwakilishi wa Jimbo la Muyuni (CCM) Jaku Hashim Ayoub aliyetaka kujua kwa nini watoto wenye umri chini ya miaka 18 wanaendelea kuhifadhiwa katika mahabusu kwa kuchanganywa na watu wazima.
Mwakilishi huyo ambaye kujitokeza kuwa ni muulizaji wa masuala mengi zaidi katika baraza hilo alisema kuwa hali hiyo inaifanya Zanzibar kwenda kinyume na haki za binaadamu na kupuuza haki za watoto ambapo Tanzania imetia saini mkataba wa azimio la kuheshimu haki za binaadamu ambapo Zanzibar ni sehemu ya Tanzania.
Akijibu suali hilo Dk Mwadini alisema serikali imeipa umuhimu mkubwa suala la haki za watoto kama inavyojionesha katiak sheria mbali mbali zilizotungwa. “Hivi sasa utaratibu umewekwa katiak vituo vya mafunzo kuwatenganisha watoto na watu wazima” alisema waziri huyo.
Aidha Dk Mwadini alisema hivi sasa serikali imeanza ujenzi wa chuo kipya cha mafunzo (jela) katika eneo la hanyegwa mchana wilaya ya kati unguja, watoto watakuwa na sehemu yao maalumu na kupatiwa huduma zote wanazostahiki.
Alisema sio kweli kuwa serikali haijachukua hatua na inawapuuza watoto wanaohukumiwa kwa makosa mbali mbali na kupelekwa jela. Wajumbe mbali mbali wa baraza la wawakilishi wamekuwa wakilalamikia watoto kuchanganywa na watu wazima katika jela za Zanzibar hali ambayo inawaweka watoto katika hatari ya kunyanyaswa pamoja na kubakwa.

KISHEIN HAKIOGOPI WAZANZIBARI ANAOGOPA WAKURIA WALIOMUWEKA MADARAKANI!!!!!


WAZANZIBAR MUSIMKASIRIKIA KWA ANACHO SEMA LAZIMA ASEMA HIVI KUWAFURAHISHA WATANGANYIKA SISI UZI ULE ULE TUNATAKA NCHI YETU KAMA WEWE UNATAKA MUUNGANO NENDA BARA NA WEWE PIA USITUCHAFUWE NA KUMBUKA M/MUNGU ANAKUONA NA ATAKULIZA SIKU YA KIYAMA ULIWAOGOZA VIPI WAZANZIBAR UTASEMA NINI NILIRUHUSU UTALI,UNGA (DRUG)MALAYA,POMBE,MISIKITI KUPINGWA MABOMU NA WAUMINI KUPINGWA NA KUVULIWA MASHUNGI WANAWAKE WA KISLAMU HAYO NDIO UTAKAYO MUAMBI MWENYE MUNGU KWA JILI YA KUKA MADARAKANI NA KUWAFURAHISHA MABWANA ZANGU TANGANYIKA WANAO NILINDA HIVYO NDIVYO UTAMUAMBI M/MUNGU SHEIN..?
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Ali Mohamed Shein amesema ataendelea kuutetea Muungano na hakuna atakaemlaghai wala kumchezea katika uongozi wake. Kauli hiyo ameitowa jana katika mkutano wa Jumuiya ya Wastaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliofanyika Bwawani mjini Unguja.
Dk Shein amesema kwamba yeye ndie rais wa Zanzibar na ndie mwenye mamlaka na hatomuogopa mtu wala kusita kuwachukulia hatua kwa wale wote ambao watakwenda kinyume na matakwa ya kikatiba.
Alisema kuwa dhamana ya nchi hii pamoja na ile ya Jamhuri ya Muungano imo mikononi mwao kati yake na Rais Jakaya Kikwete na ndio maana wakawa wanashirikiana na kushauriana kwa yale yote ambayo yana maslahi na nchi.
“katika kuiongoza Zanzibar mimi ndie rais simuogopi mtu yeyote”, alisema kwa kujiamini Dk Shein.
Dk Shein alisema Zanzibar ni nchi ya kidemokrasia inayotoa uhuru wa maoni kwa kila mtu, lakini kwa upande wake pia  yeyé ndio mwenye dhamana kubwa ya  kuendesha nchi kwa mujibu wa katiba iliyopo. “Mimi  ndio rais siogopi mtu katika kuendesha nchi, siko tayari kuirudisha nchi katika misukosuko na kuirejesha Zanzibar kule ilipotoka wakati iko katika hali ya amani hivi sasa,” alisema katika mkutano huo.
Hata hivyo alisema kuwa Muungano upo na utaendelea kuwepo na kwani yeye ndiye rais ambaye anatokana na chama cha mapinduzi na pia ameingia madarakani chini ya ilani ya chama chake hivyo lazima afuate ilani ya chama chake ambapo alisema changamoto zilizomo zinahitaji kujadiliwa ili kuweza kuziondoa na sio kuvunja muungano.
“Hakuna mtu asiyejua kuwa kuna kero za Muungano hivyo ni vizuri tukajitokeza kwa wingi katika kutoa maoni yetu juu ya katiba na sio kukaa pembeni yanazungumzwa mengi kuhusu mimi lakini yote nimeyapokea kwa kuwa ukubwa ni jaa”, alisema Dk Shein bila ya kutaja jina lakini alikuwa akijibu hoja zilizokuwa zimeibuka kuwa hana uwezo wa kuchukua maamuzi magumu katika suala la uongozi.
Aliwaeleza wastaafu hao kwamba Muungano una kero, zinazojadiliwa na ndio maana njia nyingi, ikiwemo ya mawasiliano baina ya Rais wa Zanzibar na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zimeanzishwa ili kuzitafutia ufumbuzi ambapo alisema njia hizo zitaendelea kutatua mambo ya muungano.
Aidha Dk Shein alisema kazi hiyo anaifanya kwa umakini ili kuhakikisha kuwa Muungano upo na unazidi kuwepo na kwamba wasioutaka wasubiri tume ikija  ndio watoe maoni yao na sio kuanza kutoa maoni hivi sasa kabla ya wakati hufika.
“Hakuna asiyejua katika Muungano kuna kero,…wananchi wazijadili kupitia tume ya mabadiliko ya katiba, na kwa nini tunaanza kusema sema… subirini tume mkatoe maoni yenu” alisema.
Katika hatua nyengine Dk Shein alisema kwa sababu hiyo anaagiza kutokufanyika kwa maandamano ya aina yoyote kuhusiana na suala hilo na  kuwataka wazanzibari  kutoshiriki hadi pale wanaotaka kufanya hivyo wanaporuhusiwa kuandamana na jeshi la polisi kwa kufuata taratibu za kisheria.
“Naagiza maandamano  yasifanyike,…wakiruhusiwa kufanya basi msiende kushiriki,” alisisitiza Dk Dk Shein alikuwa akizungumza na zaidi ya watu 500, waliohudhuria katika mkutano huo,  ambao ni wastaafu wa taasisi za Muungano waliopo Zanzibar.
Katika waliohudhuria katika mkutano huo ni taasisi mbali mbali pamoja na Bunge, Ulinzi na Uslama,  Mambo ya Nje, Mamlaka ya hali ya hewa (TMA), Mamlaka ya Kodi na mapato (TRA), Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Idara ya Uhamiaji, Shirika la Posta na Simu, na taasisi za masuala ya elimu na ufundi.
Sambamba na hayo aliwataka vijana kuthami ni jitihada, michango na maelekezo ya wastaafu kwa kutambua kuwa uzoefu wao katika maisha ni sehemu muhimu kwa maendeleo yao.
“Sote hatuna budi kuelewa kuwa iko siku tutakuwa wastaafu hivyo ni muhimu kujitayarisha hasa kwa kujenga tabia ya kujiwekea akiba na matayarisho mengine ya lazima kwa maisha ya wastaafu”, alisema.
Akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti wa jumuiya hiyo , Mohamed  Ali Maalim, alisema miongoni mwa majukumu ya jumuiya hiyo ni kudumisha Muungano kwa sababhu unalinda maslahi ya wastaafu wote nchini.
Katika risala yao wastaafu hao wamesema kwamba wanakabiliwa na changamoto mbali mbali ndani ya Jumuiya yao ikiwemo uwezo mdogo wa uendeshaji na usimamizi wa ofisi ikiwemo ukosefu wa ofisi ya kutosheleza mahitaji.
Katibu mkuu wa Jumuiya hiyo Rashid Ali alitaja changamoto nyengine ni kukosekana kwa wataalamu na waratibu wa kusimamia utekelezaji wa mipango ya Jumuiya, ukosefu wa vitendea kazi, ukkatika kutekeleza malengo yao.
Jumuiya ya wastaafu Zanzibar imeanzishwa mwaka 2009 ina wanachama 537 ambapo 486 kati ya hao ni wastaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania.

NCHI ZA JIRANI ZINA MAKAMO WA RAISI SISI ZANZIBAR TUNA ZIMWI


PICHA HII ILIPINGWA ALIPO FIKA HARAKA PWANI MCHANGANI ALIPOSIKIA VIBANDA VYA WAUZA UNGA(DRUGS)NA MALAYA NA WABAKAJI WA WATOTO VIMEPINGWA MOTO KUWAPA POLE NA KUWAPA PESA WAJENGE TENA WAENDLEZE LANA NDANI YA NCHI YETU YA ZANZIBAR HII NI WIKI YA PILI SASA TOKA WANAWAKE NA WANAUME WALIOPINGWA VIBAYA NA POLISI MAHONDA NA DONGE TENA NDANI YA MSIKITI NA KUVULIWA MASHUNGI YAO NA KUFATHEHESHWA NA KUTHARAULIWA NA KUVUNJIWA HISHMA HAIKUISHIA HAPO BALI WAKACHOMA MAZULIYA YA MSIKITI NA KUPIGA MABOMU NA KUVUNJA VIOO VYA MADIRISHA NA MILANGO ILA HILI ZIMWI KIMYA HATA KWII KWII HALI JASEMA WAZENJI TUAMKE UZI ULE ULE MPAKA TUIPATE NCHI YETU NA MINAFIKI KAMA HII HAAAAAAAAA
SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imesema haina msimamo na wala haiwezi kuwashawishi wananchi wakaseme nini katika tume ya kuratibu na kukusanya maoni ya katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kauli hiyo imetolewa jana Makamo wa pili wa rais, Balozi Seif Ali Iddi alipokuwa akitoa ufafanuzi wa masuala mbali mbali ya katika kikao cha baraza la wawakilishi Njini Zanzibar. “Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar haina maoni wala haina msimamo kwa wananchi wake kuhusu katiba mpya na pia hatuwezi kuwashawishi wananchi wala kuwaandaa utaratibu maalumu wa suala hilo…. maoni ya wananchi yatakuwa ndiyo ya mwisho na yataheshimiwa tunawataka wawakilishi muwaongoze wananchi wakatoe maoni yao katika tume” alisisitiza Balozi Seif.
Aidha aliwatumia lawama wajumbe wa baraza hilo katika suala zima la katiba kutokana na kushindwa kutoa elimu katika majimbo yao na badala yake kuwaachia watu wengine kuwapotosha wananchi. “Serikali haina maoni lakini sisi tuliopo hapa ndio twende kwa watu kwa sababu wajumbe wa baraza hili wamechaguliwa na watu huko majimbo kwani hivyo nyinyi muwawakilishe wananchi katika suala hili muwaelimishe wananchi wenu majimbo lakini msiwapotoshe ….” Alisema.
Na kuongewa kwamba “Tena tunawaomba sana wawakilishi muwe mnawakusanya wananchi majimboni mwenu kuwapa elimu wananchi kwa sababu naamini mpaka sasa hakuna hata mwakilishi hata mmoja aliyewaita wananchi wake jimboni na kuwaeleza suala hili la katiba” alisema.
Alisema hilo ndilo lengo na majukumu ya wajumbe wa baraza la wawakilishi kutoa elimu kwa wapiga kura wao zaidi katika suala la muungano ikiwemo faida zake, matatizo yake na faida ikiwemo na madhara ya kuvunjika muungano.

HASARA YA KUVUNJIKA MUUNGANO NI KUWA WEWE UTAKUWA HULI TENA NYAMA BALOZI NJAA YAKO IWEZE UNAONA BORA NCHI IANGAMIYE LAKINI YAKO YAWE..?
“Huo ndiyo wajibu wa wajumbe wa baraza la wawakilishi katika majimbo ya uchaguzi……kutoa elimu kwa wananchi kuhusu muundo wa Muungano na faida zake na hata hasara ukivunjika lakini msiwasemee nyinyi waacheni wenyewe waseme” alisisitiza balozi Seif.
Makamo wa pili wa rais alisema serikali katika suala la katiba limetoa fursa kubwa kwa kuwapa wananchi uhuru wa kutoa maoni kwa njia za salama na kuonya kwamba serikali haitamvumilia mtu ambaye atakwenda kinyume na sheria za nchi.
Kauli ya Balozi Seif imekuja kufuatia maombi ya baadhi ya wawakilishi walipokuwa wakichangia bajeti ya wizara yake ambapo pamoja na mambo mengine waliitaka serikali kutoa muongozo na msimamo wa pamoja kuhusu katiba mpya ili wananchi wasiweze kubabaika waktai wa kutoa maoni katika tume itakapoanza kukusanya maoni mwanzoni mwa wiki ijayo.
“Sio kazi ya serikali kuwashawishi wananchi kuhusu Muungano na kutoa maelekezo yake mbele ya Tume ya marekebisho ya katiba kwani tunaamini suala hilo serikali inawaachia wenyewe wananchi kutumia fursa ya demokrasia kuamua mfumo wanaoutaka wa serikali” alisema Balozi Seif.
Akizungumzia suala la elimu kwa wananchi Balozi Seif alisema wananchi wa Zanzibar wanao ufahamu mkubwa kuhusu suala zima la katiba na kuzitambuwa kero mbali mbali ziliomo katika Muungano ambazo zimekuwa kikwazo kwa maisha yao hivyo hawahitaji kupewa muongozo na serikali.
Akionesha kukerwa na badhi ya watu wanaotumia kampeni ya kukusanya saini za watu kukataa muungano, alisema anapinga kampeni hiyo na kuwataka wananchi waache tabia hiyo na badala yake wajitayarishe kutoa maoni wakati tume itakapofika kuwahoji wananchi.
“Naomba nitoe wito kwa wale wenye kupita kila nyumba usiku na kukusanya saini za watu wakatae muungano naomba waache tabia hii mara moja na wasubiri tume wende wakatoe maoni yao” alisema Balozi.
Alisema tabia hiyo sio nzuri ya kuwasemea watu ambayo inadumaza demokrasia iliopo na kuwataka wananchi waache kufanya hivyo kwani kila mmoja atapewa fursa ya kusema mwenyewe na na hakuna sababu watu kuzungumza na niaba ya wengine.
Akifafanua mambo mengine alitaja masuala ya migogoro ya ardhi kuwa bado yanaendelea kuisumbua serikali lakini aliahidi kuendelea nayo na kamwe serikali haitasita kuchukua hatua za makusudi katika kukabiliana na matatizo hayo.
Aliwaambia wajumbe wa baraza la wawakilishi kwamba migogoro ya ardhi kwa kiasi kikubwa imechangiwa na viongozi lakini utatuzi wa migogoro hiyo bado inaendelea na sio kweli kama walivyosema baadhi ya wajumbe kwamba nguvu ya soda ambapo alisema utatuzi wake unahitaji busara za hali ya juu kwani matatizo hayo yameanzia ngazi za juu hadi chini.
Alisema migogoro ya ardhi ni moja ya tatizo ambalo limekuwa likiisumbuwa Serikali akiwemo rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Sheni ambaye amelivalia njuga kulipatia ufumbuzi wake kwa kuwataka wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya na watendaji wengine kulishungulikia katika ngazi za chini.
“Dawa ya migogoro ya ardhi ipo wala mimi sijavunjika moyo….lakini Serikali inalifanyia kazi tatizo hilo kuona kwamba ufumbuzi wake unapatikana, kwani tukumbuke tatizo hili linahitaji busara katika utatuzi wake” aliwaahidi wajumbe hao.
Hata hivyo alisema amepata moyo na matumaini makubwa kwamba baadhi ya maeneo yameanza kupata ufumbuzi wa kero hizo zinazohusiana na migogoro ya ardhi katika ukanda wa pwani ambapo baadhi ya wananchi wamepata muamko wa kwenda mahakamani kuhusiana na kesi hizo.
Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa sauti moja jana walipitisha makadirio na mapato na matumizi ya bajeti ya ofisi ya makamo wa pili wa rais kwa mwaka wa fedha 2012-2013.

MBUNGE KHATIBU SAID HAJI AJA JUU KWA KUITETE NCHI YETU YA ZANZIBAR


MBUNGE wa Konde, Khatibu Said Haji (CUF), ametoa mpya bungeni baada ya kudai kuwa Zanzibar imegeuzwa mwanasesere.
Kutokana na hali hiyo, mbunge huyo aliwataka wabunge wote kutoka Zanzibar kutounga mkono Bajeti ya Waziri Mkuu mizengo pinda kama haitatengewa fedha za rada.
Akichangia mjadala wa hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake, mbunge huyo alisema serikali imekuwa ikipoteza fedha nyingi kufanya sherehe za Muungano ambazo hazina matunda wala faida yoyote kwa Wazanzibari.
Alisema mambo mengi ambayo Wazanzibari wanataka kuyafanya huwa yanapigwa chenga na kudharauliwa kama mwanasesere na ndio mambo ya msingi na yamaendeleo kwa zanzibar na wazanzibari wenyewe lakini yanapingwa chenga sana na kupotezewa muda na fedha katika sherehe za muungano.
Alidai kuwa kwa muda mrefu Wazanzibari wamekuwa wakitaka kujiunga na Jumuiya ya Kiislamu (OIC) na kuondoa mafuta katika suala la Muungano lakini mambo hayo hayajafanyika, jambo alilosema kuwa ni kuwacheleweshea maendeleo wazanzibari.
“Hoja za msingi za Zanzibar huwa hazifanyiwi kazi lakini hoja zisizo za msingi zinapewa kipaumbele,” alisema.
“Sisi fedha za mfuko wa jimbo za kila mbunge zinatusaidia nini wala suala la malipo ya umeme. Nitawalipia bili Wazanzibari wote, lakini msikubali kupitisha bajeti ya waziri mkuu kama hawatatenga fedha za rada kwa ajili ya maendeleo ya Zanzibar,” alisema Haji.

Wednesday, June 27, 2012

MAKOMADO WAMELETWA WAJE KUMUUWA SHEIKH FARID NA WENZAKE ILI KUZIMA Z,BAR ISIJITENGE JE NI TANGANYIKA AU SMZ...?



WASIWASI umetanda kuwa huenda kuna watu wanataka kumuuwa Sheikh Farid.
Hiyo ni kutokana na kile kilicho ajiri hivi karibuni ambapo watu waliokuwa katika gari aliyokuwa kapanda SHEIKH FARID Ilifukuuzwa na gari nyengine hatimai gari aliyokuwa ikifukuza gari ya SHEIKH FARID ilianza kupiga risasi, lakini kwa bahati nzuri Sheikh alikuwa hayumo ndani ya gari hiyo.Wakati huo huo,mwanamke mmoja aliyekuwa akishikilia bendera ya Uamsho yenye maandishi ya Laaila hail allah,ameshushiwa kipigo kikalina polisi wa kikuria alipokataa kuachia bendera hiyo.“ amesema mwanamke Huyo polisi mmoja alikuwa akinilazimisha nimpe bendera, nikamwambia mimi hii siitoi hata kama utaniuwa, basi bora nife nayo mkononimwangu hii ina Laila hailaa allah…sikupi akaendelea kunipiga kwa kile kirungucha polisi alichokuwanacho…akanipiga tenanikaanguka chini naakawa naivuta bendera yangu tu ikawa tunanyanganyiana.”Amesema Bi Riziki akiongea na mwandishi wetu wa siri wa FREE-ZANZIBAR PEOPLE FROM MKOLONI MWEUSI juzi.Bi Riziki Omar Chande(42) ni mmoja wa wanawake kadhaa waliojitokeza nakueleza jinsi walivyopigwa na kudhalilishwa na polisi WA KIKURIA.Riziki Omar Chande(42) mkaazi wa Mfenesini anasema kuwa baada yakusikia kuna mhadharaDonge, yeye alitoka mapema na kwenda kupanda gari kuelekea Donge kama wenzake lakini baada yakufika Mahonda jeshi la polisi lilisimamisha msafarana kuwataka watu wote warejee mjini.Hata hivyo anasema kuwa viongozi wa msafara waliwataka wasiondoke mpaka viongozi wakuu watakapofika.Ilikuwa ni katika muda huo huo Sheikh Farid Hadi Ahmed na wenzake walifika katika eneo la Mahonda na kutaka jeshi la polisi kuacha kuhatarisha amani kutokana na kitendo chao cha kuwazuiya watuwaliokuwa wakielekea Donge kuhudhuria mkutano uliokuwa ufanyike katikaMsikiti wa Donge.Hata hivyo badala yakuwasikiliza na kujadiliananao, polisi WA KIKURIA waliwafukuza wananchi wenye haki na nchi yao ya zanzibar kwenda wanako taka kwa mabomu ya machozi na risasi za mipira na kuwapinga na virungo na kusababisha wanawake katha kumia vibaya na hata wengine bado wako hospitali pamoja na wanaume wengine pia wako hospitali.basi wanawake na wanaume wakaa anzakukimbizana na ndipo walipoamuwa kuingia msikiti wa ijumaa wa mahonda pamoja na masheikh walipoingia Msikitini.Taarifa kutoka eneo latukio zinafahamisha kuwa polisi waliwafuata huko huko Msikitini polisi hao wa kikuria walingia na viatu na kuwapinga mabomu wananchi wa zanzibar wasio na hatia na kuwatawanya kwama bomu na kuvunja vioo vya madirisha na kuchoma mazuliya ya msikiti ambapo Sheikh Farid na wenzake waliruka ukuta na kukimbia kwa miguu katika pori kutoka Mahonda kuelekea njia ya Mwangapwani.Huku nyuma,wakidhani Sheikh Farid yupo ndaniya gari alilokuja nalo, watu wasiofahamika walilifukuza gari hilo na kulipiga risasi ambapo lilipinduka nakuharibikia vibaya.“Sijui kama walitaka kutuuwa au vipi, lakini bahati mimi sikuwemo katika ile gari ingawa wanadhani kwamba ile gari ni yangu,lakini niseme mimi ile gari sio yangu ila nilipewa kwa kutumia kwa ajili ya shughuli za kuendeleza hizi harakati zetu”,alisema Sheikh Farid muda mfupi baada yakurudi katika heka heka hizo ambapo walifanya mhadhara wao Mbuyuni baada yakutokufanikiwa kupenya kwenda Donge.Akielezea juu yalio mfika Bi Riziki anasema kuwa kwa vile alikuwa kashikilia bendera,ilikuwa rahisi kwake kufuatwa na polisi.“Mimi nilikuwa nimekamata bendera yangu polisi alipokuja kunichukua akanikamata mkono ananipeleka kituoni alipofika mbele kuna polisi mwenzake akawambia unampeleka kituo kama Bi Harusi, mpige virungu,…yule polisi akajibu kwa nini tumpige wakati amekubali kutii amri halali....? hapa inatuonyesha wazi kuna polisi wa kizanzibari na hawa wa kikuria kutoka mrima Bi Riziki anaendelea kusimulia Mwenzake akasema,haiwezekani hao hawana adabu lazima apigwe, yeye ndio akaanza kunipiga huku akinambia nimpe bendera yangu ya Uamsho mimi nikamwambia nipigee lakini bedera yangu sikupi ndio akaendelea kunipiga na kunipiga”, alisema Bi Riziki.“Wakawa wanatuambia maneno ya ovyo kwamba tutakoma, kwa hivyo yule polisi mmoja akawaanaendelea kunipiga alipokuja polisi mwenzake mwengina huyu sasa pia  akamwambia unampigia nini huyo wakati yeye amekubali na unpeleke kituoni ndipo waliponichukua na kunipigatena vizuri zaidi kipigo cha kweli”.Riziki ambaye aliumiasehemu ya jicho baada yakupigwa kibao na polisi wa kikuria aliye muambia Bi Riziki kama wewe muungano hutaki sisi tunautaka alimpiga kibao na jicho lotekupiga  rangi ya wekundu, anasema kilichomshangaza nikwamba kila kituo cha polisi alipokwenda alikataliwa kupewa barua ya kwenda kupata matibabu.anaendelea kusema Bi Riziki“Tunafanywa kama sio raia wa nchi hii tulipokwenda kituo walikataa kutupa barua wakati wanajua hatuwezikutibiwa kama tumeumia mpaka tupate barua ya polisi,tulipotoka Mahonda tukaja mjini tulikwenda Kituo chaPolisi Mkunazini wakakataa kutupa kibali tukenda Malindi pia wakakata wakatuambia nyinyi nendeni tu huko huko hospitali wambieni madaktari kuwa mmepigwa na polisi …hawakutupa.”Bi Riziki ambaye aliumia mkono na jicho anasemahata walipokwenda hospitali walikataliwa kupewa tiba hadi watakapokwenda na barua ya polisi. Naye Hafsa Mohammed Mahfoudh (19) mkaazi waKinuni, Magogoni anasemakana katika zahma hizo watuwengi walikimbilia Msikitini na ndipo walipoona Polisi wakiingia Msikitini nakuwapiga wanawake nawanaume na kuwatoa nje huku wakitaka wanawake wote wavuliwe mashungi yao.“Walikuwa wakisemamaneno mabaya mabaya huku wakituvuta mashungi yetu wakitwambia tokeni hapa Waislamu, Waislamu,Waislamu nini, wanafiki wakubwa, na kuna askari wa kike alinivuta sana shungi na kunipiga sana kwa virungu pia baathi ya wanawake wengine walio ungea na mwandishi wetu wa siri wa free zanzibar people from mkoloni mweusi huko donge walisema.walivamiwa msikitini na kuanza kuvuliwa shungi zao na huku wakiambiwa maneno ya kifedhuli na polisi hao wa kikuria kutoka mrima wanao wanyanyasa wazanzibar nchini kwao wakiendelea kuhadithia wanasema kunawanawake wengine walikuwa nje ya msikiti pia nao waliburuza mpaka ndani ya msikiti na kuanza kupingwa vibaya sana yaani sasa msikiti ndio umefanywa mahali pa kupigiwa na kuteswa sisi wananchi wa zanzibar hii ni nyumba ya mwenyezi mungu wao na mabuti yao na mabuduki wanatupinga ndani ya nyumba ya mwenyezi mungu...? walihoji wanwake hao.mama moja alisema ilikuwa kama tumavamiwa na jeshi la nchi jirani ambao tunauwaduwi nao,nae mama mwengine akasema katika hali hiyo sisi watu wa donge tumechoshwa na ubaguzi na udikteta unao endelezwa hapa mkoa wetu imekuwa kama sisi sio wazanzibar hatuwezi kujumuika na wazanzibar wenzetu au donge ni nchi nyengine alihoji mama huyo huko akifuta machozi kwa kanga yake.pia waksema wakina mama hao wanataka serekali iwaeleze ni kwanini wananchi wa donge wao hawana uhuru ndani ya nchi yao kuabudu au kujumuika na wenzao..?....pia dada moja kwa jina anaitwa hafsa alisema nikweli wametupiga na marungu na magongo kweli kweli mpaka tuliporudi nyumba ilikuwa kama tuliyopingwa mawe mwili mzima asema kwa yale marungu na magongo tuliyopigia maana hata mwili wangu ulikuwa hauwezi tena na miguu haikanyagi tena wametupinga sana kwenye magoti na mwili nilifikiri sita tembea tena.baada ya wanawake hao kupewa kipingo kikali sana na jeshi hili la polisi la kikuria kutoka mrima waliwachukuwa mpaka kituwo cha polisi nakuwekwa hapo kuanzia saa tisa mpaka saa nne za usiku.ambapo walitakiwa waende nyumbani na kufika kituoni hapo asubuhi mapema siku ya pili.siku yapili walipofika walisomewa mashataka yao kuwa ati wamekusanyika katika mkusinyiko usio wa halali na pia wamevunja sheria ya kuto sikia amri ya jeshi la polisi kwa sisis free-zanzibar people from mkoloni mweusi tunasema kuwa mkusanyiko una halali na wameruhusiwa kukusanyika ila hili jeshi la kikuria kutoka tangaanyika limezoea kuwathalilisha wazanzibari.hata hivyo pia thamani ilikuwa wazi lakini wanawake hao shida kubwa iliwapata baada ya masheha kukata kutowa barua za uthamini kumbuka dungu msomaji hii ndio zanzibar na hawa ni wazanzibar wamekataliwa barua ya polisi kwenda kuona daktari,wamekataliwa na madaktari kutibiwa mpaka wawe na barua ya polisi na madaktari wanajuwa kuwa wamekataliwa hiyo barua kituo cha polisi,na sasa mpaka sheha pia hataki kutowa barua ya uthamini huu ni ushahidi tosha kuwa tunatawaliwa na wakuria na hawa masheha pia sio wazanzibari wengi wao ni hao hao jama wa mrima wameva ngozi ya kondo wakati wao ni fusi puri.nusura ya wakina mama hao na dada zetu hao ni pali wakili wa kujitegemea mzanzibari mwanakindakindaki kureshi wa zanzibar alipoingilia kati na kusema thamani ya mteja mwenyewe kwa hiyo hakuna haja ya kukoseshwa haki zao kwa kuwa hawana barua ya shena na huku kila mtu anajuwa kuwa sheha hao hawataki kutowa barua hii ni haki yao kina mama.hapa pia tunajufunza kuwa hseha hana maana yoyote ila ni jutu tu liwekwa lile bure na kufitinisha watu na kupeleka habari za ufatani kwa serekali ya tanganyika ndio kazi yao sheha wote.tusichoke wazanzibari wala tusitisheke wala tusiongopa bali ndio kwanza tushikamane na kupigania nchi yetu kwa nguvu zote watatowa tu nchi hii makaburu weusi hawa kashindwa kabaru mweupe southa africa ataweza huyu kaburu mweusi mtanganyika.sisi uzi ule ule madamu tunafuta sheria basi nasiku tukichukuwa nchi yetu kila aliyetusaliti akiwa ni mzanzibari au mtanganyika kama bado yuko zanzibar hajakimbia atafikishwa mahakamani kama watu wa na majeshi ya HITLER mpaka leo wanaendele kusakwa na wakipatika tu kokote waliko wanarudishwa ujarumani na kushtakiwa na kupiwa kifungu cha maisha wakifie jela na hawa ndivyo hivyo hivyo itakavyo kuwa hakuna cha mkuu wa mkoa wa sheha wote tutawashataki na watakwenda kinawa miguu wakamalizie maisha yao kwenye ndooo.

Tuesday, June 26, 2012

MAALIM SEIF UMEMPONZA JUMBE KWA NYERERE NAONA SASA UNATAKA KUTUPONZA WAZANZIBAR KUENDELE KUTESWA NA MAKABURU WAUSI TANGANYIKA

JE DUWA ZA MAISARA ZANZA KUMUINGIA PIA MAALIM SEIF...???????????

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad amewahakikishia Wazanzibari kuwa hakuna mwananchi atakayeadhibiwa kwa kutoa maoni yake kuhusu mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, iwapo atatoa maoni hayo kwa kufuata utaratibu uliowekwa.
Amesema Tume iliyoundwa kwa ajili hiyo, itakuwa ikipokea maoni yote yatakayotolewa na wananchi, na kutoa wito kwa wananchi kutogomea utoaji wa maoni, na badala yake wajitokeze kwa wingi kuwasilisha maoni yao kwa kadri wanavyotaka mabadiliko hayo yafanywe.
Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF ametoa wito huo kwa nyakati tofauti alipokuwa akitembelea majimbo ya uchaguzi ya Chumbuni na Kwamtipura katika Wilaya ya Mjini Unguja kuangalia uhai wa Chama hicho, ikiwa ni mfululizo wa ziara zake za kutembelea majimbo mbali mbali Unguja na Pemba.
Amesema njia pekee ya kuondoa kero za Muungano ni kwa wananchi kujitokeza kutoa maoni yao mbele ya Tume ya kukusanya maoni ya mabadiliko ya katiba, na kwamba maoni yao yatazingatiwa, kuheshimiwa na kufanyiwa kazi kwa kadri watakavyoyatoa.
Amefahamisha kuwa wananchi watakuwa huru kutoa maoni yao, na kuwataka kuepuka jazba na kuvumiliana wakati wanapowasilisha maoni hayo, ili kuepusha malumbano yasiyokuwa ya lazima na ambayo hayatoisaidia nchi kwa njia yoyote, bali kuitia doa ambalo linaweza kuchukua muda mrefu kufutika.
Maalim Seif amewatahadharisha wananchi kuepuka vitendo vya vurugu na kuienzi amani iliyopo ambayo ni moja kati ya mafanikio makubwa yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwa serikali yenye mfumo wa umoja wa kitaifa

PRESIDENT ASSAD OF SYRIA - YOU HAVE A NEW FRIEND IN TANZANIA ! JK KIKWETE


President Jakaya Kikwete shows visiting President Mohamed Abdelaziz of Saharawi Arab Democratic Republic, a picture of Tanzania’s founding fathers, Mwalimu Julius Nyerere and Sheikh Abeid Amani Karume, shortly after their meeting at State House in Dar es Salaam yesterday. (Photo: Freddy Maro of State House)
Mr. President Abdelaziz please dont listen to this munafik hypocrite for what ever he is telling you is not true, i am proving to you from this pictures: This is the country that he is showing you in the picture, where he says they are in UNIT with. The lady with the flag (and other people you will see in other pictures) they where going to the Muslimgathering. His police, that is from mainland, is pressing and distroying mosques and beating Muslim women, take their hijaab off, bomb mosque of the neighbour country that he says he is in UNIT with, which is Zanzibar. The lady in the picture is holding the flag of: La Illaha Illala, his police has distroyed this flag in pieces, used the wooden stick of this flag to beat the woman and take her hijaab off.
Here is his police making a move to start to bombard the citizans of Zanzibar, again the country he is claiming to be in UNIT with, because now the citizans of Zanzibar have stand up and they want to brake this unity, not with fighting, not with a war, not even using bad language, they use the same constitution to ask for their right and asking for the freedom of their country, which was registered with the United Nations in 1963.
But he is distroying them by using force......
This is prove to show that he is distroying the people of Zanzibar, just because they are asking for their Republic of Zanzibar, smoke from their teargass, people hiding behind wall, fleeing away from the unneccessary violence against citizens. Citizens that did nothing outside the law, they have right of gathering where they was going to do their gathering, but his police stop them and start to fire teargass, rubber bullets, beating with long sticks, and when citizens looked for shelter inside the mosque, his police entered with shoes, fired teargass, burned the prayingcarpet, smashed window purposely, still went after the women inside the mosque and start beating them taking their hijabs off.
9 of the women are in very bad condition and are currently still in hospital, same goes for 25 men, 1 child got lost which up to now has not been found.
Firebombs are being targetted at crowd and mosque, fire is burning next to someone trying to hide on the compound of the mosque.
Just a little proof the the carpetwholes in the mosque.
Beaten in the face !
How painfull this burns must be !! Result of police brutaly doing to the innocent good citizens of the Republic of Zanzibar, just because they want indepence from mainland Tangnyika where he is president. Let me remind you all little bit: He was the first president to raise his voice that South & North Sudan should seperate, moreover he was guest at the festivities on the Indepence of South Sudan. I dont like to talk about religion here, but let me remind you: South Sudan is christan, and he supported them to be free.
Zanzibar which is united with his country they are 99% Muslim. He is muslim, we have many videos, blogs, radio information about Zanzibar to be a free country. Rather he keeps using his police to oppress the people of the Republic of Zanzibar !!!! So, what kind of muslim is he ? ? ?
This is the vehicle of sheikh Farid, which was targetted by his police for an accessination attempt. Luckely the sheikh was not in the car, after a police chasing that was  special drawn out personal hit. You might see the 2 "live"bullet wholes on the tire. After salting 3 times, none of the occupance of the vehicle was badly injured. So Mr. President Abdelaziz ask your friend jk kikwete why you dont let Zanzibar to be free, after all you call yourself the president of democracy !!!

WAWAKILISHA NCHINI ZANZIBAR WAANZA KUTOKA USINGIZINI NA KUTAKA PIA MUUNGANO FEKI UVUNJWE


SUALA la Muungano limezidi kutawala mijadala katika kikao cha baraza la wawakilishi kinachoendelea huku baadhi ya wajumbe wakitamka wazi kuwa hawataki Muungano. Katika kikao hicho ambacho tayari kimepitisha bajeti kuu ya serikali ya Zanzibar wajumbe wa baraza hilo jana walijadili bajeti ya ofisi ya makamo wa pili wa rais wakitaka serikali isimamie kupata uhuru zaidi wa kiuchumi katika muungano.
Ofisi ya makamo wa pili wa rais ndio inayotambulika kuwa msimamizi mkuu wa shughuli za serikali ndani ya baraza la wawakilishi.
“Mheshimiwa Naibu Spika mimi niseme wazi kwanza kwamba sitaki muungano na katika kitu ambacho nakichukia sana basi ni huu muungano maana kwa miaka 48 ya muungano huu kila siku tunaambiwa kuna kero wala hazitatuliwi basi ni uvunjike tu” alisema Mwakilishi wa Jimbo la Wawi (CUF) Saleh Nassor Juma.
Juma alisema kupigania haki ya Zanzibar haimaanishi chuki katika muungano na kwamba muungano uliyopo ni wa nchi mbili huru ambazo lazima kuwepo na haki sawa kwa pande zote mbili.
Naye Mwakilishi wa Jimbo la Kitope (CCM) Makame Mshimba Mbarouk alisema “Lazima mheshimiwa makamo wa pili wa rais tuamke muungano huu, siwo…tunataka maslahi ya Zanzibar na tunataka haki zetu zote kuanzia mapato ya gesi. Nitazuwia bajeti hii mpaka niambiwe katika accounti ya Zanzibar imepata kiasi gani kwa mapato ynayotokana na gesi maana ni haki yetu” alisema Mbarouk.
Abdallah Juma Abdallah Mwakilishi wa Jimbo la Chonga (CUF) alisema viongozi wa serikali na vyama wamewekwa madarakani na wananchi hivyo sio sahihi kubeza maoni ya wananchi ambayo hawautaki mfumo huu wa muungano na kuahidi kusimama pamoja na wananchi wa jimbo lake iwapo waamua kuukataa.
“Kiongozi yeyote kuanzia rais, wabunge na hata sisi wawakilishi tumewekwa hapa kwa kuchaguliwa na wananchi na tunasimama kuwasilisha maoni ya wananchi sasa ikiwa wananchi watasema hawataki muungano, mheshimiwa naibu spika lazima tusimame nao” alisema Mwakilishi huyo na kuongeza.
“ Mimi kama mwakilishi wa chonga nasema wananchi kama watasema hawataki muungano basi nitasimama nao na nitakuwa bega kwa bega na kwa sababu wamenichagua kwa kuniamini na pia nahitaji tena kurudi katika nafasi hii na nikidharau maoni yao au matakwa nayo hawatanirejesha tena” alisema Abdallah.
Mwakilishi wa nafasi za wanawake Asha Bakari Makame (CCM) kwa upande wake aliwaambia wajumbe wa baraza hilo kutoka CCM na CUF kwamba wanadhamana kubwa ya kuwatetea wazanzibari bila ya kuhofia nafasi zao na kwamba wazanzibari wanawatazama wao kwa kuwaamini.
“Mheshimiwa naibu spika ni CCM na CUF pekee tuliyopo humu ndani wananchi wanatuamini na lazima turejesha imani kwa wananchi wetu ikiwemo suala kuu la kutetea Zanzibar ndani ya muungano…kero gani hizi zisizokwisha?” alihoji Asha ambaye aliwahi kuwa waziri wakati wa SMZ .
Asha Bakari ambaye ni naibu mwenyekiti wa umoja wa CCM Tanzania (UWT) alisema ni umoja na mshikamano miongoni mwa wazanzibari ndio silaha pekee itakayoweza kuwavusha wazanzibari katika kudai maslahi yao ndnai ya muungano.
“Mimi siogopi chochote na kwa umri huu tena naona lolote litakalonifika ni sawa tu lakini nawaambia wenzangu kwamba tuiteteni Zanzibar na tusiwe na woga maana wengine wamezowea kututisha” alisema kwa kutoa tahadhari.
Mwakilishi wa Jimbo la Mji Mkongwe (CUF) Ismail Jussa Ladhu alisema serikali ya Zanzibar inafanya makosa makubwa ya kuridhia kila kitu ambacho kinatolewa na serikali ya muungano.
“Ni muda mrefu wimbo ndio huo huo wa ahadi ya kushughulikia kero za muungano na kero zenyewe hazishi …kwa sababu hata hizo kamati hazipo kisheria za kutatua kero” alisema.
Jussa alitaka viongozi wa serikali kuwaunga mkono wananchi katika madai yao ya msingi kwa kuwaelekeza nini waseme wakati wa kutoa maoni ya katiba mpya ya jamhuri ya muungano wa Tanzania na kwamba bila ya kutoa muongozo wananchi watababaika.
“Mimi nina imani kubwa na serikali yangu ya umoja wa kitaifa na ninaipenda lakini naomba itoe msimamo hapa katika kuwaelekeza wananchi wakadai nini wakati wa tume itakapokuja kukusanya maoni” alisema Jussa na kupigiwa makofi na wajumbe wenzake.
Aidha mwakilishi huyo aliwataka wananchi na viongozi wa siasa kutokuchanganya misimamo ya siasa pamoja na dini katika kutoa maoni kwani inaweza kuharibu na kuwagawa wazanzibari.
Awali akiwasilisha hutuba ya bajeti ya makamo wa pili ya kuomba kuidhinishiwa shilingi billioni 12.3 kwa mwaka wa fedha za 2012/2013 Waziri wa nchi Ofisi hiyo Mohammed Aboud Mohammed alisema juhudi zimekuwa zikiendelea katika kutatua kero za muungano na kwamba wajumbe wa baraza la wawakilishi wawe wavumilivu.

Monday, June 25, 2012

MKUU WA MKOA SASA PIA ANA AMRI YA KUWAMRISHA JESHI LA KIKURIA LA TANGANYIKA KUWAPINGA NA KUWATHALILISHA WAZANZIBAR

mwanamke jasiri
HUYU NI MWANAMKE JASIRI ALIYA SIMAMA KWA JINA MWENYEZI BILA YA KUWAOGOPA JESHI LA KIKURIA LA KITANGANYIKA LILILO WAPINGA VIBAYA NA KUWANAJISI WANAWAKE NDANI YA MSIKITI WA IJUMAA MAHONDA NA KUPIGA MABOMU NA KUCHOMA MASULIYA YA MSIKITI HUU TUNAMPA HONGERA SHEIN NA MAALIM SEIF NA SEREKALI YAO

SASA tunalo tatizo sugu na la msingi Zanzibar – utawala mbaya. Chembechembe za utawala wa aina hii zinapoachwa na kukua, matokeo yake ni kupandikiza chuki kati ya dola na wananchi. Pale utawala na wananchi wanapochukiana, watategana, wataviziana, watatunishiana misuli. Kila upande utataka kujithibitisha ulivyo na nguvu. Ni kawaida kwa dola kuwa na nguvu nyingi. Hizi huchangiwa na ile asili ya dola kuwa ni chombo cha mabavu; lakini pia kwa sababu utawala utataka kuthibitishia wananchi kuwa chombo hicho kweli ni cha mabavu.
Zanzibar sasa inashuhudia utawala kutaka kuthibitisha unazo nguvu kubwa kuliko raia. Lakini, laiti kiongozi mkuu, rais, angefikiri vizuri na kutanabahi, wala asingehitaji kuthibitisha nguvu za dola – zinajulikana.
Hakuna hata chembe ya haja kwa serikali kuonyesha nguvu zake kwa wananchi. Nguvu za serikali zipo tu hata iweje; zinajulikana vema, zinatajwa mpaka kwenye katiba ya nchi.
Katiba ya Zanzibar, 1984, iliyorekebishwa mara ya mwisho 2010 na kuruhusu kura ya maoni, inazitaja nguvu hizi. Inasema kutakuwa na rais, ambaye atachaguliwa na wananchi.
Utaratibu umesema atachaguliwa kila baada ya miaka mitano na atakaa kwa kipindi kingine cha miaka mitano, iwapo atachaguliwa tena, ambapo atalazimika kustaafu.
Katiba hiyohiyo inabainisha majukumu na wajibu wa rais. Basi inaelezwa atakuwa hivi; atakuwa vile; atafanya hili; atafanya lile.
Jinsi alivyo “mtu mkubwa mwenye nguvu kubwa” imeelezwa kuwa rais atakuwa mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, ataapisha watendaji wote aliowateua, na yeye pia ni sehemu ya baraza la wawakilishi, chombo cha kutunga sheria.
Hayo ni mamlaka makubwa, ya kutosha kabisa kwa binadamu wa kawaida. Lakini je, madaraka hayo yanatumika vizuri, rais anayatumia vizuri, kwa manufaa ya wananchi? Hili ndio swali muhimu hapa.
Sasa, ni muhimu sana kwa utawala, Rais Dk. Shein, kujua kuwa kadiri unavyojitutumua na kutaka kuthibitisha nguvu zake kwa raia ndivyo anavyojiruhusu kuchukiwa na wananchi.
Hakuna mwananchi atakayekubali kuuvaa ujinga na kuridhia kuiunga mkono serikali iliyoanza kutunisha misuli – kutumia askari wake wenye silaha – dhidi ya raia haohao.
Tarehe 26-27 mwezi uliopita, mji wa Zanzibar ulikumbwa na fadhaa kutokana na machafuko yaliyozushwa na utendaji usio wa “Polisi Jamii” wa Jeshi la Polisi.
Walimkamata mmoja wa wahadhiri wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu (JUMIKI) Zanzibar, Ustadh Mussa Juma Issa, magharibi akiwa msikitini Kwa Biziredi.
Mwalimu huyu alikamatwa kishenzi-shenzi maana aliyetumwa kumfuata, alikosa busara na hata hekima pamoja na kujua fika wanayemtaka hana silaha yoyote. Uthibitisho ni kilichotokea baada ya wadai haki kubaini mwalimu wao alikamatwa kishenzi-shenzi.
Wakatimkia kituo kikuu cha polisi cha mkoa wa Mjini Magharibi, Muembemadema. Wakamdai mwalimu wao. Polisi wakaendelea kuzika busara na hekima, wakaamua ni bora watu wengi wakusanyike hapo lakini siyo kumuachia kwa dhamana mkamatwaji.
Basi usiku huo, kucha yake na kutwa ya siku ya pili, Jumapili, mitaa ya mji ikahanikiza sauti na mivumo ya risasi za mipira na mabomu ya kutoa machozi dhidi ya raia.
Silaha hizo zikatumika kuharibu afya za raia wazima na pia wagonjwa waliokuwa majumbani. Zikaharibu mali za watu ikiwemo ofisi ya mawakili. Tafrani kubwa ikatokea mitaani.
Hayo ndo matokeo ya matumizi mabaya ya nguvu za dola. Harufu ya kemikali mtindo mmoja, watu, hadi vitoto na vikongwe, kukohoa ovyo. Niliposema Dk. Shein asisikilize fitna za baadhi ya wasaidizi wake, nililenga kutoa nasaha kwamba fitna huzaa maafa. Ndio haya yanayotokea.
Kumbe Polisi na washirika wao hawajaelewa somo. Labda wameelewa lakini wameelekezwa kwa hayo wanayoyafanya. Bado nasema, hakujapatikana sababu ya maana inayojali maslahi ya umma na hata nchi, ya Polisi kupiga raia kipindi hichi. Haipo.
Uamsho wanafanya kazi yao. Wanafuata sheria. Laa kama hawafuati, mbona tukiwauliza huwa wanasema hawajazuiwa kwa namna yoyote ile rasmi na serikali, isipokuwa kukurupushwa na Polisi wenye silaha?
Sasa Jumamosi na Jumapili zinakuwa siku za giza Zanzibar. Siku ambazo akili za Polisi huelekezwa katika kutumia risasi dhidi ya raia. Ile iliyopita ilikuwa Jumamosi na Jumapili; basi Jumapili wiki hii Polisi wakajipanga tena. Kwa bahati mbaya, mkuu wao Zanzibar akawa tayari kwa lolote.
Kweli, akaamuru askari wawapige wananchi waliokuwa wanakwenda kushiriki mhadhara kwenye msikiti wa Donge, kaskazini Unguja. Msafara wa wana-Uamsho ulipofika Mahonda, karibu na kituo cha polisi, ukazuiwa. Kisa? Eti Polisi wamepokea barua ya Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini, ya kuzuia msafara huo kwenda Donge. Yote hayo ni kuzuia Muungano kuguswa!
Ni hoja dhaifu sana tukizingatia dhana ya utawala bora. Kwamba bosi wa mkoa ameamuru polisi wazuie msafara wa wananchi kwenda Donge, yeye amepata wapi mamlaka hayo? Kwani yeye na sheria afatwe nani? Mtendaji yeyote mwenye kufikiri vizuri atafuata sheria si mtu anayeitwa mkuu wa mkoa.
Tatizo ni kwamba hawa wakuu wa mikoa, kama walivyo wa wilaya, hawatii sheria, bali mabavu. Ndio maana haishangazi leo kukuta hata masheha, viongozi wa hadhi ndogo mno katika mtiririko wa uongozi wa serikali, wanahalifu sheria na hawaulizwi kitu.
Penye utawala bora, utawala mzuri, mkuu wa mkoa alitakiwa aite viongozi wa Uamsho. Akae nao ofisini huku akionyesha uchangamfu. Yeye si ni mtumishi wa watu?
Labda aseme anamtumikia rais. Mbona rais mwenyewe anatumikia watu, au Dk. Shein amepa kutumikia Chama Cha Mapinduzi (CCM)? Mamlaka ni ya wananchi siyo chama.
Mkuu wa mkoa angewaeleza Uamsho rai yake. Angewasikiliza nao wanasemaje. Rai yake ingejadiliwa. Wangejadiliana. Mwisho, wangeafikiana au kutofautiana. Amani ingedumu. Mkubwa huyu hakufanya hivyo.
Aliamuru Polisi. Hawa ni watumishi wa kupokea amri tu. Kweli, historia ya Zanzibar inaonyesha polisi hupokea hata amri za Masheha na maskani za CCM..Polisi wangekuwa wanafanya kazi vizuri, wangekuwa wamefuta mapema maandishi ya uchochezi yaliyoandikwa kwenye ubao wa maskani ya CCM Kachorora. Siyaandiki hapa maana yanatapisha.
Polisi wamelazimisha msafara usipite Mahonda. Wenye haki ya kutembea nchi yao na kushiriki mijadala hai siyo hoi, wakahoji sababu ni nini? Ati nini? Mkuu wa Mkoa ameagiza tuwazuie msiende Donge, anasema mkuu wa polisi. Lahaula.
Mbinu za watawala wabaya. Dola inayotumia polisi kuogopesha raia, kukandamiza haki zao na kuwazuia watu kufikiri na kuamua, haina jina tamu isipokuwa “dola kandamizi.”
Haya twendeni. Dola sakama Uamsho, wakandamize kisawasawa, bali waachie wanamaskani watambe. Tutaona mwisho wa safari hii ya ovyo ambayo serikali ya Dk. Shein imeanzisha. Kweli tutaona.

Sunday, June 17, 2012

KAITWA DODOMA KURUDI TU KAMTEUWA HUYU MKURIA.


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohammed Shein amemteua Marina Joel Thomas kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi

WATU WATAKUPENDA NA KUKUPA MADARAKA UKIWATHALILISHA KWA KUWA WEWE ATI UNAJESHI MWISHO WAKO NDIO KAMA HUU SHEIN KIJITI NA MACHO KIJITI NA MACHO NA KIYAMA KINAKUJA UTAULIZWA YOTE WEWE NA SEIF WANANCHI WANATAKA ZANZIBAR YAO NYINYI BADO MUNABABAISHA WATU NA UTANGANYIKA HAYA HATA MWENYEZI MUNGU BASI HAMUMUOGOPA MUNAOGOPA DODOMA KULIKO MWENYEZI MUNGU NYINYI SEIF NA SHEIN.KAYAMA CHAAJA CHAAJA KIYAMA.

JESHI LA KIKURIA LA KITANGANYIKA NCHINI ZANZIBAR LINAENDELE NA UKABURU WAKE KWA KUWAPINGA WAZENJI WALIO KUWA WANAKWENDA KWENYE MHADHARA DONGE BIDI KUHAIRISHWA


Waislamu waliofika katika viwanja vya Malindi baada ya kutawanywa na jeshi la polisi la kikuria huko Mahonda ambapo walikuwa wakienda Donge kwenye muhadhara ambao umebidi uhairishwe baadhi ya watu wameumizwa baada ya kupata kipigo kutoka kwa polisi wa kikuri wanao tawala zanzibar kwa mabavu toka 1964 kutoka nchi jirani tanganyika.wame wapinga wanawake pia vibaya sana  ambao ilibidi wakimbilia msikitini ili wahifadhike na polisi hao wa kikuria waliokuwa wakiwapiga pasi na huruma lakini haikuwa dawa kukimbilia msikitini maana waliwafuata humo humo msikitini na kuwapa kichapo huko huko ndani ya msikiti nakuwapinga risasi na mabomu ya machozi.HONGERA SEREKALI YA SHEIN NA SEIF SHARIFF.

Ipo wapi imani na hadhi ya wazanzibar? katika kipindi cha mwisho wa uongozi wa DR Amani Abeid Karume zanzibar ilisifika sana kwa utulivu na mpaka kuwa mfano kwa mataifa mengine ya afrika. Hii imetokana na kuonekana uchaguzi umeisha kwa salama na amani, vile vile katika hotuba ya DR Shein aliyohutubia baraza la uwakilishi wakati anaingia madarakani alisisitiza amani na utulivu iendelee zanzibar na pia alisisitiza mwezi uliopita kwa kusema “asieitakia amani zanzibar ahame”
Jioni ya leo kwa masikitiko makubwa jeshi la polisi limewazuia waumini ambao walikua wakienda katika mhadhara ambao ulikua ufanyike Donge na kusababisha majeruhi wengi sana. Jeshi la polisi liliekaa mahonda na kuzuia waumini wasipite kitendo ambacho kiliwafanya waumini hao ambao wanadai haki yao wabaki katika msikiti mkubwa wa mahonda huku wakiwasubiri viongozi (maamiri) wao waamue nini kifanyike, cha kushangaza kwamba viongozi walipowasili na kutaka kuonana na jeshi la polisi ilitoka amri kwa kiongozi wa jeshi hilo kwamba wawapige waumini ambao walikuepo hapo.
Kwa kua amri ndio ishatoka jeshi la polisi likaanza kutawanya mabomu kama ilivyo kawaida yao na kusababisha kina mama wengi kupata kichapo ambacho hastahiki kufanyiwa mwanamke,
Jambo ambalo la kusikitisha ni pale ambapo waumini walipoamua kujihami na kuamua kuingia ndani ya msikiti ili wapate usalama kwa kuamini serikali inaheshimu nyumba za ibada lakin kumbe imekua makanisa ndio yanaheshimiwa. Kwa kweli jeshi la polisi limevamia msikiti wa mahonda ambamo waumini wengi walijificha humo nakuanza kupigwa mabomu ambayo yana risasi za mipira na hatimae msikiti kuwa na kuenea damu nyingi z waislamu vile katika msikiti wa Donge nako waislamu wamepigwa ndani ya msikiti na kuumia vibaya.
Jumuiya imejaaribu kuwahudumia baadhi ya majeruhi ambao waliokuwa nao na kuwapeleka katika spitali ya ARRAHMA kwa ajili ya matibabu mpaka sasa idadi ya majeruhi haijajuilikana kwasababu kila muda imekua gari za wagonjwa zinapishana hospitalini hapo. mpaka sasa viongozi wote wa jumuiya wapo katika hali ya usalama na wamesema siku ya jumatano ndio watatoa tamko la jumuiya.

WAKOLONI WEUSI TANGANYIKA NA MIAKA 50 YA UHURU WA ZANZIBAR HAPA NDIO WALIPOTUFIKISHA KIELIMU


Takribani miaka 50 baada ya Uhuru na Mapinduzi, bado hizi ndizo skuli wanazosoma watoto wetu. Nchi inahitaji "KUJIKOMBOWA KTK UKOLONI HUU ULIOINGIZWA KWA KIINIMACHO NA WATANGANYIKA AMBAO SASA WANATUTAWALA KWA MABAVU NA NGUVU ZA JESHI NA POLISI HAWA HAWANA TAFAUTI YOYOTE NA MAKABURU NDIO MAANA TUNAWAITA MAKABURU WEUSI WAMEISHIKA NCHI HAWATAKI KUITOWA.HUKU WAKIELIMISHA WATOTO WAO NA MASKULI MAZURI MAPYA MAPYA WAKIJENGA NA VYUO VIKUU LAKINI HUKU SISI WAKITUTHALILISHA KISKULI NA WAKIJALIWA KUSOMA MPAKA JUU WANAWAFELISHA TUNATAKA JUMHURI YA WATU WA ZANZIBAR IRUDI HATUTAKI KATIBA WALA SEREKALI TATU WALA SEREKALI YA USHIRIKISHO TUNATAKA JAMHURI YA WATU WA ZANZIBAR.

Saturday, June 16, 2012

MHADHARA WA WANAWAKE ULIO FANYIKA LEO NCHINI ZANZIBAR


wanawake wa kiislamu wakisikiliza mada mbali mbali katika ukumbi wa skuli ya haile mjini Unguja nchini zanzibar mwenyezi mungu awalinde na awape pepo siku ya kiyama mpaka kieleweke.

KINIMACHO NA CHANGA LA WATANGANYIKA KUWAMALIZA WAZANZIBARI KWA KATIBA MPYA

Unajua kama utafuatilia sana suala zima la Muungano (ukiachilia ule mkataba halisi wa 1964), mazonge yamekuwa mengi, udanganyifu, ujanja na hadaa zinazofanywa na Tanganyika zinachupa viwango – yaani Tanganyika wameilalia sana Zanzibar – wameidhulumu kwa kila hali.
Mtakumbuka kuwa mwaka 1992/93 ulipoanzishwa mfumo wa vyama vingi TZ, ilipitishwa sheria maarufu Bungeni inaitwa ‘Mabadiliko ya 11 ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa TZ”,(tanganyika) mabadiliko haya – Ibara ya 11, ndio yalimuondeshea Rais wa Zanzibar kuwa Makamo wa Rais TZ (na kuvunja mkataba wa Muungano wa 1964). Dhulma na ujanja huo.
Hii haikuletwa BLW wala BLM wala popote pale Zanzibar – Zanzibar kuweza kuijadili na kuipta ridhaa, na hata Wabunge wa Zanzibar wakati ule pia hawakuipigia kura maana walitoka nje na kususa kikao. Spika wa siku zile, Msekwa alisema kwa dharau kuwa ‘ni kweli wabunge wa Zanzibar hawakuipa ridhaa mabadiliko ya ibara hii ya 11 kwa sababu walikwenda kusali’. Mnaona dharau hiyo?
Hii ya jana na juzi, Mabadiliko ya 8 -2012 ya Katiba eti inaletwa BLW kama ‘taarifa’ – hii kali na inaonyesha kini macho cha hali ya juu kwa Tanganyika v.s Zanzibar. Mimi hii sijawahi kuisikia popote duniani kuwa bill /au sheria inaletwa Bungeni/BLW kama ‘tarifaa’ – dharau ya mwisho!
Kama nilivyosema ‘bad start or wrong approach haiwezi kuleta good results’.
Msimamo wa Tanganyika ni kuwa Zanzibar si chochote si lolote; lakini wao wanaitumilia sana Zanzibar kwa kupata tija halisi hasa kipato na kuijenga nchi yao na kuiwacha nchi yetu ikidorora.
Mfano, ilipovunjika Jumuiya ya Afrika Mashariki 1977, Edwin Mtei alikuwa Ganava wa Benki Kuu ya TZ;(tanganyika) siku zile EAC ilitoa mgao wa pesa kwa Zanzibar tu, ambazo ndizo zilizoanzisha BoT. Msekwa aliandika barua kwa EAC na kudai pesa za ziada na sehemu ya barua yake ilisomeka hivi (roughly) kuwa “….sisi ni nchi mbili tofauti, na mgao mliotupa ni kidogo sana kwa nchi mbili kwa hivyo tunaomba sehemu mgao wa Tanganyika kama nchi…..”. Naam, EAC walitoa kasma nyengine kwa ajili yao. Haya leo ni nchi ‘moja’; yakiwepo maslahi – zinakuwa nchi mbili? Kiini macho hicho.
[naomba mtembelee archive ya Nairobi, Kenya mtaziona na hata katika report ya tume ya Amina Salim Ali ameziweka kama appendix/annex]. Hii report SMZ wameificha maana imefuchua mambo mengi mazito juu ya Muungano hasa kuhusu pesa.
Msekwa yupo hai, na Edwin Mtei yupo hai – waulizwe kama ni kweli au uwongo, record za barua zipo na record za malipo zipo (unless wazichakachue leo na kesho). JK upo?
Sasa, tunapodai haki zetu za msingi – iwe UAMSHO au Jumbe, au Maalim Seif na timu yake (enzi zile, sio leo tena), au Kamandoo Salmin au yeyote yule – inakuwa NOMA. WHY WHY WHY kikwete..?
Tanganyika wajue kuwa tuna madai mengi kwao, na wajue kuwa hizi ni haki zetu za msingi na sio ‘kiini maacho au lele mama au sumsumia’.
BLW limepokea mabadiliko ya katiba kama ‘taarifa’ huo ndio upumbavu wa mwisho kwao na Wazanzibari.
Wallah ingalikuwa tuko serious hawa wote wawakilishi wangalipaswa kujiuzulu na BLW kuvunjwa kama kitu ‘constitutional crisis’ .
Kwa nini basi ile ibara ya 11 iliyomuondoshea rais wa Zanzibar kuwa makamo haikuletwa BLW, kwa nini sheria ya kuanzisha TRA 1998/99 haikuletwa BLW na zinafanya kazi hapa Zanzibar kwa mabavu..?
Hata hivyo, haya yote ni makosa yetu – tumezubaa mno; vipi BLW ikubali upuzi huu, vipi Katibu wa BLW, Mh.Yahya Khamis Hamad — tunayemjua sisi akubali comedy kama hii?
Suluhisho
Kama kweli JK na serikali yake wana dhati ya nchi ya TZ na hasa Zanzibar – basi nakubali kura ya maoni ya watu kulizwa kama WANAUTAKA au HAWAUTAKI au basi bill ile aliyoitia saini irejeshwe AG office DAR ifanyie a small review au mapitio, na iende tena bungeni as an emregency document, bunge waijadili tena – (kidogo tu) na halafu irejeshwe BLW kwa kupata idhini, then aitie saini kama sheria – plus aivunje tume ile fake ya kukusanya maoni aliyoiyunda maana ile sio tume ni majambaza natulishasema mwisho msasani tume ile,au aunde nyengine (kwa sababu hii iliyopo sio halali kabisa, as sheria yenyewe kama ilivyokuwa sio halali).
Wazanzibari wengi wana shaka na uundwaji wa katiba mpya maana haukufuata utaratibu – lakini jana Maalim seif, VP1 amewatoa ‘shaka’ wananchi na kusema kuwa eti ‘tume itafuata kile kitachosemwa na wananchi’wananchi washasema HAWATAKI MUUNGANO wanataka kura ya maoni kusikia husiki basi hata kuona huwoni maalim...?  I doubt Maalim Seif – wewe unawajua vizuri wajomba zako akina Kikwete, Pinda, Msekwa, Mwinyi, Mkapa n.k – hawa kukubali HAKI kwao ni mwisho – ndio wameumbwa hivyo na wameumbika hivyo.
Mimi nitaona ajabu sana kama watachosema Wazanzibari ndicho kitachosikilizwa na kukubalika. I bet! Kwa sbabu watanganyika wameondosha uaminifu kwetu tokea 1964, wao wamechukua nafasi kama ndio wafalme, watawala, mabosi na wakoloni badala ya Mngereza; and not otherwise.

MAALIM SEIF HAPO VIPI..?


MAALIM JIUNGE NA WAZANZIBAR WALIO KUWEKA KATIKA UMAKAMO USIWACHE WAKAITWA KUWA WAO NI BUKO HARAMU,ALQAIDA NA AL SHABABBA HALI YAKUWA WEWE UNAJUWA KUWA WAO SIO HAO BALI NI WAZANZIBAR WANAO TAKA NCHI YAO.
Picha hii iliyopigwa tarehe 25 Julai 2010 inamuonesha Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, akipiga kampeni ya NDIO kwenye kura ya maoni ya uundwaji wa serikali ya umoja wa kitaifa.swali linakuja kuwa yeye kafanya wazanzibari waungane wawe kitu kimoja vipi leo wazanzibari washasimama kuwa kitu kimoja kuikombowa nchi yao yeye anasema watu kwanza wakachakachuwe mswaada wakati wanchi washasema hawana haja ya katiba mpya mpaka wapate kura ya maoni kulizwa kuwa wanautaka au hawautaki.kwanini asisimame tena nakusema wasikilizwe wananchi na kura ya maoni ipingwa kama ilivyo pingwa wakati wa kutaka serekali ya umoja wa kimataifa kwa nini asifanye hivyo..? au ile ilikuwa ni mbinu tu ya yeye kutaka kurudi madarakani..? tukumbuke alikuwa akipinga muungano kambla ya kuwa makamo wa raisi vipi leo autete muungano huwo ambao yeye mwenyewe anajuwa ndio maradhi sugu yanayo wamaliza rai wa zanzibar walio wanyonge wa maisha na hali duni.je maalim kachoka..? je maalim anasiri iliyo nzuri ya kuikomboa zanzibar ila hataki kutuambiya..? au maalim karidhika na fupa la umakamo wa raisi..?kwa nini asipige tena kampeni ya NDIO kwenye kura ya maoni ya kulizwa kama wazanzibar wanautaka au hawautaki hapa alikuwa ni katibu mkuu wa CUF na alifanya hivi leo ni makamu wa raisi kwali ndio hawezi kufanya hivyi au anaogopaaaaaaa.maalim wazanzibar tutaka WATUWACHIYEEE TUPUMUWEEEEEE

MINAFIIKI NA MIJITU ILIYOHADAIKA NA DUNIA YAJAJU KWA KUPONDA UISLAMU NA DINI YA KISLAMU ILI KUHIFADHI THULMA NA UNYANGANYI WALIO ZOEA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
MAONI YA VYAMA VYA UPINZANI VYA TADEA, SAU, NLD NA AFP KUHUSU TUKIO LA VURUGU LILILOTOKEA HIVI KARIBUNI.
Ndugu waandishi wa habari na wananchi,
Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukutana nanyi leo tukiwa katika hali ya uzima na afya. Pili napenda kushukuruni nyinyi kwa dhati kwa kukubali mualiko wetu na kuhudhuria kwa wingi kwenye mkutano wetu huu muhimu kwa wananchi wa Zanzibar hasa wale wenye kuitakia amani, utulivu na maendeleo nchi yetu hii.
Ndugu waandishi na wananchi,
Mtakumbuka kuwa Mei 26, mwaka huu, Zanzibar tulishuhudia tukio lisilo la kawaida la uvunjwaji wa amani lililofanywa na wenzetu ambao tumekuwa nao katika harakati mbali mbali za maendeleo. Wananchi hawa walisababisha maduka kuvunjwa, nyumba za ibada kuchomwa moto, mipira ya gari kuchomwa barabarani na kusababisha uharibifu wa miundo mbinu ambayo imejengwa na wageni waliokuwepo nchini. Watu walishindwa kufanya shughuli zao hasa maeneno ya mjini. Mitandao na vyombo vyote vya habari vilijaa habari mbaya kuhusu Zanzibar. kwa ufupi hali ilikuwa ni ya kutia aibu na mbaya sana kwa upande wetu hasa ukizingatia taswira nzuri iliyojengeka chini ya uongozi wa pamoja wa Serikali yetu. Tunahisi ushirikiano bado unahitajika sana katika kuweka hali ya utulivu sambamba na juhudi kubwa ambazo Serikali imekuwa ikizichukua. Kwa moyo safi kabisa, leo hii tumeamua kuitisha mkutano wetu huu maalum kuzungumzia hali halisi iliyojitokeza ndani ya nchi yetu.
Hatuna lengo la kulaumu upande wowote kutokana nay ale yaliyotokea, lakini ili kuepuka masuala yale yasitokee tena, ni vyema tukaangalia chanzo cha tukio lenyewe na mazingira yake ili baadae tuweze kuchukua hatua zinazofaa. Sote ni mashahidi kwamba sababu ya vurugu ni mihadhara na maandamano yaliyokuwa yakiendeshwa na Jumuiya ya Uamsho. Harakati za muda mrefu za Jumuiya hiyo ndizo hatimaye zilitoa mianya kwa watu wengine kuifikisha pabaya nchi yetu, ambayo mwelekeo wake kiuchumi ilishaanza kuonesha mafanikio makubwa. Jumuiya ya Mihadhara ya Kiislam yenye kuzungumzia Uamsho ni Jumuiya ya Kidini kwa mujibu wa usajili wake.
Mimi binafsi nashangaa kuona kwamba pamoja na taratibu nzuri zilizowekwa za watu kutoa maoni yao kwa salama na amani, Jumuiya hii inahamasisha watu kufanya mambo kinyume na utaratibu uliowekwa. Harakati za Jumuiya hii zilianza kwenye Misikiti, kuingia mitaani na sasa viwanjani. Hii inaonesha dhahiri kwamba kundi hili lina agenda ya siri na lieltwa makusudi kuchafua hali ya siasa, amani na utulivu na nchi yetu, na dalili za vurugu zimeanza kuonekana.
Sisi kama wanasiasa tunafahamu kwamba jina la Jumuiya hii linatumika kama kivuli, lakini harakati hizi zinaendeshwa na viongozi ambao wamo ndani ya Serikali na ndani ya vyama vya siasa. Tunalaani vikali vitendo vya Jumuiya hii kwani havina maslahi ya nchi yetu. Aidha, tunafahamu kwamba Jumuiya hii inapata ufadhili wa kifedha kutoka nje ya nchi.
Ndugu Waandishi,
Ushahidi wa haya ninayoyazungumza hauhitaji taaluma kubwa kuweza kujua chama kipi cha siasa kinahusika. Harakati za Jumuiya hii zinaendeshwa kwenye maeneo na wafuasi wa Chama hicho ninachokizungumza. Lakini hata viongozi wake wanashindwa kuzilaani hadharani harakati za Jumuiya hii, licha ya athari zilizojitokeza za kuharibu vibaya jina na sifa ya visiwa hivi, vinavyoendelea kujijengea umaarufu katika maendeleo. Nchi nyingi zimevutiwa sana na hatua zinazochukuliwa na nchi yetu katika kuleta maendeleo.
Kupitia mkutano huu tunawaomba sana Wananchi wa Zanzibar, Unguja na Pemba na wale wanaoishi nje ya Visiwa hivi kuwa makini sana na kundi hili. Tunawatanabahisha akinamama wasikubali kutumiwa namna hiyo kwani hatua hiyo inaweza kuwaletea maafa. Dalili zinaonesha kuwa viongozi hao wako tayari kusababisha maafa na kuwatupia lawama watu wengine mradi tu waweze kufikia malengo yao. Ninawasihi sana wasicheze ngoma wasiyoijua. Sehemu nyengine duniani, vikundi kama hivi vimesababisha matokeo mabaya sana na kusababisha maafa makubwa. Kwa mfano Alkayda, Bokoharam kule Nigeria, na Al-Shabab kule Somalia. Hali za nchi zenye makundi haya zinasababisha kuondoka kwa hali ya usalama na amani.
Ndugu Waandishi wa Habari na Wananchi,
Tumepata taarifa kuwa kundi jengine la wananchi wa Zanzibar linalopendelea Muungano tayari linaanzisha harakati dhidi ya wale wanaoupinga Muungano, wakidai kuwa udongo uliochanganywa katika kuunganisha nchi mbili hizi ulitoka Unguja na Tanganyika na sio Pemba. Kwa msingi huo basi wananchi wa Pemba hawahusiki na Muungano, kundi hilo linadai kuwa wasiotaka Muungano ni Wazanzibari kutoka kisiwa cha Pemba. Kutokana na sababu hizo, kundi hilo linawaomba wasioutaka Muungano waondoke Unguja kwa hiyari yao warudi kwao walikotoka.
Ndugu Waandishi wa Habari,
Hizi ni athari za ubaguzi na kwa kweli ni hatari kwa hatma ya nchi yetu. Tunapaswa tukumbuke kuwa Zanzibar kwa muda mrefu tulikuwa tumefarikiana kwa sababu za kisiasa. Mungu ametujaalia miaka miwili iliyopita tumekaa pamoja na tumeondosha tofauti zetu na matunda yake yameonekana kwa kipindi kifupi sana katika kuinua pato letu la Taifa sote tumeshuhudia mafanikio makubwa yaliyopatikana katika sekta ya Kilimo na hasa Karafuu na utalii nchini.
Taarifa za uchumi zinaonesha kuwa tumepata mafanikio makubwa ya kukuza uchumi wetu ndani ya kipindi kifupi. Kwa mujibu wa bajeti ya Serikali ya mwaka wa fedha 2012/2013, pato la mtu mmoja limeongezeka kutoka wastani wa Tsh. 782,000 mwaka 2010 na kufikia Tsh. 960,000 mwaka huu.
Haya ni mafanikio makubwa ambayo hayakupatikana katika nchi nyengine duniani. Kwa wenzetu wa Chama Tawala – CCM tayari wameshavuka lengo lao la miaka mitano katika muda wa miaka miwili tu. Wao walilenga pato la mwananchi lifikie wastani wa Tsh. 884,000 ifikapo 2015.
Ndugu Wanahabari,
Hapa ndipo inapokuja hofu kwamba kuna mkono wa siasa kuvuruga mafanikio haya hasa kwa vile hayo ni matunda yanayotokana na hali ya amani, utulivu na mshikamano wa Wazanzibari, ambapo wananchi waliweza kuendelea na shughuli zao za uzalishaji na biashara bila ya sumbufu, wageni waliendelea kufurika nchini na wawekezaji wameedelea kuwekeza.
Ndugu Waandishi,
Mafanikio ya kukua kwa uchumi wetu yanaendelea kutupa funzo juu ya umuhimu wa kuilinda amani, utulivu na mshikamano wetu ambao umetujengea sifa kubwa. Hivyo napenda kuitumia fursa hii kwa niaba ya vyama vya upinzani kusisitiza mambo yafuatayo:-
1. Tunaiomba Serikali kuangalia usajili wake Jumuiya ya Mihadhara ya Kiislam kutokana na kwenda kinyume na masharti ya usajili wao na kwamba mwelekeo wake ni kuirejesha Zanzibar kwenye mafarakano, vurugu, siasa za chuki na uhasama miongoni mwa Wananchi.
2. Serikali ichukuwe juhudi maalum kuhakikisha kuwa vurugu zilizotokea hazitokei tena, na vyombo vya sheria viwachukulie hatua kali za kisheria wale wote watakaohusika katika kuanzisha na kuendeleza harakati za uamsho za kupinga Muungano.
3. Tuweke mbele maslahi ya nchi yetu kwa maslahi yetu na vizazi vijavyo. Kwa kufanikisha hili, tujitahidi kadri tuwezavyo kuepuka vitendo vyote ambavyo hatimaye vitavuruga mshikamano wetu, amani na utulivu uliopo.
4. Tunawasihi Masheikh na Maulamaa wote wasitumie dini kama ngao ya kuwapotosha wananchi na kusababisha vurugu ndani ya nchi.
5. Tunawaomba Wananchi walioanza harakati za kutaka kuigawa nchi misingi ya uzawa, kuachana na kasumba hizo kwani hazina hatma njema miongoni mwa Wazanzibari.
6. Tunawaomba viongozi wote wa kisiasa kulaani vikali harakati za Uamsho na vitendo vyote vyengine kuashiria uvunjifu wa amani kama ambavyo amekuwa akifanya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamu wa Pili wa Rais.
7. Tunaungana na viongozi wetu wa vyama siasa na Serikali waliojitokeza hadharani kulaani matukio yenye mwelekeo wa uvunjifu wa amani na tunatoa wito kwa wale ambao bado hawajafanya hivyo wafanye kwa haraka na kwa nguvu zote kwani hatua hiyo itaonesha nia yao ya dhati katika kuleta maendeleo ya nchi yetu.
8. Tunapongeza kwa dhati juhudi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa chini ya Uongozi wa Dkt. Ali Mohammed Shein kwa mafanikio makubwa ya kiuchumi, kijamii na kimaendeleo katika kipindi kifupi tokea Serikali hiyo iingie madarakani.
DAIMA TADEA UMOJA NA AMANI
Tunawashukuru sana kwa kutusikiliza

BARUA YA WAZI KWA UMMA WA WAZANZIBARI WALIO NDANI YA NCHI NA WALIO NJE YA NCHI NA WALIMWENGU KWA UJUMLA.

HII NI BARUA YA JUMUIA NA TAASISI ZA KIISLAMU ZANZIBAR. Na Masoud Ali
Kwa ndugu waislamu na wote wapenda haki na wanaoipendelea maslahi mema zanzibar.
Umoja  wa Jumuiya na taasisi za kiislamu Zanzibar umeamua kuandika barua hii ya wazi kwa ummma wa Wazanzibar, viongozi na wananchi kutokana na tuhuma kadhaa zilizoelekezwa kwa jumuiya ya Uamsho.
Awali tunapenda ifahamike kuwa harakati za kuikomboa Zanzibar ili ipate mamlaka yake kamili na kuirejeshea heshima yake ni harakati zinazosimamiwa na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu si jumuiya ya Uamsho peke yake kama wanavyojaribu kwa makusudi vyombo vya habari kupotosha ukweli ili kudhoofisha harakati hizo za ukombozi kuipelekea Zanzibar kupata mamlaka kamili (sovereign state).
Kumejitokeza maadui wengi wa harakati hizi kwa kuituhumu jumuiya hiyo ina uhusiano na makundi yenye msimamo mkali wa kiislamu na wengineo wamekua wakisema wazi kuwa Uamsho ina uhusiano na makundi ya Al-Qaeda, Alshabab, Boko haramu na mengineyo. Uvumi mwengine ni kua jumuiya ya Uamsho inashirikiana na Marekani katika kuendesha harakati zake, vile vile ina uhusiano na chama cha Hizbu Tahrir na Chama Cha Wananchi – CUF.
Tuhuma hizo zimetolewa na viongozi wa makanisa sambamba na viongozi wa CCM kama NAPE pamoja Mh. ALI HASSAN MWINYI na wenziwe pamoja na watu wanaoheshimika na wenye dhamana kubwa katika jamii na kwa hamasa kubwa sana, hayo yametamkwa hadharani bila ya kuwa na ushahidi wowote. Tuhuma hizo zimetolewa ili kuwapoteza malengo Wazanzibar na kuvuruga umoja wao katika kudai haki zao za msingi ambazo ni kudai utaifa wa nchi yao. Njama za kuvuruga umoja wa Zazanzibar hazikumalizia katika tuhma tu bali hivi sasa zinaandaliwa nama za kughushi  Account katika mabenki ambazo zitaihusisha jumuiya ya Uamsho kuwa inapokea misaada kutoka makundi ya Al-qaeda, Al-shabab na mengineyo na njama nyengine ambazo hazijatajwa kwenye maelezo haya. Zaidi kuliko hayo viongozi wa kanisa wameanza harakati za kuziburuza serikali zote mbili na kutumia vyombo vya dola kwa lengo la kuvunja katiba na amani ya nchi kwa kuzitaka serikali kuingilia uhuru wa kuabudu na uhuru wa maoni kwa kuwanyima waislamu  na kuwapiga marufuku haki yao ya kuabudu na uhuru wa maoni kupitia mihadhara, dua, itikafu, nk. Ifahamike kwamba katiba zote mbili zinalinda haki hiyo ibara ya 19. ya katiba ya Jamhuri ya Muungano inasema (1,2) kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo ,imani na uchaguzi katika mambo ya dini…..kazi ya kutangaza dini kufanya ibada na kueneza dini ni huru na jambo la hiari….shughuli na uendeshaji wa jumuiya za kidini zitaka nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.(rejea ibara ya 18,19,20 ya katiba ya zanzibar).
Hivyo umoja wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu inapenda kuwataarifu wananchi wa Zanzibar, wanaoipendelea mema Zanzibar na wapenda haki kote duniani kuwa Jumuiya ya Uamsho haina uhusiano wowote na makundi yaliyotajwa hapo juu kwani hakuna haja wala hoja ya kutaka misaada yeyote kutoka kwao. Pia inasisitiza kuwa Junuiya ya Uamsho ni vuguvugu la umma la Wazanzibar ambao hawajajiambatanisha na makundi yoyote yenye kufanya mapambano na tawala zao kwa njia ya silaha, wala haijajiambatanisha na nchi au taasisi yeyote ya nje ya nchi na ndani kwani hakuna haja wala hoja ya kufanya hivyo.
Jumuiya ya Uamsho inafanya kazi hiyo kwa kushirikiana kikamilifu na Jumuiya na Taasisi za Kiislamu tofauti nchini Zanzibar kwa kutetea maslahi ya kupatikana kwa mamlaka kamili ya Serikali ya Zanzibar kutokana na kushindwa kwa vyama vya siasa kutetea utaifa wa Zanzibar kwa sababu vyama vya kisiasa vimezingirwa na katiba  ya Jamhuri ya Muungano wa Zanzibar na Tanganyika.
Katika hali hiyo ni nani angejitolea kulizungumza jambo hilo? Chombo pekee ambacho ndicho kinawakilisha umma wa Zanzibar ni Jumuiya na Taasisi za Kiislamu na kukabidhiwa jukumu la mambo tofauti. Jumuiya ya Uamsho ambayo ndio yenye sauti pekee katika jamii na kwasababu hiyo imelazimika kutoa sauti ambayo hakuna mwengine angeliweza kutoa.
Watu wa Zanzibar wajuwe kuwa wachache wasioipendelea mema Zanzibar hawatasita kuunda kila njama za kuharibu vuguvugu la kudai mamlaka kamili ya Zanzibar. Viongzi wa jumuiya wanawataka Wazanzibar watambue njama hizo na wasiyumbishwe katika msimamo wao.
Jumuiya ya Uamsho si kundi la magaidi, wala si kundi la wachoma  moto makanisa au waporaji wa mali za umma. Jumuiya  ya Uamsho inatoa sauti kwa njia za amani bila ya kutumia nguvu za silaha bali kwa kutumia nguvu za hoja na inaendesha harakati zake juu ya misingi ya sheria za nchi  na katiba.
Wananchi wa Zanzibar kudai uhuru wa kujiamulia mambo yetu ni haki yetu ya msingi na kwa hilo HATUNA MJADALA MPAKA KIELEWEKE, tutaendelea kudai haki zetu kwa kila hali bila ya kuvunja sheria za nchi.
Tunasisitiza kuendelea na kudai Zanzibar huru ingawa tunaelewa gharama ya kufanya hivyo ni kubwa ikiwemo kupoteza roho zetu kwa mfano aliekua Rais wetu wa kwanza Almarhum Abeid Aman Karume alipoteza uhai wake baada ya kuanza kuugusa muungano pale alipopiga marufuku azimio la Arusha kutumika Zanzibar na kusema mwisho wake Chumbe pia na kusema muungano ni kama koti likikubana unalivua haukupita muda alipoteza uhai wake.
Mzee wetu mheshimiwa Aboud Jumbe alipotengeneza mazingira ya muungano wa haki alikwenda Dodoma akiwa RAIS alirudi akiwa raia wa kawaida aliuzuliwa urais. Hayo ndio  matokeo ya kuugusa muungano. Watu walipoteza mali zao, heshima zao na roho zao eti kwa sababu ya kuugusa muungano.
Wazanzibar tutaendelea kudai Zanzibar yetu huru. Kama sheria zinavyoelekeza ikiwemo kudai kuwepo kwa KURA YA MAONI kwa njia ya amani.
                                           TUWACHENI TUPUMUE!!!!!!!
WABILLAHI TAUFIQ….

Friday, June 15, 2012

MBUNGE AWAPA UKWELI WANAFIKI WA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU KUCHOMWA NA KUPINGWA MABOMO MISIKITI NCHINI ZANZIBAR

15th June 2012 Mbunge wa Chakechake, Pemba, Rajab Mbaruku Mohammed (CUF), amevishutumu vyombo vya habari kwa madai ya kuandika upande mmoja wa vurugu zilizotokea Zanzibar, akidai havikuripoti uchomaji wa misikiti na mali za watu na badala yake vilitangaza kuhusu uchamaji wa makanisa pekee.
Hata hivyo, wakati Mbunge huyo akitoa tuhuma hizo, kwa mujibu wa taarifa rasmi zilizotolewa na Jeshi la Polisi Zanzibar kuhusiana na matukio hayo, hakukuwa na taarifa za misikiti kuchomwa moto.
Huku akirejea vurugu zilizotokea nchini Kenya baada ya uchaguzi mkuu wan chi hiyo ambapo mamia ya watu waliuawa na mali zao kuharibiwa, Mohammed alisema ripoti ya uchaunguzi ilionyesha kuwa, vurugu hizo zilichochewa pia na
vyombo vya habari.
Aliishauri Serikali ya Muungano na Zanzibar kuunda tume huru ya uchunguzi ili wahusika wavurugu za Zanzibar wachukuliwe hatua na kudhibiti hali hiyo isitokee tena.
“Katika vurugu zilizotokea Zanzibar Mei 26 na 27 mwaka huu, vyombo vya habari havikuripoti uchomaji wa baadhi ya misikiti na mali na badala yake viliripoti kuhusu uchomaji wa makanisa na mali zake…viliripoti habari za upande mmoja tu, sasa unasemaji kuhusu vyombo hivyo vilivyotoa taarifa za upande mmoja,” alihoji.
Akijibu Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alisema: “Rai ya kuunda tume huru ya uchunguzi ni nzuri lakini siwezi kulisemea moja kwa moja hapa, tutawasiliana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kuona hatua walizofikia kumaliza tatizo hilo na kama kuna haja ya kuunda tume.
Kuhusu uandishi wa habari alisema ni lazima habari ziandikwe kwa ulinganifu. Hata hivyo, alisema jambo kubwa hapa ni kudhibiti chanzo. “Ni vizuri jambo hili likadhibitiwa, lisiendelee.” Alisema.

FREE ZANZIBRA PEOPLE FROM MKOLONI MWEUSI.
DR SHEIN,MAALIM SEIF,BALOZI IDDI mume bana kimya na munajuwa misikiti imepingwa mabomu na kuchomwa moto na nyinyi ati ndio maraisi wa nchi hii munabebe tu mambo mutakwenda kumueleza vizuri mwenyezi mungu nyinyi.kama walivyo juwa kumshika sheikh mussa na hao polisi walio choma moto msikiti na kuipinga mabomo walikuwa washtakiwe na wafungwe maana nyinyi ni viongozi mukisema tu ni nani aliyefanya hayo atajulikana ila mume bana kimya munawachiya watu waendele kuipaka matope uamsho ili izimwe ila kwa uwezo wa mola haitazimwa ile mpaka nchi yetu ya zanzibar iwe huru na nyinyi kaliyeni madaraka tu na kula raha za dunia kumbukeni kiyama hakiko mbali kaburi haliko mbali.

MWANDISHI JACKTON MANYERERE AKIMHOJI SHEIKH FARID NA UAMSHO NCHINI ZANZIBAR


Mahojiano Ya Mwandishi Jackton Manyerere Na Wana- Uamsho Zanzibar
5 June 2012
*Wasema bayana kwamba wanataka Zanzibar iwe ‘Sovereign State’, ijitawale yenyewe
*Wasema Dar es Salaam ilikuwa ya Zanzibar, maili kumi kuingia ndani, mikataba ipo ila wazanzibar ni wakarimu hawana hata ya Dar es Salaam watawachiya wao.
*Kiongozi ahoji: Kilomita chache zinakushughulisheni wakati mna mapori tele
Jumuiya ya Uamsho ya Visiwani Zanzibar hivi karibuni ilijikuta matatani, baada ya Jeshi la Polisi kutumia mabomu ya kutoa machozi kutawanya wafuasi wake. Mwandishi wa gazeti la JAMHURI, Manyerere Jackton, amefanya mahojiano ya ana kwa ana na Amiri Mkuu wa Jumuiya ya Maimamu Zanzibar, Sheikh Farid Hadi Ahmed, aliyeeleza lengo kuu la Jumuiya hiyo ya Kiislamu.
JAMHURI: Ni nini chanzo cha vurugu za Mei 26?
Sheikh Farid: Kilichotokea hapa kwa muda mrefu, japo inasikika Jumuiya ya Uamsho ndiyo inayofanya mihadhara, lakini ni Umoja na Jumuiya za Kiislamu ambazo zimekuwa zinaendesha mihadhara. Tumefanya mihadhara zaidi ya mia moja hadi sasa – mikutano zaidi ya mia pamoja na makongamano tofauti. Na lengo zaidi hapo awali lilikuwa ni kuwaelimisha watu kujua Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na kuona ni jinsi gani inawabana Wanzibari na haijawapa ile haki yao ya kuujadili Muungano.
Na baada ya hapo kilichokuwa kinazungumzwa zaidi ni kuwaelimisha wananchi kujua haki yao kujua mustakabali wa nchi yao na umuhimu wa kuuhoji Muungano au kuujua Muungano. Wazanzibari wao kama washirika na Watanganyika wana haki ya kuuhoji Muungano. Sasa hii mihadhara imeendelea kwa muda mrefu na ilikuwa inakwenda misafara ya mbali mingine hadi shamba. Na ilikuwa misafara mikubwa inaweza ikabeba magari mia mbili, mia mbili na zaidi, kuna mapikipiki, watu wanakwenda wanarudi kwa usalama wala hakuna tabu na matatizo yoyote. Hayo yote ndiyo kwa jumla yamefanyika.
Sasa kilichojitokeza hivi karibuni ni kuwa lilifanyika kongamano. Katikati ya lile kongamano watu waliamua kutembea, kama ni matembezi tu lakini si maandamano hasa. Maandamano ni kitu ambacho kimeandaliwa, kina slogan yake, kina ujumbe, kinaenda maeneo maalumu kufikisha ujumbe maalumu. Haikuwa hivyo.
JAMHURI: Je, Polisi walivamia?
Sheikh Farid: Polisi hawakuvamia, hawakuwahi kuvamia. Na walipokuja kwa kweli walikuja matembezi yameanza kutoka maeneo ya Lumumba. Watu wote wameacha baiskeli zao, vifaa vyao palepale na walinzi walibaki eneo lile. Watu wametoka wametembea mpaka hapa Michenzani, katika roundabout, wameshuka chini mpaka maeneo ya Kariakoo. Kwa hiyo watu wakaenda moja kwa moja wakarudi kwenye kile kiwanja walichoanzia. Wakarudi palepale wakaaa kitako. Wakawa wanaendelea na shughuli zao. Wakazungumza, wakazungumza mpaka wakamaliza. Walipomaliza kuzungumza wakatawanyika wakaenda majumbani mwao salama salmini.
Nashangaa sasa alipokuja Waziri, Jeshi la Polisi wamemdanganya. Na alipokuja IGP wamemdanganya wamemwambia uongo. Wanamwambia kuwa Jeshi la Polisi limejaribu kuzima fujo, lakini si kweli. Ni uongo huo. CD zipo zinauzwa kila pahali. Wazi kabisa. Zinaonyesha maandamano kitu mbali, na zile fujo kitu mbali kabisa. Hayo matembezi kitu mbali na hizo fujo kitu mbali kabisa.
JAMHURI: Nini chanzo kilichosababisha fujo?
Sheikh Farid: Fujo ilisababishwa na Jeshi la Polisi kukosa utaratibu, kuchukua mazoea yale yale ya uhuni na mabavu. Ndicho kilichofanyika kwa sababu kati ya mmoja wa watu waliohudhuria pale kwenye viwanja palipokuwa na mdahalo ni Maalim Musa Juma, yeye ni mmoja katika wahadhiri wala si kiongozi wa Jumuiya ya Uamsho, lakini ni mwalimu ambaye anahadhiri, anafundisha. Sasa siku ile yeye alikuwa si mzungumzaji, alikuwa mkaribishaji wa wazungumzaji. Walichokifanya wakati wa majira ya saa moja na kidogo usiku, yumo msikitini mwake anasomesha, alikwenda mtu ana shida naye. Alipomwita, kutoka nje kuwafuata wale watu wakamkamata kwenye kiuno, na wengine watano wamekuja wamemzoa wamemshindilia kwenye gari wakampeleka kituo cha Polisi. Wale vijana waliokuwa pale – wanafunzi na watu ambao wanampenda, na sasa kimekuwa kitu sensitive kwa sheikh kumdharau. Sasa hii dharau iliyofanyika, wananchi hawajakubali kwa hiyo wakaanza kupigiana simu wote kwamba Sheikh wetu kakamatwa, twendeni tukamdai kwanini kakamatwa, na tujue. Kama kumchukulia dhamana tumchukulie.
JAMHURI: Lipi jina sahihi la Jumuiya hii? Ni Uamsho au Muamsho?
Sheikh Farid: Hizi harakati zinazoendelea hapa nchini (Zanzibar) zinafanywa na Umoja wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu. Ndiyo wanaofanya hizi harakati zote. Isipokuwa katika utaratibu wa mambo ya mihadhara, Jumuiya pekee ina uzoefu mkubwa kwenye mihadhara ni Jumuiya ya Uamsho.
JAMHURI: Taasisi ya kidini kwanini ijikite kwenye siasa?
Sheikh Farid: Hakuna tatizo lolote. Hakuna tatizo kikatiba, hakuna tatizo kidini yetu, hakuna tatizo kimtazamo sahihi wa wanasiasa. Kote hakuna tatizo. Mtazamo sahihi wa wanasiasa. Tumchukue Rais wetu wa hapa Zanzibar, Mheshimiwa Jumbe ameandika kitabu na kuna sura maalumu anaita “Dini na Siasa”. Kaeleza mengi. Kaeleza jinsi watu wengine walivyo katika dini zao, lakini akaelezea ama upande wa Uislamu huwezi kutenganisha dini na siasa. Hilo moja. Basi kama watu wanajua wanasiasa, huyu mwanasiasa anatamka kwenye kinywa chake. Alikuwa Rais wa Zanzibar, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Tanzania. Alikuwa pia Makamu wa Mwenyekiti wa CCM na kaeleza wazi kabisa kwenye Uislamu huwezi kutenganisha dini na siasa.
Ukija kwenye Koran, Uislamu unahesabu kuwa dini ni mfumo kamili wa maisha ya mwanadamu, ikiwamo sehemu ndogo inayoitwa “siasa”. Siasa kwenye Uislamu au kwenye lugha ya Kiarabu, neno hilo hilo siasa kama lilivyo, maana yake ni “uongozi”, kwa hiyo uongozi ni sehemu ndogo, ni mlango katika maisha ya mwanadamu au katika dini ya Kiislamu. Kwa hiyo sisi kuzungumza siasa ni sahihi kabisa.
JAMHURI: Nyuma ya Uamsho kuna msukumo wa kisiasa?
Sheikh Farid: Uamsho haina uhusiano na CUF. Hili suala limeanza ilipokuja hii rasimu ya Katiba, ilipokuja kama rasimu, Serikali nzima iliikataa, Wazanzibari waliikataa wakaona wamedharauliwa. Iliporudi ikaja na dharau nyingine, badala ya kuletwa kama rasimu ikaletwa kuwa ni sheria sasa…kinguvu. Unaposema sheria maana yake ni nguvu, utake usitake. Ikaletwa kama sheria na ilikuwa iletwe kama rasimu. Hilo tatizo la mwanzo. Tatizo la pili, ndani ya rasimu ile kama alivyosema Mheshimiwa Kikwete mwenyewe wakati anazindua Tume, hakuna mjadala wa Muungano mle ndani yake, ni kwenda mbele tu kuuboresha, lakini suala la kutazama mustakabali wa Zanzibar je, inafaidika na Muungano? Hilo hakuna. Imeshapita miaka 48 na hawajawahi kuulizwa huko nyuma. Sasa sisi hapa ndipo tulipoona kuna haja ya kuulizwa, na njia ya kufanya hivyo ni kupitia kura ya maoni.
JAMHURI: Kuna umuhimu wa kuwapo Muungano wa Tanganyika na Zanzibar?
Sheikh Farid: Sisi tunachotaka ni kura ya maoni. Wazanzibari waseme wenyewe. Hakuna mtu amepewa kibali cha kumsemea mtu. Hakuna Mtanganyika wala Mzanzibari. Kila mtu aseme mwenyewe na hiyo ndiyo demokrasia, kwa hiyo sisi kama Jumuiya ya Taasisi za Kiislamu tunasema iitwe kura ya maoni. Nisiseme mie, mie nitasema kwenye karatasi. Kila Mzanzibari atasema kwenye karatasi. Kura ya maoni ni nyepesi tu.
JAMHURI: Mbona hamjasikika mkilaani kuchomwa makanisa? Mnaunga mkono kitendo hicho?
Sheikh Farid: Tumeshatoa taarifa nyingi sana. Tatizo unajua hakuna uadilifu kwenye uandishi wa habari. Hakuna uadilifu hata kwenye hii TV yetu iliyopo hapa (ZBC), hata redio zilizoko hapa hakuna uadilifu bwana. Hii ni kwa mtu anachukia kitu anakuwa si mwadilifu. Na haya ndiyo yanayosababisha matatizo kama haya kuzuka. Mtu unamnyima haki yake anafika mahali hawezi kustahamili. Kwa hiyo sisi kiufupi tunalaani vibaya sana suala zima la kuchoma makanisa, dini haisemi hivyo. Si dini yetu wala si nyingineyo, haisemi hivyo. Lakini tunashangazwa vilevile, tumechoma makanisa, sisi ameuliwa imam ndani ya msikiti na Jeshi la Polisi…ameuliwa imam ndani ya msikiti, huko Mwembechai kwenu huko Dar es Salaam ameuliwa Muislamu ndani ya msikiti. Acha kuchoma makanisa. Sisi tunalaani uvunjifu wa amani wa aina yoyote – ikiwa wa ubaguzi wa kidini wa kuchoma makanisa, ikiwa wa kuwahujumu watu, tukubali haya si mafunzo maana hata kwenye nyumba yangu wamekuja wamehujumu ndani, wamepiga mabomu ndani ya nyumba, wamevunja mlango.
JAMHURI: Mambo gani ambayo Zanzibar haitendewi haki ndani ya Muungano?
Sheikh Farid: Ni mamlaka kamili ya kimaamuzi ya kimataifa, ya ndani na nje ya nchi. Hiki ndicho tunachokosa Zanzibar. Wanaita Sovereignty, Zanzibar inakosa sovereign yake kwa hiyo tunataka sovereign state. Kama ni Zanzibar iheshimike, kama ni Rais wa Zanzibar aheshimike, Serikali ya Zanzibar iheshimike ndani na nje ya nchi. Iwe na mamlaka kamili. Na wao wenyewe (Wazanzibari) wataona utaratibu nini watafanya. Kwa hiyo wananchi waulizwe, chepesi tu hakina tabu. Si waliulizwa kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa na hakupigwa mtu?
JAMHURI: Marekani majimbo yale ni nchi – ni Muungano, mbona majimbo hayana mamlaka kamili kama nchi?
Sheikh Farid: Mbona upo muungano tofauti na huo. Kama Umoja wa Ulaya si upo? Upo vipi? Katika Umoja wa Mataifa si kila nchi ina kiti?
JAMHURI: Huo si muungano ni kama jumuiya tu.
Sheikh Farid: Huo ni muungano, si wameungana katika vitu maalumu? Wamarekani wameamua wao vile. Sisi tumeamua hivi. Wao hatuwasemei. Sie tunaamua tunachotaka sie. Na sisi hawezi kutulazimisha mtu tuamue kwa akili za Kimarekani. Wamarekani wataamua wao wenyewe Kimarekani, haki za Kizanzibari zitaamuliwa Kizanzibari-Zanzibari.
JAMHURI: Ungependa Muungano wa uwe wa namna gani?
Sheikh Farid: Mie ninachosema ule mchakato wa Katiba imekuwa sawa na kumchukua ng’ombe na gari ya ng’ombe halafu ng’ombe ukamweka nyuma gari ya ng’ombe ukaweka mbele. Au mashine ukaweka nyuma, gari ukaweka mbele. Sijui itakwenda vipi. Sasa tunashangaa, watu wataalamu wana akili lakini inaonyesha akili zao zimefika mahali wanatuona sisi wapumbavu. Sisi bwana tunasema ilivyo kitu kinachowafungamanisha Wazanzibari na Watanganyika ni Muungano. Ninyi mnataka kujadili Katiba ya Muungano, hili tatizo la Muungano kwanini msilizungumze mwanzo? Hili la kuzungumza mwanzo. Kwanza, lizungumzwe hili kwanza mpaka likae sawasawa halafu ndiyo tuzungumze Katiba.
Sasa unasema mimi na wewe tunataka kufanya biashara njoo tufunge mkataba mimi na wewe. Si tuzungumze tukubaliane kwanza halafu ndiyo tuandike mkataba kwa sababu Katiba ndiyo umefunga kila kitu. Kitu kinachotufungamanisha tukizungumze mwanzo. Wananchi wapewe fursa wazungumze mwanzo. Watu wanapewa fursa hizo wasiokuwa na nchi mwanzo…hii ni nchi. Hii ni nchi. Ilikuwa ni nchi tena kubwa mpaka Dar es Salaam yote ilikuwa yetu ile, tena mikataba ipo ya kimataifa ya kuonyesha Dar es Salaam yote ile ni yetu sisi. Na kuingia ndani huko maili 10.
JAMHURI: Je, mtaidai Dar es Salaam?
Sheikh Farid: Hatuna shida nayo hiyo. Tutakuachieni. Sisi watu makarimu sana sie. Tutawaachieni. Nashangaa nyie tu hizi kilomita za mraba ngapi zinakushughulisheni nyie wakati mna mapori tele kule juu, na mna ardhi ya kwenda na kurudi, mashamba ya kwenda na kurudi mnang’ang’ania hiki tu!
JAMHURI: Muungano ukivunjika, nini hatima ya Wazanzibari wanaoishi/waliowekeza Bara?
Sheikh Farid: Jawabu moja, wewe huwajui Watanzania wanaofanya biashara Kenya? Uganda? Hatima yao ipo vipi? Sasa ninyi inaonyesha kuna watu wana fikra mbovu katika vichwa wanaona maana yake tukiwa hivi (tukitengana) tutakuwa maadui, hata! Udugu lazima utabakia. Tumeoa kule. Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar usingizi wake (mkewe) ni wa kule (Bara) au hujui wewe? Hatuwezi kuachana bwana, watu watabakia, mapenzi yapo, undugu upo, ujirani mwema kabisa, waliokuwapo hapa Watanganyika watabakia, Wakristo hapa watabakia, itakuwa kila kitu kina utaratibu. Si maana yake kwamba mmetengana muwadhulumu wale ndugu zenu (walio Bara). Mkiwadhulumu sawa! Sisi kawaida yetu hatuko hivyo.