Sunday, July 29, 2012

MASHINDANO YA KUHIFADHI QURAAN KWA MIAKA 20 YAKIENDELA NCHINI ZANZIBAR


MAJAJI WAKIFUATILIA WASOMAJI WALIO HIFADHI QURAAN JUZUU 30 YALIYO WASHIRIKISHA WANAFUNZI WA KIKE KATIAK UKUMBI WA SALAMA BWAWANI KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA KUHIFADHI QURAAN HAPA NCHINI ZANZIBAR

SHAMSI VUAI NAHODHA AJA NA FITINA MPYA ZA KUTAKA KUWAFITINISHA WAZANZIBARI


SI ULIKUWA WAZIRI KIONGOZI WEWE MBONA HUKUSEMA KUHUSU WIZI WA ARDHI
AU WAKTI ULE WEWE PIA ULIKUWA UKIBA NDIO MAANA HUKUSEMA KITI..?
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha, amewaponda baadhi ya viongozi wa Zanzibar wanaozungumzia kero na Muungano kwa nia ya kuficha makucha ya ufisadi wao.
Alishusha kombora hilo wakati akichangia hoja kwenye semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi iliyofanyika juzi mjini hapa.
Alisema kuna ubadhirifu, wizi, uporaji wa ardhi na rasilimali za Zanzibar unaofanywa na baadhi ya vigogo wa Zanzibar lakini vitendo hivyo vinafumbiwa macho.
“Viongozi wanaozungumzia matatizo ya Muungano kwa jazba hapa Zanzibar kwanza wanatakiwa kupima uadilifu na matendo yao ziwemo pia sheria zitakazowabana kujua walipataje mali walizonazo”, alisema
Nahodha ambaye aliwahi kuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kuanzia mwaka 2000 hadi 2010 kwenye awamu ya Rais Amani Karume alisema hakuna Mtanganyika anayepora ardhi, fedha au kodi za wananchi ila viongozi wa Zanzibar.
Alisema yeye ni muumini wa Muungano wa serikali mbili uliopo na kupendekeza suala la mafuta na gesi asilia litolewa kwenye Muungano kwa kufuata taratibu zilizoliingiza jambo hilo katika orodha ya masuala ya Muungano.
Pia Waziri Nahodha alimuuliza Waziri wa zamani wa SMZ na Serikali ya Muungano Hassan Nassor Moyo kueleza matukio yaliyolitishia usalama wa ndani kuanzia mwaka 1964 hadi 1972.
Moyo akionekana kubabaika, hakujibu swali hilo na kujikuta akipata wakati mgumu kutokana na kutokea kifo cha Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume aliyepigwa risasi na Luteni Homuod Mohamed.
Nahodha alisema ana hakika ya kutokea matukio 14 ya njama kwa maelezo ya kiintelijensia yalipangwa kuipindua SMZ ambayo yaliandaliwa na wapinzani na kwamba tukio la 15 katika njama hizo lilifanikisha kifo cha Mzee Karume April 7 mwaka 1972.
Moyo alieleza msimamo wake kuwa Muungano uliopo wa serikali mbili unahitaji kufanyiwa marekebisho na maboresho makubwa ili uendane na wakati.

WATALI NI WACHAFU.WANATUPOTEZEA MELA,UTAMADUNI NA USTARABU WA WAZANZIBARI VIONGOZI PUNGUZENI TAMAA


HUYU NI MZUNGU WA KIKWETE KUTOKA NCHINI TANGANYIKA NA WAZUNGU WENZAKE KUTO NCHI ZA ULAYA WAKIJIVIJARI KWENYE NCHI YATU YA ZANZIBAR ILIO SAFI WAO WANAINAJISI KWA UCHAFU WAO WAKWENDA TUPU NA MENGINE MENGI TU HATA HAYASEMEKI.
ZANZIBAR ni njema…atakaye aje. Huu ni usemi maarufu wa wahenga wa Visiwani ambao umekuwa na lengo la kuwaonesha majirani zake na ulimwengu kwa ujumla kwamba Zanzibar hakuna matatizo ya kimaisha pia ulikuwa ni msemo wakuwatarifu wazanzibari walio kimbia mauwaji ya 1964 kuwa sasa nyumbani ni kwema na ataye aje.Walilenga kuuambia umma kuwa Wazanzibar ni ni wema, wakarimu na atakaye kwenda kuishi au kutembelea Zanzibar anakaribishwa kwa mikono miwili na moyo mkunjufu.
Kumbukumbu zinaonyesha jamii yoyote ile duniani, bila ya kujali imani zao, tofauti za dini au makabila, siku zote huwa inapendelea na kuweka sheria zitakazohakikisha mila, utamaduni na desturi za watu wake zinaendelezwa na mtu yeyote yule, awe mwenyeji au mgeni, anayezibughudhi , kuzikejeli au kuzidharau huonekana hana nia njema na jamii hiyo adhabu hupata mtu huyo ya kifugo au kutolewa kabisa katika nchi.
Ni kweli katika zama hizi za hivi sasa za utandawazi dunia imeshuhudia mabadiliko mengi ya kijamii na maisha kwa jumla. Jambo ambalo miaka ya nyuma hapa kwetu lilionekana sio la kawaida.
Kama mwanamume kuvaa herini au kidani, limekuwa likikubalika siku hizi. Wapo walioipokea hali hio kwa furaha na wapo walioiridhia kwa shingo upande, lakini hio ndio hali ya dunia ya leo.
Mambo kama haya ndio yaliyosababisha Waswahili wa kale kusema kiingiacho mjini sio haramu, lakini wapo watu hii leo wanaotofautiana na kauli hii na kusema si kila kinachoingia mjini ni halali.pia kuna msemo usamao hatakama ni kuinga basi usiige ovyo inamanisha yako ya kuingwa na mangine bora hata usiyangaliye.
Katika mambo ambayo watu wa Zanzibar wamekuwa wakiyajali sana na kutoyafanyia mzaha ni mavazi. Kwenda uchi au nusu uchi hadharani ni mambo ambayo watu wa Visiwani wamekuwa hawayakubali na hata anapotokea mtu mwenye matatizo ya akili anafanya hivyo watu hujitolea kumsitiri kwa kumvisha nguo. Hayo ndiyo maisha ya watu wa Zanzibar.Visiwa hivi vimekuwa kwa muda mrefu na sheria zake za mavazi. Sheria hizi zilikuweka miaka na kaka na baadaye zilitiliwa mkazo zaidi baada ya Mapinduzi ya 1964 ambapo hata watalii waliokuja Zanzibar wakiwa na mavazi ambayo kwa mila, silka, desturi na utamadini wa Zanzibar hayakubaliki walitakiwa kuchagua – kununua doti ya khanga au kitenge na kufunika sehemu ambazo watu wa Visiwani wanaona hazifai kuanikwa hadharani.
Rais wa kwanza wa Zanzibar, hayati mzee Abeid Amani Karume, aliwahi kusema : “Fedha za kigeni za watalii hazina thamani inayozidi mila na desturi zetu. Akitaka kwenda mtu uchi aende kwao si hapa kwetu Zanzibar.”huyu alikuwa raisi wa kwanza japo nae hakuchanguliwa kikura lakini alipenda nchi na kuioneya uchungu tafauti na hawa wanaojita mapidunzi daima wana wa kampuni ya mapinduzi daima wamekuwa hawajali ni mila wa nini disturia za visiwa hivi wao pesa tu basi.hata kama nchi nzima watu wako kama wanyama wao hawajali kwa kuwa kuna pesa hawa kweli ni viongozi hawa au ni madudu mwitu yanayo ila zanzibar na kuifisidi..?Katika mwaka 1965, aliyekuwa Rais wa Liberia, William Tubman, alipokuwa amepanga kufanya ziara ya Zanzibar alitaka watu wote watakaokwenda Uwanja wa Ndege wa Zanzibar kumpokea wavae suti.kumbuka yeye ni raisi wa nchi nyengine anatowa amri kwa raisi wa nchi nyengine nini kilotoke.Marehemu mzee Karume alikasirishwa na maelekezo yale na yeye alimpelekea salamu Tubman kumwambia kuwa mgeni yeyote anayefika Zanzibar kwa matembezi ya kiserikali basi lazima avae kanzu, koti, kofia na viatu vya makbadhi.hii inatufundisha ukiwa raisi wa zanzibar uwe mjasiri na mkakamavu na usikubali kusikiliza amri ya raisi yoyote kutoka nchi za jirani bahati mbaya toka kufa mzee karume nchi hii inaendeshwa na DODOMA na maraisi wamegeuzwa na kuwa mawaziri wasio kuwa na wizara maluum msiba msiba msiba mkubwa.Matokeo yake baada ya mazungumzo marefu ya kidiplomasia Tubman alikuja Zanzibar akiwa amevaa suti yake na watu waliompokea walivaa kanzu, koti, kofia na makbadhi yao na alipewa vazi hilo kama zawadi alipoondoka. Hili lilikuwa somo kuwa watu wa Zanzibar hawakuwa tayari kuona wageni wanachezea utamaduni wao.
Wakati ule watalii walielezwa tokea huko kwao kabla ya kufanya safari ya kuja Zanzibar aina ya mavazi ambavyo wanatakiwa wavae wanapokuwepo Visiwani na kuambiwa kuwa kutotii maelekezo hayo ni kosa la jinai.
Wapo watalii waliojaribu kukejeli maelekezo hayo na matokeo yake ni kusukumwa jela kwa wiki kadhaa na kunyolewa vipara. Hili lilikuwa fundisho kwa wengine.
Hivi sasa sheria hizi bado zipo, yaani hazijafutwa. Lakini kinachoonekana ni kufumbiwa macho na kupelekea watu kulalalama pembeni na hadharani kwamba utalii unavuruga mila, utamaduni na desturi walizorithi watu wa Zanzibar kutoka kwa wazee wao.
Ni kawaida siku hizi kuona kundi la watalii wanatembea na vichupi katika soko kuu la Zanzibar na kuwabakisha watu wanatikisa kichwa na kujiuliza: Hii ndiyo Zanzibar tunayoitaka?
Huko vijijini mambo hayasemeki. Watalii wanaofikia katika hoteli za fukwe za bahari huenda vijijini kutembea wakiwa wamevaa bikini (vazi la chupi na sidiria) na kupelekea vizee kukimbilia nyumbani kwao kujificha kwa vile macho yao hayawezi kuona aibu ile.
Ni kweli utalii kwa hivi sasa unaiingizia Zanzibar asilimia 73 ya pato lake la fedha za kigeni na kuchangia wastani wa asilimia 25 ya pato la taifa kila mwaka. Hapa suala linalofaa kujiuliza ni je, ni haki na sawa kwa fedha za kigeni ziruhusiwe kuvuruga utamaduni, mila na desturi za watu wa Zanzibar?
Ni vizuri kwa wahusika katika serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuitafakari hali hii kwa sababu manung’uniko ya wananchi juu ya watalii kwenda uchi au nusu uchi hadharani, mambo ambayo hata huko kwao hawayafanyi, yamekuwa makubwa na yanawaudhi watu.Hivi sasa watu wanalalamika na wanaonekana kuvumilia mwenendo huu kwa unyonge, lakini ipo hatari ya kutokea watu namanisha wazee na vijana kuonyesha hasira zao na matokeo yake kuwa mabaya. Ni kweli watu wanao uhuru wa mavazi, lakini si kwenda uchi hadharani.Inawezekana wakatokea wale ambao watasema huwezi kuwachagulia watu aina ya nguo za kuvaa, lakini hapa tukumbuke kuwa hao wazungu wanaokuja kwetu na kutembea nusu uchi pia wanazo sheria za mavazi huko kwao .Miongoni mwao ni kukataza wanafunzi wasivaie hijabu wanapokuwa shule na wale wanaojifunika gubi gubi au kuvaa “Ninja” kutoruhusiwa sehemu nyeti, kwenye benki,ofisi za serekali,hospitali pia kuna nchi nyengine hata ukiliva vazi la ninja nje tu sio kuwa unakwenda kweye benki au ofisi ya serekali laa nje tu pia unatozwa faini au unaishia jela washapitisha sheria hii france,belgum,swiss na holland pia na hili ni vazi la hishma la kujifinika gubi gubi au ninja lakini haliendani na madili yao au desturi zao ndio hawalitaki kwa nini sisi hapa zanzibar tuwaone haya kuwambia kuwa hilo vazi la vichupi pia kwetu hapa sio vazi la heshma na haliendani na mila na desturi zetu..kwanini hatuwambi hivyo..? na kuwalazimisha wavae vizuri.ila hilo halipo maana akili za viongizi wetu ziko kwenye wimbi la pesa tu basi hata kama mila,desturi zinaharibika wao wanapata pesa basi ni poa tu maneno ya mtaani poa tu.Sasa kama watu wengine wanaweza kuwa na sheria za mavazi na kuambiwa lengo lake ni kulinda usalama wao, kwa nini Zanzibar ione tabu kuendelea na kuwa na sheria za mavazi za kulinda mila, utamaduni na desturi za watu wake?Hili ni suala nyeti ambalo kampuni ya Mapinduzi Zanzibar haistahili kulipuuza.naita kampuni ya mapinduzi zanzibar kwa sababu mimi naona hatuna haswa serekali maana kama tuna serekali nchi hii sio ya kuwa ovyo ovyo kama tambara la kupingia decki. hii nchi sio maaskhara ukijuwa historia yake huko ilikotoka leo ipo ipo tu kama kishungu cha taka kinasubiri rikwama la wazoa taka lije likiondoshe.Ni ukweli usiokuwa na ubishi kuwa zaidi ya aislimia 99 ya watu wa Zanzibar ni Waislamu na imani ya dini yao ndio siku zote imekuwa mhimili mkuu wa sheria za nchi na mwenendo wa maisha yao. Utandawazi isiwe sababu ya kuvuruga mwenendo wao wa maisha.Watalii wanaweza kuvaa hizo bikini zao vyumbani mwao, kwenye ufukwe wa bahari au wanapokuwa kwenye maeneo ya hoteli walizofikia, lakini si kwenda na vivazi hivyo sokoni au mitaani na kuwaudhi watu ambao hawataki mila na utamaduni wao kuvurugwa na wageni wala wenyeji.Watu kuingilia mila na tamaduni zao na Wazanzibari wanayo haki ya kuringia mwenendo wa maisha waliorithi kutoka kwa wazee wao.Kama wengine watasema watu wa Visiwani hawajaendelea ieleweke kuwa Wazanzibar maendelo kwao si kwa mwanamume kuvaa herini au kidani, watu wa jinsia moja kufunga ndoa au mtu kwenda uchi hadharani.Ni matumaini yangu kuwa kiu ya kupata fedha za kigeni kutokana na sekta ya utalii haitakuwa sababu ya kuvuruga mila na utamaduni wa watu wa Visiwani.
Zanzibar inaweza kubakia kuwa ni njema na atakae aje, lakini aje kwa heshima, wema na hisani na anapaswa kutodharau mila, utamaduni na desturi za wa watu wake.
VIONGOZI MUONGOPENI MWENYZI MUNGU MUTAULIZWA SIKU YA KIYAMA ULIZICHUMA VIPI PESA ZAKO NA HATA RIZIKI ULIO KULA UMENUNU NA PESA ZIPI. 

Saturday, July 28, 2012

VIDEO-WASHENZI WA SHEINI WAMPIGA BOMU MFANYA BIASHARA NDANI YA DUKA LAKE SHEINI WAONE WASHENZI WAKO

MSIKITI UKO WAPI NA MADUKA YAKO WAPI NA HAWA WASHENZI WA SHEINI WANAPIGA TU MABOMU HII NDIO ASANTE YA SHEINI KWA WAZANZIBARI YEYE ANAJUWA KUWA HAKUSHINDA UCHANGUZI KAEKWA TU NA WAKURIA KUTOKA MRIMA NA SASA WAKURIA WANAKEREKA WAKISIKIA HATUTAKI MUUNGANO HATUTAKI MUUNGANO KWA HIYO WAKURIA NA WASHENZI WASHEINI LAZIMA WAFANYA HAYAA KUFURAHISHA DODOMA NA MRIMA SHEINI LAZIMA ANAYAMAZE MAANA AKISEMA TU ATAITWA DODODMA AVULIWE UWAZIRI ASIYEKUWA NA WEZARA

VIDEO-WASHENZI WA SHEINI WAKIWAPINGA MABOMU WAZENJI NA KUIBA

ANGALIA VIDEO HII KWA MAKINI NDIO UTAJUWA KUWA
ZANZIBAR HAKUNA SEREKALI KUNA WAHUNI TU KUANZIA SHEINI
NA MAKAMO WAKE WOTE WAWILI MPAKA MASHEHA WOTE WAHAUNI MAANA
KAMA SIO WAHUNI MBONA TOKA LITOKEA TUKIO HILI HATUJAMUONA SHEINI WALA
YOYOTE KUSEMA KITU KUHUSU KUPINGWA WASLAMU NA KUNAJISIWA MISIKITI KWA MAJIBWA YA HAWA WASHENZI SIKU WALIPOCHOMA MAKASI WASHENZI  HAWA HAWA NA KUWASINGIZIA WAZANZIBARI KISHEINI KILISIMAMA KIDETE NA KUROPOKA MPAKA POVU LA MDOMO LINAMTOKA LEO WAISLAMU WAMEVUNJIWA NYUMBA ZAO MISIKITI IMENAJISIWA NA MBWA NA MAJI YA KEMEKALI YOTE NAJISI TUPU NA WAISLAMU KUVUJIWA IBADA YAO SHEIN KIMYA KWUBWA ZAIDI SHEINI ANGALIA WASHEZI WAKO WANAVYO IBAA VYOBO VYA RAI KAMA VILE BAISKELI,PIKIPIKI,VESPA NA KATHALI SHEIN ANGALIA WASHENZI WAKO SHEINI UNACHUGA KULA YAKO USINYANGANYWE HATA KAMA WASHENZI WAKO WANAICHEZEA NYUMBA ALIYEKUPA PUMZI HAYA MUTAKWENDA KUMELEZA M/MUNGU

WAZANZIBAR WALIO NJE WATAKA HARRISON MAKYEMBE NA MKURUNGEZI WA BANDARI YA TANGANYIKA,BALOZI ALI IDDI NA MOHAMMED ABOUD WOTE HAWA KUSHTAKIWA KESI YA MADAI


· Ni lazima Wawajibike kisheria.
· Wadai Wazanzibari wanaoishi nje:

Na Free-Zanzibar People From Mkoloni Mweusi
Wazanzibari wanaishi nchi za nje na ambao jamaa zao walipoteza maisha yao na wengine kuathirika kiafya katika msiba wa kuzama boti ya MV Skagiti na MV Spice wamezungumza kwa sauti moja kutoka London, Toronto na Washington,Berlin,Paris,Dubai,na waliokuwepo nchini  ya Malesia baada ya kuhojiwa na muandishi wetu na kusema kwa pamoja kuwa watampeleka Mr Harrison Makyembe na mkurugenzi wa bandari ya tanganyika plasi VIP2 Balozi Ali Iddi na Mohammed Aboud kwa kile walichokiita kutowajibika na kutokufanya kazi zao sawasawa kama alivyohitajika na ile Kamati ya Sheini ya mwanzo iliyoundwa baada ya meli ya mwanzo kuzama iliyokuwa ikielekea Pemba katika mwaka 2011.
Wameelezea Wazanzibari hao kuwa kwa wakati huu wa uwazi na ukweli,kujiuzulu kwa Hamad Masoud ilikuwa ni vizuri sana lakini hata hivyo wahusika haswa bado wako madarakani waliofanya dungu zetu watoke roho zao mbichi na haya ni makosa ya jinai yametokea chini ya uongozi Mr Harrison Makayembe na mkurungezi wa bandari ya tanganyika na huyu VIP2 Balozi Ali Iddi n Mohammed Aboud. “Kwa kweli hawajawajibika bado mpaka watakaposimama mahakamani na kuwaeleza wote wale waliopoteza jamaa zao na ndugu zao kwanini meli iliachiwa kujaza watu kuliko kiwango chake ilipokuwa ikiondoka Dar Es Salaam.” Wameelezea Wazanzibari hao kwa uchungu sana walipohojiwa kwa njia ya simu na muandishi wetu wa Free Zanzibar People From Mkoloni Mweusi.
 alitakiwa Mr Harrison Makyembe n Mkurungezi wake wa bandari ahakikishe kuwa meli hazijazi abiria zaidi ya kiwango lakini imedhihirika kuwa wao hawajali wazanzibari wakifa na inaonyesha wanafurahia wazanzibari wakifa maana hata meli ilipoanza kuza walitowa tarifa ili wasaidiwe kuokowa watu lakini tanganyika haikufanya kitu chochote. ” Waliendelea Wazanzibari hao huku wengine wakilia kwenye simu.
“Ni kweli Mr Harrison Makyembe asingeliweza kuizuwia hali ya hewa kuchafuka au kuzuwia kasi ya mawimbi ya bahari, lakini kama boti ile ingelikuwa na abiria 250 tu ambao ndio kiwango chake basi msiba ungelikuwa mdogo kwa wananchi kuliko ulivyokuwa hivi sasa.au kama wangelitowa boti zao za uwokozi kwenda haraka kuokowa watu. baada ya tarifa waliopewa yasingelitokea haya ila ni wazanzibari wanao zama sio watanganyika ndio maana hawakujali hata baada ya kuwa na tarafa kama meli ya MV Skagit inazama” Waliendelea Wazanzibari hao
Wazanzibari hao wanakusudia kwa pamoja kumpeleka Mahakama Kuu ya Dar-Es-Salaam ‘a class-action lawsuit’ dhidi ya Mr Harrison Makyembe na Mkurungezi wake wa bandari ya dar es salaam,ambayo itamtaka awalipe ndugu wote wa Wazanzibari wote waliopoteza maisha yao na wale walioumia kwenye hili balaa, kwasababu wanasema yeye wao wanahusika moja kwa moja Mr Harrison Makayembe  na Mkurungezi wa Bandari ya dar es salaam.
Pia, wanaeleza kuwa kama Mr Harrison Makyembe angelisimamia vizuri usafiri wa meli baina ya Bara na Visiwani kushirikiana vizuri na Hamad kama walivyotakiwa na ile Kamati ya Sheini basi maafa yaliotokea yasingeli kuwa makubwa hivyo.
Wazanzibari hao wanastaajabu vipi baada ya kuelezwa na Kitivo Cha Hali ya Hewa cha DSM kuwa bahari itakuwa chafu boti ndogo kama hii ya MV Skagit iliweza kuruhusiwa kuanza safari yake na huku ikiwa imechukuwa watu zaidi ya kiwango chake. “ Hii ni miradi ya wakubwa na kama boti isingelisafiri watu wangelikosa sehemu yao”, ndio maana wakairuhusu iende ingelikuwa ni katika ziwa victoria wangelianchiya kweli ..? walihoji Wazanzibari hao.
Wazanzibari hao walivyoulizwa watadai kiasi gani walipwe kwa kila aliepoteza ndugu/jamaa yake walisema kwa sauti moja kuwa ” Nia yetu sio kutafuta uchumi bali kuwapa fundisho hawa wakubwa wa kitanganyika walio zoea kutuuwa”.
 Wazanzibari hao ambao hawakutaka majina yao yatajwe kwa sababu lawsuit bado haijaenda Mahakama Kuu,Dar Es Salaam.
Wazanzibari hawa walisema Mr Harrison Makyembe  tokea hapo alikuwa akijipendekezesha sana kwa wale wenye kumiliki vyombo vya usafiri Visiwani”, alieleza jamaa mmoja, kwa simu yake ambayo ilikuwa Aionyesha amehadhibishwa sana na tokeo la meli hii ikiwa ni ya pili kuza. ” Vipi  mwaka mmoja nyuma alipoulizwa juu  yakuwa unafikiri litatokea tena akasema no no no  na  meli mpya ya Azam alisema eti kuwa meli hio inakuja na itafanya safari kwa kukuwakikishia wazanzibari usafiri wa usalama na kusaidia wananchi. Huu ni uwongo na inaonesha vipi Mr Harrison Makyembe alikuwa anajikomba na wamiliki wa biashara za usafiri hapa Visiwani”na kujipingia hisabu za mamillioni mangapi atajiingizia meli hii ikija hapa nchini.
“Hawa wote ni wanyonyaji na wanajaza abiria kwenye meli/boti zao kama dagaa.” Alieleza huyu Mzanzibari mwenye simu hasira kweli kweli, huku akionesha kufoka zaidi na zaidi na  hasira kwenye matamshi yake.
“Ni lazima Mr Harrison Makyembe na Mkurungezi wake wa bandari ya dar es salaam pamoja na VIP2 Balozi Ali Iddi na Mohammed Aboud wafikishwe kortini kujibu hoja za wananchi, kama sio hivyo midudu hii Tanganyika siku zote itakuwa wanatumaliza na baadae kulazimisha mawaziri wetu wanajiuzulu tu” Alinena Mzanzibari mwengine kwenye simu kutoka nje.
Wachunguzi wa siasa wanasema kama hii class-action lawsuit itapelekwa Mahakama Kuu huko Dar es salaam basi labda itakuwa ni onyo kwa wale wote wanaopewa madaraka nchini nchini humo Tanganyika.

Friday, July 27, 2012

WAZIRI ASIYEKUWA NA WIZARA SHEINI AMEAGIZA WIZARA YA FEDHA KUSAKA FEDHA ZA KUNUNUWA MELI


Waziri asiye kuwa na wizara maluum wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Ali Mohamed Shein, ameiagiza Wizara ya Nchi Afisi ya Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo kuandaa utaratibu wa kupata fedha ndani ya wiki moja kwa ajili ya kununua meli kubwa mpya ya abiria wapatao 1000 na yenye uwezo wa kuchukua mizigo ya tani 100.
Shein ametoa agizo hilo leo wakati alipokuwa na mazungumzo na uongozi wa Shirika la Meli pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Shirika hilo ambapo pia kikao hicho kilihudhuriwa na uongozi wa Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano na Wizara ya Nchi Afisi ya Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo. Katika kikao hicho maalum
Shein ameiagiza Wizara hiyo kutafuta fedha hizo kutokana na vianzio vya ndani au nje ya nchi ama kutokana na taasisi zinazohusiana na mambo ya fedha.
Alieleza kuwa katika kipindi kisichozidi miezi miwili ujumbe maalum uende kwa Kampuni zinazotengeneza meli nchini Korea Kusini, China au Japan kwa ajili ya kuwasilisha fedha za utangulizi kwa ajili ya ujenzi wa meli hiyo.
Mapema uongozi wa Shirika la Meli, ulimueleza Shein kuwa kwa kawaida ujenzi wa meli yenye ukubwa huo, huchukua mwaka mmoja kukamilika.
Kikao hicho ambacho kilikuwa na lengo la kuangalia mwelekeo na Mipango ya Shirika la Meli pia, kilijadili hali halisi ya meli za Shirika la Meli na baadae kujadili masuala ya ununuzi wa meli mpya itokayowaondoshea usumbufu wa usafiri wa baharini wananchi wanaosafiri kati ya Unguja, Pemba na nchi ya Tanganyika.

HILI NDIO FIRAUNI LILILOTOWA AMRI WAISLAMU WAPINGWE MABOMU MSIKITI WA MBUYUNI

“Alaisallahu biahkamil haakimiina.”Kwamba, “Je, Mwenyezi Mungu si Hakimu muadilifu kuliko mahakimu wote?”Ikiwa na maana kuwa lazima atawalipa watu wote kwa uadilifu kutokana na matendo yao.Kamanda Azizi Juma Mohamed, amesema kuwa“wafuasi wa Uamsho wakiwa
M O J A y a A d h k a r iwaliyoleta Waislamu pale Masjid Mbuyuni ni kusoma kipande cha aya ya suratut tiin inayosema:
na bendera walianza vurugu,kupanga mawe barabarani na kuchoma moto matairi.Kufuatia hali hiyo, Jeshi
la Polisi likaamua kutumia nguvu kuwatawanya kwa mabomu ya machozi na maji yenye kemikali za kuwasha.”Vyombo vingine vya habari vikadai kuwa Uamsho walianza kuwashambulia Polisi kwa mawe.
“Alaisallahu biahkamil haakimiina.” Hapana shaka ipo siku ukweli utadhihiri na kila aliyeumia siku ile ama kupotelewa na kitu,atasimama kudai haki yake.Yote mpaka kauli hii kwamba Masheikh wa “Uamsho wakiwa na bendera walianza vurugu, kupanga mawe barabarani na kuchoma moto matairi”, itadhihirishwa na kutolewa hukumu na Hakimu Muadilifu.Hiyo ndiyo Siku ambayo vitafunuliwa vitabu ambapo“ u t a w a o n a w a k o s e f u wanavyoogopa kwa yale yaliyomo humo (katika vitabu vyao). Na watasema:Ole wetu! Kitabu hichi kina nini! Hakiachi dogo wala kubwa ila huliandika? Na watayakuta yote waliyo yatenda yamehudhurishwa hapo. Na Mola wako Mlezi h a m d h u l u m u y e y o t e . ”(18:49).Hata hili la Msikiti wa Mbuyuni nalo limeandikwa? Watahoji na kushangaa w a l i o a m u r u k u p i g a Waislamu mabomu na wale waliotekeleza amri hiyo.“Watasema: Ole wetu!Kitabu hichi kina nini!Hakiachi dogo wala kubwa ila huliandika.”Tunaambiwa Yeye ndiye Mfalme pekee siku hiyo-Maalik yaumiddiin. Siku hiyo hatakuwa na nafasi Obama, Kikwete wala Rais na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi.L e o K a m a n d a w e t u Azizi katika matukio kama hili la kupigwa waumini wakiswalia maiti, ndio msemaji. Ndio tunamsikiliza atupe taarifa rasmi. Ila Siku hiyo tunaambiwa“laayatakallamuuna ila man adhina lahur rahmaanu waqaala swawaaba.”Hiyo ndiyo siku ambayo Qu’ran imeisifu ikisema siku watu watakapoiona “kila mwanamke anyonyeshaye atamsahau amnyonyeshaye (mwanawe) na kila mwenye
mimba ataiharibu. Utawaona watu wamelewa, kumbe hawakulewa, lakini ni adhabu ya Mwenyezi Mungu kali mno.”Niseme kuwa ilikuwa ni msiba juu ya msiba pale p o l i s i w a l i p o w a v a m i a Waislamu wakiswali Swala ya Maiti Ghaibu na kuwapiga mabomu ya machozi. Binafsi nilibahatika kuwepo katika
swala ile. Nilishuka bandarini kiasi saa tisa kasoro na kuelekea moja kwa moja katika Msikiti wa Mbuyuni.
Nilipofika nilikuta Waislamu wakiendelea na Adhkari mbalimbali.“Hasbunallah waniimal w a k i l ” , n d i y o a d h k a r i niliyoikuta ikafuatiwa na kusoma kipande cha aya ya surat tiin inayosema:“Alaisallahu biahkamil
haakimiin.”Baada kumaliza adhkari,m s h e r e h e s h a j i ( M C )alitangaza ratiba ambapo alisema kuwa tutaswali swala ya maiti ghaibu,kisha itapigwa adhana na kufuatiwa na rakaa mbili za suna kabla ya kusimama kwa ajili ya swala ya Alasiri.Aidha ilifahamishwa kuwa baada ya swala kungekuwa na nasaha kwa ufupi kabla ya kuomba dua ya pamoja kufunga shughuli.Mpaka sasa najiuliza, lakini bado sipati jibu. Kitu gani kiliwafanya polisi kuvamia na kuwapiga mabomu Waislamu waliokuwa pale Mbuyuni?Katika kutafakari, nikasema labda ni kutokana na yale yaliyosemwa na Masheikh waliopata fursa ya kutoa nasaha. Hata hivyo kwa vile nilikuwepo, nilisikia mwenyewe kilichosemwa,sio maneno ya kuambiwa,bado nashindwa kukubali kwamba hiyo ndiyo ilikuwa sababu.Wa l i o p a t a f u r s a y a kuzunguza walikuwa watu wawili, Sheikh Farid na Ustadh Suleiman. Ilikuwa asimame Sheikh Msellem baada ya Sheikh Farid, lakini ile anakaa tu Farid, Mvua ya mabomu ikaanza.Sheikh Farid aliongea mambo mawili tu. Kwanza
alisema kuwa wanajitahidi katika yale wanayosema k u y a w e k a p i a k a t i k a maandishi maana baadhi ya watu wamekuwa wakipotosha.Akatoa mfano wa Mwakilishimmoja katika Baraza la Wawakilishi ambaye alidai kuwa Uamsho wanawahimiza watu wakatoe maoni katika Tume ya Katiba na waseme kuwa hawautaki muungano.Akasema, wao wanasema na wanachofanya ni kutetea haki ya Wazanzibari, kutetea
heshma ya Rais wa Zanzibar kama Rais wa nchi. Kwamba w a t u w a k a t o e m a o n i ambayo yatawahakikishia Wazanzibari haki yao ya kuwa na nchi huru na serikali yenye mamlaka kamili (Sovereign
State).Jambo la pili akaeleza kwa ufupi ni kwa nini wanaungana na Waislamu Tanzania Bara kukataa zoezi la sensa ya watu na makazi mpaka kipengele cha dini kiinginzwe. Hoja alizotoa ni zilezile ambazo zinatolewa na Waislamu Bara. Binafsi sikusikia neno lolote ama linaloweza kuitwa kuwa ni tusi, kutukana au la
uchochezi.Ustadh Suleiman ndiye aliongea kwa muda mrefu kidogo na ndiye aliyeanza.Yeye alizungumzia mambo matatu: Kwanza alieleza ni kwa nini wameamua Waislamu kufanya dua ya peke yao kuliko kungoja ile ya kiserikali ambayo hukusanya Waislamu, wanasiasa na Wakristo. Akasema, katika dua hiyo ya watu wa imani tofauti, kuna wanaoanza kwa kumkufuru Mungu.Akatoa mfano kwa Wakristo ambao huomba kwa jina la Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.Katika ufafanuzi wake akanukuu aya ya Qur’an isemayo: “Na (makafiri)h u s e m a : “ ( M w e n y e z iMungu) Mwingi wa rehma amejifanyia mtoto. Bila
shaka mumeleta jambo lichukizalo kabisa (kwakusema hivyo). Zinakaribia mbingu kutatuka kwa (tamko)hilo na ardhi kupasuka na vipandevipande. Kwa kule kudai kuwa (MwenyeziMungu) Mwingi wa rehema ana mtoto.) (19:88-91).Ndio akasema, itakuwaje t u k a e m a h a l i a m b a p o yanasemwa maneno ambayo
mbingu zinakaribia kuanguka k w a u z i t o w a d h a m b i inayotokana na maneno hayo,kisha tunanyanyua mikono tunamwomba Mwenyezi Mungu awarehemu maiti wetu. Akatoa mfano wa kibinadamu, kwamba jaaliya mtu kaja nyumbani kwako akakunasa kibao au akakupiga bakora safi, kisha anakuomba maji ya kunywa. Ni katika kuzingatia hayo akasema kuwa wao waliona ni bora Waislamu kufanya dua ya peke yao.
Na hili ndilo alilofanya pia Rais Dr. Ali Mohamed Shein katika swala ile iliyoongozwa na Mufti Sheikh Swaleh Omar Ka’bi pale Masjid Mushawwara,Muembe Shauri. Hapana shaka katika waliokufa wapo pia Wakristo, lakini mara hii serikali haikufanya Dua ya mseto w a Wa i s l a m u n a Wa k r i s t o.Walifuata nyayo z a Wa i s l a m u waliokusanyika Masjid Mbuyuni Ijumaa iliyopita.Jambo la pili alilozungumza n i k u o n y e s h a jinsi viongozi w a s e r i k a l i wanavyohusika na majanga haya ya kuzama meli na watu kupoteza maisha. Alisema,watu wasikimbile katika Qadari y a M w e n y e z i M u n g u.W a s i p e l e k e
l a w a m a k w a A l l a h , b a l i w a t i z a m e kwanza, iwapo hawana mchango k a t i k a j a n g a h i l o ? A l i t o a mfano wa mtu kuacha mlango w a z i h a l a f u unatawakal.K a t i k a uchambuzi wake mdogo akasema k u w a a n a o n a kuna uzembe.Kwamba taasisi z a s e r i k a l i h a z i w a j i b i k i
ipasavyo. Akatoa mifano ya meli mbovu ambazo h u r u h u s i w a k u f a n y a k a z i wakati vyombo vya usimamizi vipo. Lakini pia akazungumzia uzembe kwamba b a a d a y a a j a l i k u t o k e a h a p a k u w a n a u h a r a k a w a vyombo husika k u p e l e k a h u d u m a z a uokozi. Vyombo vya uokozi vilikwenda
takriban masaa matatu baada ya tukio. Akasema kuwa hata pale walipokuja watu binafsi wazamiaji wakataka wapelekwe kwenye tukio,wakasaidie kuokoa watu,waliambiwa vyombo havina mafuta. Na hili limesemwa n a k u t h i b i t i s h w a n a waokoaji wenyewe. Ndio alipofika hapo akasema, hivi wangeambiwa kuna meli inaondoka imebeba karafuu za magendo, wangesema vyombo havina mafuta? Na
mbona magari ya kuwavamia Uamsho hayakosi mafuta hata siku moja! Mbona magari yao
(wakubwa) hatujaambiwa kuwa yanakosa mafuta?Ila mafuta ya vyombo vya kuokoa watu, ndiyo kila wakati hakuna mafuta. Lakini pia akasema kuwa katika jambo linalozua maswali mengi yasiyo na majibu ni
pamoja na hili: Kwamba m e l i i m e z a m a e n e o l a Tanzania Bara, kwa nini havikuja vyombo vya uokozi kutoka Tanzania Bara? Na hili alilisema akinunukuu katika yale wanayozungumza na kuhoji watu mitaani na watu waliohusika na uzamiaji kuokoa watu na kuopoa maiti.Lakini akasema pia kuwa hakubaliani na hoja ya serikali kwamba haina fedha za kununua meli kubwa na mpya ambayo ingesaidia kuondoa tatizo la usafiri kwa Wazanzibari.Kwa msisitizo kabisa akamuelekea Rais Jakaya Mrisho Kikwete na Rais wa Zanzibar Dr. Shein akiwakumbusha kuwa kwa mujibu wa Dini wanayoifuata,yaani Uislamu, mtu akiuwa
mtu mmoja ni sawa na kuuwa watu wote. Kwa hiyo, waone umuhimu wa kuwawajibisha wale wanaofanya uzembe na wale wasiowajibika katika nafasi zao hadi kusababisha vifo kama hivi vya ajali ya meli. “Msiwafanye watu dagaa tonge”, alisema msemaji akimaanisha kuizindua serikali kujali maisha ya watu.
Akaenda mbali zaidi kwa kusema kuwa kwa jinsi hali inavyokwenda, itafikia mahali watu watachoka. Watatoka mitaani kama serikali inataka iwauwe wote. Wabaki wao wenyewe viongozi wa serikali na wake zao asibakie mtu wa kuwabughudhi.Binafsi naamini kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohammed Shein amesikia kilio cha Ustadh Suleiman na Waislamu wote ndio maana
amekubali ombi la Waziri Masoud kujiuzulu. Ingekuwa alichofanya Ustadh Suleiman Dua ya kuhitimisha, hapo ndipo vijana wa Nchimbi w a l i p o v a m i a . G h a f l a zilionekana gari za FFU zikivamia eneo hilo na k u a n z a k u v u r u m i s h a mabomu. Kutokana na kizaa zaa hicho,watu walianguka na kukanyagana wakiwemo w a n a w a k e n a w a t o t o.Wachache waliobaki kutaka kujinusuru hapo hapo ndani ya msikiti walikuta kuwa napo hakukaliki kwa sababu ya moshi wa mabomu.Kutoka eneo la Msikiti wa Mbuyuni, polisi walianza kuranda mitaani na kupiga mabomu ovyo, hali iliyowatia m o r i n a k u w a c h e m s h a vijana mitaani nao wengine wakaanza kuchoma moto matairi barabarani. Nikitokeameneo la Mbuyuni, nilipita vichochoroni hadi kutokea e n e o l a M a s j i d S a l a m nakutembea kando kando ya barabara kuelekea Michenzani.Hapo nikakuta FFU wakipita na gari zao huku wakipiga mabomu ovyo. Kwa hakika
ilikuwa vigumu mtu kujua nini kilikuwa kikiendelea. Watu wanapita mitaani, wengine wapo katika sehemu zao za biashara na katika makazi yao wanaendelea na shughguli zao, mara zinapita gari za FFU wanarusha mabomu. Hali hiyo iliendelea mpaka usiku wa manane hali iliyosababisha watu wengine kushindwa kabisa kutekeleza ibada yao ya Tarawehe na Qiyamul laili.Wakati napita mitaani,nakutana na watu wanalaani.“ T u m e w a f a n y a n i n i ?Tumepotelewa na ndugu zetu na mpaka hivi sasa maiti hawajapatikana, tunapigwa
mabomu. Tumekosa nini?“Msiba haujamalizika wanatupiga. Tumefiwa,tuna majonzi, wengine hata maiti hatujapata, tunapigwa.Haya ndiyo (Rais) Kikwete aliyokuja kutuletea! Haya ndiyo Waziri wake Emmanuel
Nchi aliyokuja kutuletea!K u m b e z i l e s a l a m u n a masikitiko ilikuwa sawa machozi ya mamba.”“ H a t u t a k i c h o c h o t e,unasema hivi sasa hatutaki chama chochote, sisi sote  t u n a k i m b i l i a U a m s ho,
tumechoka.”Hiyo ilikuwa kauli ya msafiri mmoja katika boti ya Kilimanjaro 2 iliyoondoka Zanzibar Jumamosi saa moja asubuhi kwenda Dar es Salaam.Na kwa hakika haya ndiyo yalikuwa mazungumzo katika boti hiyo kila mmoja akieleza kwa namna yake lakini ujumbe ukiwa mmoja: kuwa watu wamechoka. Hawathaminiwi.W a n a d a n g a n y w a .Wanaonewa. Wanahujumiwa na kudhalilishwa.Haya ndiyo aliyovuna M h e s h i m i w a Wa z i r i Emmanuel Nchimbi kwa ule ‘ubani’ wa mabomu kwa wafiwa Zanzibar pale Masjid Mbuyuni.Ipo kauli ya Qur ’an kwamba mengi ya majanga yanayowakumba wanadamu,wanayachuma kwa mikono yao. Ubani huu wa mabomu kwa Waislamu wanaoswalia maiti na kuwaombea Dua, ndio unayowafikisha Wazanzibari kuwaona viongozi wa Serikali ya Muungano Tanzania kama maadui wa Wazanzibari. Na hii huzidi kupandisha lile joto la kutaka nchi huru yenye mamlaka kamili.

ZANZIBAR ISHAKUWA SYRIA KWA SABABU HATUNA RAISI


Siku ya tarehe 20 july jumuiya ya uamsho iliamua kufanya sala ya maiti na dua maalum kwa ajili ya kuwaombea marehem waliofariki katika ajali ya kuzama kwa meli ya mv skigat karibu na eneo la kunduchi linalijuilikana kwa jina la fungu yasini, ambapo watu kadhaa walifariki, sala na dua ilifanyika katika msikiti wa mbuyun karibu na kiwanja cha mchezo wa mpira  wa miguu.
baada ya kumaliza jukumu hilo la ibada ya sala  na dua jumuiya ikaamua kutumia haki yao ya kimaumbile na kikatiba kuzungumza maneno machache yaliojikita katika hoja ambazo zina mashiko ya msingi ambayo ni haki ya  MZANZIBAR katika kuchanganua mambo muhimu yasio na majibu wala ufumbuzi wa hakika au wakudumu katika jamii yetu huku wakiwa katika hali ya amani kwa muda wote.
Ilipoendelea hali hiyo ghafla jeshi la polisi lilivamia na magari yapatayo sita yakiwa yamejaa askari polisi, mawili yakumwaga maji ya sumu yenye kemikali ya kuwasha  na moja iliyobeba majibwa na hatimae kuanza kutumia nguvu kubwa kuwahujumu  na kuwafanyia unyama mkubwa wananchi wasio na hatia
UNYAMA ULIOFANYIKA
1-Kuwaathiri kwa makusudi raia  wasio na hatia ndani ya majumba yao na kupelekea kuwahujumu vibaya watoto wadogo wa umri wa miaka 2,3,na 4, isitoshe wakawapiga  na kuwatishia kuwauwa wanawake na vijana wadogo wasiotambua chochote.
2-Mtoto mdogo mwenye umri wa siku kumi alihujumiwa na kuathirika vibaya uwezo wake wa kupumua kwa muda wa siku kadhaa.
3- vijana wa kiume walipigwa mateke ya nguvu na maaskari waliovalia viatu vizito, na wengine walipigwa maeneo ya kichwani kwa kutumia tako la bunduki.
4-Msikiti wa mbuyuni waliuchafua kwa kuumwagia maji ya najis,milango yalivunjwa madirisha,baskeli za raia wasio na hatia zilichukuliwa bila ya sababu ya msingi huu ni wizi na hati hawa ni askari. silaha zilipigwa kwa makusudi ndani ya majumba ya chini na ghorofa na kupelekea kuhatarisha kuwaka moto.
SHERIA  NA UHURU WA RAIA
Katiba  ya jamhuri ya muungano ibara ya 18. kila mtu
1-Anao uhuru wa kuwa na maoni  na kuelezea fakra zake.
2-Anayo haki ya kutafuta, kupokea na kutoa habari habari bila ya kujali mipaka ya nchi.
3-Anao uhuru wa kufanya mawasiliano na kutoingiliwa kati mawasiliano yake.
4-Anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbali mbali muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia kuhusu masuala muhimu kwa jamii.
 KATIBA YA ZANZIBAR, ibara 18.(1) bila ya kuathiri sheria za nchi kala mtu yupo  huru kuwa  na maoni yeyote na kutoa nje mawazo yake , kutafuta, kutoa habari na dhana kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia una uhuru wa mawasilano yake kutoingiliwa kati.
KWA HIYO WASHENZI HAWA WA SHEINI WAMEVUNJA KATIBA ZOTE MBILI.
MUONGOZO WA HAKI ZA BINAADAMU KWA POLISI
1-Kila mtu ana haki ya uhuru wa kufikiri na kujieleza, uhuru wa kujielezea ni muhimu kwani bila ya uhuru huo uhuru wa kufikiria hauna maaana.
2-kila mtu ana haki ya uhuru wa kufanya mikutano na watu wengine na kujumuika kwa amani.
3-Ni wajibu wa jeshi la polisi kuheshimu utu wa mtu na kusimamia na kuenzi haki za binaadamu za kila mtu.
Baada ya kuona sheria hizo na matukio yalivyotokea  ni wazi kwamba pametokea ukiukwaji mkubwa wa sheria ambapo inawezekana ulifanywa kwa makusudi kutimiza malengo fulani yalokusudiwa.
Kwa hivo waziri useyekuwa na wizara maalum Ali M Sheini unatakiwa uwe shahidi kwa wananchi mbele ya MOLA wa mbingu na ardhi dhidi ya uonevu na dhulma inayotendeka katika ardhi ZANZIBAR, inaaminika ya kwamba labda  yeye hahusiki na unyama huu ila baada ya hawa washenzi kufanya hivi si sio mara ya kwanza utawachukulia hatuwa ngani..? au utanyamaza tu kwa kuwafurahisha mabwana zako wa tanganyika.pia kuna kila dalili kwamba unyama huu unatekelezwa na Serikali ya Tanganyika.
Hivyo ni vyema ikaeleweka kwamba kwa shaka hiyo hatuna sababu kwanini
tusipate shaka ya kutokua na imani na KAMISHNA WA POLISI ZANZIBAR, INSPEKTA JENERAL WA POLISI na WAZIRI WA MAMBO YA NDANI.
Kwa hivo hakuna sababu ya kuiepuka tabia ya kimaumbile ya kukaribia kukosa uvumilivu na uonevu uliokithiri kwa raia wasio na hatia, hivyo jeshi la polisi lifate sheria kwani harakati za kupigania haki ya jamii hazatazimwa kwa nguvu za mabomu au maji ya muasho kwa hiyo harakati za haki zitasimama pale wanaostahiki haki kupata haki yao.
UBAGUZI WA KIDINI
Chakusikitisha ambacho kiko hadharani ni ubaguzi wa kidini ulioo ndani ya jeshi la polisi katika utendaji wake kwasababu haijawahi kutokea hatasiku moja kufanya kitendo cha kuvamia KANISA kwa kufanya hujuma kama hizo.Ajali na matukio ambayo yalisababisha kuathiri kwa makanisa Serikali ilitoa tamko kali na ilifidia uharibifu huo uliofanywa  na jeshi la Polisi na huku tukimuona Waziri mkuu  MIZENGO PINDA akitetea makanisa ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano.
WAISLAMU wanajiuliza hivi waziri huyu anatumikia KANISA Tu..?
Ni jambo lakushtua na kushangaza jinsi unyama wa jeshi la Polisi walioufanya dhidi ya WAISLAMU katika maeneo yao ya makaazi na ibada ni kuona serikali zote mbili zimekaa kimya, hakuna tamko wala kemeo lolote dhidi ya jeshi la polisi hii inatuthibitishia sisi kuwa serekali zote mbili ni serekali za kanisa.na ndio maana serekali haikeme kupingwa mabomu misikiti na kunajisiwa na maji ya muasho na majibwa na polisi kuingia na viatu misikitini serekali zote kimya maana ni serekali za kanisa kisha munasema SEREKALI HAINA DINI WANAFIKI WAKUBWA.hata shein waziri asiyekuwa na wizara maalum alikemea na kuja kwenye TV na kurupoka mpaka anatokwa na kipovu cha mdomo ila sasa misikiti inanajisiwa kimebana kimya kama sio unafiki nini ..? Jumla ya watu zaidi ya 50 walikamatwa na wengine walitafunishwa mbwa, walipigwa na kupasuliwa vichwa, nakuathiriwa  vibaya kwa kipigo hicho, na kipigo kiliendelea mpaka ndani ya kituo cha polisi MADEMA, juu ya unyama huo uliofanyika hakuna mtu yoyote aliepatikana na hatia au kupelekwa katika vyombo vya sheria isipokua dhulma na unyanyasaji wa hali ya juu ndivo vilivotawala;;;;;
                 WAZANZIBAR WAMECHOSHWA NA MUUNGANO KWA NINI HAWAACHIWI WAPUMUE……………………………………….?
       WAZANZIBAR MNATAKA NINI?
     MNAUTAKA MUUNGANOOO?

JAHAZI LAZAMA LILILOKUWA LIKITOKEA PEMBA JE WAZIRI MPYA ATAJIUZULU PIA...?


Mtoto Isack Hamis Suluhu (5), amefariki dunia na wengine saba wamenusurika baada ya jahazi walilokuwa wakisafiria kutoka Pemba kwenda Unguja kuzama katika Bahari ya Hindi.
Tukio hilo limekuja wiki moja tu tangu boti ya MV Skagit ilipopinduka na kuzama katika mkondo wa dar es salaam na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 100.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kusini Pemba, Hassan Ali, alisema jahazi hiyo inayojulikana kama Safina ilizama katika eneo la mkondo wa Nungwi juzi jioni.
Alisema kati ya walionusurika mmoja hali yake ni mbaya na amelazwa katika hospitali moja mjini Pemba na kwamba wengine saba wakiwemo watoto wawili hali zao ni nzuri.
Kamanda Ali alisema chanzo cha ajali hiyo ni kujaza mizigo na abiria wengi kupita uwezo wake na kwamba watu hao kwa kuwa ni wazoefu na shughuli za uvuvi walijiokoa wenyewe kwa kuogelea.
Kumekuwa na mfufulizo wa matukio ya meli na jahazi kuzama katika Bahari ya Hindi hali ambayo inatishia usalama wa maisha ya watu wanaotumia usafiri wa majini.na hasa hasa uzembe uliyo kuwa mkubwa ni kujaza vyombo hivi kupita kiasi.kubwa zaidi ni kampuni hii ya mapinduzi zanzibar kuwa haijali kuchunguza chombo kipi ni cha abiria na kipi ni cha mizigo imekuwa kila chombo sasa ni abiria na mizingo na kujazwa kupita kiasi lawama zote tunazitupia hii kampuni ya mapinduzi daima maana sio serekali hii ni kampuni tu.

Thursday, July 26, 2012

BAKH-RESA MFANYA BIASHARA ANAMILIKI MELI NA BOTI ZA KISASA SEREKALI YA ZANZIBAR HIMILIKI HATA BOTI YA DAGA-UJUHA WA MAPINDUZI DAIMA


MAKAMO MZEMA WA RAISI ATI ANAKWENDA NYUMBANI KWA KABACHORI KUPIGA MAGOTI KUSAIDIWA KUKOPESHWA MELI TOKA NENDA NCHI ZA NJE UKAONE MELI NA MABOTI YA ABIRIA ACHENI UJINGA NA UZUKA UNA KITU HICHI UNAKWENDA KWA KABACHORI ATAKUPA NINA KAMA SIO DENGU CHEE BAJIA CHEE HATUNA VIONGOZI ZANZIBAR TUNA MAJUHA NA WAHUNI BASI WAKUUWA WATU KWENYE MISIKITI NA SI ZA UCHANGUZI LAKINI VIONGOZI HATUNA KABISA.
Baada ya kujiuzulu kwa alie kuwa Waziri Mawasiliano na Miundo mbinu Mh. Hamad Massoud inaonekana wazi kwamba amewajibika kisiasa.Kwa mara ya mwanzo Zanzibar tumeshuhudia kiongozi wa ngazi ya juu kuchukua uamuzi mgumu kama huo. Iwavyo na iwe ikiwa kaladhimishwa au yeye mwenyewe ameamua ,ngoma imekuwa ngumu basi na iwe hivyo cha msingi ni kwamba Waziri huyo hayupo tena katika wadhifa wake, hili ni jambo la msingi kisiasa.Jee kwa sasa ni ipi hatma ya nchi yetu baada ya majanga yaliotokea ?
Nimesema kisiasa nikiwa na maana kwamba hapa kilichofanyika sio kuboresha au kutengeneza bali ni kiini macho tu,udhaifu na ukosefu wa utendaji upo pale pale,Serikali yetu ni kampuni ya Mapinduzi LTD.Naamini kuna watu wamefurahi kuundoka kwa Mh Hamad ni sawa na ndivyo ilivyo kimsingi lakini tujiulize jee hili ndio suluhisho la Wizara hii nyeti ? Tusisahau kwamba Serikali imekuwa kama  kampuni kwani suala la utendaji sio kigezo kwa  mhusika isipokuwa kauli ya tajiri na wapambe wake ndio wenye uwezo .
Wananchi walio wengi  wanashindwa kuelewa kwamba Zanzibar hatuna Serikali bali tuna kikundi cha Wahafidhina ambao wanatumiliwa na kuifanya Zanzibar kama kampuni ya Biashara na sio Serikali. Kampuni hii ambayo huendeshwa kwa njia ya majungu,chuki na ubinafsi ndio unaowafanya Wazanzibar hadi leo kuwa katika hali duni ya umaskini na unyonge usio kikomo.Viongozi wetu wanachojali ni kuvimbisha matumbo yao,huku wananchi wanateseka na wengine kupoteza maisha yao kwa uzembe ambao inawezekana kuepukika.
Hapo zamani Kampuni hii ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilikuwa ikitumia kila mbinu kuwatesa Raia wake kwa kisingizio cha siasa, lakini baada ya joto la kisiasa kuwa kubwa na Wananchi wanaokandamizwa kuwa wengi, Kampuni hii imekuja na mbinu mpya sasa kuwapunguza Raia wake kwa Majanga ya uzembe na utendaji mbovu. Majanga haya ya uzembe yakitokea moja kwa moja hupelekewa Muumba kwamba yeye ndie alietaka hilo litokee.Lakini iman hizi kwa watawala wetu sio kweli,ukweli ni kwamba huko ni mafichoni kwao ili watu washindwe kujadili,waone hii ni kudra ya Muumba, lakini wanasahau kwamba wanajificha gongo nje,kwani huyo wanaemtupia lawama ndie huyo huyo wanaemtilia moto nyumbani kwake na kunajisi (Misikitini)
Inashangaza kuona kwamba Viongozi wengi wa Serikali yetu ni watu ambao hawana”VISION” yeyote ya uongozi wala utendaji,walaji rushwa,wazembe na viongozi ambao ni mbumbumbu, nashindwa kuelewa kwamba hawana Elimu lao ni  kasumba tu na ujinga walionao hawa Wahafidhina,hili nashindwa kulielewa.Mara nyingi ushabiki wa Serikali yetu hujipanga katika dhulma kwa kuwasulubu Wananchi wake bila kuwa na kipande cha huruma na ubiadamu na kusahau hata ule wajibu wao kama Viongozi.Inashangaza kuona Jeshi la polisi linawashambulia raia wake bila makosa lakini hata kuvamia nyumba za ibada wakati mwengine,huu ni uhuni si vyenginevyo.
Nasema hivi kwa sababu Nchi hii Muasisi wake Hayati Karume hakuwa msomi lakini aliiongoza nchi hii kwa ufanisi mkubwa tu,licha ya kufanya mabaya kwani hakuna mkamilifu lakini mazuri mengi alioyafanya hadi hii leo yanaonekana. Ukweli ni kwamba alioyafanya Karume hakuna hata kiongozi mmoja hadi hii leo alieyafanya hata wakia wa mazuri yake.Leo hii tunaambiwa kwamba Zanzibar tunaongozwa na Madokta wenye PHD lakini Serikali hiyo inashindwa hata kujua wapi pakununulia licha ya meli hata boti ya mtumba.Raia zake kila kukicha wanaliwa na kina na kiza  kinene cha mawimbi makubwa ya bahari na kuwa kitoweo cha samaki.
Nchi hii imegeuzwa kama kampuni binafsi ya Wahafidhina,inashangaza kumuona Makamo wa pili wa Serikali ambae ndio kiini cha utendaji katika Serikali yetu anatafuta meli kwa niaba ya Serikali na kumfuata mtu nyumbani kwake mambo haya viereje,hii inashangaza na ni aibu kweli.Hivi huu ni mtindo gani wa uendeshaji wa Nchi,inakuwaje Waziri anatoka mguu mosi ,mguu pili mpaka ”local shop” anaenda kununua vifaa vya uokozi kwa kutumia fedha ya serikali kiholela kama hivyo?Halafu anakuja anasema Serikali imenunua hichi na kile, hata hiyo kampuni ya mtu binafsi lazma kuwe na utaratibu wake.Hapa rushwa ndipo inaponukia na kuibiwa kwa Wananchi.
Leo hii napata picha halisi kwamba vile watani wetu wa jadi Watanganyika wanaposema kwamba Zanzibar ukivunjwa Muungano wata shindwa kujiongoza inawezekena kuwa na ukweli fulani kama viongozi wetu watakuwa ni hawa Wahafidhina akina Balozi Seif na wenzake akina Vuai na Borafia.Mimi nobe,basi nikiwa na nia ya kununua meli kwa ajili ya biashara yangu binafsi sio serikali basi lazima nifanye uchunguzi wa kina siwezi kumfuata mtu tu ”private” kiholela holela kama anavyofanya Mh,makamo wa Rais ambae yeye ndio kitovu cha utendaji katika kampuni hii ya Mapinduzi ya Zanzibar.Hii ni ishara mbaya na mwisho wake sio mzuri kwa maslah ya nchi.
Angalieni Watanganyika ni karibuni tu Mizengo pinda alikuwa korea kufuatilia utengenezwaji wa meli yao ya kufanya utafiti wa Mafuta kwa Tanganyika ,vile ndivyo anavyotakiwa Waziri Mkuu utendaji wake.Sisi Wazanzibar tunakaa na kutupiana lawama pamoja na kupikiana majungu. Serikali haiwezi kununua vitu kama vile kariakoo au Darajani,kunahitajika uchambuzi wa kina sio kwenda kwa Magabachori na kuwaangukia miguuni,eti tunataka mutukopeshe meli, huku ni kujidhalilisha kiserikali na Wazanzibar.Wahafidhina kubali matokeo,wapeni watu wenye uchungu wa Zanzibar waendeshe nchi yetu,mumeshindwa kuongoza,uongozi sio majungu ni utendaji na uwajibikaji.
Haingii akilini kuona kwamba Serikali inashindwa na mfanya biashara mdogo tu ,eti Serikali mzima inashindwa kununua meli yake basi hata boti , basi kuna haja gani ya kuwa na Serikali na mashangasha kibao pamoja na ving’ora badala yake tukamchagua Bakh-resa kuwa Raisi wetu yeye peke yake tukaachana na hawa wakuu wa mikoa manake wameshindwa kutuongoza.Leo hii mfanya biashara anamiliki,boti za kisasa,viwanda vya kila aina lakini Serikali wao ni kuwapiga raia na kuendeleza ujinga wa Mapinduzi daima,hivi jamani hamufikiri basi hata macho hamna. Tumechoka na kampuni hii ya Mapinduzi

MELI TATU ZAFUTIWA LESENI YA KUFANYA KAZI NCHINI ZANZIBAR NA KUPEWA MWIZI MOJA KUONDOKA NCHINI HUMO


Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Usafiri wa Baharini Zanzibar Abdullah Husein Kombo
Mamlaka ya Usafiri wa Baharini Zanzibar imezifutia rasmi hati ya kufanya kazi Meli ya Mv.Kalama, Mv.Seagul na Mv.Sepideh kutokana na meli hizo kutokukidhi hali ya usalama wa abiria katika meli hizo. Aidha meli hizo zimepewa muda wa mwezi mmoja kuanzia leo kuhakikisha zimeondoka katika maeneo ya Zanzibar kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa dhidi ya wamiliki wa Meli hizo.
 Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Usafiri wa Baharini Zanzibar Abdullah Husein Kombo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Afisini kwake kuhusu hali ya usafiri wa baharini na usalama Zanzibar.
Amesema Mamlaka hiyo imefanya tathmini na uhakiki wa kutosha na kujiridhisha kuwa Meli hizo hazifai kufanya kazi katika maeneo ya Zanzibar jambo ambalo limepelekea kuchukua hatua za kufuta hati za kufanyia kazi meli hizo.
Amefahamisha kuwa sababu kuu zilizopelekea Mamlaka kufanya maamuzi hayo ni pamoja na uchakavu,umri wa meli hizo kuwa mrefu na kupata matatizo mara kwa mara katika safari zao.“Tnafanya operesheni kabambe hadi  meli zote ambazo hazina kiwango zimeondoka katika bandari yetu” alisema Kombo ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri baharini Zanzibar.
Kombo amefahamisha kuwa Sheria ya Mamlaka ya Usafiri na Bandari Zanzibar ya mwaka 2006 kifungu cha 17.1 inampa mamlaka Msajili wa Meli kuifuta meli yoyote ambayo itakuwa haikidhi usalama wa abiria.
Kufuatia sheria hiyo Kombo amesema watawataka wamiliki wa Meli hizo kuzirudisha hati za kufanyia kazi meli hizo ili waende kutafuta sehemu nyengine za usajili kinyume na maeneo ya Zanzibar.
Akizungumzia Meli ya Mv.Serengeti Kombo amesema wamelazimika kuiagiza meli hiyo kupunguza idadi ya abiria kutoka watu 800 hadi 350 na tani za mizigo kutoka 100 hadi 50  hadi pale ambapo watajiridhisha kutokana na hali ya meli hiyo ilivyo.
Aidha amegusia kuwa Kampuni ya Bakhresa italeta Meli kubwa ya abiria itakayofanya kazi zake Zanzibar ambapo pia Serikali ya Mapinduzi nayo iko mbioni kuhakikisha wanaleta meli inayokidhi mahitaji ya wananchi wa Zanzibar.

VIDEO-MRC-FREE PWANI PEOPLE FROM WAKOLONI WAUSI KENYA

PWANI SI KENYA PWANI SI KENYA PWANI SI KENYA
YALE YALE WANAYO FANYA MIJITI YA BARA MIPOLISI YA BARA
KULE ZANZIBAR KUWASHIKA MASHEIKH WETU NDIVYO WANAVYO
FANYA MIPOLISI HAYA YA BARA KUTOKA KENYA KUWASHIKA MASHEIK WA PWANI
NA SASA PWANI WANATAKA NCHI YAO WAPEWE TU KAMA NORTH SUDAN
I LIVYO WAPA WATU WA SOUTH SUDAN WATU WASHACHOKA KUTAWALIWA
NA NYINYI MIKOLONI MWEUSI YA KENYA TUNASEMA TENA PWANI SI KENYA PWANI SI KENYA PWANI SI KENYA.


VIDEO-MRC-ZANZIBAR SI TANZANIA.PWANI SI KENYA PWANI HATUTAKI TENA KUISHI NA MIJITU YA KENYA

MRC NI SIO CHAMA BALI NI WANANCHI WOTE WA PWANI WANAO DAI
INCHI YAO ILIYO SIGN NIWA KATIKA MKATABA WA KWANZA WA MFALME
KUWAPA WAENGERA BANDARI YA MOMBASA WAKATI HUWO HAKUNA KENYA
KISHA PIA BAADA YA UHURU WA KENYA RAISI KINYATA ALISAINI TENA MKATABA
NA WAZIRI KIONGOZI WA KWANZA NCHINI ZANZIBAR MOHAMMED SHAMTE KUWA AMUWACHIYE MOMBASA MPAKA 2013 SASA WATU WA PWANI HAWATAKI TENA KUWA NA WAKENYA WANATAKA NCHI YAO WAPEWE TU.


VIDEO-HIJABU NZURI LAKINI MNAFIKI MKUBWA NA ANASOMA HABARI ZA KINAFKI

JE NI UAMSHO NDIO WALIO KWENDA KWENYE KAMBI ZA JESHI
LA POLISI KURUSHA MAWE..? AU NI POLISI NDIO WALIO
TOKA KATIKA KAMBI ZAO NA KWENDA KWENYE MSIKITI
WA WAUMINI WAKISLAMU NA KUPIGA MABOMU NA KURUSHA
MAJI YA MUASHO..?
SOMA HABARI ZA UKWELI HII DUNIA YA UKWELI WACHA KUENDEKEZA
UKEREKETWA DUNIA ISHABADILIKA BORA UKATAE NA WAKUFUKUZE
HAPO TVZ KULIKO KUSOMA HABARI ZA UWONGO NA UNAFIKI


ASP NDIO CHAMA CHA WAZANZIBARI CCM ILILETWA NA NYERERE KUWAPINDUWA WAZANZIBARI

Mansour ‘Kaz buti’ – sisi tuko nyuma yako, si leo wala jana miaka mingi tuko nyuma yako.
Ila ujue kuwa wewe sio wa mwanzo katika kutaka kunyanganywa kadi ya CCM wala wewe sio wa mwisho kunyanganywa kadi ya CCM kwa hivyo usiwe na wasi wasi kwanza hatunahaja ya CCM,CUF wala chama chengine chochote sisi wazanzibari chama chetu sasa ni ZANZIBAR HURU ndio chama chetu sasa.nataka nikukumbushe watu walio nyanganywa kadi kabla yako.                                                                    Aboud Jumbe alinyanganywa kadi, akafukuzwa na hatimaye kudhalilishwa kama sie aliyekuwa Raisi wa NCHI hii. Mpaka sasa anaishi maisha ya idhlali kubwa.
Ramadhan Haji Faki, waziri kiongozi mstaafu, kadhalilika, amefukuzwa ndani ya chama na kudhalilishwa.
Wakafuata akina Maalim Seif na timu yake walifukuzwa, walinyanganywa kadi, na walidhalilishwa na isitoshe  wakafungwa na jela, just kwa sababu wamedai haki ya Zanzibar.
Walifuata wengine hapo, akina Hafidhi Suleiman na wenzake pia.
Akafuata Marehemeu Idrissa Abdul Wakil – raisi wa zanzibar/ pia alitakiwa ajiuzulu ama ajiuzulu au atauzuliwa. Yeye walimheshimu kidogo kwa sababu ya utu uzima na alikuwa mtu alimu mzuri. Naam, alijiuzulu at the airport wakakti anakwenda Ujerumani umesikia wapi mambo haya katika ulimwengu huu ni hapa zanzibar tu.                                                                                                                                Wengine kuna foleni kuwa ya wazanzibari waliofukuzwa kazi, kushushwa vyeo, kufungwa n.k just kwa sababu wamehoji Muungano, na wamedai haki ya Zanzibar.
Zaidi ya yote – juzi tu: Hassan Nassor Moyo amesema wazi wazi kuwa sera ya serikali tatu – si ya leo wala jana, enzi zao wakati wa Karume Sr. walidai na walaiandika mfumo waserikali tatu: then Karume alinuna. Sasa, bado nini tena.mimi nataka kuwatowa watu tongo za macho kuwa CCM sio chama cha wazanzibari bali CCM ni cha cha kuwapinduwa wazanzibari kwa sababu kama kingelikuwa ni chama cha wazanzibari basi kigelikuwa mstari wa mbele kuilinda zanzibar na kudai haki za zanzibar.lakini mtu yoyote namanisha mtu yoyote hata huyu kisheini leo hii akisema tu kuwa zanzibar lazima iwe na haki zake kamili basi atauzuliwa kama karatasi ndio maana akasema simuogopi mtu na muungano nitaulinda maana anajuwa nini kitamkuta.sasa CCM ni ya wazanzibari kweli au CCM kazi yake ni kuwapinduwa wazanzibar..? chama chetu sisi kilikuwa ni ASP baada ya kunganishwa vyama hivi cha ASP na TANU ilikuwa kwisha habari yetu.ilikuwa tayari wazanzibari tushapinduliwa na mpaka leo tuko chini ya ulizi mkali na ndio maana hakuna mtu anaye thubutu kusema kwii akisema tu kanyangwanywa madara na kadi kama bahati yako mbaya unaishia jela au unatupwa kati maisha ya idhalali kabisa kwa hiyo wazanzibari tuamke na tusema kweli kuwa CCM sio chama chetu ni chama kilicho letwa kuja kutupinduwa chama chetu ni ASP tukirudishe.

laa sivyo mambo ndivyo kama tunavyo yaona lazima ujichanganye na wahafidhina wasio taka maendeleo ya nchi wao wakotayari wapewe hivyo viposho vya laki tatu kila wiki kuliko kubadilika na kufikiria fikra mpya nini tufanye ili nchi yetu inuke na iwe nchi nzuri watu wanakula vizuri wanaishi vizuri polisi wanadabu ya kuhishimu rai na maji taa madawa na hata kusafiri nchi za nje na huku tunajulikana kuwa hawa ni wazanzibari. hayo wao hawayaoni maana wana fikra mgando kama ulivyo sema mansoor kwali kabisa wao wanafikiri maishi zanzibar ibaki kama ilivyo kisha sherehe za mapinduzi zeji mapinduzi daima mapinduzi daima mumempinduwa nani basi..? mazumbukuku nyie masiki hawajuwi kuwa wao ndio waliopinduliwa na watanganyika yao yanawaende vizuri zanzibar imeka kama ina maradhi ya ukomaa wa vidole kila kukicha vinamumunyuka tu vidole. havikuwi huu sio wakti tena wakutishana huu ni wakati wa kuangalia maslahi ya wazanzibari kwa wote wote wote sote sote sote. sio wakati wa kusema sisi tulipinduwa haapa ujiga mtupu ulipinduwa nini kisahani cha chai walio pinduwa washakufa na wote wamekufa vifo vibaya sana sote tosome tusiwe wajinga na akila za kuwaza njia moja tu. tunatowa onyo kwa hao wanaojita wakereketwa kuwa wakiendele na tabia yao yakutia fitini ila wazanzibari tugawike tena basi wajuwe siku zanzibar ikiwa huru wao wahamiya bara kabisa maana tutawafungulia mashtaka ya kuwagawa wazanzibari hatutaki ubaguzi zanzibar.zanzibar moja watu wamoja sote tukinya mavi yananuka hakuna hata moja wetu akinya yake yananukia udi au viluwa hakuna chama cha ASP sasa ni wakati wake kirudi kiungane na UAMSHO tupate zanzibar yatu.

MANSOOR-SIMBA LIKINGURUMA MAFISI HUUFYATA MIKIA NA KUKIMBIA


Mweka Hazina wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar, Mansoor Yussuf Himid amesema yupo tayari kunyanganywa kadi ya chama hicho lakini hataregeza msimamo wake juu ya kuitetea Zanzibar katika Muungano. Kauli ya Mansoor imekuja siku chache baada ya chama hicho wilaya ya mjini kutoa maamuzi ya kuwataka viongozi wenye kupingana na msimamo wa chama kurejesha kadi za chama hicho au kuacha tabia hiyo mara moja.
Akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya Radio ya Ujerumani (DW) jana Mansoor alisema kamwe hawezi kuogopa vitisho vinavyotolewa na watu wenye kujipa madaraka na udikteta ambao hawataki mabadiliko wala mawazo tofauti.
Mansoor aliahidi kuendelea na msimamo wake katika kudai mabadiliko katika muundo wa Muungano na kusema kwamba msimamo wake hautabadilika licha ya vitisho vya baadhi ya Viongozi wa Chama hicho.
“Nimesema hayo tokea muda mrefu chama hiki kimetukuka na kina heshima na maadili yake ni baadhi ya watu wanataka kutuziba midomo lakini
Mimi sijasema leo nimesema tokea 2008-2009 juu ya msimamo wangu juu ya mfumo wa muungano na leo naendelea kusema tena hata ikipidi kunyanynganywa kadi mimi narejea tena kuwa mfumo huu wa serikali mbili sikubaliani nao na nitaendelea kusema ahivyo hivyo siwezi kubadilisha maoni yangu leo baada ya kuwa na msimamo miaka yote hayo” alisisitiza Himid ambaye ni Mjumbe wa NEC.
Aidha alisema Chama Cha Mapinduzi wilaya ya mjini hakina mamlaka ya kuitisha kikao na kutoa maamuzi kama hayo ambapo alisema ni watu wachache wenye nia ya kutaka kuwanyamazisha watu wenye maoni tofauti na wao.
“CCM wilaya ya mjini hawana mamlaka hayo, lakini pia hawana uwezo wa kutunyamazisha kwani CCM haijakataza wanachama wake kuwa na mawazo tofauti sasa nashangaa hao wanaosema sisi tumekiuka msimamo wa Chama ni msimamo upi maana mchakato wa katiba upo huru na kila mtu anatakiwa kutoa maoni yake” Alisema Himid.
Katika kuonesha kukasirika kwake na uamuzi huo wa kutaka kuwanyanganya kazi, Muweka Hazina huyo wa CCM alisema kwamba ni jambo la aibu kwa CCM Wilaya ya Mjini kufanya vitendo vya kibaguzi na vya udikteta kutaka kuwafunga midomo watu wasitoe maoni yao.
Alisema hakuna makosa kwa wana CCM kuwa na mawazo tofauti kwani kila mmoja ana haki ya kutoa maoni na kueleza msimamo wake na tabia ya kikundi cha watu kujiona wao ndio wenye mamlaka na wenye chama ni kosa na halipaswi kuachiwa.
Hao ni ni wabaguzi hawataki watu waseme ukisema unaonekana msaliti, hao ni watu wenye mawazo mgando hawataki kusikiliza fikra nyengine wanataka wanachosema wao ndio kiwe hicho hicho hilo haliwezekani na hatutakubali” Alisisitiza.
Hata hivyo alisema zama za kusema tunakwenda na fikra za mwenyekiti umepitwa na wakati na sasa jamii kubwa inakwenda na vijana amabo wanataka mabadiliko nchini hivyo aliwashauri wana CCM kuwaachia watu watoe maoni yao kwa uhuru kwani katiba tayari imetoa uhuru huo hivyo CCM hawawezi kuwa juu ya sheria.
“Hii nchi sio ya CCM peke yake hapa kuna CUF kuna Chadema na pia kuna vyama vyengine lakini wengine hawana hata vyama sasa hatuwezi kuendelea na watu ambao hawataki kuwa na mabadiliko wenye mawazo mgando …zama hizo zimeshapitwa na wakati wakati wa kwenda na fikra za mwenyekiti umekwisha” alisema Mansoor ambaye ni Waziri aisye na wizara maalumu.
Mmweka Hazina huyo ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, alisema kitendo kilichofanywa cha kutishiwa kunyanganywa kadi ya CCM na baadhi ya viongozi hao ni cha fedheha na kimekitia aibu Chama cha CCM mbele ya wana jamii.
Himid alisema yeye ametokana na mifupa ya Chama cha Afro Shiraz (ASP) hivyo suala la kuwepo kwa dhana ya wanachama wa madaraja ndani ya CCM halipo kwa kuwa Chama hicho kinaheshimu misingi ya haki za binadamu na kuwataka wenye kudhani kwamba wao ndio wana mamalaka zaidi kuliko wengine waache tabia hiyo.
Hivi karibuni chama cha mapinduzi CCM wilaya ya mjini kilitoa tamko la kuwataka wajumbe wa baraza la wawakilishi, akiwemo Muweka Hazina wa CCM Zanzibar, Mansoour na makamo mwenyekiti wa CCM Zanzibar kuacha mara moja kukiuka maadili ya chama chao kwa kuwa na mtazamo hasi dhidi ya muungano.
Jana akihojiwa na DW, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisikika akisema kwamba viongozi wanaokwenda kinyume na madili ya chama chao watatakiwa kwenda kujieleza katika vikao na iwapo watathibitika wamekwenda kinyume basi watanyanganywa kazi au kufukuzwa.
Nape alisema mwana yoyote CCM hawezi kwenda kinyume na maadili ya chama chake na iwapo atakuwa na msimamo mwengine usiokuwa wa chama hicho basi atatakiwa kuwasilisha maoni yake ndani ya vikao na iwapo maoni hayo wajumbe hawatayaridhia basi atalazimika kurejesha kazi ya chama hicho iwapo yeye hatokubaliana na msimamo wa kikao.
Akijibu suala hilo Himid alisema kuwa Nape hawezi kugawa matabaka wanachama wa CCM, wale wa Tanzania Bara na Zanzibar kwani wote ni wanachama wanahaki sawa mbele ya sheria na katika CCM.
“Sisi Watanzania hatuna uhuru, yeye amegawa kwa utabaka, sisi ni watu wazima tuna haki na uhuru,  Nape hawezi kutwambia sisi watu wazima kwamba tukasema anayotaka yeye, ule wakati wa ndio Mwenyekiti haupo kila mtu ana haki yake kutoa maoni na hata Tume ya Jaji Warioba inasema hivyo” Alisema Himid. Na kuongeza kwamba.
“Mimi naichukulia kuwa hii ni njama ya kutaka kuwaziba midomo Wazanzibari, hatujakiuka miongozo wala sheria tutaendelea kusema kutaka mabadiliko ya muundo wa Muungano, hii nchi asilimia kubwa ni vijana na vijana wanataka mabadiliko na hilo haliwezi kukwepwa” Aliongeza.
Licha ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Pius Msekwa mbali ya kueleza msimamo wa Chama hicho, lakini amesema wanachama wake hawafungiki kuwa na maoni na mitazamo tofauti katika mchakato wa katiba mpya.
“Mie nadhani kuna baadhi ya watu wana fikra za udikteta, haiwezekani twende kwenye kutoa maoni tukasema tunataka Serikali mbili kama ilivyosema CCM sisi ni watu wazima tuna haki zetu na tusichaguliwe la kusema na kwa nini tuzibwe au tufungwe midogo?” Alihoji.
Mansoor amesema msimamo wake kuhusu mfumo wa muundo wa Muungano utabakia kama ulivyo kutaka kuwepo kwa mabadiliko makubwa katika muundo huo kwani kwa muda mrefu kumekuwa na malalamiko kutoka Zanzibar ambayo hayapatiwi ufumbuzi kutokana na kuwepo kwa muundo dhaifu wa Muungano.
Alisema hakuna mtu mwenye nia ya kuvunja Muungano, lakini ni lazima kukawepo kwa Muungano wenye maslahi ambayo hautakuwa na kero na ndio maana wamekuwa wakitoa maoni ya kutaka mabadiliko ya muundo na sio kuvunja.
“Mimi pia nakubali muungano una manufaa, lakini sikubaliani na mfumo wa Muungano na ndio maana tunasema kwa mfumo huu sebu(sitaki)” alisema Mweka Hazina wa CCM Zanzibar.
Tokea kuanza kwa machakato wa katiba wazanzibari wengin wamekuwa na maoni ya aina mbili tofauti ambapo wapo wengine wakitaka muungano kama ulivyo uendelee na wengine wakisema wanataka muungano wa serikali mbili zenye mamlaka kamili na zenye kuirejeshea Zanzibar ya kuingia mikataba na nchi za nje na baadae kuwe na mkataba.

Wednesday, July 25, 2012

VIDEO-UKATILI WA MOHAMMED ABOUD NA VIP2 BALOZI ALI IDDI KWA KUWAULISHA WATU-HAWA PIA WAJIUZULU

HUYU NDIE MOHAMMED ABOUD
BAADA YA BALOZI ALI IDDI KUSITISHA ZOEZI LA KWENDA KUANGALI MAITI
MADAIVA NA WAVUVI HAWAKUKUBALI NA WAKAMUWA KWENDA TENA LEO NA
WAMEFANIKIWA KUPATA MAITI TENA NYENGINE TANO NA NYINGINE TANO KIZIWACHA ZIKIELEA MAANA BOTI NI DONGO HUYU JINA ALIVYO SIKIA TU KAJA HARAKA HARAKA BANDARINI ILA NINI KAFANYA NIKUJIONYESHA JUSO LAKE TU KWENYE KAMERA WASIKILIZE MADAIVA WANAVYO SEMA NA YEYEYUKO HAPO HAPO HASEMA OK NITAWAPA ILI MUZIDI KUOKOWA WATU 
HUYU MOHAMMED ABOUD NA BALOZI ALI IDDI PIA WAJIUZULU HAWA MAANA BALOZI NDIO ALIYE SEMA ZOEZI LISIMAMISHO NA HUKO YEYE AKUSANYA PESA ZA RAMBI RAMBI BONA HAKUSEMA PESA PIA ZISITISHWA..? 


VIDEO- UKATILI WA VIP2 BALOZI ALI IDDI NA MOHAMMED ABOUD. PIA WAJIUZULU

ONA WALIVYO WAKATA ROHO WANAWAKE NA WATOTO
KWA UZEMBE WAO WAKUTO WAJIBIKA KUWAOKOWA WATU
WALIPOKUWA WAKIZAMA SHEINI USIPO WAFUKUZA BALOZI ALI IDDI
NA MOHAMMED ABOUD TUTAJUWA HUOGOPI MTU ILA HAWA WAUWAJI
UNAWAOGOPA.


VIP2 BALOZI ALI IDDI NA MOHAMMED ABOUD MPAKA WAZANZIBARI WANGAPI WAAFE NDIO MUJIUZULU



Nimasikitiko makubwa kuona kwamba kwa kipindi cha mwaka tu watu wapatao 2000 wameuliwa kwa uzembe wamakusudi wa Upakiaji mbaya au Usajili wa Vyombo Vibovu hapa nchini zanzibar.
Nimatumaini yangu kwamba kila kilichotokea ktk Matukio haya mawili ya mv spicer na sasa mv skagit Hamadi Masoudi Ndie aliye laumiwa peke yake na lawama zote juu yake kama vile yeye ndie Waziri anaeshughulikia Maafa na Uokoaji wakati yakitokea Maafa. Wakati Wizara yake ni ya Usafiri na Miundo Mbinu lakini ndani yake kuna Idara ya Maafa.Sisemi kuwa yeye alikuwa abaki madarakani laa khasha ilaa kwa nini Balozi iddi seif na Mohammed Aboud wao wabaki madarakani..? ilipaswa na wao pia wajiuzulu maana hii ilikuwa ni kazi yao iko katika wizara yao.Kwa nini Wanuka DAMU WAUWAJI CCM Maskani na Watanganyika WAKOLONI WEUSI au Wazanzibari wengine Wamewanyamazia wahusika wakubwa wa Ajali hii..?Office ya Makamo wa 2 Balozi Iddi Seif  na Naibu wake Mohammed Aboud Mohammed ndio Viongozi ambao wanatakiwa wawe makini katika matukio ya Hatari au ajali. Wizara yao Ndio inayopanga mipango ya Uokoaji wa majini na Angani na Sio kukusanya Misaada ya Wafiwa nakutumia fedha hizo kichama na kulisha familia zao kama wanavyo fanya hivi sasa Balozi iddi na Mohammed aboud wanakusanya michango kama hawana akili vizuri.Leo hii tumeona jinsi Mh. Hamadi Masoudi alivyoshinikizwa ajiuzulu…Jee Mohamedi Aboudu yeye atalindwa na Wana CCM SMZ kwa sababu Nchi ni yao..? Jee balozi iddi naye pia atambiwa ajiuzulu au ndio atalindwa na wana CCM SMZ kwa sababu Nchi ni yao..?Wale wazee na watoto wa Raia waliopoteza maisha yao bila yakupata Msaada wa Uokoaji kutoka kwa Wizara hii VIP2 Balozi iddi na naibu wake Mohammed aboud watawafahamu nini viongozi hawa madhalim..? Jee Hawajui kwamba Ukipigao Ndio Ukufukuzao...?Wizara ya VIP 2 ndio muhusika mkubwa wa Uzamishaji wa Boti ya kwanza ya MV Spice Islander baada yakuachia Boti kujaza bila ya kiasi na kuiruhusu boti hiyo kuondoka katika Dom Duck Night. Meli ilipokua inaanza kuzama waliwasiliana na ZMA ili wapatiwe Usadizi wa Uokoaji lakini Wizara husika ikiongozwa na Balozi Seif Ali Iddi na Mohamed Aboud walishindwa kufanya Hivo wazembe wakubwa.wakanyamaza kimya na kuwaulisha wanawake na watoto chungu nzima.Wakati huo Hamadi Masoudi alikua hata hayupo Nchini alikua Nje kuhangaikia Misaada ya Maendeleo ya Ujenzi wa Miundo Mbinu ilioko kwenye Wizara yake. Jee hapa nani wakulaumiwa..? Ajali ya MV Skagit ilitokea wakati wa saa Saba mchana kweupe na ajali hio ilitokea karibu na Dar-es-Salaam.sio kama walivyo sema kuwa ni chumbe hii ni kuonyesha wazi watanganyika pia wanamkono wao hapa wakutuuwa maana meli imezama dar es salaam ila wao hawakutowa msaada wa aina yoyote hao tunaowaita dungu zetu hao. Captain wa Boti hiyo alitoa taarifa kwa SUMATRA na ZMA ambayo kuwa meli inazama pia aliwataarifu akina Mohamedi Aboud na Balozi Seif Iddi. Lakini Kilichotokea ni Uzembe kama uliofanywa kwenye MV Spice Islander . Yes Mohamedi Aboud hakuweza Kuchukua hatua yoyote akawacha watu waafe kwa sababu waliokua ndani ya Boti sio wanawe wala wake zake. Na Balozi Seif Iddi ambaye ni Kiongozi lililokoma na DAMU YA UMAPINDUZI na CCM GOGO pia hakuchukua hatuwa yoyote.bayaa zaidi Hakuweza hata ku-react katika tukio hilo sio Moral wala practice.maana kichwani mwaka ashapiga hisabu millioni mangapi yata letwa katika msaada wa wafiwa na ngapi atachukuwa huku watu wanakufa yeye anafikiria pisa za hao wanaokufa atazitumia vipi inalilahi waina ilehi rajiuni. Hatimaye Watu walikunywa maji mpaka wanakufa mmoja mmoja huku wakiiona Dar ile pale. Wazanzibari tunajua kuna vikosi vya KMKM na kambi zipatazo 25 kwa Unguja tu hiyo ambazo zina Vijana wa JWTZ. Kwa nini Serikali ya Sheini haikuchukua hatua yaku Mobilise Vikundi hivi kwa Imagancy Disaster wakati ule liilpotokea Tokeo la kuzama kwa Spice Islander..? watasema ilikuwa usiku wamelala je hili la mv skagit mchana mchana pia mbona hawakufanya kitu kisha sheini nakidomo chake siogopi mtu sawa m/mungu jee.?Mohamedi Aboud na Bosi wake Seif Ali Iddi watawaelezaje wananchi kuhusu tukio hili ikiwa wao ndio Wahusika wa Maafa na Uokoaji..? ila imekuwa kinyume chake wao ni wahusika wa kukusanya misaada ya wafiwa na kujirudikia mali.Kwa nini SMZ CCM imewaachia Wauwaji hawa kuendelea kula pesa za walipa kodi wakati wamefeli kufanya kazi zao..? Jee aliestahiki kujiuzulu ni Hamadi Masoudi peke yake au Na Mahommed Aboud , na Seif Ali Iddi pia..? kisheini jiulize swali ikiwa hawa jamaa watabaki madarakani na kuendele kula raha huku wananchi wanakufa kama kuku wa kifaduro wananchi watakufikiria vipi wewe..? wewe sheini ndie unaye baba DAMU ZA WATU WALIO ZAMA NA HAWA MAJANGILI HAWAKUFANYA KAZI ZAO KAMA ILIVYOTAKIWA NA KURUKIA KUKUSANYA MAPESA.
Wako wapi KMKM na JWTZ kwa nini walifika katika matukio hayo saa 12 za jioni wakati Boti imeanza kuzama toka saa saba mchana..? na Waliarifiwa masaa 5 kabla. Tunaomba Serikali ya Dr Sheni CCM itueleze haswa nini kazi ya KMKM na JWTZ..? ile kauli yako siogopi mtu mbona hukuitumiya kumuambiya balozi ali iddi wewe na mohammed aboud pia mujiuzulu mbona hukusema umebana kimya kama kijibwa koko unawapiga mabomu waislamu kwenye misikiti na ramadhani hii.
1.Hivyo KMKM kazi yao Nikupiga Watu nakuingia Misikitini na Mbwa..?
2. Hivi KMKM kazi yake ni kupiga watu wanaosafirisha karafuu tu..?
3. Au KMKM kazi yake ni Kulinda usalama wa majini na angani na kuokowa watu yakitokea maafa kama haya..??
1. JWTZ kazi yake nikuchukua Balot Peper za Kura nakuwapigia kura CCM waliopo Madarakani..?
2. JWTZ kazi yake nikujibadilisha Usiku nakua Majambazi, kuvunja Nyumba za Watu nakuiba..?
3.JWTZ kazi yake ni kupinga watu siku na kuharibu wanawake na kuuwa watu siku za changuzi..?
4. Au JWT kazi yake nikulinda Usalama wa raia nakuwa Alat na matukio ya Ajali kama ya Meli..?
Kwa nini Vyombo hivi vilichelewa kufika kwa wakati , Mohamedi Abudu na Seif Ali Iddi Tunataka nawao pia wajiuzulu kama ni Viongozi wanao jali maisha ya Wananchi na Sio uroho na  kupenda Madaraka…

WEE KISHEIN ANGALI WASHENZI WAKO WANAVYO WATESA WANANCHI HAPA ZANZIBAR NDIO MAANA WEWE KISHEIN WEWE UKAFANYA KIBRI CHA KUSEMA SIOGOPI MTU SIO..?

ASKARI ANAEJULIKANA KWA JINA LA HABIBU NDIE ALIYEKUWA
AKIPINGA MABOMU HAPA TUNAONA KUWA MWENYEZI MUNGU SIKU
ZOTE HAMFICHI MNAFIKI HUYU HABIBU ALITHANI AKIVA NGWANDA LA
KIJANI AU KAMA NDIO LA BRAUNI HATA JULIKANA SASA YEYE ANAWAPIGA
WAZANZIBARI WENZAKE KISA MSHAHARA MNONO ANAOPEWA NA WAKOLONI
WEUSI TANGANYIKA HABIBU UMESAHAU KUWA KUNA MUNGU..? UMESAHA KAMA
UTAKWENDA ULIZWA KIYAMA UASKARI WAKO UMEUTUMIYA VIPI..? SISI HATUKUONI
UNAVYO TUPIGA MABOMU JE M/MUNGU HABIBU PIA HAKUONI..? RUDI KWA MOLA WAKO KABLA MOLA HAJAKUTELEKEZA NA RAMADHANI HII DUWA YA MDHULUMIWA HABIBU SIO KITU CHA KUCHEZEA.


Tuesday, July 24, 2012

VIDEO-THIS IS ZANZIBAR NOT PALESTAINI

WAZANZIBARI WAKO TAYARI KUFA KULIKO KUENDELEA NA MUUNGANO HUU USIO NA TIJA NA WAKULAZIMISHWA KWA NGUVU ZA KIJESHI LA KIKURIA KUTOKA TANGANYIKA WAKOLONI WEUSI MAKABURU WEUSI KAMA WALIVYO KIMBIA HAPA NA RAMADHANI HII INSHAA ALLAH WATAKIMBIA WAVUKE
BAHARI WARUDI MAKWAO BUKOBA,ARUSHA NA MWANZA NA KWENGINEKO
NA RAMADHANI HII 

VIDEO-WAZANZIBAR WANAVYO UPOKEA MFUNGO WA RAMADHAN KWA MABOMU!!!

HILI NDIO JESHI LA KISHEIN LA KIKURIA LINAVYO WATESA WAZANZIBARI
NA KUWAKARIBISHIA MWEZI MTUKUFU WA RAMADHA KWA MABOMU
NA GARA LA MAJI YA MUASHO HATA NCHI ZA KIKAFIRI HAZIFANYI
HAYA ILA HAPA KWETU KUNA MARAISI WATUTU NA WOTE WAISLAMU
HII NDIO HALI ENDELE TU KISHEIN NA KUWANYANYASA WAISLAMU UTAUWONA
MWISHO WAKO JIDANGANYE HIVYO HIVYO NA UWAZIRI WAKO USIO
KUWA NA WIZARA MAALUM TUKUONE UKUFAE KABURINI
KITUMWA CHA WATANGANYIKA WEEE KISHEIN KIBARAKA CHA
NYERERE HONGERA HONGERA KWA RAMADHANI YA MABOMU.

VIDEO-NI KWELI NIMEJIUZULU – HAMAD MASOUD HAMAD

HONGERA SANA HAMAD KWA KUJIUZULU UMEONYESHA KUWA KWELI HUKO KATIKA MADARA KWA AJILI YA TUMBO BALI UKO KATIKA MADARA ILI KUJENGA NCHI NA KUSAIDI WANANCHI NA KUTOKANA  NAKUTOKUFANIKISHA LENGO UMEONA BORA UJIUZULU ILI AJE MWENGENE ATAKAE WEZA KUKAMILISHA
SASA TUONE SHAMHUN,BALOZI IDDI,MOHAMMED ABOUD NA WENGINE WALIO UZO PIA KAMA NAO PIA WATAJIUZULU KWA FAIDA YA NCHI AU NDIO MATUMBO YAO HAWAYAWEZI WATAENDELE KUBAKI NA KUKUSANYA PESA ZA RAMBE RAMBE ILI WAKIENDESHE CHAMA CHA CCM NA PESA ZA WATU WANAO KUFA KATIKA AJALI ZA MELI

KISHEIN UNASEMA HUOGOPI MTU MBONA WIZARA HIZI ZINACHEZEWA NA WEWE HUSEMI KITU WAZIRI USIYEKUWA NA WIZARA MAALUM.


Tumeona mfano mzuri alioonyesha Mh.Hamad Masoud Hamad na kuonyesha kuwajibika kisiasa. Ameweka historia katika siasa za Zanzibar. Hata hivyo, yeye si wa mwanzo. Nakumbuka Waziri Taimur Saleh alijiuzulu nafasi hiyo kufuatia ndugu yake kuhusishwa na kile kilichodaiwa wakati ule ‘kuripuliwa kwa kinu cha umeme Mtoni’.Itakavyokuwa, tumeona ukomavu wa kisiasa kwa Hamad Massoud hata tuseme iwe ni kisiasa tunaiita ‘at gun point’ maana yake ni kuwa serikalini itakuambia ‘ama jiuzulu au tutakufukuza sisi’. Lakini inapokuwa katika public inaletwa kuwa ‘fulani amejiuzulu’.Lakini jana nimeuliza watajiuzulu wangapi..?ndio pia husema bora wajiuzulu wote katika serekali ya mapinduzi
1. Wizara wa Sheria Abubakar imeoza na inanuka,dhulma imezidi – mfano:zile kesi zinazowahusu ndugu zetu wa UAMSHO.Wanakamatwa vijana bila sababu yeyote, hata inashindikana kuunda au kutengeneza charge ya kubuni. Mbaya zaidi, siku hizi polisi wanataifisha vyombo vya moto katika mihadhara hiyo,na kama utakwneda kudai, unaambiwa ‘ahh wewe ndiye tuliyekuwa tunakutafuta’ hivyo uko chini ya ulinzi.
Baadhi ya vespa, baiskeli tayari wanaendesha askari polisi, wamewanyanganya watu hivi hivi.je kama sio thulma nini..?
Baadhi ya gari za wafuasi au viongozi wa uamsho – zinahujumiwa na kuvunjwa kwa makusudi. Kweli haki hiyo, bwana Abubakar..? Haya yanatokea mchana na wizara yako inahusika na inajuwa kila kitu ila umebana kimya unaacha dhulma endele–kisha mnakaana  nakupiga kelele kuwa mnataka haki ya zanzibar ndani ya Muungano wakati nyinyi hamfanyi haki hata chembekwa rai wenu ndani ya nchi yenu.
Tunataka haki Abubakar na wewe ushalikoroga sana kwa hiyo ujiuzulu pia.
2.Rushwa iliyokithiri ndani ya mahakama, majaji, hupati haki kama hujatoa rushwa tunakufa kwa mengi, sio kupinduka kwa meli tu.Ama pale Wizara ya Elimu nayo kumeoza, harufu mbaya ya kila uoza: vyeti zaidi ya 200 fake, wanalipwa bure na hatimaye wanazalisha wanafunzi fake. Hivi karibuni walikuwa wanafanya uhakiki SMZ wote watumishi kumbe ilikuwa KIINI MACHO -yaani wanataka kujua nani na nani yumo na nani na nani hayupo, ili wawezi kupenyeza watu wao waziwa wa elimu pia ajiuzulu.
Kuna ofisa mmoja ya wizara ya fedha yeye huwa ana kwenda Pemba kila mwisho wa mwezi, na ukimtaka utampata pale Island hotel chake chake, na usiku pale kwa‘hababuu panapo uzwaa mishkaki’near Madungu huyu kazi yake ni kwenda kukusanya mishahara hewa ya wafanyakazi hewa.
Huu ndio uoza uliojaa ndani ya SMZ-GNU: hili Kishein pamoja ya kuwa ‘huogopi mtu’unalijua,maalim Seif-1 na balozi Seif-2 pia mnalijua lakini hamuthubutu na hamuwezi kuchukua hatua yoyote ya kubadilisha thulma hii je kishein hivyo ndio huogopi mtu kweli..?, maana wanaofanya haya ni watoto wenu wenyewe. hamuwezi kufanya chochote. Mtabaki kuuwa watu kwa boti au kuwapiga mabomu wanyonge katika misikiti na kuendele kutuletea vyakula vibovu kutoka bara na nje.
3.Wizara ya Afya, hakufai: dawa takriban 100% zinazoletwa Zanzibar ni fake na mbovu zishakwisha mdaa wake lakini munazileta ili masikini tufu watoto wenu watajirike maana ndio biashara zao,nasi tunaendele kufa kwa mengi.waulizeni watu idara ya mkemia mkuu wa serikali, wanajua lakini wanaogopa kusema, wanafumba macho maana ni biashara ya wakubwa na watoto wa wakubwa. Rushwa,rushwa,rushwa
4.Wizara ya Biashara imeoza inanuka: mpaka leo,tende mbovu ndio zinazoletwa hapa nchini Zanzibar, mchele mbovu,wa mabembe,na unga wa ngano mbovu ukitowa rushwa OK, utaruhusiwa, na kama hujatowa basi mchele wako utamwagwa: philosophy yetu: UKITAKA KULA, NA WEWE LAZIMA UKUBALI KULIWA.TUNAKUFA KWA MENGI NA TUTAZIDI KUFA SIO KWA KUZAMA MELI TU BALI KWA VYAKULA VIBOVU, DAWA MBOVU, NA ELIMU MBOVU,NA JESHI SIO LA ZANZIBAR WA POLISI WOTE NI WAKURIA WATAENDELE KUTUUWA WEEE MPAKA MWISHO WA HABARI.
Msisahau rushwa na dhulma iliyojaa katika sekta ya ardhi,mawaziri wanaiba ardhi za wananchi kwa kutumia nguvu zao za mamlaka ya dola, na raisi Kisheini analijua hili, ila anasema ‘wanaosababisha migogoro ya ardhi wataitatua wenyewe. Umeona wapi mhalaifu akajihukumu mwenyewe..?

Monday, July 23, 2012

SHEIN NA WEWE PIA UJIUZULU HUO UWAZIRI WAKO USIO KUWA NA WIZARA MAALUM

Inasikitisha sana kuona kuwa suala la kuzama kwa meli hii ya pili ambalo limepoteza watu zaidi ya 200, limechukuliwa kirahisi na serikali  hii ya mapinduzi daima na sasa inapinduwa tu maboti ikiuwa.
Kujiuzulu kwa Hamad siyo mwisho wa sakata la tukio hilo, pamoja na lile la kupigwa watu mabomu ya gesi wakiwa msikitini wakiwaombea marehemu dua kutokana na msiba huo. Siku ya Ijumaa ni siku tukufu kwa waislamu na ilikuwa ndiyo fursa ya mwanzo ya viongozi wa dini kuchukuwa nafasi ya kuwaombea dua waliokumbwa na janga ambalo ukiangalia kwa kina, uzembe wa serikali hii ya mapinduzi daima.
haikuwa jukumu la waziri peke yake bali ni jukumu la serikali yote pamoja na Baraza la Wawakilishi, ambalo limefikisha kuchangia bajeti za ofisi ya Sheini na za Seif Iddi na kuzipitisha bajeti zao bila kuuliza nini kimefanywa na serikali kuhusiana na fedha zilizochangwa kusaidia maafa Zanzibar, wakati meli ya Spice Islander ilipozama na bila hata ya kuona haya seif iddi ashaanza kupokea pesa za rambe rambe nyengine za mv skagit.Kama kweli wa semavyo kuwa wameunda serikali na uongozi bora au kama wanavyoita “Utawala Bora”, basi Dr. Sheini alivunje  Baraza lake la Mawaziri, Baraza la Wawakilisi na yeye Dr. Sheini mwenyewe pia AJIUZULU WADHIFA WAKE ALIYO PACHIKWA NA SEREKALI YA WAKOLONI WEUSI TANGANYIKA KISHA WAKAMFANYA KUWA WAZIRI HANA WIZARA MAALUM AJIUZULU HUO UWAZIRI WAKE USIO KUWA NA WIZARA MAALUM.
Tukio la kuwapiga mabomu wananchi katika ibada na Sheini akashindwa kutoa ufafanuzi, pia ni kitendo haki wezi kudharauliwa na wananchi, na hana budi kutoa maelezo na kujiuzulu mara moja. Matukio kama hayo: Kuzama kwa meli zaidi ya tano sasa na kupigwa watu mabomu misikitini wakiwa na lengo la kuwaombea dua marehemu, ni vitendo vya kikatili na halijawahi kutokea hata katika nchi za kikafiri kama Amerika na Ulaya.
TUNATAKA SHEINI AJIUZULU HARAKA KWA KUFUATA UTARATIBU KAMA ALIVYO FANYA WAZIRI MASOUD NA KISHA YASIMALIZIKIE HAPO ASUBIRI KUJIBU MASHTAKA MAHAKAMANI KWA NINI ANAWAPIGA MABOMU RAI WAKE WAKIWA KATIKA IBADA..? AJIBU SHTAKA HILO MAHAKAMANI.HILI LIWE FUNZO  KWA VIONGOZI WENGINE NA UTARATIBU WA UTAWALA BORA NA DIMOKRASI.
Wazanzibari wamechoka na dhulma zinazofanywa na viongozi wote wa serekali ya mapinduzi pamoja na raisi huyu wa kupachikwa ambaye ni Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum.

WAZIRI HAMAD MASOUD HAMAD AMEJIUZULU.HONGERA SANA


Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano wa Zanzibar, Hamad Masoud Hamad amejiuzulu wadhifa wake leo jioni imeelezwa. Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu  wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Dk. Abdulhamid Yahya Mzee ilisema tayari Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk. Ali Mohammed Shein amekubali ombi la Waziri Hamad Masoud kujiuzulu.
“Tarehe  20 Julai,2012 Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Mheshimiwa Hamad Masoud Hamad alimuandikia barua Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk Ali Mohammed Shein ya kumuomba ajiuzulu kufuatia ajali ya kuzama kwa meli ya Mv. Skagit iliyotokea Julai 18,2012” Ilisema taarifa ya Dk. Mzee.
Kufuatia kujiuzulu kwa waziri huyo, Rais Dk Shein amemteua Mwakilishi wa Jimbo la Ziwani(CUF) Rashid Seif Suleiman kuwa Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano.
“Kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano,Rais amemteua Rashid Seif Suleiman kuwa  Waziri wa Miundombinu na Mawasiliano” Taarifa ya Ikulu ilisema.
Uteuzi wa Waziri mpya wa Miundombinu na Mawasiliano umeanza Julai 23 mwaka huu.
NA MULIO BAKA MAMBO YASHAWASHINDA ACHIENI NGAZI NDIO HESHIMA SIO KINGANGANIZI KAMA SHAMHUNA