Sunday, December 30, 2012

NCHI YA ZANZIBAR INABATIZWA KWA LAZIMA KISA PADRI KAJERUHIWA



Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefika njia panda kutokana na matukio mabaya na ya ghafla yanayotokea hapa Zanzibar, hasa yanayobeba sura ya ‘hit and run attacks’ ambayo pia yanaingia katika sura ya visasi (revenge) — kuanzia lile la Soraga hadi la huyu Padri.
Kuna nadharia nyingi hapa zinazohusu uhalifu (theories on criminology) — au hata conspiracy theory.
Nadharia 1: hujuma inafanyika lakini hakuna clue/au hata alama ya namna uhalifu ulivyofanyika — hapa inakuwa taabu kwa wapelelezi kugundua namna ya uhalifu huo ulivyofanyika, au vipi umefanyika, na hata kuanzia pa kufanya upelelezi.
Nadharia ya 2: Uhalifu umefanyika, aliyefanyiwa uhalifu yuko hai, na kauli thabit anaweza kusema. Hapa inakuwa rahisi sana sana kwa makachero kujua na kuanza upelekezi wa kina. Kesi zote mbili zilizotokea Zanzibar (Soraga na Padri zinaingia hapa).ila ya soraga ishafukiwa hii ya padri itakuwa hai mpaka mwisho wa dunia.
Wote wazima na wote wana kauli thabit. Padri ameweza kuzungumza na kuweza kuidhalilisha POLISI kama taasisi pale alipotoa kauli yake kumpinga RPC Aziz.
Kauli ya Padri dhidi ya jeshi la polisi inaonyesha dhahir kuwa kanisa linataka watendewe vile wanavyotaka wao; na sio hali halisi ilivyo. Ingawa hakusema wazi wazi, lakini indirectly, ana maana ya kusema kuwa ‘polisi ni muongo, au waongo’. Hii ni idhalali kubwa kwa jeshi la polisi.
Kw auhakika ni kuwa padri huyu alikuwa anashika pesa, whether awe mhasibu by professional or not. Kwa uhakika 100% padri huyu ndiye signatory wao.
Bila yeye haitoki pesa. Je, na hili atalipinga. Naomba hao makachero wa kutajika kutoka Dar, waanzie hapa kama ndio ‘lead’ yao. Tumelewaana..? Muanzie hapa. Je, haiwi kuwa ‘internal job’.
Angalia sequence za kihalifu zilizofanyika Tanganyika nchini kwao hivi karibuni:
i. Afisa wa kuzuia rushwa apigwa na kuuliwa na mwenzake Dar
ii. RPC Mwanza apigwa risasi na kuuliwa Mwanza.
iii. Pesa nyingi zimeibiwa duka la Dar (150m) — kitendawili mpaka leo...? Au kwa sababu hili limetokea nchini Zanzibar. Achane kuwa bias!!!
iv. Kuna mauwaji mengi yametokea Dar during chrismas time, mzungu mmoja amenyongwa hotelini, na wengine kuuwawa kikatili …kimya!!! kimya!!! hakuna upelelezi wala mavi kimya zanzibar tushamwangiwa makachero wala hawatarudi kwao Tanganyika ndio washakuwa rai wa zanzibar hao.hivi ndiovyo walivyo na ndivyo wanavyo letana hapa nchini kwetu zanzibar
Nadharia 3: Nadhani kanisa, CCM Tanganyika na serikali zote zitafurahi sana kama report ya makachero hayo zitasema kuwa ni UAMSHO ndio waliofanya kosa hilo. Mimi naomba kuwasaidia kitu hao makachero mavi.
Mpaka sasa, ukweli ni kuwa, waislamu wa Zanzibar na Tanganyika kwa ujumla, hawajafikia level hiyo ya kutumia silaha au kuhujumu. Hili linajulikana na liko wazi. Kisaikolojia, bora hata siasa Zanzibar zinaweza kuwa ni ‘problem’ kuliko hata dini.
Mimi naomba serikali ya JK,Mtumwa Shein na IGP Said Mwema muwe waangalifu sana na trend hii inayojitokeza. Mjaribu sana kuwa fair na wakweli – otherwise, mnaimaliza nchi hivi mnajiona. Your careless minds — JK,Mtumwa Shein, Mwema and others — inaweza kuleta bad feelings kwa waislamu ambayo wanaamini kuwa Zanzibar ni nchi yao na nchi ya kiislamu. Hivi JK kuoni fakhari kuwa hivyo, yaani Zanzibar ndio kama kigezo kwa dunia v.s Tanganyika.
Kumbuka kuwa mnapewa pesa za bure na nchi za kiislamu kupeleka hajji waislamu (ni kupitia mgongo wa Uislamu wa Zanzibar, na sio Tabora au Singida n.k); then mnachagua wakereketwa kwenda huko Hajji na kuacha waumin wa kweli.
Chokochoko hizi za dini, na hasa ukiristo — hautoijenga Tanganyika, ila itaivunja vunja vipande vipande – angalia secratian war — Northern Ireland, former Yugoslavia [Kosovo, Serbia n.] Iraq n.k.
Mtumwa Shein na JK mnakaa na kubabaishwa na washauri wenu; na hamtaki kutumia akili zenu mlizojaaliwa hata 0.01%. Hebu tafuteni ukweli wa mambo. Huu ndio ushauri w abure kutoka kwangu.
* Na balozi Seif Ali Iddi acha kuwa bias. Mbona hujaenda kumuona Fadhil Soraga mpaka leo..? umeamua kwenda wewe na Mohammed Aboud kumuona Padri na aila yake na wafuasi wake.
* Naomba tena hao makachero mavi waliokuja nchini kwetu Zanzibar waanzie pale benki anapokwenda kuchukua ‘hela’ padri huyu ambaye pia ndiye signatory mkuu, benki xxxx! nendeni hapo mkaone transaction alizokuwa anazifanya padri huyo, na kama kuna bank reconciliation zinazokubalika — au shaghla baghala tu.
* Na kama je, hali ya makusanyo na matumizi ya kanisa hili yanaridhia financial regulations za Tanganyika, Zanzibar na bank of Tanzania. Check …kama kuna a kind of money laundry hapo?
Kwa ufupi matukio haya bado yamebaki kuwa kitendawili (unresolved mystery).

Friday, December 28, 2012

WAZANZIBARI TUMEPINDULIWA 1964 NA SASA TUNAPINDULIWA KIKATIBA


KAMA KWELI WAZANZIBARI TUNAITAKA ZANZIBAR YETU YENYE MAMLAKA KAMILI BASI KWANZA TUMUONDOWE DIKTETA SMZ KAMA ALIVYO ONDOLEWA GADDAFI,BEN ALI,HUSSENI MUBAROUK,SALEH NA WENGINEO LA SIVYO ITAKUWA TUNACHEZA MDUWARA TU.


Tarehe 19 December ilikuwa siku ya mwisho kwa Tume ya Kukusanya maoni ya upatikanaji wa katiba mpya. Tume ilifanikiwa kutemebelea nchi nzima na kukutana na wananchi walioweza kutoa dukuduku lao na vipi katiba mpya itapatikana.
Kwa mujibu wa hadidu rejea za tume hityo zilizotolewa ni kwamba baada ya kumaliza kazi ya ukusanyaji maoni kwa wananchi kutakuwa na mabaraza ya katiba.
Hivi sasa hapa Zanzibar kuna taarifa za kuaminika kwamba baadhi ya wizara zimetowa toleo maalim (circular) la kuwataka wafanyakazi wa serikali watowe maoni yao ya kwa njia za maandishi. 
Toleo limepelekwa idara mabalimbali za serikali kuwataka wafanyakazi waandike maaoni yao juu ya mchakato wa katiba. Hili ni lakushangaza kwamba waliotoa toleo hili sio Tume ya Katiba wala halimo kwenye hadidu rejea za Tume hiyo. Hivyo kutia wasiwasi muelekeo wa upatikanaji wa katiba mpya Tanzania kugubikwa na magube ya kimapinduzi.
Zipo dalili za dhahiri za kukengeukwa na kudharauliwa maoni ya wananchi kama vile walivyotumia juhudi zao, wakavunja shughuli zao, wakatumia muda wao, na mwisho kile walichosema kuanza kukidharau. 
kauli ya Prof baregu ni ushahidi tosha na mwanzo wa kuthibisha hili. Dharau yake kwa maoni ya wananchi hasa Wazanzibar, sio suala la kuvumiliwa. Ipo haja kwa nguvu zote tuisute tume pale itakapozidisha dharau zake kutothamini maoni ya wananchi.

Wednesday, December 26, 2012

FATHER AMBROS AJERUHIWA KWA RISASI KWA MAKUSUDI ILI MAKANISA YAPEWE ULIZI ZAIDI NA SMZ NCHINI ZANZIBAR



Watu wasiojulikana leo wamemjeruhi kwa risasi Father, Ambros Mkenda wa Kanisa Katoliki la Mpendae Nchini Zanzibar nje ya nyumba yake majira ya saa 12 jioni wakati akitokea kanisani.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Aziz Juma Mohammed amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo alisema Father amejeruhiwa kwa risasi na ameumizwa sehemu ya kichwa na amekuwa akitoka damu nyingi kichwani na tayari anapatiwa matibabu katika hospitali kuu ya Mnazi Mmoja.
Alisema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini wahusika walifanya uhalifu huo kwa madhumuni gani kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria.
“Sisi tunahesabu kuwa kitendo hiki ni kitendo cha kihalifu na tunawatafuta wahalifu waliofanya kitendo hiki kwa hivyo bado ni mapema kusema kwamba kitendo hiki kimefanywa na nani kwa kuwa bado uchunguzi wetu unaendelea na hadi sasa hakuna mtu tuliyemshika kuhusikana na tukio hili” alisema Kamanda.
Kamanda Aziz akisimulia tukio hilo alisema walipata taarifa majira ya saa 2 na kwenda katika eneo la tukio ambapo Father alikuwa akitokea kanisani na kutaka kuelekea nyumbani kwake wakati akiwa ndani ya gari ndipo aliposhambuliwa na watu wasiojulikana na kuanguka.
“Tumekuta mabaki ya risasi ndani ya gari yake na katika vioo vyake vya gari vimevunjika na tumekuta damu chini pale” alisema Kamanda.
Aidha Kamanda Azizi alisema Father Ambros yeye ni mhasibu pale kanisani na hivyo mara nyingi watu wananaamini kwamba katika siku za krismass mara nyingi sadaka hukusanywa fedha nyingi na hivyo wanamini kwamba alikuwa fedha mikononi na ndipo inawezekana waliamua kumjeruhi kwa risasi wakitaka kuchukua fedha hizo.
Hata hivyo alisema uchunguzi wa awali ndio utakaoeleza ni suala gani lililopelekea kujeruhiwa kwa risasi lakini wanaendelea na uchunguzi huo ambapo uchunguzi ndio utakaojulikana sababu kamili ya tukio hilo.
“Kamanda Azizi pia alisema Sisi hatuamini kwamba kuna kisasi kwa viongozi wa dini lakini tunachukulia hilo ni tukio la kihalifu na pia hatuna vipeperushi vya aina yoyote vinavyoelezea kuwatisha viongozi wa dini kwa hivyo tunachukulia hayo ni matukio ya kihalifu na wala hatuamini kwamba matukio haya ni ya dini fulani” alisema Kamanda Azizi.
Akielezea kuhusiana na hilo Kamanda Aziz alisema jeshi la polisi limejipanga na kuzidisha ulinzi katika maeneo yote ya makanisa ambapo kumesambazwa polisi wa kutosha kwa kuwa wanajua wakati wa sherehe mambo ya kihalifu hujitokeza.
“Sisi kawaida huwa tunaweka ulinzi siku za sherehe zozote lakini ulinzi upo wa kutosha” alisisitiza Kamanda Aziz. kwamba makanisa yote yamewekewa ulinzi wa kutosha kabisa ila wahalifu wanajuwa mbinu gani na saa ngapi na watafanya uhalifu huo wapi,  lakini wahalifu wanapotaka kufanya uhalifu huwezi kujua wataufanya wapi mpaka waufanye.

Tuesday, December 25, 2012

2015 RAISI WA JMAHURI YA MUUNGANO AWE SHEIKH FARID MAKAMO WAKE SHEIKH MSELLEM KAMA KWELI NCHI YA TANGANYIKA WANATAKA MUUNGANO UWENDELE BAINA YAO NA ZANZIBAR



Miaka mitatu kutoka sasa, Tanzania itafanya uchaguzi wake mkuu utaohitimisha miaka kumi ya utawala wa Rais Jakaya Kikwete. Tanzania kama nchi nyengine duniani, inafata mfumo wa demokrasia ya vyama vingi. Katika mfumo wa vyama vingi, na iwapo kuna demokrasia ya kweli, basi ni matarajio yetu kuwa chama chchote kitakachoshinda kitapewa haki yake na ridhaa ya kuongoza nchi.
Lakini pamoja na hayo, suali la uwiano wa Ugombea wa kiti cha Urais kwa pande mbili za Muungano, limekuwa likipuuzwa sana kuanikwa katika mijadala mbalimbali nchini. Suali la makubaliano ya mapokelezano ya wadhifa huu mkuu wa nchi baina ya sehemu mbili za Muungano, haujawekwa sawa na ni moja kati ya changamoto kongwe zinazoungana na mkururo wa kero za Muungano hapa nchini.
Tangu tuungane, ni miaka takribani 49 sasa. Wakati Zanzibar ikiwa na marais saba tangu 1964,Tanganyika ndio inatimiza nusu tu ya wale waliokwisha tawala Zanzibar, ikiwa na marais wanne tu hadi sasa. Mara baada ya Muungano, Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalim Julius Nyerere, alishika hatamu ya kuiongoza Jamhuri hadi pale ‘alipong’atuka’ madarakani kwa kulazimishwa kabla haja anza kuitwa dikteta mwaka 1984/85.
Katika kipindi hichi cha miaka 20, Mwalimu hakuwahi kueleza wala kufafanua lolote kuhusu mpokezano wa madaraka kwa zamu baina ya nchi zetu hizi mbili Zanzibar na Tanganyika. Naamini alifanya hivi sio kwa kutojua umuhimu wa kitendo hicho muhimu. Kitendo ambacho kingeashiria usawa mkubwa na haki inayosimamiwa na Muungano wetu. Mwalimu hakulijadili hili kwa sababu alijua wazi kufanya hivyo kungeviza ajenda yake binafsi ya kuimeza Nchi ya Zanzibar ndani ya matumbo ya Tanganyika na kuiondoa kabisa katika ramani ya dunia. Hili ndio lililokuwa lengo lake, bila shaka yoyote shabashiii.
Mungu akikupangia nakama, huna ujuzi wala ujanja. Kwani hayati Sheikh Abeid Karume, ambae ndie aliyekuwa Rais pekee wa Zanzibar aliekuwa akithubutu kumhoji na kumjibu Mwalimu lolote, lakini lakuvunda halina ubani, Sheikh Karume alikufa mapema mno. Tena wakati huo anakufa, bahati mbaya zaidi, ilikuwa Muungano huu haujawa na sura mbaya iliyo wazi wazi kama sasa, japo kiwingu cha dalili hizo mbaya kilianza kuonekana kwa mbali. Sheikh Karume akauwawa, na sababu ya kifo chake, ikafikichwa fikichwa, kisijulikane cha ukweli hadi leo.Ni begeje tu. Na kwanini, watu washuhulike na hili wakati, kufa kwa panzi ni neema ya kunguru? Aliekufa ndio kafa!!!!
Rais Jumbe, alijaribu kwa sana kuhoji hali kama hii. Lakini alichelewa mno.Na kwa jinsi Mwalimu alivyokuwa amejipanga kikazi kiulinzi na kiusalama, juhudi za Sheikh Jumbe zikawaka na moto. Zikaunguwa na kusakatuka kama kijungu kidogo tu cha dagaa tonge, kilicho sahauliwa na mpishi aliekwenda kujisuka akisahau kuwa moto hauna sumile. Sheikh Jumbe akang’oka kama Mbuyu uliopigwa halbadiri mbayana. Akakunguzuka na mashina yake yote!!! Njia nyeupe!!! mambo yakazidi kuwa mazuru kwa nyerere.
Baada ya majaribio haya mawili ya kujitokeza kwa Wazanzibari waliowakijifanya hawaogopi kumuhoji Nyerere, kilichofata ni mpango wa kudhibiti nani awe Rais wa Zanzibar. Ikawa Rais anaewekwa huku kwetu si katika yoyote anaeweza kuuhoji wala kuujadili Muungano, ‘imma faimma’ Nyerere awe hai, au awe ameshakufa. Na hili likafanikiwa. Bahati nzuri tu ‘Mtu si mbwa’. Hawa unaowaona walihoji kidogo wakaitwa ‘samaki’ na wavyele wao, ni matokezeo tu. Kwani haki haizami na dhulma haidumu.
Viongozi wetu wa Zanzibar, ni watu waliopangwa maalum kufuata utaratibu waliopangiwa na wakubwa zao kule kwa makaburu weusi Tanganyika. Na kwa maana hii hakuna aliyewahi tena kuhoji kuhusu mgawano wa nafasi ya Urais wa Muungano. Ambapo, penye Uungwana na haki ndani ya Muungano huo, bila shaka tulikuwa tupokelezane zamu. Hata kama tuko katika mfumo wa vyama vingi kiasi gani.
Kwa upande wa CCM huko kwa mkoloni mweusi Tanganyika, hili walikuwa walione pia. Hasa wao wakiwa kama chama chenya nguvu na chenye kushika hatamu. Ipo haja, tena bila kuzozana, kuipa nafasi Zanzibar kuongoza katika Jamhuri ya Muungano ya kinafiki iliyo undwa kumaliza Zanzibar, tena katika wadhifa wa Urais, jambo ambalo linaonekana kuwa zaidi ya ndoto ya ‘Alinacha’ kwa sasa.
Suali la kumpa Mzanzibari Urais wa Muungano ni ndoto ya Alinacha kwa sababu nyingi. Kwanza tuchukulie chama cha CCM kiwe na matumaini makubwa ya kushinda. Ukweli ni kwamba CCM na Muungano ni mtu na mama yake mzazi. Nasema ni mama kwa sababu hutokea watoto wasio baba kabisa, wala watu wengine, lakini hakuna mtoto asie na mama. Na mapenzi ya mama kwa mtoto hayana mfano wake wala kipimo chake. Na tunategemea vivyo hivyo kwa mtoto na mama yake. Kama haya ni kweli, na dhamira ya Muungano ni ile ile ya kuelekea nchi moja. Tena wakati ambao Wazanzibari wanahitaji ‘kupumuwa’ kwa nguvu zote. Hili ni gumu.
Isitoshe, ukiwauliza zamu ya Zanzibar lini, wanakujibu kuwa Mwinyi alikuwepo hapa. Hivi Mwinyi ni Mzanzibari...? Kwa kigenzo kipi...? Na haya naawe huyo Mzanzibari kama ataamuwa kujinadi hivyo, lakini sula linabaki kuwa Marais wawili sasa, yaani miaka 20, Urais uko Tanganyika tu. Kuna ubaya tena gani wakitupa tena kumi, kama kweli tuna nia njema..?Hapa panahitajika tuwe wakweli wadadisi kidogo juu ya hili.
Ama kwa upande wa CHADEMA, naona wazo hili si mahala pake hata kidogo. Ingawa CCM na chadema lao moja, na ndio ukaona CHADEMA iliibuka tu kutoka katika ombwe, na kuja kuwa chama chenye nguvu hata kuliko CUF kule bara ambayo ilikuwa inaimarika vizuri siku hadi siku. Lengo, ni kuiondoa na kuizima nyota ya CUF kule wakiamini kuwa, kuanguka kwa CUF Nchini Tanganyika ni mafanikio makubwa ya kuzima nguvu ya wazanzibari kutaka kujitawala na ‘kupumuwa’. Na hili wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Kuna kila dalili kuwa CHADEMA, hawana mpango na Zanzibar zaidi ya kuimaliza zaidi. Na kama hili linasomeka hivyo katika ajenda zao za siri, hawana mpango wa kumpa Mzanzibari nafasi yoyote ile hata ya Ubunge sembuse Urais. Na hii ni kwa sababu moja kuu: CHADEMA ni wabaya zaidi ila uzuri wao wanakuuwa ukiwaona kuwa wanakuuwa CCM wao wanakuuwa kidogo kidogo ndio kama tunavyo ona jinsi CCM ilipotufikisha wazanzibari tu hoi bini tabani,CHADEMA wao ni ubaya ubaya tu wao hawajifichi. Isitoshe, mfungamano wao mkubwa na kanisa ambalo kwa kiasi kikubwa ndio linaloipa kiburi CHADEMA, unaifanya hali ya uwezekano wa Zanzibar wa kuwa na nafasi kubwa kama hio katika Muungano kuwa ya tembo kupenya tundu ya sindano.
Pamoja na hayo, tusikate tamaa. Ipo haja kwa kila mmoja wetu wakiwemo viongozi kuhoji nafasi ya Zanzibar katika uongozi wa juu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Ijapokuwa tunaonekana kukubaliana na kuridhika kabisa na kitazonge, na changa la macho la kupewa kwetu Umakamo wa Rais. Nafasi ambayo haina athari yoyote kwa taifa zaidi ya kufunguwa vikao,na maskani za CCM kujulia wagonjwa na kuhutubia mikutano ya mazingira na Ukimwi.
Pia tumeridhika na suala la Rais wetu kuwa Waziri katika Jamhuri ya Muungano, jambo ambalo haliingia akilini kabisa. Maana naamini wazi Makamo wa Rais Tanganyika, kiitifaki ni mkubwa zaidi kuliko Waziri, ambae pia ni Rais akiwa Zanzibar. Huu ni mchezo wa kitoto au wa kuku lala, tustiane majivu ya macho. Ukweli tunatakiwa tusitosheke na hapo. Tuhoji, tudai, na tutoe kauli moja, ‘Mara hii Urais wa Muungano, ni Zamu ya Zanzibar’ na ni SHEIKH FARID. Tuwatazame na pumzi zao!!!! TUACHIWEEE TUPUMUWEE

NANI ANATAKA KUWA MSANI MPYA WA BONGO FLAVA..?


AFANDE SELE VIPI TENA..?

WASANI WA BONGO FLAVA WAMEISHIWA SASA WANAVUWA NGUO NA KUONYESHA MATAKO

MTOTO MDOGO ANA MWAGA RAP SIO ZA KAWAIDA

ZIJUWE AINA NNE ZA WATU HAPA DUNIANI


SHAMHUNA YUKO KATIKA AINA GANI KATIKA HIZI NNE WACHA KOMENTI YAKO

Kuna yule ajuae, na ajua yuajua
Tatizo mpelekee, lolote atatatua                                 
Yuajijua mwenyewe, kwamba yeye yuajua
Kuwa karibu na yeye, elimuye kuchukua
Mwengine ni ajuae, na hajui yuajua
Elimu i tele naye, hana asichokijua
Ela aonavyo yeye, yu juha wa kurembewa
Huyu na ashituliwe, hadhi yake kuijua
Na kuna asiyejua, na ajijua hajui
Mambongwa huyakimbia, watuni yeye hakai
Adhara aichelea, kuja tolewa nishai
Huyu si wa kuzomewa, ni wa kufunzwa kwa rai


Wa nne ni asojua, na hajijui hajui
’kiitwa kuhutubia, himahima hakatai
Maringo kujisifia, yukajifanya nabii
Huyu ni kushushuliwa, yukaambiwa hajui

Wa kwanza ni ajue, akajua yuajua
Wa pili ni ajuae, na asijue ajua
Wa tatu ni asojua, akajijua hajui
Wa nne ni asojua, yusijijue hajui

UAMSHO KWALI INAMUOGOPA M/MUNGU AU INAOGOPA SMZ NA MACHOGO...?



Amiri wa muda wa jumuiya ya uamsho na mihadhara ya kiislamu Zanzibar  amekanusha madai yaliodaiwa kwamba waislamu wameiomba serikali iwatoe viongozi wakuu wa jumuiya ya uamsho kabla ya sikukuu ya krismas ambao wapo rumande kwa muda wa takriban miezi  miwili kwa sasa.
Hivyo amewaomba waislamu na wananchi kuwa wastahmilivu katika kipindi hiki ambacho maoni ya ukusanyaji wa maoni yamekamilika kwa upande wa Zanzibar hivyo amewaomba wazanzibar kusubiri utekelezwaji wa matakwa yao.
 Akizungumzia vipeperushi vilivyosambazwa hivi  karibuni vya kutoa onyo ikiwa maamiri hawaataachiwa huru ikifika siku ya krismas na mwaka mpya watachukua hatua. Hivyo Amesema vipeperushi hivyo havikutolewa na viongozi wa jumuiya hiyo na amewataka waislamu kuwa makini dhidi ya maadui wasioitakia mema Zanzibar.
 Amesema vipeperushi hivyo vilivyodaiwa vimetoka masjidi jibril mkunazini kwamba havihusiani na msikiti huo wala taasisi yeyote ya kiislamu Zanzibar,
 Aidha amebainisha ya kwamba vipeperushi hivyo vina lengo la kuwashawishi wananchi kuchochea vurugu ambazo hazina faida kwa maendeleo ya Zanzibar, hivyo Amewafahamisha wananchi na waislamu kwamba suala la kuingilia mahakama kwa sasa ni kosa kisheria  hivyo amewataka wazanzibar kutoshabikia masuala hayo wakati huu ambapo  kuna mambo muhimu yanayolikabili taifa.
Na baadhi ya waislamu ambao huswali msikiti huo wamewaomba wale wote amabo wanauchezea uislamu waache tabia hizo kwani misikiti ni nyumba tukufu kwa ajili ya ibada na sio kwa ajili ya kuwagawa wananchi..

Sunday, December 23, 2012

BREAKING NEWS-TANGAZO KWA WAZANZIBARI WOTE WALIO NJE NA NDANI YA ZANZIBAR NA WAISLAMU WOTE ULIMWENGUNI


UJUMBE MUHIMU KWA WAISLAMU WOTE.

WANANCHI NA WAISLAMU WA ZANZIBAR TUMECHOKA KUDHALILISHWA NA KUDHALILISHIWA VIONGOZI WETU WA DINI YA KIISLAMU.

KWAMBA KATIKA NCHI HII HATUJAONA TANGU UHURU WA MAPINDUZI KUDHALILISHWA KWA MKIRISTO YOYOTE WALA KIONGOZI YOYOTE WA KANISA.

UDHALILISHAJI HUU UNATOKANA NA VIONGOZI WA SERIKALI DHIDI YA UISLAMU KUTOKANA NA SHINDIKIZO LA MAKANISA

INAONEKANA KUWA VIONGOZI WA SERIKALI WAKO TAYARI KUDHALILISHA HESHMA YAO, DINI YAO, WATU WAO NA NCHI YAO KWA AJILI YA KUTII AMRI ZA MAKANISA

KUTOKANA NA HAYO SISI WAISLAMU WA ZANZIBAR AMBAO TUMECHOSHWA NA VITIMBI UDHALILISHAJI WA DINI YETU,TUNAOMBA SERIKALI IWAACHIE HARAKA VIONGOZI WA KIISLAMU KABLA YA KRISMAS TAREHE 25/12/2012

ENDAPO MAOMBI HAYA YA WAISLAMU NA WANANCHI YATADHARAULIWA NA KUPUUZWA.WAISLAMU WATAAMUA CHA KUFANYA.
TUTAENDELEA KUTHALILISHWA MPAKA LINI...?
TUTAENDELEA KUTHALILISHWA MPAKA LINI.................?
 

Tuesday, December 18, 2012

WANAFUNZI WA SHULE ZA NCHI YA TANGANYIKA WANAWABAKA WALIMU WAO.


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa

MISHENZI NI MESHENZI TU NDIO MAANA WAZANZIBARI HATUTAKI MUUNGANO
 
WALIMU wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Ruaruke wilayani Rufiji, Mkoa wa Pwani, wameitelekeza shule hiyo kutokana na kukithiri kwa vitendo vya baadhi ya wanafunzi kuwadhalilisha kimapenzi, ikiwamo kuwabaka baadhi yao.
Habari zilizolifikia FREE ZANZIBAR PEOPLE FROM MKOLONI MWEUSI jana zimeeleza kuwa mbali na udhalilishaji huo, wanafunzi hao wamekuwa wakiwatishia maisha walimu wao kwa namna mbalimbali. Katika moja ya vitisho hivyo, wamechoma moto nyumba zao tatu.

Habari hizo zimeeleza kwamba walimu hao wamelazimika kuikimbia shule hiyo baada ya baadhi ya walimu wa kike kutongozwa na wanafunzi, kupigwa mabusu kwa nguvu hadharani, kutishiwa kuchomwa visu ikiwa hawatakubali kupingwa pini na wanafunzi hao na kuchorwa vikatuni vya kudhalilisha.

Mmoja wa walimu hao ambaye hakutaka kutajwa jina lake akihofia kushughulikiwa na wanafunzi hao alisema amelazimika kuikimbia pamoja na walimu wenzake wote, kwa kuwa wameshindwa kudhibiti tabia hiyo kutokana na vijana hao kuungwa mkono na wazazi wao.

Akizungumza kwa simu akiwa Dar es Salaam, nchini Tanganyika mwalimu huyo alisema shule hiyo yenye wanafunzi 485, imepoteza mwelekeo, haitawaliki na mazingira yake hayavutii walimu, hasa wa kike, kuishi na kufanya kazi.

“Tumevumilia vya kutosha, lakini kila kukicha hali inazidi kuwa mbaya. Walimu wanafikia mahala wanabakwa!!!! Kibaya zaidi wazazi na mamlaka nyingine hazionyeshi ushirikiano kwetu, wazazi wanawa-support wao hata tukiwambia huyu mwalimu kabakwa jana wanasema hakubakwa kakaribishwa (wanawaunga mkono) watoto wao,” alieleza.
Hata hivyo, mwalimu huyo hakuwa tayari kueleza kwa undani kuhusu vitendo hivyo vya ubakaji lakini alieleza kwamba vimekuwa vikitokea walimu hao wanapokuwa katika matembezi usiku.

Vitendo hivyo vimekuwa vikitokea baada ya wanafunzi hao kuwatongoza walimu wao na kukataa kufanya nao mapenzi.

Mwalimu huyo alidai kuwa walimu wamekuwa wakitishiwa kuchomwa visu na nyumba zao kuchomwa moto, huku walimu wanne wa kike wakidhalilishwa kimapenzi kwa kupigwa mabusu na kutongozwa na wanafunzi.
“Wanafunzi wamefanya mtihani wa kidato cha pili chini ya ulinzi wa askari polisi wenye silaha kitu ambacho si cha kawaida,” aliongeza.
Alipoulizwa kuhusu tukio hilo, Ofisa Elimu Sekondari, Adnan Mwenda alisema asingependa kuzungumzia tatizo hilo kwa kuwa siyo msemaji. Akashauri atafutwe mkurugenzi wa wilaya… “Unaweza kuzungumza mambo mengine yakakuletea matatizo,” alisema Mwenda kabla ya kuelekeza atafutwe mkurugenzi.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rufiji, Leonard Rwegasira alithibitisha walimu hao kuikimbia shule hiyo na kusema kuwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, itakutana hivi karibuni kujadili suala hilo.
“Ni kweli shule hiyo imetelekezwa, walimu wamekimbia na wanafunzi hawaendi shule. Tatizo tunalifahamu na Mkuu wa Wilaya anafanya jitihada mbalimbali kurekebisha tatizo hilo,’ alisema.

Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ruaruke, Hemedi Mpullu pia alithibitisha walimu hao kuitelekeza shule hiyo na kusema Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Nurdin Babu ameagiza kufanyika kwa kikao cha dharura ili kupatikana mwafaka kati ya walimu hao, wanafunzi na wazazi.
“Mbunge wa Kibiti, Abdul Marombwa amepanga pia kufanya mkutano hapa Ruaruke ili kutafuta mwafaka,” alisema Mpullu.
Katibu wa Chama Cha Walimu (CWT), Wilaya ya Rufiji, Manyama Lazaro alisema kuondoka kwa walimu hao, kumefanya shule hiyo ijifunge yenyewe, kwani wanafunzi nao sasa hawaendi shule.

“Wanafunzi wamefikia hatua ya kuwachora walimu wa kike wakifanya mapenzi na walimu wa kiume katika kuta za vyoo! Huu ni udhalilishaji mkubwa,” alisema.
Lazaro alieleza kuwa katika siku za hivi karibuni, wanafunzi hao walichoma moto nyumba tatu za walimu na Bodi ya Shule iliamua kuwa wanafunzi hao waitwe na wazazi wao ili walipe gharama za uharibifu.

WAHAFIDHINA NCHINI ZANZIBAR HAWANA PAKUKIMBILIA WAMUWA KUBADILIKA.UKUSANYAJI WA MAONI BAADA KUMALIZA ZANZIBAR NZIMA


MAONI KWA ZANZIBAR NZIMA:
Ukichukua mwelekeo wa maoni yote yaliyotolewa hadharani katika mikutano yote iliyofanywa na Tume ya Kukusanya Maoni ya Katiba katika visiwa vya Zanzibar unapata picha ifuatayo:

Waliotaka Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa na kufuatiwa na Muungano wa Mkataba kati yake na Tanganyika ni 14,998 sawa na 65.98%. Waliotaka muundo wa sasa wa Muungano (Serikali Mbili) uendelee ni 7,034 sawa na asilimia 30.94%. Waliotaka Serikali Tatu ni 105 sawa na 0.46%. Waliotaka Serikali Moja ni 22 sawa na 0.9%. Waliotoa maoni mengine ni 573 sawa na 2.52%.

MTAZAMO BINAFSI: Inafurahisha kuona wapenda mabadiliko (progressives) katika Zanzibar kwa ujumla asilimia yao imebakia takriban ile ile 66% ambayo ndiyo iliunga mkono kuanzishwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa mwaka 2010. Kwa upande mwengine,wahafidhina wanaokataa mabadiliko katika jamii ya Zanzibar wanazidi kupungua kutoka asilimia 33% hadi
asilimia 31%.

Monday, December 17, 2012

BILALI ATAMUKIWA NA DUNIA NA KUANZA KUJIDAI KUWAPA USHAURI WAISLAMU ILI AENDELE KULA RAHA ZA DUNIA. BILALI KWANI WEWE MUISLAMU....???

NI

Makamu  wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal,  amewataka Waislamu nchini kuweka juhudi zaidi  katika elimu ya dini pamoja na ya dunia ili kuepuka matatizo mengi yanayosababishwa na ukosefu wa elimu hiyo.
Makamu wa Rais aliyasema hayo katika sherehe za mwaka mpya wa Kiislamu zilizofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Alisema matatizo mengi yanayolenga Uislami yanatokana na ukosefu wa elimu ya dini hiyo,  pamoja na elimu  ya dunia.
“Jambo la kushangaza na la kutia huzuni ni Waislamu kukosa elimu,  aya  ya mwanzo alizoshushiwa  Mtume Muhammad,  ni kusoma,  hakuambiwa kusali  au kufunga,”  alisema na kuongeza:
“Uislamu na Waislamu hatunabudi kufuata kanuni za msingi ili tuusaidie Uislamu wenyewe na nchi yetu,  njia ya msingi ya kufanya hivyo ni elimu.
Aidha Dk. Bilal, aliwataka Waislam kufuata kanuni za msingi za dini yao, ili kuepuka machafuko yanayoweza kujitokeza.
“Utaratibu huu wa kiislam kuwa na kanuni za msingi ni  muhimu sana, na tutakapoacha kuufuata ndipo tutakapoanza kuuana na kuua kwa kisingizio cha dini. Kanuni za msingi za kiismlam ndizo zinazolinda dini ya kislam, Waislamu wenyewe pamoja na dunia nzima,” alisema.
Makamu wa Rais alisema: “Nimeeleza hayo kwa sababu  mimi na wenzangu serikalini tumeanza kuingia wasiwasi kwani hivi karibuni kumetokea vurugu ambazo hatimaye zimeashiria kuvunjika kwa amani ya nchi, mali zimepotea na wengine wamepoteza maisha kwa kisingizio cha dini.”
Pia alisema kila Muislamu lazima afundishwe namna ya kuwa Muislamu wa kweli na anayefahamu Qur-an,  na kufundishwa namna ya kuwa na amani na upendo  utakaowakomboa watu wote.

Saturday, December 15, 2012

JUMLA YA MAONI YA KATIBA FEKI INAYOPANGWA KUIMEZA NCHI YETU YA ZANZIBAR– ZANZIBAR NZIMA



SHEHIASER 1SER2SER3MKATABAMAONI MENGINEYO
Chachani042415734
Tibirinzi01211113
Mfikiwa2901261
Wawi1482631
Vitongoji02611140
Chanjamjawiri1690913
Pujini0240842
Gombani02121431
Wara0190945
Ndagoni01310460
Wesha0182860
Ng’ambwa02101080
Ziwani1133480
Makombeni0690503
Ng’ombeni0921933
Mbuguani06601780
Kangani02602092
Chokocho05601560
Mkanyageni010201960
Mtambile03101860
Kengeja03501000
Kiwani05102506
Muambe06701290
Ukutini02201980
Ngwachani04002300
Wambaa03031370
Polisi09010
Mzuri0200500
Mtende0400250
Kibuteni02130
Michamvi0170153
Kizimkazi051270
Kizimkazi0240230
Kitogani0380110
Muyuni0160470
Jambiani0550440
Paje0250468
Makunduchi0780394
Kajengwa0690484
Mwera01420261
Kiboje01360111
Ndijani05901082
Charawe0470571
Bambi0660183
Umbuji034033
Uzini01365400
Mchangani0570200
Chwaka07702795
Uroa0820221
Bungi111301430
U/Ukuu06305010
U/Ukuu0613486
Uzi05102080
Selemu21501381
Utaani11301960
Pandani11301983
Bopwe020013316
Ukunjwi0701052
Limbani019019314
Gando01102740
Raha0101249
Kangagani010017911
Ole0802300
Kiyuyu01001774
Kambini0402637
Shengejuu0501352
Kiungoni0501852
Kojani09016119
Chwale05013610
Maziwani070964
Uondwe08016010
Makongeni0441734
Mzambarauni0111652
Kisiwani0611775
Junguni01101397
Piki0201847
Fundo01001649
Finya0110471
Kinyasini0130618
Mgogoni0706811
Kifundi07011510
Konde0907811
Msuka Magharibi0811264
Msuka Mashariki0501843
Kipange0001364
Tondooni01501169
Makangale0905314
Kinoe1311802
Chimba0601284
Tumbe mashariki03014812
Tumbe magharibi010858
Sizini0601526
Shumba viamboni020999
Majenzi022353
Micheweni0302915
Shumba mjini0714717
Mjini wingwi084507
Maziwa ng’ombe162373
Kiyuyu Mbuyuni0110465
Mapofu050672
Njuguni0205612
Wingwi kinazini040467
Mtemani31501615
Wingwi mjananza12211715
Fukuchani0120100
Kidoti1350272
Kilimani0180295
Tazari0301371
Kilindi030764
Nungwi0231373
Potoa0222311
Muange0171402
Pita na zako0100201
Kibeni0160251
Kivunge0170160
Mkwajuni0150291
Kandwi040212
Pwani Mchangani0100303
Kigomani0150293
Kijini0200341
Chutama0331171
Moga034020
Masingini030010
Chaani Kikombweni0210200
Kinyasini0360160
Kisongoni0180111
Banda Maji036070
Mkokotoni0200270
Mto wa pwani031070
Pale023081
Tumbatu Jongowe0100232
Tumbatu Gomani0180130
Kilombero021312
Upenja1151111
Kiwengwa020080
Mgambo016081
Mahonda024130
Kitope020040
Kazole021030
Fujoni017081
Mangapwani021210
Bumbwini misufini0110120
Makoba014080
Kidazini013130
Kiongwe080150
Bumbwini Mafufuni0110140
Muanda024030
Donge vijibweni023000
Donge kipange026100
Donge Karange025000
Donge Mbiji017100
Donge Mtamble023000
Donge Mnyimbi017000
Mbaleni035020
Mkadini027070
Zingwe Zingwe020000
Kinduni021040
Pangeni019020
Kiomba mvua011091
Donge njia mbili019092
Mtoni kidatu0472525
Mtoni0160813
Sharifumsa1161342
Mtopepo0161541
Mwanyanya0282742
Bububu1242707
Kihinani02351143
Mfenesini1246792
Mbuzini1582271
Kama0154741
Mwakaje01581100
Kizimbani01200120
Kianga0871510
Kibweni0540140
Mwera0730265
Mtofaani0760750
Welezo0400490
Kwerekwe0350441
Melinne0841670
Tomondo0350811
Fuoni0740540
Kijitoupele0740510
Dole0119070
Kinuni03401350
Kiembe Samaki0710191
Pangawe0480660
Magogoni0330660
Mombasa0720481
Fumba0290343
Maungani0740103
Dimani0870250
Chukwani0510260
Shangani02001005
Malindi0200803
Kisiwandui0470450
Muemberikunda0740840
Kwahani0610210
Kibandamaiti0570570
Kwaalimsha0670490
Magomeni00000
Meya0260920
Mpendae00000
Matarumbeta0950350
K/Chekundu0870462
Jang’ombe Urusi0820731
Migombani0710911
Nyerere0730850
Sebleni0810621
Rahaleo05601210
Makadara 0 84 0 61 3
Kwamtipura
Mkele
Chumbuni
Karakana
Kilimahewa
JUMLA22685010314826572