Sunday, March 31, 2013

FAR-RIGHT DUTCH POLITICION FINDS ISLAM ALHAMDULILAHI


AMSTERDAM – A leading member in far-right Dutch politician Geert Wilders’ party has reverted to Islam after an extensive study about the Islamic religion and Muslims.
“I can understand people are skeptic, especially that it is unexpected for many of them,” Arnoud Van Doorn told Al-Jazeera English satellite channel.
“This is a very big decision, which I have not taken lightly.”
The news about Doorn’s reversion first came to the surface last month when he tweeted “new beginning”.
He later posted a tweet in Arabic pronouncing the Shahadah (proclamation of faith).
The politician later announced that he reverted to Islam, giving no more information about the reasons behind the decision.
“In my own close circle people have known that I have been actively researching the Qur’an, Hadith, Sunnah and other writings for almost a year now,” he said.
“In addition, I have had numerous conversations with Muslims about the religion.”
Driven by his party’s anti-Islam discourse, Doorn decided to dig in for the truth about the religion himself.
“I have heard so many negative stories about Islam, but I am not a person who follows opinions of others without doing my own research,” he said.
“Therefore, I have actually started to deepen my knowledge of the Islam out of curiosity.
“My colleague Aboe Khoulani from the City Council in The Hague has brought me further into contact with the as-Soennah mosque, which has guided me even further.”
A member of the Dutch parliament and The Hague city council, Doorn’s name has long been associated with Wilders’ anti-Islam, far-right PVV party.
Wilders himself is known for his rants against Islam, Muslims and the Noble Qur’an.
New Beginning
Doorn’s decision to embrace Islam has won mixed reactions in the Netherlands.
“According to some people I am a traitor, but according to most others I have actually made a very good decision,” he told Aljazeera.
“The reactions are generally positive and I also received quite some support via twitter.
“It feels good that people who do not know me personally have understanding of my situation and support me in my choice.”
For the Dutch politician, finding Islam was finally guiding him to the true path in his life.
“I have made mistakes in life as many others. From these mistakes I have learned a lot,” Doorn said.
“And by my conversion to Islam I have the feeling that I finally found my path.
“I realize that this is a new start and that I still have much to learn as well.”
Departing from his earlier life as a PVV member, Doorn expects much resistance in his political life.
“The expectation is that I will continue to face much resistance, also from certain government institutions,” he said.
“I have all faith in Allah to support me and to guide me through these moments.”
MASHAA ALLAH.

WAZANZIBARI MTAKUBALI NCHI YENU KUNAJISIWA....???

Kwa upande wa nchi ya Tanyika ijitayo ((Tanzania Bara)) ikiwa wao watasema nchi yao haina dini basi kivyao huko huko Tanganyika kwenye nchi yao. maana takwimu za wapi na wapi wengi zinagongana huko nchini Tanagnyika. wakristo wasema wao ni wengi na waislamu husema hivyo hivyo sasa wameamua kuiachia Serekali yao ya Tanganyika kusema na kujita kuwa haina dini.
Lakini kwa upande wetu wa nchi yetu ya  Zanibar nchi yetu ina dini kuanzia viongozi wetu wa Smz japokuwa ni wanafiki lakini ni waislamu mpaka raia wake (wananchi wa Zanzibar ) % 100 ya Wazanzibar ni waumini wa dini ya kislamu na ndio wenyeji hilo mukitaka musitake ndivyo ilivyo .
Sasa kusema kuwa nchi ya Tanganyika haina dini na sisi nchini kwetu Zanzibar tutawangalia tu.lakini mukitaka kutulazimisha na sisi pia kuwa nchi ya Zanzibar kwa kuwa tuna muungano feki basi pia sisi hatuna dini hilo halitokuwepo hatuta kubali kulishwa matapishi ya siasa kwa maelekezo ya Kanisa katoliki ,kuwa mtu anaweza kuishi popote katika nchi hizi mbili na kuhubiri dini popote pasipo na kuingiliwa ni moja.
Hili ni kosa na ndio mwanya wanao utumilia kanisa kwa kueneza ukristo katika nchi yetu ya  Zanzibar na kutuharibia mila zetu na utamaduni wetu asilia ambayo inatokana na dini yetu, hii ndio shabaha na agenda kubwa ya kanisa kotoliki kuifunika nchi yetu ya  Zanzibar kwa kujiegemeza kisiasa Zanzibar na kuwazowa mawazo viongozi wa Smz kwa kujifanya Maskofu siku zote wao ni victim wa waislamu wa Zanzibar. kama huyu moja aliyesema na kutia fitina namnuku((Matokeo yanayotokea Zanzibar mathalan, Wakristo wanaoishi huko yamewasababishia hofu, hivyo wengi kuanza kuvikimbia visiwa hivyo na kukimbiliaTanzania Bara.”)) alikuwa aseme kweli kuwa hatufanikiwi Zanzibar kama tunavyo taka na sasa rai wetu wa Tanganyika wanarudi nyumbani. lakini kasema vile kama kwamba ni wote ni wazaliwa wa Zanzibar na hawaishi kwa raha na inawabidi wakimbiye huu ni umoja wa uchocheze na kupandikiza chuki.
Hizi ni mbinu tena hatari na muelekeo wa viongozi wetu wa Smz inaonekana ni mbaya na huenda wakapotea/kupotezwa na kubebeshwa zima mbele ya Allah.
Ikiwa leo nusu ya Masheikh wetu wako magerezani kwa mbinu na ujanja wa maskofu wa kanisa katoliki sumu zao , hii ni hatari maana wenyeji hawana right katika ardhi yao lakini Maskofu wakuja wana amri na inatekelezwa zidi ya kuhujumiwa waislamu na uislamu ndani ya ardhi yao nihatari tena kubwa sumu hii wanayo spry Maskofu wa kutoka nchini  Tanganyika ambayo imeshika kasi.
Hivi karibuni tu askofu mkuu Pengo katowa amri mumeona kimetokea nini  nchi Zanzibar. sasa kanisa limeshika hatamu Zanzibar na viongozi wetu wa Smz wako nyuma ya kanisa bila kujijuwa wapi wanatoka na wao ni nani mbele ya Wazanzibar walio wengi.
Hii ni hatari na ikiwa tutacheka nayo basi viongozi watatupoteza na kutafuta njia ya kutokea itatushinda na sote itakuwa ndio tulokula hasara mbele ya Allah.
Mimi naona kuchelewa kuufa au kuuwa huu Muungano feki ndio kunaipa nguvu kanisa na watu wake kutuletea mambo ya kimajabu katika ardhi yetu na dini yetu kuingiliwa na kuharibiwa kwa hujuma za Muungano feki.
TUTAKWENDA KUMUAMBIA NINI MWENYEZI MUNGU IKIWA TUTAIWACHA ARDHI ALIYOTUPA KUFISIDIWA....??? VIONGOZI,RAI,WANAUME,WANAWAKE NYOTE MTAULIZWA VIPI ULITETEA NCHI YAKO NA ARDHI NILIYO KUPA KUMBUKA MZANZIBARI MAUTI HAYAPO MBALI NA MASWALI NI MENGI.

Friday, March 29, 2013

BALA NCHINI TANGANYIKA JUMBA LA GHOROFA LAPOROMOKA


jengo la ghorofa languka jijini dar nchini Tanganyika


hamkani zaenea jijini dar nchini Tanganyika

hii ndio kasheshe iliyo zuka nchini Tanganyika kwa kuanguka jengo la ghorofa huku raia wakishuhudia na kupiga picha  


raia wakijarabu kuchimba chimba kutafuta maiti na watu ikiwa kutakuweko aliyekuwa hai


wakiendelea kuchimba na kutowa magari yaliyo angukiwa na jumba hilo la ghorofa

SHEIKH RASHID NASSOR AL-BATASHI AFARIKI DUNIA


Tunapenda kuwatangazia kifo cha Sheikh wetu Rashid Nassor Al Batashi kilichotokea leo huko Hospitali ya Mnazi Mmoja na mwili wake utasaliwa katika Msikiti wa Jumuiya ya Waarabu Rahaleo baada ya sala ya Ijumaa na maziko yake yatafanyika nyumbani kwake Mlandege. Inshallah Mwenyeenzi Mungu amrahisishie safari yake na ampe kauli thabit na ampe pepo. Ameeen
Sheikh Rashid ni miongoni mwa wanazuoni maarufu hapa Zanzibar na wamefanya kazi kubwa katika kuitangaza dini ya kiislamu na kufundisha maadili ya dini hiyo, mchango wake kwa jamii ni mkubwa sana mbali na taaluma yake ya kufundisha darsa lakini alikuwa akisomesha watu katika maisha kawaida na namna ya kuishi kwa kufuata kitabu kitukufu cha Allah Quraan, na akiwausia vijana sana suala la kumcha Mwenyeenzi Mungu na kuachana na utamaduni usiokuwa wetu wa kuishi na wanawake kabla ya kufunga ndoa, Sheikh Rashid atakumbukwa kwa mengi lakini suala hilo alikuwa akilikemea kwa nguvu sana Allah atampa ujira wake inshaallah.Sheikh Rashid alikuwa akiudhika sana wanaume na wanawake kuishi pamoja kinyumba au kutenda maovu kabla ya kuoana zinaa, Sheikh Rashid katika uhai wake tunafahamu alikuwa akifungisha ndoa lakini ni mtu pekee akionesha msimamao wake hadharani bila ya kujali kwamba anaowafungisha ndoa ni watu wa karibu yake au jamaa zake au ni watu wenye familia kubwa kubwa na iwapo watakuwa anaotaka kuwafungisha ndoa wametembea kimwili kabla ya kufunga ndoa alikuwa akikakabili kwanza na kuwauliza na iwapo wamefanya hivyo alikuwa akikataa kuifunga ndoa hiyo na mara kadhaa ameshawahi kwenda kuzivunja ndoa hizo akisema hataki kuchukua jukumu mbele ya Allah.
Sheikh Rashid alikuwa kiishi maisha ya kawaida sana na kama mnavyomuona hapo kwake yeye mkubwa mdoo ni sawa na akiwa heshima sana akipenda sana kusimama na kuwasalimia watu na hawezi kuwasalimia tu bali hukupa maneno mawili matatu ya hekima na kuwaombea dua kabla ya kuondoka. Basi kwa wema na matendo hayo ambayo mengi ameyafanya na kuyatenda wakati wa uhai wake basi hatuna budi kwa pamoja kumuombea dua kwa Mola wetu Mlezi Mwenyeenzi Mungu amlaze mahali pema na amjaalie kaburi lake liwe miongoni mwa mabustani ya Peponi Yarabbiy. (AMEEN)

SALIM HEMED KHAMIS MBUNGE WA CHAMBANI PEMBA(CUF)AFARIKI


KWA UFUPI
HUZUNI,MAJONZI,MASIKITIKO,VILIO VYA ENEA BAADA YA KIFO CHA SALIM HEMED KHAMISI ALIYEKUWA MBUNGE WA CHAMBANI PEMBA(CUF)
Mbunge wa Chambani (CUF), Salim Hemed Khamis (60) amefariki dunia jana katika hospitali ya Taifa Muhimbili nchini Tanganyika (MNH) alikokuwa amelazwa baada ya kuanguka ghafla juzi kwenye Ofisi za Bunge, Dar es Salaam.
Kifo cha mbunge huyo kimewagusa wakiwemo wabunge na raia wa kawaida. Ofisi ya Bunge imethibitisha kutokea kwa kifo hicho cha mbunge huyo na kueleza kuwa, alipatwa na ugonjwa wa kiharusi uliosababishwa na ugonjwa wa moyo (Hypertension).
Khamis anatarajiwa kusafirishwa kisha kuzikwa leo kijijini kwao Chambani, Pemba baada ya jitihada za kumsafirisha jana kushindikana na wabunge wengi kuomba kushiriki katika maziko yake.
Mbunge huyo atasafirishwa leo asubuhi baada ya shughuli ya kuaga itakayofanyika kwenye Viwanja vya Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
 
Khamis alianguka juzi saa 10.50 asubuhi wakati akishiriki kwenye kikao cha Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kilichofanyika katika ofisi za Bunge jijini Dar es Salaam.
Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel alisema wamepokea taarifa za kifo hicho kwa masikitiko ambacho kilisababishwa na kupasuka kwa mshipa wa damu kichwani.
“Tumeelezwa na daktari kuwa Mbunge Salim amefariki kutokana na kupasuka kwa mishipa ya damu ambayo ilimiminikia kwenye ubongo wake na kuenea kichwani,” alisema Joel. Alisema kutokana na hali hiyo shughuli zote za uchambuzi wa bajeti zilizokuwa zikifanywa na kamati za Bunge, zimeahirishwa kwa mujibu wa taratibu zilizopo hadi tutakapomaliza shughuli za mazishi.
Joel alisema kwa upande wa Bunge, shughuli za msiba zitaongozwa na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ambayo marehemu alikuwa mjumbe.
 
Wabunge, CUF waomboleza
Baadhi ya wabunge jana walionekana kuchanganyikiwa baada ya kupata taarifa za msiba huo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti walisema kuwa kifo hicho ni cha ghafla kwa sababu Salim alikuwa kwenye vikao vya Bunge tangu walipoanza vikao vya kamati.
“Tangu tuanze vikao vya kamati tulikuwa naye na alionekana kuwa mwenye afya, kwangu mimi ni pigo nimepata kwa sababu alikuwa mwalimu kisiasa katika Chama cha CUF,” alisema Rajab Mohamed Khamis, ambaye ni Mbunge wa Ole (CUF).
Kwa upande wake, Mbunge wa Peramiho CCM, Jenister Mhagama alishtuka na kuonekana kutoamini taarifa hizo, jambo ambalo lilimfanya ashindwe kuzungumza chochote.
Wabunge wengi walionekana wakihaha kutafuta usafiri ili wawezekwenda Muhimbili huku baadhi yao wakienda kujiandaa na safari ya kwenda Pemba.

Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro alisema chama chake kimepata pigo kubwa kutokana na kifo cha Mbunge, ambaye amemwelezea kwamba alikuwa nguzo muhimu kwa chama hicho.
Mtatiro alisema marehemu alikuwa na mchango mkubwa kwa chama chake kutokana na shughuli mbalimbali alizokuwa akizifanya katika chama hicho.
Alisema kuwa marehemu ndiyo alikuwa Mnadhimu Mkuu wa Wabunge wa CUF, pia alikuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi wa chama hicho kuanzia mwaka 2010 hadi 2012.
“Pia alikuwa anatusaidia sana wakati tukiwa na migogoro kwani kutokana na busara zake alikuwa anaheshimika sana,” aliongeza Mtatiro.
Kuumwa kwake
Alianza kujisikia vibaya akiwa kwenye kikao cha kamati juzi na alianguka hivyo wabunge wenzake kwa kushirikiana na Ofisi ya Bunge walimchukua na kumpeleka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu.
Alilazwa kwenye chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu, hadi alipokutwa na mauti jana.
Miezi mitatu iliyopita alikuwa nchini India katika Hospitali ya Apollo kwa ajili ya matibabu na alirejea nchini na kuendelea kushiriki shughuli za Bunge na za chama chake.
Hoja ya mwisho kuchangia katika vikao vya kamati ni ile ya Machi 26, mwaka huu, pale alipoukosoa Mpango wa Afrika Kujitathmini Kiutawala Bora (APRM) kwa kushindwa kutoa taarifa za kweli kuhusu rushwa kwenye taasisi nyeti zikiwemo polisi, magereza na hospitali.
Rekodi Bungeni
Khamis aliingia bungeni kwa mara ya kwanza 2005 na kuchaguliwa tena 2010. Katika Bunge la 10 aliuliza maswali ya msingi matano, ya nyongeza saba na alichangia hoja mbalimbali mara 18.
Historia yake
Mbunge huyo, ambaye alizaliwa mwaka 1952, alisoma Shule ya Msingi Pandani kati ya 1959 na 1960 na kumalizia katika Shule ya Msingi Kengeja kati ya 1960 na 1967.
Elimu ya sekondari aliipata kati ya 1968 mpaka 1969 katika Shule ya Chambani na kuhamia Shule ya Fidel Castro aliposoma kati ya 1970 mpaka 1971. Kati ya 1972 hadi 1973 alikuwa katika Chuo cha Lumumba kwa shahada yake ya kwanza ya Kilimo.
Alisoma shahada yake ya uzamili katika Chuo cha Commonwealth Mycological cha Uingereza kati ya 1988 hadi 1989.
Kabla ya kuwa mbunge alifanya kazi sehemu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwa Mwalimu kati ya 1974 mpaka 1978, huku 1984 mpaka 1996 akifanya kazi katika Kampuni ya Mohamed Sugar.
1997 alijiunga na Kampuni ya SAS Ltd alipofanya kazi mpaka 2001 kabla ya kupata Ubunge 2005 hadi mauti ulipomkuta.
Salim ni mbunge wa kwanza kufariki kwa mwaka huu, ingawa katika Bunge hili anakuwa Mbunge wa nne.

Wabunge wengine waliofariki ni Mussa Khamisi Silima wa Zanzibar, Mbunge wa Viti Maalumu wa Chadema Regia Mtema pamoja na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Jeremia Sumari.

Thursday, March 28, 2013

MBUNGE WA CHAMBANI (CUF) ANGUKA BUNGENI DODOMA


Mbunge wa Chama Cha Wananchi (CUF) Jimbo la Chambani,
Salim Hemed Khamis afariki dunia,
Mbunge huyo ambaye siku za hivi karibuni ametoka nje ya nchi kwa matibabu ya afya yake amefikwa hali hiyo na kubebwa na baadhi ya wabunge kwa kushirikiana na baadhi ya wandishi wa habari kutolewa nje ya chumba cha mkutano na kupelekwa hospital ya taifa ya Mhimbili kwa uchunguzi na matibabu zaidi.
Mwenyekiti wa kamati ya bunge ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Edward Lowasa jana amethibitisha kutokea kwa tukio hilo la kuanguka ghalfa.
Mbunge huyo jana alikutwa na mtihani huwo jana na alikimbizwa hospitalini kwa matibabu ambako alilazwa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu (ICU).
Wajumbe wa kamati hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Edward Lowassa, na Makamu Mwenyekiti, Mussa Hassan Zungu na baadhi ya wajumbe walimtoa nje ya ukumbi na kumpepea kwa kutumia magazeti na majarida ili apate nafuu.

Hata hivyo, hali yake ilizidi kuwa mbaya huku akizungumza kwa tabu kuwa alikunywa dawa za shinikizo la damu (BP) kabla hajala chochote na hivyo kuzidiwa.
Wabunge hao na maofisa wa Bunge, waliendelea kumpepea ili apate afueni, lakini hali ilizidi kuwa mbaya na kushindwa kuongea kila alipoulizwa jambo.
Walimbeba na baada ya muda waliomba msaada kwa wanahabari waliokuwapo eneo hilo huku wakiwazuia wasipige picha za tukio hilo kwa maelezo kuwa si kila kitu ni habari.
Waandishi watano walisaidiana na wabunge hao kumbeba kwa kupitia mlango wa dharura na alipakiwa kwenye gari la ofisi ya Bunge lenye namba za usajili STK 2178 likiongozwa na pikipiki ya polisi yenye namba za usajili PT 2591.
Gari iliyombeba Mbunge huyo iliondoka kwenye ofisi hizo saa 5:15 asubuhi na habari zilizopatikana baadaye zilieleza kuwa alipelekwa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Baadhi ya wabunge walisema kuwa Khamis akiwa amekaa, ghafla alianza kutapika huku akilalamika kuwa hajisikii vizuri baada ya kunywa dawa za (BP) na hali yake kubadilika na walisaidiana kumtoa nje ya chumba cha mkutano.
Waliomsindikiza hospitalini ni Mbunge wa Mpanda Mjini, Said Amour Arfi (Chadema) na Mbunge wa Gando, Khalifa Suleiman Khalifa (CUF).
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kurejea kutoka Muhimbili, Khalifa alisema Khamis alipokewa na alikuwa anaendelea kupatiwa matibabu.
Khalifa alifafanua kuwa Khamis anasumbuliwa na tatizo la shinikizo la damu. Mwenyekiti wa kamati hiyo, Edward Lowassa, alisema hali yake ilikuwa inaendelea vizuri na kuthibitisha kuwa amelazwa ICU. Lowassa alisema kuwa miezi mitatu iliyopita Khamis alikuwa India kwa matibabu. Ofisa Uhusiano wa Muhimbili, Aminiel Eligaesha, alipoulizwa kwa njia ya simu, alithibitisha kuwa mbunge huyo kupokewa hospitalini hapo na kuongeza kuwa alipatiwa matibabu na anaendelea vizuri. Hata hivyo, alisema taarifa kamili itatolewa na ofisi za Bunge.
Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel, alisema hadi jana jioni mbunge huyo alikuwa bado ICU chini ya uangalizi wa madaktari. “Bado yuko ICU. Wanamwangalia. Presure (shinikizo la damu) iko juu, tunampumzisha kidogo,” alisema Joel akijibu swali kuhusu maendeleo ya afya ya mbunge huyo. Akijibu swali iwapo kuna mpango wowote wa kumpeleka mbunge huyo kupatiwa matibabu zaidi nje ya nchi, alisema: “Tunasubiri ushauri wa madaktari.”

Wednesday, March 27, 2013

MASWALI TELA MTAKAYO ULIZWA JE MNAYAJUWA ......??????


M/MUNGU ANAYAJUWA YALIYOKUWA NDANI YA VIFUA VYENU ANAJUWA YALIYO NDANI YA NYOYO ZENU NA SIKU YA KIYAMAA MUTAULIZWA JE MULIKUWA VIONGOZI WADILIFU..?
VIONGOZI MULIO CHANGULIWA NA UMMA..?
VIONGOZI WENYE KUJALI WATU AU FAMILIA ZENU TU..?
VIONGOZI WAUMINI WA KWELI AU RIYAA TU KUONYESHA KAMA NI WAUMINI KUMBE SIO..?
VIONGOZI MULIO KULA MISHAHARA YA HALALI..?
NA MENGINE MENGI YATAFUATIA JITARISHENI MZEE KARUME YUKO WAPI..?
NYERERE YUKO WAPI..?
SOKOINE YUKO WAPI..?
DR OMAR ALI JUMA YUKO WAPI..?
 HAPA NDIPO KILA MOJA ANAJUWA KUWA MOLA HANA CHA RAISI WALA MUUZA DAGA,MBUNGE WALA MUUZA MADAFU MAKAMO WA RAI WALA MPIGA DEBE
NYUMBA ULIZOJENGA MAGARI ULIYO JINUNULIA MASHAMBA ULIYO NYANGANYA YOTE UTAYAWACHA HAPA HAPA DUNIANI HUMU UTAINGIA NA SHUKA JEUPE TU SANDA

MKOA WA ZANZIBAR UMEPATA NINI KUJA KWA RAISI WA CHINA..????



YEAAAA MIMI PIA NIMEMPA MKONO RAISI WA CHINA YEEEEEEE HAHAHAHAH

YUSSUF MZEE UNASAINI MIKATABA MKOA ZANZIBAR UMEPATA NINI KATIKA KUSAINI KWAKO..??

KATI YA CHADEMA NA CUF NANI NI CCM B..????

Chama cha Demokrasia na Maendeleo – CHADEMA, kuelekea uchaguzi wa 2010 kilikuja na mkakati wa kupambana na vyama wenzake vya upinzani hususan CUF kwa lengo la kushikilia nafasi ya chama cha kwanza chenye nguvu cha upinzani. Kilitekeleza na kinaendelea kutekeleza mkakati huu kwa kutumia mbinu mbali mbali kama vile kukituhumu chama cha CUF na kukihusisha na Uislamu na Kukibandika jina la CCM-B. Pumbazo hilo lilisimamiwa vyema na CHADEMA na watanganyika wakapumbazika na kudhani CHADEMA ndio chama mbadala cha kuwatetea wanyonge na makabwela wa Tanganyika.
Sababu kuu iliyotolewa na CHADEMA juu ya u-CCM B wa CUF ni hatua ya kuundwa kwa serikali ya Umoja wa kitaifa Zanzibar baina vyama vya CUF na CCM baada ya uchaguzi mkuu wa 2010. Chadema waliipa CUF tuhuma hii ya u-CCM B wakifahamu kwamba serikali hiyo ya umoja wa kitaifa ya Zanzibar imeundwa ili kuzima chuki, ubaguzi, migogoro, hasama na mpasuko mkubwa wa kisiasa uliodumu Zanzibar kwa miaka mingi, na hivyo kuwa njia pekee ya suluhisho la wazanzibari kuishi kwa amani na utulivu. CHADEMA haikufurahia hayo na inafahamu kwamba hakuna chama kilichoungana na mwenzake kati ya vinavyounda serikali ya Umoja wa kitaifa Zanzibar. Kila kimoja kati ya hivyo kina ajenda zake, mitazamo yake, misimamo yake na sera zake. Kila chama kati ya hivyo kinazisimamia itikadi na imani zake kwa nguvu zote. Jambo hili liko wazi kabisa kwani ukiachilia hali ya amani na utulivu iliyopatikana nchini Zanzibar tofauti za mitazamo na mapambano ya hoja na mijadala mikali baina ya CUF na CCM Zanzibar juu ya agenda mbali mbali za kisiasa zipo pale pale. Halkadhalika CHADEMA wanafanya hivi wakifahamu kuwa serikali za pamoja, serikali za mseto na serikali jumuishi ndio mifumo ya kisasa ya kiserikali duniani huku na wao wakiwa ni chama rafiki na vyama kadhaa vinavyounda serikali za aina hii duniani.
Uchaguzi mdogo wa jimbo la Bububu uliyofanyika nchini Zanzibar mwezi wa Septemba 2011 ndani mfumo wa serikali ya umoja wa kitaifa umeonyesha wazi kwamba hakuna vyama vilivyoungana kwani CUF ilipambana kama kawaida yake kudhibiti wizi wa kura unaofanywa na CCM miaka yote huku na CCM nao wakitumia ubabe na hata kufikia kutumia risasi za moto ili kushinda uchaguzi huo kwa hila. Hata hivyo wakati CHADEMA wakiita CUF ni CCM B, chama hicho kimekuwa kikitumia wanasheria wake na makada wake kuwatetea watuhumiwa wakuu wa ufisadi mahakamani. Chama hicho pia kimekuwa kikishuhudiwa kuwa na utamaduni wa kubadilishana wanachama baina yake na CCM. Utamaduni uliozoeleka wa mwanachama wa CHADEMA anapoamua kukihama chama hicho huhamia CCM badala ya kuhamia vyama vyengine vya upinzani ni suala linoloashiria usiri mkubwa juu ya kuwepo mahusiano maalum baina ya vyama hivi viwili.
 
 

hii ni siku ya uchanguzi wa bububu uliosababisha polisi kuwafatulia risasi wafuwasi wa cuf na kusababisha kifo cha mtoto mwenye umri wa miaka 14
 
Makada na matajiri wa CCM wazi wazi wamekuwa wakikifadhili chama cha CHADEMA kwa mamilioni huku CCM ikikaa kimya wakati Bahresa aliwahi kutuhumiwa tu kuifadhili CUF na kupelekea CCM kuharibu mali zake za mamilioni ya pesa. Baada ya kubainika suala hilo ni uzushi, Bakhresa alishinda kesi mahakamani na kulipwa fidia. Mbona Mustafa Sabodo hapokei bugudha yoyote katika biashara zake au kufukuzwa uwanachama wa CCM kwa tabia yake ya kuifadhili CHADEMA mamilioni ya pesa? Viongozi wa CUF walikuwa wakikamatwa ovyo na kufikia hadi kufungwa miaka kadhaa jela bila ya kuwa na hatia. Viongozi wa CHADEMA wanaonekana wazi wakihamasisha na wakifanya vitendo kadhaa vya kuvunja amani ya nchi huku CCM na dola ikiwatazama na ikiwaogopa na wao wanaendele kupeta tu
Jeshi la polisi likiandamana na kuwalinda CHADEMA katika barabara
 
Wanachama wa CUF walipoamua kudai haki zao dhidi ya unyanyasaji wa dola walikiona cha moto kwa kuvamiwa vijiji vyao, kuvunjiwa nyumba zao, kuibiwa mali zao na kuharibiwa mali zao, kubakwa, kupigwa risasi, kutiwa ulemavu na kuuliwa. Wakati hayo yamekuwa yakifanywa na CCM dhidi ya CUF inaonekana hali ni tofauti kwa CHADEMA, kwani ama huachiwa wafanye watakavyo au kwa ustaarabu polisi hupambana na CHADEMA bila ya kufanya unyama wa mauwaji ya kutisha kama wanavyofanyiwa CUF, ubakaji na uharibifu wa mali kama inavyofanywa kwa CUF na wana CUF kulazimika kuhama majumba yao na miji yao kwa miezi kadhaa huku familia zao zikiteseka. Hali hufikia mbali zaidi kwani viongozi wa dola huchukua hatua ya kuwaita viongozi wa CHADEMA na kuzungumza nao na kuweka makubaliano ili kuepusha shari jambo ambalo halikuwahi kufanywa kwa CUF. Ipi ni CCM B kati ya CHADEMA na CUF dungu msomaji tupe jibu..???
Kada wa CCM, Mustafa Sabodo akimkabidhi Mbowe burugu la mamilioni kama msaada wake kwa chama hicho cha CHADEMA.
 
Kama hilo halitoshi kiashiria kipya kimepatikana kinachowapa watanganyika ushahidi wa wazi kwamaba CHADEMA ni CCM iliyovaa nguo nyengine na kamwe haina nia wala shabaha ya kupigania maslahi yao. Kile kinachozungumzwa na Viongozi wa CUF kwamba Tanganyika ((Tanzania)) hakuna chama kinachoonyesha nia safi ya kupigania maslahi ya watu zaidi ya CUF kimebainika. Katika sura ya kuwashangaza wengi chama cha CHADEMA kupitia kurugenzi yake ya Ulinzi na Usalama kimekua kikiandaa utekaji nyara wa watu na kuwapa mateso mabaya kwa watu kadhaa kwa malengo tofauti ya kujitafutia umaarufu na kuwapumbaza watanganyika. Hili halina tofauti na vitendo walivyovizoea watanganyika vinavyofanya na dola na wanamgambo wa CCM vya kuwavamia watu na kuwapiga, kuwanyanyasa na hata kuwauma bila ya sababu za msingi.
Matokeo kadhaa ya utekaji nyara na utesaji hapa nchini yamekuwa yakiumiza haswa wazanzibari mpaka kufikia kuomba ukimbizi Kenya na nchi nyengine. vichwa vyao na mara kadhaa kutupiwa lawama idara ya usalama wa Taifa kuwa inahusika. Imebainika kuwa si idara ya usalama wa taifa pekee kumbe na idara ya usalama ya CHADEMA ni mwanafunzi aliyehitimu kutekeleza vitendo hivyo vya kimafia vya CCM. Mkanda wa video uliochukuliwa kwa utaalamu wa hali ya juu uliomrekodi Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA sura halisi ya msingi wa utekaji nyara wa watu kadhaa hapa nchini na kuwatesa vibaya. Kiongozi wa Jumuiya ya madakatari Dr Ulimboka, mwanahabari mashuhuri Bwana Absalom Kibanda na wengine ni miongoni mwa watu waliotekwa nyara na kuteswa vibaya katika matukio tofauti.
Tanganyika na Zanzibar zimeshtushwa mno baada ya kupatikana ushahidi wa kutosha wa jambo hili kwamba kumbe CHADEMA na viongozi wake wanahusika katika kuratibu matukio haya kwa malengo binafsi na maslahi binafsi ya kisiasa ili kuwapumbaza watu. Inasemwa kwamba malengo makuu ya CHADEMA katika kufanya umafia huu ni 1. Kuyahusisha matukio hayo na idara ya usalama wa taifa kwa kuwa ndio iliyokuwa imezoeleka kufanya hivyo ili wananchi wazidi kuichukia serikali na CHADEMA izidishe matarajio umaarufu wake kupitia hadaa hiyo. 2. Kuwakomoa, kuwatisha na kuwaweka katika hali ya hofu na kutojiamini waandishi wa habari na wahariri ambao wanaonekana kuandika ukweli, kashfa na mwenendo usiofaa wa chama hicho na chama cha CCM pia.'
 
Mkurugenzi wa ulinzi na Usalama wa CHADEMA akiwa katika mpango wa utekaji nyara na umafia
natuone hatamu yake kama kweli ataishia jela au geresha tu kisha anachiwa na kula kuku wake
 
Watanganyika wanataka uchumi badala ya umasikini, wanataka amani badala ya mitafaruku na migogoro, wanataka umoja badala ya utengano na mifarakano, wanataka haki na usawa badala ya upendeleo na ubaguzi na ufisadi na wanataka kusonga mbele badala ya kurudi nyuma. Siamini hata chembe kama vita hivi vinaweza kushindwa kwa kufanya dhambi mbadala. Hivi ni kweli tunaweza kushinda rushwa kwa kuendesha vitendo vya rushwa mbadala..??? Kama hapana ndio hivyo hivyo hatuwezi kushinda vita dhidi ya maonevu na unyanyasaji unaofanya na CCM na dola kwa kufanya unyanyasaji mbadala tena dhidi ya wasio na hatia yeyote. Hivi ndivyo inavyofanya CHADEMA katika mwenendo wake mpya wa kufanya siasa zake za matayarisho ya kuchukua dola la TANGANYIKA na KULIONGOZA MWAKA 2015.
Siasa hizi za kigaidi na kijambazi za CHADEMA na viongozi wake ndio zinazopangwa kuitawala Tanganyika kigaidi na kijambazi pale watakaposhinda uchaguzi wa mwaka 2015. Watanganyika amkeni, si CHADEMA si CCM, vyote hivi si vyama vya kuyatetea maslahi ya watanganyika wanyonge. Vyote ni vyama vya unyanyasaji, mateso, uonevu, ukosefu wa huruma na ubinafsi. Tuviepuke kama ukoma. Mbadala wa siasa safi za Tanganyika na Zanzibar ni chama cha wananchi CUF chenye misingi imara ya kutetea haki sawa kwa watu wote vilivyo baki ni kufurisha matumbo yao na familia zao.


Tuesday, March 26, 2013

MASHEIKH WA UAMSHO WARUDISHWA TENA RUMANDE KESI HII KWELI ITAKWISHA HIII!!!!


  • Haieleweki ni vipi viongozi hao wanashikiliwa huku upelelezi au uchunguzi ukiwa haujakamilika je nikushikiliwa au nikuwakomowa..?
KESI ya jinai inayowakabili viongozi wa Dini wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI) imeanza kusomwa upya leo katika Mahakama Kuu ya Zanzibar baada ya maamuzi ya awali kutenguliwa.
Kesi hiyo namba 9 ya mwaka 2012 ilisomwa mbele ya Jaji Fatma Hamid Mahmoud na Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ramadhan Nassib, ambae aliwataja washitakiwa hao kuwa ni Farid Hadi Ahmed (41) mkaazi wa Mbuyuni,Msellem Ali Mselem (52) mkaazi wa Kwamtipura, Mussa Juma Mussa (47) mkaazi wa Makadara na Azzan Khalid Hamdan (48) mkaazi wa Mfenesini mkoa wa Mjini wa Magharibi Unguja.
Wengine ni Suleiman Juma Suleiman (66), mkaazi wa Makadara, Khamis Ali Suleiman (59) mkaazi wa Mwanakwerekwe, Hassan Bakari Suleiman (39) mkaazi wa Tomondo, Ghalib Ahmada Juma (39) mkaazi wa Mwanakwerekwe na Abdallah Said (48) mkaazi wa Misufini mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.
Washitakiwa wote kwa pamoja walisomewa mashtaka matatu ikiwemo kuharibu mali, Uchochezi, Ushawishi na kuhamasisha fujo na kosa la tatu ni kula njama ya kufanya kosa huku kosa la nne likimkabili mshitakiwa namba nne Azan Khalid ambae anadaiwa kufanya vitendo vinavyoweza kusababisha uvunjifu wa Amani.
Makosa yote hayo yandaiawa kufanyika kati ya Oktoba 17,18 na 19 katika maeneo tofauti ambapo washitakiwa hao walipotakiwa kujibu tuhuma zao walizikana.
Mara baada ya kuwasomea mashitaka hayo, Mwendesha Mashtaka wa Serikali,. Nassib alidai kuwa upelelezi wa shauri hilo tayari umeshakamilika lakini hata hivyo aliiomba mahakama hiyo kufanya subra ya kuweza kuamuwa maamuzi yoyote kutokana na upande huo wa mashtaka kukata rufaa kitendo ambacho alisema kwamba iwapo mahakama hiyo itaendelea na kesi hiyo kunaweza mahakama ya rufaa ikatoa maamuzi ambayo yataweza kuathiri maamuzi ya mahakama hiyo.
Kwa upande wa mawakili wa watetezi uliokuwa ukiongozwa na Salim Toufiq, Abdallah Juma na Suleiman Abdallah, uliiomba mahakama hiyo kuwapatia dhamana washitakiwa wake hao hasa ikiangaliwa kuwa tayari washitakiwa hao wameshakaa ndani kwa muda
mrefu.

“Mheshimiwa Jaji tumefurahi kuona kwamba kwa mara ya kwanza upande wa mashtaka unatamka kuwa upelelezi umekamilika lakini isiwe sababu ya kuendelea kubakia rumande wateja wetu kwa vile muda wa kukaa kwao umekuwa mwingi na kupelekea haki yao ya msingi ya dhamana kunyimwa”,
alisema. Toufiq
Hata hivyo Jaji Fatma alisema kuwa atayachukuwa maombi ya pande yote mbili na kuyapitia kwa umakini ili baadae aweze kutoa maamuzi yaliyo sahihi kutokana na kuwa ni mgeni wa kesi hiyo na jalada lake amelipokea kwa muda mchache ambao haukupata nafasi ya kuipitia vizuri.
“Nayachukuwa maombi yote mawili nitayatafakari kwa kina na kuja kutoa uamuzi unaofaa”,
alisema Jaji huyo ambaye ni mtoto wa aliyekuwa Jaji Mkuu wa Mahakama hiyo aliyemaliza muda wake wa kustaafu mwaka jana.
Katika maamuzi ya Jaji Abraham Mwampashi alisema kesi hiyo inapaswa kuanza upya kutokana na kuwa mrajis hana mamlaka na pia kupinga maamuzi ya Mkurugenzi wa Mashtaka DPP kuwanyima dhamana wahutumiwa hao ambao wanakabiliwa na makosa mbali mbali ikiwemo kuhatarisha usalama wa nchi na kuharibu mali za watu binafsi na serikali, hata hivyo serikali ilikata rufaa kupinga maamuzi ya Jaji Mwampashi na kupangiwa jaji Fatma, kesi hiyo ameakhirishwa hadi Machi 27 mwaka huu, je kama si danadana ni nini..???

Sunday, March 24, 2013

MVUA YAZUWA MAFURIKO MAKUBWA NCHINI TANGANYIKA




  Mvua kubwa iliyonyesha nchini Tanganyika jana jijini Dar es Salaam, ilisababisha mafuriko makubwa katika baadhi ya maeneo, hivyo nyumba kadhaa kujaa maji na baadhi ya watu kulazimika kuyahama makazi yao.
Mafuriko hayo yaliyosababishwa na mvua iliyoanza kunyesha muda wa asubuhi, pia yalisababisha hasara kubwa kutokana na vitu na mali mbalimbali kuchukuliwa na maji.
Muandishi wetu alitembelea maeneo mbalimbali na kushuhudia wananchi wakihangaika kuokoa mali zao, baada ya nyumba walizokuwa wakiishi kujaa maji.
Barabara kadhaa zilikuwa hazipitiki kutokana na kujaa maji, huku baadhi ya nguzo za umeme na simu ambazo zilikuwa karibu na mifereji ziliharibiwa na kusombwa na maji.
Mafundi wa Shirika la Umeme Tanganyika (Tanesco) walionekana katika maeneo kadhaa ya jiji wakihangaika kuokoa baadhi ya nguzo hizo.
Athari kubwa ya mafuriko hayo ilitokea katika eneo la Kigogo Darajani ambako baadhi ya nyumba zilikuwa zimejaa maji na baadhi ya vitu vilionekana vikielea kwenye mikondo mikubwa ya maji.
Mmoja wa waathirika hao, Andrew Simon (35) alisema nyumba yake ilijaa maji kwa takriban futi nne kwenda juu na kusababisha hasara ya mali ambayo alikuwa bado hajafahamu thamani yake.
“Sisi tulitoka kwenda kwenye shughuli zetu, baadaye tulipigiwa simu kwamba kuna mafuriko jambo lililonifanya nirudi haraka ndiyo nikakuta nyumba yetu ikiwa imefurika, huku vyombo vyote vikiwa vimeharibika,” alisema Simon.
Kuhusu kutii agizo la Serikali ya Tanganyika la kuwataka wananchi wa mabondeni kuyahama makazi yao, Simon alisema yeye ni mpangaji hakufahamu kuwa mafuriko yangetokea.
Mbali na Kigogo Darajani maeneo mengine ya Ubungo, Tabata, Magomeni Kagera, Jangwani, Msasani, Mikocheni, Kimara na Mbezi pia yaliathiriwa na mvua hizo hali iliyozua hofu miongoni mwa wakazi wa maeneo hayo.
Pia hali ilikuwa mbaya eneo la Tabata Relini nyumba na magari vilifunikwa na maji na kuwafanya watu kupanda kwenye mapaa ya nyumba zao.
Reli inayopita katika eneo hilo ilifunikwa na maji kiasi cha kusababisha kuwapo kwa wasiwasi kama treni ya usafiri wa abiria itafanya kazi leo.


NCHINI TANGANYIKA WATOTO MALAYA UMRI MIAKA 13,14,15,16 WASEMA KUINGILIWA KINYUME CHA MAIMBILE INALIPA



Ni usiku wa saa 4 nipo katika eneo maarufu la Buguruni lililopo jijini Dar es Salaam nikiwa nimekaa napata kinywaji kwenye kioski kimoja.

Katika eneo hilo ambalo lipo pembezoni mwa Barabara ya Mandela si tulivu sana kutokana na pilika pilika za magari na watu wanaopita karibu kwa shughuli mbalimbali.
Huku nikiendelea kupata kinywaji mara naona wasichana wadogo wenye umri wa miaka 14 hadi 16 wakizunguka zunguka katika eneo hili la Buguruni.

Awali nilifikiri walikuwa wakitafuta msaada au wakipita kuelekea nyumbani kwao, kwani umri wao haukunipa picha kwamba walikuwa kazini wakati huo wa usiku wa kiza kinene.
Kilichonifanya niwaangalie kwa udadisi zaidi ni kuona jinsi walivyovaa nguo ambazo zilionyesha nusu ya sehemu zao za mapaja, huku kifuani wakiwa wamevaa blauzi zilizobana zikionyesha matiti yao madogo ambayo yanaanza kuchipua.

Kilichonitisha zaidi ni kuona wasichana hawa ambao wakati huo walipaswa kuwa nyumbani wakiwa mkononi wameshika vinywaji vikali aina ya ‘viroba’ na wengine wakivuta sigara.
Hawa ni sehemu ndogo tu ya wasichana wadogo ambao hukesha usiku kucha katika baadhi ya mitaa ya jiji la Dar es Salaam wakitafuta wateja ili wapate fedha za kujikimu.
Mwandishi wetu wa siri analazimika kuwadadisi wasichana hawa ili kujua nini kilichosababisha waingie katika biashara hii ya umalaya.

Inavyokuwa
Mwandishi ana mwita mmoja wa wasichana hawa jina tumelihifadhi (16) na kuongea naye katika sehemu tulivu katika baa moja hapo Buguruni huku wakitumia vinywaji kunogesha mazungumzo.

Neema akiwa mwenye kujiamini na kazi yake bila ya kutetereka kumbuka msomaji ni msichana wa umri wa miaka16 anasema kazi hiyo aliianza zaidi ya miezi sita nyuma huku akiwa tayari amekutana na idadi ya wanaume ambayo haikumbuki kutokana na wingi wake.

“Kwa siku moja nakutana na wanaume katiya watano hadi saba na hii hutegemea siku na siku, kwani kuna siku huwa na biashara ya kutosha na tunapata fedha za kutosha,” anasema Neema.

Neema akieleza ujira ambao hulipwa anasema ni Sh3,000 hadi Sh5,000 kwa muda usiozidi dakika 30 kwa mwanamume mmoja huku wakati kwa yule anayetaka kulala naye hadi asubuhi hutakiwa kulipa Sh10,000 hadi Sh15,000.

“Baadhi ya wanaume wamekuwa wakitufanyia vitendo vya kikatili kwa kutuingilia kinyume cha maumbile, lakini kutokana na hali ngumu ya maisha hukubali kwani dau huwa kubwa Sh10,000 hadi Sh12,000,ukikubaliana nao lakini wengine hutumia ubabe tu na kututumia bila kutulipa,” anasema Neema na kuongeza;

Neema alizaliwa mkoani Arusha eneo la Sakina na kusoma katika Shule ya Sekondari Usa na kuishia kidato cha pili kutokana na kuugua kila alipoingia darasani.

Kitu gani kilichosababisha Neema aje Dar na kufanya biashara hiyo ya umalaya.???
Anasema ni kutokana na ugomvi baina ya baba na mama yake ambao walikuwa wakikorofishana mara kwa mara kwa sababu mama yake alidai kuwa bibi mzaa baba wa Neema ni mchawi na ndiye aliyemroga Neema na kumsababisha augue kila anapoingia darasani.

Neema anasema hatimaye mama na baba yake waliachana na yeye na mama yake wakaja Dar es Salaam na kuishi maeneo ya Tabata Reli.
Na msichana mwengine mwenye umri wa miaka (15) mzaliwa wa Mbeya anasema anaifanya kazi hiyo kutokana na ugumu wa maisha na hana njia nyingine ya kujiingizia kipato.

Anasema ameanza kazi hiyo mwishoni mwa mwaka 2011 alipokuwa anaishi na shangazi yake Vingunguti na huko alikuwa akikutana na vijana mtaani kwao.

Aliongeza kuwa alipoanza biashara hiyo hali yake ilianza kubadilika, kwani wateja walikuwa wengi kutokana na wanaojiuza kama yeye kuwa wachache, lakini sasa wanaojiuza nao wamekuwa wengi.

msichana mwengine yeye anafurahia kazi hii ya umalaya
Kwa upande wake msichana huyo mwenye umri wa miaka(15) anasema huwa anafurahia kazi hiyo kutokana na kujiingizia kipato cha kutosha kwa siku.
“Unajua kwa siku moja hukusanya Sh50,000 hizo si pesa kidogo hizi sio pesa kidogo kabisa, sidhani kama kazi hii naweza kuiacha kwani ina kila aina ya starehe,” anasema msichana huyo.Anasema mara ya kwanza kuingiliwa kinyume cha maumbile nilijisikia maumivu, lakini niliporudia tena na tena kitendo hicho na ukilinganisha na gharama yake kuwa kubwa hawezi kuacha alisema msichana huyo.
“Hapa dau huwa kubwa kwani kwa mwanamume mmoja tu kuniingilia kinyume cha maumbile ni Sh15,000 na hii ni muda mfupi,” hivyo nikitembea na watatu ninakuwa na fedha za kutosha,” anasema msichana huyo mwenye umri wa miaka (15). Wakati hayo yakiendelea Buguruni, katika maeneo ya Manzese Mburahati, Uwanja wa Fisi karibu na kumbi za starehe wakati wa usiku huwezi kukosa kuwaona wasichana wadogo wenye umri kati ya miaka 13 hadi 14 wakitembea kutafuta wateja wa kufanya nao ngono watoto hawa wamekuwa malaya hali ya kuwa umri wao ni mdogo sana hata ukiwa ni mkubwa malaya sio kazi kabisa.

Wanaume wanena
Baadhi ya wanaume tuliyo wahoji kuhusu kuwachokora watoto wadogo kama hao wanasema kuwa wamekuwa wakifika kupata huduma kutoka kwa akina dada hao kutokana na kuepuka gharama.
“Unajua ukiwa na msichana wa kudumu na maisha yako yakiwa si mazuri atakusumbua, lakini ukija hapa hakuna noma wala tatizo mnakutana siku moja na kuachana kila mtu kivyake,” anasema Samson Frank.

Saturday, March 23, 2013

RAISI WA CHINA XI JINPING-(BANDARI YA BAGAMOYO)ATATUWA NCHINI TANGANYIKA NI ZIARA YAKE YA KWANZA BARANA AFRIKA



Dar es Salaam. Rais wa China, Xi Jinping anatarajiwa kuwasili nchini Tanganyika kesho kwa ziara ya siku moja, ambapo pamoja na mambo mengine atasaini mikataba 17, kati ya nchi hiyo ya china na Tanganyika, ukiwamo wa ujenzi wa Bandari  mpya ya kisasa ya mji wa Bagamoyo mkoani Pwani.je nini thamira ya nchi ya Tanganyika kujenga bandari hii..???                                                                                                                                                                                    Ujenzi huo utakaofanywa na Kampuni ya Merchants Holding ya China, utakwenda sambamba na ujenzi wa barabara inayounganisha bandari hiyo na Reli ya Kati na Mamlaka ya Reli ya Tanganyika na Zambia (Tazara).              Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alisema ujio wa rais huyo aliyechaguliwa wiki mbili zilizopita, utakuwa wa manufaa makubwa kwa nchi yetu ya Tanganyika.
“Mbali na mkataba huo pia tutasaini mikataba wa kidiplomasia. Vilevile, China imefungua soko la Watanganyika kuuza tumbaku nchini humo na mkataba wa kuliendeleza Shirika la Utangazaji Tanganyika (TBC),” alisema Membe.
Waziri huyo alisema kiongozi huyo wa China pia atafungua jengo la kisasa la mikutano la Mwalimu Nyerere.
“Kwa kuwa anakuja Afrika kwa mara ya kwanza huku Tanganyika ikiwa nchi ya kwanza, Jinping pia atatoa hotuba yake juu ya msimamo wa China kwa Tanganyika na Afrika kwa jumla,” alisena Membe.
DR KUMBI SHEIN JE KIKWETE KAJA KUKUOMBA RUHUSA YA KUJENGEWA BANDARI BAGAMOYO..???

Friday, March 22, 2013

WAISLAMU 52 NCHI TANGANYIKA WATUPWA JELA NA MAHAKAMA YA NCHI YAO YA KINAFIKI.



WAKOMBOZI 52 wa Watanganyika na Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda Issa Ponda, waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya kusingiziwa kufanya maandamano ya haramu, wamehukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu jela kwa kila mmoja.

Hukumu hiyo ilitolewa na Mahakama ya wanafiki na maduwi wa uislamu nchini Tanganyika juu ya Hakimu Mkazi Kisutu jana, baada ya wafuasi hao kukutwa na hatia kwa makosa matatu kati ya manne yaliyokuwa yakiwakabili. Hata hivyo watakaa jela kwa mwaka mmoja kutokana na adhabu zote kwenda kwa pamoja.

Hata hivyo aliyekuwa mshtakiwa wa 48, Waziri Omar Toy, aliachiwa huru baada ya Mahakama kuridhika kwamba hana hatia kutokana upande wa mashtaka kushindwa kuthitibisha madai dhidi yake!!!

Baada ya Hakimu Mkazi, Sundi Fimbo kusoma hukumu hiyo, ilizuka tafranwi miongoni mwa ndugu wa washtakiwa hao ambapo wengine waliangua vilio na wengine kuanguka chini.Mwanamke ambaye ni ndugu wa washtakiwa hao, alionekana kama mtu mwenye hasira sana na kutaka kumvamia askari wa kike.

Hakimu Fimbo mnafiki mkubwa katika hukumu hiyo alisema baada ya kusikiliza ushahidi na hoja za pande zote pamoja na vielelezo vilivyowasilishwa mahakamani hapo ameridhika kuwa upande wa mashtaka umethibitisha mashtaka matatu dhidi ya washtakiwa hao.

Hata hivyo, Hakimu Fimbo alisema kuwa katika shtaka la uchochezi lililokuwa likiwakabili washtakiwa wanne, upande wa mashtaka umeshindwa kulithibitisha!!!!

“Mahakama imeridhika na ushahidi uliwasilishwa na upande wa mashtaka kuwa umethibitisha mashtaka dhidi ya washtakiwa wote isipokuwa mshtakiwa wa 48,” alisema Hakimu Fimbo na kuongeza:

“Hivyo Mahakama imewatia hatiani washtakiwa wote isipokuwa mshtakiwa wa 48, katika shtaka la kwanza, la pili na la tatu na katika shtaka la nne, Mahakama imeona kuwa washtakiwa hawana hatia.!!!!

Washtakiwa walikuwa wakikabiliwa na mashtaka ya kula njama za kutenda makosa, kufanya maandamano yaliyozuiwa na Polisi na kwa pamoja kufanya mikusanyiko haramu na kusababisha uvunjifu wa amani.

Akitoa adhabu kwa washtakiwa hao baada ya kuwatia hatiani, Hakimu Fimbo alisema: “Nimezingatia kuwa karibu kila mshtakiwa ana majukumu ya kifamilia na kwa kuzingatia `nature’ (asili) ya mashtaka.!!!

Aliongeza: “Katika kosa la kwanza ninawahukumu kifungo cha mwaka mmoja jela na kosa la pili pia mwaka mmoja jela na tatu mwaka mmoja jela. Adhabu zote zinakwenda kwa pamoja.”Kauli za Mawakili
Kabla ya adhabu hiyo, Wakili wa Serikali, Ladislaus Komanya aliyekuwa akisaidiana na Wakili Joseph Maugo, aliieleza Mahakama kuwa hawana kumbukumbu za makosa ya jinai kwa washtakiwa hao na akaiomba Mahakama iwape adhabu kwa mujibu wa sheria.

Kwa upande wake, Wakili wa washtakiwa hao, Mohamed Tibanyendela aliiomba Mahakama iwaonee huruma kwa kuwaachia huru washtakiwa hao au kwa kuwapa adhabu ndogo sana.
Wakili Tibanyendelea alidai kuwa washtakiwa hao ni mara yao ya kwanza kutenda makosa hayo na kwamba wana familia ambazo zinahitaji huduma kutoka kwao huku akidai kuwa wengine tangu walipokamatwa, familia zao hazijui waliko.

Pia Wakili Tibanyendelea alidai kuwa washtakiwa wengine wanaumwa kisukari na shinikizo la damu, huku akitoa mfano wa mshtakiwa wa 21, Kassim Mohamed Chogo, aliyefutiwa mashtaka kuwa alikuwa mgonjwa na ameshafariki dunia.

Thursday, March 21, 2013

NI KWA NINI MZEE KARUME NA NYERERE WALIMUOGOPA SANA NA KUMUONDOSHA KANALI ALI MAHFDHU NCHINI ZANZIBAR NA TANGANYIKA PIA.???


NI UPI MCHANGO WAKE KWA ZANZIBAR..?
KWA NINI HATAJWI WAKATI WA SHEREHE ZA MAPINDUZI YA ZANZIBAR..?
KWA NINI ALIKUFIA MOZAMBIQ NA SIO KWAO NCHINI ZANZIBAR..?
KWA NINI NYERERE ALIMUOGOPA KANALI ALI MAHAFDHI..?
KWA NINI MZEE KARUMA ALIMUOGOPA KANALI ALI MAHAFDH..?
KANILI ALI MAHAFDHA ALIJIFUNZA WAPI AU NCHI GANI UJESHI..?
NI NANI HASWA HUYU KANALI ALI MAHAFDHI...?

MUNAYAITA MAPINDUZI MATUKUFU!!! WAKATI MAITI ZA WANAWAKE ZILINAJISIWA HALIYAKUWA WANAWAKE WASHAKUFA.


John Okello alitoka kwao Uganda, Injin aliyetoka kwao Kenya na Mfaranyaki aliyetoka Tanganyika,wote hawa sio wazanzibari ni mitwana ya kutoka bara au nchi jirani na kuja kuivamia nchi huru usiku wa manane watu wamelala wa kuamkia tarehe12 Januari 1964. Wananchi, mafisadi kwa sababu ya maslahi ya nafsi zao hawakuhisi uchungu kuipoteza nchi yao, wala kuzipoteza roho za wazee wao, za ndugu zao na za marafiki zao. Kwa mujibu wa kitabu cha huyo aliyejipa ujamadari wa hayo 'mavamizi' ya Januari 12, 1964, John Okello, amesema kuwa watu waliyokufa katika 'mavamizi' hayo ni 13,000. Hii ni idadi ndogo kabisa aliyopenda kuitaja ila tukumbuke walikuwa ni Wazanzibari walio uliwa na mitwana ya kutoka Uganda,Kenya na Tanganyika. 

Ukatili, ushenzi na unyama uliofanywa katika visiwa hivi ulikuwa haujapata kutokea ulimwenguni kote kabisa kabisa tofauti na nchi hii ya Zanzibar ilivyokuwa na ustaarabu wa kupigiwa mfano, hauwezi hata kuhadithika. Wengi waliokuwa wanaijua Zanzibar, waliona taabu kuyaamini waliyokuwa wameyasikia yametokea Zanzibar kutokana na hayo yenye kuitwa 'mapinduzi matukufu astahafiru allah na anaeyaita ati ni muislamu'. Ilifika hadi, siku hiyo ya 'mavamizi' washenzi na makatili hao kuwanajisi maiti wa kike. Kitendo hicho hakijawai kufanyika katika nchi nyingi ulimwenguni za kunajisi maiti za kike lakini hapa zanzibar yametokea hayo na ni nchi moja katika nchi zenye ubinaadamu na ustaarabu wake. Lenye kuzidi kushangaza na kusikitisha ni kumsikia mwananchi mwenye kujulikana kuwa yeye ndiye mwongozi wa hao wenye kujiita "progressives" akasema kuwa, watu waliyouliwa katika hayo yenye kuitwa 'mapinduzi' ni 491! Duh! 

Mwenyewe Okello alieongoza hayo mauwaji amesema kuwa wamekufa wananchi 13,000. Hata wangekuwa watano tu, bali ni binaadamu, ni wananchi, jee, ndio wawe wamestahiki kuuliwa kwa kuvamiwa nchi yao na wageni ambao wewe na wenzio kama wewe mmechanganyika na hao wageni katika kuifisidi nchi na wananchi wake..? La kustaajabisha zaidi - ni pale ilipojulikana kuwa haya yote yalipangwa kabla - kwa siku 30 tu yaaani Desemba 10 mpaka Januari 11 ilitosha kujuwa uovu wa Serikali hata ikastahiki kupinduliwa..? Hata ingelikuwa ni ovu hivyo, bali njia za kuiondowa za kikatiba zilikuwepo ambazo zingaliweza kutumika, khasa na hao Wapinzani. Haikuhitaji hata kidogo kutumia nguvu. Lakini hakika khasa ni kuwa mambo yalikwisha pangwa zamani kuwa nchi ya zanzibar ivamiwe na washenzi na wafanye uchafu wao waliotaka kufanya na mumefanikiwa,na hayo yalikuwa ni matekelezo tu!!

mbona hamuwataji tena kwenye historia yenu kina 
1)Abdulwahid 
2)Ally Sykes 
3)Hamza Mwapachu,
4) Tewa Said Tewa,
5)Ali Migeyo , 
6)Suedi Kagasheki,
7)Dossa Azizi,
8)Abdulkarim Karimjee,
9)Chifu Abdieli Shangali wa Machame, 
10)Kleist Sykes,
11)Abdulwahid Sykes,
12)Othman Shariff KABURI LAKE LIKO WAPI TUMTILIYE UBANI..?
13)Kassim Hanga,KABURI LAKE LIKO WAPI TUMTILIYE UBANI..?
14)Twala,
15) Ringo,
16) Majura,
17) Saadalla, 
18)Aboud Nadhif, 
19)Mdungi Usi.
20)Luteni Hamoud Hamoud KABURI LAKE LIKO WAPI TUMTILIYE UBANI..?
21)Kanali Seif Bakar,
22)Jenerali Said Natepe,
23)Kanali Ali Mahfudhi  au ukipenda utamwita  Komandoo.
24)Faki Mohamed Faki,
25) Abdurahman Mohamed Babu,
26) Said Iddi Bavuai,
27) Saidi Washoto,
28)Ramadhan Haj.
29)mzee hassan nassor moyo,
30)mzee aboud jumbe,
31)mzee abeid amani karume.
wote hawa wako wapi sasa..? jibu ni wazee na wengine washakufa haswa hata hawapo tena duniani je Dr Kumbi Shein na kundi lako munajifunza nini kwa hawa watu wote waliokuwa wakijivuna na kupinga watu na kuuwa watu na kuthulumu mashamba ya watu na mali za watu na kuowa watoto wa kike bila ya ridha zao au wazee wao au hata kuwanajisi na kuwapiga bakora majela na kutesa watu kinyama wote wako wapi sasa..?? wako wapi sasa..?? mbona hata kidole chao hatukioni hapa ZANZIBAR..? basi mukae mukijuwa na nyinyi mtapita tu kama mvuwa ya masika.

Wednesday, March 20, 2013

MNAOLILIA URAISI NYAMAZENI MPISHENI DR SALIM AHMED SALIM AINGIE


Mnaolilia Urais Nyamazeni, Mpesheni Dk Salim Ahmed Salim Aingie

imeandikwa na Joseph Mihangwa.

PATASHIKA nguo chanika inaendelea kichini chini kwa vingunge wa vyama vya siasa kuendesha kampeni za urais kwa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka 2015. Majina kadhaa yanatajwa na wao kutokanusha, na wapambe wao kuzizima.

Kwa upande wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wanatajwa Waziri Mkuu Mstaafu (kwa kashfa), Edward Lowassa, Waziri wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe, Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, Waziri Mkuu wa sasa, Mizengo Pinda na wengineo wachache.

Kwa vyama vya upinzani, anatajwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk Willibrod Slaa, Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho na mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, wakati kwa upande wa Chama cha Wananchi (CUF), anatajwa Mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Lipumba. Wote wanaojinasibu na kinyang’anyiro hicho, wanatoka Bara. Wazanzibari hawatajwi, kana kwamba Zanzibar si sehemu ya Tanzania.

Kwa CCM, ni utamaduni uliozoeleka kwa mgombea kutokana na Kamati Kuu ya Chama hicho, lakini kinyume na matarajio, hao wanaotajwa kuukamia urais wamefyekwa katika Kamati hiyo kwa sababu zisizofahamika.

Kuteuliwa kwenye Kamati Kuu ya CCM kwa mwanasiasa mkongwe na mwanadiplomasia wa kimataifa, Dk Salim Ahmed Salim bila matarajio ya makada wengi wa chama hicho, kumezua minong’ono, kiwewe na taharuki kwa wanyemeleaji wa nafasi hiyo kwamba huenda Dk Salim anaandaliwa kwa mambo makubwa zaidi.  Hata hivyo, wanajiliwaza kwamba kwa umri wake wa miaka 73, Dk Salim hizi si zama zake za kuongoza nchi!

Lakini pamoja na hayo, wanafahamu kwamba katika hali ya sasa ya taifa kupoteza dira na mwelekeo, panahitaji Rais makini kutawala awamu moja tu ili kuweka mambo sawa, bila kujali umri wala itikadi ya chama chake, mradi tu awe mzalendo na mkombozi wa wanyonge.

Lakini Mungu si Athumani; lolote laweza kutokea kwa mazingira ya sasa ya kuchafuka kwa bahari ya kisiasa, kiuchumi na kijamii, hivyo kuhitaji nahodha mkongwe kuinusuru meli kwenye tufani. Tayari CCM imeweka wazi kuwa kinakusudia kurejea kwenye misingi ya uadilifu wa enzi za TANU na ASP ili kurejesha heshima ya taifa hili.

Ni nani awezaye kufufua misingi hiyo kwa uhakika na umakini mkubwa mbali na wa zama za Dk Salim Ahmed Salim? Jukumu hilo muhimu, kama tunavyoshuhudia, haliwezi kutekelezwa na wanasiasa wa zama za ‘Bongo fleva,’ au wale wanaotamba kwa ufisadi wao nchini. Taifa linayumba kwa kukosa viongozi wenye busara na hekima.


Taifa liko njia panda likiweweseka kwa dhambi kuu nne za maangamizi. Mosi; ni nchi kukosa itikadi na dira ya maendeleo. Tunaimbishwa Ujamaa huku tukichezeshwa ngoma ya Ubepari, ya kila mtu kuishi kwa ukali wa meno yake. Pili; ni kutoweka kwa maadili na utamaduni wa taifa hili kwamba nchi inabugia sumu, makapi ya kila aina kwa maangamizi yake. Nchi inapokosa utamaduni wake, ni sawa na mti usio na mizizi, kuweza kuangushwa na upepo duni tu.

Tatu; ni kutoweka kwa heshima ya Mtanzania katika duru za kimataifa, tofauti na enzi za Serikali ya awamu ya kwanza ambapo alisifika kama mpigania haki, usawa wa kijamii, amani na utulivu. Nne; ni kuibuka kwa udini unaotishia kuipasua nchi vipande vipande, na pengine kuitupa kwenye janga la umwagaji damu.

Tano; ni kero za Muungano ambapo Zanzibar sasa inataka itambuliwe kama nchi. Tayari Wazanzibari wamezika tofauti na uhasama wao wa siku nyingi na kufanikiwa kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa; uhasama uliowagawa na kuwadhoofisha kisiasa na kijamii kuweza kufinyangwa finyangwa ndani ya mfumo tata wa Muungano. 

Leo wanaweza kuzungumza kwa herufi kubwa ndani na nje ya Muungano; na tayari wamesema sasa ni zamu yao kutoa Rais wa Muungano. Je; Wabara ambao ndio walio wengi, watakubali hilo, katikati ya mikanganyiko ya kisiasa na kidini inayolikumba Taifa letu hili?

Misingi ya TANU na ASP ndiyo iliyozaa kile tunachojivunia sasa kama ‘hali ya amani na utulivu’ ambavyo vinatoweka haraka kutokana na uongozi wa nchi kuwa mikononi mwa nyang’au walafi na ubinafsi. Misingi hiyo ilikuwa ni usawa wa binadamu, vita dhidi ya rushwa, unyonyaji, uonevu na maisha bora kwa wote.

Chama Tawala kama CCM, hakiwezi kusalimika kama Chama iwapo wanachama wake, hasa viongozi, watautazama utendaji wake (Dk Salim) kwa maslahi yao binafsi badala ya maslahi ya umma. Uanachama na uongozi wa aina hiyo, ni ugonjwa (ukoma) ndani ya Chama.


Kinachopotea haraka hivi sasa, kwanza; ni uhuru wa kitaifa, kwa maana ya uwezo wa wananchi kuamua juu ya hatima yao ya kujitawala bila kuingiliwa na watu wasio wazalendo. Pili; ni kupotea kwa uhuru dhidi ya njaa, magonjwa na umasikini kwa kuwa tu siasa, uchumi wa nchi na rasilimali za Taifa zimehodhiwa na kikundi kidogo cha wahujumu uchumi na mafisadi na Serikali ikasalimu amri kwa wadhalimu hao.

Tatu; ni kutoweka kwa uhuru binafsi, haki ya kuishi maisha ya heshima na usawa kwa wote, uhuru wa mawazo na wa kushiriki katika maamuzi yanayogusa maisha ya watu. Hivi leo,  mambo hayo ni kwa kudra ya Mungu, kwa kuwa kundi la walionacho halimjui mdunda kazi mwenye njaa. Na ingawa kuna Bunge linalopashwa kumsemea, limetekwa na ufisadi na kujipambanua kama taasisi ya ulaji na ya kuzika demokrasia.

Kurejea kwa wakongwe wenye kumbukumbu sahihi ya mambo haya kwenye ulingo wa CCM, kama vile Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Philip Mangula, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Mohamed Seif Khatib na wengineo, ambao hapo nyuma walipigwa buti kuachia nafasi vijana (ma-bongo fleva), ni ishara ya kutambua usemi kwamba ‘lazima utazame nyuma ili uweze kwenda mbele,’ na ni dalili pia ya kushindwa kwa kizazi kipya kuongoza nchi kwa mafanikio bila kuingiza busara na hekima ya wakongwe. 

Ilivyo sasa, CCM imegeuka kokoro lenye kuzoa kila uchafu na kutishia amani na usalama wa taifa kutokana na ukweli kwamba Chama lege lege huzaa Serikali legelege!

Kwanini tusiwe na kina Salim Ahmed Salim na kina Philip Mangula, Mohamed Seif Khatibu na wengineo wachache, kurejesha heshima ya Taifa hili baada ya kizazi cha ‘Bongo fleva’ kuonyesha wazi kushindwa kuhimili changamoto za utawala wa nchi?

Kuongoza nchi bila itikadi wala maadili ya taifa, ni sawa na nahodha asiyejua bandari aendayo. Kwa nahodha kama huyo, hakuna upepo ulio mwafaka kwake. Na ndimo tulimo hivi sasa, kwa nchi yetu kugeuzwa shamba la bibi pasipo mtu wa kukemea; uzalendo unayoyoma haraka kwamba tusishangae kuona siku moja Bunge likiongozwa na Spika Mjapani, au nchi kuwa na Waziri Mkuu Mmalaysia, kadri tunavyozidi kuruhusu nguvu ya fedha kuchukua nafasi ya uzalendo, kwani tayari wahaini hawa wanazungumzia uraia popo wa nchi mbili!

Nchi inakabiliwa na janga hatari jipya la mgawanyiko kwa misingi ya udini na uhasama unaokithiri, kati ya Wakristo na Waislamna kutishia amani. Haya yote ni ishara ya kudhoofika kwa uzalendo, umoja wa kitaifa na kiitikadi. 

Kama hali hii itaachwa kuendelea, uchaguzi mkuu ujao utakuwa mgumu kwa sababu kila kundi litataka achaguliwe Rais wa dini yake kwa gharama ya utaifa. Kwa hali ilivyo, hakuna mgombea mwingine anayeweza kuleta suluhu ya makundi haya mawili zaidi ya Dk Salim Ahmed Salim ambaye anakubalika kwa Wakristo na kwa Waislamu; tangu kale, juzi, jana hadi leo.

Dk Salim si mdini, si mhafidhina wa kisiasa, ni mwanademokrasia jamii. Kikundi cha Wazanzibari, kilichojiita ‘Liberators’ (Wakombozi) na kuzoea kumhujumu ili kulinda ‘ukale’ kinajua hilo na hakimuwezi tena.

Na kwa kuwa Wazanzibari sasa wamezika tofauti zao za kiitikadi za miongo mingi na kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa, sasa ni dhahiri zile hujuma walizokuwa wakimfanyia Dk Salim, kwamba yeye ni mwanachama wa zamani wa Zanzibar Nationalist Party (ZNP) hazina mshiko tena. 

Kwa sababu hiyo, anaweza kuwa mgombea pekee wa urais, akipenda, anayekubalika vizuri na pande zote za Muungano pamoja na makundi ya kidini yanayoibuka kuliko mwanasiasa mwingine yeyote yule, Bara na Visiwani, licha ya umri wake mkubwa uraisi sio kubeba zegeeee.


Heshima ya Mtanzania imeporomoka mara dufu kimataifa tangu enzi za awamu ya pili. Kiongozi wa Kitanzania wa sasa si yule wa enzi za awamu ya kwanza, aliyechukia udhalimu, uonevu, unyanyasaji na ukoloni wa kimataifa, bali viongozi wa sasa ni mazuzu tegemezi, wasaliti na wakumbatia rushwa, ufisadi na mamluki wanaonunulika kirahisi kwa maangamizi ya nchi na wananchi.

Kuna mantiki gani kupinga maoni yaliyotolewa na Mwingereza, Bi Sarah Hermitage hivi karibuni kuhusu ufisadi, dhuluma na rushwa serikalini? Kuna mantiki gani kwa mafisadi wa nchi hii kuchochea vijana waandamane dhidi yake kwa madai ya kutudhalilisha badala ya kumsapoti?

Watuambie, iko wapi chenji ya vijisenti vya rada tuliyoambiwa vitalipwa..? Kwa nini tunaficha nyuso juu ya ufisadi mkubwa wa Meremeta, Richmond/Dowans, Deep Green na mwingine wa aina hiyo..? Wanafiki wapevu hawa! !!Wahaini, wasaliti wa taifa!!!! kama munataka raisi wa kweli ni Dk Salim Ahmed Salim tu lau kama munataka msaani wa BONGO FLEVA basi sawa chaguweni hao mafisadi waimalize kabisa nchi hii.

Tumejenga utamaduni tata wa kupata marais kutokana na mawaziri wa Mambo ya Nchi za Nje, kuanzia na Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Rais wa sasa Jakaya Kikwete; na leo Waziri wa sasa wa wizara hiyo, Bernard Membe anapiga jaramba kufuata nyayo. 

Yote haya eti ni kwa lengo la kutia ubani uvundo wa nchi katika medani za kimataifa! Kama kweli hiyo sasa ndiyo tiketi ya urais, basi hakuna Mtanzania aliye hai wa kuweza kumfikia Mwanadiplomasia Dk Salim Ahmed Salim!

Dk Salim Ahmed Salim, kama alivyokuwa Mwalimu Julius Nyerere, ni mwanasiasa, mwanadiplomasia wa kimataifa na msomi mwenye historia ndefu ya harakati za mapambano dhidi ya uonevu; mwenye kiu ya haki na usawa kwa wote. Wengi tunamkumbuka miaka ya karibuni kama Balozi, Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (sasa Umoja wa Afrika) na msuluhishi wa migogoro kimataifa.

Mwamko wake wa kisiasa unaanzia miaka ya 1950 huko Zanzibar enzi za mapambano ya kudai uhuru wa visiwa hivyo, kama Katibu Mwenezi wa Umoja wa Vijana uliojulikana kama Youths Own Union (YOU), uliounga mkono harakati za chama cha mrengo wa kushoto cha Zanzibar Nationalist Party (ZNP).

Wakati huo, vijana wa Kizanzibari walijipambanua na harakati za kupinga ukoloni kitaifa na kimataifa, kuanzia harakati nchini Algeria dhidi ya ukoloni wa Kifaransa, na Ghana dhidi ya Waingereza, Mau Mau (Kenya) na Afrika kusini dhidi ya tawala za kibaguzi za Wazungu, na kutoka harakati za ukombozi wa Wapalestina hadi vita ya Vietnam, kwanza dhidi ya Wafaransa na baadaye Marekani.


Dk Salim, kama msemaji wa YOU, alikuwa mtu wa kwanza Afrika Mashariki kutahadharisha juu ya uwezekano wa Waziri Mkuu wa Kwanza wa Congo, Patrice Emery Lumumba, kuuawa na mabeberu, ilipotangazwa kwamba amepotea. Alishambulia (Dk Salim) vikali Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) kwa hujuma hiyo; na leo historia imethibitisha kuwa alikuwa sahihi.

Ni Dk Salim aliyewaongoza vijana wa Kizanzibari kupinga hatua ya Marekani kujenga Kituo cha Kijasusi (tracking station) Zanzibar sehemu ya Tunguu, hadi kikaondolewa. Ni katika harakati hizi dhidi ya ukoloni na ubeberu, alikutana na mwandani wake, Mama Amne Ali Rifai wakaoana.

Ni kutokana na kuundwa kwa chama cha harakati za ukombozi cha Umma Party visiwani Zanzibar, kwa vijana wanaharakati kujiengua kutoka ZNP, wakiongozwa na Abdulrahman Babu mwaka 1963, kwamba Dk Salim alianza mikiki mikiki ya kibalozi, kwanza nchini Cuba na baadaye Misri. 

Alikuwa Cuba wakati Rais wa nchi hiyo, Fidel Castro alipotangaza azimio lake mashuhuri la Havana (the Havana Declaration), na Dk Salim akalikariri sehemu zake muhimu kwa lugha ya Kihispaniola. Baada ya Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 12, 1964, Serikali mpya ya Mapinduzi ilimteua kuwa Balozi nchini Misri akiwa na umri wa miaka 22 tu. Na Muungano waTanganyika na Zanzibar ulipozaliwa, Aprili 1964 alibakia Misri kama Balozi wa Tanzania.

Alitumika kama Balozi kwa mara ya mwisho nchini China ambako alikuwa rafiki kipenzi cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Chou-en-Lai, kabla ya kuteuliwa Balozi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa (UN), alikotumikia kwa miaka kumi. 

Akiwa huko, alitoa mchango mkubwa na kuiletea heshima kubwa nchi yetu, kwanza kwa kuchaguliwa Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya UN ya Ukombozi dhidi ya Ukoloni, kisha Rais wa Baraza la Usalama la UN na Rais pia wa Baraza Kuu la Umoja huo. 

Aliwania nafasi ya Katibu Mkuu waUN na kuungwa mkono na mataifa yote wanachama, lakini alishindwa kwa kura turufu (Veto) ya Marekani kwa sababu tu alijipambanua na siasa za mrengo wa Kisoshalisti. Ndiyo kusema kwamba mchango wa Dk Salim kwa ukombozi wa Bara la Afrika na dunia kwa ujumla, hauwezi kupuuzwa wala kusahaulika.

Kama Watanzania wanatafuta Rais wa kurejesha amani na utulivu, mshikamano wa kitaifa, usawa na demokrasia ya kweli nchini na heshima inayopotea, ni nani zaidi ya Mtanzania huyu asiyejua lugha ya ulafi, ufisadi, udini wala kulipiza kisasi, Dk Salim Ahmed Salim? Tunahitaji mtu wa aina yake kwa kipindi kimoja tu cha uongozi kunusuru nchi yetu!

Mwisho.