Friday, April 26, 2013

KILA ATAKAE JARIBU KUZUNGUMZA MUUNGANO ATAKIONA CHA MTEMA KUNI


LULA ANAONA KUWA WAZANZIBARI WANA UHURU ZAIDI NA KUFANYA WANANVYOTAKA KATIKA MUUNGANO HUU KULIKO WATANGANYIKA ANA HAYA YA KUSEMA
Lula wa Ndali Mwananzela
GARIMOSHI la Katiba mpya linaendelea kwenda kasi na hakuna dalili ya kukoma mpaka Katiba “mpya” itakapopatikana. Msisitizo hadi sasa umekuwa juu ya ujio wa “Katiba mpya” hata kama upya wake utakuwa bado na mambo ya zamani. Mchakato huu ambao ulikosewa toka mwanzo una kila dalili ya kufanya zoezi la Katiba mpya kutofanikiwa na kutokukidhi mahitaji ya Watanganyika.(Watanzania).

Sheria inayosimamia mchakato huu na ambayo iliweka uwezekano wa tume ya Katiba kuundwa imeweka wazi mambo kadhaa ambayo wananchi (yaani wenye nchi) hawapaswi kuyazungumzia na kuyabadilisha isipokuwa tu kujadili kwa namna ya kuboresha. Yaani, wananchi (wenye nchi) wakitaka kuondoa jambo fulani kati ya haya, sheria inakataza.
Kifungu cha 9 cha Sheria hiyo ya 2011 kifungu kidogo cha 2 kimeweka orodha ya mambo ambayo ni lazima yadumishwe kwenye Katiba mpya na la kwanza kati ya hayo ni “kuwapo kwa Jamhuri ya Muungano”.
Jambo hili kwa haraka laweza kuonekana kuwa ni jema, lakini tukiangalia kwa karibu tutaona kuwa kwa maamuzi ya watu walioko madarakani mojawapo ya matatizo makubwa kabisa ya kisiasa ambalo Taifa linahangaika nalo ni hili – uwepo wa Jamhuri ya Muungano.
Ikumbukwe kuwa tulipoungana na kuunda taifa la ((Tanzania)) tulikuwa nchi mbili kila moja ikiwa na hakimiya kamili. Kulikuwa na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na kulikuwa na Jamhuri ya Tanganyika. Nchi hizi mbili ziliungana na kuunda nchi hii ya ((Tanzania)). Tangu wakati huo hadi sasa hata hivyo Muungano wetu umekuwa sababu ya fahari lakini pia sababu ya maswali.
Miaka ya karibuni maswali haya yameanza kugeuka na kuwa shari baina ya watu wa pande zetu mbili. Kuna mgogoro ambao tayari umehusisha viongozi wa kitaifa. Wapo wananchi wa Zanzibar ambao wanaamini kuwa pamoja na kuingia katika Muungano, Zanzibar ilibakia kuwa nchi na imeendelea kuwa nchi. Hawa wanachodai ni kuwa kilichopotea baada ya Muungano ni serikali ya Tanganyika lakini Zanzibar imeendelea kuwapo.
Matokeo yake ni kuwa Wazanzibari wameendelea kushikilia Zanzibar lakini wakati huo huo wanadai ((Tanzania)) ((hapa nitakujibu hakuna mzanzibari anae shikila Tanzania na ikiwa yupo basi anasili ya Tanganyika)). Wazanzibar wana haki zote kama Wazanzibari na wana haki zote kama Watanzania.((huwo ni uwongo kabisa wazanzibari hawana haki hata ndani ya nchi yao zanzibar kwa kutawaliwa na nyinyi wakoloni weusi)) Wazanzibar wanaweza kuteuliwa katika ajira Zanzibar na wanaweza kuteuliwa katika ajira Bara;((huu pia ni uwongo)) wanaweza kuomba kazi Zanzibar wanaweza kuomba kazi Bara;((uwongo)) wanaweza kumiliki ardhi Zanzibar na wanaweza kumiliki ardhi Bara. Wazanzibar wakija Bara kwamba wanatoka Zanzibar haichukuliwi kwa namna yoyote tofauti((wanachukuliwa na kubaguliwa na kuitwa wapemba nyie wapemba rudini kwenu labda wewe hujuwi)).
Hivyo, Mzanzibari anaweza kwenda Bukoba, Iringa, Mwanza au Tanga na kufanya shughuli zake akijua yuko ndani ya nchi yake((hapana wanajuwa wapo ugenini kama walivyo ugenini katika nchi nyengine ulimwenguni)). Lakini pamoja na hayo bado ana haki ya kipekee Zanzibar((ndio maanake ndio nchi yao wewe ukienda india muhindi anahaki sio wewe ukienda canada mcanada ana haki sio wewe chaajabu kipi hapa au kwakuwa ni zanzibar..??))
Mtu wa Bara (Mtanzania anayetoka Bara) ((sema mtanganyika akitoka tanganyika hakuna mtanzania)) akienda Zanzibar hana haki zile zile isipokuwa kama vile ni mgeni (alien). Hana haki ya ajira au kuteuliwa kwenye nafasi mbalimbali.((huwo ni uwongo sepetu ni mtu wa wapi kama sio mbara..? ofisi nzima ya TRA ni wabara watupu na majaji ni wabara polisi wabara majeshi wabara ajira ngani unayozungumzia wewe..?? ya uchukuzi na kubeba mizigo na kuuza vibuwa ndio labda wanayofanya ni wazanzibari)) Rais wa Zanzibar hawezi kumteua mtu wa Bara kufanya kazi za Zanzibar bila kuonekana ameenda ‘nje’ ya Zanzibar kutafuta ajira japo Mzanzibari naye ni Mtanzania na mtu wa Bara naye ni Mtanzania.((usiseme mtu wa bara sema kweli mtu wa tanganyika)) Mtu wa Bara ni Mtanzania akiwa Tanzania lakini akiwa Zanzibar yeye ni Mbara kwani Zanzibar ni ya Wazanzibari lakini Tanzania ni yetu sote.((hapana zanzibar ni ya wazanzibari na tanganyika ni yawatanganyika na tanzania ni ngozi tu ya kondo ambayo tanganyika imeiva wasijulikane kama wao ni fisi bali ni kondo huku wakilaa zanzibar taratibu.))
Mtu wa Bara kwa Zanzibar yeye ni mgeni. Na tumeshuhudia baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wakijaribu kutunga sheria zenye kuwashughulikia watu wa Bara kama wageni Zanzibar ndani ya Muungano huu huu.((wewe kweli kipofu baraza la wawakilishi ni watumwa wenu nyinyi wakoloni weusi kama sio wao leo hii hakuna muungano ila wao ndio wanaowarudisha na kuwafunga wazanzibari wanaotaka zanzibar huru))
Inaonekana walioungana ni watu wa Bara lakini watu wa Zanzibar wao bado hawajaungana.((hapa umepatia kabisa wazanzibari hawajaungana na wala hawataungana na watanganyika)) Wanataka chetu kiwe cha wote lakini cha kwao kiwe cha kwao.((hata mtanganyika ndio anataka cha wazanzibari kiwe chao na chawatanganyika kiwa cha watanganyika,ushahidi ni madini mbona mukipata pesa hatugawani nusu nusu..? gasi..? ubalozi nchi za nje..? lakini toka musikie zanzibar kuna mafuta sasa haraka haraka munataka kunda katiba mpya ili muifanye kuwa ni nchi moja muimeze zanzibar na kuipoteza katika ramani ya dunia asiyejuwa ni nani..?? Kisingizio (haiwezi kuwa sababu) ni kuwa ati “Zanzibar ni ndogo”.((ni dongo kweli sio uwongo wala kisingizio nyinyi mkoa moja tu unawatu millioni ngapi..?? na zanzibar nzima ina watu millioni ngapi..? nusu mkoa ukiwa utakuja zanzibar na kila ajae anapewa shamba au kiwanja kutakuwa hakuna tena zanzibar wewe vipi.))
Hivyo, kutokana na udogo wake basi ni lazima kuwe na nafasi za kuwalinda Wazanzibari.((ndio kabisa ))Hivyo ardhi ni kwa ajili ya Wazanzibar na ajira mbalimmbali ni kwa ajili ya Wazanzibari.((ndio kabisa ndio wenye nchi ati)) Ni sawa sawa na kule Marekani ati mtu wa California akienda Michigan aonekane ni mgeni na asiwe na haki hizo japo na yeye ni Mmarekani.((ile ni marekani hii ni zanzibar na tanganyika unajuwa ni nchi ngapi zile za marekani au wewe unathani ni nchi moja tu..?))
Katika mfumo huu ambao tunaambiwa una kero nyingi mara nyingi kinachoitwa “kero” ni kile ambacho Muungano unaathiri Zanzibar.((ndio kabisa muungano umeimaliza zanzibar sio kuiathiri tu bali imeuwa kabisa zanzibar)) Lakini maoni yangu ni kuwa kama kuna kero kubwa ya kimfumo ni ile ambayo inawabagua watu wa Bara wanapoenda Zanzibar au wanapotaka kuishi na wao kunufaika na Zanzibar kama sehemu ya nchi yao.((kwa nini iwe lazima zanzibar na sio Kenya,Uganda,Burundi,Rwanda ambazo mumepakana mipaka huku mpaka muvuke bahari kwa nini..??)) Wakati Bara mtu anaweza kutoka Kigoma na kwenda Arusha au kutoka Mwanza kwenda Tabora kujaribu maisha na asipate shida yoyote ya kuonekana mgeni alimradi yeye ni Mtanzania((sio mtanzania mtanganyika na yote hiyo ni mikoa ya tanganyika sasa tabu iko wapi na nyinyi nyote ni watanganyika ni nyinyi kwa nyinyi tabora arusha mwanza kigoma mumeungana mulikuwa na nchi zenu kwanza..??)) mtu huyo huyo akienda Zanzibar ataonekana mgeni na hatopewa ule ulinzi wa kisheria ambao yeye kama Mtanzania anao katika nchi yake.
Mtu wa Bara anapoenda Zanzibar ni kana kwamba anakwenda nchi nyingine((ndio ni nchi nyengine ushasahau kama tuliungana..??)) lakini Mzanzibari akija Bara anaenda sehemu ya nchi yake.((hata siku moja tunajuwa tukija bara ni wageni tena ndio mukatuita wapemba au wewe hujuwi..??)) Hivyo, swali ambalo huwa watu wanauliza kwanini Wazanzibari wanapewa ajira kwenye wizara zisizo za Muungano lina makosa kwa kiasi chake. Lina makosa kwa sababu Mzanzibari ana haki zote kama Mtanzania lakini si kila Mtanzania ana haki sawa Zanzibar – japo nayo ni Tanzania.((nikuwa hakuna tanzania ni ngozi tu))
Mzanzibari anapo omba nafasi kwenye chuo kikuu chochote Bara anafanya hivyo kama Mtanzania na nina uhakika Bodi ya Mikopo inatoa mikopo kwa Wazanzibari vilevile – kwa sababu na wao ni Watanzania.((huwo ni uwongo wazanzibari kibao wemenyimwa mikopo ili waendele kuwa wajinga na watanganyika waerevuke ili muendele kututawala.))  Mzanzibari anaweza kuomba kazi kwenye idara au vitengo vya Bara ambavyo si vya Muungano na akapewa ajira hiyo((hata siku moja unaota wewe)) – si kama mgeni (kwa mfano Mkenya au Mganda) bali akapewa nafasi kama Mtanzania kwani hiyo ni haki yake.
Lakini mtu wa Bara hawezi kuomba ajira kwenye idara au kitengo Zanzibar akachukuliwa kama Mtanzania tu; itapaswa ajibu swali kama yeye ni Mzanzibari. Kwani Wazanzibari wana urithi Zanzibar na wana urithi Bara.((hapa wazanzibari wanaurithi wa zanzibar yao tu na urithi ulikuwepo tanganyika wazanzibari hata mukitupa hatutaki chukueni nyinyi ndio maana hatutaki tena tuna taka kila moja awe na nchi yake kama tulivyokuwa awali))
Ni katika hili tunaweza kuona kuwa kutozungumzia uwepo wa Jamhuri ya Muungano ni kosa kubwa. Kama Wazanzibari wanataka kuendelea kuwa na nchi yao na ambayo watoto wao watairithi basi wapewe nafasi hiyo.((habu muambiye raisi wenu wa tanganyika kikwete afanye hivyo)) Watu wa Bara nao wapewe nafasi ya kufurahia urithi wao bila watu “wengine” kupewa urithi wasioutaka.((haswana tutaendele kuishi kwa amani na kama majirani))  Kosa hili la kutokuzungumzia “uwepo wa Muungano” ni kosa ambalo bado litaendelea kutuandama kama jinamizi.
Watu wa Bara nao wataanza kuchoka kuona nafasi “zao” zinachukuliwa na Wazanzibari wakati wao hawawezi kuchukua nafasi kule Zanzibar((hata tatizo wabara hawataka kutupa uhuru maana wao ni wakoloni weusi mumetupinduwa mwaka 1964 na mpaka leo zanzibar ni koloni la tanganyika ndio ukaona watanganyika wamengangania kuizuwia zanzibar maana wanajuwa ikipata uhuru tu basi)) bila ya kuonekana wanachukua nafasi za “Wazanzibari”. Hivyo, japo ni kweli wanaweza kutuletea Katiba mpya, ((sisi wazanzibari hatuwaletei nyinyi katiba mutajiletea wenyewe maana katiba yenu imeja viraka zanzibar inakatiba yake haina wasi wasi))hali halisi ni kuwa bado tutakuwa na tatizo lile lile la zamani; Muungano. Hata tukiwa na serikali tatu bado matatizo yatakuwa yale yale.
Je, Wazanzibari watakuwa na haki zozote Tanganyika..? Je, Watanganyika watakuwa na haki zozote Zanzibar..? Kosa hili litakuja kutugeuka mbele ya safari na kutuumiza kama Taifa.((litawaumiza nyinyi watanganyika wazanzibari tushaumia tushakufa tushafufuka na sasa tunataka nchi yetu nyinyi hata kuamka bado na kuuliza viongozi wenu nchi yenu ya tanganyika iko wapi hamuwezi je atakae umia nani..??)) Tufikirie

No comments:

Post a Comment