Friday, April 5, 2013

KUMBE ZAWADI YA SH/MILLIONI 10 KAMISHNA MUSSA ALI MUSSA ALIKUWA ANAZITAKA YEYE DUUUUUH!!!!


HII NI SIKU YA MUSSA ALI MUSSA ALIPOKATHIBIWA UKAMISHNA NA WAKOLONI WEUSI TANGANYIKA NA KUAMBIWA WASHUGHILIKIE WAZANZIBARI NA ANAJITAHIDI ILA THULMA HAIDUMU M/MUNGU ASHANZA KUMUMBUWA AIBU TUPU SASA KWA MUSSA NCHINI ZANZIBAR.

BAADA ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar (DDP MASHUZI) kulitaka Jeshi la Polisi kumwachia mtuhumiwa Mussa Omar Makame kutokana na ushahidi kutojitosheleza na kufahamu kuwa hii sasa ni thulma anafanyiwa kijana wawatu,(DPP MASHUZI) akamuwa aoshe mikono yake na kufuta mathila yasije yakamkuta siku ya kiyama kwa kumthulumu, kijana huyu na kuamuwa kulitupilia mbalini faili la uwongo na jeshi hilo sasa limeingia kwenye mkorogano.
Wiki iliyopita jeshi hilo lilitangaza rasmi na kwa vishindo vikubwa kuwa wamemkamata Makame pamoja na watuhumiwa wengine na kudai kuwa ndiye aliyemuua Paroko wa Parokia ya Mpendae, Padri Evarist Mushi, kwa risasi huku wenzake wakitajwa kuhusika kuwajeruhi viongozi wengine wa dini hapa nchini Zanzibar.
Tukio hilo pia liligusiwa na Rais Jakaya Kikwete katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi Machi, akisema limehusisha vyombo vya nje vikishirikiana na jeshi la polisi nchini kauliwa sheikhe kitope tena kwa mapanga Kikwete kimyaaaa.
Hata hivyo, jeshi hilo jana lilikana kabisa kuwa halikushirikiana na vyombo vya nje katika uchunguzi huo uliomtia hatiani Makame baada ya ushahidi wao kukataliwa na Mkurugenzi wa Mashataka, Ibrahimu Mzee Ibrahimu.VICHEKESHO HIVYO.
Katika mahojiano na Muandishi wetu wa siri, Kamishna wa Polisi nchini Zanzibar, Mussa A. Mussa, alikanusha kata kata jeshi lake la polisi kushirikiana na kikosi cha upelelezi cha Marekani (FBI) ili kumkamata Makame.duuuuuuh
Laa jabu sasa tunaona kuwa Kauli yake inakinzana na ile aliyoitoa Machi 23, mwaka huu sio hata baada ya miaka kumi laaa mwaka huhu na ashasahau kasema nini ujuwe kuwa ni muungo,mnafiki,fitna na mzandiki anataka kumthulumu kijana wa watu ili achukuwe yeye hizo pesa m/mungu mkubwa anamumbuwa huyu.Pia kamishna aliposema uchunguzi huo ulikuwa ukifanywa na makachero wa polisi kwa kushirikiana na wapelelezi kutoka Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) na kufanikisha kumkamata mtuhumiwa huyo.
Hatua hiyo ilikuwa ni baada ya jeshi hilo kulaumiwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam, nchini Tanganyika Mwadhama Polikarp Kardinali Pengo, kuwa limekuwa kimya kuhusu matukio hayo na kusingizia kwamba yanafanywa na vikundi vya wahuni kwa kutaka kumfurahisha mfalme wake ndio wakamtia mbaroni kijana wa watu.
“Mhusika wa mauaji ya Padri Mushi tayari amekamatwa na ametambuliwa na watu walioshuhudia tukio hilo la kupigwa risasi na kusababisha kifo,” alisema Mussa katika mkutano wa wanahabari na muandishi wetu wa siri wa free zanzibar people from mkoloni mweusi alikuwepo akimsikiliza tu anavyo bwabwaja tu.
Aliongeza kuwa picha ya kuchora ya mtuhumiwa huyo pamoja na taarifa za kiintelijensia zimesaidia kwa kiwango kikubwa kukamatwa kwake kamishna Mussa A Mussa akiendele kubwabwaja na kujifaharisha.
“Baada ya kuitoa picha ya mchoro katika vyombo mbalimbali vya kiulinzi, wananchi, vyombo vya habari na mitandao ya kijamii, mtuhumiwa ametambuliwa,” alisema kamishna Mussa A Mussa.
Kamishna Mussa alifafanua kuwa mtu aliyesaidia kupatikana kwa mtuhumiwa huyo atakabidhiwa zawadi yake ya sh milioni 10 kimya kimya kutokana na sababu za kiusalama. VICHEKESHO HIVYO.
Katika mkorogano huo wa taarifa kuhusu Makame, tamko rasmi la Jeshi la Polisi nchini lililotumwa kwa vyombo vya habari halikumtaja mtuhumiwa kwa jina likidai uchunguzi unaendelea lakini Kamishna Mussa kwa kutaka kujifaharisha na kujionyesh na kuzidi kuwaonyesha wafalme wake Tanganyika kama yeye ni goood boy alimtaja kuwa ni Mussa Omar Makame.
Kamishna Mussa jana alimueleza muandishi wetu wa siri wa free zanzibar people from mkoloni mweusi kuwa licha ya DPP kusema Makame hana hatia, wataendelea kumshikilia kwa uchunguzi zaidi!!!! MANENO HAYOO mtu hana hatia na wewe bado unamshikilia sheria ya wapi hiyooo..???
“Sisi tutaendelea kumshikilia hata kama DPP hakuridhika na upelelezi tuliofanya, tuna taratibu mbalimbali ambazo si lazima kuzitaja kwa sasa,” alisema kamishna Mussa A Mussa. POROJO HILOO SASA.
Alipotakiwa kufafanua kama ni kweli (FBI) hawakushirikiana nao katika uchunguzi huo,pia ni kweli kuwa (FBI) waliondoka bila yeye kujuwa na hata hawakumuaga kamishna huyo aliomba apigiwe simu baadaye kwa madai kuwa alikuwa na kazi, lakini alipotafutwa tena hakupokea tena simu yake. duuuuuuuuuuuuuuuuuuuh
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai nchini, Isaya Mungulu, alipotakiwa kuzungumzia mkorogano huo wa kauli, alidai apigiwe Kamishna wa Zanzibar ndiye anayejua vizuri kuhusu ishu hiyo.kwa mara nyengine tena tunagunduwa kuwa polisi viongozi wetu wote wa nchi yetu ya Zanzibar hawana haki ya kuwa na kazi hizi walizo nazo maana hawajuwi hata kazi zao wao wamo wamo tu alimuradi tunge yende kinywani na watoto wake wanasoma skuli za bei juu na kujijengea majumba makubwa makubwa kwa pesa za wizi za wavuja jasho masikini za mungu.

No comments:

Post a Comment