Tuesday, April 2, 2013

WAKIRISTO KUTOKA NCHI YA TANGNYIKA WAISHIO NCHINI ZANZIBAR WAMEPATA ULINZI WALIO KUWA WAKIULILIA


Padri Cosmas Shayo wa kutoka nchini Tanganyika abae anaishi nchini Zanzibar katika kanisa katoliki nchi  Zanzibar.
Waumini na rai wa nchi ya Tanganyika wa dini ya Kikristo waishio nchini Zanzibar wamesali ibada ya Pasaka wakiwa chini ya ulinzi mkali wa askari polisi wenye silaha katika makanisa mbalimbali nchini humu Zanzibar.
Uchuguzi wa free zanzibar people from mkoloni mweusi mjini Zanzibar umebaini hali hiyo imetokana na hofu ya viongozi wa dini hiyo kuwa woga ile mbaya na kuhisi kutetemeka pasi na kujulikana ni nini haswa kinacho zidi kuwatia hofu.
Askari hao walianza kuimarisha ulinzi Ijumaa na kuendelea hadi jana katika makanisa mbalimbali likiwamo kanisa la Katoliki la mtakatifu St. Joseph lililopo eneo la shangani katika mji mkongwe wa nchi Zanzibar na kanisa la Anglikana Mkunazini.
Makanisa mengine ni kanisa la Kijili la Kilutheri Tanganyika (KKKT) na kanisa la Assembly of God Tanganyika, (TAG) askari walionekana kuimarisha ulinzi nyakati za kuingia na kutoka kwa waumini hao ambao wengi ni watu wakutoka nchi jirani ya Tanganyika kwenye makanisa hayo.
Aidha, pengine kutokana na hofu hiyo iliyopo nchini Zanzibar, makanisa madogo (vigango) kwa mara ya kwanza hayakutumika kwa ibada ya Pasaka na waumini wote walitakiwa kusali kwenye makanisa makubwa ili waweze kujihisabu ni watangnyika wangapi na ni wakiristo wangapi ambao bado wanaendele kuishi nchini Zanzibar huku ratiba ya ibada ya mkesha ikifanyiwa marekebisho makubwa kwa sababu uwoga wao na hofu iliyo waingia na kutetemeka mwili mzima.                                                                                                                                                                                               
Askari polisi walikuwa wakiisaidiana na askari maalumu wa makanisa wakiwahoji watu kabla ya kuingia kanisani wakiwamo waandishi wa habari kutakiwa kuonyesha vitambulisho vya kazi zao.
Wakizungumza na muandishi wetu wa siri wa free zanzibar people from mkoloni mweusi baadhi ya waumini hao wenye asili ya Kitanganyika walisema tunawalipogeza hatua sana sana polisi kwa kuimarisha ulinzi na doria wakati wote wa ibada yetu ya Pasaka na shamrashamra zake visiwani humu  Zanzibar.
“Tangu viongozi wetu kushambuliwa kwa risasi na kuuliwa tumekuwa tuikiishi kwa hofu,woga,nakutetemeka mili, hatua hii ya polisi kutulinda sisi wakiristo na nyumba zetu za ibada za kikiristo hapa janjibali kunahitaji kupongezwa,”Alisema Johm na mwakajiru wa Kanisa Katoliki.
Padri Cosmas Shayo  wa kanisa katoliki mjini hapa alisema walichukua hatua za tahadhari kwa ajili ya waumini wao kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi.
Hata hivyo, akizunguza katika ibada ya Pasaka Mchungaji Emanuel Masoud wa kanisa Anglikana alisema, SMZ ni lazima ilinde uhuru wa kuabudu kwasababu ni haki ya kila raia na mwananchi wa Zanzibar.
Aliwataka waumini wake kujiepusha na visasi na kuwataka mambo yote wamuachie Mungu kwasababu hata Mungu kupitia maandiko matakatifu amesema Yesu akikataza kulipa visasi.

No comments:

Post a Comment