Saturday, June 29, 2013

KUNA CCM YA NYERERE NA CCM YA MABEPARI NA MABEBERU NA ZOTE HAZIFAI CCM YA ZANZIBAR NI SAMAKI WALIO OZAA


Dodoma.Rais Jakaya Kikwete ameshauriwa kuondoa kigugumizi na masuala ya kulindana, ili kuinusuru nchi ya Tanganyika isitumbukie katika shimo refu zaidi la umasikini kuliko ilivyo sasa.
Wito huo ulitolewa jana na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Tawi la Afrika Kusini na nchi zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara, Kelvin Agutu Nyamori, alipozungumza na muandishi wetu wa siri wa FREE ZANZIBAR PEOPLE FROM MKOLONI MWEUSI nje ya viwanja vya bunge mjini Dodoma.
Nyamori alibainisha kuwa kinachoiua Tanganyika ni kitendo cha kuoneana haya ndani ya CCM na Serikalini ambako kunafanywa na viongozi wa juu akiwemo Rais Jakaya Kikwete.
“Nikisema rais ana kigugumizi na amekuwa akiwaonea haya zaidi watu sio kwamba namkashifu wala si kwamba nimemdharau, bali nataka atimize wajibu wake kwa kuwawajibisha wabovu na wazembe na kuwapa nafasi wachapa kazi kusonga mbele,” alisema Nyamori.
Alisema ukimya wa rais unafanya wananchi waamini na ndivyo ilivyo kwamba hakuna kiongozi mzuri atakayekuja kupatikana kutokana na wengi kuendelea kurithishana nafasi za uongozi kwa hofu ya kulinda vitumbua vyao,lakini bado kiongozi mkuu anashindwa kuwawajibisha wenye mitazamo hiyo.
Mwenyekiti huyo aliwatupia lawama washauri wa Rais Ikulu,kwamba wameshindwa kutimiza wajibu wao kiasi cha kumfanya aonekane kama hafai kwa jamii anayoiongoza.
Akizungumzia msimamo wa CCM kwa sasa, alisema chama hicho kikongwe kimepoteza mwelekeo kwa kiasi kikubwa na kimegawanyika kutokana na maslahi na matakwa ya wanasiasa ambao wengi sio wema.
“Tuna vyama vya CCM viwili kwa sasa, kimoja ni CCM ya Mwalimu Nyerere ambayo ni CCM nambari One, na ya pili ni CCM ya mabepari na mabeberu ambayo haijui kama kuna watu wa kada ya chini na badala yake wao wanajipendelea wenyewe,” alisema.
Alishauri kuwepo na mabadiliko makubwa ya kiuchumi kwa Watanganyika bila ya kujali itikadi zao za vyama vya kisiasa kwani Tanganyika kwanza mambo mengine nyuma.

Friday, June 28, 2013

VIDEO-CCM NA CUF NANI MWENYE MATUSI..? BALOZI MDOGO WA NCHI YA TANGANYIKA ALALAMIKA KWA KUPEWA MAJINA.


Balozi mdogo wa nchi ya Tangnyika aliye nchini Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd amehadharisha kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa inaweza kumeguka, iwapo viongozi wataendelea kutumia vibaya majukwaa ya kisiasa kwa kutoa kauli za chuki na matusi na kukashifu Serikali kwa maslahi binafsi.
Ingawa Balozi Idd alisema uhusiano wa viongozi wakuu watatu wa nchi ni mzuri: Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad na yeye Balozi Seif Ali Idd, wanafanya kazi vizuri.
Balozi huyo mdogo wa nchi ya Tanganyika, alikishutuma Chama cha CUF kwa kutumia majukwaa ya kisiasa vibaya. Alidai kinatumia lugha za matusi dhidi yake na kumpa majina mabaya.
Alisema kasoro kubwa zinajitokeza katika majukwaa ya kisiasa ambako viongozi wamekuwa wakitoa kauli za chuki zenye kutia wasiwasi mkubwa wananchi na kuhoji uhusiano wa viongozi hao kiasi cha kutukanana hadharani.
Akifanya majumuisho na kujibu hoja za Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliyochangia Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais kwa mwaka ujao wa fedha juzi, Balozi Idd, alilaumu hususan viongozi wa CUF.
Maalim Seif ni Katibu Mkuu wa Chama hicho, alisema katika mikutano yao yote wanayofanya, wamekuwa wakitumia vibaya majukwaa kumtukana yeye binafsi na kumchonganisha na wananchi na Serikali iliyopo madarakani.

“Napenda kuwaambia wananchi uhusiano wa viongozi wakuu wa Serikali ni mzuri sana…lakini majukwaa ya kisiasa yanatumiwa vibaya kutukanana…Tukiendelea hivyo hatufiki pahala na tutarudi tulikotoka,” alisema Balozi huyo wa nchi ya Tanganyika Balozi ali iddi.
Kwa mujibu wa Balozi huyo wa nchi ya Tanganyika, alisema amekuwa akipewa majina mabaya na viongozi wa CUF katika mikutano ya kisiasa; likiwemo ‘LAANATULLAHI’ wakimaanisha kumlaani. Jambo ambalo alisema anawauliza “amewakosea nini”?. ULICHO WAKOSA WAZANZIBARI NIKUWALAZIMISHA KUBAKI NA MUUNGANO FEKI WA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA NA KUWAFITINISHA ILI WAANZE KUKOSANA ILI WEWE UWATAWALE NA USHA ANZA KUWAFITINISHA NA KUSEMA UTAWARUDISHA WALIKO TOKA KAMA SIO FITINA NI NINI..? PIA KUJIJEGEA MAISHA MAZURI NA KUIBA PESA ZA WAVUJA JASHO NA KUZIPELEKA TANGANYIKA KWA MASULTANI WAKO NA LAMWISHO UKATIA FITINA MPAKA MASHEIKH WAKASHIKWA NA KUTUPWA JELA UNAFIKIRI HATUJUWI. KAMA HUJUWI LEO TUNAKUAMBIA FITNA ZAKO MWAKA HUU ZIMEPIGA MBIZI KWENYE MAJI YA UGOKO.
Balozi Idd, aliwahadharisha viongozi hao kwamba lengo la Serikali ya Umoja wa Kitaifa ni kuleta mshikamano kwa Wazanzibari wote.(MASHEIKH WA UAMSHO NI WAZANZIBARI WATOWENI BASI JELA KAMA KWELI MNATAKA KULETA MSHIKAMANO KWA WAZANZIBARI WOTE NA WAO PIA NI WAZANZIBARI LAKINI NYINYI NI KUSEMA TU NYOYO ZENU ZIMEJA KUTU ZA KUTAKA KUUWA NA KUTESA WATU ILI MUDUMU MILELE KWENYE MADARAKA ASIYE JUWA NINI).
Alionya, kwamba watu wanaweza kurudi ambako walikuwa hawazikani wala kushirikiana katika matukio kutokana na siasa za chuki na uhasama kutawala tangu ulipoingia mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992.
“Tuache kutukanana katika hadhara za majukwaa ya kisiasa…Hawa CUF sijui nimewakosea nini na kama majina yanachuna basi tayari ngozi yangu ingeathirika,” alisema Balozi Idd.
Alikumbusha viongozi na wananchi kwamba kilichounganishwa ni Serikali yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa, lakini vyama vya siasa na sera ni tofauti na hakuna sababu ya kulumbana katika hilo.
Awali, Waziri wa nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud alisema Tume ya uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) iko kwenye mchakato wa kuboresha daftari la wapiga kura nchini kote.
Alitaka wanasiasa kujenga tabia ya kuwaamini watendaji wa taasisi hiyo na kuacha kuwahukumu kwa kuwashutumu, kitendo ambacho kinaweza kuzorotesha utendaji wa kazi hiyo.
“Tume hii imefanya kazi vizuri sana tangu mchakato wa kura ya maoni mwaka 2010 pamoja na kusimamia uchaguzi mkuu ambao ulikwenda vizuri na vyama vyote kuridhika,” alisema Aboud.
Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, iliundwa baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, 2010 kutokana na matakwa ya wananchi kupitia kura ya maoni na kushinda kwa zaidi ya asilimia 64.
Muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, unajumuisha Vyama vya CCM na CUF, ulifikiwa ili kuondoa siasa za chuki na uhasama katika visiwa vya  Zanzibar..

WEWE BALOZI NDOGO WA TANGANYIKA HEBU ANGALIA HIZI VIDEO KESHA JIULIZE NI NANI NA NANI ANAYEFANYA MKUUTANO NA KUTUKANA.WEWE NI MOJA KATI YA WATU AMBAO MULIPINGAA KWA GUVU ZOTE KUSIWE NA SEREKALI YA UMOJA WA KITAIFA LAKINI IKAJA NA GUVU ZA MOLA NA WAZANZIBARI WENYEWE SIO CCM WALA CUF WALA HUWO MUUNGANO WAKO FEKI UNAO UKAZANIA UBAKI WALA WAZANZIBARI HAWATARUDI WALIKOTOKA WAZANZIBARI WATAUNGANA NA KUPIGANA MPAKA TUPATE NCHI YETU NA WEWE BALOZI MDOGO WA WATANGANYIKA UKITAKA UNGANA NASI AU HAMA ZANZIBAR UKAISHI TANGANYIKA ULIKO EKEZA LAKINI HAPA NI ZANZIBAR TU KWANZA SHENGESHA BAADAYEE.

Thursday, June 27, 2013

BI FATMA FEREJI NA BAJETI YAKE YA KUMALIZA NYUMBA YAKE NA MAPAZI MAPYA


kiasi cha sh 3.20BILLIIIIIIIIIIIIIONI zitatumika katika ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,katika mwaka wa fedha 2013/2014,
Hayo yalibainishwa na Waziri katika ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,Fatma Ahabibu Fereji alipokuwa akisoma bajeti hiyo.
Kiasi cha SH 1 Bilioni kwa ajili ya kuendeshea kazi za Ofisi ya Makamo wa kwanza wa Rais.duuuuuh bi fatma wee huwachiiiiiiiii
Kiasi cha SH 510.07 Milliioni zitatumika kwa shughuli za makamo wa kwanza wa rais kwa kazi za kawaida. duuuuuuuuh bi fatma unataka kuezeka nyumba yako nini..???
Kiasi cha Sh 257.28 Milioni za mishahara za ofisi ya makamo wa kwanza wa Rais. duuuuuuuh kwa lipi munalo fanya mpaka mujilipe mishahara hii..?? wakati walimu mpaka leo mishahara yao duni.
Kiasi cha 768 Millioni kwa ajili ya Shughuli za ukimwi. duuuuuuh!!!!!!!
Pia bi Fatma  aliwaomba wajumbe wasisite waipitishe bajeti hiyo. hataka kama washakushtukizia kuwa unaziibaa wasisitishe wakuachiye tu ukazivurunge sio bi fatma fereji..?
Jamani Jamani Jamani kuna skuli hazina madeski mpaka leo,kuna barabara hata vumbi hazina tena,kuna watu wanaishi kwa njaa hata mlo mmoja hawana,kuna wajane ,mayatima,mafukara jamani msalieni Ntume nyuso zimewapara kwa kuiba hata haya hamuna tena
Hivi mumewekwa mle au musaidie wananchi SHAME ON 
YOU ALL.MUOGOPENI MWENYEZI MUNGU NYINYI.

Wednesday, June 26, 2013

SERIKALI YA TANGNYIKA MJINI DODOMA YATOA TAMKO KUHUSU KAULI YA WAZIRI MKUU. YADAI POLISI WANARUHUSIWA KUPIGA NA KUUA KISHERA!!!!!!!!! DUUUUUUUUUUUUUUUH

BOSS WAKE KANYWA MKOJO YEYE ANAKULA MAVI HASWAA  AMAKWELI UDIKTETA NI UDIKTETA TU UTAJIFICHA MWISHO UTATHIHIRI TU NDIO HUU SASA KISHA WANASEMA NI  NCHI YA DIMOKRATI MAVI YENU.
Serikali ya Tanganyika imetoa tamko bungeni kuhusu mauaji ya raia mikononi mwa polisi ikieleza kuwa ni sheria ya kanuni ya adhabu inaruhusu kutumia nguvu za kadiri hata kiasi cha kusababisha madhara au kifo.
Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda anaye wapinda Watangnyika  kunukuliwa bungeni akiwataka polisi kuwashughulikia kwa kuwapiga watu wote wanaokaidi kutii sheria.
Namnuku,  Nasema wapigwe tu, maana tumechoka sasa,” alisema Pinda alipojibu maswali ya papo hapo Alhamisi iliyopita.
Akisoma tamko hilo bungeni jana, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alisema kuwa kifungu cha 18(B) na 18(C) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu kinatoa uwezo kisheria wa kutumia nguvu za kadiri hata ikibidi kiasi cha kusababisha madhara au kifo katika mazingira ya kisheria.
Aliyataja mazingira hayo kuwa ni pamoja na kuokoa uhai wa mtu mwingine, kuzuia madhara makubwa ya mwili yasitokee kwake au kwa mtu mwingine na kumzuia mtu anayetenda tendo ovu la kubaka au kunajisi mtoto au kufanya vitendo kinyume na maumbile.
Pia kumzuia mtu anayevunja nyumba usiku au unyang’anyi wa kutumia silaha au kuchoma nyumba moto au kufanya kitendo chochote kinachohatarisha uhai wa mtu au mali.
Alieleza kuwa Kifungu cha 18 na 18(A) cha Sheria ya Adhabu Sura namba16 iliyofanyiwa mapitio mwaka 2002, kinampa haki mtu yeyote akiwemo askari kujilinda, kumlinda mtu mwingine, kulinda mali yake au mali ya mtu mwingine ikiwemo ya Serikali na taasisi zake, ambayo iko chini ya uangalizi wake kisheria.
Kauli hiyo ya Serikali ya Tanganyika kuhusu mauaji ya raia mikononi mwa polisi, ilitolewa ikiwa ni ufafanuzi wa jibu la swali la nyongeza lililoulizwa bungeni Mei 28,2013 na Rashir Ally Abdalah (Tumbe-CUF), ambapo Silima alisema mauaji yanayofanywa na askari polisi ni mauaji ya kisheria.    duuuuuuuuuuuuh 
Kutokana na kauli hiyo, Mbunge wa Wawi, Hamad Rashi Mohammed aliomba mwongozo wa spika kupata ufafanuzi wa kauli hiyo, na jana Silima kutoa kauli ya Serikali kujibu mwongozo huo.
“Ikumbukwe pia kuwa, kifungu cha 29 cha Sheria ya Jeshi la Polisi na Polisi wasaidizi Sura322, pamoja na Kanuni za Kudumu za Utendaji za Jeshi la Polisi Na274, vinampa haki ya kisheria askari polisi kubeba na kutumia silaha za moto ikiwamo bunduki na mabomu katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku..,”alisema Silima.
Alifafanua kwamba katika kutafsiri sheria, kanuni na taratibu mbalimbali ikiwamo alizozitaja, mahakama katika nyakati tofauti imetoa msimamo wa kisheria juu ya suala hilo.
Akitoa mfano alisema: “Mathalan katika kesi ya Seif Mohamed Senzagala dhidi ya Jamhuri ya mwaka 1994 kama ilivyonukuliwa na Tanzania Law Report ukurasa wa 122, ambapo mshitakiwa (mwomba rufaa) alimjeruhi kwa panga mlalamikaji ambaye alimfuata nyumbani kwake na kuanza kumshambulia.”
Alisema katika kesi hiyo,mahakama ya rufaa pamoja na kuridhia uamuzi wa mahakama ya awali wa kumtia hatiani kwa kutumia nguvu kupita kiasi, ilibainisha kuwa mshtakiwa hakustahili adhabu kwani alitenda kosa lile wakati akijihami dhidi ya mashambulizi toka kwa mlalamikaji.
“Kwa msingi huo, tarehe 28 Mei, 2013 wakati nikijibu swali Na 290, nilitumia maneno ‘mauaji yanayofanywa kisheria’ nikimaanisha mauaji yanayotokea katika mazingira niliyoeleza..,”alisema Silima.
Hata hivyo alisema siyo nia ya Serikali ya Tanganyika kuhalalisha vitendo vya matumizi mabaya ya silaha ambavyo vinaweza kufanywa na askari wasio waadilifu.
Alibainisha kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria, kuheshimu haki za raia na kutumia busara kutatua migogoro.
Hata hivyo, Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni imelaani kauli ya Serikali ya Tanganyika kuhusu mauaji ya raia mikononi mwa polisi iliyoitoa jana na kueleza kuwa haikubaliani nayo kwa kuwa inatoa baraka kwa polisi kuendeleza mauaji ya raia.
Akizungumza na mwandishi wetu baada ya kikao cha bunge kuahirishwa, Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani wa kambi hiyo rasmi, Vicent Nyerere alisema kauli hiyo ingekuwa na uthabiti kama askari polisi wangekuwa waadilifu.
“Kauli ingekuwa thabiti kama polisi wangekuwa waadilifu. kabla ya kutoa kauli hiyo, Serikali ilitakiwa kuchuja miongoni mwa askari wa jeshi la polisi, wa ngazi zote na kuwaondoa wasio waaadilifu ndipo wakatoa kauli hiyo wananchi wataielewa Serikali ya Tanganyika,”alisema Nyerere ambaye pia ni Mbunge wa Musoma Mjini(Chadema).
Kwa upande wake, Mbunge wa Ole, (CUF) Rajab Mbarouk Mohammed akizungumzia kauli hiyo ya Serikali ya Tanganyika alisema kuwa majibu ya Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima ni ya kisiasa.
Alisema kwamba kauli hiyo ni mwendelezo wa kauli iliyotolewa Alhamisi iliyopita na Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akiwataka pilisi kuwashughulikia kwa kuwapiga watu wote watakaokaidi kutii sheria.
“Hakuna mwenye haki ya kuua, kuua ni kuua tu. Mahakama pekee ndiyo ina haki ya kuhukumu kifo baada ya kumtia hatiani mshtakiwa husika. Lakini kuwa polisi wanafundishwa utii, siyo kuua,”alisema Rajab.
Alifafanua kuwa kazi ya polisi ni kulinda raia na mali zao na kwamba kuruhusiwa kujihami haimaanishi kuua raia.
Nao Wabunge Aeshi Hilaly na Aly Keissy walisema ni vizuri raia wakatii mamlaka iliyopo na kutekeleza utii wa sheria bila shuruti.
Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Murtaza Mangungu alisema: “Maoni yangu haki za watuhumiwa lazima ziheshimiwe.”
Rais wa Chama cha Wanasheria nchini Tanganyika, (TLS), Francis Stola alisema hakuna sheria inayompa mamlaka askari polisi kutumia nguvu za ziada ikiwemo kupiga raia pindi anapotekeleza majukumu yake,isipokuwa tu anaweza kutumia nguvu kiasi iwapo raia anayekabiliana naye anaonyesha vitendo vya kukaidi amri ama kuhatarisha usalama.
Stola ambaye alikuwa akitoa ufafanuzi wa kisheria kuhusiana na kauli bungeni alisema kuwa kwa kufuata sheria polisi haruhusiwi kupiga raia. “ Ukisoma sheria hakuna mahala utakuta kuna neno limeandika piga…. Askari polisi anachoweza kufanya ni arrest(kamata) na siyo vinginevyo, hana mamlaka kabisa ya kupiga raia”
Alisema sheria imetamka wazi kuwa kunapojitokeza hali yoyote inayopaswa kdhibitiwa na vikosi vya ulinzi, nguvu inayopaswa kutumika ni ile ya kawaida na kwamba kitendo cha kutumia risasi za moto ama kupiga raia ni ukiukwaji wa sheria za nchi.
Alisema polisi anapaswa kutoa mwongozo kwa raia kumwelekeza jambo la kufanya iwapo kunajitokeza hali ya sintofahamu,lakini hapaswi kutumia nguvu kupita kiasi ikiwemo kuwapiga raia
“ Sheria inasema wazi kwamba panapojitokeza hali yoyote korofi, polisi wanatakiwa kutumia nguvu ya kawaida tu kukabiliana na hali hiyo na wala siyo kutumia silaha za moto… silaha za moto zinaweza kutumika tu iwapo kunajitokeza tukio ambalo linaweza kuhatarisha usalama wa maisha ama mali isipotee” alisema
Kuhusu wananchi kufanya maandamano, rais huyo alisema maandamano ni haki ya msingi ya kila raia,lakini yanafanyika katika utaratibu maalumu. “ maandamano ni haki ya kila raia lakini panapaswa kuwa na utaratibu maalumu…. Kama kunajitokeza maandamano ambayo hayana utaratibu polisi wanapaswa kutumia reasonable force (nguvu ya kawaida) kudhibiti maandamano hayo na wala siyo kutumia nguvu za ziada.

Tuesday, June 25, 2013

RAISI UHURU KENYATTA ZIARANI NCHINI URUSI, CHINA NA JAPAN WIKI HII.


Nairobi. Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, anatarajiwa kuanza ziara ya wiki tatu katika mataifa ya Ulaya Mashariki na Asia, katika kile kilichoelezwa kwamba ni kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na kiuchumi kati ya nchi hizo na Kenya.
Uhuru anatarajiwa kuondoka mjini Nairobi wiki hii kuelekea Moscow, Russia kabla ya kuzuru China na hatimaye Japan.
Uhuru anafanya ziara hiyo na huku  Rais Barack Obama wa Marekani anayetarajiwa kutua nchini Tanganyika wiki ijayo.
Kiongozi huyo wa Marekani anakuja nchini Tanganyika akiwa katika ziara yake ya pili katika bara la Afrika.
Uhuru  itakuwa ni safari yake ya kwanza kuzuru nchi za mataifa ya Ulaya Mashariki na Asia katika mabara hayo.
Hata hivyo ziara hiyo haitamfikisha katika nchi ya asili yake, Kenya raisi Obama.
Katika siku ambazo Obama atakuwa nchini Tanganyika, Uhuru atakuwa nchini China, moja ya mataifa hasimu ya Marekani, akitokea Russia, taifa hasimu kwa Marekani pia.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa wasaidizi wake wakuu, Rais Uhuru anahitaji kutumia fursa ya umuhimu wa mataifa ya mashariki katika kukuza uchumi wa Kenya kwa kuimarisha zaidi uhusiano wa kibiashara.
Akiwa nchini Urusi, Uhuru atatembelea viwanda vya silaha na kukutana na maofisa wa juu wa Serikali, kisha kutia saini makubaliano yanayohusu biashara baina ya nchi yake na Urusi.
“Ziara hii ilipangwa mahususi kwa Rais Uhuru Kenyatta kutembelea nchi rafiki na haikuwa na uhusiano wowote na ziara ya Obama nchini Tanganyika,” alisema mhadhiri Profesa Munene Macharia.
Alisema nchi hiyo kwa sasa inajaribu kutoa kipaumbele kwa nchi marafiki zinaonyesha utayari wa kushirikiana na Kenya, akizitaja kuwa ni Urusi na China.
Kuhusu ziara hiyo, wasaidizi wa Rais Uhuru wamekanusha taarifa kwamba imenuia kujenga himaya mpya na nchi mahasimu wa Marekani katika kipindi ambacho Obama anatembelea bara la Afrika.

ASHA BAKARI NA MUNGU WAKE WA MWENGE-WAZANZIBAR NA M/MUNGU NA MAMLAKA KAMILI YA ZANZIBAR NANI ATASHINDA..???

SERIKALI ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar,inasikitisha sana sana baada ya kuanza kupata mpasuko kutokana na mawaziri wake kukosa umoja na kujitenga kwa baadhi ya shughuli za viongozi wa juu wa seriakli hiyo.
Aidha, imeelezwa katika mpasuko huo unaodaiwa kuikumba serikali hiyo, ni mawaziri wake kukosa ushirikiano kwa kushindwa kuwapa mapokezi stahiki, viongozi wake wa kitaifa.
Hayo yalielezwa juzi katika Baraza la Wawakilishi na Wajumbe kutoka vyama vya CCM na CUF wakati wakichangia Bajeti ya ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, iliyowasilishwa na waziri wa nchi wa ofisi hiyo, Mohamed Aboud.
Akichangia hotuba ya makadirio ya ofisi hiyo Mwakilishi wa viti maalumu, Asha Bakari (CCM) alisema lengo la kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar, limepoteza mwelekeo.
Alisema mawaziri wa serikali hiyo kutoka upande wa CUF, wamekuwa wakikwepa baadhi ya shughuli za kitaifa zinazofanywa na viongozi wa juu wa serikali hiyo, kwa kutoa mfano:
Mawaziri wote wa CUF ndani ya serikali hiyo, kushindwa kuhudhuria katika sherehe za uzinduzi wa MWENGE wa uhuru uliyowashwa na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohame Shein, Chokocho Pemba May 6, mwaka huu.
Alisema kitendo cha mawaziri hao kutokuhudhuria shughuli hiyo ya kitaifa, kinakwenda kinyume na lengo la kuundwa kwa serikali hiyo, iliyoazimia kudumisha amani na umoja wa Wazanzibari:
“Mawaziri wanafika kukimbia shughuli za MWENGE wa uhuru…hali hii ni kwenda kinyume na malengo ya kuanzishwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa,” alisema Asha Bakari. Hapa ndio muandishi wetu wa siri aliye ndani ya baraza la wawakilishi alipo pingwa na butwa kuona mama huyu badala yakuzungumza mambo ya maana kama maji,umeme,afya,madawa hospitalini,barabara,bei za vyakula n.k. yeye anazungumzia MWENGE  haswa katika kipindi hichi kigumu kabisa kwa wananchi wa Zanzibar kuwa wanataka nchi yao na kuwa na mamlaka kamili yeye ndio kwanza yuko katika miaka ya sitini MWENGE DAAAAAAAAAAAAH!!!!!!!!!!!!
Naye, Mwakilishi wa Kwahani, Ali Salum (CCM) ambaye alishadidia suala hilo alisema hofu ya wananchi kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa, kushindwa kufikia malengo yake, imetimia.
Alisema wananchi wa Zanzibar, mapema walionekana kuwa na wasiwasi wakati wa kubadilishwa kwa Katiba, na kuingizwa mfumo mpya wa serikali ya umoja wa kitaifa, kutokana na kutokuwepo kwa nia njema ya kujenga Zanzibar, yenye umoja:
“Wananchi wengi wa Zanzibar walikuwa na wasiwasi kuhusu serikali ya umoja wa kitaifa nikiwemo mimi…leo wanaona wenyewe utendaji kazi wa viongozi wao wakiwemo mawaziri,” alisema Ali Salum.Na huyu nae badala ya kujenga anakuja kubomowa kabisa anajisema mwenye alikuwa na wasi wasi na serekali ya umoja wa kitaifa lazima uwe na wasi wasi maana hii sio ile serekali ya kufitinisha watu wala sio serekali ya kubaguwa watu na wewe hilo ndilo unalolijuwa sasa utafanya kazi gani na hupati kufitini wala kubaguwa watu..??? 
Hata hivyo, hoja hizo zilikumbana na kisiki, zilipingwa na Wawakilishi wa CUF, Hamad Masoud (Ole) pamoja na Ismail Jussa wa Mji Mkongwe, ambao waliibua hoja kali.
Jussa alisema viongozi wa CCM ndiyo chimbuko la tatizo, akidai kuwa: “Wameshindwa kumpa heshima Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad kwa kushindwa kujitokeza kumpokea wakati anaporudi safari za ndani na nje ya nchi,” alisema jussa:
“Ukipanda mbigiri utavuna mbigiri…mimi nimekuwa Naibu Katibu Mkuu wa CUF wakati mwengine nilikuwa nakwenda kumpokea Makamo wa Kwanza wa Rais bila kuwapo mkuu wa mkoa wala mawaziri kutoka CCM,” alisema Jussa.
Kwa upande wake, Hamad Masoud alisema wapo watu hawana nia njema na serikali hiyo, lakini alisema malengo yao hayatatimia kwa sababu imewekwa kwa mujibu wa Katiba na kwa ridhaa ya wananchi wa Zanzibar:
Alifafanua: “Katibu Mkuu Kiongozi ndiye aliyeanza kuzorotesha serikali ya umoja wa kitaifa kwa kitendo cha kutupilia mbali MAPENDEKEZO ya muundo na mfumo wa serikali hiyo,” alisema na kuongeza:
“Kukosekana kufuatwa kwa mapendekezo yale yaliyokuwa na sura halisi ya mfumo wa kitaifa kwa watendaji wa serikali kumesababisha serikali kuwa na viongozi wa kisiasa tu bila mfumo huo kuhusisha watenda wake,” alisema Hamad Masoud.
Hamad Masoud ambaye pia ni Mwakilishi wa Ole, akijadili na kuchangia Bajeti ya ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar, alitilia shaka utendaji wa Tume mpya ya uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) Na alisema:
“Ipo hatari kwa Tume ya uchaguzi ikarudisha migogoro ya kisiasa kwa sababu watendaji wake hawataki kubadilika,” alisema Hamad Masoud.

Sunday, June 23, 2013

NCHINI TANGANYIKA KIKAO KIKUBWA CHA WAKOLONI WEUSI TANGANYIKA NA WAHAFIDHINA WA KIZANZIBARI KINAENDELEA DODOMA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiongoza Kikao cha SMZ na SMT, kiliochofanyika Dodoma Hoteli, leo Juni 23, 2013. Kulia ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda, na (kushoto) ni Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Idd
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Tanganyika, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, leo ameongoza Kikao cha SMT na SMZ, kilichofanyika kwenye ukumbi wa Dodoma Giningi ya CCM na machinjio ya Wazanzibari Hoteli, mjini Dodoma, leo Juni 23 nchini Tanganyika.
Kikao hicho kimehudhuriwa pia na mhe. Waziri Mkuu Mizengo Pinda anaewapindisha Watangnyika, Balozi mdogo wa nchi ya Tanganyika nchini Zanzibar, Balozi, Seif Idd, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amani, Ali Juma Shamhuna muza bahari ya Wazanzibari kunemesha tumbo lake lisilo jaa na Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Tanganyika Samih Suluhu pamoja na washiriki wa kikao hicho Mawaziri kutoka serikali zote mbili za Tanganyika na nchi ya Zanzibar.
Mawaziri mbalimbali walioshiriki kwenye kikao hicho.
Mawaziri mbalimbali wanao shirikiana na wakoloni weusi Tanganyika kuibiya nchi yetu ya Zanzibar pia walikuwepo kwenye kikao hicho.
Mawaziri mbalimbali walioshiriki kwenye kikao hicho.
Mawaziri mbalimbali wanao ibiyaa nchi yetu ya Zanzibar kwenye kikao hicho wavuta fikra vipi tutawaibia zaidi Wazanzibari na kuwakandamiza maana Wazanzibari washamka na wanataka nchi yao na wahafidhina wetu washajulika kuwa na wahafidhina sasa tufanye nini wanaulizana.

Saturday, June 22, 2013

VIDEO-MLIPUKO WA BOMU KATIKA MKUTANO WA CHADEMA ARUSHA NCHINI TANGANYIKA-15 JUNE 2013

CCM OYEEEE CCM OYEEE CCM OYEEE
HAYA TUMEFANYIWA SANA SISI WAKATI WA UCHANGUZI HAPA ZANZIBAR HASWA HASWA PEMBA KWA KUDAI HAKI YETU WATU WAKAJITIA HAMKANI KUWA TUNAVURUGA AMANI TUKAULIWA WEEE WAZANZIBARI WATANGANYIKA MUKAWA MUNACHEKA NA KUSEMA WAPEMBA NYINYI WAKAIDI SANA MUME SAHAU KUWA M/MUNGU SIO ATHUMANI, MUMESAHAU USIMCHEKE KILEMA,PIA MUMETUOMBEA MABAYA TELE KUWA ZANZIBAR IKIVUNJA MUUNGANO TU BASI TUTAUWANA WAZANZIBARI MBONA MUNAA ANZA KUWANA NYINYI NA MUUNGANO NDIO KWANZA UNAREWAREWA. DUWA YA KUKU HAIPATI MWEWE.NDIO HII KAMA HAMUJUWI.
FREE ZANZIBAR PEOPLE FROM MKOLONI MWEUSI TUNALANI VIKALI MAUWAJI HAYA NA PIA TUNATOWA POLE KWA WALE WOTE WALIO FILIWA NA JAMAA ZAO NA PIA WALE WOTE WALIO JERUHIWA TUNAWAPA POLE.

NCHINI TANGANYIKA-JE ALIYERUSHA BOMU ARUSHA NI POLISI..???


Arusha: Mashuhuda wa tukio la mlipuko wa bomu uliotokea mwishoni mwa wiki iliyopita Jijini Arusha, wamedai kumwona na kumtambua mtu aliyehusika na tukio hilo lakini wanasema walishidwa kumkamata kutokana na “kushambuliwa kwa risasi na polisi”.

Mlipuko huo ulitokea katika Viwanja vya Soweto kwenye mkutano wa kuhitimisha kampeni za udiwani jijini humo na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi zaidi ya 100.

Mashuhuda hao ambao wote walijeruhiwa kwa risasi wanasema mlipuaji wa bomu alikuwa amevalia shati la kijivu lenye mistari myeusi na suruali ya jeans yenye rangi ya blue na kwamba wajihi wake ni mtu wa kimo cha kati.

Mmoja wa mashuhuda hao ni mlinzi katika Kikosi cha Ulinzi cha Chadema (Red Brigade) ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini, alidai kwamba alimwona mtu aliyerusha bomu mara tu baada ya tukio hilo.

Mlinzi huyo ambaye alipigwa risasi za mguuni na kifuani wakati akimkimbiza mtu huyo; alisema bomu hilo lililipuka mara tu baada ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe kumaliza kuhutubia na kushuka jukwaani.
“Baada ya Mwenyekiti Freeman Mbowe kushuka jukwaani, nikawapanga walinzi kwa ajili ya kuwalinda viongozi waliokuwa wakichangisha fedha. Ghafla nikasikia mlipuko, sikujua ni nini, lakini kuna mama mmoja alikuwa karibu yangu akanionyesha mtu aliyelipua, akisema yuleee…” alisema na kuongeza:

“Alikuwa amevaa shati la kijivu lenye mistari myeusi na suruali ya jeans ya blue. Ni mtu wa kimo cha kati. Watu walianza kumkimbiza kuelekea upande wa Magharibi wa Uwanja kwenye nyumba za NHC. Tuliruka uzio alipopita yule mtu, mara nikasikia risasi imenipata mguuni.”

“Tulikuwa na uwezo wa kumkakata yule mtu, lakini nikaona risasi zimezidi upande wetu nikaona nigeuze na hapo hapo nikapigwa risasi ya kifuani, nikaishiwa nguvu, sikuweza kufahamu mtu huyo alikoishia. Nilijikongoja na kurudi uwanjani.”

Mlinzi huyo ambaye amelazwa katika moja ya hospitali za jijini Arusha anasema alilazimika kuhama hospitali ya Seliani alikokuwa amelazwa awali baada ya kuandamwa na polisi. “Nilikaa siku tatu hospitalini bila kupata huduma yoyote, lakini kila siku madaktari walikuwa wakinihoji maswali,”alisema na kuongeza:

“Mwisho nikaambiwa kwamba nitahamishiwa ghorofa ya chini, nilipouliza sababu wakasema eti Waziri Mkuu atakuja kuniona… Niligoma mwisho daktari akaniambia kuwa kuna polisi waliovaa majoho  ya udaktari ndiyo waliotaka nihamishwe”.
Maelezo yake yanafanana na yaliyotolewa na majeruhi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Abdallah Alila ambaye alisema kuwa alimwona mtu aliyelipua bomu “akiingia kwenye gari la polisi”.

“Baada ya mlipuko, sikujua kama nimeshapigwa risasi, lakini niliona watu wakimkimbiza mtu baada ya mama mmoja kusema kuwa ndiye aliyerusha bomu.
Watu waliokuwa wakimkimbiza mtu huyo aliyerusha bomo walikuwa wakipigwa risasi na polisi ili wasimkamate. Baadaye nilimwona mtu huyo akipanda gari la polisi. Nashangaa tena kusikia polisi wakimtafuta huyo mtu,” alisema kijana huyo.

Polisi wodini

Mbali na taarifa kwamba polisi walikuwa wakizunguka katika wodi za wagonjwa wakiwa wamevalia majoho ya madaktari, pia mgonjwa mwingine amedai kwamba askari wamekuwa wakimfuatilia kila kukicha.

Peter Mshanga ambaye amelazwa katika Hospitali ya Selian hivi sasa kutokana na kujeruhiwa kwa risasi katika mguu wake wa kushoto alisema awali alipelekwa katika hospitali ya St. Elizabeth lakini alihama baada ya kuandamwa na askari kanzu.

“Mara baada ya bomu nilipelekwa Hospitali ya St. Elizabeth na huko nilishangaa kuwaona askari ninaowafahamu wakizingira kitanda changu. Hata nilipokwenda chooni askari mmoja alinifuata, nikamuuliza anataka nini, yeye akanijibu eti anataka kunisaidia, nikamkatalia akatoka nje,” alisema Mshanga na kuongeza:
“Waliendelea kuzingira kitanda changu kwa siku kadhaa, siku ya tatu daktari akasema nitakiwa nihamishiwa hospitali ya Mount Meru, nikapinga”.

Wakati huo walikuwa tayari wameandaa ambulance (gari la wagonjwa) na gari la polisi ili wanihamishe. Ndugu zangu walipinga ndipo nikahamishiwa hapa Seliani,”anasema.

Kuhusu kujeruhiwa kwake, Mshanga alisema baada ya mlipuko alishtukia ameshajeruhiwa mguuni na akaanguka chini.

“Nilikuwa nimeshika Sh500 mkononi nikisubiri kutoa sadaka yangu. Mara nikaona watoto wanaanguka mbele yangu, nikasikia kishindo kikubwa, kisha nikakimbia kubeba mmoja wa watoto, na mimi nikaanguka, kumbe nilikuwa nimejeruhiwa,” alisema.

Jana muandishi wetu wa siri wa free Zanzibar people from mkoloni mweusi alimtafuta Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas kuzungumzia suala la polisi kuwafuatilia majeruhi lakini alipopokea simu alisema hawezi kuzungumza kwa wakati huo kwa kuwa yuko kwenye kikao. “Niko kwenye kikao,” alisema Sabas na kukata simu yake.
 
POLISI ASEMA HAKUPINGWA MTU RISASI
Wakati Serikali kupitia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu sera na Uratibu wa Bunge, William Lukuvi ikitoa kauli kuwa polisi walijihami kwa kuwapiga wananchi risasi na mabomu ya machozi, mmoja wa maofisa polisi aliyekuwa uwanjani wakati wa mlipuko ambaye pia hakutaka jina lake litajwe amekanusha kupiga watu risasi. “Mimi ndiyo nilikuwa pale uwanjani, baada ya bomu kulipuka wafuasi wa Chadema walianza kutushambulia tulipojitokeza kubeba majeruhi hadi wakavunja kioo cha gari yetu. Niliwaamuru askari warushe risasi hewani, hakuna hata mtu mmoja aliyepigwa risasi,” alisema na kuongeza 
“Unajua wafuasi wa Chadema wamelishwa chuki na viongozi wao, kama Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema ambaye alisema akivamiwa na majambazi heri afe kuliko kumpigia simu RPC. Ndiyo maana watu walijawa chuki wakaja kutushambulia.”

Aliendelea: “Baada ya kuona mashambulizi yamezidi tukaondoka, lakini baadaye tukarudi na kukuta majeruhi wote wameshaondolewa na wafuasi wa Chadema. Baadhi ya askari kanzu waliwafuatilia majeruhi ili kujua majina na idadi yao ili tutoe taarifa”.

Kama ni risasi basi wamepigwa na viongozi wa Chadema kwani maganda mengi ya risasi yameonekana kuwa ya bastola na viongozi wao wengi wanazo,”alisema.

Friday, June 21, 2013

PINDA ASEMA SASA PIGA TU-AVUNJA KATIBA BILA YEYE MWENYEWE KUJUWA

 Katika swali la nyongeza, Mangungu alisema kutokana na hali iliyokuwapo, sasa wananchi wengi wamekuwa na hofu, lakini pia hata shughuli za uzalishaji mali zimeingia kwenye shaka na kuumiza uchumi wa nchi.
 “Serikali ipo tayari kiasi gani kuweza kubainisha na kuchukua hatua stahiki badala ya kusakama makundi fulani. Tujue chanzo halisi cha vurugu hizi na matatizo haya na jinsi gani, ambavyo vyombo vya dola vinashughulikia..??” alihoji na kuongeza:
“Maana yapo malalamiko katika baadhi ya maeneo kama Mtwara, wananchi wanapigwa na vyombo vya dola. Sasa serikali ipo tayari kutoa kauli ni kiasi gani wamefanya uchunguzi na kupata suluhisho la kudumu la matatizo hayo..??”
Akijibu swali hilo, Pinda alionekana kukerwa na swali la nyongeza, hasa pale mbunge huyo aliposema kuwa wakazi wa Mtwara wanapigwa na vyombo vya dola.
“Hapa unaona anasema (Mangungu) vyombo vya dola vinapiga watu. Ukifanya fujo wakati umeambiwa usifanye hiki, ukaamua wewe kukaidi utapigwa tu, maana hakuna namna nyingine lazima wote tukubaliane kuwa nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria,” alisema na kuongeza:
“Kama wewe umekaidi hutaki, unaona kwamba ni imara zaidi,  wewe ndiyo jeuri zaidi watakupiga tu na mimi nasema muwapige tu alisema pinda. Kwa sababu hakuna namna nyingine. Maana tumechoka sasa.”
Akiendelea kusema juzi alimsikiliza mbunge mmoja, ambaye anadhani anatoka Mtwara, naye alijaribu kugusia gusia kwamba, vyombo vya dola vinakamata watu vinapiga watu.
“Mara ya mwisho nilisema tunataka turejeshe hali ya amani katika maeneo hayo ya Mtwara…tukawaambia Watanganyika tunawaombeni radhi sana katika jambo hili tutakapoanza kufuatilia mtu mmoja mmoja. Tunajua kuna watu watajitokeza kuanza kuvisema vyombo vya dola.
“Nikawaomba msamaha. Tuacheni tufanye hiyo kazi Mtwara. Pale tuna orodha sasa ya watu, ambao wanasemekana ndio vyanzo vya matatizo na vurumai mnataka tusiwakamate..??? Lazima tuwakamate na katika kuwakamata wakifanya jeuri jeuri watapigwa tuuuu kabla ya kuwapeleka wanapotakiwa kupelekwa.”
Alisema hawawezi kuendelea na hali hiyo na wakadhani kwamba, watafika wanakokwenda.
Alisema ni lazima serikali ijitahidi na kwamba, vyombo vya dola vijipange imara ili kuhakikisha wanadhibiti hali  hiyo na kuirejesha hali ya utulivu maana hakuna namna nyingine.
Mbunge wa Konde (CUF), Khatib Said Haji, alihoji kauli ya awali aliyoitoa Pinda kuwa watu wapigwe tu.
“Katiba ya Jamuhuri ya Muungano katika Ibara ya 13 kifungu kidogo cha pili inasema ni marufuku kwa mtu yeyote aliyeshtakiwa kwa kosa la jinai kutendewa kama mtu mwenye kosa hilo hadi hapo atakapothibitika kutenda kosa hilo,” alinukuu.
Alisema pia Katiba hiyo Ibara 12 inasema ni marufuku kwa mtu yeyote kuteswa ama kuadhibiwa kinyama na kumpa adhabu, ambazo zinamtesa mtu na kumdhalilisha.
“Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kauli yako nzito hiyo uliyoitoa huoni kwamba, umevunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanganyika ((Tanzania))..????” alihoji Haji.
Akijibu, Pinda alimtaka kuweka tofauti ya mtu aliyekamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria na kwamba, hapo ndipo Katiba inamwelekeza kuwa asifanye jambo lolote katika eneo hilo.
“Mimi nazungumza ni pale mtu ameamua kufanya vitendo hajakamatwa. Ndiyo maana nilisema nikikwambia usiandamane, hapa hutakiwi kwenda. Wewe ukaamua kutumia mabavu kwa sababu mpo wengi ukaenda,” alisema na kuongeza:
“Ndiyo maana nikasema hawa watu tutashughulika nao hivyo hivyo. Sizungumzi mtu ameshakwenda mahakamani na kukamatwa hata kidogo. Mtanganyika awe mwepesi wa kutii sheria bila shuruti.”

VIDEO-KAMATI YA MARIDHIANO SIX;MKUTANO WA MAMLAKA KAMILI DAY';01/06/2013 KIBANDA MAITI A.K.A.KIBANDA HAI.

FUATILIA MKUTANO MZIMA
ZANZIBAR KWANZA SHENGESHA BAADAYE

VIDEO-SHEIKH ATOWA SIRI ZA WAFANYAVYO WAGANGA PART 1

DUNGU MUISLAMU ANGALIA VIDEO HII UELIMIKE NA WAJULISHE NA WENZIO PIA ILI WAPATE KUELIMIKA

VIDEO-SHEIKH ATOWA SIRI ZA WAFANYAVYO WAGANGA PART 2

DUNGU MUISLAMU ANGALIA VIDEO HII UELIMIKE NA WAJULISHE NA WENZIO PIA ILI WAPATE KUELIMIKA

Thursday, June 20, 2013

VIDEO-NAFASI YA WAISLAM NA KATIBA MPYA YA TANGANYIKA ((TANZANIA)) ZANZIBAR - USTADH ILUNGA

HUYU NI MOJA KATIKA MASHEIKH AMBAO CD,DVD ZAKE ZIMEKATAZWA ZISIONYESHWE WALA ZISIUZWA HAPA NCHINI ZANZIBAR JE MZANZIBARI ULIO NDANI YA NCHI NA MULIO NJE YA NCHI MSIKILIZE KISHA JIULIZE NI KWA NINI SEREKALI YA ZANZIBAR IMEPIGA MARAFUKU CD NA DVD ZA SHEIKH HUYU NA WENGINE..??

VIDEO-KAMATI YA MARIDHIANO SIX: MKUTANO WA CCM ULIOFANYIKA WA FITNA KUBWA NA MATUSI KIBAO

HUYU NI WAKUWA MSTARI WA MBELE KUITETEA NCHI YA ZANZIBAR NA KUONDOWA UMASIKI KAMA ALIVYOTAKA KUWONDOWA MZEE KARUME KWA KUJENGA MAJUMBA YA MICHEZANI,VIWANDA,NYUMBA ZA VIJIJI NA KATHALIKA LAKINI WAPI MZEE KAMA HUYU ANAKA JUU NA MATUSI NA KUCHAMBUWA WANAUME WENZAKE KAMA...... DAAAAAH KWELI NCHI YA ZANZIBAR ITAENDELEA IKIWA HAWA NDIO WAITWA VIONGOZI WANAO ONGOZA WATU..? NATUMAI MZEE UTAJIANGALI MWENYEWE HAPA UNAVYO SEMA NA KUAKTI KISHA JIULIZE JE KWA UMRI ULIO NAO WEWE NI WAKUFANYA HAYA..? JE VIJANA WAKIZANZIBARI WAKUCHUKULIA WEWE NI KAMA NANI KATIKA MATUSI HAYA NA AKTI HIZI..?

VIDEO-KAMATI YA MARIDHIANO SIX: MKUTANO WA CCM ULIOFANYIKA KWA FITNA KUBWA NA MATUSI

WAZANZIBARI TUNATAKA UMOJA,MSHIKAMANO,UPENDO,MASIKILIZANO,KUKUBALIANA HATA KAMA TUNATAFAUTI ZETU NI ZETU HAPA HAPA NCHINI KWETU SIO MATUSI NA KUTUGAWA ILI MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA APATE NGUVU ZAIDI YA KUTUTAWALA NA VIBARAKA WAKE HAPA NCHINI KWETU.


VIDEO-KAMATI YA MARIDHIANO SIX: MKUTANO WA CCM ULIOFANYIKA KWA FITNA KUBWA NA MATUSI

SIKILIZA ANAVYOSEMA HUYU JAMAA KISHA JIULIZE MTU KAMA HUYU AKIPEWA UWONGOZI KWELI MAENDELEO ATAYALETA VIPI KATIKA NCHI SIASA HIZI ZITAKWISHA LINI HAPA NCHINI KWETU ZANZIBAR..?? KWELI WEZENJI HIZI NDIO

SIASA TUNAZO ZITAKA KATIKA MIAKA HII 2013


VIDEO-WAKURIA NA VIBARAKA WAKITANGANYIKA WANAO JITA POLISI-NDIO WAUWAJI NA WIZI WAKUBWA WANAOTAKA KUIGAMIZA NCHI YETU YA ZANZIBAR

HAWA KWELI UTAITA POLISI HAWA..??

NCHI YA ZANZIBAR ILIKUWA WAPI NA LEO HII IKO WAPI MASIKINI ZANZIBAR YETU


AMRIT WILSON, US Foreign Policy and Revolution; The Creation of Tanzania,
Introduction by A. M. Babu, London, Pluto Press, 1989. ISBN 1-85305-051-2.

The capital of the Indian Ocean Island of Zanzibar had street lighting powered by electricity when London had to make do with gas lamps.This was benefit of East African's first electric power station,built in Zanzibar by the United States and one of Amrit Wilson"s instances of long standing US interest in Zanzibar.She alson remarks on visits by American merchant ships of the spice and Ivory trade to the shores of Zanzibar and frequent calls by Zanzibar dhows to the port of Boston.by the mid-nineteenth century British influence in the Island sultanate was dominant, and US influence waned.

      Ms Wilson" study focus on the Zanzibar revolution in January 1964 against the Sultan"s regime in the wake of an independence accorded by Britain in December 1963. Her particular concern is with the US role in the events including the Union of  Zanzibar with Mainland Tanganyika in present-day Tanzania. Her argument is that the US state Department played a decisive part in determining the outcome of events, even more so than the comparable British authorities. The new source material on which she relies is State Department letters and telegrams deposited in the official paper at the President Lyondon B. Johnson Library in Austin, Texas,
      Wilson"s reading of the historic changes differs substantially from previously published  accounts, A detailed narrative wa given by a British military historian.
Anthony Clayton (The Zanzibar Revolution and its Aftermath, London,C, Hurst,1981). Clayton rather dismisses the US rsponse as a panicky evacuation of families of the staff at a US satellite-tracking station and possibly premature closing of that station,Clayton give credence to a role in the revolution by the self-styled; Field Marshal'' John Okello; this bizarre personality is only contingently featured in the wilson book.
                              The major personality here is Abdul Rahman Mohammed Babu, chairman of the Umma Party of Zanzibar, Foreign Minister of the People'' Republic of Zanzibar, later a Minister in the United Republic , a political prisoner and exile. Babu contributes an introduction saying that the book confirms suspision held in the 1954-64 and of the US orchestration of the overthrow of the Zanzibar revolution of 1964 and of the deliberate cretion of the Union of Tanganyika and Zanzibar in a pro-West Tanzania; He provides too the first appendix on the background to the revolution which is a succeinet discussion of class force in the various political groupings of the run-up to independence, and a gentle  advertisement for the relevance of his own Umma Party. It was Babu''s identification with socialism and with Chinese communism in particular that the State Department feared.
      Wilson  does reveal new detail on US  manipulation of the Zanzibar situation. But in an economy based  on cloves and serving a population of around a third of a million the wonder is not so much that the US more or less succeeded, but that they bothered at all. After the violent overthrow of the Sultan''s regime, the US,  according to a diplomatic cable, viewed the situation as one where (1) Okello supported by forty Cuban trained armed gunmen... still wields undiminished power and (2) Abeid Karume and nationalist faction steadily losing power to pro-Communist Babu-Hanga clique''
         Over time,  Okello went abroad and was barred from returning to Zanzibar, Karume tyranny was a high price the US wished on the Zanzibari people against Babu who, in the CIA assessment,  is describe as the most energetic, able and ambitious member of the Zanzibari political group; What comes through the whole book is the degree to which US policy makers were ready to make arbitrary decisions about political events, situation and personalities, in areas where it is more generally assumed  that the British Foreign Office is the critical external factor , and on matters where US knowledge is at best superficial and often over reactive. It leads to Kissinger-style diplomacy where by Ian Smith is told when his time is up in Rhodesia, and the prospect of the Angolan people are subordinated in US thinking to rivalries with the USSR. This case study on Zanzibar is on a slender scale and its documentary sources supplemented by too narrow a range of informants, but it helps illustrate what theoretical United States means i practice.


                                                                                             MICHAEL WOLFERS

JUSSA AMULIZA YUSSUF MZEE KUHUSU WIZI WA MCHANA KWEUPE WANAO TUFANYIA NCHI YA TANGANYIKA MZEE AJIFICHA HATAKI KUJIBU


Very interesting leo Mhe. Omar Yussuf Mzee alipokuwa akifanya majumuisho ya mjadala wa bajeti ya SMZ (wind-up of the budget speech) aliamua kuzinyamazia kimya na hakujibu kabisa hoja nilizozitoa jana kuhusu wizi wa mchana kweupe wanaotufanyia Tanganyika katika mafungu ya fedha za misaada ya kibajeti (GBS), fedha za mifuko ya miradi kisekta na fedha za miradi ya maendeleo zinazotoka kwa washirika wa maendeleo zinazoombwa na kutolewa kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ambazo ukifanya hesabu ya Zanzibar kupewa ule mgao wa 4.5% tu basi zinafikia TShs. 163 bn.
Ukiacha hizo kuna na zile za mikopo ya elimu ya juu ambazo kama Zanzibar ikipewa 4.5% tu kutoka SMT basi ni TShs. 14.6 bn. wakati mahitaji ya Zanzibar kuwapatia mikopo wanafunzi wote wanaoomba ni TShs. 5 bn.
Mbali ya hizo nilihoji gawio la Zanzibar kutoka taasisi za Muungano kama TCRA, TCAA, TTCL, TPC na TPDC ambazo zinakusanya mapato na nyingine Zanzibar ina hisa kabisa lakini hakuna tunachokipata. Chukulia mfano mdogo tu karibuni Vodacom peke yake ililipa TCRA kodi ya TShs. 36 bn. Je, ukichanganya na Zantel, Tigo na Airtel mbali na tozo na ada nyinginezo.
Ukiacha hizo hata kodi ya mapato (PAYE) inayotokana na wafanyakazi wa Taasisi za Muungano waliopo Zanzibar na ambao wanatumia huduma zote za hapa zinazolipiwa na walipa kodi wa Zanzibar nazo hazilipwi sawa sawa.
Halafu anatokezea mtu anasema Zanzibar inanufaika na mfumo uliopo wa Muungano na kwamba eti tunabebwa. Nani anambeba nani hapa? Nini faida ya Muungano wa aina hii?
Ndiyo maana tunasema hatupokei chochote pungufu ya MAMLAKA KAMILI ya Zanzibar kitaifa na kimataifa. Na tutahakikisha katika rasimu ya Katiba tunayarejesha kwenye mamlaka ya Zanzibar mambo yafuatayo ili tuweze kusarifu na kupanga uchumi wetu kwa maslahi ya nchi yetu na watu wetu. Mambo hayo ni:
1. Mambo ya Nje;
2. Sarafu na Benki Kuu; na
3. Uraia na Uhamiaji

FREE ZANZIBAR PEOPLE FROM MKOLONI MWEUSI TUNAMULIZA DAFTARI BAADA YA KUMALIZA KUPALILIA MATUTA YA MIKARAFU HUKUTAKA KURUDI KWENU TANGANYIKA UMEJIFICHA KWENYE KICHAKA CHA CCM LAKINI SASA UMEJICHIBUWA MAANA UNAONA ULWA UNAKUTOKA UKAE UKIJUWA FITINA ZOKO ZITAKURUDIENI WENYEWE HUKO HUKO TANGANYIKA MUSHANZA KUPIGANA MABOMU KAMA UNATAKA KUISHI ZANZIBAR KUWA NA ADABU DAFTARI HEBU SOMA HAPA KISHA UJIULIZE KATI YA TANGANYIKA NA ZANZIBAR YUPI MWENYE PESA ZA KUENDESHA NCHI..? ZANZIBAR HAENDELEI KWA SABABU YENU NYINYI KINA MADAFTARI NA WENGINE PESA MNAIBA MUKITUTIA UFUKARA NAKUAMBIA TENA KAMA UMEIBA USHAIBA NA KAMA HUJAIBA HUTAIBA TENA TUBIA KWA MOLA WAKO KABLA HUJAFA MAMA USHAZEKA BADO TU UNATAKA DUNIA.

Wednesday, June 19, 2013

MABOMU YARIDIBA ARUSHA NZIMA YANAYO RUSHWA NA POLISI-WATANGANYIKA MLISEMA MUUNGANO UKIVUNJIKA PEMBA NA UNGUJA WATABAGUWANA WATANGANYIKA MBONA NYINYI MUNAUWANA NA MUUNGANO HAUJAVUNJIKA..??


MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR HATA HAUJAVUNJIKA MUSHAA ANZAA KUTWANGANA NA MABOMU JE UKIVUNJIKA SIMTAMALIZANA NYINYI KWA UROHO WA MADARAKA.
Arusha. Wabunge wanne wa Chadema, Said Arfi (Mpanda Mjini), Tundu Lissu (Singida Mashariki), Mustapha Akunaay (Mbulu) na Joyce Mukya (Viti Maalumu) wamekamatwa wakituhumiwa kuhusika na mkusanyiko usio halali kwenye Uwanja wa Soweto jana.nacheka kwanza hahaha hibu niwakumbushe kidogo kuwa kuna masheikh kule nchini Zanzibar wamekamatwa bila ya hatia yoyote na wanasota jela.haya sasa WAKOLONI WEUSI TANGANYIKA sasa munaanza kukamatana wenyewe kwa wenyewe.

Mkuu wa Operesheni wa Polisi, Kamishna Paul Chagonja alisema jana kwamba pamoja na wabunge hao pia wamewakamata watu wapatao 60 kutokana na vurugu zilizozuka jana baada ya Polisi kuwatawanya kwenye uwanja huo waliokuwa wamekusanyika kuomboleza vifo vya watu watatu;napenda kuwakumbusha tena meli ilizama nchini Zanzibar na Wazanzibari wakamuwa kukusanyika na kuwaombeya duwa walo zama WAKOLONI WEUSI TANGANYIKA mkatowa mri kwa kuwatuma watumwa wenu vibaraka wenu Zanzibar polisi wakapiga watu ndani ya msikiti haya sasa munapigana katika kuomboleza mazishi wenyewe kwa wenyewe Watanganyika. Judith Moshi, Ramadhan Juma na Amir Ally waliofariki kwenye mlipuko wa bomu uliotokea kwenye uwanja huohuo, Jumamosi iliyopita.

Mbali ya viongozi hao, alisema wanawasaka Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

“Tunawasaka wabunge ili tuwajumuishe na watu hawa kwa kosa la kuhusika na mkusanyiko usiokuwa halali. Hadi sasa tumefanikiwa kulinasa gari la Mbowe,” alisema Chagonja.
Pia kamatakamata hiyo imemkumba Mpigapicha wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Ashraf Bakari. Polisi walilazimika kutumia nguvu kuwatawanya waombolezaji hao.

Awali, Kamishna Chagonja alisema jana asubuhi kuwa wamelazimika kuzuia viwanja hivyo kutumika baada ya wamiliki wake, AICC kuzuia shughuli za Chadema kwenye eneo lao.

Kamishna Chagonja aliwaonyesha waandishi wa habari barua aliyosema imeandikwa na uongozi wa AICC kuzua Chadema kuendelea kuutumia Uwanja wa Soweto.

Mabomu yarindima

Dalili za kuzuka kwa vurugu zilianza kuonekana asubuhi baada ya polisi kuzingira uwanja huo na kuzuia watu waliokuwa wameanza kufurika katika eneo hilo kuanzia saa moja kuingia kwa ajili ya maombolezo.

Wakati Polisi wakiwa uwanjani, wananchi walijaa nje ya uwanja na kuonekana kama wamewazingira.

Viongozi wa Chadema wakiongozwa na Mbowe waliwasili uwanja hapo yapata saa nane mchana na kukuta zuio hilo na kuanza kuzungumza na wananchi ingawa FFU walikuwa wakiwataka watu kutawanyika. Mabomu yalianza kurindima wakati Arfi aliposimama na kuwahimiza wananchi kuelekea Hospitali ya Mount Meru kwa ajili ya kuaga miili ya marehemu.“Tuna muda mfupi sana wa kuzungumza hapa, tunaomba wote tuelekee Hospitali ya Mount Meru kuaga miili ya marehemu kwa sababu uwanja huu umezuiwa na polisi,” alisema Arfi kabla ya kukatishwa na milipuko ya mabomu.
Awali, Lissu ambaye pia ni Mwanasheria wa Chadema alitoa msimamo wa chama hicho kuwa Mwenyekiti wao, Mbowe na Lema hawatatoa ushahidi wa tukio la bomu wala kujisalimisha polisi kwa sababu hawana imani na jeshi hilo.

“Namtaka Chagonja atangulie mahakamani, tutakutana hukohuko. Mbowe na Lema hawatatoa ushahidi wala kujisalimisha polisi...” alisema Lissu na kuongeza:

“Kisheria haiwezekani polisi ambao ndiyo watuhumiwa ndiyo wadai kukabidhiwa ushahidi ili wauharibu.”

Mapema Kamishna Chagonja aliwataka Mbowe na Lema kutoa ushahidi wa polisi kuhusika na tukio la kurusha bomu kwenye mkutano wa Chadema la sivyo polisi watatumia sheria kuwalazimisha kufanya hivyo.

Hekaheka

Baada ya polisi kuanza kutupa mabomu saa 8.45 mchana, wabunge, viongozi waandamizi wa Chadema na watu waliokuwa wamekusanyika walilazimika kutimua mbio.
Watu walioshuhudia tukio lile wanasema viongozi hao akiwamo Mbowe na mwenzake Lissu walikimbilia kwenye magari yao. Lema alilazimika kukimbilia kwa wachoma nyama ya nguruwe, (kitimoto) kwenye maeneo ya Kaloleni.

Kabla ya polisi kurusha bomu mahali alipokuwapo Lema, mbunge huyo alisikika akisema:

“Jaribuni kuvumilia, tunajaribu kuwasiliana Serikali ya Mkoa, ili watupe kibali cha kuleta miili ya wapendwa wetu hapa, kuweni wastaarabu kwa sababu mbele yetu kuna wana usalama ambao wanalinda amani, ingawa kufa ni kufa tu, wenzetu wameshakufa na sisi ipo siku tutakufa, lakini kila anayetangulia lazima tumzike kwa heshima zote.”

Kauli hiyo iliwachefua polisi ambao walishatangaza amri ya watu kutawanyika katika viwanja hivyo na kwamba hakutakuwa na suala la kuaga miili ya watu hao katika eneo hilo. Ghasia hizo zilisababisha kusimama kwa shughuli za biashara na kijamii kwa muda jijini Arusha huku watu waliokuwa katika nyumba zilizokuwa karibu na maeneo yalikorushwa mabomu wakilazimika kutoka nje kupata hewa safi baada ya nyumba hizo kujaa hewa ya mabomu.

Polisi waliokuwa wakirusha mabomu waliwakimbiza wananchi hadi maeneo ya Sakina huku wakiendelea kufyatua mabomu kila walipoona mkusanyiko wa watu.mwambiyeni raisi wenu awachiye masheikh wote waliofungwa bila ya hatia yoyote au kwa guvu za mola mutapigana wenyewe kwa wenyewe mpaka mukome.

Tuesday, June 18, 2013

NCHINI TANGANYIKA-MTOTO ASEMA NIMEPINGWA RISASI NA POLISI-ARUSHA-CCM OYEEEEEEE


Arusha/Dodoma. Wakati watu waliofariki kwenye tukio la kurushwa bomu katika mkutano wa Chadema ukizidi kuongezeka baada ya jana kufariki kwa mtoto Amir Ally (7), mtoto mwingine wa miaka kumi na moja aliyejeruhiwa vibay, amesema kwamba alipigwa risasi na polisi kwenye tukio hilo.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe naye ametoa tamko kuwa chama chake kina ushahidi wa kutosha wa watu waliohusika na tukio la kurushwa bomu katika mkutano wa kampeni wa chama hicho.

Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Arusha Medical Lutheran Center (ALMC), Dk Paul Kisanga alisema jana kuwa, Amir alifariki jana asubuhi baada ya kupata majeraha makubwa kichwani yaliyodhuru ubongo wake.

Dk Kisanga alisema huyo ni mmoja wa watoto watano, waliojeruhiwa wakati wakitoka madrasa huko Kaloleni, jirani na Uwanja wa Soweto kulipokuwa na mkutano na alifariki jana asubuhi hospitalini hapo.

Alisema watoto wengine wawili ambao ni ndugu; Fatuma na Sharifa Jumanne wamepelekwa Nairobi kwa matibabu zaidi baada ya miili yao kukutwa na vyuma. Dk Kisanga aliwataja watoto wengine waliojeruhiwa kuwa ni Fahad Jamal (7) ambaye yupo ICU akisubiri timu ya madaktari kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na hali yake kutoruhusu kusafirishwa. Pia yupo Abubakar Adam (11) ambaye amejeruhiwa mguuni na amelazwa katika Hospitali ya Mkoa, Mount Meru.
 

Mtoto aeleza kupigwa risasi

Adam alisema jana kuwa alipigwa risasi na mtu aliyekuwa amevalia sare za polisi, wakati akitoka madrasa akiwa na ndugu yake, Fahdi katika eneo la Soweto.

Alisema akiwa njiani, aliona watu wakimkimbiza mtu na ghafla alishangaa kupigwa risasi na kuanguka chini.

“Namkumbuka aliyenipiga risasi alikuwa amevaa sare za polisi,” alisema Adam mwanafunzi katika Shule ya Msingi Levolosi huku akitokwa machozi.

Muuguzi wa zamu, katika katika wodi ya watoto katika Hospitali ya Mount Meru, Asha Semdeli alisema jana kuwa mtoto huyo ana vyuma viwili katika mguu wake.

“Tunasubiri afanyiwe upasuaji kwani tayari mashine ya X-ray inaonyesha vyuma kuwepo katika mguu wa Adam siwezi kusema ni risasi au la,” alisema Semdeli.