Sunday, September 15, 2013

SHEIN ASEMA KITENDO CHAKUMWANGIWA TINDI KALI PADRI NI KITENDO CHA KIKATILI JE SHEIN CHA WEWE KUWAFUNGA JELA MASHEIKH WA UAMSHO JE...???


Nchini Tanganyika jijini Dar. Siku moja baada ya Padri wa Kanisa Katoliki Parokia, Mkoa wa Kusini Unguja nchini Zanzibar, Joseph Mwang’amba kumwagiwa tindikali na watu wasiojulikana,ameamuwa kurudi kwao nchini Tanganyika pia inasemakana kuwa atii alitishiwa kuuwawa miezi mitatu kabla ya kukutwa na tukio hilo chaa jabu mbona hakuripoti polisi na kusema kuwa kuna watu wamemtishia kuumuwa kwa mara nyengine tena tunaona kuwa ni mbinu za MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA Kutaka kuwatia ubaya Wazanzibari na kufitinisha ili kuuanzisha vita vya kidini.

Wakati Padri huyo akieleza hayo, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Ali Mohamed Shein, ameijia juu polisi kwa kushindwa kudhibiti matukio ya viongozi wa dini na serikali nchini humo Zanzibar, kushambuliwa kwa kumwagiwa tindikali huku akilitaka kuwakamata waliohusika na tukio hilo swali Shein hutaki akamatwe alimpiga mapanga Sheikh wa KITOPE mpaka kufa ila aliyemrushia padri ndio wakamatwe uko wapi uwadilifu wako....???

Kiongozi huyo wa dini, aliyejeruhiwa maeneo ya usoni, mikononi na kifuani baada ya kumwagiwa tindikali alisafirishwa jana na ndege ya kukodi ya Shirika la Coastal kutoka nchini Zanzibar hadi nchini Tanganyika jijini Dar es Salaam kwao alikotokea na baadaye kupelekwa Hospitali ya Taifa ya nchi yao ya Tanganyika Muhimbili (MNH) kwa matibabu zaidi.

Shein alisema Polisi inatakiwa kuongeza nguvu za uchunguzi ili kukabiliana na matukio ya kikatili ya umwagaji wa tindikali, yanayoshamiri nchini humo Zanzibar hivi sasa.
“Hatuwezi kuviacha vitendo hivi viendelee … ni lazima Jeshi la Polisi lijitahidi kuwatafuta wahusika ili sheria ichukue mkondo wake,” alisema Shein.

Sheni alisema, kitendo hicho ni cha kikatili na kisichovumilika na kuongeza kuwa wahusika lazima wasakwe na kuchukuliwa hatua za kisheria tunamuliza shein kitendo cha kuwafunga Masheikh wa Uamsho bila kosa ni kitendo cha burudani...??? au pia ni kitendo cha kikatili na chakishenzi na wewe ndio umewafunga basi wewe shein katili mkubwa kuliko wa tindi kali.

Kwa upande wake, Padri, Thomas Assenga aliyefuatana na kiongozi huyo mpaka MNH, alisema siku za nyuma Padri Mwang’amba alitolewa vitisho na mtu ambaye hamfahamu wakati akienda kutoa huduma katika kituo cha wazee cha Welezo.

Alisema kabla ya kufika kituoni hapo, kuna eneo ambalo nyakati za asubuhi watu hufanya mazoezi barabarani ambapo kuna mtu mmoja alimtolea maneno ya vitisho.

“Unajua kawaida ya watu wa Zanzibar hufanya mazoezi barabarani, sasa kipindi anapita eneo hilo katika kilima, kuna mtu alimwambia atamfanyia kitu kibaya ambacho hatujui ndiyo hiki au laa,” alisema Padri Assenga na kuongeza:

Alisema Juni mwaka huu mara baada ya kupewa vitisho hivyo alikwenda kutoa taarifa kwa Sheha wa eneo hilo na. “Mara baada ya kutolewa vitisho hivyo Juni mwaka huu, alichukua jukumu la kwenda kutoa taarifa kwa mkuu wa eneo hilo (Sheha)

Akielezea tukio la kumwagiwa tindikali Padri Mwang’amba, alisema alimwagiwa saa 9:45 alasiri juzi wakati akizungumza na simu nje ya internet café iliyopo eneo la Mlandege
Padri Assenga alisema kabla ya kumwagiwa tindikali, Padri huyo alikuwa ndani ya internet akitoa ‘photocopy’ za nyaraka. Alipokuwa akitoa ‘photocopy’ (nakala) alipigiwa simu na mtu ambaye anamfahamu hivyo ikabidi atoke nje kuongea naye, lakini alivyokuwa akiongea alimwona kijana akija na kikopo alichokishika mkononi na kummwagia na kukimbia kuelekea katika mitaa ya eneo hilo,” alisema Padri Aseenga.

Alisema mara baada ya hapo, alipelekwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, kwa matibabu baada ya kujeruhiwa usoni, kifuani na mikononi ambapo hivi sasa afya yake inaendelea vizuri.

Naye , Msemaji wa Jeshi la Polisi, nchini Zanzibar Mohamed Muhina alisema, hana taarifa hizo za vitisho na kuahidi kulifanyia kazi. “Tukio limetokea mchana kweupe na watu walikuwapo lakini wananchi wamekuwa hawatupi ushirikiano hivyo tunawaomba kutupa ushirikiano ili kukomesha vitendo hivi,” alisema Muhina.

Tukio lilivyokuwa

Akifafanua zaidi kuhusu tukio hilo, Padri Mwang’amba alisema kwamba lilitokea nje ya duka linalotoa huduma za mawasiliano ya mtandao (Sun Shine Internet Caffee) liliopo eneo la Mlandege Wilaya ya Mjini Unguja nchini Zanzibar, ndipo alipotokea kijana mmoja na kumwagia tindikali.

Padri Mwang’amba akimweleza Dk Shein kuwa hali yake ni nzuri na anaweza kuona vizuri, lakini anatarajia kupata nafuu zaidi baada ya uvimbe kupungua katika sehemu za usoni na machoni mwake.

“Hali yangu ni nzuri lakini natarajia uvimbe ukipungua nitaona vizuri zaidi,” alisema Padri Mwang’amba na kuongeza kuwa ilikuwa ni bahati kwake kwa kutoathirika sana.

Uwanja wa Ndege

Katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Kiongozi huyo aliwasili saa 4.16 asubuhi na ndege ya Shirika la Costal akiongozana na Padri Assenge.

Kiongozi huyo aliyekuwa akitembea taratibu, huku akijitahidi kujifunika mwili wake na kanga kuzuia mwanga wa Jua kutokuathiri zaidi mwili wake ulioathiriwa na tindikali.

No comments:

Post a Comment