Tuesday, January 28, 2014

ZANZIBAR SIO NCHI WALA HAINA RAISI-NDUGU ZETU MULIO NJE KUTOWA NI MOYO SIO UTAJIRI TUMSAIDIYE NDUGU YETU MANSOOR.

IMG_5343
FREE ZANZIBAR PEOPLE FROM MKOLONI MWEUSI
Tunasikitika sana na serekali yetu ya Wauwaji wa Wazanzibari kuwa haina hata habari jinsi inavyo uwa rai wake na hata kuwajali haiwajali. Serekali hii ni domo kaya tu mapinduzi daima smz ukwakwasi. Serekali ya kitaifa uvundo mtupu hamuna lolote washenzi wakubwa kazi kujirundikia mali na wake zenu na watoto wenu basi huku watoto wa Kizanzibari na taifa la kesho linazidi kuangamia.  kwa kujivuna tu serakali hii imepindukia mpaka inaleta maendeleo hebu someni hii stori ya huyu kijana mutuonyeshe hayo ndio maendeleo...? kijana anataka millioni ishirini tu makelbu nyie ndani ya baraza la wawakishi mamillioni mangapi mumejirundika millioni ishirini kwa nyinyi ni kama elfu mbili tu lakini wapi nyinyi sio watu wala binadamu nyinyi ni wanyama hatari na nyoka wenye sumu kali sana ndio maana mumekazania mapinduzi daima makelbu nyieee. Mumeharibu mabillioni mangapi kwa sherehe zenu za mapinduzi watu kufanya laana na machafu usiku kucha huku mambo muhimu kama haya utasikia serekali hai pesa kelbu wakubwa nyiee.muko bizi kuhonga na kulisha watu mavyakula na ukiritibwa kwenye jimbo la kiembesamaki pesa munazivuruga huyu kijana na wenzake wengine wengi na rai wengi wanalala na njaa na kuteseka na maradhi nyinyi sio wetu nyinyi astahafiru laaa hata sijuwi niwaite nini midubwana nyiee.
Salma Said, 
Ni mwenye furaha usoni mwake, huwezi kuamini kama ni mgonjwa huwezi kukubali kama ana machungu ndani ya moyo wake kwa kuwa sura yake ni ya kutabasamu wakati wote na kuonesha matumaini ya kuishi kwa amani lakini utagundua tu pale utakapomsikiliza kwa umakini sana katika maelezo yake na ukimtulizia jicho ndipo utakapogundua kama kweli kijana Mansoor Hamad Saleh (21) ana majonzi na maumivu makali anayoyapata katika kiwiliwili chake.
Ni miaka mitatu sasa tokea Mansoor alipoanza kulala kitandani kutokana na matatizo ya kupooza miguu yake yote miwili chanzo chake khasa cha ulemavu huo kilikuwa ni kuanguka juu ya mnazi huko Maangwe Wete Pemba alipokuwa amepanda kwa ajili ya kuangua nazi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kwao.
Mansoor ni mwanafunzi wa kitatu cha pili ambaye alikuwa akijitayarisha na kufanya mitihani lakini kwa bahati mbaya sana kabla ya kuanza tarehe za mitihani alipata mtihani mkubwa wa kuanguka kutoka juu ya mnazi hadi chini na kusababisha matatizo makubwa ya kumlaza kitandao hadi leo hii akiwa hana matumaini tena katika maisha yake.
Hata hivyo Mansoor anajipa moyo kwamba iwapo atatibiwa na atafanikiwa kupata fedha za kumfikisha nchini India ataweza kurejea katika hali yake ya kawaida na amekuwa akiomba apate matibabu hayo ili aweze kurejea shuleni kuendelea na masomo yake kama kawaida.
Awali Mansoor alipoanguka kutoka juu ya mnazi miaka mitatu iliyopita alikimbizwa katika hospitali ya Chake Chake Kisiwani Pemba na alilazwa hapo kwa muda wa mwaka mmoja chini ya uangalizi wa Daktari Shaaban wa hospitali hiyo kabla ya kusafirishwa na kuletwa Unguja katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja kwa amtibabu zaidi lakini licha ya matibabu hayo ya mwaka mzima hakuweza kupata nafuu na bado yupo kitandani.
Kwa kuwa ni kijana mdogo hapendi kulala muda wote na amekuwa akipenda sana kujishughulisha ingawa hawezi lakini anajilazimisha kukaa ingawa kwake yeye ni vigumu kukaa katika kiti muda mrefu lakini amekuwa akijaribu kukaa na kulala mara kwa mara.
“Napenda niendelee kusoma lakini siwezi kwenda skuli na hiki kigari changu kwa sababu kila wakati naumia sana mgongo wangu kwa hivyo inanibidi kila wakati nilale kidogo ninyanyuke nikae kidogo nikale kidogo hivyo hivyo kutwa nzima na nikijilazimisha basi naumia sana” alisema huku akionesha kukunja uso kwa maumivu.
“Sehemu ya kiuno hadi miguu kwenye nyayo iliathirika na kutofanya kazi na Ex Rays zinaonesha kuwa ameumia maeneo ya uti wa mgongo” imesema ripoti yake ya hospitali.
Licha ya matibabu aliyofanyiwa Mansoor alipatiwa madawa mbali mbali ya kuamsha hisia za mwili wake na kuondosha maumivu, kulazwa katika sehemu maalumu ili kunyoosha mgongo wake vile vile kufanyiwa mazoezi mepesi ya kusimamishwa ili viungo vyake viweze kufanya kazi katika kipindi chote cha kuumwa kwake lakini matibabu hayo hayajaweza kuleta mafanikio.
Mansoor baada ya kufanyiwa vipimo vya Computer Tomography Scan (CT SCAN) vinaonesha athari aliyoipata katika mgongo wake anahitajika kusafirishwa na kupelekwa India kwa matibabu kwani ameumia katika uti wake wa mgongo.
Kwa mujibu wa maoni ya madaktari wameshauri Mansoor kupelekwa India kufanyiwa operesheni kwa kuwa operesheni yake haiwezi kufanyika hapa ncini Tanzania na hivyo kila anapoendelea kukaa madhara yanaweza kuongezeka zaidi.
Mansoor anahitaji kusafirishwa kupelekwa nchini India kwa matibabu na kwa mujibu wa madaktari waliomchunguza wanasema ni jumla shilingi millioni 20 zinahitajika kwa makisio ya matibabu yake ya kumfikisha nchini humo.
Makisioa ya fedha hizo ni pamoja na gharama za usafiri kutoka Zanzibar hadi India, vipimo vya uchunguzi, matibabu na gharama za malazi na fedha ya kufuatana na Daktari dhaZ Q1 mana atakayeweza kuondoka naye hapa nchini hadi India.
Matatizo yake makubwa kwa sasa Mansoor ni kuwa hawezi kusimama kwa vile amepata athari katika viungo vyake vya chini (Nyayo) kukosa hisia na pia hawezi kuzuwia choo kutokana na kuathirika kwenye uti wa mgongo.
Wazazi wa Mansoor wamekuwa wakitafuta misaada mbali mbali kutoka kwa watu lakini bado hawajafanikiwa kukusanya kiasi chochote cha fedha licha ya kuandika barua kadhaa kwa wafadhili “Sisi wazee wake Mansoor baba na mama wazazi sote ni masikini sana hatuna uwezo wa kumsafirisha mtoto wetu kwa ajili ya matibabu, mtoto wetu anakabiliwa na ulemavu wa kudumu, tunaleta kilio chetu kwa lengo la kupata msaada wa tiba ya mtoto wetu huyu wa kwanza” imesema moja ya barua yao ya maombi wazee hao ya hivi karibuni ambayo iliandikwa 15/9/2013.
Bi Farashuu Mansoor Mohammed ni mama mzazi wa Mansoor mwenye familia ya watoto wanane kati yao ni wanawake wawili na Mansoor ndio mtoto wake wa kwanza anashukuru kuona mwanawe upo hai bado licha ya hali mbaya na ya kusikitisha kutokana na maumivu ayapatayo mwilini mwake.
“Mwanangu alikuwa akijitayarisha na mitihani ya darasa la kumi na mbili lakini akapata mtihani huu maana na huu ni mtihani mwengine mkubwa zaidi ya huo mtihani wake wa darasani” alisema Mama Mzazi wa Mansoor, Bi Farashuu
Bi Farashuu mwenye watoto saba kati ya hao wanawake ni wawili anasema amefanya juhudi mbali mbali za kutafuta misaa kwa ajili ya kumuokoa mwanawe ili aweze kurejea katika afya yake lakini ameshindwa kutokana na familia yao kuwa masikini sana na haina uwezo wa kuchangishana fedha kwa ajili ya matibabu ya mwanawe huyo.
“Jamaa zangu wanataka kunisaidia lakini jambo kubwa wamenambia wao hata familia nzima ikichangishana haitaweza kupata hata milioni tano na ndio maana nakuwa napata wakati mgumu na wakati mwengine nachanganyikiwa nikimuona mwanangu anavyoteseka na maumivu” alisema huku akiwa na uso wa huzuni sana.
Bi Farashuu anasema mwanawe amekuwa akitaja mara kwa mara kufanya kazi iwapo atakosa matibabu na kushindwa kuendelea na kusoma hivyo angependelea kufanya kazi gereji kutengeneza magari.
Mansoor anapoletewa supu kwa ajili ya kunywa ili kurejesha afya yake amekuwa akisema bora hao kuku anaoletewa kwa ajili ya supu apewe mwenyewe aweze kuwafuga waweze kuendeshea maisha yao yeye na ndugu zake wengine.
“Mwanangu ameshakata tamaa kama baba yake na ndio maana nakhisi kama hatokuwa tena na akili ya kuendelea na masomo na ndio maana anakuwa anataja sana kutaka kufanya kazi gereji kutengeneza magari” alisema Bi Farashuu.
Ameongeza pia kusema “Aanapoletewa supu anywe basi anawaambia nileteeni hao kuku nitafuga mwenyewe kwa sababu akifuga atapata pia kuuza na watazaa wengine na hivyo atapata kuendeleza mifugo na pia atasaidia ndugu zake” alisema ambapo hivi sasa ameshapata makoo wawili kwa ajili ya kuwafuga.
Mansoor anahitaji kupata banda la kuku dogo ili aweze kuwaweka kuku wake ambao wameletewa na jamaa zake baada ya kukataa kupikiwa supu kwa ajili ya kuimarisha afya yake “Nikifuga kuku nitapata kuchinja nipate supu lakini pia nitapata pesa kwa ajili ya kuwasaidia wenzangu” alisema Mansoor.
Baadhi ya majirani wanasema maisha ya Bi Farashuu na Mume wake Bwana Hamad Saleh ni magumu wakati mume hana kazi ya kufanya Bi Farashuu anahangaika na kupika maandazi kwa ajili ya kuendeleza maisha yake na familia yake.
“Mwanadishi ngoja mimi nikuambie ukweli maana yeye mwenyewe anaona aibu kusema kwa kweli maisha yake ni magumu sana kuliko unavyomuona hapa maana ananunua unga na kukanda maandazi 20 kila siku na maandazi hayo 10 anauza na maandazi 10 anakula na wanawe kila mtoto anakula andazi moja” alisema Sada Hamed Rashid ambaye ni jirani yake.
Kufuatia hali yao ngumu ya maisha na wanataka kumtibu mtoto wao wameamua kuuza nyumba yao kwa tahamani ya shilingi millioni 30 lakini tokea wameanza kutangaza bei hadi leo hii haijanunuliwa huku baadhi ya jamaa zao wakikataa nyumba hiyo isiuzwe kutokana na kuwa watapata tabu na kukosa sehemu ya kuishi.
“Jamaa zangu wengi wamenishauri tusiiuze nyumba yetu wanasema tutapata tabu ya makaazi ya kujisitiri mimi na wanangu lakini hali ndio ngumu mtoto anateseka kwa hivyo lazima tutafte namna ya kutatua tatizo hili lakini pia ni mtihani maana hiyo nyumba pia hatujapata mteja” alisema Bi Farashuu.
Idadi ya watu wenye kupata ulemavu imekuwa ikiongezeka kufuatia kuanguka juu ya minazi lakini zaidi wanaoanguka juu ya mikarafuu ambapo baadhi yao huvunjika viungo vya miili yao na wengine kupooza na kuwa walemavu.
Kwa mujibu Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko, Nassor Ahmed Mazrui amesema ni kweli wapo watu ambao huanguka mikarafuu lakini idadi haifiki 200 kwani baadhi yao kati ya hao wanaotajwa ni wameanguka mikarafuu, Minazi na wengine wamepata ajali mbali mbali ikiwemo Vespa na Gari hivyo ndio maana idadi inaonekana ni kubwa zaidi lakini katika kipindi cha mwaka jana wizara yake imeshuhudia watu watatu walioanguka mikarafuu ambao wamepata majeraha na ulemavu.
Msomaji wa Makala hii kumbuka kwamba kutoa ni moyo na sio utajiri kwa hivyo utakachoweza kutoa wewe toa tu na kitasaidia hata kama ni shilingi elfu tano (5,000) utakuwa umemsaidia Mansoor katika matibabu yake kwani hii ni sadaka yako na utakuwa unamkopesha Mwenyeenzi Mungu na bila ya shaka utakikuta mbele ya safari Inshallah.
Mtu ambaye ataguswa na matatizo ya Mansoor awasiliane na Mwandishi wa Makala hii Salma Said kwa email muftiiy@yahoo.com au simu +255777477101 au Tigo Pesa  +255715477101

No comments:

Post a Comment