Friday, June 27, 2014

KARIBU MWEZI MTUKUFU WA RAMADHANI

WAHIMIZENI WAUME ZENU,KAKA ZENU,WAJOMBA ZENU,BABU ZENU IKIWA WANAJIWEZA KUSWALI TARAWEHE IN SHAA ALLAH


SECOND MARRIAGE-A STORY THAT WILL MAKE YOU CRY(WACHENI WAUME ZENU WAOWE WAKE WENGINE MUSTIRI UMMAH MUSIWE MABAHILI WA WAUME ZENU)


Second Marriage – A Story That Will Make You Cry

by Sana -June 11, 2014

The words reverberated through my brain. Why..? Am I not 
good enough..? Never! I will never accept a second wife! If 
you want a second wife you can go out and get one as long 
as you know that I will not be here when you come back..!!!
Those were my words to my husband a few years ago when 
he mentioned to me that he is intending to marry again a 
second time. It was a woman recently divorced, 4 children. 
She is having a hard time, he said, she don’t know where 
the next meal is coming from or how to provide adequately 
for her children. “Where is their father..?” I asked, “Can’t he 
take care of his own kids..? Why do you a strange man 
have 
to carry another man’s burden..? Surely there are other 
ways 
that you can help her out financially without having to 
MARRY her!
I could not imagine myself in a plural marriage. Sharing my 
husband with another woman. Sharing his love, his smiles, 
his jokes with a woman other than myself. I could not 
fathom 
him holding her close and whispering loving words in her 
ears. It was unacceptable. An outrage. After all I have been 
to him. Wife, lover, mother, doctor, housekeeper. I raised 3 
of his beautiful children. How can he insult me by marrying 
another woman as if I am not good enough. Not pretty 
enough. Not young enough or just plain not ENOUGH.!!!
NO..!!! I could not accept that and I vehemently made my 
stance clear to him. If she walks in, I walk out! Plain and 
simple. If he is willing to risk our marriage, our life, our 
children for another woman, then he must go ahead. I will 
not stand for it!
It all seems so many years ago now. When I thought that 
life 
would last forever and that nothing will ever change. But it 
did..
My husband did not get married to a second wife. After all 
my warnings and threats of leaving he abandoned the 
idea. 
don’t know what happened to the women and children. My 
guess is that they moved on to another town.
He never mentioned a second wife again and I was happy 
with that. I managed to hang on to my husband but I didn’t 
know that our time was running out.His last words to me 
were that he had a headache and is 
going to lie down till Esha. He never read Esha namaaz that 
night, because he never woke up.
I was devastated by his sudden death. The man whom I 
have spent my life with, snatched away from me in a 
second. 
I mourned him for a long, long time.
Neglecting my children and the business. Soon all went to 
waste and we started losing everything one by one. First the 
car then the shop, then the house.
We moved in with my brother and his family. My 3 children 
and I crowded the house and my sister in law soon became 
annoyed by our presence. I needed to get out, to work and 
find a place of our own instead of living off the leftovers of 
others. But I had no skill.When my husband was alive we 
lived comfortably. I had no 
need to go out and work or or equip myself with a skill. Life 
was very difficult for me and my children and I wasn’t young 
anymore. I missed him everyday with every beat of my 
heart. 
How could ones condition change so drastically..?
One day my brother told me that someone he knew is 
looking for a wife. He was a good person, good akhlaq 
(manners) and very pious. Perfect for me, but he wants me 
to be his second wife.
It’s the second time in my life that the word second wife was 
mentioned to me. But how different the circumstances.
He came to my brothers house to see me. There was an 
immediate connection between us. I liked him and I liked 
everything about him. He told me that his first wife knows 
that he is intending to marry again but that she is obviously 
not supportive of the idea and that he doesn’t know what 
her 
reaction will be when he tells her that he had found 
someone. His answer he said, will be dependent on her 
acceptance of Polygamy.
I started reading Istikhara that night. I so desperately 
wanted 
it to work out. I remembered so many years ago when the 
life of another woman depended on my decision and what 
my decision was. I felt contrite, I felt that because I did not 

give another woman a chance, a space in my life, that Allah 
will punish me this time around. I repented, not once in my 
life did I think my action worthy of repentance because I had 
done nothing wrong. I only protected what was mine.
Now that I am on the receiving end, I realized how wrong I 
was in denying another woman this PRIVILEGE of a 
husband.
I prayed that she will accept me.
He phoned me a few days later telling me that his wife is 
having a hard time accepting it but that she is willing to 
meet 
me.
I was nervous the day of the meeting. I prayed a lot the day 
before and asked Allah to help me. When I met her, she 
was 
a person, a woman like me . A woman who loves her 
husband and fears losing him.
She took my hand and with tears in her eyes said: ” This is 
very hard for me, but I hope that we can be sisters”..
Her words broke my heart. All I needed in these dark days 
was a hand reaching out to me and embracing me, giving 
me hope and the will to carry on.
His wife was to me, the woman that I could not be and I will 
be forever grateful for that. I thought that no one could love 
her husband the way I loved mine, but she taught me the 
true meaning of unconditional love.

Wednesday, June 25, 2014

MALI ZA MBUNGE MOJA WA NCHI YA TANGANYIKA KUPIGWA MNADA (itabidi acheze mnanda sasa) NDIO MAANA WANAJIDA SEREKALI TATU ZINA GHARAMA KUMBE MAJIZI MAKUBWA YANAWANYONYA TU RAI

bbh
Kapteni John Komba
Waziri Mkuu Pinda aingilia bila mafanikio
ZIMESALIA siku tano tu, kuanzia Jumatano wiki hii, kabla ya baadhi ya mali za Mbunge maarufu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kapteni John Komba, kupigwa mnada ili kufidia deni kubwa alilonalo katika Benki ya CRDB.
Kwa mujibu wa nyaraka mbalimbali zilizopatikana, Komba anayemiliki shule kadhaa jijini Dar es Salaam, ikiwamo ya Bakili Muluzi, anadaiwa na Benki ya CRDB zaidi ya Sh bilioni moja, ikiwa ni deni la msingi pamoja na riba ya asilimia 17 katika miaka mitano anayodaiwa kushindwa kulipa deni hilo.
Deni la msingi ni Sh milioni 900, lililotolewa katika mikupuo miwili; kwanza Sh milioni 300 na baadaye Sh milioni 600, baada ya maombi ya mkopo aliyoyatuma CRDB mwaka 2007, kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa madarasa, nyumba za wafanyakazi, mabweni, uchimbaji wa visima na ununuzi wa samani kwa ajili ya madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule yake hiyo ya Bakili Muluzi.
Marejesho ya mkopo huo uliopaswa kulipwa ndani ya miaka mitano, yalitakiwa kufanyika katika mikupuo 22 na kumalizika Juni 30, 2014.
“Januari 14, 2009, Mbunge huyo alipewa na CRDB mkopo wa jumla ya Sh milioni 900 zilizopaswa kulipwa kwa ‘installments’ (mikupuo) 22 na kukamilika Juni 30, 2014,” alisema mtoa habari wetu ambaye ni wazi jina lake hatuwezi kuliweka gazetini kwa sasa.
Katika makubaliano hayo, mbunge huyo kupitia taasisi isiyo ya kiserikali (NGO) anayoimiliki, alipewa ‘grace period’ (kipindi cha muda wa matazamio) wa miezi sita, lakini hata alipoanza kulipa, malipo yake hayakwenda kama ilivyotarajiwa.
“Dhamana ya mkopo huo iliyowekwa benki ni hati tatu za viwanja anavyovimiliki namba 121244 (Plot No, 167/1 Block 1), namba 121245 (Plot No 167/2 Block 1 na namba 55920 (Plot No 1030) vyote vipo Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam,” alisema mtoa habari wetu huku nyaraka kadhaa zikithibitisha.
Uchunguzi zaidi wa Rulibaini kuwapo kwa jitihada za dhati za Mbunge huyo kulilipa deni lake hilo, lakini hadi Aprili 16, mwaka jana, alikuwa amelipa malimbikizo ya deni ya Sh 214,126,678 ambapo Sh 146,126,678 zililipwa katika Akaunti ya Benki ya CRDB, Lumumba namba 01J1008525300.
Fedha nyingine kati ya hizo ambazo ni Sh 68,000,000 zililipwa kwa Mbunge huyo na Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanganyika (TACAIDS) katika akaunti yake iliyopo CRDB Tawi la Kijitonyama, jijini Dar es Salaam na kisha yeye mwenyewe akazihamishia Tawi la CRDB Lumumba.
Muandishi wetu halikuweza kufahamu mara moja sababu za TACAIDS kumlipa Mbunge huyo kiasi hicho kikubwa cha fedha.
Kutokana na kuchelewa kulipa deni katika mtiririko waliokubaliana, hadi Novemba 2011, miaka miwili tu tangu apewe mkopo huo, deni hilo liliongezeka na kufikia Sh 1,252,110,349.14, kitendo kilichosababisha Benki ya CRDB kutafuta dalali wa Mahakama na kumtaka akamate mali za mbunge huyo na kuzipiga mnada wa hadhara.
Dalali huyo, Bani Investment Limited, alipewa kazi hiyo Februari 8 mwaka jana, lakini kabla ya kufanya hivyo, Mbunge alikimbilia Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi kuweka pingamizi, ingawa tayari wanafunzi kadhaa wa shule anazozimiliki walilazimika kuhamia shule nyingine kutokana na kutofahamu mustakabali wao.
“Wakati wa mgogoro kati yake na CRDB, Mbunge huyo alikuwa akihaha kuhamisha umiliki wa shule zake, kiasi cha kufikia makubaliano na kampuni ya IKS Tanganyika kuiendesha moja ya shule zake kwa miaka mitano huku ikilipa deni hilo kwa niaba ya Mbunge, lakini suala hilo lilishindikana,” taarifa zaidi zinafafanua.
Baada ya kuona kuwa suala hilo linazidi kuwa gumu kwake, Muandishi wetu akafahamu kwamba, Mbunge huyo ambaye ana uhusiano mzuri na baadhi ya viongozi wa juu wa CCM na Serikali, aliiomba Ofisi ya Waziri Mkuu (PMO) kuingilia kati suala hilo na kumshawishi Mkurugenzi wa CRDB, Dk. Charles Kimei, amuongezee muda wa kulipa deni lake.
Aprili 23, 2012, PMO ilimwandikia barua Dk. Kimei ikimshawishi kuangalia uwezekano wa kumwongezea muda wakati huo Serikali inatafuta namna stahiki ya kumsaidia kwa kuzinunua shule zake, lakini CRDB iliendelea na msimamo wake wa kutoongeza muda zaidi.
Machi 21 mwaka jana, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliijibu barua ya Mbunge huyo ya Februari 20 mwaka huo huo ambayo haikuwa na kumbukumbu namba, ikimtaarifu kuwa pamoja na kupokewa kwa barua hiyo, Taarifa zilizokifikia chumba cha habari zilisema kwamba, maombi ya Jiji kununua shule na ardhi anayoimiliki, kwamba yatashughulikiwa na Kamati ya Huduma za Jamii; na hadi sasa hakuna majibu aliyopewa.
Kwa sasa, zikiwa zimesalia siku hizo tano tu kufika Juni 30, 2014 ambayo ni siku ya mwisho wa makubaliano, CRDB imekuwa ikiiomba Mahakama Kuu Kitengo cha Ardhi kuiruhusu kuuza mali zote za Mbunge huyo kufidia deni lao, lakini Mbunge anadai kuwa thamani ya shule zake na ardhi ipatayo mita za mraba 34,735, ni zaidi ya deni analodaiwa.
Mbunge huyo pamoja na mkurugenzi wa CRDB Dk. Charles Kimei hawakuweza kupatikana hadi tunakwenda mitamboni, simu ya Dk. Kimei ikiita bila majibu wakati simu ya Komba ambaye mwandishi wetu hakuweza kumpata licha ya kumfuatilia bungeni mjini Dodoma ana kwa ana, haikuweza pia kupatikana.

WATANGANYIKA 65 WABEBA UNGA (DRUGS) WANATARAJIWA KUNYONGWA NCHINI CHINA HUKU WENGINE WAKIOZEA MAJELA NCHI TAFAUTI

IMG_0437XX
LUKUVI
madawa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu wa nchi ya Tanganyika, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi, akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Dawa ya Kulevya Duniani yanayotarajiwa kufanyika kitaifa jijini Mbeya kesho. 
Vijana 65 wa nchi ya Tanganyika wamehukumiwa adhabu ya kifo nchini China baada ya kupatikana na hatia ya kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.
Vijana hao ni kati ya zaidi ya 403 wa nchi ya Tanganyika wanaoshikiliwa katika nchi mbalimbali duniani kwa tuhuma ya kujihusisha na biashara hizo.
Hayo yalisemwa jana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu wa nchi ya Tanganyika (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, mjini Dodoma wakati akizungumzia Maadhimisho ya Siku Dawa za Kulevya Duniani yanayofanyika Juni 26 kila mwaka.
Lukuvi alisema kuwa kwa mwaka huu maadhimisho hayo ya kesho, kitaifa yatafanyika katika viwanja vya shule ya msingi Nzovwe jijini Mbeya na Makamu wa Rais wa nchi ya T,anganyika Dk. Gharib Bilal, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.
“Tangu mwaka 2008 kumekuwa na wimbi kubwa la vijana wenye asili ya Kitanganyika kujihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi yao ya Tanganyika, mpaka hivi sasa idadi yao ni kubwa kiasi cha kufikia zaidi ya 400, na wanashikiliwa katika nchi mbalimbali ambazo pia adhabu zao zinatofautiana kulingana na sheria za nchi hizo,” alisema Lukuvi.
NCHI WANAKOSHIKILIWA
Alizitaja baadhi ya nchi ambako vijana hao wanashikiliwa kuwa ni Brazil (108), Hong Kong (118), Kenya (34), Pakistan (16) na China 65.
Nyingine ni Japan (7), Malawi (5), Uganda (3), Uswisi (2), Marekani (2), Uturuki (1), Botswana (5) na Msumbiji (1).
“Orodha ya nchi waliko vijana hao ni defu zaidi,” alisema.
Akizungumzia maadhimisho hayo kwa nchini, Lukuvi alisema kauli mbiu yake kwa mwaka huu ni ‘Uteja wa dawa za kulevya unazuilika na kutibika, chukua hatua’.
Alisema nchi ya Tanganyika imeendelea kuwa miongoni mwa nchi zenye tatizo kubwa la dawa za kulevya kulingana na takwimu za ukamataji wa dawa hizo.
Kwa mujibu wa Lukuvi, kuanzia Januari hadi Juni mwaka huu kiasi cha kilo 220 za dawa hizo aina ya Heroine na watuhumwa 18 walikamatwa huku pia kilo 15.4 za Cocaine zilikamatwa na watuhumiwa saba.
Lukuvi alisema kwa sasa dawa za kulevya ni tishio kubwa kwa maendeleo ya taifa kwa sababu imethibitika kuwa matumizi yake hupunguza tija na ufanisi wa nguvu kazi ya taifa.
SHERIA MPYA YAJA
Alisema katika kukabiliana na tatizo hilo, Serikali ya Tanganyika imekamilisha muswada wa sheria ya dawa za kulevya ambao kama utapitishwa bungeni na kuwa sheri kama ulivyo, unaweza kusaidia kwa Kiwango kikubwa kupunguza tatizo hilo.
Lukuvi alisema tofauti na jinsi ilivyo sheria ya sasa, sheria mpya itaondoa adhabu ya faini na watuhumiwa kunyimwa dhamana wanapokamatwa, hali ambayo itasaidia kukabiliana na wasafirishaji na wauzaji wa dawa hizo.
Kwa mujibu wa Lukuvi, sheria hiyo itakwenda sambamba na uundaji wa chombo imara cha kushughulikia dawa za kulevya ambacho kitakuwa na uwezo wa kupeleleza, kukamata na kushitaki watuhumiwa wa dawa za kulevya kama ilivyo kwa Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Alisema kuwa muswada huo tayari umekamilika na kwamba wakati wowote unaweza kuwasilishwa bungeni ili upitishwe hatimaye kuwa sheria.
Alisema maadhimisho hayo pia yatafanyika katika ngazi ya mkoa nchini na kuwaomba wananchi kujitokeza kushiriki ili waweze kupata elimu ya kutosha juu ya madhara na vita dhidi ya dawa hizo.
KANDORO ANENA
Naye Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, amewataka wananchi mkoani mwake walioathirika na dawa za kulevya kujitokeza kwa wingi kupima afya zao, kupata tiba na ushauri katika maadhimisho hayo.
Kandoro alifafanua kuwa maadhimisho hayo yanafanyika mkoani humo kutokana na takwimu kuonyesha una kiwango kikubwa cha tatizo la dawa za kulevya kutokana na mwingiliano mkubwa wa watu na kutoa mfano wa bangi ambayo inalimwa kwa wingi.
“Kama mnavyojua, mkoa wetu upo mpakani hivyo tuna changamoto kubwa sana ya uingizaji wa dawa hizi, mara nyingi watu hukamatwa katika mipaka ya Tunduma na Kasumulo, hivyo ni budi elimu hii kutolewa kwa wananchi ili tushirikiane wote katika kutokomeza vita hii tuliyonayo,” alisema Kandoro.
Alisema kuwa pombe aina ya viroba vya bei nafuu vitokavyo Malawi ni changamoto pia kwani vijana wengi wanavitumia, hivyo kuathirika kwa kiasi kikubwa.

Sunday, June 22, 2014

BAINA YA UDUGU NA UWADUI KATIKA DUNIA HII

Almuakkhir
Naaswir Haamid
Ni kutokana na ujinga na dharau zetu ndio tumeufikisha Uislamu kwenye hali iliyopo sasa. Sio tu kwa kukosa dira ya kufuata au Kitabu cha kusoma, la sivyo! Bali pia ni kwa kuwafanya maadui wa Uislamu kuwa ni wenzetu wa karibu mno kuliko hata ndugu wa Kiislamu walio na imani thabiti.
Tunakosa kupata taathira ya kumsujudia Muumba mara 34 kwa siku kwa kuwa hatujayakinisha kuwa Uislamu ni dini ya haki. Iweje basi Muislamu atamke kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) ndiye Mola wake na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ndie kiongozi wake lakini bado akawa hana tofauti na Manaswara na Mayahudi? Iwapi tofauti yao? Ndio maana Muislamu huyu anaona ni sawa kupitishwa pombe mbele yake na kuyatoa nuru macho kwa kukodolea wanawake watembeao uchi. Ni Muislamu huyu huyu anayedhamini mashindano ya urembo na hata kutia saini mikataba ya pombe. Na ndio maana hata Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akikashifiwa kwa kuchorwa kikatuni au kutusiwa kwa namna nyengine yoyote, yeye anakuwa hana mshituko wowote! Subhaana Allaah.
Ni lazima tukumbuke kuwa tupo ndani ya mpambano na wala hautaisha hadi Qiyaamahkisimame. Tutakapoelewa muongozo sahihi wa dini yetu ndipo tutakapoweza kupambana na hila hizi. Sio kabisa kuitamka Shahaadah hali ya kuwa hakuna hata maendeleo yoyote ya ulinganiaji au elimu inayofundishwa. Na hata kama zikifanyika zinakosa usahihi wa Sunnah.
Waislamu tuelewe kwamba kufanya urafiki na Muislamu mwenzetu mwenye imani thaabitni bora zaidi kuliko kuwaweka nyoyoni wasiokuwa Waislamu. Sisi ni jengo moja lililo imara na haitakikani kuwaingiza maadui ndani ya harakati zetu abadan.
Hatuna haja ya kuwaorodhesha ni nani maadui wa Uislamu, kwani ni wengi. Kinyume na uadui ni kufanya nao urafiki. Kitu ambacho katu hakikubaliki ndani ya Uislamu. Tuishi nao kwa usalama na ubinaadamu pale wanapoheshimu miiko ya dini yetu. Kinachoamrishwa hapa chini sio amri ya fulani bali ni kanuni ya Muumba Anayetuamrisha:
{{Enyi mlioamini! Msiwafanye adui Zangu na adui zenu kuwa marafiki; mnaowapelekea (habari zenu) kwa ajili ya urafiki, hali ya kuwa wamekwishaikanusha haki iliyokujieni…}} [Al-Mumtahinah: 1]
Tufahamu ya kwamba kampuni zilizo nyingi zinaongozwa na Mayahudi wakisaidiana na Manaswara. Kuanzia vyombo vya habari, vyakula, vivazi na mengineyo chungu nzima. Tuwe makini na kinachozalishwa humo kwani ni mara nyingi kinakuwa ni chenye kuleta madhara kwa Waislamu na Uislamu wao. Hata kazi kadhaa zinazofanywa humalizia kukejeli dini tukufu ya Uislamu. Tuzifuatie hila hizi na kuzipinga angalau tu kwa kutozitumia.
Kuna mengi ambayo yanafanywa na sisi wenyewe tunayashuhudia. Maadui zetu wanachora vikatuni vya kumkashifu[1] Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na wengine wanaandika vitabu maalum[2] ambavyo ndio vinawapatia tuzo za heshima kwa kumkashifu Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) tu! Maoni ya kupunguza kasi ya Ukimwi yamefanywa kuwa ni chambo ya kuutukana Uislamu kwa kueleza kwamba mgao wa mirathi unachangia kumtelekeza mwanamke na kumsababishia kuingia kwenye biashara haramu.[3]Inafikia hatua ya Mbunge kupeleka mapendekezo maalum kwenye bunge kwa ajili ya kuudumaza Uislamu tu[4].
Tukumbuke kwamba kuendelea kunyamaza kimya ndio tunapoendelea kudhalilika na kudhoofika. Wengi wetu ndio tunaangukia kwenye udhaifu wa imani kwani twaona maovu yanayotendwa mbele yetu lakini hatuna tunachokemea.
Kutoka kwa Mtume wetu mpenzi (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Hadiyth iliyosimuliwa na Abuu Sa’iyd Al-Khudriy (Radhiya Allahu  ‘anhu) ambaye amesema: Nilimsikia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)  akisema: “Yeyote yule atakayeona kitendo kiovu basi akiondoe (akibadilishe) kwa mkono wake, ikiwa hawezi basi kwa ulimi wake (alikemee au kukataza), na ikiwa hawezi basi kwa moyo wake (achukie) na huo (yaani kuona baya na kunyamaza) ni udhaifu wa Imani)) Muslim
Hivyo, tuelewe ndugu zangu wa Kiislamu kwamba tupo baina ya mstari mwembamba ndani ya mapambano ya Udugu wetu Waislamu na Maadui ambao ndio wengi mno. Nao wanashambulia kutoka kila kona ya ulimwengu huu na kwa hila tofauti zilizo dhaahir na zilizo siri.
Tushikamane na tufuate Sunnah sahihi ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa kuisoma vyema Qur-aan na kufuata maadili mema ya Uislamu wetu. Insha Allaah tukiwa imara, Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Atatupatia ushindi kwa nia na vitendo vyetu.
[1] Gazeti la Gulf News la 14/02/08 uk. 23 limetangaza kwamba magazeti 17 ya Denmark yamemtukana Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).
[2] Salman Rushdie, Aya za Shetani SATANIC VERSES, (1988).
[3] Rudia Ripoti ya Jumuiya ya Wanasheria Wakike Tanzania, REVIEWS AND ASSESSMENT OF LAWS AFFECTING HIV/AIDS IN TANZANIATAWLA, Magdalena K. Rwebangira na Maria Tungaraza, (2003), uk. 29, 30 na 43.
[4] Pamoja na mambo mengine, Ibara ya 2 (c) ya Hati ya Uingereza kwa Uislamu na Waislamu inaeleza kwamba taasisi za Kiislamu ziwaeleze vijana wa Kiislamu kwamba sheria za kijamii za nchi ni bora kuliko Shariah (Qur-aan na Sunnah). Rudia A Proposed Charter of Muslim Understanding by Sam Solomon, Foreword by Gerard Batten, UK Independence Party, Member of the European Parliament for London, December 2006.

Sunday, June 15, 2014

MCHANGO WA WAISLAMU KUPIGANIA UHURU WA NCHI YAO TANGANYIKA NI MKUBWA SANA LAKINI KWA NINI LEO WAO NDIO WANAO ATHIBIWA...???

WAZEE WA TANU
Waliokuwa Katika Picha Hii ni Wazee wa TANU waliopigania uhuru wa Tanganyika wa Kristo ni wawili 2 kwenye list hii.
Kila anaye kata kuto kuikubali Tanganyika au kuto kuizungumzia Tanganyika anaogopa haya maana anajuwa wakizungumza kuhusu Tanganyika itakuwa je nani walio gombea uhuru wakitajwa wengi wao huwa hawafurahi wataje kwa kuwa ni waislamu au kwa sababu zao nyengine wenyewe wanazijuwa wenyewe ndio ukaona wanashika bango la nyerere weee nyerere weee wakati nyerere mwenye alipojiunga na TANU watu walikuwa tayari washagombania uhuru kwa miaka mingi nyuma kabla yeye toka enzi za chama cha TAA na kabla ya chama cha TAA waislamu walikuwa wakidai uhuru leo hii wamekuwa kama wageni kaika nchi yao au mayatima.
1. Abdallah Shomari (Tandamti No. 3)
2. Nassoro Kalumbanya (Simba)
3. Said Chamwenyewe (Aggrey/Congo)
4. Mtoro Ally (Muhonda)
5. John Rupia (Misheni Kota)
6. Julius Nyerere (Pugu Sekondari)
7. Said Chaurembo (Congo/Mkunguni)
8. Jumbe Tambaza (Upanga)
9. Sheikh Suleiman Takadir (Mafia/Swahili)
10. Dossa Aziz (Mbaruku/Somali Kipande)
11. Mshume Kiyate (Tandamti)
12.Juma Sultani (Kitchwele Karibu na Kanisa Dogo)
13. Maalim Shubeti (Masasi/Likoma)
14. Rajab Simba (Kiungani)
15. Waziri Mtonga (Kilosa 18, Ilala)
16. Mwinjuma Mwinyikambi (Mwananyamala)
17. Makisi Mbwana (Aggrey/Congo)
18. Usia Omari (Sungwi, Kisarawe)
19. Sheikh Issa Nasir (Bagamoyo).
Hakuna shaka kuwa mchango wa waislamu katika harakati za kupigania uhuru wa nchi ya Tanganyika ulikua mkubwa lakini baada ya uhuru na mpaka leo hii jee waislamu walithaminiwa au kanisa lilichukua mkondo wake....????

Saturday, June 14, 2014

KAMA KAWAIDA KISONGE NA CHUKI ZAO NA UBAGUZI WAO WANAENDELEA JE POLISI MAGUGU HAMOYAONI MUNAYAONA YA GAZA TU...???


KAMISHA WA POLISI NCHINI ZANZIBAR HAMDAN OMAR MAKAME UMESOMA KISONGE LEO INAVYO FITINISHA WAZANZIBARI JE MUTAWASHUGHULIKIA KISONGE..?
IMG-20140613-WA0025

MKADAM KAMA UNATA KUJUWA WANAO CHAFUA AMANI NDIO HAO KISONGE JE UMESOMA UBAO WA LEO JINSI UNAVYO PANDIKIZA CHUKI NA UBAGUZI JE MUTAWASHUGHULIKIA KISONGE...?

Hakuna shaka kua hali hii ya kuachiwa Ubao wa ccm wa Kisonge umekuwa  ukazalisha Fitna na chuki zakujaribu kuwagawa jamii ya wananchi wa nchi ya Zanzibar kwa misingi ya Upemba na Unguja kwa kipindi kirefu sana sasa.
Hali hii sikwamba viongozi wa ccm/Smz wauwaji hawaioni au hawaijuwi kua haina tija yoyote zaidi ya kupanda mbegu ya Ubaguzi na Fitna za kuianganiza jamii ya wananchi wa nchi ya Zanzibar.
Ikiwa Serekali ya Smz wauwaji italifumbia jicho Fitna hizi na chuki hizi basi wasije kujilaumu pindipo mbegu hii ikipata rutba na kumea.
Kila kukicha viongozi wetu huhubiri Amani na Utulivu uliopo nchini hapa Zanzibar lakini leo Kisonge imekua ndio kichecheo no one kupandikiza chuki ,Fitna na Ubaguzi kujaribu kuwagawa Wananchi wa nchi ya Zanzibar kwa kisingizio cha Upemba na Unguja ,Uarabu na Uhadimu Udini na Ukabila.
Jambo hili sikwamba Serekali hawalioni ,lakini wao inaonekana wamelipa baraka zote na ndio ukaona wanashindwa hata kukemea vitendo wanavyo fanya Kisonge ndani ya nchi yetu ya Zanzibar.
Tukumbuke tu kua nchi hii si shamba au mali ya ccm, kila Mzanzibar ana haki na thamani kama Mzanzibar yoyote ndani ya nchi yake.
Serekali inapo ruhusu kundi au watu fulani kuwa wao ndio wako juu kuliko wengine , hio nikuonyesha kua imeshindwa kazi ya kuwahudumikia raia ndani ya nchi yao.
Ikiwa Ubao wa ccm wa kisonge utaendelea kupata baraka za Serekali na chama cha ccm basi wasije wakajuta na kujijutia hali ikibadilika na historia kuwahukumu kwa walicho kipanda na kumea.
M/mungu ibariki Zanzibar na watu wake.

JESHI LA POLISI NCHINI ZANZIBAR NI LA KUFUNGA MASHEIKH NA WATETEA MAMLA KAMILI SIO KUSHIKA WAHALIFU WANAO WASHAMBULIA WANANCHI KWA NJIA TAFAUTI


kijana moja afa baada ya kurushwa bomu na watu wasio julikana nchini Zanzibar

VYEO KIBAO KATIKA BEGA VYA KULA PESA ZA BURE TU HUKU WANANCHI WANAISHI KWA WASI WASI NDANI YA NCHI YAO BORA HIVI VYEO UKAUZEYE MBATATA ZA OROJO NA ZANZIBAR PIZZA
RPC Mkoa wa Mjini Maghar Mkadam Khamis wakakati akizungumza akizungumza na vyombo vya habari


Jeshi feki la walala hoi na kujuwa peke kushika masheikh lakini wahalifu wa kweli hawawashiki la nchini Zanzibar limesema bado halijabaini mtu yoyote au kundi lolote kuhusika na uripuaji wa Bomu katika eneo la jana mjini magharibi nchini Zanzibar.
Kauli imetolewa na RPC Mkoa wa Mjini Maghar Mkadam Khamis wakati akizungumza na kupitia simu yake ya mkononi na baadhi ya vyombo vya habari.
Amesema katika tukio hilo mtu mmoja amefariki dunia na wengine saba kujeruhiwa baada ya kutokea mripuko huo wa bomu.
Taharuki hio imetokea wakati waumini wa Dini ya kiislamu walipokuwa wanatoka msikitini wa Darajani ambapo kulikuwa na mawaidha baada ya kumalizika kwa sala ya Ishaa.
Akibainisha kutokea kwa tukio hilo RPC huyo ,amesema kwamba watu waliokuwa ndani ya gari ndogo aina ya Vits walirusha bomu hilo na kukimbia kusiko julikana wakati waumini wa Dini ya kiislamu walipokuwa wanatoka msikitini.  ((nchi hii ya Zanzibar ina ukumbwa gani ambao gari ikikimbia huwa haijulikani ilikotokomeya Maghar Mkadam Khamis...???))
Hadi sasa Jeshi la Polisi bado halijabaini iwapo bomu hilo ni lakutengeneza kwa kutumia baruti au ni bomu wenyewe ambalo limetengezwa kwa njia ya kitaalamu. ((ni lini jeshi hili la polisi hapa nchini Zanzibar lilibaini jambo lolote la kishenzi wanalofanyiwa Wazanzibari....???))
Alieleza kuwa aliefariki katika tukio hilo ni Khatibu Mkumbiladuha (26) mkaazi wa Mkoa wa Tanga ambae alikuwa miongoni mwa wahadhir waliofika msikitini hapo.
Aidha RPC Mkadam amewataka wananchi wa Zanzibar kuwa watulivu katika kipindi hichi huku wakiliacha Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini wahusika wa tukio hilo na hatimae kuwafikisha katika vyombo vya sheria.
RPC Mkada je mume wabaini walio mpiga risasi yule padri..? je mume mbaini aliyempiga risasi yule padri mwengine na kuumuwa...? je mume mbaini yule aliye mpiga mapaga sheikh kule kitope..? je mume mbaini yule aliye mrushia sheikh tindi kali...? je mume mbaini yule aliye mrushia padri tindi kali....? je mume mbaini yule aliye warushi tindi kali wale wasichana wakizungu kutoka uengereza n.k. hamna leno moja kazi kula pesa za bure basi nakujuwa kufunga masheikh jela.
Katika kipindi cha hivi karibuni nchi ya Zanzibar imekuwa akikubwa na matukio mbali mbali ya uchafuzi wa amani ikiwa pamoja na kuwawa kwa sheikh kwa mapanga kitope na baadhi ya matukio mengine kadhaa ya uchafuzi wa amani.
Lakini nashauri uchunguzi huo uanzie kwa akina salmini awadh,asha bakari,lukuvi,jon komba na mussa ali hassan,kwani katika wao na wenzao ni baadhi ya watu ambao wameanza kuonyesha na kutoa kila dalili mbaya na ukilinganisha na matokeo kama haya.mfano
mussa ali hassan alisema katika bunge la katiba kua ukawa watoke zanzibar si hivyo wao watawatoa maana wao ni wapiganaji mahiri sasa kauli kama hizi wazanzibari zinatutia mashaka.

Friday, June 13, 2014

NCHI YETU YA ZANZIBAR TULIKUWA TUKILALA MLANGO WAZI LEO HII NI KAMBI YA MAJAMBAZI WENYE SILAHA ZA MOTO (AKA 47,BASTOLA n.k)

Msikecorner199
Kutoka kwenye kulala mlango wazi mpaka sasa tunamageti na pia hatuna tena salama katika nchi yetu ya Zanzibar na hii yote inasababishwa na kutokuwa na kizuizi cha ingia toka katika mwambao wa visiwa vyetu vidogo vidogo na nchi yetu Zanzibar kwa ujumla watu wanaingia tu kama vile jalalani maana hata choo pia kinahishima yake maana lazima ugonge mlago ujuwe kama kuna mtu utasubiri kama hakuna ndio utaingia lakini jaani unakwenda tu na kutupa uwoza wako ndio nchi yetu ya Zanzibar ilivyo fanywa na wahafidhini ganga njaa ya matumbo yao,
 ile sifa na haiba ya Amani na Utulivu katika visiwa au nchi yetu ya Zanzibar imeondoka na sasa imebakia ni kisiwa cha Majambazi na vitendo vya Uharamia wakutisha hata wizi wakutumia silaha za moto (Risasi) sasa limekuwa ni jambo la kawaida good jobb asha bakari makame na balozi mdogo wa tanganyika.
Huko Nyuma Wananchi wa nchi ya Zanzibar hatukuzowe kuona haya na hivi sasa ni hali ya kawaida tu katika nchi yetu ya Zanzibar kuyaona haya au kusikia vitendo hivi vikifanyika ndani ya nchi yetu ya Zanzibar.
Hali hii ni yakujaa Zanzibar na sio utamaduni ulozoweleka kwa Wananchi wa nchi ya Zanzibar.
Hivi sasa akina mama wanashindwa kutembea peke yao ikingia kiza tu kwa kuogopa na hofu ilotanda wakati ilikuwa baada ya maghari mama zetu huka barazani na kupunga upepe wa marashi ya karafu sasa kuna jipepo la majambazi nje hakukaliki ,ukenda badhi ya maeneo kama vile Masokoni majumba yalokua yamejengwa hayaja malizika kuna makundi ya wageni wenye kulala lala ovyo Serekali haina ijuwala zaidi ya fitina na ubaguzi na chuki basi wananchi wa nchi yako hawana raha wao habari hawana kazi kuiba mapesa na kupandikiza chuki.  
Wengi wao wanakua ndio hao majambazi na wenye kupora watu wamo katika majumba ambayo hayajamalizwa ndimo wanamo lala na kupanga jinsi gani ya kuwahujumu rai na wananchi wa nchi ya Zanzibar.tumulize Shein lile jeshi lako la polisi lililokwenda kuwapinga watu msikitini kwajili yakuwaombea watu walio zama na meli linafanya kazi gani...? au ile ndio kazi yao kuwahujumu wananchi wa Zanzibar kama wanavyo hujumiwa na hawa majambazi...?
Serekali ya majambazi Smz hebu wambiyeni hao majambazi wenu watafute kwengine kwa kwenda la sivyo yatakayo wakuta musije kuwalaumu Wazanzibari na nyinyi SUK nilazima iwe na operation malumu ya walala lala ovyo musituzinguwe.