Friday, August 29, 2014

ZAHOR MAZRUI AWAPA JESHI LA POLISI LA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA LILIOPO NCHINI ZANZIBAR VITENDA KAZI TUNAKUKUMBUSHA ZAHOR MAZRUI USISAHAU KUWALETEA MAJITI NA CHUPA PIA NI VITENDA KAZI ILI WAWATHIBU VIZURI WAZANZIBARI

Bwana Zahor Mazrui akimkabidhi radio call kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Omar.
Jeshi la Polisi la Mkoloni Mweusi Tanganyika liliopo nchini Zanzibar limesema litaendelea kuthamini jitihada za wasamaria wema wenye nia ya kulipatia jeshi hilo msaada wa vitu mbali mbali kama vitendea kazi.
Kauli hio imetolewa na Kamishna wa Jeshi la Polisi la Mkoloni Mweusi Tanganyika liliopo nchini Zanzibar Hamdani Omar Makame, wakati alipokuwa akipokea msaada wa vitu mbali mbali kwa ajili ya kupeleka mbele harakati za Jeshi hilo kukabiliana na Wazanzibari wote wanao pigania haki ya nchi yao kuwa huru na kujivuwa katika mikono ya Mkoloni Mweusi Tanganyika pia aina mbali mbali kama kuwatharaulisha Masheikh,Wazanzibar kwa ujumla Nchini huko makao makuu ya Polisi Ziwani nchini Zanzibar.
Hamdan ameleza kuwa msaada huo uliotolewa na Katibu mtendaji wa jumuia ya Zanzibar Cheretable Society Bwana Zahor Mazrui umekuja kwa wakati muafaka kutokana na changa moto kadhaa zinazolikabili Jeshi la Polisi la Mkoloni Mweusi Tanganyika liliopo nchini Zanzibar.
Akibainisha miongoni mwa Changamoto zinazolikabili Jeshi la Polisi la Mkoloni Mweusi Tanganyika hapa nchini Zanzibar Kamishna huyo amesema ni uhaba wa majengo sambamba na vitendea kazi.
Hivo ametoa wito kwa wasamaria wema wenye moyo kama wa Bwana Zahor Mazrui kujitokeza kwa ajili ya kulisaidia jeshi hilo la Mkoloni Mweusi Tanganyika ili liweze kufanya kazi zake kwa ufasaha wa kuwathibiti Wazanzibari wote wao taka nchi yao kuwa huru.
Mara baada ya kukabidhi msaada huo wa Computer 10 radio call 30 printer 2 pamoja na calculate 90,Mkurugenzi mtendaji wa Zanzibar Cheretable Society Bwana Zahor Mazrui amesema ameamua kutoa msaada huo kwa jeshi la polisi ili wawe na nyenzo imara za kufanyia kazi ili kudhibiti wahalafu nchini Zanzibar.
Amebaisha kuwa msaada huo kwa jeshi hilo la Mkoloni Mweusi Tanganyika hautokuwa wa mwanzo na ataendelea kila pale anapopata wasaa kwani si jambo baya kusaidia Polisi.
”Wako watu wananishangaa sana kwa nini nawapa msaada jeshi la polisi la Mkoloni Mweisi Tanganyika lakini sitosita kwa sababu msaada utawafanya watende kazi zao kwa uadilifu”alieleza Bwana Mazrui.
Sambamba na hayo ametoa shukrani zake kwa jeshi hilo la Mkoloni Mweusi Tanganyika kupokea hicho kidogo alichokitowa na amewataka wasimchoke pale anapohitaji kutoa msaada mwengine zaidi.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO HAITAKUFA SIKU HIYO.

No comments:

Post a Comment