Friday, November 28, 2014

MAHAKAMA YA KISUTU BAADA YA KUPATA PIGO KUWA HAIAMINIWI NA WANANCH NA MAHAKI WAO PIA YA AMUUWA KUJISAFISHA NA KUMFUTIA SHEIKH MPONDA KESI HALI WANAJUWA KUWA TOKA MWANZO KULIKUWA HAKUNA KESI BALI KUBABIKIZIWA TU


Nchini Tanganyika Dar es Salaam. Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imemtakasa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanaanyika, Sheikh Issa Ponda dhidi ya hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliyomtia hatiani katika kesi ya jinai iliyotokana na mgogoro wa ardhi wa Chang’ombe Markazi. Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Agustine Shangwa baada ya kuridhika na hoja za rufani za Sheikh Ponda kupitia kwa Wakili wake, Juma Nassoro kupinga hukumu na hatia ya Mahakama ya Kisutu. Mbali na kumfutia hatia hiyo, pia Jaji Shangwa alimshauri Sheikh Ponda kufungua kesi ya madai dhidi ya Baraza Kuu la Waislamu Tanganyika (Bakwata), pamoja na Kampuni ya Agritanza Ltd iliyonunua eneo la Chang’ombe Markazi. Ponda alikata rufani mahakamani hapo akipinga hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliyomtia hatiani katika kesi ya jinai namba 245 ya mwaka 2012, iliyokuwa ikimkabili yeye na wenzake 49. Katika rufaa hiyo, Sheikh Ponda kupitia kwa wakili wake, Nassoro aliwasilisha jumla ya hoja sita za kupinga hukumu hiyo. Hoja hizo zilikuwa ni pamoja na ya kudai kuwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilikosea kumtia hatiani kwa kuwa hapakuwa na ushahidi wa kutosha kumtia hatiani kwa kosa hilo la kuingia kwa nguvu katika eneo hilo la mgogoro. Pia alidai kuwa mahakama ilikosea kumtia hatiani na kuwaachia huru washtakiwa wenzake. kwa kutumia ushahidhi huohuo, na kwamba kesi hiyo ilikuwa ikihusu mgogoro wa ardhi hivyo Polisi walipaswa kumshauri mlalamikaji akafungue kesi ya madai katika Mahakama ya Ardhi. Hata hivyo katika hukumu yake Jaji Shangwa alijikita katika hoja moja tu kama kulikuwa na ushahidi wa kutosho kumtia hatiani mrufani.
Akijibu hoja hiyo katika hukumu yake, Jaji Shangwa alikubaliana na Wakili wa mrufani kuwa hapakuwa na ushahidi wa kutosha kumtia hatiani mrufani bila kuacha mashaka. Jaji Shangwa alisema kuwa hakuna ushahidi kuwa mrufani aliwashinda mkono au kuwahamaisha wale watu aliokuwa akishitakiwa nao kwenda katika eneo hilo, bali wale watu walikwenda pale wenyewe baada ya kutangaziwa katika misikiti yao kuwa kuna ujenzi wa msikiti wa muda katika eneo hilo. “Kama hakufanya hivyo utasema kuwa aliingia kwa nguvu..???? Nakubaliana na hoza za wakili wa mrufani, Nassoro kuwa hakuna ushahidi wa kutosha mahakama kumtia hatiani mrufani bila kuacha mashaka.”, alisema Jaji Shangwa. Alisema kuwa hata katika maelezo ya Onyo, ya baadhi ya waliokuwa wakishtakiwa pamoja, hakuna hata mmoja aliyesema kuwa alipelekwa katika eneo hilo na Sheikh Ponda na kwamba walikwenda kwa utashi wao baada ya kutangaziwa kuwa kuna ujenzi wa msikiti. “Hivyo ninatengua hukumu ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, ilioyomtia hatiani kwa kosa la kuingia kwa nguvu katika eneo la Chang’ombe Markazi na kumwachia kwa masharti.”, alisema Jaji Shangwa. Hata hivyo licha ya kumfutia hatia hiyo Jaji Shangwa alimshauri Sheikh Ponda asiende kudai hilo eneo kwa njia nyingine isipokuwa kwa njia ya mahakama. Alisema kuwa hadi sasa kuna mkataba kuwa Bakwata waliiuzia Agritanza kwa Sh150 milioni pamoja na eneo lingine la hekari 40 Kisarawe.
Alisema kwa kuwa wanadai kuwa eneo hilo ni mali ya Waislam lililowekwa wakfu na hivyo halikustahili kuuzwa, basi washauriane na wakili wao ili wafungue kesi ya madai dhidi ya Agritanza na kuliunganisha Bakwata, kupinga kuuzwa kwa eneo hilo. Katika kesi ya msingi, Ponda na wenzake walikuwa wakikabiliwa atii mashtaka ya kula njama, wizi wa mali yenye thamani ya Sh 59.6 milioni na kuingia kijinai kwa nia ya kujimilikisha isivyo halali eneo la ardhi inayomilikiwa na Kampuni ya Agritanza Ltd. Ponda na mwenzake Mukadamu Swaleh kwa pamoja walikuwa wakikabiliwa na shtaka linguine zaidi, la uchochezi. Mahakama ya Kisutu katika hukumu yake iliyotolewa na Hakimu Mkazi Victoria Nongwa, Mei 9, 2013, ilimtia hatiani Ponda peke yake kwa kosa la kuingia kijinai katika eneo la ardhi ya Agritanza Ltd, lakini ikawaachia huru washtakiwa wengine wote. Hata hivyo licha ya kumtia hatiani Ponda, mahakama hiyo ilimwachia huru kwa masharti ya kutokutenda kosa lolote katika kipindi cha miezi 12 (mwaka mmoja), chini ya kifungu ncha 25 (g) cha Sheria ya Kanuni za Adhabu (Penal Code- PC). Hata hivyo licha ya kushinda rufaa hiyo Sheikh Ponda alirudishwa mahabusu kutokana na kesi nyingine ya jinai inayomkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro, ambapo dhamana yake imefungwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP). Katika kesi hiyo jinai namba 128 ya mwaka 2013 Morogoro, Ponda anakabiliwa na mashtaka ya kufanya uchochezi katika maeneo mbalimbali mjini Morogoro na kukaidi amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, kumtaka asifanye kosa lolote katika kipindi cha miezi 12. Kutokana na hukumu hiyo Wakili wake, Nassoro alisema sasa watawasilisha nakala ya hukumu hiyo katika Mahakama ya Morogoro na kuomba afutiwe shtaka hilo la kukaidi amri ya Mahakama ya Kisutu.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

NCHINI TANGANYIKA WANAMWITA ATI WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA KUMBE NI JAMBAZI KUUUUU DUUUUUH !!


SIKU ZA MWIZI KWELI NI ARBAINI ATI WAZIRI MKUU YAGUJUUU JAMBAZI KUBWA WATANGANYIKA MPOOO AU BADO MELALA FOFOFO BURKI NA FASO WAMEFANYA KWELI KWA MIJITU YA AINA HII NYINYI MUNAWACHEKELEA TU

Giningi Dodoma. Hatimaye mtikisiko wa tano umetimia na nchi Tanganyika kutikiswa; ripoti ya Kamati ya Hesabu za Serikali ya Tanganyika  (PAC) imependekeza kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda Mr Zanzibar si Nchi, Mwanasheria Mkuu, Waziri wa Nishati na Madini, naibu wake na katibu mkuu wa wizara hiyo wawajibishwe kutokana na kuhusika kwao kwenye sakata la uchotwaji wa Sh306 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow. Akaunti hiyo ilifunguliwa kwa ajili ya kutunza fedha za gharama za uwekezaji (capacity charge) baada ya kuibuka mzozo wa kimkataba baina ya Shirika la Umeme Tanganyika (Tanesco) na kampuni binafsi ya IPTL ambayo iliingia mkataba wa kufua umeme na kuliuzia nishati hiyo shirika hilo la umma. Ripoti hiyo ilisomwa jana Giningi Dodoma bungeni kwa kupokezana kati ya Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe na Makamu mwenyekiti, Deo Filikunjombe baada ya majadiliano marefu kwenye vikao vya ndani vya CCM na Kamati ya Uongozi wa Bunge na jitihada kubwa za kutaka isisomwe na kujadiliwa. Ripoti hiyo ilitokana na ukaguzi uliofanywa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambayo ilianika ukiukwaji mkubwa wa taratibu wakati wa uchotaji wa fedha hizo pia mahojiano na mkurugenzi mkuu wa Takukuru na Mamlaka ya Mapato Tanganyika (TRA).
Waziri Pinda ametiwa hatiani na kamati hiyo kutokana na kujua kuwapo kwa ufisadi huo na kauli zake kuwa fedha hizo hazikuwa mali ya umma, wakati Mwanasheria Mkuu Jaji Frederick Werema ameonekana kutoishauri vizuri Serikali na pia kuagiza fedha hizo zitolewe kwenye akaunti hiyo, wakati Waziri Sospeter Muhongo hakuchukua hatua wakati akijua kuwapo kwa sakata hilo, huku naibu wake, Stephen Masele akitiwa hatiani kwa kulidanganya Bunge. Kamati pia imependekeza uteuzi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakimu Maswi utenguliwe kutokana na kuingia makubaliano ya kutoa fedha bila ya kujiridhisha kikamilifu kuhusu uamuzi wa hukumu ya mahakama ya Kituo cha Kimataifa cha Utatuzi wa Migogoro ya Kiuwekezaji (ICSID). Iwapo mjadala huo, unaotazamiwa kuendelea leo, utaafiki hatua hizo zichukuliwe, Rais atalazimika kuunda Serikali upya kwa mara ya pili tangu alipofanya hivyo mwaka 2008 wakati wa sakata la Richmond, ambalo lilihusu umeme. Pia atakuwa akifanya mabadiliko ya mawaziri kwa mara ya tano kutokana na wasaidizi hao kujikuta kwenye kashfa Je Kikwete Raisi wa nchi ya Tanganyika atawawajibisha majambazi hawa wanao wafisidi na kuwangamiza mamillioni ya watanganyika wakilala na jaa wao wakizifisidi pesa za wananchi wavuja jasho au atawabadilisha wizara wafunike kombe mwanaharamu apate upenyu wa kupita....???
Jambazi Kuu Pinda Mr Zanzibar si Nchi.
MASULTANI WEEE MASULTANI WEEE ZANZIBAR SI NCHI WEE ZANZIBAR SI NCHI WEE
Akiwasilisha ripoti ya kamati hiyo, Makamu Mwenyekiti wa PAC, Filikunjombe alisema katika suala hilo, Pinda anahusika kwa kuwa katika Katiba Ibara ya 52(1) inaeleza kuwa waziri mkuu atakuwa na madaraka ya juu ya udhibiti, usimamiaji, utekelezaji wa siku hata siku wa kazi na shughuli za Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika. Pia ibara ya 52(2) inasema waziri mkuu atakuwa kiongozi wa shughuli za Serikali bungeni. Kutokana na ibara hizo, Filikunjombe alisema baada ya kupitia vielelezo vilivyomo kwenye ripoti ya CAG, kamati imejiridhisha pasipo shaka kwamba Waziri Mkuu alikuwa ana taarifa zote kuhusiana na mchakato mzima wa kuchotwa fedha katika Akaunti ya Escrow. “Ushahidi uliotolewa na CAG kwenye kamati unaonyesha kuwa waziri mkuu alikuwa akipata taarifa za jambo hili na kamati imesikitishwa kuona kuwa Waziri Mkuu hakuchukua hatua zozote kuzuia muamala huu usifanyike,” alisema Filikunjombe.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

Wednesday, November 26, 2014

SHEIN WEWE NI KOBE HUKUPANDA MTI UMEPANDISHWA ENDELEA TU KUBWABWAJA

2758
Raisi wa Maskani ya Kisonge nchini Zanzibar  Shein
MKUTANO WA MABALOZI WILAYA KATI
Tuesday, November 25, 2014 
RAIS wa Maskani ya Kisonge nchini Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha CCM cha Mkoloni Mweusi Tanganyika   Shein amesema kuwa Zanzibar ina Mamlaka yake kamili na yeye ndie Rais na kuwashangaa wanaodai Mamlaka ya Zanzibar hii leo. Hayo aliyasema leo katika Mkutano kati yake na viongozi wa Mashina na Maskani za CCM chama cha Mkoloni Mweusi Tanganyika za Wilaya ya Kati Unguja, Mkutano uliofanyika katika viwanja vya Hoteli ya Tamarind Uroa, Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja nchini Zanzibar. Shein aliwashangaa wanaodai Mamlaka ya nchi ya Zanzibar kwani Zanzibar inamamlaka yake kamili kwani ina nguzo zake tatu muhimu ikiwemo Mahakama Kuu ya Zanzibar, Serikali ambayo yeye ndie Rais pamoja na Baraza la Kutunga Sheria ambalo ni Baraza la Wawakilishi kwa hapa Zanzibar.(swali tunamuliza kama inamahakama yake kweni Wazanzibari wakishikwa usiku usiku na kusafirishwa kwa Masultani wako Shein huko Tanganyika...?)
Alisema kuwa zipo alama mbali mbali zinazoonesha kuwa Zanzibar ina Mamlaka yake kamili zikiwemo Bendera, Wimbo wa Taifa, na nyenginezo na kusisitiza kuwa yoyote anaejiita msomi ni lazima aheshimu taratibu za nchi yake, viongozi wake pamoja na wananchi kwa jumla.(wewe Shein mbona huheshimu wananchi wanavyotaka nchi yao ya Zanzibar iwe n mamlaka kamili....?) Aidha,  Shein alieleza kuwa Serikali ya Mamlaka Kamili Zanzibar haiji kwa sababu tayari Zanzibar ina Mamlaka yake kamili na kinachofanyika hivi sasa ni upotoshwaji tu kwa wananchi. Pamoja na hayo,. Shein alisema kuwa Katiba iliyopendekezwa ni ya Mfumo wa Serikali mbili hivyo aliwataka wapinzani wasiwapotoshe wananchi na kusisitiza kuwa maelezo yake juu ya Katiba hiyo atayasema wakati wa Kampeni ukifika ambao utakuwa ni muda wa siku 30.‘Waamuzi wa kuamua ni Wazanzibari wote”,alisema Dk. Shein. Ameeleza kuwa ametiwa moyo na mahudhurio makubwa aliyoyapata vyama wanataka kuviondosha lakini mawe, tunaijua historia ya nchi yetu kabla hutajatawaliwa hadi pale kutawaliwa na wakoloni wakiwemo Sultani wa Oman.(Na sasa wewe shein unatumaliza na Jisultani lako la kitanganyika au sio..?)
“Mapinduzi ya Januari 12, 1964 ndipo palipoanza ukombozi na ndio yalioikomboa Zanzibar na kufika hapa tulipofika hadi leo…. CCM haitokuwa tayari kuwarejesha watu walioko nje ya Zanzibar, Wazanzibari wenyewe wako macho”,alisema Dk. Shein. Makamu Mwenyekiti huyo wa CCM wa chama cha Mkoloni Mweusi Tanganyika nchini Zanzibar aliwatanabahisha WanaCCM kwa wale waliokuwa na ndoto za kuirejesha Zenj Empire ambayo ilikuwepo wakati wa ukoloni na baada ya Mapinduzi ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964 Serikali ikaunda Baraza la Manispaa liliopo hivi waondoshe ndoto zao hizo za mchana. Shein alieleza kuwa Mabalozi wana dhamana kubwa sana na kuwataka kuzingatia nafasi, Katiba na Utaratibu uliowekwa na chama chao na kuwataka wawajibu wale wote wanaokibughudhi chama hicho pamoja na  Serikali iliyopo madarakani majibu sahihihi na yenye umakini na busara. Aidha, Shein aliwataka viongozi hao kuwapitia wanachama wao pamoja na wale wasiokuwa wanaCCM, na kusisitiza kuwa kiongonzi hanuni na badala yake huwajali wanachama wote wanaomuunga mkono na wasiomuunga mkono ili kuwavutia waingie katika chama chake. (Umechelewa kibushuti)  Alisisitiza kuwa CCM inawajali sana Mabalozi wake licha ya kuwepo uchache wa nyenzo za kufanyia kazi lakini chama hicho hakiko tayari kukiachia chama chengine kuiongoza nchi.  (badala ya kujali wananchi munajali mabalozi wana maskani hivi munakili nyinyi....? )
Aidha, Shein alitumia fursa hiyo kueleza mafanikio ya Muungano huku akisisitiza kuwa kamwe Muungano huo hautovunjia na kuelezaa kuwa ataendelea kuulinda Muungano wa Serikali mbili kama alivyoahidi wakati wa Kampeni za uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010. (unajifundisha udekteta na msimamo wa serekali mbili japokuwa wananchi hautaki mulize Gaddaf wa libya huko kaburini aliko na kibri chake yuwapi...?)   Shein aliwataka wananchi kutouchezea Muuungano uliopo na wasidhanie kuwa Katiba haipo na kuwataka kuheshimu Serikali iliyopo huku akisisitiza kuwa vyama vingi vimekuwja kuimarisha demokrasi na si kuja kukashifu serikali. Sambamba na hayo,  Shein aliwataka wapinzani kutumia busara kwa serikali iliopo madarakani na kusisitiza kuwa Katiba ipo na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ipo, hivyo heshima ni lazima iwepo kwa madhumuni ya kuendeleza nchi.  (wewe mbona huna heshima ya kuwasikiliza Wazanzibari wanataka nini mbona huna heshima hiyo wewe kibushuti...? ) Aliwataka wanaCCM kuweka mazingira mazuri ya kushinda uchaguzi kama inavyoeleza Katiba ya CCM kuwa ni lazima kushinda uchaguzi kwani hakuna historia wala rekodi ya CCM kushindwa uchaguzi.  (bora nicheke hahahahahaha kisha ati unaswali wewe astahafiruh allah) 
Aliwahakaikishia WaCCM kuwa uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2015 utakuwa uchaguzi huru na wa haki pamoja na kuwa uchaguzi wa amani na salama, na kuwahakikishia wananchi kuwa kila mmoja atapata nafasi ya kumchagua kiongozi anaemtaka. Aliwataka kuwashajiiisha vijana kwenda kujiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Kupiga kura ili wawe na haki ya kupiga kura huku akiwataka wazee na wazazi kuwasomesha vijana wao ili waelewe jinsi nchi ilivyokuwa hapo kabla, ilivyo hivi sasa na itakavyokuwa hapo baadae. Kwa upande wa kilimo, Dk. Shein alisema kuwa katika awamu ya saba, ruzuku, mbegu bora, dawa, pembejeo na masuala mengine ya kilimo na kueleza kuwa Serikali imefidia kwenye kilimo na tayari yapo matrekata mapya 20 na hivi sasa Serikali ina nia ya kuingiza matrekta 50 mapya kwa ajili ya kuimarisha sekta hiyo. Alisema kuwa CCM ni chama kikubwa na sio kama vyama vyengine na ndicho kilichoikomboa Tanzania na katika ukanda mzima wa Afrika ndio miongoni mwa chama kinachoendelea kuongoza Dola hadi leo. Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM cha cha Mkoloni Mweusi Tanganyika nchini Zanzibar, Vuai Ali Vuai akimkaribisha Shein katika mkutano huo alieleza kuwa wanaCCM, viongozi na wananchi wote wa wilaya kati walitoa pongezi kwa  Shein kwa kusimamia amani na usalama wao hasa pale palipojitokeza watu wachache kutaka kuvuruga amani. ( wapi ipi lini...?)
Alieleza kuwa kumekuwa na upotoshwaji wa makusudi kutoka kwa wapinzani kuwa Katiba iliyopendelezwa inawakandamiza Wazanzibari jambo ambalo sio la kweli na kuaeleza kuwa Katiba hiyo ina maslahi kwa Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla. ( maslahi yapi basi mbona hamuyasemi wananchi tukawasikia au maslahi ya matumbo yenu na familia zenu...?) Vuai alieleza juu ya upotoshwaji unaoenezwa hivi sasa kuwa Katiba inayopendekezwa haimpi Mzanzibari hata Unaibu Spika wakati Ibara ya 150 kifungu kidogo cha nne, kinaeleza kuwa Spika na Naibu Spika watachaguliwa kutoka sehemu zote za Jamhuri ya Muungano endepo Spika atatoka sehemu moja Naibu atatoka upande mwengine wa Jamhuri ya Muunganao ambapo Katiba ya 1977 haikuonesha hayo. Aidha Naibu Katibu Mkuu huyo wa CCM Zanzibar alieleza juu ya Katiba iliyopendekezwa katika Kifungu cha Uhusiano na Uratibu wa mambo ya Muungano ambacho kinaeleza shughuli za Tume ya Usimamia na Uratibu wa mambo ya Muungano na si kama inavyopotoshwa hivi sasa. “Wao waache watoe kejeli sisi tunasonga mbele katika kuimarisha miradi ya maendeleo na kuimarisha uchumi wa nchi…. kamwe Muungano hautovunjika”,alisema Vuai.
Katika risala yao viongozi hao walieleza furaha yao walioyonayo kwa kuona na kufaidika na matunda ya  Shein katika utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi wa CCM ya mwaka 2010-2015 katika maendeleo kwenye sekta mbali mbali za afya, elimu, na miundombinu ikiwa ni pamoja na kufunguliwa kwa kituo cha afya Ghana na kupatiwa huduma bora katika kituo cha afya Mwera. Aidha, walieleza kuwa kufunguliwa skuli ya Chekechea ya Cheju, skuli ya Uzini Sekondari, Ujenzi wa barabara unaoendelea katika kijiji cha Umbuji, mradi wa barabara ya Jumbi-Koani, Jendele-Unguja Ukuu pamoja na nyumba za makaazi ya wananchi Mpapa na usambazaji wa maji katika Shehia ya Dunga Bweni. Mbali na mafanikio hayo, makubwa waliyoyaeleza viongozi hao pia, walieleza changamoto kadhaa zinazowakabili katika uendelezaji na uimarishaji wa chama hicho ambapo Makamo Mwenyekiti aliahidi kutekelezwa hatua kwa hatua kwa mashirikiano ya pamoja kati yake na viongozi pamoja na wanachama wa chama hicho. Walimuhakikishia Shein kuwa CCM itashinda kwa kishindo katika uchaguzi Mkuu ujao na kuahidi kupiga kura ya na kumuahidi kuwa wataendelea kushirikiana nae katika kutekeleza na kuleta maendeleo na kumuhakikishia kuwa CCM itaendelea kuwa imara katika Mkoa wao. Viongozi hao pia walipata fursa ya kutoa michango, mawazo pamoja na kuuliza masuala mbali mbali kwa  Shein kwa lengo la kuimarisha na kukiendeleza chama chao huku wakimpongeza kwa umahiri wa anaoonesha katika kuongoza Serikali ya Umoja wa Kitaifa sambamba na utekelezaji wa Ilani ya CCM.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

Tuesday, November 25, 2014

VIDEO-KAMATI YA MARIDHIANO SIX PART 1/5 KONGAMANO 23RD NOVEMBER BWAWANI

PART 1
PART 2
PART 3
PART 4
PART 5

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

VIDEO-CCM HEBU ANGALIENE HIZI VIDEO KISHA MUTUMBIYE ABU DHABI,DUBAI,ZANZIBAR,MASCUT NA SHARJAH NI WAPI KUNAONYESHA KUMENDELEA...???

ABU DHABI 2014
HII NDIO ABU DHABI HEBU ANGALIA ILIVYO KISHA JIULIZE CCM KILA SIKU INASEMA INALETA MAENDELEO KWA MUDA WA MIAKA 50 SASA NUSU KARNE HAMA MAJI YA KUNYWA YAMEWASHINDA KUWALETEA WANANCHI MAJI SAFI JE HAYO MAENDELEO WANAYO SEMA NI MAENDELEO YAPI......?
DUBAI 2013
HII NI DUBAI HAYA SASA CCM MAENDELEO YENU MUNAYO TUMBIA KUWA MUNALETA MAENDELEO NI YAPI NA MBONA IMECHUKUWA MIAKA 50 HATA RABO YA HII DUBAI HAMUJA IOTA JE CCM TUKIWAMBIA MAENDELEO YENU NI DOMO TUPU MTAKATA...?
CCM AHA AHA CCM TUTAWALETEA MAENDELEO CCM AHA AHA CCM 
ZANZIBAR 2014
MASCUT 2014
HII NDIO MASCUT KILA KWENYE MKUTANO WA CCM UTASIKIA WAMON WANAITAKA NCHI YETU NYIE CCM HEBU ANGALIENI WENYEWE MULIVYO IFANYA ZANZIBAR KWA MUDA WA MIAKA 50 SASA KISHA ANGALIENI HII VIDEO WAOMANA WALIVYO IFANYA OMAN KISHA MUJIULIZE NANI ANA MAENDELEO....?
SHARJAH 2014
HII NAYO NI SHARJAH HAYA CCM MPOOO MAENDELEO SIO KUSIMAMA KWENYE VIRIRI MKITUKANA WATU NA UBAGUZI LAA MAENDELEO HULETWA KWA KUJENGWA NCHI SIO DOMO TUPU KAMA TARUBETA HIVI MKISEMA MNALETA MAENDELEO HUWA MUNAMANISHA NINI HASWA NYINYI CCCM...?

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

Saturday, November 22, 2014

BADALA YA KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO YAMEBAKI MAENDELEO YA DOMO TUPU HUKU WAKISHUHULISHWA NA KUTEREMSHA BENDERA





SIMO katika wananchi wanaolaumu ubaya wa serikali ya umoja wa kitaifa (SUK). Hapana. Mimi nishatoka hapo, ninavoisema serikali, wewe msomaji ujuwe ninamlaumu Shein kama kiongozi mkuu wa Maskani ya Kisonge.
Kwa hivyo, mwanzo kabisa wa mjadala huu leo, nifahamike namtupia lawama Shein kwa sababu ni Rais wa Maskani ya Kisonge na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi aliyeapa kutumikia nchi ya Zanzibar. Na kwa sababu ninamlaumu. Shein kwa sababu ndiye kiongozi mwenye dhamana kuu ya umma kuiongoza hapa nchini Zanzibar, yenye mchanganyiko wa wananchi, na mchanganyiko wa fikra na misimamo vilevile, basi nawatoa lawamani na shutumani viongozi waliomo Baraza la Mawaziri, wanaotoka Civic United Front (CUF) Chama cha Wananchi. Viongozi wa CUF walioko ndani ya safu ya mawaziri wa Shein, nataasaf kwamba hawahusiki na ujinga mkubwa wa kiuongozi huyu Shein unaofanywa na serikali anayoiongoza.
Ni kweli Shein anaongoza SUK. Lakini kwa mambo yanayofanywa na serikali, si rahisi kuwajumuisha mawaziri aliowateua kutokea CUF. Viongozi hawa hawahusiki kwa kweli na uovu unaodhoofisha umoja wa kitaifa wa nchi ya Zanzibar. Hicho sicho walichoahidi kukitekeleza kwa umma. Waliahidi neema chini ya misingi ya uongozi ulio mwema. CUF haijapata kuahidi ujinga wala upuzii. Haijaahidi watu ukandamizaji na kuuwauwa kisiri siri. Ni CCM wanaostawisha ukandamizaji na kuuwa watu kila wanavyopata nafasi. Hili si jambo la ajabu na uongo. Hili lipo kwenye rekodi wazi. Serikali zao zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar au SMZ Wauwaji, zinaua raia, achilia mbali kuwanyima haki zao za msingi. Kuwatesa na kuwadhalilisha.
Kwa sababu hiyo basi, nataka ieleweke vizuri, Shein anaingia lawamani kwa sababu kwa muda mwingi anakaa zaidi na mawaziri wanaotokea Chama Cha Mapinduzi (CCM) cha Mkoloni Mweusi Tanganyika. CCM ndio chama atokacho yeye. Ni chama hichi kilichomteua Shein agombee urais mwaka 2010. Ni viongozi wa chama hichi waliopanga kwa namna mbalimbali na wapuuzi katika Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar – Zanzibar Electoral Commission (ZEC) – kupika matokeo ya urais na hatimaye Shein akatangazwa mshindi japokuwa yeye mwenyewe anajuwa kuwa hakushinda na watu wote wanajuwa kuwa hakushinda. Jambo hili lilikuwa likiwahangaisha Wazanzibari wengi kwamba ni kweli ndivo ilivyokuwa pale wakati umma wa wananchi wakisubiri matokeo yatangazwe kupitia hadhara iliyokutanishwa ndani ya ukumbi wa Salama wa Hoteli ya Bwawani.
Mwenyeezi Mungu ameleta kudra yake na kuwatoa hofu wananchi juu ya utata wa matokeo yale yaliyotangazwa na Tume. Amelisema hili kwa uwazi muasisi wa Mapinduzi, Muungano na CCM, mzee Hassan Nassor Moyo –  Shein “alitangazwa tuuuuuu rais.” Mzee Moyo, memba wa CCM anayeshika Kadi Na.07 ya uanachama, anasema yeye ndiye aliyeongoza ujumbe   wa kwenda kumshawishi Maalim Seif Shariff Hamad akubali matokeo ya kushindwa. Maana yake aliyetangazwa mshindi, hakushinda kweli fatheha juu ya fetheha kwa anaye jinata kuwa ni rais hali anajuwa kuwa sio rais ni kidampa tu kimewekwa. Watu wanakumbuka hali iliyotangulia utangazaji wa matokeo yale yaliyompa ushindi batil Shein. Wanakumbuka umma ulivoshtadi kwenye geti la kuingilia Bwawani. Pale viongozi wakubwa walipopeleka salamu kwa viongozi wa CUF, eti wakawatulize na kuwapa matumaini kuwa hakuna lililoharibika.
Hali ilikuwa mbaya. Ilikuwa mbaya kwa sababu wapigakura waliokusanyika Bwawani, asilimia kubwa walikuwa ni wafuasi wa CUF na wapenda mabadiliko. Walitumaini mgombea wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, atakuwa rais wao. Walikuwa wanayo sababu ya kutumaini hivo. Walizipiga kura nyingi kumuelekea yeye. Waliamini, na bado wanaamini,nawataendelea kuamini kwamba yeye ndiye rais wao. Wanamuamini Maalim Seif kuwa ndiye mwanasiasa anayewafaa kuiongoza nchi yao wanayo ipenda ya  Zanzibar. Ukweli huu unajulikana zamani. Maalim mwenyewe alichangia kuchukuliwa mwanasiasa anayeaminika. Alijichunga kiuongozi akijipambanua na viongozi asi kwa wananchi. Alijiweka kiongozi kioo cha jamii katika dhana ya uongozi mwema na mpenda nchi kweli kweli. Ni mtizamo huo aliouchukua, na kuukomaza kwa wananchi alipotoa ahadi kwamba atakuwa pamoja na Wazanzibari, tena wote wa asili ya Unguja na wote wa asili ya Pemba, akiwa ndani au nje ya serikali. Maalim Seif amekuwa akienena na ahadi hii aliyoitoa tangu miaka ya 1980 pale utawala ulipoanza kumfanyia visa asiinuke kiuongozi.
Sasa kwa kuwa wananchi wamempa imani Maalim Seif, wanamuamini kuwa ni kiongozi bora anayependa watu, anayezijali raslimali za nchi hii ya visiwa iliyozungukwa na bahari kubwa ya Hindi kwenye pande zote, kila unapokuja wakati wakaipata nafasi ya kupiga kura ya kuchagua   viongozi, wanamtilia yeye. Kwa hili, wala Wazanzibari hawapapasi kalamu. Wao wakiishika tu karatasi ya kura, kwa sababu dhahiri shahir wanajua kitu wanachokitaka, hawababaiki. Wao taratibu wanatia NDIO penye nafasi ya picha ya Maalim Seif. Wao wanashuhudisha imani yao kwake. Wanamchagua. Basi Wazanzibari walio wengi walimchagua Maalim Seif hata siku ile ya uchaguzi mkuu tarehe 31 Oktoba, 2010. Kila mtu anajua hamu ya Wazanzibari, ni mabadiliko ya uongozi wa juu wa nchi yao. Akishakaa pale kiongozi wanayempenda, watatumaini mengi ya kheri kuliko kinyume chake. Wazanzibari wanauhakika Maalim Seif akiongoza nchi, atajitahidi kuondoa shari miongoni mwao. Atajitahidi kushamirisha uongozi mwema, ambao ameuahidi kila wakati wa uchaguzi. Wanaamini atalinda haki zao na kutumia vizuri raslimali zao katika nchi yao.
Wazanzibari wanaamini Maalim Seif ataongoza nchi ya Zanzibar kwa kuzingatia sheria, imani ya dini yake na mapenzi makubwa kwa watu. Atalinda heshma zao, utu wao, ubinaadamu wao, mali zao, aila zao, matumaini yao. Katu haiwapitikii akilini mwao kuwa Maalim Seif amekuwa adui wa Wazanzibari leo. Asilan abadan. Wanamuamini angali anakumbuka fadhila za kuaminiwa. Hawezi kuwa kiongozi mpuuzi asiyejitambua. Huyo si Maalim Seif wanayemfaham. Chini ya uongozi wake Maalim Seif, hakuna mwananchi anayetarajia atakamatwa usiku wa manane nyumbani kwake na kusafirishwa nje yao ya Zanzibar akatungiwe mashitaka. Hili halitatokea kwa sababu mwenyewe anakemea hadharani ujinga huu. Akiwa yeye Rais, Maalim Seif hata mara moja hatarajiwi kuagiza serikali yake ikapambane na bendera ambazo ni vitambaa tu walivyochagua wenye asasi yao iliyosajiliwa kwa mujibu wa sheria za nchi yao ya Zanzibar. Leo nchi ya Zanzibar ipo kwenye nakama. Inayo serikali inayopambana na bendera za asasi ya UAMSHO – Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislam – ambayo ni taasisi iliyopatiwa usajili wa Sheria ya Usajili wa Vyama/Mashirika ya Hiari ya nchi ya Zanzibar.
Ni hivi: Msaidizi mkuu wa Shein anayeitwa Seif Ali Iddi, ambaye kabla ya jina lake hilo anatangulizwa kwa jina la Balozi – utafikiri ni balozi wa maana sana –kumbe dude debe tupu limo limo tu ametoa amri kwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja nchini Zanzibar, asimamie askari wa serikali waondoe bendera zote za Uamsho mkoani kwake. Kwa hivyo, baada ya amri hii, Mkuu wa Mkoa, Juma Kassim Tindwa juha jengine nalo likaanza kutimiza amri msaka tonge, amepita akataka wananchi wote wa mkoani anakoongoza, Kaskazini, waziondoe bendera za jumuiya hii ambayo kwa ukweli hasa wanaoifuata ni watu je kuna ubaya gani...? wanaoongozwa na watu wenye upeo mkubwa katika Uislam na asili zake zote hasa hapo kosa liko wapi....?? Wananchi hawakujali amri hiyo. Kwanza, hawaoni kama ni kosa kisheria mtu kuchomeka bendera ya kitu au chama anachokipenda, cha aina yoyote ile hata kama si chama cha siasa. Pili, hawaoni kama bendera tu inaweza kumkosesha mtu usingizi au amani katika nchi yao. Kwamba eti bendera ile nyeupe yenye maandishi tu ambayo si kwamba yanapinga lolote lile la serikali, imnyime raha Shein, au Makamo wake, Balozi Seif, au mawaziri wa CCM katika serikali ya Shein, au ikinyime raha chama cha mapinduzi ni jambo la jabu kabisa.
Na kama bendera tu ile ya Uamsho inaweza kuwa kero kwa CCM chama cha Mkoloni  na viongozi wake hao Wasaka Tonge kwa mpangilio huo au hata akiwa ni Katibu Mkuu wao, Abdulrahman Kinana, au Makamo wao wa huko nchini Tanganyika, Philip Mangula, au hata Mwenyekiti wao, Jakaya Mrisho Kikwete, basi Watanganyika hao wasaka tonge walio nchini Zanzibar basi wana shida kubwa na viongozi wao. Viongozi wanaokasirikia wananchi kwa sababu wamepachika bendera kwenye maeneo yao, lazima waonekane wamefilisika kisiasa. Hao ni viongozi waliochoka kufikiri. Ni viongozi muflis ambao wamejitoa katika kuwa watu wanaowaza ni vipi wataondosha shida tele zinazowakabili wananchi walioapa kuwatumikia. Ni ujinga mtupu viongozi watu wazima kuacha mambo ya maana katika kuwatumikia wananchi, wakatoa matamko na amri kwa wasaidizi wao washughulike na bendera. Hivi bendera ndiyo inayopambana na umasikini...?? Hivi bendera ndiyo inayosaidia serikali kujua kama inapendwa na wananchi wake...?? Hivi bendera ndiyo inayoizuia serikali kuhudumia wananchi kwa elimu, tiba, maji,umeme,nyumba nzuri za kuishi na tuseme kufikia malengo ya milenia..??? Siamini hata kidogo. Bendera haiwezi kuwa jambo la maana sana kwa viongozi wa serikali isipokuwa kama wameishiwa busara kwa kuwa wameshindwa kufikiria njia za kuondoa shida za wananchi basi ndio hubaki kupigana na bendera.
Viongozi hawa ambao ndio maana nikasema mwanzoni kabisa mwa mjadala huu, kwamba simo katika kuamini kuwa mawaziri waliotoka CUF wanaweza kuwa sehemu ya ushetani huu wa kupambana na bendera. Simo mimi. Ujinga huu wa kuituma dola ishughulike na bendera ni wa aina yake ambao watu wenye akili nzuri ya maendeleo ya wanadamu hawawezi kushiriki. Viongozi wa CUF waliomo katika SUK pamoja na Maalim Seif hawawezi kushiriki kuagiza upuuzi kama huo. Shein yeye anaweza. Kwanini asiweze...?? Anaweza kwa sababu anayajua yote yanayofanywa na msaidizi wake mkuu, Balozi Seif, wanayetoka pamoja CCM chama cha Mkoloni Mweusi Tanganyika, chama kinachoshika udhibiti wa uongozi wa nchi ya Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika. Anajua kwamba serikali yake ndiyo inayohusika kushughulika na bendera, kitambaa, tu cheupe.badala ya kushughulikia hospitali,madawa,barabara,maji,umeme,ajira kwa vijana,kuhimili kodi ya vyakula ili masini nao wale mara tatu na sio mlo moja au hawana kabisa nyumba nzuri za kuishi n.k. Lipo tatizo kubwa katika nchi ya Tanganyika maana sio nchi ya Zanzibar peke yake. CCM chama cha Mkoloni Mweusi Tanganyika ambayo ndiyo inaongoza dola, imechoka sana sana na wala haijuwi tena ni vipi ilete maendeleo kwa wananchi walio wengi tabani bin hoehe. Haina tena nguvu ya kuongoza bali ina nguvu ya kukandamiza rai wake kuuwa rai wake kunyanyasa rai wake na kuendele kujitajirisha wao kwa wao viongozi na kuwasahau kabisa rai wao.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

Thursday, November 20, 2014

VIONGOZI WAKIUMWA WANAENDA KUTIBIWA NJE YA NCHI RAI KUFANI KATIKA MAKABWELA MPAKA LINI..??




KWA muda mrefu sasa, baada ya kila muda mfupi, tumesikia kiongozi mmoja wa nchi ya Kiafrika baada ya mwengine, amekwenda nje ya nchi yake kuchunguzwa afya au kupata matibabu. Wengi wao, wamefia huko na wengine, kama Leopold Sedar Senghor wa Senegal baada ya kutoka madarakani waliamua kuishi Ulaya haswa na walipoiaga dunia ndipo maiti zao zikarejeshwa nchini kwao kwa mazishi. Senghor ambaye alikuwa na mabilioni ya dola katika mabenki ya Ulaya na majumba katika nchi za Ulaya aliishi Ufaransa na kufia huko. Alipoulizwa kwa nini hakubaki Senegal baada ya kustaafu kuongoza nchi hio kutoka 1960 hadi 1993, alisema hakuna mtu asiyependa maisha mazuri na Afrika bado haijaendelea. Siku hizi ni kawaida ukiona Rais au Waziri Mkuu wa nchi ya Kiafrika amefika hospitali, basi ni kuangalia mgonjwa au kwa shughuli za kiserikali na sio matibabu, kama vile hospitali hizo haziwahusu au wao ni marufuku kutibiwa hapo.
Hata viongozi waliojigamba kuwa wazalendo wakubwa na kujinata kuwa chini ya uongozi wao nchi zao zilipata maendeleo makubwa katika sekta ya afya walikimbilia nje ya nchi kwa matibabu. Wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema sababu kubwa za watu hawa kufanya hivyo ni mbili. Moja ni hofu ya usalama wao kutokana na kutoamini madaktari wazalendo na nyingine ni huduma duni znazoambatana na ukosefu wa vifaa na dawa katika hospitali hizo. Kwa maana nyengine hospitali hizo zimejengwa kwa mkabwela tu kama vituo vya afya vya daraja la chini na hazina sifa za kuitwa hospitali wala kutibu wanadamu unaweza ukasama hivyo. Ni aliyekuwa Rais wa Afrika ya Kusini, Nelson Mandela, licha ya hali yake kuwa mbaya, ndiye pekee hakupelekwa nje ya nchi na alipata matibabu Afrika ya Kusini hadi alipofariki.
Lakini wengine wamekuwa siku zote kiguu na njia kwenda nje ya nchi zao kupata matibabu na kuwaacha makabwela wategeemee huduma mbovu za matibabu ziliopo nchini kwao na kwa uhakika hakuna haswa hizo huduma ni majengoo tu yapo yapo na jina kumbwa HOSPITALI lakini sio ya kuitwa hospitali hata chembe.Hebu tuanze na Marisi kidogo Rais wa Guinea, Ahed Sekou Toure, aliyekuwa akisifu huduma za afya nchini kwake tokea kupata uhuru, alikimbizwa Marekani mwezi Machi 1984, wakati akiwa na miaka 62, kupata matibabu. Alifarikia miaka 26 baadaye, lakini wakati wote alikuwa akitibiwa Saudi Arabia, Ufaransa au Marekani. Katika mwaka 2005, baada ya kutawala kwa mkono wa chuma kwa miaka 38, Rais Gnassingbe Eyadema wa Togo, alifarki akiwa ndani ya ndege iliokuwa inampeleka nje ya nchi kwa matibabu. Zilikuwepo taarifa kuwa alikuwa ameshakata roho alipopakiwa kwenye ndege lakini akapelekwa hivyo hivyo.
Katika mwaka 2008, Rais Levy Mwanawasa wa Zambia, akiwa na miaka 59, alifariki akiwa kwenye matibabu nchini Ufaransa. Naye Rais Lansana Conté (74) wa Guinea, alifariki mwaka huo huo nchini kwake muda mfupi tu baada ya kurudi kwenye matibabu Uswisi akiwa na shehena za zawadi kwa wana familia na rafiki zake. Rais Omar Bongo wa Gabon alifariki mwaka 2009 akiwa kwenye matibabu Hispania akiwa na miaka 73. Aliitawala nchi hio yenye utajiri mkubwa wa mafuta kwa miaka 38. Alichojali zaidi ni kujijengea Ikulu za fahari na ndege za kisasa na kuhakikisha mwanawe anamrithi uongozi imekuwa mafuta ya nchi ni yake yeye na familia yake sio wananchi wote. Katika mwaka 2010, Rais Umaru Musa Yar’Adua wa Ngeria alifariki akiwa na miaka 58 nchini kwake muda mfupi baada ya kurejea kwenye matibabu yaliyochukua miezi miwili nchini Saudi Arabia.
Rais John Atta Mills wa Ghana alifariki nchini kwake akiwa na miaka 68 wiki chache baada ya kurudi kutoka Marekani alipokwenda kwa matibabu. Naye Rais Bingu wa Mutharikia wa Malawi aliiga dunia miaka miwili iliopita akiwa na miaka 78 katika jiji la Lusaka, Zambia. Kabla ya hapo alikuwepo Afrika ya Kusini kwa matibabu. Rais wa Ethiopia, Meles Zenawi, naye alifariki miaka miwili iliyopita akiwa na miaka 57 wakati akiwa Ubelgiji kwa matibabu ambapo alikuwa akienda mara kwa mara na kundi kubwa la mawaziri na wasaidizi wengine ati nakwenda matibabu huyu. Novemba 2012, Guinea Bissau ilipokea maiti ya Rais wake aliyefariki katika hospitali moja ya matajiri nchini Ufaransa. Hivi kribuni tu, Rais Michael Sata wa Zambia, alifariki akiwa London kwa matibabu. Hapo kabla alitibiwa Afrika ya Kusini na India.
Orodha ya viongozi wa nchi ya  Tanganyika na  nchi yetu ya Zanzibar, waliopo madarakani na waliostaafu, wanaokwenda nje kwa matibabu mara kwa mara ni ndefu mno. Hivi karibuni tu Rais Jakaya Kikwete wa nchi ya Tanganyika naye alikuwepo Marekani kwa matibabu ya upasuaji wa tezi dume. Naye Rais Abdelaziz Bouteflika wa Algeria hivi sasa anapata matibabu nchini Ufaransa. Bouteflika ambaye sasa ana miaka 77 alipata ugonjwa wa kiharusi mwaka jana na amekuwa akitembea kwa kutumia kigari. Vile vile anazungumza kwa tabu na mara husahau alilolisema dakika chache zilizopita lakini kingngnizi bado aupenda Uraisi na yuko nje akipatiwa matibabu. Bouteflika aliwafukuza wasaidizi wake wote waliomshauri aachie uongozi baada ya kuugua ugonjwa wa kiharusi kwa madai kuwa anao uwezo mkubwa wa kuendelea kuwatumikia wananchi wa Aligeria. Alisema wale waliomshauri apumzike hawakuwa wanaitakia mema Aligeria kwa hiyo akawapumzisha wao.
Kwa kweli hali hii iliyopo hapa chini na katika nchi zote za Kiafrika za viongozi wake kwenda nje kwa matibabu, isipokuwa Afrika ya Kusini, unaweza kusema ni ya aibu. Hii inatokana zaidi na kwamba nchi nyingi za Kiafrika zimetimiza zaidi ya nusu karne tokea kupata uhuru. Hakuna takwimu sahihi ya kiwango cha fedha ambacho viongozi wa nchi za Kiafrika hutumia kwa matibabu nje ya nchi zao, lakini ukweli ni kwamba laiti fedha hizo zingetumika kuimarisha hospitali za nchini kwao, wananchi wengi wangelifaidika na huduma bora za afya. Kinachoonekana na baadhi ya wachambuzi wa mambo ya kisiasa ni kwamba viongozi wengi wa Kiafrika wanajali zaidi afya zao na zile za familia zao na sio za wananchi kwa jumla. Katika nchi nyingi za Kiafrika hivi sasa, pamoja na nchi ya Tanganyika na nchi ya Zanzibar, tunasikia malalamiko ya upungufu mkubwa wa dawa na vifaa vya kisasa vya matibabu. Hata hizo fedha kidogo zinazotolewa kwa sekta ya afya huliwa na wajanja na sio kawaida kuona mafisadi wanaohusika kuwajibshwa kisheria.
Hapana takwimu sahihi za kila nchi inatumia kiasi gani kutibu viongozi wake nje, lakini wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema ni fedha nyingi sana na kwa kiasi fulani ziaongeza umaskini katika nchi hizi za Afrika. Kinachoonekana kupewa umuhimu na viongozi wengi wa nchi za Kiafrika ni kutumia fedha nyingi kwa ulinzi ili wakae milele madarakani au hata kama sio milele lakini akae madarakani japo kuwa rai hawamtaki na hawakumpigia kura, sherehe zisiokwisha za upozi mtupu na safari za viongozi nje ya nchi kila kukicha. Baadhi yao wanatumia muda mrefu zaidi nje ya nchi zao kama vile wafanyavyo marubani wa ndege za kimataifa. Hali hii ya kupuuza sekta ya afya inakwenda sambamba na kutojali kiwango cha elimu. Matokeo yake ni kwamba watoto wengi wa viongozi wameamuwa wawasomeshe Ulaya, India, Marekani na Canada maana wanajuwa kuwa nchini hakuna skuli ni midabwada tu. Wakati umefika kwa nchi za Kiafria, ikiwa pamoja na nchi ya Zanzibar na nchi ya Tanganyika, kufanya tathmini itakayosaidia kuimarisha sekta ya afya na hata viongozi nao wachunguzwe afya zao na watibiwe katika nchi zao hapana tena kwenda Ulaya wa India wala Marekani wa Canada kama wao hataki makabwela ni sisi pia hatuyataki.
Vinginevyo, raia wa kawaida naye kila anapohitaji kuchunguzwa afya yake au kupata matibabu naye apelekwe nje ya nchi na hospitali zetu zibakie kuwa mapambo ya miji yetu au kama majumba ya makumbosho tu. Wakati tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 moja ya ajenda inayofaa Wazanzibari na Watanganyika kuishikia bango ni vipi hao wanaogombea urais wataimarisha sekta ya afya. Vile vile watakiwe kutoa ahadi kwamba watachunguzwa afya zao na kupatiwa matibabu hapa hapa nchini. Wale wanaotaka kwenda nje kwa matibabu watumie fedha zao wenyewe kutoka katika mishahara yao au mifukoni mwao na watoto wao wote wasome hapa hapa nchini na sio pesa  za walipa kodi.
Tukiamua inawezekana.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

KADA WA CCM AELEZAYALIO MOYONI MWAKE KUHUSU CHAMA CHA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA CCM

iddi
BALOZI MDOGO WA NCHI YA TANGANYIKA TING TONG A.K.A BALETOLI AJIDANGANYA KUWA ATI YEYE NDIO ANAFAA KUWA RAISI WA NCHI YA ZANZIBAR 2015
• Kada wa CCM aeleza wazi kwamba hakuna njia ya kuwazuia wapinzani nchini Zanzibar kushinda Uchaguzi wa 2015.
• Asema CCM imekufa hapa nchini Zanzibar, haikubaliki tena na imekimbiwa na idadi ya wanachama wengi katika kipindi cha karibuni kutokana na mchakato wa katiba Mpya.
• Asema kwa hali ilivyo sasa ni wazi wazanzibari wanaiona CCM kuwa sio chama chao tena kinachotetea maslahi yao
• Agusia mpango wa Makamo wa pili wa raisi kutaka kumpikua Dr. Shein katika uchaguzi wa kumpata mgombea wa uraisi wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM 2015.
Kada mkongwe wa chama cha mapindizi ambae ni rafiki mkubwa wa makamo wa pili wa rais wa nchi ya Zanzibar ameamua kuzungumza yaliyo moyoni kuhusiana na mwenendo wa siasa za nchi ya Zanzibar zinavyokwenda na jinsi CCM ilivyojimaliza wenyewe katika kuendesha siasa zake.
Kada huyo maarufu asikitika akisema kwamba “CCM kwa sasa ipo katika wakati mgumu kisiasa kutokana na kukwepa maoni ya wazanzibari katika mchakato wa katiba, na nikwambie jambo moja kwa hali inavyokwenda achilia mbali wilaya zenye mabadiliko makubwa ya kisiasa hapa Zanzibar, CCM huenda ikapoteza viti viwili ndani ya wilaya ya Kati na Kusini katika uchaguzi mkuu ujao”
“Tumeshafanya vikao vya ndani vya chama na kujiridhisha kwamba matawi yetu yamekufa; ndio unaona sasa tunataka kuziingiza maskani zetu katika katiba ya chama ili kutambulika, vijana ambao ndio mwega wa kukiinua chama cha siasa wametukimbia, idadi ya wanachama wetu imepungua na hata wazee hawatutaki na wanatwambia kwamba hawana tena imani na sisi baada ya kuipitisha katiba iliyopendekezwa kule Dodoma” alieleza kada huyo kwa sharti la kutotajwa jina lake kutokana na ukaribu wake na viongozi wakubwa wa chama na serikali.
“Juzi moja nilikua nikizungumza na makamo wa pili, aliniambia wazi nia yake ya kutaka kugombea uraisi wa Zanzibar 2015, kwa kweli sijui amejipanga vipi....?? anasema kwamba rais Shein hatakiwi tena na CCM wa Zanzibar (Unguja) hasa kutokana na asili yake, ingawa kuna taarifa za Shamsu Vuai Nahodha na Dokta Mwiji Haji Makame kujiandaa kuwania nafasi hiyo, yeye anaamini atawapiku wote na kupitishwa kuwa mgombea wa CCM; 2015”
“Balozi pia amenambia kwamba anavyojua yeye huenda Shein asigombee kabisa uraisi 2015, suala hilo litamrahisishia yeye kushinda uchaguzi katika CCM, lakini mimi nadhani endapo atapitishwa CCM itajimaliza zaidi kwakua rafiki yangu hakubaliki kwa wana CCM na wazanzibari wengi hasa kwa siasa anazoziendesha”
Mbali na hayo kada huyo amesema pia kwamba CCM haiwezi kushinda Uchaguzi wa 2015 ikiwa wazanzibari wengi watajitokeza kupiga kura; kwakua hata makambi na vikosi ambavyo vinatayarishwa kwa ajili ya uchaguzi havitoweza kuhimili mabadiliko yaliyopo Zanzibar na Tanganyika, huko bara kuna UKAWA na huku Zanzibar CCM imekufa inachotegemea ni vyombo vya Dola kuisaidia katika uchaguzi ujao.
Kwa mwenendo wa mabadiliko ya kisiasa ya Zanzibar na hasa jinsi Chama cha Wananchi – CUF kinavyokwenda sambamba na mabadiliko hayo kitendo cha kubadilisha mgombea wa uraisi wa Zanzibar hakitowasaidia CCM badala yake kitawaangusha vibaya katika uchaguzi ujao, CUF imebadilika sana kisiasa na itawashangaza wengi 2015.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

Thursday, November 13, 2014

VIDEO-KIGALI NA MAENDELEO SHEIN NA MNARA WA MAPINDUZI


KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

MH KHATIB SAID HAJJ MBUNGE WA KONDE PEMBA AIPA DOZII BAKWATA NALO LAAZA KUPANDA MAPEPO



BAKWATA YACHAGAWA
BARAZA KUU ATII LA WAISLAMU NCHINI TANGANYIKA (BAKWATA)
Limekuwa Likimtumia MESSEGE na simu za VITISHO Mbunge wa Konde Pemba, Mh Said Hajj, Kufuatia shutma alioitowa Mbunge huyo Bungeni 11/10/2014, kwa BAKWATA na serikali kutokana na ukimya juu ya malalamiko ya udhalilishwaji wa vyombo vya dola kwa Masheikh waliotolewa nchini Zanzibar na kupelekwa nchini Tanganyika.

Atii kwa tuhuma za ugaidi

Moja ya ujumbe aliyotumiwa Mheshimiwa huyo ni huu

Tunasikitishwa Sana kwa kitendo chako ulichokifanya jana katika bunge la jamhuri ya muungano ya Tanzania
Wewe ukiwa mbunge muislam haikuwa sahihi kukisema chombo cha waislamu Bakwata kuwa ni chombo cha kinafiki na baya zaidi kuisema jumuiya hii kuwa ni moja kati ya taasisi ya za CCM kama ilivyo jumuiya ya vijana ya CCM.
Na baya zaidi wewe ukiwa ni muislam kuliomba baraza kuu la maaskofu kuwatetea masheikh eti wanaothalilishwa katika magereza ya Tanzania bara. Jambo ambalo Halina uthibitisho wowote Bali ni maneno ya mitaani uliyokubali kulishwa nawe ukayameza bila kujitambua. Sisi kama taasisi ya kiislam inayotambuliwa kisheria na serikali yetu tukufutunakulaani sana kwa kuikashifu Bakwata na tunaanda Taratibu za kisheria kupitia wanasheria wetu kuona hatua za kuchukua dhidi yako ili iwe fundisho kwako na wale wote wenye tabia za kuidhakilisha jumuiya hii ya waislamu Tanzania
Wabillahi tawfiq
Sisi vijana wa Bakwata
Kny sheikh wa mkoa wa Dsm shk Alhad Mussa Salim;
BAKWATA HAMNA INTERNETE KWENYE OFISI ZENU..??


Na Mh Khatib kwa ujasiri mkubwa akawajibu kwa kuwatumia ujumbe huu
Mukienda mahkamani mutanikuta nimeshafika nawasubiri
Nilisema bungeni kila mtu ameona na nyinyi kama taasisi inayojiamini semeni au jibuni hadharani waislamu watapima wataamua Nani mkweli au muongo Hii ya kunitumia sms kwangu nahisi ni ishara ya woga mumewatawala! Niwahakikishie tu mimi najiamini na Allah pekee Ndio tegemeo langu
Allah aalam!
DUA NA USHIRIKIANO WA WAISLAMU UNAHITAJIKA KATIKA HILI KWA NDUGU KHATIB SAID HAJJ
TAFADHALI SAMBAZA UJUMBE HUU KWA WAISLAMU WOTE

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

MANDELA,GANDI,JE WALIKUWA MAGAIDI..?? VIPI LEO UAMSHO NA WAZANZIBARI KWA UJUMLA KUTAKA MAMLAKA KAMILI YA NCHI YAO YA ZANZIBAR WAWE NI MAGAIDI.....????

pope-resigns-reax


Habari kubwa wiki hii imekuwa ni ile ya Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu kwa ufupi na kwa umaarufu zaidi UAMSHO. Viongozi wa Serikali ya nchi ya Zanzibar na wale wa Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika wamekuwa wakiitaja hadharani.
Makamo wa Rais wa nchi ya Tanganyika. Muhammed Gharib Bilali ameitaja kuwa ni hatari na kufika hata kuiweka kundi moja na Al Qaida, Al Shabab; Nae balozi mdogo wa nchi ya Tanganyika anaishi nchini Zanzibar Balozi Seif Ali Idd ametoa agizo kuwa bendera zote zipachuliwe na Rais wa Maskani ya Kisonge Ali Muhammed Shein amesema kuwa yeye hapaswi kulaumiwa kwa kuchukuliwa viongozi wa UAMSHO kushtakiwa Dar es Salaam nchini Tanganyika kwa hoja kuwa hata viongozi wa Kiafrika hupelekwa The Hague kushtakiwa. ((SHEIN UMEFYATA))
Kwa wasiojua basi UAMSHO ni jumuia halali iliyosajiliwa hapa nchini Zanzibar na mpaka leo hivi kadri ninavyojua usajili wake bado upo na kwa hivyo wallahi inanishangaza mno kauli na vitendo dhidi yake vinavyofanywa na Serikali hizi mbili ya Tanganyika na ya Zanzibar, ilhali ikibakisha uhalali wake
.
UAMSHO ilipata kusikika zaidi baada ya kujitokeza kupinga muundo wa Muungano Feki wa (Tanzania,) kiongozi wake Farid Hadi kuichana Rasimu ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba mbele ya Samuel Sitta na Samia Suluhu na pia vurugu ya wiki moja iliyotokea mwezi Oktoba, 2012.
Jumuia hiyo imehusishwa na matukio kadhaa yanayotajwa kuwa ni ya ugaidi kama vile kuchomwa sehemu za kuabudia za Wakristo, miripuko ya mabomu, mashambulizi ya tindi kali dhidi ya wageni na viongozi wa Kiislamu na kushambuliwa viogozi wa Kikristo kwa tindi kali na risasi kama yule padre aliyeuliwa.
Hadi sasa kwa upande wa nchi ya Zanzibar hakuna hata kesi moja ya UAMSHO ilowatia hatiani washitakiwa wake na kwa kiasi kikubwa kwa kweli kesi hizo zipo zipo tu Mahakamani, yaani zimedorora. Kwa kuwa bado zimo mchakatoni tunajizuia kutoa maoni yoyote ili tusikhalif sheria.
Lakini kwa miezi minne iliyopita viongozi kadhaa wa UAMSHO wamekuwa wakichukuliwa kushtakiwa kwa makosa ya ugaidi na inaelekea kwa vitendo vilivyotokea nchini Zanzibar na vile vya nchi ya Tanganyika  kwa kuunganishwa na washtakiwa wengine na wanasheria kadhaa wa nchi ya Zanzibar pamoja na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu Othman Masoud wamesema ni kinyume cha sheria.
Pia kumekuwa na madai makubwa ya utesaji yanaendelea katika sehemu wanazoshikiliwa washtakiwa hao lakini si Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar, si taasisi za haki za binaadamu na wala si ofisi za kibalozi zilizotoa katazo au kemeo la vitendo hivyo vya utesaji, ambavyo vinakiuka haki za wafungwa au watu wanaozuiliwa rasmi.
Makala hii haikusudii kuhoji nafasi ya Serikali kulinda raia wake na kuhakikisha kuwa usalama upo kwa raia, wageni na mali zao, lakini hatujizuwii wala tusizuiliwe kuhoji juu ya namna hatua hizo zinavyochukuliwa, migongano katika kauli za viongozi na pia maamuzi yanayofanywa ambayo hayana tija.
Kauli ya  Bilal kwa kweli inatisha na inatufanya wengine tuamini kuwa yeye kama kiongozi wa kitaifa ana taarifa za kutosha za kuweza kufananisha UAMSHO na makudi makubwa na sugu yajulikanayo kuwa ni ya kigaidi. Na ndipo ninapojiuliza iwapo hali imefikia hivyo ni kwa nini usajili wa UAMSHO usifutwe tukaelewa kuwa haipo tena kisheria...?? Na kama hali haipo hivyo jee huku si kuiweka nchi ya Tanganyika na nchi ya pabaya kwenye macho ya dunia.....??
Viongozi wa nchi ya Zanzibar hivi karibuni walitoa amri ya kupachua bendera za UAMSHO huko Mkoa wa Kaskazini, Unguja ambako ndiko zilikotanda na kukubalika sana. Siku chache baada ya kauli ya Balozi Seif Ali Idd ndipo Mkuu wa Mkoa Juma Kassim Tindwa akaendesha operesheni ya kuzipachua bendera za UAMSHO, tabaan kwa kutumia vyombo vya ulinzi.
Ingawa hilo si ajabu kwa nchi ya Zanzibar, baada bendera za CUF zilikuwa zikipachuliwa kwa staili hiyo hiyo, lakini mtu aweza kujiuliza uhalali wa hatua ya SMZ dhidi ya taasisi ambayo bado ina usajili halali wa kufanya kazi ikiwa ni pamoja na kueneza fikra zake na kutumia nembo na alama zake na UAMSHO ikiwa pia huko nyuma kupatiwa hata kibali cha kuwa Muangalizi wa Uchaguzi.
Kuna busara yoyote kuzipachua bendera hizo kwa nguvu....?? SMZ inadhani kuzipachua bendera hizo kutazuia kuungwa mkono UAMSHO....?? Jee kupachua bendera hizo kutazuia kazi ya kuhamasisha watu kuujuburi muundo wa Muungano ambao wanaona haona faida yoyote kwa nchi ya  Zanzibar....?? Na jee kutawafanya wananchi waichukukie na kuitosa jumuia hiyo?
Na kauli ya  Shein Raisi wa maskani ya Kisonge huko Pemba kuwa yeye asilaumiwe kwa kunyakuliwa viongozi wa UAMSHO na kushtakiwa nchi ya Tanganyika itasaidiaje katika suala hili....?? Itawasaidia kuwatoa watu kwenye mahaba ya UAMSHO na kuwakurubisha kwa Serikali...?? Itawaondosha imani yao kwa viongozi wao wa kidini...?? Itamfutia lawama  Shein hasa kwa jinsi watu wanavyosikia viongozi wao wakiteswa na kukashifiwa....??
Jee kauli na vitendo vya kuitenga UAMSHO havitakuwa na athari ya kuisukuma kwenda mafichoni na kufanya kazi chini kwa chini.....?? Bila ya kutoa maoni kuhusu mashtaka yalio mahakamani, ni imani ya watu wengi kuwa viongozi wa UAMSHO wako mashitakani zaidi kwa sababu ya misimamo yao ya kuukataa Muungano Feki, na wanaoamini hivyo huna vya kuwabadilisha.
Fikra zangu suala hili linataka umakini zaidi maana binaadamu husukumwa kuenda katika mawazo hasi kadri anavyotendewa visivyo, kukosa haki, kukosa nafasi na kukosa sauti. Bado tuna wakati wa kutafakari kwa sababu ukweli ni kuwa UAMSHO iko katika nyoyo za Wazanzibari wengi.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

Wednesday, November 12, 2014

MAANDAMANO YA KUITAKA SMZ IWARUDISHE VIONGOZI WA KIISLAMU ZANZIBAR


Ndugu Wazanzibari kwa heshima kubwa na taadhima tunapenda kutumia fursa tulionayo kikatiba kuwasilisha malalamiko yetu kwa Viongozi wa SMZ kwa njia ya Maandamano.
Maandamano hayo yatafanyika mara tu baada ya sala ya Ijumaa. Maandamano yatakuwa kwa njia ya amani na tusingelipenda kumuona mtu yeyote yule kuchukua silaha ya aina yoyote au hata bakora.
Tunatumia fursa hio ikiwa ni haki yetu kikatiba na pia tunaumwa na matendo wanayofanyiwa Binaadamu wenzetu Wazanzibar wenzetu bila ya kujali dini zao.
Ikumbukwe pia kukaa kimya ni udhaifu na nikuonesha tunaridhia hayo wanayofanyiwa na njia pekee ya kuonesha tunakerwa na hilo ni kuilazimisha serikali iwarudishe haraka Zanzibar na wawashitaki Zanzibar kama vile wanavyoshatakiwa watuhumiwa wa ugaidi waliokamatwa Arusha ambao na wao wanashtakiwa hukohuko Arusha na sio Zanzibar au Dar es salaam.
Maandamano hayo yataanzia misikitini na kuongozwa na masheikh baada ya sala ya Ijumaa na kumalizikia Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha malalamiko hayo. Maandamano hayatamilizika hadi pale ambapo viongozi husika waliobeba dhima ya kuilinda na kuwalinda Wazanzibar watakapotoa jibu ni lini Viongozi hao waliokamatwa watarudishwa Zanzibar.
Hili ni wajibu wetu sote Kwa kusimama mbele ya muonevu(dhaalimu) kadri ya uwezo wetu na kumsapoti(ALIYEONEWA) iwe kwa uhai,pesa au dua mpaka arudishiwe haki yake . Kuna malipo makubwa katika hili. Mtume(saw) amesema :”Allah humsaidia mja wake madamu tu mja (huyu) humsaidia ndugu yake muislamu”.(MUSLIM).
Pia Mtume(saw) amesema, “Muislamu ni ndugu wa muislamu mwenzake, hivyo asimuonee(asimdhulumu), wala asimkamatishe(asimkabizishe) kwa muonevu(dhaalimu).Yeyote mwenye kumtimizia (kumtatulia) mahitaji ya ndugu yake (muislamu), Allah atamtimizia (atamtatulia) mahitaji yake.
Na yeyote mwenye kumuondolea yasiyomridhisha(matatizo,ugumu,shida nk) ndugu yake (muislamu), Allah atamuondolea yasiyomridhisha(adhabu nk) siku ya kufufuliwa,na yeyote mwenye kumsitiri muislamu,Allah atamsitiri siku ya kufufuliwa.”. Hivyo tuwasaidie na ndugu zetu waislamu waliodhulumiwa kwa kuwalinda wao,haki zao na heshima zao.
Tunashauriana na Wanasheria kama kuna ulazima wa kupata kibali.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.