Saturday, March 28, 2015

BALOZI MDOGO WA NCHI YA TANGANYIKA SEIF ALI IDDI AINGIA KITOPE NA KUWADANGANYA KWA MIPIRA NA JAZI SERA ZA MIAKA YA TISINI WAPE MAJI NA SABUNI KWANZA WAFUWE NGUO ZAO.

Balozi ndogo wa nchi ya Tanganyika Seif Ali Iddi akimkabidhi Seti za Jezi na Mipira Mmoja wa Viongozi wa timu 60 zilizomo ndani ya Jimbo la Kitope hapo Kijiji cha Kipandoni Upenja Wilaya ya Kaskazini “B”.
Aliyepo kati kati yao ni Mke wa Balozi wa Balozi huyo wa nchi ya Tanganyika Seif Mama Asha Suleiman Iddi.

Baadhi ya Timu za Mitaa zilizomo ndani ya Jimbo la Kitope zilizopata vifaa vya Michezo vilivyotolewa Balozi ndogo wa nchi ya Tanganyika Seif Ali Iddi sibora ugewapa sabuni na maji safi kwanza wakafuwa nguo zao.Mambo yale yale toka miaka ya tinsini jazi,mipira,jembe,panga,shoka,kanga,vitenge kila baada ya miaka 5 wanakuja tena mchezo ule ule.... jazi,mipira,jembe,panga,shoka,kanga,vitenge na hawa watu sijuwi wataerevuka lini.

Kocha na Kepteni wa Timu ya Soka ya Kipandoni Star Jeilan Omar Jeilan akipokea mchango wa shilingi 500,000/- Balozi mdogo wa nchi ya Tanganyika Seif Ali Iddi kwa ajili ya kununulia Posi na Nyavu kwa ajili ya Kiwanja chao.

Balozi mdogo wa nchi ya Tanganyika Seif Ali Iddi leo amekabidhi vifaa vya michezo kwa makocha na viongozi wa timu hizo zinazo thaniwa atii ni  Timu 60 za Mpira wa soka zilizomo ndani ya Jimbo hilo ili kusaidia nguvu na chachu ya kuimarisha Michezo katika Jimbo la Kitope.swali kwa nini hakuwaba baada ya uchanguzi wa 2010 ulipomalizika anawapa leo....? kwa kuwa mwezi wa oktoba unakuja sio....?

Vifaa hivyo ambavyo ni seti za Jezi na Mipira vyenye Thamani atii ya shilingi Milioni Nane, Laki Nne na Hamsini Elfu { 8,450,000/- }  vimekabidhiwa kwa timu hizo hapo Kipandoni Wadi ya Upenja Wilaya ya Kaskazini “B”. na Balozi huyo mdogo wa nchi ya Tanganyika Seif Ali Iddi.

Balozi mdogo wa nchi ya Tanganyika Seif akiambatana na Mkewe Mama Asha Suleiman Iddi pamoja na baadhi ya Viongozi wa Wadi ya Upenja na Jimbo la Kitope akikabidhi Seti za Jezi na Mipira kwa Timu za Jimbo hilo zinazoshiriki Ligi ya Kanda ya Unguja,Daraja la Pili na daraja la Tatu.

Na pia akakabidhi mipira kwa 36 ya Mitaani pamoja na timu mbili za watoto wadogo wa  Kijiji cha Kipandoni na kuahidi kuonyesha nia ya kusaidia kuwatengenezea Kiwanja watakachokichaguwa ili kiwe na hadhi ya michezo ya Kitaifa  ndani ya Wilaya ya Kaskazini “B”.

Akizungumza na Wanamichezo hao Balozi huyo wa nchi ya Tanganyika Seif Ali Iddi  aliwataka Vijana hao kujiepusha na makundi ya baadhi ya watu wanaojaribu kuwashawishi wajiingize katika mambo yaliyo nje ya Sekta ya Michezo.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO

No comments:

Post a Comment