Sunday, June 7, 2015

VIDEO-MTOTO WA BABA WA TAIFA WA NCHI YA TANGANYIKA AGOMBEA URAISI ASEMA VIBAKA WATURUDISHIE CCM YETU VIBAKA RUDISHENI NCHI YETU


Mbio za kusaka urais kwa makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimezidi kushika kasi baada ya mtoto wa tano wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere, Charles Makongoro Nyerere kujitosa kwenye kinyang’anyiro hicho.
Makongoro
MZEE WASIRA YUPO MZEE WASIRA YUPO MZEE WASIRA YUPO
MAKONGORO NYERERE AWARIPUWA WALA RUSHWA
KATIKA CHAMA CHAKE CHA CCM
Akitangaza nia yake katika eneo la Mwitongo kijijini Butiama jana, Makongoro aliwashambulia makada wenzake ndani ya CCM ambao wanaongoza makundi ya kuwania urais kwa kuwaita ni ‘vibaka’ wanaokivuruga chama hicho kwa maslahi yao binafsiAkitoa mfano kwa baadhi ya makada wanaoongoza makundi ndani ya chama hicho, Makongoro aliwataja kwa majina kuwa ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda Mr Zanzibar si nchi, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Naibu Waziri wa Fedha,Mwigulu Nchemba na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Steven Wasira. Alisema makada hao kwa muda mrefu wamekuwa wakitumia fedha nyingi kuendesha makundi ya urais na akahoji sababu za kutafuta cheo hicho cha juu kwa fedha.
"CCM irudishwe kwa wazalendo kwa sababu vibaka wamekuwa na mlengo mbaya wa kukiendeleza chama hicho," alisema.
Alisema ndani ya chama hicho kumekuwa maradhi ya rushwa ambayo yameiambukiza nchi nzima. Makongoro alisema yeye ni mzalendo wa kweli na anataka kuirudisha nchi katika misingi ya uadilifu endapo CCM itampa ridhaa ya kupeperusha bendera katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.Alisema ndani ya chama hicho kumeibuka genge la watu wachache ambao utajiri wao ni wa shaka na umejijenga kwa fedha chafu.
“Ndani ya chama tawala wamekuwapo ‘vibaka’ wachache… unajua kibaka ni kibaka tu hata kama kapewa gari la Serikali lina bendera ya taifa mbele atabaki kuwa kibaka tu.
“Wananijua vizuri huwa siwaonei haya kuwaambia ukweli, hawa ndiyo wanaotuvurugia chama na hawamheshimu Mwenyekiti wa chama, Rais Jakaya Kikwete,” alisema Makongoro.
Katika hotuba yake ambayo alitumia saa mbili, Makongoro alijikita kuzungumzia madhara yanayotokana na rushwa ndani ya CCM. Alisema baadhi ya makada wanaotumia rushwa wamezalisha makundi na mipasuko isiyo ya lazima huku akisisitiza kuwa anachukia kuwapo makundi ndani ya chama hicho. Kwa mujibu wa Makongoro, hali hiyo imechochea badhi ya viongozi wa CCM katika ngazi mbalimbali wakiwamo wenyeviti wa mikoa na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho kuishi kama mifugo. Alisema hali hiyo imesababisha baadhi ya viongozi hao kuishi maisha ya kusukumwa kwa upepo wa makundi yanayomilikiwa na watoa fedha.
“Vibaka waturudishie CCM yetu, watambue wao ni wachache na sisi wazalendo ni wengi, hawatushindi na fedha zao na kitaeleweka tu.
“Leo hii viongozi wetu wa CCM wamekuwa ni watu wa kuendeshwa na vibaka hawa wanahongwa fedha ovyo…wao wana mifugo yao ndani ya NEC basi mimi sijafuga hata kuku, nasema kitaeleweka tu,” alisema Makongoro.
Alisema yeye hawezi kufanya hivyo kwa sababu rasimu ya ilani ya chama hicho bado haijapitishwa na chama, hofu yake ni kwamba anaweza kutoa ahadi na zikawa kinyuume na ilani ya chama chake.
“Nimewasikia wanajinadi,nawashangaa sana, najiuliza kwani wao ni akina nani watoe ahadi kabla ya ilani ya chama...?? Ikitokea ahadi yako ikaenda kinyume na ilani si ndiyo mwanzo wa kuwa na rais muongo…sitaki kuwa rais muongo nitaheshimu chama changu kwa kila mchakato na maelekezo,” alisema Makongoro.
Aliwaasa Watanganyika wawaogope watu wanaoonekana kuwa na haraka ya kukimbilia kutawala nchi.
  
“Ukiona watu kazi inatangazwa ifanywe kwa utaratibu wake na mtu aliyeiomba kazi hiyo anakiuka taratibu, muogopeni sana huyo hafai kukukuongoza maana hata akikuongoza ataendelea kukiuka taratibu ili ajinufaishe,” alisema Makongoro.
Makongoro alisema anakerwa na siasa chafu dhidi yake zinazoenezwa na baadhi ya wanasiasa wenzake ndani ya CCM. Alizitaja siasa hizo kuwa ni tuhuma za kulaaniwa na baba yake, ulevi na mtu anayependa wanawake.
Akijibu tuhuma hizo, Makongoro alihoji umati uliomiminika kumsikiliza kwamba, “jamani naonekana nimelaaniwa..? Naelekea kuokota makopo...? Jamani mnanionaje, naonekana mlevi....? na umati ulikataa kwa kusema, “hapana hapana”.
“Eti wanasema Makongoro anapenda wanawake sasa wanataka nipende wanaume...? Wanawake wananipenda na mimi nawapenda, hizi siasa chafu wanazonituhumu hazinisumbui langu ni moja tu vibaka rudisheni nchi yetu,” alisema. 

Naye Mbunge wa Musoma Vijijini , Nimrode Mkono alisema atakuwa bega kwa bega na Makongoro kuanzia sasa katika safari yake ya kuwania urais mpaka hatua ya mwisho.
“Wapo wengi walionifuata niwe nao katika harakati zao za kuwania urais, sasa nawaambia ‘bye bye’ nipo na Makongoro na wasijihangaishe kunitafuta,” alisema Mkono.

Mbunge wa Bunge la Afrika Mashari, Shyrose Banji na mwanamuziki wa kizazi kipya, Judith Wambura ‘Lady J Dee’ nao walihudhuria kikao hicho. Awali kabla ya Makongoro kutangaza nia ya kugombea urais,baadhi ya viongozi wa dini walimuombea ambako Mchungaji wa Kanisa la Anglikana, Jackob Ngagani alimfananisha na Daudi. Alisema anaamini Mungu atamuongoza Makongoro kushinda ushindani wa kupata mgombea urais kupitia CCM. Kabla ya dua ya viongozi wa dini, wazee wa kabila la Wazanaki, walimvisha vazi la asili la kabila hilo na kumkabidhi fimbo kwa ajili ya kuwaongoza Watanganyika.
Naye Chifu wa Kabila la Wazanaki, Japhet Wanzagi alisema Makongoro ni simba na kusisitiza kuwa kabila lao huwa halibahatishi.

KILA MZANZIBARI ATAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO

No comments:

Post a Comment