Sunday, May 22, 2016

TAARIFA ZIMEVUJA KWAMBA WANASIASA WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM WALIO FILISIKA KISIASA WANATAJWA KUSHINIKIZA JESHI LA POLISI KUMKAMATA MAALIM SEIF SHARIFF HAMAD



UNGUJA NGANGARI

PEMBA NGANGARI
TAARIFA zimevuja kwamba, wanasiasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanatajwa kushinikiza Jeshi la Polisi kumkamata Maalim Seif Sharif Hamad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF),
Jumapili, Mei 22, 2016
Si Maalim Seif pekee, viongozi wengine wa chama hicho wanaoundiwa mkakati wa kukamatwa ni pamoja na Mansour Yussuf Himid na Mohamed Ahmed Sultan (Eddy Riyami), kwa sababu za kisiasa. Taarifa hizi zinathibitishwa na Nassor Ahmed Mazrui, Naibu Katibu Mkuu wa CUF-Zanzibar ambaye amesema: “Tunazo taarifa kwamba kuna wanasiasa wameliagiza Jeshi la Polisi kuandaa mashtaka kwa ajili ya kumshitaki Maalim Seif kwamba alipokuwa Pemba alifanya maandamano bila ya kibali wakati hakukuwa na maandamano yoyote.” Mazrui amesema hayo leo wakati wa Uzinduzi wa Taarifa ya Uvunjwaji wa Haki za Binadamu Zanzibar kwa mwaka 2015/2016. Hafla hiyo ilifanyika mjini Dar es Salaam. Mazrui amesema: “Viongozi hao wamepangiwa kukamatwa na kuletwa katika magereza ya Tanzania Bara kwa lengo la kuwanyamazisha Wazanzibar ili wasipaze sauti zao kupinga utawala wa kidikteta uliowekwa madarakani kwa nguvu za dola kinyume na matakwa ya kidemokrasia ya wananchi wa Zanzibar.”
Akizungumzia uzinduzi wa Taarifa ya Uvunjwaji wa Haki za Binadamu Zanzibar 2015/2016 amesema, CUF inajiandaa kuchukua hatua kutokana na uharibifu uliofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar/CCM visiwani humo. Mazrui akimwakilisha Maalim Seif kwenye uzinduzi wa ripoti hiyo amesema, nakala ya ripoti hiyo pia watamkabidhi Rais John Magufuli kwa lengo la kujua kilichofanyika na kinachofanyika Zanzibar: “Baada ya hatua ya leo ya uzinduzi wa taarifa hii, CUF kimejiandaa kuchukua hatua ikiwemo ya kumuandikia rasmi Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli na kumkabidhi nakala ya taarifa hii ili ajue kinachofanyika nchini na hasa akiwa Amiri Jeshi Mkuu,” amesema Mazrui. Hatua nyingine zitakazochukuliwa na CUF ni pamoja na kuiwasilisha taarifa hiyo pamoja na vielelezo vyote katika Jumuiya, Taasisi na Mashirika ya Kimataifa yanayotetea haki za binadamu ulimwenguni ili kuchukua hatua zao. “Pia tutaiwasilisha taarifa pamoja na vielelezo vyote katika Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora hapa nchini ambayo hata katika mkutano wa Geneva, ilitambuliwa uwepo wake,” amesema Mazrui na kuongeza.
“Na katika Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar (ZLSC) pamoja na taasisi nyingine zinazoshughulikia masuala ya haki za binadamu hapa nchini.” Mazrui amesema: “Hatua nyingine itakayofuata ni kufungua kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania dhidi ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) kuhusiana na matendo yanayohusisha Jeshi la Polisi visiwani Zanzibar. Hatua nyingine itakayochukuliwa na CUF ni kukamilisha taratibu zitakazoiwezesha Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) kuanzisha uchunguzi dhidi ya watu wenye dhamana mbalimbali ambao wamehusika kuchochea, kutoa au kusimamia maagizo yaliyoepelekea makosa dhidi ya binadamu na makosa yaliyoilenga jamii ya watu fulani.
KISHA NYINYI MUNAYAITA MAPINDUZI MATUKUFU HIVI KWELI NYINYI MUNAJUWA UTUKUFU NI NINI AU DUNIA IMEWAVA KISAWA SAWA MPAKA MNAKUFURU MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA KATUPINDUWA TENA WAZANZIBARI NA KUWEKA VIONGOZI WAWATAKAO WAO WAKINA BT TUNAENDELEA TENA KUKA CHINI YA SERIKALI YA KIKOLONI YA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA MPAKA MIAKA MITANO IMALIZIKE KISHA TUTIWE TENA KATIKA SHENGESHA LA UCHAGUZI NA KUPIGA KURA KISHA WAZANZIBARI WAPIGE KURA NA KUCHAGUWA VIONGOZI WAWATAKAO MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA ATAKUJA NA STYLE MPYA YA KUZIPIGA KURA ZA WAZANZIBARI CHINI NA KUTUEKEA VIONGOZI WAWATAKAO KISHA TUTAKA TENA CHINI NA KUSUBIRI UCHAGUZI WA 2025 MAMBO YATAKUWA HIVYO HIVYO KISHA TUTAKA CHINA NA KUSUBIRI UCHAGU WA WA 2030 TUKIWA HAI KAMA HATUKO TENA WATAKAO BAKI WATAFANYIWA TENA HIVYO HIVYO NA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA KISHA WATAKA CHINI WASUBIRI......>>> MPAKA KIYAMA KISIMAME BASI NI BORA TU TUKUBALI KUWA NDIO TUMEKUBALI KUWA CHINI YA MKONI MWEUSI TANGANYIKA KULIKO UPUMBAVU HUU WA UCHAGUZI AMBAO KILA MOJA WETU HAPA ZANZIBAR KAMA UCHAGUZI WA MARA HII HAUJAWASOMESHA WALA HATUTA SOMA TENA MILELE. 

KILA MZANZIBARI ALIYE IPIGIA KURA CCM AU MPAKA WAKATI HUU BADO ANAISAPOTI CCM ILI IBAKI MADARAKANI JAPO KUWA CCM IMESHINDWA UCHAGUZI AJUWE NA YEYE ANACHANGIA KUENDELEZA DHULMA NA KUFUNGWA KWA MASHEIKH NA KUTHALILISHWA KWAO NA KUENDELEZA DHULMA KATIKA NCHI YA ZANZIBAR UKAE UKIJUWA UTAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA,KUDHULUMIWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

No comments:

Post a Comment