Monday, February 27, 2017

WAISLAMU NI WENGI SANA NCHINI TANGANYIKA LAKINI NI NINI KINACHO WASUMBUWA WASIENDELE MBELE NA KUENDELEA KUWA NYUMA NA KUTESEKA KIMAISHA....??

Afbeeldingsresultaat voor wazee wa uhuru wa tanganyika
Ndugu waislaam popote mulipo
ASALAAM ALEIKUM
Tanganyika ni nchi yenye waislaam wengi . Idadi ya waislaam waliopo Tanganyika ni zaidi ya M 30 ambao ni sawa na asilimia 66%. Kabla ya Uhuru wazee wa kiislaam ndio walioasisi chama cha TAA kupigania UHURU na UKOMBOZI dhidi ya wakoloni na mabeberu kutoka nchi za ulaya. Baadaye chama hicho cha kizalendo kikapata wafuasi na kutanuka . Na kupata umaarufu na kuzaliwa kwa TANU 1954 ambacho ni mwana wa TAA .
Harakati za kujikomboa zilianzia misikitini na mabarazani ktk mitaa ya uswahilini .Ujiji Kigoma, Tanga, Iringa, Lindi , Morogoro na Dar es Salaam.
Wazee wakiislaam wakamchagua Mwalimu Nyerere kuwa msemaji wao ktk kuiwakilisha nchi ya Tanganyika huko Uingereza. Na baada ya kupatikana uhuru ..1961 Mwalimu Nyerere akawa ndiye Waziri Mkuu wa kwanza wa Kiafrica kuitawala nchi ya Tanganyika.
Nyerere hakupendelea kuunda baraza la mawaziri lenye kuvaa kanzu na vibarakashia. Ingawa aliwachagua wachache wasomi akawa nao hadi 1964 ulipofanyika Muungano wa kuziunganisha Visiwa vya Zanzibar na Tanganyika.
Hapo ndipo kukawepo na balance ya uongozi . Kwani mawaziri wote kutoka Zbar waliounda serikali ya Muungano walikuwa waislaam. Na Makamo wa Rais wakati huo alikuwa Hayati Mzee Abedi Karume.
Hata hivyo, Nyerere alianza kuunda mikakati yake mapema ya kuwapunguza mawaziri wenye majina ya kiislaam na kubadilisha Muundo wa serikali kwa kutumia Mfumo ulioitwa " Azimio la Arusha" Ni ktk mwaka huo huo 1967 Viwanda na Majengo ya watu binafsi pamoja na shule na taasisi mbalimbali za kidini zikataifishwa..kwa maana nyengine serikali iliwadhulumu wananchi haki zao za umiki wa majengo , ardhi , viwanda na shule .
Pamoja na hali hiyo, Mwalimu Nyerere kwa chini chini alianza kuwadhibiti WAISLAAM ...ktk nafasi za masomo ndani na nje, nafasi za juu za serikali ...alihakikisha anateua aidha MKATOLIKI au MKRISTO wanaofana kiitikadi. Hali kadhalika alifanikiwa kuvunja chombo kikubwa cha waislaam kilichowaunganisha waislaam wa Africa Mashariki ( Jumuiya ya waislaam ya Africa Mashariki ) . Ili kuwababaisha waislaam aliwaundia chombo ambacho kinakuwa chini ya udhibiti na uangalizi wa serikali
Image may contain: 1 person
 = BAKWATA.
Nyerere ndie Mtawala wa kwanza kuleta MFUMO KRISTO nchini Tanzania. Mbegu hiyo iliimarika na kustawi baada ya chama kushika hatamu na kuunganishwa kwa vyama viwili vya kisiasa TANU na ASP na kuzaliwa CCM ..hiyo ilikuwa ktk miaka 1977.
Chini ya MFUMO KRISTO waislaam walijikuta wakidhulumiwa haki zao na kukoseshwa nafasi za masomo ya juu kwa makusudi , hatimaye uteuzi wa wakuu wa serikali pamoja na mashirika ya umma ulikuwa ukifanywa kwa upendeleo mkubwa. 
Image may contain: 1 person
Hata hivyo sababu kubwa ya kuwepo hali hii nchini Tanzania ni kutokana na UNAFIKI wa baadhi ya Masheikh wa Kiislaam ambao wapo tayari kuuza imani zao kwa thamani ndogo kbs za kidunia. Wapo Masheikh ambao wanatumiwa na viongozi wa juu kwa maslahi ya serikali na chama. Masheikh wa aina hii huwa hawafatilizii shida na kero wanazopata waumini wa kiislaam bali wao huwa ndio nyundo ya kuwakandamiza waislaam . 
Image may contain: 1 person
Kazi zao kubwa ni kuwapigia debe viongozi wakuu wa chama na wale wa serikali kwa ajili ya kipato kidogo tu cha dunia.
Bila shaka Maskheikh wa aina hii ndio wale waliotabiriwa ndani ya Quraan kama ilivyokuja ktk surat Nissaa Aya 146 " HAKIKA WANAFIKI YATAKUWA MAKAZI YAO CHINI KABISA NA MOTO WA JAHANNAM "
Na wapo miongoni mwao ambao huyavaa mavazi ya kiislaam na kuonekana ndani ya jamii kwamba ni Masheikh kumbe ni watu walioajiriwa USALAMA wa TAIFA .