Sunday, December 15, 2019

VIDEO-MAALIM SEIF AIAGA PEMBA NA KURUDI UNGUJA

MAALIM SEIF AIAGA PEMBA NA KAULI BIU 
ALIYO KUJA NAYO NI SASA BASIIII
MTAZAMO WA MWANASHERIA KUHUSU
ZIARA YA MAALIM SEIF.

VIDEO-MASAUNI URAISI WA NCHI YA ZANZIBAR UTAUSIKIA TU KATIKA MABOMBA

JIMBO LAKO LA KIKWAJUNI UMELILETEA MAENDELEO
GANI MPUMBAVU WEWE USIE JIJUWA UNAROPOKA
KAMA ULIYE SHIBA TONGWA
ATI HUYU NAE ANATAKA KUWA RAISI WA 
NCHI YA ZANZIBAR 2020 DAH!

Saturday, December 14, 2019

VIDEO-MKUU WA MKOA WA KUSINI PEMBA ANAMPANGO WA KUVUNJA AMANI PEMBA

ACT WAZALENDO PEMBA

VIDEO ZOTE ZA MAALIM SEIF KUIONYA CCM NA KUWAMBIA WAZANZIBARI KUONEWA SASA BASIIIIII

TUSHAONEWA SANA SASA BASIIIIIIIIII
VIJANA PEMBA WAITOWA FYUZI MITAMBO YA BASHIRU
MAALIM SEIF AWAMBIA CCM MSIMAMO NI ULE ULE HAKUNA
TENA KUONEWA SASA BASIIIIIIIIIIIIIIII
MAALIM SEIF AWAONYA BASHIRU NA SHEIN

VIDEO-NCHI YA TANGANYIKA NA ZANZIBAR HAKUNA MUUNGANO BALI NI KULAZIMISHANA NA TANGANYIKA KUTAKA KUITAWALA ZANZIBAR KWA GUVU ZA JESHI

NYERERE ALIMTISHA MZEE KARUME ILI AKUBALI
MUUNGANO FEKI AMBAO NIA YAKE NI KUIMEZA NCHI
YA ZANZIBAR KAMA WALIVYO KIMEZA CHAMA CHA ASP
KATIBA LAO HATULITAKI TUNAKATIKA YETU NCHI YA ZANZIBAR
WANATULETEA UBAGUZI KWA MAKUSUDI ILI WATUTAWALE MILELE
WAKOLONI WEUSI HAWA TANGANYIKA

VIDEO-WANANCHI WA PEMBA BADO WAMUUNGA MKONO MAALIM SEIF ILA MARA HII HAWATAKI TENA SUBIRINI WALA NGOJENI.

WANANCHI WA PEMBA WAMUULIZA MAALIM SEIF 
LILE JAMBO LETU VIPI....
WANANCHI WA PEMBA WAHAMASIKA WATAKA MAALIM SEIF
KAMA HAWEZI AKAE PEMBANI VIJANA WAFANYE KAZI

VIDEO-MAALIM SEIF AENDELEA KUWAELEMISHA WAZANZIBARI JINSI YA KUPATA HAKI YAO BILA YA WOGA SASA BASI.


MAALIM SEIF AMUWEKA SAWA MASAUNI
UROHO WA MADARAKA WA MASAUNI WAMPAGAWISHA NA KUJIFANYA
RAISI BANDIA NA KUWAFUKUZA KAZI RPC WAWILI NA MOJA KUMPUNGUZA 
CHEO UMEISHIWA MASAUNI

Wednesday, July 24, 2019

MUUNGANO ULIKUWA NI WA NYERERE NA KARUME SASA NI WA SHEIN NA MAGUVULI SIO WANANCHI

Afbeeldingsresultaat voor shein na magufuliDawa pekee ya kumaliza Kero za Muungano, Wananchi wa sehemu zote mbili Tanganyika na Zanzibar, waulizwe swali moja tu kuwa: Je, wanautaka au la.
Taifa lolote duniani linafanikiwa kutokana na raia wake kuishi kwa furaha, kusikilizwa matakwa yao, siyo kuongoza kwa kulazimisha kwa mabavu na vitisho.
Miaka 55 ya Muungano ni muda mwafaka wa kuwasikiliza wananchi kuhusu Muungano, kama wanauhitaji au laa. Muungano ni hoja ya wananchi. Viongozi wanapaswa kuacha kiburi na hofu.
Picha na maelezo yalipo juu ni sehemu ya maoni kulingana na habari iliyopo chini kuhusu Kero za Muungano, amabzo sasa ni kidondandugu kisichopoa.
Imetimia miaka 55 tangu Tanganyika na Zanzibar zilipoungana, lakini muungano huo bado umekuwa na kero nyingi zinazoibua mijadala mara kwa mara.
Tangu Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Amani Karume walipounganisha nchi hizi bado kulikuwa na masuala mengi yaliyohitaji ufafanuzi au kuwekwa sawa, lakini fursa hiyo haikupatikana, wala hata mijadala ya wananchi kuhusu jambo hilo haikuruhusiwa.
Ili kuthibitisha kuwepo kwa nyufa katika muungano huo, Tume kadhaa zilizoundwa na serikali ilionyesha kasoro kwenye muundo wa muungano wenye Serikali mbili. (Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar)
Tume ya Jaji Francis Nyalali iliyoundwa kuwahoji wananchi kuhusu mfumo wa vyama vingi, katika mapendekezo yake iligusia suala la muungano ikijenga hoja kwamba muundo wa serikali mbili hautekelezeki kwa mfumo wa vyama vingi.
Ilitaja masuala ya uraia, milki ya fedha za kigeni, ukusanyaji na mgawanyo wa mapato kutokana na kodi na ushuru wa forodha, tatizo la kanuni ya kuchangia gharama za uendeshaji Serikali ya Muungano.
Hata hivyo, mapendekezo ya Tume ya Jaji Nyalali hayakufanyiwa kazi.
Mbali na Tume ya Nyalali, mwaka 1998, Rais wa awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa aliunde tume iliyoongozwa na Jaji Robert Kisanga, ikapeleka kwa wananchi waraka wa serikali, maarufu ‘Whitepaper’, kama ilivyokuwa kwa Tume ya Nyalali, tume hii nayo ikarudia yaleyale kuwa muundo wa serikali mbili haufai.
Ripoti ya Jaji Kisanga ilitaja kasoro za muungano zilizobaki hazirekebishiki. Maana yake ni kwamba kunahitajika mfumo wa muundo wenye kukidhi mahitaji ya sasa na ya baadaye utakaokuwa tiba ya matatizo mbalimbali. Vilevile mapendekezo hayo hayakufanyiwa kazi.
Mbali na tume hizo mbili, Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba iliibua suala la muungano kwa kupendekeza Serikali ya Shrikisho la Serikali tatu, yaani ya Shirikisho, ya Tanzania Bara na Zanzibar, huku mambo ya muungano yakipunguzwa kutoka 22 hadi kubaki saba.
Sura ya kwanza ya Rasimu ya Katiba mpya iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba inasema:
“1(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi na Shirikisho lenye mamlaka kamili ambalo limetokana na muungano wa nchi mbili za Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ambazo kabla ya Hati ya Makubaliano ya Muungano ya mwaka 1964, zilikuwa nchi huru. Inaendelea,
“(2) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Shirikisho la kidemokrasia linalofuata mfumo wa vyama vingi vya siasa, usawa wa binadamu, kujitegemea, utawala wa sheria, kuheshimu haki za binadamu na lisilofungamana na dini.”
“(3) Hati ya Makubaliano ya Muungano iliyorejewa katika ibara ndogo ya (1), ndio msingi mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba hii, kwa kadri itakavyorekebishwa, itakuwa ni mwendelezo wa makubaliano hayo.”
Mvutano wa muundo wa muungano haupo kwenye muundo pekee, bali pia kero zake. Hayo ni mambo ambayo yamekuwa yakileta mijadala mikali hata bungeni.
Hivi karibuni tu mjadala huo umeibuka tena bungeni ambapo, Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea alitoa hoja bungeni akihoji lini serikali itabadilisha katiba ili kutoa ufumbuzi wa kudumu.
“Hii ni moja ya kero za muda mrefu za muungano. Sasa ninavyotaka, waseme lini huo mchakato wa kubadilisha katiba, lakini waziri anasema tutaleta, tuko kwenye majadiliano kwenye Baraza la Mawaziri,” alisema Kubenea.
Hoja ya Kubenea iliungwa mkono na Mbunge wa Moshi Vijijini, Anthony Komu akisema wakati Muungano ukitimiza miaka 55 serikali imeshindwa pamoja na mambo mengine kuiruhusu Zanzibar kukopa kwenye vyombo vya kimataifa ili kutekeleza masuala ya msingi kama kufanya upanuzi wa uwanja wa ndege na bandari.
Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe alifafanua kuhusu suala hilo akisema serikali haitekelezi ahadi zake kuhusu muungano na hivyo kuifanya isiaminike.
“Mwaka 1977, katiba ibara ya 134 ilianzisha Tume ya pamoja ya fedha. Ilichukua mpaka mwaka 1996 Serikali ya CCM kuandaa muswada wa tume hiyo ya fedha.
“Ilichukua tena muda mpaka mwaka 2013 Serikali ya CCM kuleta kanuni ya kutekeleza hiyo sheria. Mpaka sasa tume haijaanza kazi,” anasema Zitto.
Amedai kuwa uchambuzi uliofanywa na Tume ya pamoja ya Fedha, inaonyesha mapato ya muungano yanayopaswa kugawanywa kwa pande zote mbili za Muungano yanatumiwa na Tanzania Bara, Zanzibar haipati chochote.
Hata hivyo, Mbunge wa Uyui (CCM), Almasi Maige anapinga hoja hiyo akisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar haijazuiliwa kukopa bali hutoa tu taarifa kwa Serikali ya Muungano.
Kwa nini?
Miongoni mwa waliokuwa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Awadhi Said anasema sababu ya mvutano huo kuendelea kuwepo licha ya tume zote kubainisha kasoro za Muungano, ni hofu ya CCM kushindwa uchaguzi.
“Ni matokeo ya hofu ya CCM, kwa sababu wanataka kutawala serikali zote. Wanahofu ya kushindwa uchaguzi Zanzibar,” anasema Awadhi.
Anaongeza kuwa hofu hiyo ndiyo ilisababisha ikaundwa kamati ya Jaji Mark Bomani, mwaka 1994 ambayo ilibadili muundo wa vyeo vya Muungano ambapo Rais wa Zanzibar aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais akabadilishwa na kuwekwa cheo cha mgombea mwenza ambaye huwa Makamu wa Rais, huku Rais wa Zanzibar akibaki huru.
“Waliona ingekuwaje endapo Rais wa Zanzibar atakuwa wa upinzani? Wamechukua mfumo wa Marekani wa mgombea mwenza,” anasema Awadh.
Hata hivyo, alisema Rais wa Zanzibar amefanywa kuwa mjumbe wa Baraza la Mawaziri la Muungano. Lakini bado wanadhibiti uchaguzi wa Zanzibar, kwa sababu akishinda mpinzani atalazimika kuingia kwenye Baraza la Mawaziri jambo ambalo kwao ni tatizo.
“Muungano una matatizo mengi, lakini yanafichwa kwa kuhakikisha upande huu anatawala mkubwa na mwingine unatawaliwa na mdogo,” anasema Awadh.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba, Hebron Mwakagenda anasema suluhisho la kero za Muungano ni wananchi kudai katiba mpya.
“Suluhisho ni wananchi kudai katiba mpya. Kwa sababu katiba ni ya wananchi wenyewe. Hata Rais mstaafu Jakaya Kikwete kuruhusu mchakato wa katiba ilitokana na msukumo wa wananchi na hata katiba ya sasa inasema serikali inapata mamlaka kutoka kwa wananchi,” anasema Mwakagenda.
Ameendelea kusisitiza umuhimu wananchi kudai katiba akisema viongozi wamekuwa na tabia ya kuweka katiba zinazolinda masilahi yao na si ya wananchi kwa jumla.
“Sisi wananchi ndiyo tunataka katiba mpya. Katiba siyo ya kiongozi, kwa hiyo tuendelee kudai mpaka ipatikane,” anasema Mwakagenda.

SALALAA MAPINDUZI YA 1964 YA ZANZIBAR YAMEUWA MPAKA MAPISHI NA BIASHARA ZA HAPA NA PALE

Gerelateerde afbeelding
TWAYIB! Imeingia Ramadhani na tupo barazani. Sijui kwanini Ramadhani hii inanikumbusha ya 1964 mwaka ulioiweka njia panda historia ya Zanzibar. Mapinduzi yalikuwa bado mabichi, hayakutimu hata mwezi, ulipoandama mwezi wa mfungo wa Ramadhani.
Sizisahau siku hizo za mwanzomwanzo wa Mapinduzi. Kila jioni kukaribia kufungua mwadhini nikipanda baiskeli kuelekea jela ya Kiinua Miguu.
Nilikuwa nikimpelekea futari Sheikh Amor Zahor, jirani yetu aliyekuwa miongoni mwa wafungwa wa mwanzo wa kisiasa baada ya Mapinduzi.
Alikuwa baba wa Biubwa Amor, mfuasi wa Umma Party na mwanamke pekee wa Kizanzibari aliyekuwa akitembea na bunduki siku za mwanzo za Mapinduzi. Sheikh Amor alikuwa pia mkwe wa Ali Sultan Issa, mmoja wa viongozi wa Umma Party.
Yeye mwenyewe Sheikh Amor alikuwa miongoni mwa viongozi wa chama cha Zanzibar Nationalist Party (maarufu kwa jina la Hizbu). Alifungwa akafunguliwa halafu akakamatwa tena na akawa mmoja wa wazalendo wa mwanzo waliodhulumiwa roho zao mwaka huohuo wa 1964.
Ninawakumbuka askari wa Tanganyika walioletwa Unguja baada ya Sheikh Abeid Amani Karume, Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, kumuomba Rais Julius Nyerere wa Tanganyika amletee askari kusaidia kuimarisha amani na utulivu.
Karume akiwahitaji askari hao pia wawe kama kinga ya kuzuia asipinduliwe. Nyerere baadaye alitishia kuwaondoa askari wake katika njama za kumshinikiza Karume aukubali Muungano.
Imenijia hamu ya kuzichakurachakura kumbukumbu za utotoni nikivikata akilini mwangu vichochoro vya Mji Mkongwe nilikozaliwa na kukulia. Bado zinanijia harufu na sauti zilizokuwa zikihanikiza.
Ukisikia mlio wa vikombe vya kahawa ukijua tu huyo ni Karama au Awadh au “Bwan” Salim anayeinadi kahawa yake kwa mlio mahsusi wa vikombe vyake.
Mlio huo ukisababishwa na namna muuza kahawa akiwa na dele la kahawa mkono mmoja, alivyokuwa akivichezesha vikombe vya kahawa kwa vidole vya mkono wake wa pili.
Kuna mengi yaliyobadilika Mji Mkongwe. Mfano ni hao wauza kahawa waliokuwa wakiranda mitaani na madele yao ya kahawa kutafuta washtiri. Wala hawaonekani tena wauza maziwa wakiendesha baiskeli zao nyuma wakiwa wamepakia matangi ya maziwa.
Walikuwa wakitumwa kuyauza maziwa ya wenye maziwa. Wauza maziwa wa mjini karibu wote walikuwa na ng’ombe na mabanda yao yalikuwa eneo la Marhubi.
Baadhi yao wakifuga ng’ombe wao mashambani, kama babake Inspekta Ramesh Misra, Ramji China, Baniyani aliyekuwa akiishi Mkunazini karibu na ilipo hoteli ya Luqman. (Kwetu Zanzibar, hoteli huitwa hoteli lakini mikahawa kama Luqman au “Passing Show” nayo pia huitwa hoteli. )
Ng’ombe wakiagizwa kutoka Kenya na wakiwekwa karantini Mpigaduri baada ya kuteremshwa melini.
Siku hizo biashara kubwa ya maziwa ikifanywa na Wazanzibari wenye asili za kigeni na wa mjini kama hao Wahindi kina Ramji China. Jamii mashambani walikuwa wafugaji wadogo.
Wengi wao wakiishi karibu na Mjini, wakileta matangi yao juu ya baiskeli marikiti ya mboga kukaguliwa na idara ya kilimo halafu wakifungiwa madumu kabla ya kuwauzia bidhaa yao kwa wateja.
Na alikuwako Sharif Maziwa (mjomba wake Profesa Ibrahim Noor Sharif) katika eneo la Shangani. Kwa Sharif Maziwa kuko lakini wenyewe hawako. Hakuuzwi tena maziwa. Wenyewe wanakula raha, au kama tusemavyo wanakula unyunyu, kwingine kwa vile Mapinduzi yamewakimbiza.
Siku zile Mchambawima ndiko kulikokuwa kukiuzwa maziwa mengi. Mchambawima nako kuko lakini mengi yaliyokuwako huko hayako
Bibi yangu mzaa mama akitaka nitie mwili kwa hivyo alikuwa na dasturi ya kunipeleka Kizingo kuogelea pwani alfajiri na baadaye akinipeleka Mchambawima, karibu na markiti ya mboga, kwenda kunywa gilasi ya maziwa ya moto katika moja ya maduka ya maziwa yaliyokuwapo kwenye jumba lililokuwa la Mzee Boga.
Takriban milango yote ikiuza maziwa. Wa kwanza na uliokuwa mkubwa ulikuwa wa Madhani, Muismaili aliyekuwa pia dalali wa gazeti la Daily Nation la Kenya.
Maduka mingine yalikuwa ya Wahindi, jamii ya Makumbaro. Mawili ya kati yalikuwa ya familia ya Haji Omar Madhapuria na nduguze Essak na Yakub. Mimi nikipelekwa kwa Madhapuria ambako ndani mlikuwa na meza ndogo.
Wachezaji maarufu wa soka wa timu ya Vikokotoni kina Abdul Majham na Shioni Mzee wakenda huko kunywa maziwa baada ya mechi. Watoto wengine wakenda kununua malai kwa pesa nne.
Wamiliki wa ng’ombe walikwenda kapa kwani mabanda yao yote ya ng’ombe ya Marhubi yalivamiwa na wapinduzi.
Wengi wa wafugaji wa ng’ombe na wauzaji maziwa walikuwa Makumbaro waliokuwa wakiishi karibu na markiti.
Walianza kwa biashara ya mbuzi, Wengine walikuwa ni Maagha, Watu wengi huwaita Mabaharani, yaani Wazanzibari wenye asili ya Bahrain. Lakini kwa hakika, mababu zao walitokea Iraq.
Baadhi ya mabinti zao ndio walioolewa kwa nguvu kwa amri ya Serikali ya Mapinduzi na kuiaibisha nchi yetu mbele ya macho ya ulimwengu.
Nadhani moja ya dosari zinazoizuia Vatikani, makao makuu ya Papa, yamfanye Mwalimu Nyerere kuwa mtakatifu ni aibu hiyo iliyotokea alipokuwa Rais wa Tanzania. Alishindwa kuzizuia au hata kuzilaani ndoa hizo za haramu.
Madhani na Madhapuria waliendelea na biashara ya maziwa mpaka siku za Mapinduzi. Baada ya hapo wafanyakazi wao waliwatafuna na biashara yao ikafa.
Mabadiliko ya tabianchi, ukame na upungufu wa mashamba karibu na mji, yote hayo yalichangia kuzidi kuiua biashara hiyo iliyokuwa ikistawi Mchambawima. Usiniulize nani aliyekuwa akichamba wima hata eneo hilo likabandikwa jina hilo.
Vichochoro viwili vitatu kutoka hapo unaelekea upande wa pili wa markiti kwa kina Abdulrahman Mohamed Hamdani maarufu kwa jina la Abdulrahman “Guy”, mwanzilishi wa Chama cha Kikomunisti cha Zanzibar ambako nilikuwa na mazoea ya kupitapita kusoma magazeti ya bure.
Siku za mfungo wa Ramadhani vichochoro vyote hivyo vikinukia maandazi au maandalizi mengine ya futari.
Mapinduzi yamepindua mengi yakiwa pamoja na utamaduni wa vyakula.
Sitoshangaa endapo wazee wenzangu watatamani ujana wao urudi ili waushtakie masaibu yaliyowafika uzeeni. Si hasha wanatamani, kama mimi, irudi mikate ya mofa, ya manda na ya ana.
Hii mikate ya ana ilikuwa ya duara kama mikate ya ufuta lakini ilikuwa haitiwi ufuta, ilikuwa minene zaidi na ikitiwa sukari kwa mbali hivi.
Katika zungukazunguka zangu nimeikuta mikate ya mofa ikiuzwa Mombasa, Kenya, kwenye mkahawa wa Barke kule Kibokoni.
Ya manda, yenye kupikwa kwenye majani ya mgomba, nimeikuta Comoro ambako inaitwa “mikate ya bwan tamu” lakini ladha yake tofauti kidogo na ile tuliyoizoea Unguja.
Zamani karibu hoteli zote (mikahawa) zikimilikiwa na Mahadhrami, watu wenye asili ya Yemen kutoka Hadhramout, ingawa Zanzibar wote huitwa Washihiri. Wakipika chai kwa maziwa ya mkebe na vyakula walivyokuwa wakiviuza vilikuwa vya ladha.
Ukiweza kununua kaimati, visheti, bokoboko, vyakula vya nazi, mikate ya mofa na ya ufuta, ingawa mimi udogoni mwangu nikitumwa kununua mikate ya ufuta darini juu kabisa kwenye jumba la Bwana Burhan al Amawi hapo Mkunazini karibu na Msikiti wa Memon. Mikate ya huko ilikuwa laini kama sufi na ikiyayuka mdomoni.
Nazikumbuka legeni za kuokea mikate ya kumimina. Siku hizo mikate ya kusukuma ilikuwa mikate ya kusukuma tu. Haikuwa na majina mbadala ya chapati au parata, Vipopopoo vilikuwa vipopoo na si matobosha.
Zama zetu vyakula vilivyopikwa vikapikika, kwenye maseredani na majiko ya kuni, vilikuwa mfano wa nyimbo za taarab – vilijaa hisia mbalimbali.
Ukistarehe kula maandazi yaliyotiwa hiliki na arki ya vanilla ili yawe na harufu nzuri na ladha zaidi. Leo wapi! Labda upikiwe majumbani kwa jamaa wa mjini. Na hata huko kuna mengi yanayokosekana kama samli ya Kismayu ambayo siku hizi imepotea.
Siku hizi mengi yameharibika. Ubora wa vyakula mahotelini umeanguka. Wapishi hawana fahari na mapishi yao. Wanavifanyia uchoyo viungo kwa sababu bei zimekuwa ghali.
Jioni karibu na msikiti Ruta kwa Mzee Khamis tukinunua sambusa na kuku wa kuchoma wa Abdillahi.
Tukinunua sharubati za kila aina lakini tukitaka maji ya machungwa au ya ukwaju tukikimbilia kwa Khamis Machungwa, mishikaki ya urojo tukiipata karibu na sinema ya Majestic, mikate ya Ajemi kwenye hoteli moja ya Wahindi iliyokuwa marikiti, na haluwa Mtendeni kwa Mahruki.
Upande wa mwisho wa Sokomuhogo mtaa niliozaliwa karibu na kwa Adnani muuza mbatata za urojo, kulikuwa kukiuzwa tende kwenye duka la kina mwanaharakati Fatma Aloo. Na wao wakinunua nyuzi na nyaya za shaba na vinginevyo hata kutoka kwa watoto.
Jamaa yake Profesa Abdulaziz Lodhi, Haji Omar Essak akipika haluwa ya lozi na tamu tamu za kihindi kama ladu, nankhatai (nangatai) na biskuti za siagi.
Wengi wa wakazi wa leo wa mjini wametoka sehemu nyingine za Zanzibar na hawakuzoea mchanganyiko wa watu wa mjini wenye nasaba na tamaduni tofauti.
Ni kinyume na ilivyokuwa zama zetu. Lakini tena kila kizazi kina mambo yake. Kilichosalia cha zama zetu ni kumbukumbu za mazoea. Maisha yamekuwa magumu, bei za vitu ziko juu na mapato madogo.

HISTORIA YA BABU

ashura bilal 2
KAMA ndiyo mara yako ya kwanza kusikia jina la Abdulrahman Mohamed Babu, ngoja nikurahisishie kazi kidogo. Nitakueleza machache kumhusu ili ufahamu alikuwa mtu wa namna gani.
Mwaka 1959, miaka minne kabla nchi ya Zanzibar na miaka miwili kabla nchi ya Tanganyika na nchi yoyote ya Afrika Mashariki haijapata Uhuru, yeye tayari alikuwa mtu wa kwanza kutoka nchi ya Zanzibar au eneo hili Afrika Mashariki kwenda nchini China na kufanya mawasiliano na Chama cha Kikomunisti.
Katika safari hiyo, mwenyeji wake alikuwa Chou En Lai na yeye ndiye alikuwa mwananchi wa kwanza kutokea nchi ya Zanzibar na Afrika Mashariki kukutana na kuzungumza na Mwenyekiti Mao Ze Dong.
Kabla ya Baba wa Taifa la nchi ya Tanganyika, Mwalimu Julius Nyerere, hajajiingiza katika masuala ya Umajumui wa Afrika, Babu akiwa Mzanzibari alikuwa miongoni mwa Waafrika mashuhuri waliohudhuria mkutano wa All African People Congress uliofanyika Novemba 1958 nchini Ghana na kuhudhuriwa na wanasiasa kama Kwame Nkrumah, Kenneth Kaunda, Nnamdi Azikiwe, Patrice Lumumba na Frantz Fannon.
Ndiye mwanasiasa maarufu wa nchi ya Zanzibar anayeweza kuwataja watu kama Ernesto Che Guevarra na Malcolm X kama marafiki zake. Kimsingi, katika baadhi ya duru za kimataifa, Babu alikuwa maarufu kuliko Mzanzibari yeyote Kiongozi yoyote wa nchi hizi za Afrika Mashariki yani Kenya,Uganda na Tanganyika kwenye miaka ya 1960. Na hapo najumlisha na Nyerere.
“Kusema ukweli, kama leo tunasema kuna uhusiano wa kihistoria baina ya China na Nchi ya Zanzibar au nchi ya Tanganyika, ni lazima tuseme kwamba Babu ndiye aliyeziunganisha nchi hizi Tatu. Kuna mtu anaitwa Ali Sultani, Mzanzibari, aliwahi kwenda China lakini akitokea Uingereza kwa masuala ya kupigania Harakati za Wafanyakazi lakini ni Babu ndiye alikwenda China na kuitambulisha nchi ya Zanzibar na nchi ya Tanganyika,” anasema Mama Ashura Hilal maarufu kama Ashura Babu, aliyekuwa mke wa mwanasiasa huyo kwa zaidi ya miaka 30.
Bi Ashura kwa sasa anaishi nchini Marekani. Amekuja nchini Zanzibar na atatembelea nchi ya Tanganyika pia kushuhudia ndoa ya mmoja wa wajukuu zake na ilikuwa bahati tu kwamba Muandishi wetu kuarifiwa mapema kuhusu ujio wake huwo.
Akiwa amezaliwa katika eneo la Mwembeladu, nchini Zanzibar, mwaka 1942, mama huyu sasa ni mtu mzima mwenye umri wa miaka 73. Hata hivyo, ana udongo mzuri na utaweza kuamini hata akikwambia ana umri wa miaka 55 Mashaa Allah.
Wakati nilipokutana naye,Bi  Ashura hakuwa na sura ya kinyongo wala huzuni kutokana na madhila ya kisiasa yaliyomkumba mumewe huyo wa zamani pamoja na familia yake kutokana na harakati zake za kisiasa.
“Miye sizeeki kwa sababu sina kinyongo na mtu. Kama ningeamua kuwekea watu vinyongo ningekuwa naumwa na presha kila siku. Ninachoshukuru ni kwamba Babu mwenyewe alikuwa amewasamehe waliomfanyia mabaya na aliendelea na maisha yake,” anasema.
Kwa mara ya kwanza, walikutana na Babu kwenye miaka ya 1950 wakati yeye akiwa mwanafunzi na Babu akiwa Katibu Mkuu wa chama cha Zanzibar Nationalist Party (ZNP).
Bi Ashura alikuwa mmoja wa wasichana wachache waliokuwa wakivutiwa na siasa wakati huo. Ni mapenzi yake yaliyomfanya ajiunge na Umoja huo wa Vijana na kisha kukutana na Babu ambaye alikuwa ameshawishiwa kuhama kutoka Uingereza alikokuwa akishiriki katika harakati za Wafanyakazi.
Kwa mujibu wa Bi Ashura, aliyemshawishi Babu kurejea nchini Zanzibar ni Ali Muhsin Barwani, ambaye pia alihudhuria mkutano ule wa Ghana wa mwaka 1958 pamoja na Abeid Amani Karume aliyekuja kuwa Rais wa kwanza wa nchi ya Zanzibar bila ya kupigiwa kura wala wananchi wa Zanzibar kulizwa baada ya Mapinduzi ya mwaka mauwaji ya hali ya juu ya Wazanzibari walio uliwa bila ya hatia yoyote na wakuri walima makonge 1964 wakitokea nchini Tanganyika walio andaliwa katika mji wa Tanga.
“Babu aliporejea aliomba kuiona ilani ya ZNP. Akaifanyia marekebisho kwa mujibu wa alivyoona inafaa. Yeye ndiye aliyeweka utaratibu wa vijana kufundishwa Elimu ya Siasa (Political Education) kila Jumamosi ambayo alikuwa akifundisha yeye Mwenyewe.
“Ndiyo maana baadaye vijana wa ZNP wakawa wana uelewa mkubwa sana wa siasa kuliko wa vyama vingine vyote. Katika miaka hiyo ya 1950, Babu tayari alikuwa anajua kila kinachoendelea duniani kote kuhusu siasa na Ukomunisti.
“Ni wakati huo ndipo ZNP kilipoanza kupiga na miziki na kuwaruhusu vijana wake wa kike kuanza kuvaa sketi za khaki na kofia zenye nyota. Muziki na mavazi haya yakasaidia sana kuongeza idadi ya vijana na ZNP. Katika vijana waliokuwapo ZNP wakati huo, namkumbuka zaidi huyu Salim Ahmed Salim ambaye baadaye alikuja kushika nyadhifa nyingi za juu hapa nchini Zanzibar na hata nchini Tanganyika na duniani,”
Nilifanya mazungumzo na Bi Ashura kwenye bustani nje ya nyumba yake jijini Dar es Salaam nchini Tanganyika. Ilikuwa jioni na jua halikuwa kali. Ingawa sasa ameingia kwenye umri wa uzee, alikuwa nadhifu katika gauni lake la marinda.
Walianza uhusiano na Babu wakati huo. Hatimaye,Bi  Ashura alipotimiza umri wa miaka 18 mwaka 1960, wakafunga ndoa na mwanasiasa huyo ambaye tayari wakati huo serikali ya kikoloni ilikuwa imemuona kama mtu hatari hapa nchini Zanzibar.
Katika mazungumzo yangu naye,Bi  Ashura ananipa ukweli kuhusu jambo moja ambalo bila shaka lilikuwa halifahamiki kwa wengi. Kwamba akiwa nchini Uganda mwaka 1963, Babu alipiga simu kwa Salim Ahmed Salim na kumweleza kuwa aanze mipango ya kuunda chama cha Umma Party.
Babu alikuwa amekorofishana na wenzake ndani wa ZNP kuhusu mwelekeo wa chama hicho kwenye nchi ya Zanzibar Mpya yenye mamlaka kamili kutoka mikononi mwa Mkoloni wa Kiengereza. Wenzake, akina Ali Muhsin walikuwa na Mrengo wa Kibepari lakini yeye alikuwa na Mrengo wa Kijamaa. Tofauti hizo, ambazo zilichochewa pia na wakoloni, ndizo zilizosababisha Babu hatimaye ahame kutoka chama hicho na kuanzisha Umma Party.
“Baada ya Babu kuhama, asilimia kubwa ya vijana walihama kutoka ZNP na kujiunga na Umma Party kwa sababu walikuwa wanamuelewa kiongozi wao huyo. Wengine, baadhi yao, ni wale ambao walikwenda kufanya mafunzo ya kijeshi Cuba,” anasema Bi  Ashura.
Ni vijana hao, anasema mama huyu, ambao ndiyo waliotoa mchango mkubwa kwenye Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, wakitumia vema mafunzo ya kijeshi kwenye mapigano ya Guerrilla waliyoyapata nchini Cuba.
“Historia ya Mapinduzi inapotoshwa sana. Yale Mapinduzi ya mwaka 1964 yalifanikishwa kwa kiasi kikubwa na wapiganaji wa Umma ambao ndio waliokuwa na mafunzo ya kijeshi na waliojua mbinu za mapigano.
“Ukumbuke kuwa kwenye mkesha wa Mapinduzi, viongozi wote wa juu wa chama cha Afro-Shiraz na Umma hawakuwapo Zanzibar. Akina Karume, Babu, Kassim Hanga na wengine wote walikuwa Dar es Salaam. Wananchi wengine hawakuwa na mafunzo yoyote ya kijeshi lakini wakawa wamepewa silaha.
“Bila kutumia mbinu wasingeweza kuiteka Kambi ya Malindi ya Polisi. Hii ni kwa sababu ilikuwa imezungukwa na ukuta ambao ulikuwa na matundu ya kupitishia risasi. Mbele ya kambi kulikuwa na eneo la uwanda wa wazi kabisa. Kusogelea pale ilikuwa ni kujitakia kifo maana wangeonekana na wangepigwa risasi.
“Ni wapiganaji wa Umma ndio waliokuja na mbinu ya kuvamia kambi ile usiku tena kwa kutambaa kwa kutumia matumbo. Askari wa kambi wanakuja kushituka watu tayari wako kambini. Ile ndiyo ilikuwa namna pekee ya Mapinduzi kufanikiwa,” anasema mwanamamamapinduzi huyu.
Babu alitakiwa akamatwe siku chache kabla ya Mapinduzi hayo. Bi Ashura anasema ilikuwa bahati kwamba mmoja wa askari anayemkumbuka kwa jina moja la Barnabas, ndiye aliyekwenda kwao na kuwapa taarifa kuwa aondoke kwani atakamatwa.
“Babu alitoroka Zanzibar kwa kutumia usafiri wa ngalawa iliyokuwa nyuma ya eneo la Ngazimia, Unguja na ndiyo iliyompeleka Dar es Salaam. Mimi sikuondoka naye kwa sababu nilikuwa na watoto wadogo watatu na wasingeweza kusafiri baharini na ngarawa. Nikabaki lakini vijana wa Umma Party walikuwa wakilinda.
“Baada ya Mapinduzi, ndipo akina Babu wakarudi kwa kutumia usafiri wa boti iliyotolewa na Myahudi mmoja aliyekuwa akimiliki Hoteli ya Silversands anayefahamika kwa jina la Mischa. Hivyo hapo utaona mchango mkubwa wa vijana na chama cha Umma Party kwenye Mapinduzi,” anasema.
Mama huyu anayakumbuka Mapinduzi hayo kwa sababu nyingine ya kibinafsi. Baada ya Babu kutoroka Visiwani, binti yao mkubwa aliyekuwa akicheza nje ya nyumba yao aligongwa na gari na dereva mwanafunzi na kufariki dunia.
Babu asingeweza kurudi Zanzibar kwa sababu angekamatwa na Mapinduzi yasingefanyika kama yalivyopangwa. Ikabidi mtoto yule azikwe pasipo baba yake ingawa Babu alipewa taarifa. Bi. Ashura anasema askari walitanda makaburini wakifikiri kuwa huenda Babu angekuwepo lakini hakujitokeza.
Malcolm X na Che Guevarra
Katika matukio ya kihistoria ambayo Bi Ashura anayakumbuka; hakosi kusahau mikutano ya Babu na wanamapinduzi maarufu duniani; Ernesto Che Guevarra na Malcolm X. Hawa walikuwa marafiki wa mumewe huyo wa zamani ambao naye alikutana nao.
Mara ya kwanza walikutana na Malcolm X kwenye mojawapo ya ziara za kikazi za Babu nchini Marekani. Aliyewakutanisha alikuwa ni Mzanzibari Ali Foum ambaye baada ya Muungano alipangiwa kituo cha kazi New York, Marekani. Huyu alikuwa ni mmoja wa vijana waliolelewa kisiasa na Babu.
“ Siku moja Foum alitualika chakula cha usiku nyumbani kwake na tukakutana na Che Guevarra. Yeye ndiye akatuambia kwamba alitakiwa kuhutubia kwenye mkutano wa Malcolm X uliopangwa kufanyika kwenye ukumbi wa Audubon Ballroom, Manhattan, New York.
“ Alitusimulia kwamba ilikuwa yeye aende kuhutubia pale Audubon lakini Rais wa Cuba, Fidel Castro, alikuwa amemkataza asiende kwa sababu za kislamu. Hivyo Che akamuomba Babu akatoe salamu zake kwenye mkutano ule.
“Mimi na Babu tukaenda kwenye ule mkutano. Babu akakaa jukwaani na Malcolm, huku mimi na mke wa X, Betty Shabazz, tukikaa kwenye mstari wa mbele kushuhudia. Babu alipewa nafasi ya kuzungumza na alipoeleza kuhusu salama za Komredi Che, ukumbi mzima ulisimama na kulipuka kwa nderemo na vifijo.
“Mwaka huohuo wa 1964, kwenye mwezi wa kumi hivi, Malcolm alialikwa na Babu na akaja Zanzibar na Tanganyika. Alikwenda kwanza Zanzibar na kisha akaja Dar es Salaam. Alipangiwa hoteli lakini alikuwa akishinda nyumbani kwetu pale Mtaa wa Luthuli jirani na Ikulu.
“Malcolm X alikuwa mtu mzuri na mwenye bashasha. Alikuwa na uchungu kutokana na mateso ambayo mtu mweusi wa Afrika na Marekani alikuwa akiyapata. Alikuwa akipenda sana vyakula vya Kiafrika kama vile samaki wa kupaka (samaki wa kupikwa chukuchuku, bila kuwekewa mafuta wala viungo vingi).
“Alipokuwa Dar es Salaam, nyumba ilikuwa inatembelewa na wageni wengi. Marafiki wa Babu waliopo nchini na wapigania Uhuru wa nchi mbalimbali waliokuwa wakiishi Zanzibar na Tanganyika wakati huo.
“Walikuwa wanajifungia chumbani na kuzungumza mpaka usiku mkubwa. Mimi kazi yangu ilikuwa ni kupeleka chakula na kahawa. Wanazungumza mpaka asubuhi na ajenda kubwa ilikuwa masuala ya ukombozi, hadhi ya mtu mweusi na mapinduzi duniani kote.
“Che Guevarra na Malcolm X wote walikuwa watu wazuri. Lakini Malcolm X ilikuwa zaidi kwa sababu Betty alikuja kuwa rafiki yangu mkubwa. Nilikuwa siwezi kwenda Marekani pasipo kukutana na Betty na rafiki yetu mwingine aliyeitwa Ann.
“Watu wote hao watatu sasa hawapo tena duniani; Che, X na Babu. Wakati Malcolm alipouawa kwa kupigwa risasi, nilijisikia kama nimefiwa na mwanafamilia. bayaa zaidi aliuawa palepale Audubon. Betty alinisimulia kuwa alikuwa amekaa kwenye kiti kilekile alichokaa wakati nilipoenda. Ule msiba uliniuma sana,” alisema.
Sababu za Babu kutofautiana na akina Karume
Bi. Ashura hapepesi maneno linapokuja suala la kiini hasa cha ugomvi baina ya Babu na kundi la wanamapinduzi waliokuja kufahamika kwa jina la Liberators (Wakombozi) ambao kimsingi ni wahafidhina wa Mapinduzi ya mwaka 1964.
“Mara baada ya Mapinduzi, Rais Karume aliamua kuongeza mshahara wa wajumbe wa Baraza la Mapinduzi kufikia kiasi cha shilingi 25,000 wakati huo. Pamoja na mshahara huo, mkubwa kwa wakati huo, Karume pia aliwakopesha wajumbe hao kiasi cha shilingi 75,000 kama mkopo wa nyumba.
“Babu alipinga suala hilo. Alisema lifanyike jambo moja; ama watu waongezwe mshahara na wasipewe mkopo au wapewe mkopo na wasiongezwe mshahara. Alisema jambo hilo ni ufisadi na yeye hatochukua mkopo huo.
“Wenzake wote walikubali. Yeye alikataa. Sasa kuna watu wakaenda kwa Karume na kumweleza umbea kwamba eti Babu anamsema vibaya kwa watu kuwa wao ni wezi kwa sababu ya kujiongezea fedha hizo. Karume akachukia sana.
“Pamoja na kuombwa sana achukue, Babu akakataa. Nakumbuka mara ya mwisho ilikuwa mwaka 1970 wakati tulipoenda Japan kwenye Maonyesho ya Afro 70. Mzee Thabit Kombo alinifuata na kuniomba nimwambie Babu aache maneno na achukue zile fedha.
“Unajua Kombo alilelewa na baba mzazi wa Babu. Wazazi wa Babu walichelewa sana kupata mtoto wa kiume na wakamchukua Kombo na kumlea. Baba mzazi wa Abdulrahman alifariki dunia wakati mwanaye ndiyo kwanza akiwa na umri wa miaka miwili. Kwa hiyo, kwa Kombo, wazazi wale walikuwa kama wazazi wake.
“Watoto wangu wawili; Salma na Mohamed waliyapata majina yao kutoka kwa baba na mama wa Babu. Sasa Thabit Kombo alikuja na kuniambia; ‘Sasa Babu anataka ugomvi wa nini na watu...? Basi achukue tu mkopo ili mama yangu Salma na baba yangu Mohamed wapate mahali pa kukaa. Watoto hawa wataishi wapi akipata matatizo....’?
“Nilijua msimamo wa Babu kwenye hili lakini nikamuahidi Kombo kuwa nitajitahidi. Kweli nikamuambia lakini akanipa jibu moja; ‘Naomba hii iwe mara yako ya mwisho kuniambia kuhusu jambo hilo. Nimesema sitaki kuchukua mkopo,’. Babu akakataa. Mpaka anafariki dunia, Babu hakuacha nyumba, shamba wala mti wa mkarafuu. Hakuwa na chochote.
“Hakuamini katika utajiri wa mali. Ninachoshukuru Mungu ni kwamba hakuna mtu yeyote ndani au nje ya nchi ambaye anaweza kunyooshea kidole familia yangu na kusema tuliiba hiki au kile. Na hili si jambo dogo maana limetufanya tuishi kwa amani. Kama angetaka, Babu angeweza kuwa tajiri mkubwa maana yeye ndiye aliyekuwa anafahamika na watu wazito nje ya nchi yetu,” anasema Mama huyu.
Dalili za tofauti hizi alianza kuziona awali. Bi  Ashura anasema Karume alianza kutofautiana na wanasiasa wasomi na wenye mtazamo wa kuona mbali.
Miongoni mwa wasomi hao walikuwa ni akina Babu, Kassim Hanga na Sultani. Wote hao Karume hakuelewana nao vizuri na badala yake akajiweka jirani na akina Juma Washoto, Edington Kisasi, Brigedia Yusuf Himidi, Said Natepe na Seif Bakari.
Ndiyo maana, anasema Bi Ashura, akina Babu na Hanga walikuja kufanya kazi Tanganyika ambako usomi wao na changamoto zao zilikuwa zinavumilika kwa Mwalimu Nyerere.
Makala hii itaendelea wiki ijayo ambapo Ashura ataeleza kuhusu matukio yaliyofuata baada ya kifo cha Karume, uhusiano wa Babu na Mwalimu Nyerere na maisha yake baada ya kuwekwa kizuizini kwa Abdulrahman Mohamed Babu.

KATIKA MAKUNDI MANNE YALIOTAKA KUIPINDUWA NCHI YA ZANZIBAR NILIPI LILILOFYATUWA RISASI KWANZA


Afbeeldingsresultaat voor john  okello

Jemedari kutoka Uganda alivyoongoza Mapinduzi ya kuikomboa Zanzibar


NA JOSEPH MIHANGWA
WAKATI Abdallah Kassim Hanga na wenzake wakipanga Mapinduzi dhidi ya utawala wa Sultani visiwani Zanzibar kwa msaada wa Rais wa Tanganyika, Mwalimu Julius Nyerere mapema mwaka 1963, hawakuelewa kwamba, Mwanamapinduzi mwingine, ‘Field Marshal’ John Gideon Okello, naye alikuwa akipanga Mapinduzi kama hayo.
Hanga, mwanasiasa wa mrengo wa kushoto na mfuasi wa harakati wa aina za Mapinduzi ya Oktoba 1917 ya Urusi, alijua chuki waliyokuwa nayo baadhi ya vijana wa Chama cha Afro-Shirazi (ASP) dhidi ya utawala wa kikoloni na Serikali ya Kisultani visiwani; lakini walikosa ari ya Mapinduzi kwa sababu kiongozi wa ASP, Sheikh Abeid Amani Karume, hakupendelea njia ya umwagaji damu kutafuta uhuru badala ya sanduku la kura.
Lakini Hanga alielewa nguvu ya wanaharakati wa Kikomunisti wa chama kipya cha Umma Party (UP) cha Abdulrahman Mohamed Babu; akatamani ‘ushirika’ wa siri nao bila Karume na vijana wake kujua. Akajihoji, kama ASP ilizuia ukombozi kwa njia ya Mapinduzi, kwa nini asikubali kuitwa ‘msaliti wa ASP’ na kuleta uhuru kwa njia hiyo?
Wengine wa kundi la Hanga kutoka ASP wenye itikadi za Ki-Marx waliopanga Mapinduzi kwa msaada wa Mwalimu, huku aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ulinzi wa Tanganyika, Oscar Kambona, akiwa kiungo chao, ni Abdul Aziz Twala, Saleh Sadallah, Akida Athuman na Othman Sharrif Mussa.
Katika kipindi hicho, Mwanaharakati mwingine, ‘Field Marshal’ Okello, mzaliwa wa Lang’o, Uganda na mhamiaji Zanzibar, alikutana pia na Mwalimu Nyerere miezi michache kabla ya Uhuru wa Zanzibar, wakajadili uwezekano wa Mapinduzi dhidi ya Serikali iliyotarajiwa kuingia madarakani.
Inasemekana, Mwalimu alimpa Okello jukumu la kuisoma hali ya kisiasa na kiulinzi visiwani humo kwa maandalizi ya Mapinduzi siku itakapowadia.
Kwa nini Mwalimu alitaka Mapinduzi visiwani?
Akizungumza kwenye hafla moja ya jioni mjini Dar es Salaam kabla ya Uhuru wa Zanzibar, Mwalimu akionekana kutofurahia hali ya kisiasa visiwani humo enzi hizo, alisema:
“Kama ningeweza kukikokota kisiwa kile (Zanzibar) hadi katikati ya Bahari ya Hindi (kiwe mbali na Tanganyika), ningefanya hivyo. Sitanii! Ninaogopa huko mbele (baadaye) Zanzibar itakuwa tatizo kubwa kwetu lenye kuumiza kichwa.”
Kwa tamko hilo pekee, ni dhahiri Mwalimu hakutaka kuwa na ‘jirani’ huyo ila kama kungefanyika Mapinduzi chanya. Kwa hilo, kwa nini asifikirie kuwatumia Hanga na Okello kufanya Mapinduzi kipindi ambacho Wazanzibar wengi hawakuyawazia?
Waingereza ambao ndio waliokabidhi Uhuru kwa Serikali ya Mseto ya Zanzibar National Party (ZNP) na Zanzibar and Pemba People’s Party (ZPPP) kwa sharti la nchi kubakia chini ya himaya ya Sultani, nao waliamini kwamba Mwalimu alisimamia na kuwezesha Mapinduzi hayo; na hivyo kumfanya akane kwa kujitetea baadaye (kisiasa), akisema:
“Nilitabiri machafuko yangetokea muda si mrefu; na tazama, ndani ya mwezi mmoja Mapinduzi yakatokea… Na wote waliamini kwamba nilikuwa sehemu ya mpango wa Mapinduzi hayo. Kwa sababu tu nilitabiri matatizo, walidhani nimeshiriki!”
Lakini mtafiti na mwanahistoria mahiri wa Kizanzibari, Dk. Harith Ghassany, anaweka bayana ushiriki huo wa Mwalimu, katika kitabu chake ‘Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru’, akisema: “Maandalizi ya Mapinduzi yaliratibiwa vizuri na Mwalimu Nyerere mwenyewe, Wamakonde na wapiganaji wengine waliandaliwa katika kambi ya Sakura, Tanga.
“Alimteua Kambona na kumtuma huku na huko ili kufanikisha hilo. Ile siri (ilikuwa) ni yake na hakutaka itoke.”
Ikumbukwe, Julai 25 hadi 28, 1963, Mwalimu Nyerere alifanya ziara nchini Algeria ya Kimapinduzi, ya Rais Ahmed Ben Bella na miezi mitano baadaye kufuatia ziara hiyo; Januari 2, 1964, meli yenye shehena ya silaha, MV Ibn Khaldun, ilitia nanga Dar es Salaam na kushusha silaha nyingi kama sehemu ya maandalizi ya Mapinduzi.
Hanga kwa upande wake, alinukuliwa baadaye akisema, yeye na Abdul Twala, walikaa Tanganyika kwa miezi miwili wakifunzwa na Jeshi la Polisi namna ya kutumia silaha na kwamba, mwanzoni Mapinduzi yalipangwa kufanyika mwishoni mwa Desemba 1963, yakaahirishwa hadi Januari 7, 1964, lakini tarehe zote mbili hazikuwa nzuri.
Hanga alisema pia kwamba, siku moja kabla ya Mapinduzi, alikwenda Dar es Salaam kuchukua silaha lakini hakuweza kurejea hadi Januari 13, 1964 wakati Mapinduzi yamekwishafanyika.
Kundi la pili la Wana-ASP linalodhaniwa kupanga Mapinduzi lakini lenye siasa baridi, chini ya uongozi wa Seif Bakari, lilikuwa na Saidi Washoto, Abdullah Natepe, Khamis Hemed, Saidi Ali Bavuai, Yusuf Himid na Pili Hamis.
Wengine ni Mohamed Abdallah, Hafidh Suleiman, Hamad Ameir, Ramadhan Haji, Hamis Darwesh na Said Mfaranyaki.
Kundi hili tiifu kwa Sheikh Karume na ASP, halikuwa na programu ya Mapinduzi ya kueleweka na kwa sehemu kubwa, lilizingatia msimamo wa Karume wa kutoichokoza serikali kwa hofu ya ASP kufutwa na viongozi wake kuingia matatani.
Karume alielekeza wafuasi wake wawe watulivu hadi Uchaguzi Mkuu mwingine miaka mitatu baadaye, ambapo alikuwa na hakika ASP ingeshinda.
Septemba 1963, Field Marshal Okello kama mwanachama wa ASP, alionana na Seif Bakari, wakazungumza juu ya Mapinduzi na kubaliana, lakini dhamira ya Bakari ilikuwa dhaifu juu ya hilo.
Kwa kuchukizwa na uratibu dhaifu usio na malengo wa ASP, Okelo alianzisha kivyake mafunzo ya kijeshi ya siri kwa vijana kutoka Tanganyika, Kenya na Msumbiji kwa ‘baraka’ za Tanganyika na kushirikisha baadhi ya Wazanzibari shupavu.
Mafunzo hayo, yaliyojumuisha ‘manamba’ waliofukuzwa mashambani na Mamwinyi wa Kiarabu, pamoja na baadhi ya Askari Polisi waliofukuzwa kazi na Serikali mpya ya ZNP/ZPPP kwa kutoviunga mkono vyama hivyo wakati wa kampeni, yalifanyika vichakani chini ya minazi kwa kutumia silaha za jadi na bunduki bandia za miti.
Lengo la Okello na wapiganaji wake lilikuwa si kunyakua dola, bali kuchoma moto na kuteketeza kabisa mji wa Unguja.
Julai 1963 kuelekea Uhuru, aliyekuwa Katibu Mkuu wa ZNP, Abdulrahman Babu, alijiengua kutoka chama hicho baada ya kutofautiana kiitikadi na Rais wa ZNP, Ali Muhsin, aliyetaka Zanzibar huru ifuate siasa za Kiliberali (ubepari), wakati Babu (pamoja na Hanga wa ASP) alitaka Zanzibar iwe ya Kikomunisti.
Waliojiengua pamoja na Babu kutoka ZNP na kuunda UP ni Salim Ahmed Salim, Ali Sultan Issa, Mohamed Ali Foum na Ali Mahfoudh ambaye ndiye aliyeunda na kuongoza Jeshi la Ukombozi la Zanzibar (Zanzibar Peoples Liberation Army – ZPLA) baada ya Mapinduzi.
Akiwa Katibu Mkuu wa ZNP, Babu aliwezesha chama hicho kuanzisha ushirikiano wa kikazi na kiitikadi na nchi za harakati za ukombozi kama Misri ya Abdel Gamal Nasser, Cuba ya Fidel Castro na China ya Chou Enlai.
Kwa sababu hiyo, aliweza kupeleka huko vijana kwa mafunzo ya kijeshi mwaka 1961 ambapo miezi miwili kabla ya Mapinduzi, vijana hao ndio tu walikuwa wamerejea kutoka mafunzoni.
Dhamira kuu ya Umma Party ilikuwa ni kuanzisha mapambano kwa kushirikiana na ASP dhidi ya Serikali ya Kisultani Visiwani.
Na katika salaamu zake siku ya ‘Uhuru’, Desemba 10, 1963; Babu hakuficha dhamira yake, alisema: “Salaam! Watu wa Zanzibar na chama chao cha Umma Party, wanasubiri kunyakua madaraka na kuyaweka mikononi mwao siku na saa itakapowadia.”
Kwa mujibu wa Babu, saa na siku iliyosubiriwa ni ile ya kupinduliwa kwa Serikali ya ZNP/ZPPP na makada wa Umma Party, pengine kwa kushirikiana na kundi la Hanga.
Kufikia hapo, ni dhahiri kulikuwa na mipango ya Mapinduzi ya makundi manne yasiyofahamiana.
Kundi la kwanza ni lile la ASP la Hanga kwa kuungwa mkono na Tanganyika; kundi la pili lilikuwa la Field Marshal Okello, la walalahoi wa ASP na wasio na vyama; kundi la tatu lilikuwa la vijana butu wa ASP wakiongozwa na Seif Bakari na kundi la nne la harakati za Ki-Karl Marx, lililoongozwa na Babu.
Ni kundi lipi kati ya hayo manne, lililofyatua risasi ya kwanza ya Mapinduzi?
Jumamosi ya Januari 11, 1964, ilianza kushuhudia isivyo kawaida, mitaa myembamba ya Mji wa Unguja ikifurika nyuso ngeni zisizo za kimjini, tangu mchana hadi giza; lakini kila mtu alichukulia mambo kirahisi tu kama sehemu ya pilikapilika za maandalizi ya Sikukuu ya Ramadhani iliyotarajiwa.
Ukweli, vikosi vya Mapinduzi vilianza kuingia mjini tangu saa 10 jioni na kuendelea hadi usiku.  Sultani Jamshid bin Abdullah Khalfa Harub, alianza kuamini ule uvumi ulioripotiwa na Karume na Aboud Jumbe kwa Kamishna wa Polisi (Superintendent) J. M. Sullivan, siku mbili zilizopita, juu ya uwezekano wa kutokea machafuko.
Kama tahadhari kwa yawayo yote, askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia cha Mtoni na polisi wa Kituo cha Ziwani, walipewa amri kwenda kulinda mjini, umbali wa kilometa tano hivi ambako kulikuwa kukichezwa dansi (fete) na kubakia askari wachache tu vituoni.
Nitamke mapema hapa kwamba, wakati haya yakiendelea, Karume, Hanga na Babu walikuwa Dar es Salaam.
Karume, inadaiwa alikimbilia huko siku moja kabla, pengine kwa kuhofia yale ambayo yangeweza kutokea, Hanga alidai baadaye kwamba alikwenda kuchukua silaha wakati Babu alitorokea huko Januari 8, baada ya kutafutwa ili akamatwe na Serikali kwa tuhuma za uhaini.
Yapata saa 7.00 hivi usiku Januari 12, Field Marshal Okello, akiongoza kikosi cha wapiganaji 400, alivamia Kituo cha Polisi Ziwani kilichokuwa chini ya Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Derham, baada ya kukata waya wa uzio. Akawazidi nguvu askari na baadhi kuwaua na kuteka silaha nyingi.
Kutoka Ziwani, Jemedari Okello alishambulia na kuteka Kituo cha Polisi Mtoni na kujipatia silaha nyingi zaidi.  Vijana wa Babu (Umma Party), walijitupa uwanjani kuungana na Okello wakati kituo kikiwaka moto, huku Okello akiwa amejitosheleza kwa silaha alizoteka, tayari kuuteketeza kwa moto Mji wa Unguja.
Kuingia kwa ‘vijana wa Babu’ wenye mbinu za juu za kijeshi na Mapinduzi walizosomea China, kulibadili madhumuni ya ‘maasi’, kutoka kuuteketeza kabisa mji wa Unguja, kuwa ya kushika dola, wazo ambalo lilitolewa na Qualletin Badawi wa Umma Party.
Mbali na kuteka vituo vya polisi, ikawa pia sasa ni kukamata Uwanja wa Ndege na Ikulu ya Sultani, bila hivyo, Okello pekee angepigwa, kwani Sultani alikuwa ametuma ndege Pemba kuleta silaha nyingi, lakini wakati ndege hiyo ikirejea, tayari vijana wa Babu walikuwa wamekamata uwanja wa ndege.
Gerelateerde afbeelding
Kwa kifupi, kuanzia kutekwa kwa Mtoni na kuendelea, mapambano yaliendeshwa na kuratibiwa kwa mbinu za Vita vya Msituni (Guerrilla Warfare) chini ya uratibu thabiti wa makamandoo wa Umma Party.
Hadi saa 12.00 asubuhi, upinzani pekee ulitoka Kituo cha Polisi Malindi, karibu na Bandari ya Unguja na makazi ya Sultani; na kufikia saa 2.30 asubuhi, Malindi nayo ikawa mikononi mwa Wanamapinduzi; Sultani Jamshid na familia yake, akatimka kuelekea Mombasa ndani ya Meli yake ‘Seyyid Khalfa’ iliyokuwa ikisubiri Pwani.
Jioni hiyo, Field Marshal John Okello akatangaza kupitia Redio Zanzibar kukamilika kwa Mapinduzi, akisema: “Mimi ni Field Marshal; Enyi mabeberu, hakuna tena Serikali ya Mabeberu katika visiwa hivi; Chama cha Afro-Shirazi na Chama cha Umma vitaunda Serikali mpya; Zanzibar sasa ni Jamhuri ya Zanzibar na Pemba; Rais wake atakuwa Sheikh Karume.”
Kisha akamwamuru Karume arudi haraka Zanzibar kuja kuchukua madaraka, akisema kwa sauti ya mamlaka: “Karume, popote ulipo. Rudi haraka kuchukua kazi yako.”
Januari 13, 1964, ambayo ndiyo siku Karume, Hanga na Babu waliporejea kutoka mafichoni Dar es Salaam, Okello alitangaza Baraza lake la Mawaziri likiwa na: Abdallah Kassim Hanga (Makamu wa Rais), Abdulrahman Babu (ambo ya Nje na Biashara); Aboud Jumbe (Afya na Huduma za Jamii); Othman Sharrif (Elimu na Utamaduni); Idris Abdul Wakil (Mawasiliano na Ujenzi), Hasnu Makame (Fedha) na Salehe Saadallah (Kilimo).
Manaibu Waziri walikuwa ni Hassan Nassoro Moyo (Mawasiliano) na Abdul Aziz Twala (Ofisi ya Rais) huku yeye ‘Field Marshal’ akijitangaza kuwa Waziri wa Ulinzi na Utangazaji na Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi, akisema:  “Serikali sasa inaendeshwa na sisi – Jeshi; ni juu ya kila raia kutii amri zetu.”
Hapana shaka kufikia hapo, kwamba John Okello, ndiye aliyeongoza Mapinduzi ya Zanzibar ya Januari 12, 1964; na si Karume, Hanga wala Babu. Hata kama watu hao walikuwa na mipango ya kufanya hivyo, basi, Okelo aliwazidi kete na fikra kwa kutenda kabla yao.
Vyombo vya habari na taasisi za Kimataifa zinakiri hivyo. Gazeti la Tanganyika, The Standard la Januari 13, 1964 liliandika:  “Wapigania Uhuru waliokuwa na silaha wamekiteka Kisiwa cha Zanzibar; wamekamata majengo yote muhimu ya Serikali kwa muda usiozidi saa 24; usiku, Kiongozi wa Mapinduzi (Okello), alitangaza Muundo wa Serikali mpya ya Jamhuri ya Zanzibar na Pemba.”
Keith Kyle, wa Gazeti la ‘The Spector’, aliyekuwa Zanzibar siku ya Mapinduzi, naye aliandika: “Baada ya kukidhibiti Kisiwa cha Zanzibar, Okello alimwalika Abeid Karume kurudi Zanzibar kuchukua nafasi ya Rais asiye Mtendaji.”
Profesa Othman, Mwanazuoni mahiri wa Kizanzibari na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, naye alikiri hilo katika ‘The Influence of Nyerere [1999]’, kwamba: “Uhuru wa Zanzibar ulipatikana Desemba 10, 1963.
“Sultani akiwa mkuu wa nchi, ndani ya majuma matano tu Serikali hiyo ilipinduliwa na ‘Masiha’ mjinga, kiongozi wa wanaharakati, John Okello. Baada ya kipindi kifupi alisimika Baraza la Mapinduzi.”
Jumapili, Januari 19, 1964; Jemedari Okello, akiwa kiongozi halali wa Serikali ya Mapinduzi, aliamua kwenda Dar es Salaam kwa mapumziko na mazungumzo ya kikazi na kiongozi mwenzake, Rais wa Tanganyika, Mwalimu Nyerere, yaliyodumu hadi usiku wa manane; na katika mazungumzo hayo, Mwalimu alimsihi Okello afanye kazi kwa amani na Rais Karume.

Na haikuwa hivyo bali Okello na alizidiwa kete na Mzee Karume na kujikuta katika wimbi la maji ya bahari asio weza kuyaonga maana alijikuta Zanzibar hayupo tena na Tanganyika Nyerere alimtimuwa Uganda ambako ndiko kwao hakukumuweka maana Iddi Amin Dada hataki mchezo akaishia Kenya akiwa kama mtu wa kawaida tu au kigaragosi tu asiye na lolote wala chochote.

KARUME NA MKONO WAKE WA CHUMA NA KUCHOSHWA NA MUUNGANO

Afbeeldingsresultaat voor karume na nyerere
Miaka 40 iliyopita, Aprili 7, 1972; Rais wa Serikali ya awamu ya kwanza ya Mapinduzi na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, ambaye pia alikuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Abeid Amani Karume, aliuawa kwa kupigwa risasi katika mazingira na sababu za kutatanisha.
Risasi nane zilitolewa mwilini kwake mwili wake ulipofikishwa kwenye Hospitali ya V. I. Lemin, mjini Unguja kwa uchunguzi, sawa na idadi ya miaka minane ya utawala wake tangu 1964 hadi kifo chake.
Ilikuwa hivi:  Rais Karume na Makomredi wenzake wa Chama cha Afro-Shirazi (ASP) alikuwa na mazoea ya kucheza karata, damma au dhumuna kwenye ukumbi wa ofisi za makao makuu ya Chama hicho Kisiwandui, kila jioni kama sehemu ya mapumziko.  Siku hiyo alifika saa 11.00 jioni akiwa na walinzi wake, akaingia ndani nao wakabaki nje kulinda.
Ikafika zamu yake kucheza; akawa anacheza na Mzee Maalim Shaha Kombo ambaye alionekana kulemewa.  Ndipo Karume akamwita Mzee Mtoro Rehani ajitayarishe baada ya Kombo, naye akaitikia kwa kuaga kwanza aende msalani kujisaidia.
Sekunde chache baada ya hapo na kabla Mzee Mtoro Rehani hajarejea kutoka msalani, ghafla watu wawili wenye silaha walivamia chumba alimokuwa Karume na wenzake na kumimina risasi wakimlenga; na kufumba na kufumbua, akawa katika dimbwi la damu kimya, amepoteza uhai.  Hakuna mtu mwingine aliyeuawa mbali na kujeruhiwa tu, mmoja wao akiwa Katibu Mkuu wa ASP, (sasa) Hayati Thabit Kombo Jecha.
Risasi uaji (the fatal bullet), mbali ya risasi zote, iliyochukua uhai wa Karume ilitoka kwenye bunduki ya Luteni Hamoud Mohammed  Hamoud wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWT), ambaye ndiye alikuwa kiongozi wa uvamizi huu na aliyefyatua risasi ya kwanza wakati Karume akicheza na wenzake.  Inasemekana, Hamoud aliuawa papo hapo na mlinzi wa Karume.
Wauaji wengine waliofuatana na Hamoud katika uvamizi huo ni Kapteni Ahmada Mohamed, Koplo mmoja wa jeshi ambaye jina lake halijafahamika hadi leo, na raia mmoja aliyekwenda kwa jina la Ali Khatibu Chwaya, ambao inaelezwa wote hao waliuawa kwenye mapambano ya silaha nje ya eneo la tukio.
Dakika chache baada ya mauaji kutokea, alifika Kanali Ali Mahfoudhi na askari mwingine, Kapteni Makame Hamis, wakauchukua mwili wa Karume na kuukimbiza hospitali.
Itakumbukwa, Kanali Mahfoudhi ni mmoja wa vijana wa Umma Party (UP) cha Abdulrahman Mohamed Babu, kilichoungana na ASP baada ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964 na kuunda Serikali ya mseto. Ni kati ya vijana waliopelekwa Cuba kwa mafunzo ya kijeshi, na ni mmoja wa wapiganaji walioendesha mapambano ya kisayansi usiku wa Mapinduzi na kukamata uwanja wa ndege mchana Aprili, 1972.
Ni mmoja wa wanaharakati wa siasa za mrengo wa Kikomunisti ambao hawakutakiwa Zanzibar wakati wa utawala wa Karume, hivi kwamba kufuatia Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Aprili 26, 1964, Karume alishinikiza kwa Nyerere wapewe kazi Tanzania Bara aweze “kupumua” ambapo Mahfoudhi alipewa cheo cha Mkurugenzi wa Operesheni katika JWT.
Wengine ambao hawakutakiwa ni pamoja na Babu mwenyewe aliyepewa Uwaziri wa Mipango ya Uchumi, na kama tulivyoona makala zilizopita, hasimu mwingine wa Karume, Othman Sharrif, ambaye alifanywa Afisa Mifugo wa Mkoa, Mtwara au Mbeya, na Balozi Salim Ahmed Salim wakati huo Balozi wa Zanzibar nchini Misri ikaridhiwa aendelee kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano nchini humo.
Tuache hayo, lakini hapa swali linazuka:  Kwa kuwa Kanali Mahfoudh hakuwa kipenzi cha utawala wa Karume tangu mwaka 1964, ilikuwaje akawa Afisa wa kwanza kuwa kwenye tukio kabla ya maafisa wengine vipenzi, kama vile Kanali Seif Bakari ambaye alikuwa pia Mkuu wa Usalama wa Taifa Zanzibar ambalo halikuwa jambo la Muungano, na wengineo?
Je, alikuwa katika ziara ya kikazi wakati mkasa huu ukitokea au alijua kilichotarajiwa kutokea? Kwa nini alikuwa mmoja wa washitakiwa zaidi ya 100 kwa tuhuma za mauaji hayo, na mmoja wa watuhumiwa 18 miongoni mwa hao walioshitakiwa wakiwa Tanzania Bara, Abdulrahman Babu akiwa mmoja wao.
Kuna dhana mbili kinzani kuhusu jinsi Karume alivyouawa na hatima ya wauaji. Dhana moja inadai kwamba, watu wanne walivamia mahali alipokuwa Karume na wenzake, wakamimina risasi mara nne au mara tano hivi, risasi ya kifo ikampata Karume shingoni akafa, huku zingine zikiendelea kumiminwa kulenga meza walipokuwa.
Inadaiwa kuwa Hamoud aliuawa kwenye eneo la tukio, ambapo wawili waliuawa baadaye na vyombo vya usalama (kwa mapambano?) na mmoja alijiua.
Dhana ya pili inadai kwamba Hamoud alikufa kwenye eneo la tukio katika mazingira ya kutatanisha, ama kwa kujipiga risasi kuepuka kukamatwa hai na kuteswa baada ya kuona asingeweza kutoroka; au alijeruhiwa vibaya na walinzi wa Karume, kisha Ahmada akampiga risasi na kumuua kumwepusha kuteswa na kutoa siri kama angekamatwa hai, kisha (Ahmada) akaweza kutoroka kwenye eneo la tukio.
Juu ya utata huu kuhusu hatima ya wauaji, ni ukweli kwamba ni Luteni Hamoud pekee aliyeuawa kwenye eneo la tukio na washiriki wengine katika mauaji waliweza kutoroka eneo la tukio na baadaye kuuawa katika mazingira yasiyofahamika.
Kufuatia mauaji hayo, watu 1,100 walikamatwa na kuhojiwa juu ya kuhusika au kutohusika kwao na mauaji, wengi wakiwa viongozi na wanachama wa zamani wa Umma Party, chama cha Babu na wanachama mashuhuri wa ASP wenye siasa za mrengo wa kikomunisti.
Inaendelea...
Yote haya yanaturejesha kwenye swali letu la awali:  je, kuuawa kwa Karume kulikuwa na lengo la kulipiza kisasi kwa chuki binafsi, kama baadhi ya watu wanavyodai, au lilikuwa jaribio la Mapinduzi lililoshindwa kwa Serikali ya Mapinduzi? Ni nani huyu Luteni Hamoud Hamoud aliyeongoza mauaji na kwa nini?
Je, lengo lilikuwa ni mauaji hayo pekee au kulikuwa na mpango mkubwa zaidi nyuma? Ukiongozwa na nani?
Kupata majibu ya maswali haya, hatuna budi kuiangalia hali ya kisiasa Zanzibar baada ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964 na baada ya Muungano na Tanganyika, Aprili 26, 1964.
Kama nilivyoeleza katika mfululizo wa makala nne hivi karibuni katika gazeti hili kuhusu jinsi “Field Marshal” John Okello alivyoongoza Mapinduzi ya 1964, na kuundwa kwa Serikali ya Mseto kati ya vyama vya ASP na Umma, lengo kuu la Karume lilikuwa ni kuzivunja nguvu za wanaharakati wa Umma Party na za wakomunisti wa ASP walioshabihiana kimawazo na kimtazamo wa kitaifa na wana-Umma Party na kumnyima Karume usingizi.
Lakini tofauti na matarajio ya Karume, hatua hiyo iliwaleta karibu zaidi wanamapinduzi hao na kumnyima zaidi usingizi kwa hofu ya kupinduliwa, wakimtuhumu kushindwa kuongoza na kusimamia madhumuni ya Mapinduzi Visiwani.
Mungu bariki kwa Karume, ukatokea Muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika mwaka huo, akaona vyema awasambaratishe kwa kuwatafutia nafasi Tanzania Bara ambako wasingeweza kufurukuta.
Waliokumbwa na kadhia hiyo ni pamoja na Abdulrahman Babu (Umma) na aliyepewa Uwaziri wa Mipango na Uchumi kwenye Serikali ya Muungano; Kassim Hanga (ASP) aliyeteuliwa Waziri katika Ofisi ya Rais wa Jamhuri, Mambo ya Muungano; Salim Ahmed Salim (Umma) aliyeteuliwa Balozi nchini Misri.
Wengine ni Othman Sharrif (ASP) aliyeteuliwa Balozi nchini Marekani, lakini Karume akampinga Nyerere akidai hastahili, uteuzi ukafutwa; badala yake akateuliwa kuwa afisa mifugo katika moja ya mikoa ya Kusini Tanzania, Mbeya au Mtwara, na Kanali Ali Mahfoudh (Umma) aliyeteuliwa Mkurugenzi wa Operesheni katika Jeshi la Wananchi (JWT), na wengineo.
Kwa wale wenye maoni tofauti na ya kukosoa Serikali waliobaki Visiwani, hasira ya Karume aliyetawala kwa mkono wa damu iliwashukia, wengi walikamatwa na kutiwa kizuizini na pengine kupoteza au kuuwawa kikatili na katika mazingira ya kutatanisha. Mmoja ya waliouawa kikatili kizuizini ni Mzee (mwanaharakati) Mohamed Hamoud, baba yake Luteni Hamoud Mohamed muuaji wa Karume.
Tangu Mapinduzi ya Januari 12, 1964, Zanzibar haikuwa na Katiba wala Sheria; iliongozwa kwa Amri za Rais  (Presidential Decrees) kadri alivyoona inafaa.  Na kwa mujibu wa Gazeti la “The Tanganyika Standard” la March 9, 1968, Karume aliapa kutofanya uchaguzi wala kuwa na Katiba Kisiwani kwa miaka 50 tangu 1964 - 2014 Kwa madai kwamba  “chaguzi zote ni vyombo vya mabeberu kuwakandamiza wananchi”.
Na kadiri kalamu ya Karume ya wino wa damu ilipozidi kuandika historia ya ukatili, udikteta na umwagaji damu kwenye kurasa ngumu za kukwaruza ndivyo alivyojichongea na kujiongezea upinzani na uadui kwa jamii ya Kizanzibari.
Kufikia mwaka 1967 hofu ya Karume dhidi ya wenzake na kwa nafasi yake ilitia fora kiasi cha kuogopa kivuli chake mwenyewe. Na ili kuendelea kuwamaliza wenzake, mwaka huo zilitungwa tuhuma za uongo dhidi ya watu 14 makada wa ASP katika kumpindua, zikiwalenga hasa wenye fikra za kikomunisti.
Walioingizwa kwenye tuhuma hizo ni pamoja na mawaziri wa Serikali yake mabwana Abdallah Kassim Hanga, Salehe Saadallah Akida, Abdul Aziz Twala na makatibu wakuu wa wizara, Aboud Nadhif na Mdungi Ussi na baadaye Othman Sharrif.
Wote waliokuwa Visiwani walikamatwa, kisha Karume akamwomba Nyerere kuwarejesha Zanzibar kutoka Bara, Othman Sharrif na Hanga ili “wakahojiwe” lakini wote wakaishia kuuawa kikatili bila kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Mmoja wa mashahidi wa uongo walioandaliwa dhidi ya “watuhumiwa” kwa vyombo vya Karume, alikuwa Ahmada ambaye kwa uongo wake, watu wanne akiwamo Hanga, Twala, Saadallah na Othman, walinyongwa mwaka 1969.  Kwa uongo huo, Ahmada alizawadiwa cheo cha kapteni jeshini.  Ni Kapteni Ahmada huyu, aliyeshiriki kwenye mauaji ya Karume miaka mitatu baadaye.
Kwa hofu ya jamii ya Kizanzibari kufikiwa na fikra na mawazo mapya ya kimaendeleo, Karume alipiga marufuku vijana wa Kizanzibari kwenda nje kwa masomo ya juu ikiwa ni pamoja na Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam; alipiga marufuku pia ujenzi wa Chuo Kikuu Visiwani.
Mbali na kutokuwapo kwa utawala wa sheria enzi za Karume, unyanyasaji wa kijinsia na ubaguzi kwa misingi ya historia na kisiasa ulitia fora. Kwa mfano, mwaka 1966, alitoa amri (decree) kuwanyima wazazi haki ya kuwakataa wanaume walioposa binti zao kama njia ya kuondoa ubaguzi wa rangi.
Kwa sababu hii, wasichana, hasa wale wa Kiarabu walilazimishwa kwa nguvu ya Serikali kuolewa kwa nguvu. Karume mwenyewe, wakati huo akiwa na umri wa miaka 65, aliwania kuoa kwa nguvu, wasichana wanne wa Kiajemi, na alipokataliwa, aliamrisha wazazi wao watiwe kizuizini na kuchapwa viboko kwa kosa la kuzuia mpango wa ndoa mchanganyiko, na baadaye kutimuliwa Zanzibar.
Chini ya mpango huo, raia wa kigeni waliotaka kuchumbia wasichana wa Kizanzibari walitakiwa kuilipa Serikali Sh. 64,000,000, bila hivyo hawakuruhusiwa kuwaoa.
Karume alikuwa ameanza kuwa mwiba kwa Mwalimu Nyerere pia juu ya Muungano. Kwa mfano, alimkatalia Nyerere kwa lugha ya dharau na kejeli juu ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea na Azimio la Arusha kutumika Zanzibar.
Na kuhusu akiba ya fedha za kigeni ya Zanzibar iliyofikia dola milioni 80 mwaka 1972, alimuonya asithubutu kuitolea macho, akamwambia:  “Fedha ya kichwa cha Malkia si yako na usiniulize, labda niulize juu ya hii (sh.) yenye picha ya kichwa chako”.
Na kuhusu Muungano, Karume alikuwa ameanza kuchoka nao. Siku moja alisema, “Muungano ni kama koti tu; likikubana unalivua”.
Ufa huu kati ya viongozi hao wawili juu ya Muungano, ndio uliosababisha kamati ya kupendekeza Katiba (Constitutional Committee) isiundwe na Bunge la Katiba (Constitutional assembly) lisiteuliwe ndani ya muda wa mwaka mmoja tangu Muungano, kama ilivyotakiwa chini ya Mkataba wa Muungano wa Sheria ya Muungano ya 1964.
Wadadisi wa mambo ya siasa wanakubaliana kuwa, kama Karume angeendelea kutawala miaka kadhaa baada ya 1972, Muungano ungefikia kikomo kwa njia ya kutisha na kusikitisha.
Kufikia mwaka 1972, upinzani kwa Serikali ya Karume ulikuwa umechukua harakati za uasi wa umma, chini kwa chini kwa mara ya kwanza tangu Hanga na wenzake wanyongwe mwaka 1969.
Inaendelea...
KATIKA sehemu ya kwanza ya makala haya toleo lililopita, tuliona jinsi Rais wa Serikali ya awamu ya kwanza Zanzibar na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Abeid Amani Karume, alivyouawa kikatili na wanajeshi wakati akicheza bao, Aprili 7, 1972 mjini Unguja.
Kwa kifupi, tuliona kwamba, kwa vigezo vyovyote vile vya utawala na uongozi, Karume alitawala kwa mkono wa chuma; alitawala kidikteta katika nyanja zote za maisha ya Wazanzibari kisiasa, kiuchumi na kijamii.   Alikuwa kero pia kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kwa Muungano.
Kwa kusema haya sina maana kwamba Karume hakutenda mema kwa Zanzibar na kwa Wazanzibari; bali najaribu kutafiti tu kuona ni mazingira na sababu zipi zilizochochea na kuharakisha kuuawa kwake; kati ya sababu hizi kuu za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kimuungano.  Kwa vyovyote vile, moja au zaidi ya mambo haya manne yalichangia.
Tunajua kwa mfano, kwa baadhi ya Wazanzibari, Karume alikuwa mtawala mkatili asiye na huruma wala hakujua kusamehe; lakini pia alikuwa na sifa za pekee nzuri kama kiongozi na binadamu; alikuwa mhimili na mtetezi wa Waafrika wa Kizanzibari na hakuyumbishwa na siasa za migogoro Visiwani.
Alikuwa mwenye fikra zenye kujitegemea, alifanya maamuzi yake bila woga wala kuhofia matokeo; alikuwa kiongozi mwenye kuthubutu na mwenye kujituma.
Mwisho tutaona jinsi mpango mzima wa mauaji ulivyoandaliwa kwa wasomaji kuona kama ilikuwa chuki binafsi au mapinduzi.  Si madhumuni ya makala haya kumwona Karume kama dikteta mwema (benevolent dictator) au dikteta katili (ruthless tyrant), maana hilo ni jambo la maoni ya kila mtu binafsi.
Alitawala kwa mkono wa chuma
Tumeona jinsi Karume alivyoitawala Zanzibar kwa mkono wa chuma, na namna alivyowaengua wote aliodhani hawakuwa upande wake, ama kwa kuwahamishia kwenye Serikali ya Muungano, ama kwa kupotea katika mazingira ya kutatanisha.
Sambamba na hatua hiyo, jamii ya Kiarabu wasio Wazanzibari, iliamriwa kuondoka, na wale Waarabu raia waliobaki waliishi chini ya jicho kali la Serikali; waliweza kukamatwa, kama Wazanzibari wengine na kutiwa kizuizini bila kufunguliwa mashitaka.   Walifanyiwa jinsi serikali ilivyofikiri inafaa; mashamba na mali zao zilitaifishwa bila kufidiwa.
Wapo waliohukumiwa na “Mahakama ya wananchi” (tutaiona baadaye), kifungo na kuchapwa viboko kuonyesha kwamba Serikali ya Karume haikuwa ya mchezo; akaionya jamii ya Ki-Athnasheri wa Kiajemi kwamba kama wangeendelea kuleta “mgogoro”, wangefukuzwa wote Zanzibar licha ya kuwa raia.
Alitawala bila Sheria wala Katiba
Karume alitangaza utawala wa chama kimoja cha ASP na kuamrisha kila Mzanzibari mtu mzima, kuwa mwanachama. Kila familia ilitakiwa kutundika picha ya Karume nyumbani; kutofanya hivyo lilikuwa kosa la jinai lenye adhabu kali.
Kikosi cha Usalama wa Taifa chini ya Kanali Seif Bakari, kilichopewa jina la “Viwavi Jeshi”, na kufunzwa Ujerumani Mashariki kikaiva kwa mbinu za utesi na mauaji, kilipewa mamlaka ya kukamata, kutesa, kutia kizuizini na hata kuuwa bila mashitaka.  Yeyote aliyelalamika, hata juu ya upungufu wa chakula tu, aliitwa “adui wa Mapinduzi” na hivyo mhaini.  Enzi hizo, nduguyo akigongewa mlango usiku na kutakiwa kwa mahojiano na Serikali, usingemwona tena milele.
Wakati wa Karume hapakuwa na utawala wa Sheria wala Katiba;  amri za rais (decrees) ndizo zilizotawala nchi.  Mapema mwaka 1966, mfumo wa mahakama wa kawaida ulipigwa marufuku; na Oktoba 1966, rais alijipa madaraka ya kuteua mahakama maalumu za watu wasiozidi 14 wenye mamlaka ya kusikiliza kesi za makosa ya kisiasa kama vile uhaini, uhujumu uchumi na wizi wa mali ya umma.
Mahakama hizi hazikufungwa na kanuni zozote katika kusikiliza kesi; huduma za kisheria kwa watuhumiwa zilifutwa na mawakili kupigwa marufuku Zanzibar.  Upande wa mashitaka ndio uliokuwa pia upande wa utetezi; kwa maana kwamba, mwendesha mashtaka wa serikali alipomaliza kuwasilisha mashtaka dhidi ya mtuhumiwa aligeuka kuwa mtetezi wa mtuhumiwa.
Mahakama hizi zilipewa uwezo wa kutoa hukumu za kifo.  Mwaka huo huo (1966), Baraza la Mapinduzi lilipiga marufuku pia haki ya kukata rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa ya Afrika Mashariki [EACA] na rufaa zote zikawa kwa Rais Karume pekee.
Mwaka 1970, Karume alipitisha amri (decree) ya kuanzishwa mahakama (za kienyeji) za watu watatu.  “Mahakimu” wapya wa mahakama hizo waliteuliwa na Karume mwenyewe kutoka miongoni mwa makada wa ASP.
Moja ya sifa ya kuteuliwa ni kutokuwa msomi wa sheria, na ikiwezekana uwe hujui kusoma na kuandika.  Adhabu ya kifo ilipanuliwa kuingiza makosa kama vile utoroshaji wa karafuu, uhaini na utoaji mimba.   Matumizi ya vidonge vya uzazi wa majira lilikuwa kosa kubwa pia.
Karume alichochea hasira na chuki kubwa ya Wafanyabiashara wa Kiasia mwaka 1971, pale alipowapa notisi ya mwaka mmoja kufungasha virago kwa madai ya kuonekana kudhibiti uchumi wa Zanzibar.  Hasira yao iliungana na ile ya Waarabu ugenini waliofukuzwa mwaka 1964 na kupokonywa mali na mashamba yao bila kulipwa fidia; achilia mbali wale ambao mabinti zao waliozwa kwa nguvu kwa Wazanzibari Waafrika.
Wakati huo huo, Karume aliendelea kuwaachisha kazi na kuwatimua Visiwani, watumishi wa serikali waliojulikana au ndugu zao kuwa wafuasi wa zamani wa vyama vilivyopigwa marufuku vya ZNP na ZPPP na nafasi zao kujazwa na “watiifu” kwake.  Hata hivyo, kwa huruma ya Nyerere, walipewa utumishi serikalini Tanzania Bara.
Mapema mwezi Januari 1972, Waziri mdogo, Ahmed Badawi Qualletin, na afisa mwingine wa Serikali, Alli Sultani Issa, walifukuzwa kazi.  Kisha, Februari 1972, ujumbe mzito wa watu sita ulitumwa kwa Nyerere kumwambia awarejeshe Zanzibar, Abdulrahman Babu na wenzake kadhaa wakahojiwe kwa tuhuma za kutaka kuiangusha Serikali.
Babu ambaye alikuwa bado mwenye ushawishi mkubwa wa kisiasa Zanzibar, na aliyeamua kutorejea Zanzibar ya Karume kwa kuhofia usalama wake, kivuli chake na mzimu wa wahanga wa ukatili vilimtisha na kumnyima usingizi Karume, mithili ya Macbeth kwa mzimu wa Mfalme Duncan na Banquo, aliowaua kwa upanga ili atawale.
Nyerere, kwa kuhofia yaliyompata Hanga, Twala, Othman Sharrif na wengine kutokea alipowarejesha Zanzibar mwaka 1967, safari hii alikataa kumrejesha Babu Zanzibar, ingawa alikubali shinikizo la Karume la kumwachisha uwaziri katika Serikali ya Muungano.
Karume aliwatimua pia wataalamu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) na kufunga Kituo chao cha Utafiti na Udhibiti wa malaria Visiwani kwa madai kwamba, Wazanzibari walikuwa “malaria proof”, yaani hawaguswi wala kuugua malaria.
Kwa hatua hiyo, ugonjwa wa malaria uliongezeka kwa asilimia 45.  Na ingawa Zanzibar ilikuwa na akiba kubwa ya fedha za kigeni, zaidi ya pauni za Uingereza milioni 14 kwenye Benki ya Urusi mjini London, (taarifa nyingine zinadai dola milioni 80), Karume hakuwa tayari kutumia fedha hizo kudhibiti malaria wala kuagiza chakula; badala yake akaona muhimu zaidi kuanzisha kituo cha televisheni ya rangi na ya pekee barani Afrika wakati huo.
Mwaka huo huo (1971), katikati ya mrindimo wa njaa Visiwani, Karume alipiga marufuku uagizaji wa chakula (mchele, sukari, unga wa ngano) kutoka nje, kama hatua ya kujitegemea kwa chakula. 
Hatua hii ilizua tafrani na malalamiko na kusababisha biashara ya magendo ya chakula kushamiri; hapo, “Viwavi Jeshi” na mahakama za “kangaroo” zikapata wahanga kukamatwa, kushitakiwa na kunyongwa.  Watu wengi wakaikimbia Zanzibar. Aprili 1972, ukosefu wa chakula ulikithiri. Ni wakati huo Rais Karume alipouawa ghafla. 
Kwa yote hayo, pamoja na tabia yake ya kutoamini wasomi na kuchukia wataalamu, Karume hatimaye alianza kuchukiwa pia na Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi wenye siasa za mrengo wa ki-Karl Marx.
Karume adha kwa Nyerere na Muungano
Nyerere alikuwa ameyatoa sadaka mengi ya Tanganyika kwa Zanzibar, ilimradi tu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ufikiwe. Kwa mfano, wakati Tanganyika ilipoteza hadhi ya kuwa nchi na baadaye jina lake, pale Muungano ulipobadili jina kutoka “Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar”,  kutwa “Jamhuri ya Muungano wa Tan-zan-ia”, Zanzibar ilibakia kuwa Zanzibar, na Karume akabakia Rais wa Zanzibar na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Tanzania.
Si hivyo tu, Wazanzibari watano walipewa uwaziri kamili katika Baraza la Mawaziri 14 la Muungano.  Na ingawa idadi ya Wazanzibari ilikuwa asilimia tatu tu ya Watanganyika, lakini Zanzibar iliruhusiwa kuwa na Wabunge 52 katika Bunge la Muungano, wakiwamo Wajumbe wote 32 wa Baraza la Mapinduzi.
Licha ya upendeleo huu, Nyerere hakufanikiwa kudhibiti mhimili wa kisiasa Zanzibar chini ya Karume.  Mfano, Zanzibar chini ya Karume, ilikataa kuhamishia kwenye Muungano mambo mengi yaliyopaswa kuwa chini ya Serikali ya Muungano;  kwa mfano, iliendelea kudhibiti jeshi lake la ulinzi na Idara ya Uhamiaji, Karume akiwa amiri jeshi wake Mkuu.  Ndiyo kusema, aliuawa na wanajeshi  wa jeshi lake la Zanzibar, si Wanajeshi wa JWTZ.
Karume alikataa Serikali ya Muungano kugusa akiba ya fedha za kigeni ya Zanzibar, japokuwa fedha lilikuwa jambo la Muungano.  Aidha, Karume na Baraza lake la Mapinduzi walikiuka mara nyingi mapendekezo ya kisera kutoka Bara kiasi kwamba Nyerere hakuwa na kauli tena juu ya sera za kiserikali.
Karume akakataa pia mazungumzo zaidi ya kikatiba kwa hofu ya Zanzibar kupoteza hadhi na mamlaka yake.  Karibu kila alichopendekeza Nyerere, alipata jibu la mkato kutoka kwa Karume:  “Kama hivyo ndivyo, tuvunje Muungano”.
Mitazamo hasi ya viongozi hawa wawili juu ya Muungano, ndiyo iliyosababisha mchakato wa kupata Katiba ya Muungano ndani ya mwaka mmoja kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano usifanyike, na Muungano kuongozwa kwa Katiba ya Muda kwa miaka 13 hadi 1977 na baada ya Karume kufariki.
Nyerere alipowasilisha na kupitishwa kwenye Bunge la Muungano, Mpango wa kwanza wa Maendeleo wa miaka mitano, na kutangaza nia yake kuona unatumika pia Visiwani, Karume aliupinga; akaja na mpango wake tofauti wa miaka mitatu kwa Zanzibar ulioandaliwa na mchumi kutoka Ujerumani Mashariki.
Kwa yote hayo na mengine, Nyerere alianza kuonyesha dhahiri chuki yake kwa utawala wa kimabavu wa Karume.  Naye (Karume) alipotambua hilo, alizuia mwingiliano huru wa watu kati ya Visiwani na Tanzania Bara kwa hofu na kwa sababu zinazofahamika.
Si mara moja, hofu na wasiwasi wa kimaasi vilipojionyesha Zanzibar, mamlaka za usalama zilimshauri Mwalimu kufuta ziara zake Visiwani.  Hofu hizi zilijidhihirisha zaidi pale Othman Sharrif, baada ya uteuzi wake wa Ubalozi Marekani kufutwa kwa shinikizo la Karume na kurejea Zanzibar, alipokamatwa na kutiwa kizuizini bila kosa.
Ilibidi Nyerere aingilie kati na kumwita Karume Ikulu, kuonyesha jinsi alivyochukizwa na kitendo hicho; lakini Karume alimkatalia, kuonyesha kwamba Nyerere hakuwa na mamlaka kwake. Sharriff aliachiwa baadaye kwa hiari ya Karume, na Nyerere akamteua kuwa Afisa Mifugo Tanzania Bara. 
Hata hivyo, Oktoba 1969, wakati Nyerere akiwa ziarani nchi za nje, Sharrif alikamatwa Tanzania Bara na kurejeshwa Zanzibar alikouawa.
Zipi adha nyingine kwa Nyerere?  Ni nani huyu Luteni Hamoud Hamoud?  Kwa nini aliongoza mauaji ya Karume? 
Inaendelea...
KATIKA sehemu ya pili ya makala haya wiki iliyopita, tuliona jinsi Rais Abeid Amani Karume alivyotawala kwa mkono wa chuma bila kufuata katiba wala utawala wa sheria, na hivyo kujitengenezea maadui wengi katika jamii ya Kizanzibari na kwa makada wenzake wa ASP wenye siasa za mrengo wa kushoto ambao, alianza kuwatimua kazi au kuwahamishia kwenye Serikali ya Muungano.
Tulimaliza kwa kuona kwa sehemu tu, jinsi alivyogeuka kuwa adha na kero kubwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kwa Muungano wenyewe, kiasi cha kuuweka Muungano huo kwenye hati hati ya kuvunjika.  Tuendelee na sehemu ya Tatu, kuona kilichofuata.
Karume alikuwa mwiba kwa Nyerere
Mbali ya Karume kuweka wazi kwa kusema kwamba, “Muungano ni kama koti tu; likikubana au kukuzidishia joto unalivua na kuendelea na safari yako”, pia alijipa ujasiri usio wa kawaida kwa kumkatalia Nyerere hadharani kila mara juu ya baadhi ya mambo ya Muungano akisema: “…..kama ni hivyo, sikubali, bora tuvunje Muungano”.
Ni ujasiri huu wa Karume usio wa kawaida juu ya jambo nyeti kama hili, uliofanya Nyerere atoe tamko lake maarufu juu ya hatima ya Muungano akisema:  “Kama watu wa Zanzibar, bila ya ulaghai kutoka nje, wataona ni bora kuvunja Muungano, mimi siwezi hata kidogo kuwapiga mabomu na kuwaua wananchi wa Zanzibar.  Kama waliingia katika Muungano kwa hiari yao, vivyo hivyo wanaweza pia kujitenga kwa hiari yao.  Hatukuishinda Zanzibar (kuwafanya mateka) vitani” (Soma:  William Edgett Smith, “Mwalimu Julius K. Nyerere”, tafsiri ya Kiswahili na Paul Sozigwa, uk. 154).
Wakati Mwalimu alikuwa mstari wa mbele katika kupinga ubeberu wa Marekani wakati wa vita ya Vietnam, na kwa ukombozi wa nchi za dunia ya tatu kwa ujumla, Karume alimbeza na kutangaza adhabu kali Visiwani kwa yeyote aliyelaani na kupinga ubeberu, au kuimba nyimbo za kuikashifu Marekani.
Mwalimu alipokosana na Uingereza kwa nchi hiyo kuukingia kifua utawala wa kidhalimu, kibaguzi na wa mabavu (UDI) wa Ian Smith nchini Rhodesia Kusini (sasa Zimbabwe), na kwa sababu hiyo uhusiano wa Mwalimu na Balozi wa Uingereza nchini, Sir Horace Phillip kuingia mkwara, Karume alionyesha hadharani kila mara kusuhubiana na Balozi huyo kwa kicheko cha bashasha na uswahiba kwa chukizo kwa Nyerere.
Tunaweza kutua kidogo hapa kuangalia nyuma mazingira aliyokuwamo Karume, miezi michache kabla ya kifo chake; bila shaka tutabaini kuwa, kiongozi huyo alikuwa katikati ya uhasama na uadui wa kujitakia.
Kwanza alikuwa na uhasama mkubwa na jamii pana ya Kizanzibari kwa udikteta wake uliokithiri uliosababisha mauaji, watu kutiwa kizuizini au kuhamishiwa Bara.  Pili, kulikuwa na tatizo la njaa na mlipuko wa malaria; mambo ambayo hakuonekana kujali.
Tatu, kulikuwa na uhasama mkubwa wa kisiasa kati yake na makada wenzake wenye siasa za Ki-Karl Marx ndani ya ASP waliomtuhumu kushindwa kuongoza, achilia mbali jamii ya Kiarabu aliyoitimua kikatili Zanzibar na iliyoendelea kutema laana kwake ughaibuni.
Nne,  kulikuwa na Nyerere ambaye alianza kumuona kama mzigo na kero kwa Serikali ya Muungano na kwa siasa za kimataifa.  Yote haya yalikuwa baruti tosha kuweza kulipuka na kumdhuru Karume kwa namna yoyote iwayo.
Ni nani huyu Luteni Hamoud?
Luteni Hamoud Mohamed Hamoud, alikuwa mtoto wa mzee Mohamed Hamoud ambaye alikamatwa na kutiwa kizuizini na Karume miezi kadhaa baada ya Mapinduzi ya Januari 1964, na hatimaye kufariki dunia akiwa kizuizini.
Miaka kadhaa baadaye, wakati Hamoud Hamoud akichukua mafunzo ya kijeshi huko Tashkent nchi iliyokuwa katika  Shirikisho la Urusi ya zamani, alifahamishwa na mmoja wa wanafunzi wenzake juu ya kuuawa kwa baba yake.  Kwa uchungu mkubwa, aliapa sawia na baadaye, kwamba angemuua Karume kulipiza kifo cha baba yake.
Mfumo wa Usalama wa Zanzibar ulioenea kila mahali, ulijulishwa haraka na mmoja wa ma-ofisa usalama waliokuwa kwenye mafunzo pamoja na Hamoud, juu ya kusudio hilo la Hamoud.
Lakini cha kushangaza ni kwamba, Hamoud aliporejea Zanzibar baada ya mafunzo hakukamatwa wala kuwekwa kwenye uangalizi; badala yake alipandishwa cheo kuwa luteni usu, katika sherehe iliyohudhuriwa na Karume mwenyewe kama Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Zanzibar.
Ikumbukwe kuwa, suala la Usalama wa Taifa halikuwa jambo la Muungano; liliongezwa kwenye orodha mwaka 1984 kufuatia kadhia ya Aboud Jumbe ya kuchafuka kwa hewa ya kisiasa Zanzibar, likaunganishwa kusomeka kwa pamoja na jambo la Ulinzi kuwa “Ulinzi na Usalama”.
Pale risasi ya Hamoud ilipochukua uhai wa Rais Karume miezi kadhaa baadaye, Serikali ilisisitiza kwamba, mauaji hayo yalikuwa sehemu ya njama kubwa ya kuangamiza Mapinduzi ya 1964, kutokana kwamba, Hamoud na wauaji wenzake walikuwa wanachama wa zamani wa Umma Party, kilichokiunga mkono ASP huko nyuma, na kukipa [ASP] mwelekeo bora wa kiitikadi [Ukomunisti] na kuheshimika kisiasa.
Kufuatia mauaji hayo, watu 1,100 walikamatwa na kuhojiwa.  Babu alikamatwa na kutiwa kizuizini Tanzania Bara kwa tuhuma za kuongoza mpango mzima; nao maofisa wa ngazi za juu wa Kizanzibari Jeshini Bara, kama Ali Mahfoudh na wengine, nao walishukiwa na kuondolewa kwenye utumishi wa Jeshi Tanzania Bara bila kurejeshwa Zanzibar.
Mgongano dhana ya mauaji
Kuna dhana mbili zinazogongana, lakini zote zenye nguvu; juu ya sababu za kuuawa kwa Karume.  Dhana ya kwanza ni hii ya Hamoud kulipiza kisasi.
Lakini suala la kulipiza kisasi linakoma pale tunapoona watu kama Kapteni Ahmada na raia Ali Chwaya ambao hawakuwa na uhusiano wa kifamilia na marehemu Mohamed Hamoud aliyeuawa, kujiingiza katika kulipiza kisasi.
Lakini, kama tutakavyoona baadaye, Kapteni Ahmada alijiingiza kama hatua tu ya kujisafisha kwa kujutia ushahidi wa uongo aliotoa dhidi ya Hanga na wenzake 18 waliouawa mwaka 1969, na yeye kuonekana kama adui na msaliti wa umma wa Kizanzibari.  Inapofikia hapo, inakuwa dhahiri kwamba mpango huo ulibeba hasira za jamii pana ya Kizanzibari.
Dhana ya pili ambayo ndiyo msimamo wa Serikali ni kwamba, mauaji hayo yalikuwa mpango mpana wa kupindua Serikali.  Dhana hii inapata nguvu kutokana na watu wengi kuhusishwa na tuhuma hizi, lakini kama tu tuhuma dhidi yao zilikuwa za kweli; vinginevyo dhana ya kwanza inashinda.
Mipango ilivyopangwa na kupangika
Chuki binafsi?  Hapana, Hamoud hakuwa peke yake; ilikuwa ghadhabu ya umma kwenye jamii pana ya Kizanzibari, kila kundi au sehemu ya jamii na malalamiko yake.
Kwa mujibu wa taarifa za Usalama wa Taifa Zanzibar, mipango ya kupindua Serikali ya Karume ilianza kusukwa tangu 1967 – 1972 ndani ya Zanzibar na Tanzania Bara, ambako nyumba ya Abdulrahman Babu ilikuwa kituo cha mikutano ya Wazanzibari ya kupanga Mapinduzi hayo.
Kama hivi ndivyo, Karume alikuwa na sababu tosha kumtaka Nyerere kumrejesha Babu Zanzibar “kuhojiwa”, Februari 1972.
Mkutano wa mwisho ulifanyika Aprili 2, 1972, ambapo ilikubaliwa Mapinduzi yatekelezwe Aprili 7, 1972, yakihusisha makundi mawili: kundi la Wazanzibari kutoka Bara, wengi wao wakiwa wanajeshi, na kundi la Wazanzibari ndani ya Zanzibar, likihusisha raia na wanajeshi wachache.
Pamoja na uamuzi huo, kikao kilitoa majukumu mazito kwa baadhi ya washiriki, ikiwa ni pamoja na Hamoud na Ahmada kupewa jukumu la kuiba silaha kutoka kambi ya kijeshi, Bavuai.
Ilikubaliwa kuwa, Babu na wafuasi wake kutoka Bara wasafiri kwa mtumbwi kwenda Zanzibar Aprili 6 kuamkia alfajiri ya Aprili 7, na kufikia eneo lililopo kati ya mitambo mikuu ya mawasiliano [Cable and Wireless] na Klabu Starehe.  Baada ya hapo, Babu abakie amejificha kwenye nyumba ya Hamoud Hamoud, iliyotizamana na Klabu Starehe eneo la Shangani, kusubiri saa ya mapambano kuwadia.
Kwa mujibu wa taarifa, Babu aliondoka Dar es Salaam kwa mtumbwi uliofungwa redio mbili za mawasiliano, jioni ya Aprili 6, safari iliyoelezwa kuwa ya “kuvua samaki”; wakati madhumuni halisi yalikuwa ni kuwafikisha Babu na wafuasi wake Visiwani usiku wa Aprili 6, kwa maandalizi kamili ya kupindua Serikali
Jioni hiyo, Aprili 6, Uongozi wa Jeshi uligundua upotevu wa silaha nyingi Kambini Bavuai.  Na ingawa uongozi ulikuwa bado haujamhusisha mtu yeyote, lakini Hamoud, Hamada na askari wengine walianza kufuatiliwa kwa siri.
Yaelekea kufikia hapo, Babu alijulishwa na kuonywa kwa njia ya redio akiwa baharini, juu ya kugunduliwa kwa mpango mzima wa Mapinduzi; akakatiza safari na kurejea haraka Dar es Salaam hima.  Haijulikani kama wafuasi wake walikuwa wamekwishafika Zanzibar au la; au kama nao walijulishwa na kurejea Dar es Salaam. 
Lakini kuwapo Visiwani wanajeshi kama Kanali Mahfoudh  (Mkurugenzi wa Operesheni JWTZ, Dar es Salaam) na Luteni Hashil Seif (Kikosi cha Wanamaji, Ukonga, Dar es Salaam) saa ya kuuawa Karume, kunaonyesha baadhi yao tayari walikuwa Zanzibar kusubiri wenzao.
Saa 12.00 asubuhi, Aprili 7; Ali Khatibu Chwaya (raia) alikwenda kwa Ali Mshangama Issa (afisa wa tatu, meli M.V. Afrika, mkazi wa Zizi la Ng’ombe, Zanzibar), kumweleza juu ya kutowasili kwa kundi la Dar es Salaam. 
Baadaye asubuhi hiyo, Ali Mshangama, Chwaya, Miraji Mpatani  (karani wa shirika moja, Zanzibar), Mohammed Abdullah Baramia (Mtunza Bohari, Idara ya Elimu), Ahmada na Hamoud, walikutana nyumbani kwa Hamoud na kuonyesha kukerwa na kusikitishwa kwa kutowasili kwa wapanga mapinduzi kutoka Dar es Salaam, hasa wakijua pia kwamba, silaha zilizoibwa bado zilikuwa nyumbani kwa Hamoud, na hatari ya kuweza kugunduliwa.
Ilipofika saa 6.00 adhuhuri siku hiyo, Mshangama, Hashil Seif, Amar Saad Salim, maarufu kama “Kuku” (afisa usafirishaji, Idara ya Siha, Zanzibar) na Chwaya, walikutana nyumbani kwa Amar Saad ambako Mshangama, Hashil Seif na Baramia walipendekeza mpango wa kupindua Serikali uahirishwe hadi watakapopata taarifa tofauti kutoka Dar es Salaam.
Kwa hiyo, saa 9.00 mchana siku hiyo, saa mbili tu kabla ya kuuawa kwa Karume, Baramia alikwenda nyumbani kwa Hamoud eneo la Shangani kuwasilisha pendekezo hilo.  Alimkuta Miraji Mpatani nje ya nyumba na kumweleza Baramia kwamba, pamoja na kundi la Dar es Salaam kutowasili, Ahmada na Hamoud walishikilia Mapinduzi yafanyike tu siku hiyo, kwa sababu Ahmada alikuwa anatafutwa na maafisa wa Jeshi.
Je, ni kwa sababu hii Luteni Hamoud, Kapteni Ahmada na Chwaya waliamua kufanya Mapinduzi, licha ya wenzao kutaka yaahirishwe?.
Inaendelea...