Wednesday, July 24, 2019

SIMULIZI YA MZEE THABIT KOMBO JECHA KUHUSU MAPINDUZI

Afbeeldingsresultaat voor sheikh thabit jecha
Asimulia walivyoihadaa serikali ya wakati huo kwa kuandaa ngoma wanamapinduzi waingie Unguja
Yeye, Aboud Jumbe nusura wamshawishi Sheikhh Karume kuyasitisha saa chache kabla ya kuyatekeleza
THABIT Kombo ‘Jecha’ ni majina ambayo ukiyataja, wakereketwa wa historia ya Zanzibar lazima watapatwa na kigugumizi kwa namna mzee huyu alivyojitolea nusu ya maisha yake kupigania haki za Wazanzibari walio na tamaa ya madaraka na nusu nyingine kuulinda Muungano feki wa Tanganyika na Zanzibar pamoja na hadhi ya Mapinduzi ‘Matukufu’ ya mwaka 1964
Kila Januari 12, 2014, Zanzibar inaadhimisha miaka zaidu ya nusu karne tangu Mapinduzi hayo yaliyouondoa utawala wa kisultani visiwani humo yafanyike, ambapo wakwezi na wakulima waliungana na kusema; “uonevu sasa basi wengi wa wakwezi hao na wakulima walikuwa ni wageni tu sio Wazanzibari. Tunataka visiwa vyetu vilivyotawaliwa kwa miaka mingi bila ridhaa yetu vilejee mikononi mwetu ati wanajinadi.”
Katika kitabu kiitwacho ‘Masimulizi ya Sheikh Thabit Kombo Jecha,’ maneno au simulizi za mwanamapinduzi huyo zilizokusanywa na mwandishi, Luteni Minael-Hosanna O. Mdundo, kinaelezea kwa kina namna mzee huyo alivyokuwa na mchango mkubwa katika historia ya visiwa hivyo kukiangamiza mpaka leo tumaji.
Kama vile kukitia nakshi kitabu hicho kilichosheheni nyaraka mbalimbali muhimu za kihistoria, utangulizi wake uliandokwa kwa ustadi mkubwa na Baba wa Taifa ambaye ndiye Rais wa Kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere.
Mara nyingi Raia wa Kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Karume alipokwama katika masuala mbalimbali, mshauri wake mkubwa alikuwa Sheikh Thabit Kombo na hata Mwalimu Nyerere wakati akiwa Rais na baada ya kustaafu, alimtumia mzee huyu katika mambo mengi ya kisiasa na ushauri.
Kwa maneno yake mwenyewe Mwalimu kwenye utangulizi wa kitabu hicho, anasema: “Sheikh Thabit Kombo ndiye aliyependekeza Karume awe kiongozi wa chama kipya (Afro Shirazi Party – ASP). Karume, naamini kwa moyo na nia safi kabisa, hakutaka kuwa kiongozi wa chama kipya hicho!
“Bila busara, hekima na ujasiri wa Sheikh Thabit, pengine vyama hivyo (African Association na Shirazi Association) visingeungana au kama vingeungana, baadaye ungetokea mzozo kuhusu uongozi.
“Sheikh Thabit alikuwa kiongozi mpendwa, mwenye sifa njema, aliyependwa na watu wa kila rika kwa ushauri… Alikuwa radhi wakati wote kuwasikiliza wanyonge na wakati mwingine hata kuwavumilia wajinga na wakorofi kwa kiwango cha kushangaza.
“Nyumbani kwake na ofisini palikuwa mahali pa watu wa kila aina kuchota busara, wakiingia na kutoka mchana na usiku.”
Sheikh Thabit Kombo aliyezaliwa Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja mwaka 1904, hakubahatika kusoma sana elimu ya darasani (anasema aliishia chumba cha nne tu), lakini Mwenyezi Mungu alimjalia kipaji kikubwa cha kujifunza na kuzungumza kwa ufasaha hata kuweza kuwashawishi watu wenye mioyo migumu kuungana na vyama vya ukombozi wa Zanzibar na vya Afrika.

Anasemaje kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar?

Kuna mambo mengi ya kumzungumzia Sheikh Thabit Kombo, hata tukajaza gazeti zima hatuwezi kuyamaliza, lakini kwa kuwa leo ni siku ya kumbukumbu ya Mapinduzi ya Zanzibar, hatuna budi kumtaja kwa muktadha huo.
Kila mmoja wetu hadi leo hadithi ya Mapinduzi ya Zanzibar inamshangaza, hakuna anayeamini kama wakulima na wakwezi ndio walioyaratibu bila msaada kutoka nje!
Lakini Sheikh Thabit Kombo anasema sababu kubwa ya ufanyika mapinduzi hayo ni madhila ya Waarabu waliyowafanyia wakazi wa Zanzibar, ambayo mengine hayasimuliki kwa namna yalivyokuwa mabaya!  
Katika mazungumzo yake na Luteni Minael-Hosanna kuhusu Mapinduzi ya Januari 1964, Sheikh Thabit Kombo anasema: “Usiniulize vijana wetu walioendesha Mapinduzi walipata wapi mafunzo au nani hasa alivamia mahala gani. Mimi sijui.
“Nasikia hadithi tu kila mmoja akijinasibu baada ya kushinda, mengine ya kweli na mengine ya uwongo mtupu.
“Ninachojua mimi ni kwamba Kamati Kuu ya ASP (wakati huo yeye akiwa ni Katibu Mkuu wa ASP) ilikaa ikasononeka sana baada ya mkutano wa pili wa London (uliojadili uhuru wa Zanzibar na kuendelea kumpa Sultani mamlaka).
“Tumesononeka kwa sababu matumaini yetu yote ya kuupata uhuru wa nchi yetu kwa njia ya vote (kura) yalikuwa yamefutika; iliyobaki sasa nchi kutawaliwa maisha yetu yote na vijitu vichache ambavyo vinafurahia sana dhuluma dhidi ya Mwafrika kama ilivyo sasa vijitu vii chache vya CCM wanafurahia maisha wengi wa Wazanzibari wako ktk hali ngumu sana.
“Hatimaye tukazaa shauri kwamba baada ya uhuru huo bandia (Desemba 10, 1963), ‘British Resident’ (Kiongozi Mkazi Mwingereza) akitoka tu, basi tushike mapanga tumng’oe Sultani. Uamuzi huo najua tena wote tulikuwa na kauli moja katika siri yetu kubwa na Mwenyezi Mungu akatubarikia katika dua letu.”
Hata hivyo, Mapinduzi hayakuwa rahisi bali kuliingia fitina nyingi ambazo kwa namna moja au nyingine zilianza kuwakatisha tamaa wanamapinduzi hao, Sheikh Thabit Kombo, anaelezea kisa kimoja usiku wa kuamkia siku ya Mapinduzi.
“Saa tano asubuhi Januari 11, 1964, ulikuwa ndio wakati wa kukamilisha mipango yote na kufanya marekebisho ya mwisho kama hapana budi. Tukakutana Sheikh Karume, Aboud Jumbe na mimi, viroho vinatudunda.
“Mimi nilikuwa nimepata fununu kuwa huenda mipango yetu imegundulika. Basi baada ya mkutano wetu, nikamshauri Sheikh Karume kwa hii habari yetu ya Mapinduzi inaonekana imeenea katika mji mzima, watu wanaizungumza, Aboud Jumbe naye akathibitisha kuwa na yeye kaisikia Miembeni. Basi tukaulizana tufanyeje,” anaeleza Sheikh Thabit.
Katika maelezo yake anasema walikubaliana kumuita Ofisa wa Polisi Unguja wamweleze kuwa kuna watu wanataka kufanya vurugu mjini, hivyo polisi waimarishe ulinzi. Lengo la kufanya hivyo ni kuwa ili machafuko yakitokea basi wao wawe katika mikono salama.
“Kumbe fikira ile ya kumwita Superintendent (Ofisa wa Polisi) ilikuwa mbinu ya kufaa sana, maana askari waliokuwako Bomani walipunguzwa nguvu na vikosi vya Mapinduzi vikaweza kuingia Bomani kwa urahisi na kuchukua silaha,” Sheikh Thabit Kombo (UK.134).
Kwa maelezo ya Sheikh Thabit Kombo, vikosi vya Mapinduzi viliingia maeneo ya mjini ambako siku hiyo kulikuwa na sherehe ya ‘Fete’ kuanzia saa 10 jioni, sherehe ilifanyika na watu wa kila rangi walikusanyika kwa furaha bila hofu.
Sherehe hiyo iliandaliwa na ASP ili kuwawezesha wakulima na wakwezi waliokuwa wakiishi mashambani, kuingia Unguja mjini bila vikwazo au vizuizi kutoka serikalini kama ilivyokuwa kawaida hasa nyakati za jioni kipindi hicho.
Kama walivyoagizwa na utawala wa Kisultani kuwa sherehe ilipaswa kuisha saa sita usiku, ulipotimu muda huo, ngoma zikazimwa na hapo ndipo ikawa mwanzo wa utekelezaji wa mipango ya Mapinduzi.
“Kwa mawe, marungu na mapanga, vijana hawa wakawa na ujasiri wa kushambulia makao makuu ya Jeshi la Polisi na kuyateka haraka haraka. Halafu wakakamata Ziwani. Hapo walipata silaha nyingi na walikuwapo waliokuwa wanajua kuzitumia, hivyo hivyo wakateka kituo cha Mtoni.
“Kivumbi kikawa Malindi, kule kulitokea mapambano makali, lakini moyo wa vijana wa ASP ambao sasa walikuwa wanatumia silaha (za moto) walizokuwa wamejinyakulia Ziwani na Mtoni, ukawasukuma hadi wakashinda. Haukupita muda wakawa wameikamata Malindi pia.
“Rahaleo ndiko kulikokuwa Makao Makuu ya Mapinduzi na Sheikh Karume alikuwa kule tokea usiku hadi alfajiri wakati sehemu zote muhimu zimekwisha kushikwa na vijana wetu wote wanazo silaha. Sasa mapinduzi yakatangazwa katika Sauti ya Zanzibar,” anasimulia Sheikh Thabit Kombo (UK.134)
Awali Sheikh Thabit Kombo, alimtaja John Okello, Abdallah Natepe na Yusuf Himid kama miongoni mwa vijana waliokuwa mstari wa mbele katika kutekeleza Mapinduzi, lakini akikiri kutomfahamu vyema Okello.

Sultani otoroka
Kuhusu Sultani kuikimbia Zanzibar wakati wa Mapinduzi, Sheikh Thabit Kombo anasimulia: “Sultani hakukamatwa. Wakati vijana wanashughulikia vile vituo muhimu, yeye akapata nafasi ya kupuruchuka na kukimbilia melini na meli yake ikaeleaelea karibu na Unguja kwa muda mrefu.
“Kwa bahati nzuri sana Mwalimu Nyerere akaombwa na Serikali ya Uingereza amhifadhi Sultani hadi hapo mipango ya kumsafirisha itakapokamilika.
“Na Mwenyezi Mungu akampa Mwalimu Nyerere busara kubwa ya kulikubali ombi hilo haraka haraka. Kutahamaki, Sultani keshafika Dar es Salaam, mgeni wa Mwalimu Nyerere.
“Hata sisi (viongozi wa ASP) tulikuwa na hofu juu ya Sultani aliyepuruchuka, kama angepata akili kwenda Pemba na halafu kutoka kule akaomba msaada wa majeshi kutoka nchi za nje, hali yetu ingekuwa ngumu sana.”
SEMA HAKUWA NA AKILI HIZO MAANA HAKUJUWA CHOCHOTE KATUACHA KATIKA MASHAKA NA DHIKI MPAKA LEO HII 2019 TUNAELEKEA 2020 TUMO TABUNI YEYE SALAMA SALMINI NA FAMILIA YAKE UINGEREZA.

No comments:

Post a Comment