Wednesday, July 24, 2019

TUKAE MKAO WA KULA KWA KAMPENI ZIJAZO NA AKILI ZETU VISIWANI

Afbeeldingsresultaat voor zanzibar
KAMPENI ZA KWETU NA USHUKU WA AKILI ZETU VISIWANI
Na: Mwandishi Maalum
Kuna watu hadi leo bado wanashangaa kwa nini Zanzibar imeshindwa kujikwamua na makucha ya ukoloni mpya uliojengwa kwa misingi ya hadaa iitwayo Muungano. Kwa lugha nyepesi Zanzibar haijapata kuwa huru, tusidanganyane. Lakini hali hii pamoja na kuwa inachangiwa na mataifa makubwa ya magharibi, mchango wetu sisi wananchi wa Zanzibar kama Zanzibar ni mkubwa mno katika kujihakikishia kuwa tunabakia kuwa watumwa wa ukoloni usiokwisha wa Mkoloni Mweusi Tanganyika.
Nina kila aina ya ushahidi kuwa Wazanzibari wenyewe wanapenda kutawaliwa dumu daima. Kwa mfano, Zanzibar ilitawaliwa na Mwarabu kwa miaka karibu mia mbili. Hakukuwa na lolote la maendeleo tulilofanyiwa zaidi ya lile la kuchanganya damu baadhi yetu na kisha kuishi katika dhambi ya kubaguana kwa makabila. Dhambi ambayo bado ipo baina ya Wazanzibari wenyewe, ilhali wote au tuseme asilimia 99 tukiwa Waislamu. Na juu ya madhila yote tuliyofanyiwa, najua wengine watapinga lakini hakuna mkoloni mwema ingawa kuna watu wengi Zanzibar wanaojitanibu na Uarabu na hata wanatamani bado nchi hii ingekuwa chini ya Utawala wa OMAN. Hili moja tu.
Ushahidi wa pili kuwa sisi ni watumwa wa akili zetu, ni pale mwenyezi Mungu anaposema kuwa hatabadilisha katika watu jambo mpaka wao watakapotaka libadilike. Sasa hapa utaona, kwa vile hadi leo tunasifia na kuutamani ukoloni wa Mwarabu, wenzetu wenye nguvu ya mataifa yenye nguvu zaidi ya Waarabu, wakaitumia fursa hiyo kututawala. Wametutawala sio kwa lazima, bali kwa akili na mapenzi yetu. Hapa namaanisha kuwa akili ya Mzanzibari haijawahi kuwa huru na kwa maana hiyo, akili isiyo kuwa huru haina haja ya kupewa uhuru. Itabakia kuwa akili ya kiutumwa tu!
Sababu kubwa ya kuwa tunabakia kifungoni kama nilivyotangulia kusema, ni akili zetu. Ni uhakika kuwa wengi wetu tumenyimwa elimu ya kujitambua lakini pia hata baada ya zama za ukweli na uwazi kufika, bado inakuwa vigumu sana kwa Mzanzibari kujikwamua na makucha ama ya ukoloni mweusi na ule ukoloni wa Viongozi ambao hawana la kuwapa wananchi zaidi ya lugha chafu kila ifikapo siku za kampeni za uchaguzi na kuwadanganya tutafanya hivi na vile na hakuna moja walilo fanya zaidi ya nusu karne sasa.
Mfano mwingine ulio hai, ukitaka kujua kwa kiasi gani akili zetu na zile za viongozi wetu zimefilisika, sikiliza kampeni zetu za siasa hasa majira au tuseme msimu kama huu wa uchaguzi. Nijuavyo, na uzoefu wangu unaonyesha kuwa, watu huenda kampeni kusikiliza mipango ya wagombea juu ya murua wao na wa nchi yao. Kwa kuwa muwazi na fasaha zaidi, watu huenda kwenye kampeni kusikiliza ni kiongozi au chama gani kina sera na ilani nzuri ya maendeleo kwao ili wapate waamue nani wamchague. Hivi ndivyo kampeni za watu wenye akili timamu zinavyofanywa. Kwetu sisi hali haiko hivyo!
Ukitaka kuthibitisha fuatilia mikutano yote ya vyama vya siasa inayofanyika hapa kwetu. Tena hasa hasa mikutano ya chama fulani hivi. Utakutia mkutano wa kampeni wa masaa matatu mazima unahutubiwa na viongozi wasiopungua kumi, na hakuna hata mmoja anayezungumza la maana zaidi ya matusi. Tena matusi ambayo wale wanaoyazungumza, hawathubutu hata kuyazungumza majumbani mwao lakini ktk jukwa la kampeni wanatukana kama hawana akili vizuri hiyo ndio barabara,viwanda,hospitali,umeme,maji,skuli,elimu wanao wahidi wananchi matusi.
Kinachoshangaza sana ni kuwa, ikiwa huwezi kutumia matusi ya namna ile nyumbani kwenu au kwako, kuna haja gani uyaseme hadharani kwenye uwanja uliojaa watu – wazee, watu wenye heshima zao na hata viongozi wa dini, achilia mbali mastuhu zako na mastuhu wa wenzako?
Kampeni za kwetu visiwani, tangu kuanza kwa vyama vingi, imekuwa matusi ndio ilani ya vyama na sera zao. Na cha kushangaza wananchi, wengi wao wakiwa watu wazima waliojistiri vizuri, husafiri masafa marefu kufuatilia kampeni kama hizi kusikiliza matusi ya nguoni tu nakuchekelea!
Hili kwa kweli linanifanya nizihakiki upya akili za watu wetu hapa visiwani. Pia hali hii inanipa bishara kuwa kwa akili zetu zilivyo, maendeleo yatabakia kuwa ndoto kwani hakuna maendeleo kwa watu waliotawaliwa na wakoloni. Hakuna maendeleo pia kwa watu ambao ni watumwa wa akili zao mbovu. Na kwa maana hii, tutabakia kuwa hivi milele iwapo hatukubadilika.
Kampeni za vyama vya siasa za visiwani siku hizi ni zaidi ya kashfa. Tena kashfa ambazo hazina sitaha wala hazijali nani yupo na nani hayupo. Nani namstahi na nani simstahi. Awepo mkubwa awepo mdogo, matusi ndiyo ilani na sera ya vyama vyetu vya siasa. Kampeni zetu badala ya kutuambia kuhusu sera za kilimo, uvuvi, na maendeleo kwa ujumla zinatumia historia ya watu waliopata vyeo kwa kupiga ama kucheza Sunsumia.
Badala ya kampeni zetu kutuambia vipi ilani zao zitaboresha elimu ambayo kwa hakika inakufa kibudu kila uchao, tunaambiwa habari za vipi kiongozi fulani alipatikana ndani ya ndoa ya mama yake na baba yake. Kwa mfano, Kiongozi wa siasa anayetaka chama chake tukipigie kura, anathubutu kumsema mtu mzima mwenzake kuwa mama yake asingemzaa kama hakutoka nje ya ndoa ya baba yake. Maneno kama haya na mengine, tumeyazoea kuyasikia katika kampeni za kwetu na cha aibu zaidi, waliopo wote wanafurahia kusikia hivyo.
Nilitarajia kuwa kampeni zetu zitazungumzia namna gani zitaboresha huduma za afya kwa wananchi. Hilo sijalisikia kamwe kwa kweli. Badala yake, nasikia kuwa kiongozi fulani anataja msururu wa viongozi anaodai ni mashoga na wengine waliouza kaburi za baba zao. Haya kweli tuseme yametendeka, lakini yanatuhusu nini sisi kama wananchi ambao tunataka maendeleo yetu na ya nchi yetu?
Itatusaidia nini sisi kujua kuwa kiongozi fulani ni shoga au alikuwa mwanachama wa Sunsumia? Hii ina mshabaha gani na maendeleo yetu? Inatusaidia nini Wazanzibari kujua eti fulani mama yake kaolewa kwa mahari ya shilingi 500 alizogaiwa na kiongozi fulani na kisha akauza kaburi la baba au mama yake?
Ukweli, yote haya hayatusaidii kitu na wala si maneno ambayo watu wenye akili timamu wanaweza kuyajadili hadharani. Pia si maneno ambayo watu wenye akili timamu wanaweza kuyafuatilia kwenye kila mikutano tena kwa kusafiri masafa kuyapigia ngoma na kofi kwa kuyafurahia, ilhali huko makwao hakuna waliloacha kutokana na nchi yao kufilisika kimaendeleo. Inashangaza sana kwa kweli kuona watu wetu bado wanashabikia vyama ambavyo vimekuwa vikipata kura kwa umahiri wao wa kutukana na sio sera za maendeleo ya kweli.
Kwa hali hivi iendavyo, sasa natilia mashaka kwa kuhoji iwapo akili zetu Wazanzibari ziko sawa ama kwa lugha nyepesi naweza kusema inaonyesha hatujatulia. Na kwa hali hii hatuwezi kupata maendeleo wala kufika popote! Tutabakia kwenda katika kampeni kufurahia matusi ya viongozi ambao wapo kwa ajili ya neema zao tu na hawana cha kutupa sisi wanyonge isipokuwa lugha ya matusi iliyotokana na kufilisika kwao kisiasa. Kufilisika ambako kunazifilisi akili zetu pia na kutufanya tuamini kuwa viongozi wajuzi wa kutukana tu ndio wanaoweza kutuletea maendeleo katika visiwa vyetu. Tubadilike wananchi.

PIC ZA HISTORIA YA NCHI YA TANGANYIKA JAPO HAMUITAKI NCHI YENU YA TANGANYIKA


Hii Picha Ilipigwa Siku ya Nyerere Alipoweka Jiwe la Msingi Chuo Kikuu Cha Waislam, Chang'mbe 1968 Nyerere Anapeana Mkono na Mufti Sheikh Hassan bin Amir ...

Hii Picha Ilipigwa Siku ya Nyerere Alipoweka Jiwe la Msingi Chuo Kikuu Cha Waislam, Chang'mbe 1968 Nyerere Anapeana Mkono na Mufti Sheikh Hassan bin Amir ...

Uongozi wa East African Muslim Welfare Society katika ni Solomon Eliufoo (Waziri wa Elimu) na Tewa Said Tewa (Territorial President EAMWS) kulia kabisa aliyevaa kanzu na kilemba ni Mufti Sheikh Hassan bin Amir

uhuru day,people go berserk-kwa mbali naona ki bajaj kumbe hizi bajaj ni za siku nyingi

L - R: Sheikh Suleiman Takadir aka Makarios, John Rupia, Julius Nyerere na Bantu Group 1955

Kutoka Kushoto:Iddi Faiz Mafongo(Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na TANU),Sheikh Mohamed Ramia(Khalifa wa Qadiriyya),Julius Nyerere,Saadani Abdu KandoronaHaruna Taratibu. Picha imepigwa Dodoma

Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Al Habib Omar bin Ahmed bin Abubakar bin Sumeit Nyuma Yake ni Ali Mwinyi Tambwe, Abbas Sykes na Chini ni Sheikh Kassim bin Juma



ofisi ya taa kamba ya kuwa ofisi ya tanu

bara za wazee walio anzisha cha cha taa na kuwa tanu ndio hili


Aliyekaa Katikati ni Ilunga Hassan Kapungu na Kushoto Kwake ni Ali Salum Mkangwa na Aliyesimama Nyuma ni Mwandishi

Aliyesimama wa kwanza kulia ni Mzee Ali Msham mwenyekiti wa tawi la TANU Magomeni Mapipa wakati TANU inawaunganisha wananchi kupigania uhuru wa Tanganyika.
Bibi Titi Mohamed, Nyerere na John Rupia Mkutano wa TANU Jangwani, Dar es Salaam 1950s

Bi titi Mohamed akiwahubiri watanganyika kugombania uhuru wa nchi yao ya tanganyika



mkutano wa tanu

Urambo House, Tabora, mwaka 1951. siku hizi mnaita saloon nchini tanganyika

Kushoto Mohamed Jumbe Tambaza na Kulia ni Mshume Kiyate mashuja wa uhuru wa nchi ya tanganyika walio sahauliwa

Tawi hili la TANU Magomeni Mapipa lilikuwa na nguvu na viongozi mashuhuri wa TANU walifika mara nyingi kuzungumza na wanachama na viongozi wao.

gari la tanu nchini tanganyika


Ali Msham aliyekaa katikati katika moja ya mikutano ya ndani ya TANU aliyokuwa akifanya uani nyumbani kwake Mtaa wa Jaribu, Magomeni Mapipa

Bibi Titi Mohamed (1926 - 2000) Shujaa wa Uhuru wa Tanganyika

Waliosimama wa pili kushoto ni Ali Msham (Mwenyekiti wa Tawi la Magomeni Mapipa) na wa nne ni Bi. Khadija biti Jaffar wa tano Bi. Mtendwa biti Iddi Sudi,

Ofisi ya TANU Mtaa wa Jaribu Magomeni Mapipa kama ilivyokuwa ikionekana katika miaka ya 1950 ikiwa imezungikwa na wanachama wake.


.............?????????????????????????????.....................NDANI YA GININGI DODOMA NCHINI TANGANYIKA


GININGI DODOMA NCHINI TANGANYIKA

HII WALIPO KUTANA JIJINI DAR ES SALAAM IKULU YA NCHI YA TANGANYIKA
MBONA HUJA APISHWA NA 2020 HIYOOO INAKUJA WAPE UKWELI WAZANZIBARI MAALIM.

SIMULIZI YA MZEE THABIT KOMBO JECHA KUHUSU MAPINDUZI

Afbeeldingsresultaat voor sheikh thabit jecha
Asimulia walivyoihadaa serikali ya wakati huo kwa kuandaa ngoma wanamapinduzi waingie Unguja
Yeye, Aboud Jumbe nusura wamshawishi Sheikhh Karume kuyasitisha saa chache kabla ya kuyatekeleza
THABIT Kombo ‘Jecha’ ni majina ambayo ukiyataja, wakereketwa wa historia ya Zanzibar lazima watapatwa na kigugumizi kwa namna mzee huyu alivyojitolea nusu ya maisha yake kupigania haki za Wazanzibari walio na tamaa ya madaraka na nusu nyingine kuulinda Muungano feki wa Tanganyika na Zanzibar pamoja na hadhi ya Mapinduzi ‘Matukufu’ ya mwaka 1964
Kila Januari 12, 2014, Zanzibar inaadhimisha miaka zaidu ya nusu karne tangu Mapinduzi hayo yaliyouondoa utawala wa kisultani visiwani humo yafanyike, ambapo wakwezi na wakulima waliungana na kusema; “uonevu sasa basi wengi wa wakwezi hao na wakulima walikuwa ni wageni tu sio Wazanzibari. Tunataka visiwa vyetu vilivyotawaliwa kwa miaka mingi bila ridhaa yetu vilejee mikononi mwetu ati wanajinadi.”
Katika kitabu kiitwacho ‘Masimulizi ya Sheikh Thabit Kombo Jecha,’ maneno au simulizi za mwanamapinduzi huyo zilizokusanywa na mwandishi, Luteni Minael-Hosanna O. Mdundo, kinaelezea kwa kina namna mzee huyo alivyokuwa na mchango mkubwa katika historia ya visiwa hivyo kukiangamiza mpaka leo tumaji.
Kama vile kukitia nakshi kitabu hicho kilichosheheni nyaraka mbalimbali muhimu za kihistoria, utangulizi wake uliandokwa kwa ustadi mkubwa na Baba wa Taifa ambaye ndiye Rais wa Kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere.
Mara nyingi Raia wa Kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Karume alipokwama katika masuala mbalimbali, mshauri wake mkubwa alikuwa Sheikh Thabit Kombo na hata Mwalimu Nyerere wakati akiwa Rais na baada ya kustaafu, alimtumia mzee huyu katika mambo mengi ya kisiasa na ushauri.
Kwa maneno yake mwenyewe Mwalimu kwenye utangulizi wa kitabu hicho, anasema: “Sheikh Thabit Kombo ndiye aliyependekeza Karume awe kiongozi wa chama kipya (Afro Shirazi Party – ASP). Karume, naamini kwa moyo na nia safi kabisa, hakutaka kuwa kiongozi wa chama kipya hicho!
“Bila busara, hekima na ujasiri wa Sheikh Thabit, pengine vyama hivyo (African Association na Shirazi Association) visingeungana au kama vingeungana, baadaye ungetokea mzozo kuhusu uongozi.
“Sheikh Thabit alikuwa kiongozi mpendwa, mwenye sifa njema, aliyependwa na watu wa kila rika kwa ushauri… Alikuwa radhi wakati wote kuwasikiliza wanyonge na wakati mwingine hata kuwavumilia wajinga na wakorofi kwa kiwango cha kushangaza.
“Nyumbani kwake na ofisini palikuwa mahali pa watu wa kila aina kuchota busara, wakiingia na kutoka mchana na usiku.”
Sheikh Thabit Kombo aliyezaliwa Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja mwaka 1904, hakubahatika kusoma sana elimu ya darasani (anasema aliishia chumba cha nne tu), lakini Mwenyezi Mungu alimjalia kipaji kikubwa cha kujifunza na kuzungumza kwa ufasaha hata kuweza kuwashawishi watu wenye mioyo migumu kuungana na vyama vya ukombozi wa Zanzibar na vya Afrika.

Anasemaje kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar?

Kuna mambo mengi ya kumzungumzia Sheikh Thabit Kombo, hata tukajaza gazeti zima hatuwezi kuyamaliza, lakini kwa kuwa leo ni siku ya kumbukumbu ya Mapinduzi ya Zanzibar, hatuna budi kumtaja kwa muktadha huo.
Kila mmoja wetu hadi leo hadithi ya Mapinduzi ya Zanzibar inamshangaza, hakuna anayeamini kama wakulima na wakwezi ndio walioyaratibu bila msaada kutoka nje!
Lakini Sheikh Thabit Kombo anasema sababu kubwa ya ufanyika mapinduzi hayo ni madhila ya Waarabu waliyowafanyia wakazi wa Zanzibar, ambayo mengine hayasimuliki kwa namna yalivyokuwa mabaya!  
Katika mazungumzo yake na Luteni Minael-Hosanna kuhusu Mapinduzi ya Januari 1964, Sheikh Thabit Kombo anasema: “Usiniulize vijana wetu walioendesha Mapinduzi walipata wapi mafunzo au nani hasa alivamia mahala gani. Mimi sijui.
“Nasikia hadithi tu kila mmoja akijinasibu baada ya kushinda, mengine ya kweli na mengine ya uwongo mtupu.
“Ninachojua mimi ni kwamba Kamati Kuu ya ASP (wakati huo yeye akiwa ni Katibu Mkuu wa ASP) ilikaa ikasononeka sana baada ya mkutano wa pili wa London (uliojadili uhuru wa Zanzibar na kuendelea kumpa Sultani mamlaka).
“Tumesononeka kwa sababu matumaini yetu yote ya kuupata uhuru wa nchi yetu kwa njia ya vote (kura) yalikuwa yamefutika; iliyobaki sasa nchi kutawaliwa maisha yetu yote na vijitu vichache ambavyo vinafurahia sana dhuluma dhidi ya Mwafrika kama ilivyo sasa vijitu vii chache vya CCM wanafurahia maisha wengi wa Wazanzibari wako ktk hali ngumu sana.
“Hatimaye tukazaa shauri kwamba baada ya uhuru huo bandia (Desemba 10, 1963), ‘British Resident’ (Kiongozi Mkazi Mwingereza) akitoka tu, basi tushike mapanga tumng’oe Sultani. Uamuzi huo najua tena wote tulikuwa na kauli moja katika siri yetu kubwa na Mwenyezi Mungu akatubarikia katika dua letu.”
Hata hivyo, Mapinduzi hayakuwa rahisi bali kuliingia fitina nyingi ambazo kwa namna moja au nyingine zilianza kuwakatisha tamaa wanamapinduzi hao, Sheikh Thabit Kombo, anaelezea kisa kimoja usiku wa kuamkia siku ya Mapinduzi.
“Saa tano asubuhi Januari 11, 1964, ulikuwa ndio wakati wa kukamilisha mipango yote na kufanya marekebisho ya mwisho kama hapana budi. Tukakutana Sheikh Karume, Aboud Jumbe na mimi, viroho vinatudunda.
“Mimi nilikuwa nimepata fununu kuwa huenda mipango yetu imegundulika. Basi baada ya mkutano wetu, nikamshauri Sheikh Karume kwa hii habari yetu ya Mapinduzi inaonekana imeenea katika mji mzima, watu wanaizungumza, Aboud Jumbe naye akathibitisha kuwa na yeye kaisikia Miembeni. Basi tukaulizana tufanyeje,” anaeleza Sheikh Thabit.
Katika maelezo yake anasema walikubaliana kumuita Ofisa wa Polisi Unguja wamweleze kuwa kuna watu wanataka kufanya vurugu mjini, hivyo polisi waimarishe ulinzi. Lengo la kufanya hivyo ni kuwa ili machafuko yakitokea basi wao wawe katika mikono salama.
“Kumbe fikira ile ya kumwita Superintendent (Ofisa wa Polisi) ilikuwa mbinu ya kufaa sana, maana askari waliokuwako Bomani walipunguzwa nguvu na vikosi vya Mapinduzi vikaweza kuingia Bomani kwa urahisi na kuchukua silaha,” Sheikh Thabit Kombo (UK.134).
Kwa maelezo ya Sheikh Thabit Kombo, vikosi vya Mapinduzi viliingia maeneo ya mjini ambako siku hiyo kulikuwa na sherehe ya ‘Fete’ kuanzia saa 10 jioni, sherehe ilifanyika na watu wa kila rangi walikusanyika kwa furaha bila hofu.
Sherehe hiyo iliandaliwa na ASP ili kuwawezesha wakulima na wakwezi waliokuwa wakiishi mashambani, kuingia Unguja mjini bila vikwazo au vizuizi kutoka serikalini kama ilivyokuwa kawaida hasa nyakati za jioni kipindi hicho.
Kama walivyoagizwa na utawala wa Kisultani kuwa sherehe ilipaswa kuisha saa sita usiku, ulipotimu muda huo, ngoma zikazimwa na hapo ndipo ikawa mwanzo wa utekelezaji wa mipango ya Mapinduzi.
“Kwa mawe, marungu na mapanga, vijana hawa wakawa na ujasiri wa kushambulia makao makuu ya Jeshi la Polisi na kuyateka haraka haraka. Halafu wakakamata Ziwani. Hapo walipata silaha nyingi na walikuwapo waliokuwa wanajua kuzitumia, hivyo hivyo wakateka kituo cha Mtoni.
“Kivumbi kikawa Malindi, kule kulitokea mapambano makali, lakini moyo wa vijana wa ASP ambao sasa walikuwa wanatumia silaha (za moto) walizokuwa wamejinyakulia Ziwani na Mtoni, ukawasukuma hadi wakashinda. Haukupita muda wakawa wameikamata Malindi pia.
“Rahaleo ndiko kulikokuwa Makao Makuu ya Mapinduzi na Sheikh Karume alikuwa kule tokea usiku hadi alfajiri wakati sehemu zote muhimu zimekwisha kushikwa na vijana wetu wote wanazo silaha. Sasa mapinduzi yakatangazwa katika Sauti ya Zanzibar,” anasimulia Sheikh Thabit Kombo (UK.134)
Awali Sheikh Thabit Kombo, alimtaja John Okello, Abdallah Natepe na Yusuf Himid kama miongoni mwa vijana waliokuwa mstari wa mbele katika kutekeleza Mapinduzi, lakini akikiri kutomfahamu vyema Okello.

Sultani otoroka
Kuhusu Sultani kuikimbia Zanzibar wakati wa Mapinduzi, Sheikh Thabit Kombo anasimulia: “Sultani hakukamatwa. Wakati vijana wanashughulikia vile vituo muhimu, yeye akapata nafasi ya kupuruchuka na kukimbilia melini na meli yake ikaeleaelea karibu na Unguja kwa muda mrefu.
“Kwa bahati nzuri sana Mwalimu Nyerere akaombwa na Serikali ya Uingereza amhifadhi Sultani hadi hapo mipango ya kumsafirisha itakapokamilika.
“Na Mwenyezi Mungu akampa Mwalimu Nyerere busara kubwa ya kulikubali ombi hilo haraka haraka. Kutahamaki, Sultani keshafika Dar es Salaam, mgeni wa Mwalimu Nyerere.
“Hata sisi (viongozi wa ASP) tulikuwa na hofu juu ya Sultani aliyepuruchuka, kama angepata akili kwenda Pemba na halafu kutoka kule akaomba msaada wa majeshi kutoka nchi za nje, hali yetu ingekuwa ngumu sana.”
SEMA HAKUWA NA AKILI HIZO MAANA HAKUJUWA CHOCHOTE KATUACHA KATIKA MASHAKA NA DHIKI MPAKA LEO HII 2019 TUNAELEKEA 2020 TUMO TABUNI YEYE SALAMA SALMINI NA FAMILIA YAKE UINGEREZA.

NANI MUOGO ZAIDI BABU ALI AU MAALIM SEIF NITAPISHWA KABLA 2020 BABU ALI NITAIFANYA ZANZIBAR KUWA DUBAI


HAYA 2020 HIYOOO BABU ALI USHAKWISHA NA DHULMA YAKO MAALIM NA WEWE ULIYE JIDAI TUTADAI HAKI YETU KWA UPOLE KABLA YA 2020 TUTAIPATA HAKI YETU IKO WAPI....???





Friday, September 29, 2017

HIVI NDIVYO SEREKALI YA MAADHALI YA DR SHEIN ILIVYO MUUWA SHAHIDI ALI JUMA NA WATAENDELEA KUUWA HAWA MAANA NI KAMA MASHETANI WASHAKUNYWA DAMU


Afbeeldingsresultaat voor DR SHEIN

Jana mchana muandishi wetu wa Free Zanzibar People From Mkoloni Mweusi Tanganyika na watu wengine walipata kumtembelea Shahidi Ali Juma akiwa kitandani Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja na akamsimulia namna alivyovamiwa nyumbani kwake, kuteswa na kipigo ambacho ndicho kimekuwa ndio sababu ya kuondoka na uhai wake. Angalia vidio hii, na kisha mtakie dua shahidi huyu.Pia kaa ukijuwa kuwa Wauwaji wa Serekali Hii Ya Madhalimu bado hawaja maliza kuuwa watu na kufunga watu jela bila kosa wala sheria wamafanya hayo toka mapinduzi ya 1964 mpaka sasa ni muendelezo tu hakuna jipya ndugu yangu Mzanzibari zinduka toka katika usingizi kuwa ati Zanzibar ni nchi Zanzibar sio nchi bali ni Koloni La Mkoloni Mweusi Tanganyika na hakuna Mkoloni anaetaka kuliwachia Koloni Lake Kirahisi kwa hiyo lazima mambo mawili yafanyika tukubali kuliwa na kunyanyaswa na kuka kimya na Mkoloni Mweusi Tanganyika akiendelea kututawala kimabavu na kwa nguvu za jeshi walio wajaza hapa Unguja na Pemba au Mbwa hawa tupingane nao mpaka nchi hii waihame na kuiyona chungu kama shubili sisi ndio wa kuamuwa.

Saturday, September 2, 2017

MAHAKAMA KUU NCHINI KENYA SUPREME COURT IMEBATILISHA USHINDI WA WA URAIS WA NCHI HIYO NCHINI ZANZIBAR JECHA KAJIFUNGIA PIKE YAKE KABADILISHA UCHAGUZI MZIMA KISHA HAKUONEKANA TENA ZANZIBAR NDIO INAJUWA SIASA SIO MCHEZO

Afbeeldingsresultaat voor jecha
Afbeeldingsresultaat voor uhuru kenyatta uchaguzi

Gerelateerde afbeelding
MAHAKAMA Kuu nchini Kenya (Supreme Court), imebatilisha ushindi wa uRais wa Rais wa sasa Uhuru Kenyatta, dhidi ya mpinzani wake mkuu Raira Odinga, na kuamuru uchaguzi huo urudiwe ndani ya siku 60 kuanzia leo Septemba 1, 2017. 

Mahakama hiyo imefikia uamuzi huo, kufuatia maombi ya Mgombea Urais wa Muungano wa upinzani wa NASA, Raila Odinga baada ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa Rais, uliompa ushindi Rais Kenyatta. 

Katika maombi yake,  Odinga alisema, kura zake zilipunguzwa kwenye baadhi ya vituo na kuongezewa mpinzani wake, lakini kubwa zaidi ni kukiukwa kwa taratibu za uchaguzi ambapo baadhi ya fomu muhimu za matokeo ya uchaguzi kama vile fomu namba 34A,B na C, hazikupatikana siku ya kutangazwa kwa matoko. 

Katika uamuzi wa mahakama hiyo, majaji wanne kati ya sita (6), wamekubaliana kuwa tume huru ya uchaguzi na mipaka ya Kenya, (IEBC), imeshindwa kusimamia vema uchaguzi huo na hivyo kusababisha kasoro kadhaa ambazo zinakwenda kinyume na katiba ya Kenya. Hata hivyo, Mahakama hiyo imesema, hakuna ushahidi wowote, ulioonyesha kuwa Rais Uhuru Kenyatta, alitenda makosa katika mchakato huo wa uchaguzi.