Saturday, April 30, 2016

NCHINI ZANZIBAR HALI NDIO HII NA VIPINDUPINDU VISHAUWA WATU 80 MPAKA SASA



MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA MNAJUWA KUTUJAZIA WANAJESHI NA KUTUUWA SIKU ZA CHAGUZI ILI CCM FYOKOFYOKO IBAKI MADARANI NA UKOLONI WENU MBONA YAKITUFIKA MAAFA HATA HABARI HAMUNA NYINYI WAKOLONI WEUSI TANGANYIKA


MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA MNAJUWA KUTUJAZIA WANAJESHI NA KUTUUWA SIKU ZA CHAGUZI ILI CCM FYOKOFYOKO IBAKI MADARANI NA UKOLONI WENU MBONA YAKITUFIKA MAAFA HATA HABARI HAMUNA NYINYI WAKOLONI WEUSI TANGANYIKA


HII NDIO KAZI YENU KUUWA WAZANZIBARI NA KUWAPIGA NA KUWANYANYASA TOKA MWAKA 1964 NYERERE KANZA,MKAPA AKATUUWA PEMBA,KIKWETE KAPORA HAKI ZA WAZANZIBARI ZA UCHAGUZI ULIO HURU NA WAKI NA WEWE MR FYOKOFYOKO UKALINDA UCHAGUZI HARAMU WA HICHO KIBARAKA CHINU SHEIN NA MPAKA SASA MR FYOKOFYOKO UNAENDELEZA HARAMU NCHINI ZANZIBAR KWA KULINDA HAO MAHARAMIA SHEIN NA WENZIWE NA MKO KIMYA MAAFA YOTE HAYA YANAYO WAPATA WAZANZIBARI MNAFURAHIA HASWA MAANA WANAO KUFA NI WAZANZIBARI SAWA NYERERE YUKO WAPI KABURINI NA NYINYI PIA MTAA KWENDA MAKABURINI KISHA MUTAMUELEZA VIZURI MFALME WA WAFALME HUMO KABURINI NDIO UTAJUWA FYOKOFYOKO NI NINI KAMA WANAVYOJUWA HAO WALIO TANGULIA.



MAHEMA WANAYO LAZWA WATU WAGONJWA WALIO ATHIRIKA NA KIPINDUPINDU HATUNA SERIKALI UNICEF NDIO INAOKOWA WATU FYOKOFYOKO MBONA HAIJI KUTUSAIDIYA AU INAJUWA TU KUSEMA FYOKOFYOKO
KISHA TWAMBIWA NCHI HII IKO KATIKA MUUNGANO NA BOSI WA MUUNGANO WA HIVI SASA ANASEMA ATAENDELE KUDUMISHA NA YOYOTE ATAKAE LETA FYOKOFYOKO ATAMUONYESHA SAWA HATUJA LETA FYOKOFYOKO SASA WEWE TULETE HIZO FYOKOFYOKO ZAKO ZIJE KUYAONDOWA HAYA MAJI TULETE HIZO FYOKOFYOKO ZAKO ZITUONDOLE HICHO KIPINDUPINDU TULETE HIZO FYOKOFYOKO ZAKO TURUDI KATIKA MAJUMBA YETU YALIO JAA MAJI YA MVUA BASI MR FYOKOFYOKO.

KISHA NYINYI MUNAYAITA MAPINDUZI MATUKUFU HIVI KWELI NYINYI MUNAJUWA UTUKUFU NI NINI AU DUNIA IMEWAVA KISAWA SAWA MPAKA MNAKUFURU MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA KATUPINDUWA TENA WAZANZIBARI NA KUWEKA VIONGOZI WAWATAKAO WAO WAKINA BT TUNAENDELEA TENA KUKA CHINI YA SERIKALI YA KIKOLONI YA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA MPAKA MIAKA MITANO IMALIZIKE KISHA TUTIWE TENA KATIKA SHENGESHA LA UCHAGUZI NA KUPIGA KURA KISHA WAZANZIBARI WAPIGE KURA NA KUCHAGUWA VIONGOZI WAWATAKAO MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA ATAKUJA NA STYLE MPYA YA KUZIPIGA KURA ZA WAZANZIBARI CHINI NA KUTUEKEA VIONGOZI WAWATAKAO KISHA TUTAKA TENA CHINI NA KUSUBIRI UCHAGUZI WA 2025 MAMBO YATAKUWA HIVYO HIVYO KISHA TUTAKA CHINA NA KUSUBIRI UCHAGU WA WA 2030 TUKIWA HAI KAMA HATUKO TENA WATAKAO BAKI WATAFANYIWA TENA HIVYO HIVYO NA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA KISHA WATAKA CHINI WASUBIRI......>>> MPAKA KIYAMA KISIMAME BASI NI BORA TU TUKUBALI KUWA NDIO TUMEKUBALI KUWA CHINI YA MKONI MWEUSI TANGANYIKA KULIKO UPUMBAVU HUU WA UCHAGUZI AMBAO KILA MOJA WETU HAPA ZANZIBAR KAMA UCHAGUZI WA MARA HII HAUJAWASOMESHA WALA HATUTA SOMA TENA MILELE. 

KILA MZANZIBARI ALIYE IPIGIA KURA CCM AU MPAKA WAKATI HUU BADO ANAISAPOTI CCM ILI IBAKI MADARAKANI JAPO KUWA CCM IMESHINDWA UCHAGUZI AJUWE NA YEYE ANACHANGIA KUENDELEZA DHULMA NA KUFUNGWA KWA MASHEIKH NA KUTHALILISHWA KWAO NA KUENDELEZA DHULMA KATIKA NCHI YA ZANZIBAR UKAE UKIJUWA UTAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA,KUDHULUMIWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

Friday, April 29, 2016

CUF WATOWA TAMKO LA MVUA ZINAZO ENDELEA NA MAMBUKIZO YA VIPINDUPINDU NCHINI ZANZIBAR


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Nchi yetu Zanzibar imekumbwa na mvua kubwa zinazoendelea kusababisha madhara kwa maeneo mengi ya visiwa vya Unguja na Pemba. Mvua hizo zinazonyesha katika maeneo yote ya nchi yetu zimesababisha athari mbalimbali ikiwemo kupotea kwa baadhi ya roho za wananchi wenzetu kutokana na athari zake. Kwa mfano, mvua zilizonyesha usiku wa kuamkia Jumapili tarehe 17 Aprili, 2016 zilisababisha kifo cha Ndugu Salim Mohamed Ahmed (61) mkaazi wa Migombani kutokana na kuangukiwa na ukuta uliomong’onyolewa na mvua zilizonyesha usiku wa kuamkia siku hiyo.
Mvua hizo zilizofikia kiwango cha milimita 212.4, kama ilivyotangazwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kanda ya Zanzibar, zimepelekea, mbali na kuharibu kabisa miundombinu ya barabara, kuathirika pia maeneo yanayotumika kwa ajili ya kutolea huduma kwa wananchi. Moja ya maeneo hayo ni hospitali ya wagonjwa wenye matatizo ya akili ya Kidongochekundu ambayo ililazimika kusitisha huduma zake kutokana na kujaa kwa maji ya mvua katika maeneo ya majengo yake kama vile jengo la Block D na Block F.
Aidha, taarifa zinaonesha kuwa zaidi ya nyumba mia tisa (900) ambazo ni makaazi ya watu zimeingiliwa na maji na kusababisha athari mbalimbali ikiwemo kubomoka kwa nyumba hizo na kupelekea wamiliki wa nyumba hizo kuhama na kutafuta hifadhi kwa ndugu na jamaa zao. Miongoni mwa maeneo yaliyoathirika zaidi ni: Jang’ombe, Nyerere, Sebleni, Sogea, Karakana, Kwahani, Mpendae, Miembeni, Gulioni, Makadara, Meya, Migombani, na Kwaalinato kwa upande wa Wilaya ya Mjini Unguja.
Kwa upande wa Wilaya ya Magharibi ‘A maeneo yaliyoathirika ni pamoja na Mwanyanya kwa Goa, Bububu, Welezo, Mwera, Mtofaani, Mtopepo, Mtoni Kidatu, Kihinani, na Kibweni. Maeneo yaliyoathirika kwa Wilaya ya Magharibi ‘B’ ni Mwanakwerekwe, Tomondo, Mombasa, Fuoni Kibonde Mzungu, Pangawe, Kinuni, Kisauni, Kiembesamaki na Meli nne.
Kiwango hichi kikubwa cha mvua kuwahi kushuhudiwa hapa Zanzibar kimepelekea kutifuka kwa miundo mbinu ya maji machafu na kuathirika vibaya kwa mfumo wa kuhifadhia na kusafirishia maji machafu hasa katika maeneo tuliyoyataja kukumbwa na mvua zinazoendelea. Hadi sasa maeneo tuliyoyataja yamezungukwa na kiasi kikubwa cha maji machafu yaliyochanganyika na mkusanyiko wa takataka za kila aina ikiwemo masalia ya uchafu wa kimaumbile wa viumbe mbalimbali. Hali hii imepelekea kushamiri na kuongezeka kwa kasi kubwa kwa maradhi ya mlipuko ya ugonjwa wa kipindupindu yaliyoanza mwezi Machi, 2016.
Kwa mujibu wa taarifa tulizozipokea hapa katika ofisi zetu za Makao Makuu, kama zilivyotangazwa na Mamlaka mbalimbali za Zanzibar kama vile Mkurugenzi wa Idara ya Kuzuia na Kupambana na Maradhi Zanzibar (Director of Disease Prevention and Control) Muhammed Dahoma, maradhi haya thakili ya kipindupindu yamesababisha vifo vya zaidi ya watu thamanini (80) na wengine zaidi elfu tatu (3,000) wamelazwa katika maeneo maalum ya makambi ya wagonjwa wa maradhi hayo.
Kutokana na maradhi haya, Mamlaka za Zanzibar, ikiwemo viongozi wa kisiasa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamepiga marufuku uuzwaji wa vyakula na vinywaji vya aina zote katika maeneo ya wazi, kuanzisha makambi katika visiwa vya Unguja na Pemba ambamo wagonjwa wa kipindupindu huwekwa na kutengwa na kufungwa kwa skuli za madarasa ya awali na msingi kwa kipindi kisichojulikana.
Mbali na watendaji wa Malaka zilizopewa jukumu la kusimamia kazi ya kuhakikisha matangazo hayo yanasimamiwa kujinufaisha binafsi na kutekeleza jukumu hilo kwa uonevu na udhalilishaji, taarifa zinaonesha kuwa kumekuwepo na kasi ndogo na utekelezaji usiozingatia vigezo vya kitaalamu katika kutoa huduma kwa wahanga waliokusanywa katika maeneo ya wagonjwa wa kipindupindu kutokana na kukosekana kwa nia njema ya kukabiliana na kupambana na maradhi hayo kwa kuwatibu waathirika kutokana na kukataa kukiri kwa mamlaka hizo kukosa uwezo wa vifaa na utaalamu.
Aidha, uamuzi wa kufungwa kwa skuli za awali na skuli za msingi kama njia ya kukabiliana na maradhi ya kipindupindu unaonekana kuchukuliwa kwa kufuata mawazo yaliyojengwa kwa hamasa na kuamuliwa kwa haraka bila ya kuzingatia athari zake kwa sekta ya elimu Zanzibar. Bila ya chembe ya shaka, maradhi ya kipindupindu ni hatari kwa mustakbali wa wananchi wa rika zote katika nchi yetu, hata hivyo haikubaliki kuchukua hatua ya kufunga skuli na kuwakosesha watoto wetu haki yao ya msingi ya kupata elimu katika kipindi kisichojulikana bila ya kushughulikia msingi wa matatizo na chanzo cha maradhi ya kipindupindu kwa Zanzibar.
Ni busara kwa waliotoa tangazo la kufungwa kwa skuli kuzingatia mustakbali wa sekta ya elimu zanzibar kutokana na tangazo hilo. Katika kufanya hivyo wanapaswa kuzingatia idadi za siku za mapumziko kwa mujibu wa kalenda ya Wizara ya Elimu Zanzibar, urefu wa mitaala ya Elimu, na idadi ya siku za masomo kwa wanafunzi wa Zanzibar. Bila ya shaka, kwa kuzingatia vigezo hivyo watabaini athari za tangazo lao hilo la kufunga skuli za Zanzibar kwa muda usiojulikana kwa mustakbali wa sekta ya elimu Zanzibar bila ya kuwepo mikakati madhubuti miongoni mwa Mamlaka nyengine za kupambana na maradhi ya kipindupindu yanayojirudia kila uchao.
Kwa upande mwengine, tangu kutokea kwa mafuriko ya mvua kwa mwaka huu na kushadidi kwa maradhi ya kipindupindu, kumekuwepo na mlolongo wa ahadi nyingi kutoka kwa wanasiasa wa CCM, akiwemo Dr. Ali Mohamed Shein, Balozi Seif Ali Idd na Mohamed Aboud, kwa wananchi waliopatwa na mitihani ya mafuriko. Sisi katika CUF-Chama Cha Wananchi tunaamini kuwa ahadi hizi za wanasiasa hawa, waliojiweka madarakani bila ya ridhaa ya wananchi, ni ahadi hewa ambazo kimsingi hawana nia wala uwezo wa kuzitekeleza na kwa hakika zimelenga kuwahadaa wananchi hao ili kupunguza ghamidha za wananchi wa Zanzibar dhidi yao kutokana na matendo ya wanasiasa hao kusaliti maamuzi ya wazanzibari na kuzima sauti zao walizozitoa kwa njia za kidemokrasia tarehe 25 Oktoba, 2015.
Kutokana na muktadha wa kukosekana insafu na nia njema ya kukabiliana na kuwaondolea matatizo yanayowakabili wananchi wanyonge wa Zanzibar na mfululizo wa ahdi kemkem za viongozi walioweka mbele maslahi yao binafsi na kuwahadaa wananchi kwa malengo tuliyoyataja hapo juu:
1. CUF-Chama Cha Wananchi Kinaendelea kuwasisitiza wananchi wote wa Zanzibar kuendelea kushikamana na kusaidiana, kwa kuzingatia hali halisi ya zanzibar kwa sasa, kwa kuwasaidia wananchi wenzao waliokumbwa na maafa ya kukosa makaazi kutokana na kuharibikiwa na nyumba na mali zao kwa kuendelea kuwapatia hifadhi katika nyumba zao, na kuendelea kuwa karibu na wanafamilia za wananchi waliopoteza ndugu zao kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha kwa kuwafariji na kuwaombea dua marehemu wetu wote waliotangulia mbele ya haki ili Mwenyezi Mungu mtukufu azilaze roho zao mahali pema peponi na kuwaombea wanafamilia hao kuwa na moyo wa subira.
2. CUF-Chama Cha Wananchi kinatoa wito kwa Mamlaka zinazohusika na maafa, ikiwemo idara ya maafa Zanzibar, kuweka utaratibu mzuri unaoeleweka katika kutekeleza mipango na mikakati mbalimbali iliyokwishafanyika miaka mingi iliyopita ili kumaliza tatizo la miaka mingi la mafuriko ya maji na mvua katika miji ya Zanzibar linalojirudia kila baada ya kipindi kifupi cha muda. CUF inaamini kuwa kwa kutumia kwa vitendo mipango na mikakati iliyoandaliwa kwa gharama kubwa na iwapo kutakuwa na umakini na utayari wa hali ya juu miongoni mwa watendaji wa idara hizo, tatizo la mafuriko kwa maeneo sugu ya Zanzibar yanayokabiliwa na matatizo hayo litapungua na hatimaye kumalizika kabisa.
3. Kutokana na kuamini na kuthamini maisha ya kila mwananchi wa nchi hii, bila ya kujali uwezo wake wa fedha, asili yake, na itikadi yake ya kisiasa, CUF-Chama Cha Wananchi kinazizindua Mamlaka zilizoaminiwa na kupewa jukumu la kuhami maisha ya wananchi wa nchi hii, ikiwemo Baraza la Manispaa Zanzibar, kusimamia kikamilifu utekelezaji wa mpango wa kudhibiti maji ya mvua na mfumo wa maji taka kwa azma ya kuwaepusha wanajamii ambao wao ni sehemu yake. CUF inatoa wito wa utekelezaji, kwa vitendo, wa Master Plan kwa mji wa Zanzibar ili kufumua mfumo wa maji taka uliopitwa na wakati na kuweka mfumo wa kisasa wa ukusanyaji, ukaushaji na uhifadhi wa maji taka kwa maeneo yote ya Zanzibar.
4. CUF-Chama Cha Wananchi kinawanasihi wanasiasa wa Zanzibar kuacha mara moja kuwadhihaki wananchi wenye matatizo na kutumia matatizo hayo kuwafanyia tashtiti na kuwapa ahadi kemkem bila ya dhamira ya dhati ya kutekeleza ahadi hizo. CUF inawatanabahisha wanasiasa wote kuwa wananchi wa Zanzibar wameerevuka vya kutosha na katu hawatakubali tena kutumika kuwanufaisha wanasiasa wa hovyo hovyo walioweka mbele maslahi yao na familia zao na kuwasahau wananchi kwa kupuuza na kudharau sauti zao na matakwa yao.
HAKI SAWA KWA WOTE
………………………………….
NASSOR AHMED MAZRUI
NAIBU KATIBU MKUU CUF ZANZIBAR

SEHEMU YA 1) UKWELI NI HUU KUUSUTA UWONGO. MAVAMIZI YA NCHI YA ZANZIBAR KWA WAGENI KUUWAUWA WANYEJI KATIKA NCHI YAO NA KUSINGIZIA ((MAPINDUZI))


Nimechanguwa jina hili la UKWELI NI HUU KUUSUTA UWONGO, baada ya kuyasikia na kuyasoma mengi ya uwong na hata kufikia kusomeshwa watoto wetu katika Maskuli ya Zanzibar kuhusu hayo yenye kuitwa (MAPINDUZI) yaliyo fanyika katika visiwa vyetu vya Zanzibar mnamo Taarikh 12 januwaru 1964.

kabla ya kuingia katika hayo, nigependa kuwambia wasomaji wangu kuwa mimi si mjuzi hata kidogo wa fani hii uandishi; tena ni mbovu sana katika spellings na katika nahau za kiswahili cha kisasa. Pia nawaomba radha kwa kiswahili changu cha kizamani, Bali, kutokana na huo uzushi na kupotezwa kwa makusudi ukweli wa hayo yaliyofanyika kuhusu hayo yanayo itwa (MAPINDUZI) nimeona sina budiilla nijitole hivyo hivyo juu ya upungufu wangu wa katika fani hii juu ya uandishi. Lakini ukweli lazima niudhihirishe ili vichepukizi vyetu viweze kuyaelewa vilivyo yaliyo tendeka katika nchi yao. Kwani wengi walikuwa wadogo na wengi walikuwa hata hawajazaliwa wakati huo. Ilivyokuwa kiswahili ni lugha yangu ya kuzaliwa, basi ninaiandika kama ninavyo isema. Si shughuliki na kua au kuwa, aliniambia au aliniambiya, aliniambia au aliniambiya, ameuawa au ameuwawa, kenda au kaenda, amekwenda au ameenda; Hayo kwa watamu wa lugha ni mambo muhimu lakini kwa mimi nakutakeni msamaha juu ya hayo. Muhimu yakuyaangalia na kuyazingatia ni yale nikusudiayo kuyaeleza, kwani hayo ndio muhimu na ndio ya kweli tupu isiyukowa dosari hata chembe.

La Mwanzo nitakalo waombeni mlifahamu uzuri ni ile hakika kuwa hayo yaliyo fanyika katika visiwa vyetu Taarikh 12 januwari 1964 hayakuwa (MAPINDUZI) wala hayafai hata kidogo kuitwa mapinduzi kwa maan ya asili ya neno.Bali kwa maana zote yalikuwa khasa ni MAVAMIZI yani kwa kiengereza INVASION. Mapinduzi lazima yapangwe, yaongozwe na yatekelezwa na wananchi wenyewe kwa maslahi ya nchi na wananchi wake. Sasa tukiangalia yaliyotendeka Zanzibar, yalipangwa, yaliongozwa na yalitekelezwa na WAGENI kutoka nchi za nje za jirani zetu.(Ni wao wala si wananchi ndio waliochukuwa ngawira kubwa kubwa) Haya yathibitika zaidi kwa vile kuwa huyo jamadari aliyeyaongoza hayo mavamizi ni John Okello na wachini yake walikuwa Injini na Mfaranyaki. Nani kati ya hao aliyekuwa kitovu chake kimizikwa kisiwani...?? Okello amezaliwa na kukulia kwao Uganda, Injini amezaliwa na kukulia kwao Kenya na Mfaranyaki amezaliwa na kukulia kwao Tanganyika.Wote hao walikuja Zanzibar wakiwa watu wazima na shughuli zao,wamekuja kutafuta kibarua na kukimbia kodi za vichwa katika nchi zao.Liangalie ilo walilolita Baraza la Mapinduzi utaona sehemu kubwa ya wanachama wa baraza hilo walikuwa si Wazanzibari,Laa kuzaliwa wala kwa uchukuwa Tajnisi (kuandikisha uraia) John Okello, Khamis Darweshi, Seif Bakari, Said Natepe, Said Washoto, Muhammed Mfaume, Enditong Kisasi, Mohammed Abdallah Kaujore. Ukiwacha wengine nao vile vile walikuwa si wananchi wa Zanzibar kwa kuzaliwa, bali wao walikuja Zanzibar wakiwa katika migogo ya wazee wao na waliendelea kuishi humo visiwani kwa maisha yao yote.Na wakachukuliwa kama ni Wazanzibari japo kuwa sio Wazanzibari.


UTUKUFU NA NEEMA YA ZANZIBAR
Mwenyezi Mungu amevipa visiwa hivi viwili yani Unguja na Pemba bahati ya utukufu katika kila jambo lake.Hayo yaliendelea toke karne na karne mpaka pale ulipo tendwa ufisadi wa Taarikh 12 januari 1964,ndipo neem na utukufu wa Zanzibar ulipoanza kutoweka.Hapo tena badala ya zumari lakipulizwa Zanzibar,watu wa maziwani (Bara) walikuwa wakihemukwa,ikawa linapulizwa Bara,tuliopo visiwanitunahemukwa!!! 

ZANZIBAR NA UBAGUZI KABLA YA MAVAMIZI
Nathubutu kusema bila ya wasi wasi wowote kuwa Zanzibar hakukuwepo ubaguzi wa namna yoyote kwa maana khasa na ya wazi ya neno UBAGUZI. Kwanza Wazanzibari ni watu walio changanya sana damu hata sio rahisi kuweza kumtambuwa mtu kuwa ni mwenye kutokana na asili ya kabila fulani kwa kuangalia rangi yake au pua yake au masiki yake au kimo chake au kwa jina lake.Je watu hao watabaguwani namna gani...?? Malipo ya wafanyakazi Serikalini yalikuwa hayakupangwa ki-ukabila.Wale Serikali haikuwa na sehemu maalum katika Maskuli wala katika Mahospitali kuwa zimetengwa kwa ajili ya watu wa makabila fulani.Katika nchi za jirani zetu, Tanganyika, Kenya na Uganda kote huko kulikuwepo na ubaguzi uliokuwa ukiongozwa na serikali za nchi hizo.Malipo ya mishahara ya wafanyakazi yalikuwa yakilipwa kutokana na makabila yao wala si kutokana na ujuzi wao wa kazi kulikuwepo na African Scale Asia Scale na Europen Scale. Madaktari, Mainjinia, Waalimu na wowote nawawe wana elimu na ujuzi na maarifa ya namna moja, yani wote sawa sawa kwa elimu na ujuzi wa kazi zao,lakini mishahara yao ilikuwa tafauti kutokana na makabila yao.Waafrika ndio wenye kulipwa malipo ya chini kabisa kuliko wote.Wazungu walikuwa ndio wenye kulipwa mishahara minono (hata baadhi yao walikuwa hawana elimu yoyote isipokuwa huo uzungu wao) Waliofuatia ni Waasia. Vyoo vya njiani (Public Toilet) na sehemu za kungojelea usafiri wa reli navyo vile vile vilikuwa vikitumika kwa ubaguzi wa kikabila. Waafrika waliekewa vyoo vyao na sehemu zao za kungojelea usafiri, Wazungu walikuwa na sehemu zao, Waasia walikuwa na sehemu zao,wote mbali mbali.Lilikuwa ni kosa na kuvunja sheria ikiwa imetokea kwa yoyote kuingia katika sehemu asiyo kuwa amekhusika nayo.Khasa Muafrika awe ameingia au amekaa  sehemu za Waasia au za Wazungu.Katika Tanganyika, Kenya na Uganda kote huko kulikuwa na kodi ya Kichwa. kodi hiyo ilikuwa ikilipwa na kila mtu aliyekwisha fikia balegh katika umri wake. Nayo pia ikitekelezwa kwa njia za ubaguzi wa kikabila. Waasia na Wazungu hata ikiwa wao wamechelewa kulipa kodi zao basi walikuwa hawakamatwi majiani wala walikuwa hawaendewi majumbani mwao kukamatwa.Laikini Waafrika walikuwa wakisakwa majiani na wakiendewa majumbani mwao mnamo pinga pinga za usiku.Na wakikamatwa,basi walikuwa wakifungwa kamba za viunoni au hufungwa ncha ya shati la huyu na huyu kisha walikuwa wakiongozwa mmoja nyuma ya mmoja na huku wakipingwa mateke na kusukumwa mpaka wakifikishwa Bomani. Huko ikiwa hawatakuwa na cha kuwalipa basi walikuwa wakihukumiwa na wakifungwa.kutokana na hali kama hizo,ndipo wengi kati ya wananchi wa nchi hizo,khasa kutokaTanganyika walikimbia kutoka makwao na kuhamia Zanzibar kwa sababu ya kufuata hali njema za kimaisha.Zanzibar hakukuwepo kodi za kichwa wala ubaguzi wa vyooni wala malipo ya mishahara wala ya namna yo yote.ilikuwa ni njema na atakae naaje.

UBAGUZI UMEANZISHWA ZANZIBAR WAKATI WA SERIKALI YENYE KUJIITA YA MAPINDUZI
Mara tu baada ya kufika hiyo serikali ya mavamizi katika Zanzibar ubaguzi wa ukabila ulianzishwa kila mrangi rangi kama walivyo kuwa wakiwaita wenyewe, yaani wenye asili za kiarabu, za kihindi na za kingazija walianza kuolewa makazini bila ya kupewa hata haki zao za ufanyaji wa kazi.mashamba,majumba na hata mabiashara yao yalichukuliwa kwa nguvu na kupewa wageni ikiwa ni tunzo la ukatili na maovu waliyowafanyia wananchi katika nchi yao.Serikali ya mavamiza ya Zanzaibar ilitangaza rasmi kupitia vyombo vya khabari vya serikali kukhusu ubaguzi katika Taalimu.Waafrika wakipasi au wasipasi bali idadi yao yakuingia katika form one ya secondary school ilikuwa ni 77 katika mia (77%) Waarabu 16 katika asili mia (16%) wahindi 6 katika mia (6%) na wangazija MOJA katika mia (1%) Si hayo tu, bali serikali ya mavamizi imetumia pesa za umma kwa ajili ya kujijengea hospitali yao wao tu ya wananchama wa Baraza la Mapinduzi na Familia Zao na wameita (MAPINDUZI WING) vitanda,mabetishiti,foronya za mito,vyombo vya kulia kama sahani,vikombe,visu na nyuma (forks) vyote viliangizwa kutoka ulaya.Ilikuwa ikitokea Mheshimiwa kulazwa huko, basi na mkewe alikuwa akihamia huko huko na kulala kitanda kimoja kama kwamba wamo katika siku za fungati haya yakitendeka wakati wananchi wanyonge hawana hata dawa mahospitalini!!! huwo ulikuwa ndio usawa sio ubaguzi!!! 

ELIMU NA MATIBABU BURE
Tuunambiwa na Serikali yenye kuujita ya Mapinduzi kuwa elimu na matibabu yameanza kuwa bure kwa wananchi baada ya kupatikana serikali ya Mapinduzi huu ni uwongo uliyokuwa hauna hata kifuniko.Toka lini elimu na matibabu yalikuwa kwa malipo katika Zanzibar....?? Tangu kuanzishwa kwa skuli ya serikali ya Sayyid Ali bin Hamoud na toka kuanzishwa kwa matibabu katika mahospitali, kamwe hayapata kuwa ya malipo.Toka kwa kuangaliwa na madaktari mpaka kwa madawa,chakula,na mpaka kulala kwa kutibiwa katika mahospitali kulikuwa BURE

TAALIMU
Wananchi na wageni,kuanzia chumba cha kwanza (standard one) mpaka kufikia chumba cha nane (standard eight) masomo yalikuwa bure kwa wote. Sio hivyo tu kila mwanafunzi alikuwa akipewa madaftari ya kuandikia bure, vitabu vya kusomea bure, kalamu za kuandikia bure, vidawa vya wino na wino wake bure hata blotting paper (la kukaushia wino) pia wakipewa bure. Na kila ijumaa wanafunzi walikuwa wakipewa sabuni za kufulia bure. Skuli za mashamba, wanafunzi walikuwa wakipewa kifunguwa kinywa, kunde na uji - kabla ya kuingia katika vyumba vya masomo bure. Kuanzia chumba cha tisa mpaka cha 12, na baada ya muda katika miaka ya 1950 kuanzia chumba cha saba mpaka cha 12, wazee walitakiwa wasaidiye kitu kidogo katika masomo ya watoto wao.Malipo hayo yalikuwa ya kitu kidogo sana na si kila mzee alikuwa akilipa ada hizo. Wengi sana katika wazee walikuwa hawalipi hata senti moja. Na hao walikuwa wakilipa, wengi wao walikuwa wakilipa kuanzia kuanzia shs tano mpaka shs 20 kwa wingi kila baada ya miezi mitatu au mine. Kabla ya mzee alipe au asilipe, kulikuwepo utaratibu maalumu zilizokuwa zikifanywa.Mzee wa mtoto alikuwa akipelekewa (questionnaire) karatasi yenye masuala yaliyokhusu mapato yake, kazi yake na idadi ya watu wake wa nyumbani.kwa kutaka kuhakikisha uwezo wa mzee huyo,basi akipelekewa waraka huo kwanza sheha wa mtaa kuhakikisha yaleyaliandikwa na akisha sheha humpelekea mudiri wake humpelekea D.C. wake.Baada ya khatuwa hizo ndio tena hapo hutolewa uamuzi wa kulipa au wa kutokulipa, na kama kulipa alipe kiwango gani.Kutokana na mipango kama hiyo,zaid ya 70 katika mia (70%) ya wazee watoto wao walikuwa wakisoma bila ya kulipiwa kitu chochote na kiasi cha 20 katika mia (20%) walikuwa wakilipiwa kitu kidogo na kiasi cha 10 katika mia (10%) ndio waliokuwa wakilipiwa idadi kamili ambayo ilikuwa chini ya shillingi 200, kwa mwaka mzima.Wengi waliokuwa wakilipa kima hicho walikuwa ni wazee wenye asili za Kihindi.Wanaoitwa Waafrika na Wanaoitwa Waarabu hayo yalikuwa sio maji yao.Muhimu katika hayo si kulipa au kuto kulipa, muhimu ni thamani (quality) ya elimu iliyokuwa ikipatikana siku hizo. Je leo inapatikana....?? Hilo ndilo suala muhimu la kujiuliza na kulizingatia. Ikiwa hiyo isemwayo leo kuwa elimu bure, na imekuwa wanafunzi hawana madeski ya kukalia,hawana vitabu vya kusomea,wala chochote cha kusomea,bali zaidi hawana hata walimu wenye ujuzi wa kusomesha;basi bure kama hiyo ni bure ghali kwa hiyo bure,basi watoto wetu leo wametokwa na vibyongo kwa kuinama wakati wa kuandika.Wakirijea kutoka maskuli utadhania wanatoka kuchimba makaburi kwa mavumbi yalivyo watapaka kwa kusota chini.Elimu bure!!! Wanafunzi wapotezewa wakati wao wa masomo kwa kuchezeshwa ngoma za sindima na kuimbishwa majimbo ya kanisani ati huitwa Kwaya kuanzia Disemba Wanafunzi walikuwa wakianzishwa mazoezi ya kucheza ngoma na kuimba hizo Kwaya pamoja na magwaride kwa ajili ya kujiweka tayari kwa sherehe za hayo yenye kuitwa Mapinduzi katika mwezi wa januari. Wakimaliza tu, hawawahi hata kushusha pumzi wanangojewa kwa sherehe za kuasisiwa kwa Chama cha Afro Shirazi 2 - 2 (February 2) wakimaliza tu,hawawahi hata kunywa maji,wanazolewa tena kwa mazoezi ya sherehe za Muungano April 26. Hawawahi hata kuka kitako,wanabebwa tena kwa mazoezi ya sikukuu ya Wafanyakazi May Day hapo hupumua kidogo kisha huzolewa tena kwa mazoezi ya kusherehekea Saba Saba July 7. Hawawahi hata kwenda chafya hunyakuliwa tena kwa mazowezi ya sherehe Elimu bure!! Septemba. Wakimaliza hapo wanazolewa tena kwa mazowezi ya sherehe za Uhuru wa Tanganyika Desemba. ukiangalia utaona kuwa mwaka mzima badala ya watoto wetu kusomeshwa,walikuwa wakichezeshwa ngoma,kuchezeshwa magwaride na kuimbishwa manyimbo ya kanisani.Bado ati husema ELIMU BURE, kweli bure lakini BURE KWA MJINGA kwa kweli kiwango cha elimu Zanzibarkimeanguka kiasi kikubwa sana, kiasi cha kuitwa chini ya sufuri. Imefika hadi leo kuwa Mwanafunzi aliyemaliza hicho wanachokita kidato cha nne (Form IV) ukimuambia aandika barua ya kuomba kazi kwa lugha ya Kiingereza anashindwa hata kujaribu kuadika na ikiwa atajaribu,basi kichwa huwa miguu na miguu huwa kichwa.Hapo yalipokuwepo masomo ya kweli na walimu wa kweli wenye kufunzwa wakafunzika katika fani ya kusomesha, wanafunzi waliomaliza chumba cha nane ilikuwa wakiandika kiengereza utawavulia kofia.

MATIBABU
Tukija katika matibabu, ndiko tutakako kukuta kumeporomoka vibaya kabisa. Hospitali hazina madawa, hazina vifaa vya matibabu, hakuna hata vitanda na mabetishiti ya kutosha. Wagonjwa wanatakiwa wakenda kutaka matibabu,wachukuwe zana zao wenyewe tokea pamba,gauze,vijembe vya kunyolea na hata chupa za Drips pia wende nazo shuka za kutandika vitandani,mito na foronya zake na nguo za kujifunikia wakati wa kulala vyote hivyo lazima waendenavyo mwenyewe; kama si hivyo basi hatapata matibabu. ubavuni mwao wakitizama wanaiyona Mapinduzi Wing bwana na bibi wanaingia na kutoka. Tokea miaka yalipoanzishwa mahospitali ya serikali Zanzibar, matibabu yalikuwa BURE KW WOTE. kwa wananchi kwa wageni hata kwa wapita njia. Kuangaliwa na daktari ilikuwa bure, dawa bure, ukilazwa kwa jili ya matibabu, bure. Na Hospitali zilikuwa Hospitali kweli kwa kila kitu.Madawa ya kila maradhi yalikuwepo. Madaktari wenye ujuzi wa kazi zao, waliosomeshwa wakakhitimu walikuwepo wa kutosha.Sivyo kama ilivyo hivi sasa wauguzi (Staff Nurse) ndio madaktari tana wa kufika kuuchana na kuupasuwa mwili wa binadamu Kwenye nchi yenye sheria,pindi likitokea lolote, basi ushahidi wa watu kama hao, hauwezi kukubalika katika mahakama za sheria, kuwa ni ushahidi wa kidaktari. Lakini ndio kama ule masemo wa kiswahili, Likikosekana la mama hata la punda hufaa; Ni kweli kulikuwepo katika hospitali kuu ya serikali sehemu maalumu za kulala wagonjwa wa kulipa.Lakini hayo yalikuwa kwa kupenda kwake mwenyewe huyo mgonjwa.Malipo yenyewe yalikuwa kwa watu wenye kufanya kazi serikalini, walikuwa wakilipa shs sita kwa siku, na waliokuwa hawafanyi kazi serikali, walikuwa wakilipa shs 12. Kwa hakika hakukuepo tafauti kubwa baina ya huko kwa malipo na kwa bila ya malipo. Tafauti ziliyokuwepo baina ya sehemu za kulala wagonjwa kwa malipo na sehemu za bure za nyongeza tu, Sio ya kwa lazima. Kwa mahitajio ya kimatibabu kulikuwa hakuna tafauti hata kidogo. Tafauti zilikuwa kama hizi: katika upande wa malipo, wangonjwa walikuwa wakipewa panjama za kulalia, vyakula vyao wakiletewa katika sinia na sahani zao zilikuwa za kaure na walikuwa wakipewa chai ya kitandani (bed-tea) na pia walikuwa wakipewa chai ya alaasiri (afternoon-tea). pia walikuwa wakipewa taula ya kujifutia maji baada ya kukoga.Chakula kikubwa kilikuwa wali na mchuzi wa nyama na kibakuli cha punding. Upande wa wagonjwa wa bure,wao walikuwa wakiletewa vyakula vyao bila ya kutiliwa katika sinia na sahani zao zilikuwa senti (alimunium) chai walikuwa wakitiliwa katika makopo ya senti. Hapakuwa na tafauti kubwa ya chakula isipokuwa wao badala ya kupewa chai ya kitandani,wakipewa uji.Wagonjwa wote-wa kulipa na wa bure-walikuwa wakipewa matunda na mboga. Na ikiwa mgonjwa ameandikiwa na daktari chakula maalumu kutokana na maradhi yake,basi alikuwa akipewa chakula hicho (bila ya malipo) sawa sawa na mgonjwa aliyekuwa katika sehemu za malipo ikiwa maradhi yao ni ya namna moja.Madaktari na wauguziji walikuwa ndio hao hao kwa wote,wa kulipa na wa bure.Leo tuambiwayo kuwa matibabu bure mgonjwa akenda hospitali baada ya kuangaliwa na daktari (pengine na muuguzaji nurse tu) na akaandikiwa dawa, akifika kwa watoa dawa jawabu analolipata ni kuwa, dawa hizi hazipo, kanunuwe nje jawabu kama hizo ni za kila siku.Ukenda kuwaangalia wangonjwa waliolazwa, ukianza tu kupanda ngazi, unakaribishwa na harufu za mikojo na za mashonde kutoka vyooni.Hospitali haina maji ya kutosha.Ukiingia katika vyomba vya kulala wagonjwa,unawakuta mapaka wanacheza foliti kwa jinsi ya uchafu uliomo ndani. Makunguru wana ruka huku na huku humo vyombani, wanapita dirisha hili na kutokea jingine. Sakafu zinanata kwa uchafu. Sasa watizame hao wagonjwa namna walivyo lala humo vitandani.Vichekesho khasa.Wengine wamejifunika kanga za kisutu, wengine za mkeka,wengine za visima na za namna mbali mbali.Utadhani watoto wa kizamani walipokuwa wakitiwa kumbini (kutahiriwa) Mabetishiti yaliyotandikwa vitandani kwa ilivyokuwa kila moja kaja na lake,basi, huyu katandika jeupe la mfuto,huyu lililofumwa tausi na huku limeandikwa KARIBU MGENI,na kwa kipembani ya chumba utaona mengine yameandikwa FURAHA YA BIHARUSI, na jengine limeandikwa kwa mandishi naksi SINA MWENGINEWE,au MAPENZI YETU YA UTOTONI,au MIMI NA WEWE HATULISHANI YAMINI,mradi huwa rangi rangire.Hospitali zimepoteza jina na thamani yake kwa kila upande,haziwezi hata kidogo kutowa huduma zitarajiwazo.

Hiyo ndio hali ya hayo yanayoambiwa ni MATIBABU BURE !!! Lakini haya yote yanaowapata ni wananchi wa kawaida tu.Ama wenyewe wakina fulani na fulani pamoja na watoto wao,wao bukheri wa sururu hata hawana khabari nayo wala hawayasikii licha ya kuyaona. khalafu kwa kuundanganya umma ati husema, Tumeondoa serikali ya Kisultani na Kibwanyenye. Wakati wa huo Usultani, Mfalme wa nchi hajapata kuwa na hospitali yake peke yake.Yeye pamoja na ukoo wake wakenda katika hospitali hiyo hiyo wanayokwenda watu wa kawaida. Aliyekuwa Mfalme wa nchi, Seyyid Abdulla Bin Khalifa Bin Haroub,alipopata maradhi,alilala katika hospitali hiyo hiyo na alifanyiwa operesheni katika hospitali hiyo hiyo wanayotibiwa watu wa kawaida.Wakoloni wa Kiingereza waliweka sehemu yao ya kutibiwa waliita  European Wing kutokana na makelele ya wananchi,khasa kutokana na makala yaliyokuwa yakiandikwa katika gazeti la wananchi la mwongozi sehemu hiyo ilibadilishwa jina na bada yake kuitwa European Wing ikaitwa West Wing kutokea wakati huo ilikuwa wazi kwa yoyote mwenye kupenda kwenda sehemu hiyo ikiwa yutayari kulipa ada zilizowekwa.Leo baada ya Mapinduzi ya kuleta usawa na kuondowa Usultani na Ubwanyenye, Mheshimiwa akiumwa na mdudu upande basi mbio anachukuwa ndege anakwenda zake Uiingereza au Ujerumani kwa matibabu. Ikiwa matibabu yapo nchini BURE, mbona wao wanayakimbia na kuyafuatia ya malipo,tena katika nchi za ngambo na kwa kutumia pesa za wanyonge kwa matibubu yao...?? sasa ipi inayostahiki kuitwa serikali ya Kibwanyenye....?? Hii ya waheshimiwa waliyojitenga mbali na umma au ile ya waliyokuwa wakiishi pamoja na umma....?? Mwenye macho haambiwi tizama! Unaweza kuwandanganya baadhi ya watu baadhi ya siku, lakini huwezi kuwandanganya watu wote siku zote.
Merehemu Sheikh Amani Thani Fairuz Mwenyezi Mungu Mlaze Pema Peponi Ameen.

KISHA NYINYI MUNAYAITA MAPINDUZI MATUKUFU HIVI KWELI NYINYI MUNAJUWA UTUKUFU NI NINI AU DUNIA IMEWAVA KISAWA SAWA MPAKA MNAKUFURU MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA KATUPINDUWA TENA WAZANZIBARI NA KUWEKA VIONGOZI WAWATAKAO WAO WAKINA BT TUNAENDELEA TENA KUKA CHINI YA SERIKALI YA KIKOLONI YA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA MPAKA MIAKA MITANO IMALIZIKE KISHA TUTIWE TENA KATIKA SHENGESHA LA UCHAGUZI NA KUPIGA KURA KISHA WAZANZIBARI WAPIGE KURA NA KUCHAGUWA VIONGOZI WAWATAKAO MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA ATAKUJA NA STYLE MPYA YA KUZIPIGA KURA ZA WAZANZIBARI CHINI NA KUTUEKEA VIONGOZI WAWATAKAO KISHA TUTAKA TENA CHINI NA KUSUBIRI UCHAGUZI WA 2025 MAMBO YATAKUWA HIVYO HIVYO KISHA TUTAKA CHINA NA KUSUBIRI UCHAGU WA WA 2030 TUKIWA HAI KAMA HATUKO TENA WATAKAO BAKI WATAFANYIWA TENA HIVYO HIVYO NA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA KISHA WATAKA CHINI WASUBIRI......>>> MPAKA KIYAMA KISIMAME BASI NI BORA TU TUKUBALI KUWA NDIO TUMEKUBALI KUWA CHINI YA MKONI MWEUSI TANGANYIKA KULIKO UPUMBAVU HUU WA UCHAGUZI AMBAO KILA MOJA WETU HAPA ZANZIBAR KAMA UCHAGUZI WA MARA HII HAUJAWASOMESHA WALA HATUTA SOMA TENA MILELE. 

KILA MZANZIBARI ALIYE IPIGIA KURA CCM AU MPAKA WAKATI HUU BADO ANAISAPOTI CCM ILI IBAKI MADARAKANI JAPO KUWA CCM IMESHINDWA UCHAGUZI AJUWE NA YEYE ANACHANGIA KUENDELEZA DHULMA NA KUFUNGWA KWA MASHEIKH NA KUTHALILISHWA KWAO NA KUENDELEZA DHULMA KATIKA NCHI YA ZANZIBAR UKAE UKIJUWA UTAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA,KUDHULUMIWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

Thursday, April 28, 2016

ZITTO KABWE HATUMBUWI MAJIPU ATUMBUWA MADONDA NDUGU YALIYO FICHWA KWA KUVA MASUTI NA TAI


Mheshimiwa Spika, Tangu tuanze Mkutano huu wa Bajeti mwaka 2016 kumekuwa na malalamiko kutoka kwa Wabunge na hasa wabunge wa kambi ya Upinzani Bungeni kuhusu ukiukwaji wa Sheria mbalimbali za nchi katika masuala ya Bajeti. 

Jana jioni Mwenyekiti wa Bunge Mheshimiwa Andrew Chenge alitoa Changamoto kuwa Wabunge tuseme ni sharia gani zimekiukwa katika mchakato mzima wa Bajeti ya Nchi hivi sasa. Kwa maoni yangu, kuna ukiukwaji kadhaa wa sharia ya Bajeti, sharia namba 11 ya mwaka 2015 katika mchakato wa Bajeti ya Mwaka huu. Nitaeleza kwa ufupi.

Mheshimiwa Spika, kifungu cha 8 cha sheria ya Bajeti kinaeleza namna ambavyo mfumo wa Bajeti ya Serikali unapaswa kuwa. 

Vifungu cha 8(1)(b) na 9(1)(a) na 19(1) vinaeleza namna mchakato wa Bajeti unavyopaswa kuwa. Vifungu hivi vinataka “Planning and Budget Guidelines” zipitishwe na Bunge katika mkutano wake wa Mwezi Februari kila mwaka. Sheria inataka “budget ceilings” ziidhinishwe na Kamati ya Bajeti na baadaye Bunge linapokaa kama Kamati ya Mipango.

Mheshimiwa Spika, Bunge lilikaa kama Kamati ya Mipango na kupitisha Mpango wa Bajeti uliokuwa na Bajeti ya Tshs 23.7 trilioni kama ulivyowasilishwa na Waziri wa Fedha na Mipango. Hata hivyo Bajeti inayojadiliwa sasa ni Tshs 29.5 trilioni tofauti kabisa na sio tu viwango vilivyopitishwa na Bunge mwezi Februari bali pia hata vipaumbele vyake ni tofauti. 

Hili ni suala la Utawala bora (governance issue) kwani taratibu za utungaji wa Bajeti zimeainishwa na sheria na kama sheria hazifuatwi ni vigumu sana hata Bajeti yenyewe kutekelezwa.

Ili kurekebisha hali hii ni lazima Bunge likae tena kama kamati ya Mipango na kupitisha upya viwango vya juu vya bajeti kabla ya mjadala wa Bajeti kuendelea au angalau kabla ya kupitisha Bajeti Kuu mwezi wa Juni 2016.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Rais Ikulu inapasa kuzingatia sana sheria na taratibu tulizojiwekea kwani madhara ya kutofuata sheria ni makubwa mno.

 Kwa mfano hivi sasa Bajeti za Taasisi hazimo kwenye vitabu vya Bajeti ya Serikali kinyume na Sheria ya Bajeti ambapo hivi sasa Bajeti za Taasisi zote za Umma zinakuwa ni sehemu ya Bajeti ya Serikali na Wabunge wanapaswa kuwa na nyaraka za bajeti hizo. 

Ofisi ya TR kwa mujibu wa kifungu cha 17(a) cha Sheria ya Bajeti ilipaswa kuunganisha Bajeti za Mashirika yote ya Umma na kutoa kitabu chake kwa Wabunge.

Mheshimiwa Spika, Serikali inapaswa kutoa maelezo ya kina kwa Wabunge kuhusu masuala haya ili kuzuia ukiukwaji wa Sheria tulizojitungia wenyewe.

TAKUKURU na kesi za Ufisadi Mkubwa Nchini

1. Ufisadi wa Hati Fungani ya Tshs 1.2 trilioni Standard Bank ya Uingereza

Mheshimiwa Spika, Tarehe 8 Machi mwaka 2013 Serikali ya Tanzania ilikopa fedha $600 milioni ( 1.2 trilioni) kutoka nje kwa msaada wa Benki ya Standard ya Uingereza ambayo sasa inaitwa Standard Bank ICIC Plc. Mkopo huo wenye riba yenye kuweza kupanda (floating rate) umeanza kulipwa mwezi Machi mwaka huu ( kama Serikali imeanza kutekeleza mkataba). 

Mkopo huu utalipwa mpaka mwaka 2020 kwa mikupuo 9 inayolingana. Ifikapo mwaka 2020, Tanzania italipa deni pamoja na riba jumla ya $897 milioni ( takribani tshs 2 trilioni ).

Mkopo huu umegubikwa na ufisadi na kwa kuwa baadhi ya Watanzania wamefikishwa mahakamani kuhusiana na sehemu ya mkopo huu, sitapenda kueleza upande wa waliopo mahakamani.

Kesi iliyopo mahakamani inahusu $6 milioni ambazo inasemekana ( kwa mujibu wa nyaraka za mahakama) kuwa zilitumika kuhonga maafisa wa Serikali ili Benki hiyo ya Uingereza iweze kupata biashara iliyopata. 

Jambo la kushangaza ni kwamba wanaosemekana kula rushwa hiyo hawapo mahakamani mpaka sasa. Vile vile waliotoa rushwa hiyo hawapo mahakamani mpaka sasa. Waliopo mahakamani ni wanaosemekena kutumika kupeleka rushwa. 

Mjumbe kashtakiwa, lakini aliyemtuma hajashtakiwa na aliyepelekewa kilichotumwa hajashtakiwa. Hapa kuna tatizo la msingi ambalo tukilitatua Serikali yetu itaepuka masuala kama haya siku za usoni.

Mheshimiwa Spika, Hapa mbele yangu nina barua ambayo kundi la Watanzania zaidi ya 2000 kutoka kona zote za dunia wamesaini kutaka Benki ya Standard ya Uingereza ichunguzwe kwenye suala hili la HatiFungani. 

TAKUKURU walitumia taarifa ya Taasisi ya Uingereza ya SFO katika kuchukua hatua zinazostahili dhidi ya Watanzania wanaotajwa katika sakata hili. 

SFO haikufanya uchunguzi dhidi ya Benki ya Uingereza ya Standard Bank. Hatujui ni kwa maslahi mapana ya Uingereza au ni kwa kupitiwa. Sisi Tanzania tumejikuta tunafuata matakwa ya Uingereza katika jambo hili, kiasi cha hata kutumia ushauri wa kitaalamu wa Waingereza katika jambo hili. 

Leo hii TAKUKURU inasaidiwa katika kesi hii na wataalamu kutoka Uingereza katika kesi inayohusu Benki ya Uingereza! Watanzania walioandika petition kutaka Benki ya Standard kuchunguzwa wanataka ukweli wote kujulikana – Standard Bank walihusika kwa kiwango gani katika kutoa rushwa ili kupata biashara? TAKUKURU wanapaswa kufanyia kazi jambo hili kwa kuwafungulia mashtaka Standard Bank, mashtaka ya kutoa rushwa ili kupata biashara nchini. 

Hata hivyo TAKUKURU inaogopa wazungu, inaogopa kuwaudhi watu wanaowapa ushauri wa kitaalamu kuhusu kesi za rushwa!

Mheshimiwa Spika, maslahi ya Tanzania hapa ni makubwa mno. Iwapo tutafanikiwa kuonyesha kuwa Benki ya Standard ilihonga kupata biashara nchini kwetu Tanzania itafaidika kwa namna mbili. 

Moja, itakuwa ni fundisho kubwa kwa makampuni ya kimataifa kwamba Afrika sio mahala pa kuhonga na kupata kazi na kutoadhibiwa. Mbili, Tanzania haitalipa mkopo huu na riba zake. 

Tutakuwa tumeokoa zaidi ya tshs 2 trilioni katika Deni la Taifa na kuelekeza fedha tulizokuwa tulipe riba kwenda kwenye kuhudumia wananchi wetu kwenye Afya na Elimu. 

TAKUKURU waongozwe na maslahi mapana kwa Taifa badala ya kutafuta sifa ndogo ndogo za ‘wangapi wamefikishwa mahakamani’. Ni lazima taasisi zetu sasa zianze kutazama mambo kwa picha kubwa.

Mheshimiwa Spika, hii sio mara ya kwanza SFO kufanya ilichofanya dhidi ya Tanzania. Mnakumbuka kesi ya rada na Shirika la BAE la Uingereza. Safari hii Tanzania isikubali kubeba tu makubaliano ambayo SFO inafanya na makampuni ya kimataifa.

 Ni lazima tufanye uchunguzi wetu na tufungue kesi dhidi ya makampuni haya. Haiwezekani wawe ni Watanzania tu wanaoshtakiwa kwa rushwa na kuwaacha wanaotoa rushwa hizo wakiendelea na biashara zao kama kawaida.

Mheshimiwa Spika, Taarifa zilizopo sasa kwenye vyombo vya habari ni kwamba Benki hii kupitia tawi lake la Tanzania ( Stanbic Bank ) siku ambayo walipata ‘deal’ la Bond ndio siku hiyo hiyo walipewa kazi na Serikali ya kufungua akaunti ya Escrow kuhusu fedha za Bomba la Gesi kutoka Mtwara. 

Kimsingi biashara hii ya Escrow akaunti katika Benki hii ni kubwa zaidi kutoka ile ya mkopo kwani ni biashara ya kutunza fedha za Bomba kwa miaka 20! Benki hii ilipata biashara kubwa kama hii bila ya kuwepo kwa zabuni yeyote ile na kuleta ushindani. 

Lakini pia kama kulikuwa na umuhimu wa kufungua akaunti hii ni kwanini Shirika la TPDC halikufungua akaunti hii katika Benki Kuu ya Tanzania? Haya ndio mambo TAKUKURU wanapaswa kuchunguza katika kulinda maslahi ya nchi yetu dhidi ya makampuni makubwa kutoka nje.

Mheshimiwa Spika, Vile vile kuna taarifa kwamba hata fedha ambazo zilipatikana kutokana na mkopo huu hazikufika kule kunakotakiwa. 

Nimewasilisha maswali Wizara ya Fedha kutaka kujua miradi ambayo fedha hizi zilikwenda. Hata hivyo kutokana na orodha ya miradi niliyonayo na kutokana na habari za hivi karibuni za Serikali kudaiwa na wakandarasi, mradi wa Kinyerezi na hata mradi wa Kiwira, ni dhahiri kuwa sehemu ya fedha zilizopatikana katika mkopo huu hazikupelekwa huko. Uchunguzi wa kina unatakiwa kwenye eneo hili ili kupata ukweli na kuzuia mambo kama haya kutokea siku za usoni.

Mheshimiwa Spika, nitatumia kanuni ya 120(2) kutaka Bunge tako tukufu kuunda Kamati Teule kuichunguza Benki ya Standard ICBC ya Uingereza na kampuni yake dada ya Stanbic Tanzania kuhusiana na Mkopo wa Hatifungani $600m, matumizi ya mkopo huo na ufunguzi wa Akaunti ya Escrow ya Bomba la Gesi la Mtwara – Dar es Salaam. 

Kwa sasa ninawasilisha mezani nyaraka zote nilizonazo kuhusiana na Mkopo huu kwa ajili ya Bunge kupitia kabla ya kuwasilisha Hoja ya Kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kuichunguza Standard Bank ICBC na Stanbic Tanzania

2. Uchunguzi wa IPTL Tegeta Escrow Account

Mheshimiwa Spika, Mwaka 2014 TAKUKURU waliijulisha Kamati ya Bunge ya PAC kwamba ilikuwa inachunguza na kumaliza uchunguzi kuhusu miamala ya kutoka Akaunti ya Tegeta Escrow Benki Kuu ya Tanzania kwenda Benki ya Stanbc Tanzania.

Katika taarifa zote ambazo TAKUKURU inatoa kuhusu kesi za ufisadi, hakuna hata siku moja wanasema kuhusu uchunguzi huu na lini wahusika waliochota fedha za umma watafikishwa mahakamani. Naomba tupate kauli ya Serikali kuhusu jambo hili kwani ni moja ya JIPU kubwa ambalo tunadhani Serikali inalikimbia. 

Serikali inaogopa nini? Serikali inamwogopa nani? Kwanini kesi ya ufisadi wa IPTL unakaliwa kimya? Kwa maslahi ya nani?

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha
Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto, Mb
Kigoma Mjini

THE PRESIDENT OF TANZANIA;S DARKER SIDE

Tanzania’s new president, John Magufuli, has since inauguration in November was hailed for its fight against corruption and public waste. Less well known is restriction of freedom of speech and democratic rights.
Grete Benjaminsen
Media and connoisseurs of Tanzania in Norway has given little attention to the new president, John Magufulis small charming side – namely increasing pressure on utterance – and freedom of the press and the curtailment of democratic rights in the country. On Zanzibar many people believe that the celebration of Magufuli as a crafty corruption hunter has given him and his party the opportunity to carry out coups in the archipelago.
Inspired by Rwanda
It is said that Magufuli draw inspiration from neighboring Rwanda. After six months of self-imposed travel ban, it was precisely to Rwanda he let his first foreign trip as president. Rwanda has in recent years become a favorite among investors because of an effective state apparatus and zero tolerance for corruption. The country has shown great progress in the achievement of the MDGs, but is also known for strict media control, comprehensive monitoring and persecution of political opponents.
Also Tanzanian authorities accused of limiting utterance – and press freedom. A new law for regulating Internet use allows for at least six months’ imprisonment for publishing false and misleading information. Law ˗ which admittedly was introduced under the previous president ˗ has created uncertainty about the legality of information sharing on social media. During his campaign, the law was adopted on several occasions. Among other things, when the main opposition party Chadema premises were stormed and eight of its employees accused of publishing “inaccurate and unconfirmed information” including on Facebook and Twitter.
It has also been introduced restrictions on contact foreign embassies and international organizations may have with the authorities, as well as the opposition, representatives. Instead of sending National Assembly debates live on TV, transmitted now only summary afterwards – censored summaries according to critics. In January, the Dar es Salaam-based newspaper Mawio closed after published critical articles about the political situation in Zanzibar.
Disputed re-election in Zanzibar
And it is precisely in relation to the situation in Zanzibar that Magufuli show their least democratic pages. Zanzibar is part of Tanzania but independence within a range of policies. In addition to voting in the election on the Tanzanian president and parliament, votes zanzibarere on own president and parliament.
Since the reintroduction of multi-party system has Magufulis party, Chama Cha Mapinduzi (CCM), met strong resistance from the Civic United Front (CUF), the main opposition party in Zanzibar. After every election, however CCM been designated as wins. CUF has protested electoral fraud – often with the support of international election observers. A reconciliation process ahead of elections in 2010 led to the referendum on constitutional amendments that would ensure the two main parties place in the future governments in Zanzibar. Elections in 2010 went off peacefully. Also this time meant CUF cheated of victory, but in the streets participated CUF supporters in celebration of Zanzibar’s first coalition government.
After the election on 25 October 2015 so CUF long to win, until the electoral commission chairman, Jech Jech Salim suddenly, and without support from other commission members, annulling the entire election because of unspecified “irregularities”. An overall observation corps argued however that the elections were the best implemented in Zanzibar history and legal experts believe Jech lacked a mandate to cancel.
After unsuccessful negotiations between CCM and CUF, declared Jech new elections in Zanzibar. The disputed election took place on March 20. CUF and most other opposition parties boycotted. So did most election observers. The day after the CCM Not surprisingly declared the winner.
Threats and violence
International observers wonder that the turbulent situation in Zanzibar has not led to more unrest. Prior to the election claimed CUF authorities constantly tried to provoke reactions, including by sending groups of armed young men to intimidate the population. It may seem that people listened to CUFs requests to deal in peace. In the weeks before the election circulating images on social media by rows of military vehicle that ran ashore on Zanzibar. The streets patrolled armed Tanzanian riot police. This has probably also contributed to curbing insurgency will.
In the time before a new election came the daily reports of arrests and violence against people linked to the opposition. Government officials claimed to have been threatened with dismissal if they did not go to vote, and several CUF leaders were taken into custody. There were also journalists, including one of Zanzibar’s most famous freelancers, Salma Said. She was abducted from the airport in Dar es Salaam by unknown men two days before the election and abused before she was released on Election Day. According to Said himself said the kidnappers that they did not like the job she did.
March 24 was Zanzibar’s new government inked at a ceremony where no Western embassies were to place. Not surprisingly, do not recognize the opposition the new government. Parliament now consists only of CCM members and vice stool, in which after the new constitution should be a coalition government, remains open.
necessary cleanup
Magufuli has largely remained silent about Zanzibar. He has concentrated on convincing voters and the world in general that he is serious about its anti-corruption campaign and measures to reduce the unnecessary use of public resources. When the National Assembly was due to open again after he had been president, he canceled the traditional banquet. The money was used to purchase equipment for the country’s largest public hospital. When government formation he reduced the number of ministers from 30 to 19, and introduced a temporary halt in foreign travel for government officials. When Independence Day to be celebrated in December, dropped his party and launched instead a dugnadsdag for clearing rubbish around the country. In other words, not only in the state apparatus it should be cleaned up.
But Magufulis measures are not only of populist character. Cleanup in tax administration has so far led to more than a doubling of the monthly tax revenues. In the future they hope most ambitious observers that anticorruption measures also focus on the more structural causes of corruption in the country.
Shelf Stens shadow side
Zanzibar has Magufuli been less willing to clean up. When he has been asked to mediate in the political conflict, he replied that it would be meddling in internal zanzibariske conditions. Meanwhile, he sends as chief of police and military troops to the islands ˗ with the consequence that he is perceived more as an occupier rather than as president of many zanzibarere.
Magufulis undemocratic sides creates challenges for partner countries like Norway. Several donors are now considering what they can do. USA has already halted an infrastructure program to Tanzania worth four billion crowns. Although it is uncertain whether the stoppage of funds will lead to real change in how CCM govern the country, wanted such sanctions are welcomed by many in Zanzibar. CUF wants plus travel restrictions and closures of key CCM leaders overseas accounts.
Meanwhile CUFs leader in Zanzibar, Seif Sharif Hamad, asking people to relate in peace. During a press conference on 10 April he admonished once his supporters that “justice can only be achieved through democratic means.”
In addition to impede CUFs effort to convince people that democracy is the best way forward, helping the unilateral tribute Magufuli has received in recent months to conceal human rights violations and CCM regime attempted marginalization of political opponents. And ˗ it undermines a legitimate struggle against this.

KIKWETE JE ATAPANDISHWA KIZIMBANI....?? KWA MAKOSA YA UFISADI ULIOKITHIRI NA KUPORWA KWA HAKI ZA WAZANZIBARI KUTOKANA NA KUFUTWA KWA UCHAGUZI ULIOKUWA HURU NA WA HAKI WA OKTOBA 2015


UONGOZI ni dhamana. Ni dhamana kubwa na nzito mtu kujitwika nayo au hata kutwikwa nayo. Mzigo wa uongozi unazidi kuwa mzito uongozi huo unapokuwa uongozi wa taifa. Hili ni wazi, na halina shaka, isipokuwa kwa wasiotaka kulijuwa.
Dhamana nayo ina majukumu yake. Na majukumu hayo yanazidi kuwa nyeti dhamana hiyo inapokuwa ni dhamana ya kuliongoza dola, watu wa hilo dola, yaani wananchi, na rasilmali zake ambazo kwa hakika huwa ni rasilmali za hao wananchi.
Kuna wenye kuhoji kwamba aliyesimamia utawala wa awamu ya nne anastahiki ashitakiwe kwa matumizi mabaya ya madaraka aliyokuwa nayo.
Wanayataja mambo mawili makuu: la kwanza, ufisadi uliokithiri na la pili, kuporwa kwa haki za Wazanzibari kutokana na kufutwa kwa uchaguzi uliokuwa huru na wa haki wa Oktoba 2015.
Madai yote hayo mawili ni mazito.
Wenye kuyatoa wanaendelea kuhoji kwamba kwa kutochukua hatua imara kupambana na ufisadi Rais mstaafu Jakaya Kikwete aliwezesha pawepo nafasi kubwa iliyowaruhusu wezi kuiba mali ya serikali.
Wakati huo huo nafasi hiyo au mazingira hayo yamewawezesha watumishi wa serikali waendeshe mambo ovyo ovyo.
Kuendesha mambo ovyo ovyo, kienyeji, kwa kujizingatia “sisi kwa sisi” tu bila ya kuwajali wananchi walio wengi kumekuwa na athari zake. Athari hizo ni ovu na nyingi.
Miongoni mwazo ni kuzusha hali zinazoupalilia ufisadi wa kisiasa na wa kiuchumi, kuzusha hali au mazingira yasiyoweza tena kuudhibiti ubadhirifu wa fedha za umma. Na ni hali hizo hizo zinazoiruhusu serikali iwe inatoa mikopo kiholela, mikopo inayowafaidisha zaidi wanasiasa na watumishi wakuu wa serikali.
Kwa jumla kuna ushahidi mkubwa wenye kuonyesha na kuthibitisha jinsi ufisadi ulivyojengeka nchini, hususan katika awamu ya nne, kwa ubia uliozidi kufanikishwa baina ya wanasiasa, mafisadi katika sekta ya binafsi na watumishi wakuu wa serikali.
Hili ni jengo la ufisadi lililojengeka juu ya misingi iliyochimbwa na kusimamishwa na wanasiasa wa chama kinachotawala.
Chama hicho kimekumbwa na ugonjwa uleule uliovikumba vyama vilivyopigania uhuru katika nchi nyingi za Kiafrika. Huu ni ugonjwa wa kuamini kwamba ni vyama hivyo tu vyenye haki ya kutawala na viongozi wa vyama hivyo tu ndio wenye haki ya kuitwa watawala.
Wakishaitwa watawala, wakavikalia viti vya utawala huanza kujiona kuwa wao ndio serikali na serikali ndio dola.
Kwa hivyo, kwa kuwa wao wanajiona kuwa ndio serikali basi mantiki yao inawafanya waamini kwamba wao pia ndio dola. Siyo tu kwamba dola ni lao wao peke yao lakini wao ndio hasa dola. Wao ndio dola na dola ndio wao. Ndiyo maana wanalisarifu dola watakavyo. Chambilecho Joseph Mihangwa wanaligeuza dola kuwa “shamba la bibi”.
Kwa hakika, makala ya Mihangwa katika matoleo mawili yaliyopita ya gazeti hili pamoja na makala ya ukurasa wa mbele wa toleo la wiki iliyopita chini ya kichwa cha maneno “Nchi ilivyotafunwa mbele ya Kikwete” ni makala ambayo kila Mtanzania anapaswa ayasome.
Makala yote hayo matatu yanatoa mwanga kuonyesha jinsi utawala wa awamu ya nne ulivyokithiri si katika ufisadi tu bali pia kwa uzembe katika uendeshaji wa serikali.
Ukishayasoma makala hayo hutokuwa na shaka yo yote kwamba Rais wa awamu ya nne ni mtu anayetakiwa afikishwe mahakamani ila Katiba tuliyo nayo huenda ikamkinga. Juu ya hayo, kuna wenye kusema kwamba kwa Magufuli chochote kinaweza kuzuka na kwamba hata ile haramu ya Zanzibar inaweza ikawarejea wenyewe.
Hata hivyo licha ya Magufuli na ayafanyayo, si wengi wenye matumaini hayo. Hoja yao kubwa ni kwamba hakuna wa kuaminiwa, na kuaminika, ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Yeyote yule anayeibuka akawa na ujasiri wa kuwaambia kweli watawala kwamba wako uchi na wanahitaji wajistiri huambiwa kuwa ni msaliti na haini. Jaza yao huwa ni kudhalilishwa na kugandamizwa. Na wenye kuwagandamiza huwa ni wale wale waliokuwa wakipigania haki na usawa wakati wa kupambana na ukoloni. Mfumo wa kisiasa wa aina hiyo haukubali abadan kuruhusu pawepo na mfumo mbadala.
Hayo si mageni katika historia ya ulimwengu. Tangu Mapinduzi ya Ufaransa (1789 hadi 1799), mara nyingi wakombozi wa nchi mbali mbali wamekuwa wakigeuka na kuwa wagandamizi. Waliokuwa wakionewa wakawa ndio wenye kujitutumua kuwaonea wengine. Na wakionea na wakiwaumiza watu kwa kuzikanyaga haki zao za binadamu hawadhani kuwa wanawajibika kuwaomba radhi wananchi.
Hii ndiyo moja ya sababu zinazowafanya baadhi ya watu katika nchi za Kiafrika wawe wanahoji kimwehu kwamba bora kutawaliwa na wakoloni kushinda kutawaliwa na Waafrika wenzetu. Hoja yao kubwa ni kwamba kimsingi maisha yao ya kawaida hayakubadilika tangu enzi za ukoloni. Wanasema hawaoni tofauti kubwa kwa namna wanavyotawaliwa sasa na walipokuwa wakitawaliwa na wakoloni.
Sababu ya hayo ni kwamba hawa watawala wetu wa leo wamerithi mengi kutoka kwa wakoloni. Wamerithi sera na hata namna ya kufikiri, namna ya kuyatumia madaraka waliyo nayo na namna ya utendaji kazi wao. Wanayakumbatia na kuyapakata madaraka kama ni yao wao watawala peke yao bila ya kuwashirikisha wengi wa wananchi.
Mambo ya ufisadi hayako kwetu tu lakini wenzetu nao pia wanayo ila wao wameweza kuzitumia nguvu za umma kupambana nayo. Wameweza pia kuzitumia taasisi za kidemokrasia kuhakikisha kwamba sheria zinafuatwa. Tuchukulie mifano ya nchi kadhaa za Amerika ya Kati na Amerika ya Kusini.
Sheria katika baadhi ya nchi hizo zinaruhusu marais wastaafu na hata wa sasa wafikishwe mahakamani. Hivi karibuni marais wawili wastaafu wa Honduras na El Salvador walishtakiwa kwa ufisadi.
Serikali ya Rais mstaafu wa Honduras Rafael Leonardo Callejas ilifanya mengi katika ustawi wa jamii lakini mafanikio hayo hayakuweza kumkinga Callejas asishtakiwe. Alikabiliwa na mashtaka saba ya ufisadi alioufanya wakati wa muhula wake wa urais (Januari 1990 hadi Januari 1994). Nchini Honduras, Rais ana muhula mmoja tu wa kutawala wa miaka minne.
Mnamo 2005, Bunge la Honduras liliibatilisha sheria iliyokuwa ikiwakinga Marais wastaafu wasishtakiwe. Sheria hiyo ilipobatilishwa Callejas mwenyewe, kwa hiyari yake, alijipeleka mahakamani na akafunguliwa kesi kwa mashtaka yote yaliyomkabili. Alifanyiwa kesi na halafu Mahakama ikamwachia huru baada ya kuona kwamba hakuwa na hatia.
Halafu Desemba mwaka jana alishtakiwa na Mahakama ya Marekani kwa kuhusika na kashfa ya ufisadi ya Shirikisho la Soka la FIFA wakati alipokuwa mkuu wa Shirikisho la Soka la nchi yake.
Siku kadhaa baada ya kushtakiwa Callejas mwenyewe akenda Marekani ambako alitiwa mbaroni na siku chache baadaye aliachiwa na Mahakama kwa dhamana. Mwezi uliopita alikiri kwamba alikuwa na hatia ya kupokea hongo ya dola za Marekani 500, 000 mwaka 2012, fedha ambazo alikuwa azile yeye na afisa mwengine.
Nchini El Salvador hakimu mmoja alimuamuru Rais mstaafu Francisco Flores ashtakiwe kwa tuhuma za kuziingiza katika akaunti yake binafsi na akaunti ya chama chake dola za Marekani milioni 15 wakati alipokuwa Rais baina ya 1999 na 2004. Fedha hizo zilizokuwa zimechangwa zilikusudiwa waathirika kwa zilzala iliyotokea nchini humo.
Halafu kuna RaisOtto Pérez Molina wa Guatemala aliyechaguliwa Rais 2012 na aliyelazimika kujiuzulu urais Septemba mwaka jana baada ya kukabiliwa na mashtaka ya ufisadi. Molina hivi sasa yuko jela pamoja na aliyekuwa makamu wake. Wote wawili wanakabiliwa na mashtaka ya ulaji rushwa.
Yaliyomkuta Molina ni mara ya mwanzo kumkuta Rais aliye madarakani tangu mfumo wa demokrasia ushamiri katika nchi za Amerika ya Kusini.
Na kuna ya Brazil ambako Rais mstaafu Luiz Inácio Lula da Silva ameshtakiwa wakati uchunguzi ukifanywa kuhusu shutuma za kashfa ya ufisadi zinazoikabili kampuni ya Petrobras, ambayo ni kampuni ya mafuta yenye kumilikiwa na serikali ya Brazil.
Shutuma hizo zinazomkabili Lula ni kitisho kwa mrithi wake Rais Dilma Rousseff ambaye anayumbayumba kisiasa kwa vile Bunge limo katika mchakato wa kumshtaki kwa kutumia vibaya madaraka. Lula anasema shtuma zote hizo ni njama za kisiasa zinazopikwa na maadui wao wa kisiasa.
Kote huko katika eneo la nchi za Amerika ya Kusini Marais siku hizi wanahaha. Wananchi wa huko wakitiwa nguvu na jumuiya za kiraia, zisizo za kiserikali, wamekuwa wakipiga kelele na kuzishinikiza serikali zichukuwe hatua dhidi ya ufisadi na dhidi ya wakubwa wao wenye kushutumiwa kwa mashtaka ya ufisadi.
Rais mstaafu wa Panama Ricardo Martinelli naye anakabiliwa na mashtaka ya ubadhirifu wa fedha za umma, njama za kuwafanyia ujasusi mahasimu wake wa kisiasa na mashtaka mingine ya ufisadi. Kwa amekimbilia Florida, Marekani, lakini Mahakama Kuu ya Panama imetoa amri akamatwe na arudishwe kwao kupandishwa kizimbani
Huku kwetu Kikwete anaweza akaponea chupuchupu. Kwa hali ilivyo, Katiba ndiyo imekuwa kinga yake wakati alipokuwa Rais na sasa baada ya kuuacha urais. Si Katiba peke yake lakini ana kinga nyingine — ule moyo wa kulindana walio nao watawala wetu.
Kwa hivyo, hata kama patakuweko na kipengele cha sheria au mwanya wa kisheria utaoweza kumfanya ashtakiwe kutakuwako na huo moyo wa wakubwa kulindana ambao huenda ukakoroga mambo. Wakubwa wanaweza kufanya hivyo kwa sababu hawaitii maanani demokrasia na wamezoea kuubeza mfumo huo.
Kutokana na hayo ni kheri tuwe na demokrasia ya kibwanyenye kushinda kukosekana demokrasia ya yo yote. Angalau katika mfumo huu wa demokrasia ya kiini macho viongozi wanaweza wakawajibishwa kwa ufisadi wao. - See more at: http://www.raiamwema.co.tz/kikwete-kupandishwa-kizimbani#sthash.Dfd0cJa4.dpuf