Sunday, May 5, 2013

DR KUMBI SHEIN-UNAFUATA MKUMBO WAKUPENDA MUUNGANO ILI YAKO YAKUENDE UBAKI MADARAKANI SIO..??(MULIZE JUMBE NA KOMANDO WA UDONGOO)


Waziri asiyekuwa na wizara maalum, Dr Kumbi.Ali Mohammed Shein amekuwa anzunguka kila kona kuhubiri Muungano feki usiyotakiwa na jumla ya wazanzibari takriban wote na, kuwagomba wale wote wenye mawazo tofauti na yeye kuhusu Muungano huu feki; maneno ya kejeli, fedheha, stihzai na hata kuonyesha ubabe na ukali. Inanijia huruma kusikia anasema yale anayoyasema, maana muandishi wetu wa siri wa free zanzibar people from mkoloni mweusi anasafiri nakufuatilia na kumsikiliza anavyo bwabwaja tu kama mtu aliye payukwa. Swali la mwisho la mwandishi wetu alinalo na kujiuliza: Je, Dr Kumbi.Shein anaujua hasa Muungano feki au anachupia chupia tu.?? Anafuata mkumbo ili yake yamuendee na abaki madarakani..?? au ndio mbinu yake ya kuwafurahisha wafalme wake Tanganyika..?? Kuujua muungano feki, si kujua tarehe iliyoanzishwa Muungano feki au waliouasisi, la hasha. –”mambo yake, na vikorombwezo vyake”.
Naomba nimfahamishe Dr.Kumbi Shein na viongozi ambao ni watumwa wa mkoloni mweusi Tanganyika walio jazana katika bara la wawakilishi bila ya faida yoyote kwa wananchi na nchi ya Zanzibar hasa walioupenda Muungano feki kwa dhati, na Muungano feki ukawapenda wao na matumbo yao bila ya kujali kuwa nchi kwanza sio muungano feki wala chama kwanza:
1. Aboud Jumbe Mwinyi — alikuwa Rais wa Zanzibar. Kufa kupona, dam dam — aliupenda Muungano sana, na alichukua mpaka rasilmali za Zanzibar kuzipeleka Tanganyika na kukiuwa chama cha ASP na kutuletea mkoloni mweusi CCM anae tula huku tukijiona tunakufa. Kuna kipindi Zanzibar ama tulikopesha au tuliwapa Tanganyika pesa, kulipia mishahara yao huko. Record zipo.
Jumbe alizihaulisha taasisi nyeti za Zanzibar, na kuziingiza katika taasisi za Muungao, bila ya idhni ya mtu yeyote yule. Jumbe alichukua hata vifaa nyeti vya utendaji kama vile vya xxx….ikiwemo meli zetu (MV.Mapinduzi/Maendeleo) kwa harakati za ukombozi wa Kusini mwa Afrika, Mozambique, Namibia, South Afrika n.k
Na mengine mengi mengi mengi tu, mengine haifai kuyasema hapa. Mwisho wake ni nini..?? ni Aibu na fedheha, na idhalali juu yake. Mwisho alipouona ukweli yalimkuta yaliyomkuta. Ameondoka na legacy ya kuandika kitabu ‘Partner-ship hana mpya yuko kigamboni ajikongoja’.
2. Nitamuacha Ali Hassan Mwinyi, na Idrissa Abdulwakil.
3. Salmin Amour Juma — huyu naye alikuwa kufa – kupona, laizma Muungano feki udumishwe tu. Amefanya mengi na ameuwa watu wengi kumfurahisha bwana,duli,mfalme mweusi,mkoloni mweusi anaetaka kuhakikisha kuwa zanzibar ni fuvu tu, amedhalilisha watu, ili yake yamuendee, na abaki madarakani. Alikuja na sera za ‘ethnicity’ au kitaalamu ‘ethno-politics’ — kubagua watu kwa mujibu wanakotoka. Pemba-Unguja…CUF-CCM, na taka taka za kisiasa kama hizo, Uhizbu kidogo, Ukomredi kidogo, U-ASP kidogo n.k ili yake yamuendelee na asimame madarakani na kula uluwa hakujuwa kuwa uluwa unamwisho.
Naam, leo yuko wapi komando wa udongo yuko wapi leo..?? na ameishia vipi...?? Siku moja moja ninakwneda kumzuru, na inasikitisha sana kuona hali alivyo sasa, kama mtu aliyekuwa ‘head of state’ wa Zanzibar. Ukweli hasa anajuta tena anajuta sana sana. Mpaka anthubutu kusema kuwa ………!!!!! watu walimuambia kama tunavyokuambia wewe kibushuti Dk Kumbi Shein lakini hakutusikia leo yule pale nae pia ajikongoja hajuwi mchana wala usiku yupo yupo tu.
4. Amani Karume — naye pia amefanya mengi tena mengi mno. Huyu ndiye wa mwanzo kuichukua account ya SMZ na kuihaulisha ndani ya BoT (bank of Tanganyika), that means, mishahara na mambo mengine yote ukachukue BoT kwanza. BoT sio bure, kuna charges nyingi tu, wanaojua hesabu na mifumo ya kibenki, watasema ni how much per day.per each transaction wanatulipisha BoT na tija yao ni ngapi, wanavuna mara tatu au nne kwa Zanzibar (but no thanks). Mwisho wa utawala wake Karume mdogo ni ‘love-hate’ affair na wajomba zake wa Tanganyika. yeye alikuwa akiwaita ‘ndugu zetu wa damu’. Naam, ni kipindi hichi tumeona Watanganyika wengi wameingia Zanzibar, makanisa na mabar mengi yamejengwa Zanzibar kwa kutumia mtindo wa rushwa katika sekta ya ardhi, ambayo yeye na shemeji yake Mansour waliidhiti Wizara hiyo ya Ardhi. Na leo hii eti mansour anatetete nchi, haya labda kamka na watu wengi mnafuata mdundo tu. Kama imamu-maamuma (waladhalina-amiiin)!!!!!
5. Kuna group jengine, nimeamua kuliweka mwisho: Maalim Seif Shariff Hamad na wenzake — hawa walikuwa wamaweza kuuwa, lakini Muungano feki UDUMU, ilikuwa kwao ni fakhari sana kuwamambia kuwa ‘wanaishi Dodoma’ au wanakwenda Dodoma kuhudhuria vikao vya CCM. Tuliona wamefanywa NINI. Kiukweli hasa, Maalim Seif alikuwa anaujua  Muungano feki na anaupenda kuliko Shein. Na kama leo Maalim Seif atarudi CCM, basi atapewa hata Urais wa Muungano feki bila shaka yeyote ile, hasa ukizingatia ‘uhai wa Chama cha CCM’ kwa wakati huu kina kufa mdomo juu kama kuku anaye kunywa maji.
Mnajua Maalim alifanywa nini na hatimaye ilikuwa nini sina haja ya kuhadithia.
 Katika group la Maalim Seif, mtoe Maalim Juma Duni Haji — huyu tokea hapo awali alikuwa hana ‘taste’ na Muungano feki, alikuwa technorat mzuri tu, but rebel mzuri pia kwa suala hili la Muungano feki. Nashukuru kumuona yuko hivyo mpaka sasa (juzi tu alikuwa anasema amekereka sana kuona gazeti la rai la wiki hii limechapaisha makala ya kumtukana mwanasheria mkuu wa serikali, Othman Massoud).
Sasa, turudi tena kwa Dr.Shein — hivi ni kweli anaupenda sana Muungano feki au anatufanyia dhihaka tu na kulinda maslahi yake ya uongozi ya uwaziri asiyekuwa na wizara maalum..?? Mimi naona ni kweli, maana Dr.Shein, hana ‘vision’ ya nchi yetu ya Zanzibar wala ya jambo lolote kimaisha. Capacity yake ni finyu sana, na waliofanya naye pale Hospital wanamjua kwa hilo, hata alipokuwa Vice President wa Tanganyika na Zanzibar inasemekana alikuwa mzigo kwao kiutendaji. Inasikitisha sana kuwa kila wakati/era, Zanzibar tunapata viongozi wasiokuwa na vision wala mission, wala focus……….. !!! na mbububu tu jitu lipo lipo tu almuradi kambiwa yeye ndio kiongozi wa nchi basi hata kama mambo yanaoza na wananchi wanakufa na njaa halijali maana yeye ni kama zombi tu au robot linalo endeshwa na rimoti kutoka Tanganyika linafuata tu.
Tukumbuke kuwa ni utawala huu wa Shein na Kikwete – ndio tumeona kwa mara ya kwanza, holly Quraan imechomwa moto (Zanzibar) na baadaye Tanganyika, pia niwakati huu holly Quraan imekojolewa na misikiti imechomwa moto na kupingwa mabomu na polisi kuingia na viatu na mbwa ndani ya misikiti ni wakati huu wa watawala hawa wawili Shein na Kikwete.Baadaye wanatoa excuse hizi na zile mutakwenda kumueleza nini nyinyi m/mungu siku ya kiyama..??
Wauza Unga na watumiaji wa Unga wanaachiwa,malaya na makahaba wanazidi kumiminika kutoka Tanganyika na kuja kujiuzaa nchini kwetu  Zanzibar, majambazi na wizi wamekithiri kutoka Tanganyika na kuja Zanzibar kuiba mabaar na madanguro ya malaya yanazidi tu Zanzibar wanaangaliwa tu ndio dimokratik au sio Shein – lakini masheikh (9sio uamsho tu) hata yeyote yule, hakuna subra, wala uvumilivu, ukisema umenaswa unatupwa jela. Hao ndio Shein na Kikwete na Muungano wao feki.

No comments:

Post a Comment