Monday, August 29, 2016

VIDEO-UDIKTETA UCHWARA NCHINI TANGANYIKA UNAENDELEA VIONGOZO WA KUU WA CHADEMA WAKAMATWA

MWANA SHERIA AWADHI ALI SAIDI HAKI YA VYAMA VYA SIASA KUFANYA
MAANDAMANO NA MIKUTANO YA HADHARA
Viongozi wa Chadema wamekamatwa na polisi na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam nchini Tanganyika kwa ajili ya mahojiano.

Akizungumzia kukamatwa kwa viongozi hao Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alisema; “Tulikuwa kwenye kikao cha Kamati Kuu kilichojumuisha wajumbe na wabunge kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya chama. Jumla ya wajumbe walikuwa 170. Tukiwa kwenye kikao walikuja watu wanasema tunatakiwa polisi kwa sababu tumekiuka agizo lililokataza mikutano.”

Waliotakiwa kufika makao makuu ya polisi, ni pamoja na mwenyekiti wa chama hicho taifa, Freeman Mbowe; mjumbe wa Kamati Kuu na waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa; Katibu Mkuu, Vicenti Mashinji na naibu katibu mkuu (Bara), John Mnyika.

Mkutano wa kamati kuu ya Chadema, umeitishwa ili kujadili ufanikishaji wa maandamano ya oparesheni UKUTA.

No comments:

Post a Comment