Friday, June 28, 2013

VIDEO-CCM NA CUF NANI MWENYE MATUSI..? BALOZI MDOGO WA NCHI YA TANGANYIKA ALALAMIKA KWA KUPEWA MAJINA.


Balozi mdogo wa nchi ya Tangnyika aliye nchini Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd amehadharisha kuwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa inaweza kumeguka, iwapo viongozi wataendelea kutumia vibaya majukwaa ya kisiasa kwa kutoa kauli za chuki na matusi na kukashifu Serikali kwa maslahi binafsi.
Ingawa Balozi Idd alisema uhusiano wa viongozi wakuu watatu wa nchi ni mzuri: Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad na yeye Balozi Seif Ali Idd, wanafanya kazi vizuri.
Balozi huyo mdogo wa nchi ya Tanganyika, alikishutuma Chama cha CUF kwa kutumia majukwaa ya kisiasa vibaya. Alidai kinatumia lugha za matusi dhidi yake na kumpa majina mabaya.
Alisema kasoro kubwa zinajitokeza katika majukwaa ya kisiasa ambako viongozi wamekuwa wakitoa kauli za chuki zenye kutia wasiwasi mkubwa wananchi na kuhoji uhusiano wa viongozi hao kiasi cha kutukanana hadharani.
Akifanya majumuisho na kujibu hoja za Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliyochangia Bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais kwa mwaka ujao wa fedha juzi, Balozi Idd, alilaumu hususan viongozi wa CUF.
Maalim Seif ni Katibu Mkuu wa Chama hicho, alisema katika mikutano yao yote wanayofanya, wamekuwa wakitumia vibaya majukwaa kumtukana yeye binafsi na kumchonganisha na wananchi na Serikali iliyopo madarakani.

“Napenda kuwaambia wananchi uhusiano wa viongozi wakuu wa Serikali ni mzuri sana…lakini majukwaa ya kisiasa yanatumiwa vibaya kutukanana…Tukiendelea hivyo hatufiki pahala na tutarudi tulikotoka,” alisema Balozi huyo wa nchi ya Tanganyika Balozi ali iddi.
Kwa mujibu wa Balozi huyo wa nchi ya Tanganyika, alisema amekuwa akipewa majina mabaya na viongozi wa CUF katika mikutano ya kisiasa; likiwemo ‘LAANATULLAHI’ wakimaanisha kumlaani. Jambo ambalo alisema anawauliza “amewakosea nini”?. ULICHO WAKOSA WAZANZIBARI NIKUWALAZIMISHA KUBAKI NA MUUNGANO FEKI WA MKOLONI MWEUSI TANGANYIKA NA KUWAFITINISHA ILI WAANZE KUKOSANA ILI WEWE UWATAWALE NA USHA ANZA KUWAFITINISHA NA KUSEMA UTAWARUDISHA WALIKO TOKA KAMA SIO FITINA NI NINI..? PIA KUJIJEGEA MAISHA MAZURI NA KUIBA PESA ZA WAVUJA JASHO NA KUZIPELEKA TANGANYIKA KWA MASULTANI WAKO NA LAMWISHO UKATIA FITINA MPAKA MASHEIKH WAKASHIKWA NA KUTUPWA JELA UNAFIKIRI HATUJUWI. KAMA HUJUWI LEO TUNAKUAMBIA FITNA ZAKO MWAKA HUU ZIMEPIGA MBIZI KWENYE MAJI YA UGOKO.
Balozi Idd, aliwahadharisha viongozi hao kwamba lengo la Serikali ya Umoja wa Kitaifa ni kuleta mshikamano kwa Wazanzibari wote.(MASHEIKH WA UAMSHO NI WAZANZIBARI WATOWENI BASI JELA KAMA KWELI MNATAKA KULETA MSHIKAMANO KWA WAZANZIBARI WOTE NA WAO PIA NI WAZANZIBARI LAKINI NYINYI NI KUSEMA TU NYOYO ZENU ZIMEJA KUTU ZA KUTAKA KUUWA NA KUTESA WATU ILI MUDUMU MILELE KWENYE MADARAKA ASIYE JUWA NINI).
Alionya, kwamba watu wanaweza kurudi ambako walikuwa hawazikani wala kushirikiana katika matukio kutokana na siasa za chuki na uhasama kutawala tangu ulipoingia mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1992.
“Tuache kutukanana katika hadhara za majukwaa ya kisiasa…Hawa CUF sijui nimewakosea nini na kama majina yanachuna basi tayari ngozi yangu ingeathirika,” alisema Balozi Idd.
Alikumbusha viongozi na wananchi kwamba kilichounganishwa ni Serikali yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa, lakini vyama vya siasa na sera ni tofauti na hakuna sababu ya kulumbana katika hilo.
Awali, Waziri wa nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Mohamed Aboud alisema Tume ya uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) iko kwenye mchakato wa kuboresha daftari la wapiga kura nchini kote.
Alitaka wanasiasa kujenga tabia ya kuwaamini watendaji wa taasisi hiyo na kuacha kuwahukumu kwa kuwashutumu, kitendo ambacho kinaweza kuzorotesha utendaji wa kazi hiyo.
“Tume hii imefanya kazi vizuri sana tangu mchakato wa kura ya maoni mwaka 2010 pamoja na kusimamia uchaguzi mkuu ambao ulikwenda vizuri na vyama vyote kuridhika,” alisema Aboud.
Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, iliundwa baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, 2010 kutokana na matakwa ya wananchi kupitia kura ya maoni na kushinda kwa zaidi ya asilimia 64.
Muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, unajumuisha Vyama vya CCM na CUF, ulifikiwa ili kuondoa siasa za chuki na uhasama katika visiwa vya  Zanzibar..

WEWE BALOZI NDOGO WA TANGANYIKA HEBU ANGALIA HIZI VIDEO KESHA JIULIZE NI NANI NA NANI ANAYEFANYA MKUUTANO NA KUTUKANA.WEWE NI MOJA KATI YA WATU AMBAO MULIPINGAA KWA GUVU ZOTE KUSIWE NA SEREKALI YA UMOJA WA KITAIFA LAKINI IKAJA NA GUVU ZA MOLA NA WAZANZIBARI WENYEWE SIO CCM WALA CUF WALA HUWO MUUNGANO WAKO FEKI UNAO UKAZANIA UBAKI WALA WAZANZIBARI HAWATARUDI WALIKOTOKA WAZANZIBARI WATAUNGANA NA KUPIGANA MPAKA TUPATE NCHI YETU NA WEWE BALOZI MDOGO WA WATANGANYIKA UKITAKA UNGANA NASI AU HAMA ZANZIBAR UKAISHI TANGANYIKA ULIKO EKEZA LAKINI HAPA NI ZANZIBAR TU KWANZA SHENGESHA BAADAYEE.

No comments:

Post a Comment