Tuesday, October 13, 2015

AJIRA KWA VIJANA NI KUOKOTA MAKOPO NCHI PEKE DUNIANI INAYO ONGOZA KWA VIJANA KUOKOTA MAKOPO NI NCHI YA TANGANYIKA/NCHI YA ZANZIBAR CCM OYEEEEEEE

NairobiDump1_600_397_80
MAISHA BORA NDIO HAYA CCM OYEEEEEEE
Siku za hivi karibuni hapa nchini Tanganyika na hata nchini Zanzibar ,vijana wengi mitaani wamekuwa wakijipatia kipato chao cha mkate wao wa kila siku kupitia kazi ya kuokota makopo,bila ya kuwasahau wauza maji,mama ntilia,n.k. vijana hao huokota makopo yaliyotupwa na watumiaji ambayo awali yalikuwa na vinywaji aina tofauti tofauti,vijana hao huokota makopo hayo sio kwa kutaka kufanya kazi hio ambayo wachilia kua haina kipato cha maana pia,Ni hatari hata kwa afya zao wanaweza hata kupatwa na maradhi ya kimajabu katha wa kathalika kwa kushinda Jaani na kuchakura uchafu kama kuku almuradi wapate chochote tu chakutia tumboni mwao Viongozi wakiendelea kuwandanganya kuwa watawalete maisha bora mwaka hadi mwaka rais hadi rais hakuna liwalo zaidi ya viongozi na wake zao nawatoto wao kuendelea kutajirika pamoja na mahawara wao hao Viongozi wana wake 2,3 mpaka 4 ndio halali sio vibaya lakini bado wana wanawake wa nje na wanawahudumia kwa kila kitu na pengine wana maisha mazuri na nyumba nzuri zaidi ya wake zake aliyo wao na kuendelea kuza na hao wanawake wa nje mahawara.
Tumeambiwa atii pato la nchi limekua kwa asilimia 6%? Lakini umaskini wa maisha umekua kwa asilimia 100% .
Ukiangalia pato hilo limekua vipi utaona ni vilabu vya pombe ambavyo vimejaa hapa nchini petu Zanzibar kilakona ya mitaa yetu,maduka ya kuza vinyago na kuchonga vinyago utafikiri tuko Kenya,Mageusti House ya kwenda kufanya ufuska na ulanisi,Malaya kutoka nchi mbali mbali waote wanakuja hapa nchini petu Zanzibar,  hakuna shaka kua mila na utamaduni wa Mzanzibari umeporomako asilimia 95% kutokana na uongozi wa kibabe na wenye kuwatendea kila maovu raia wake pasipo kujali dini yetu na utamaduni wetu wa asilia .
Leo Viongozi wa CCM wametokwa na imani hata ya Uislamu,utu ,ubinadamu na huruma imekua dini yao na utu wao ni ilani ya chama chao almuradi tonge yende kinywani,kujijenge majumba kwa majumba mazuri,magari kidekede kujinunulia na starehe na wake za watu n.k.
Huu unaingia Mwaka wa tatu kama sikosei Ndugu zetu Waislamu wenzetu Masheikh wetu wanateseka magerezani bila hata huruma au kuwa na hisia Viongozi wetu watawala kua wale ni binadamu kama wao na wana majukumu yakusimamia familia zao na jamaa zao, si tu wanao teseka niwao tu gerezani laa, wanafamilia zao waloziwacha nyuma mke/wake na watoto waliotegemea baba mwenye nyumba kuwatunza.
Viongozi wetu habari hawana wamelewa na madaraka na starehe za dunia hawajali wala hawashuhuliki almuradi wao maisha yanawaendea basi wamesahau yote hayo huku Masheikh wetu wakidhalilika magerezani na wananchi wakawaida wakishinda majaani kuokota makopo , Inna Lillah Wainna Illah Rajuun, Viongozi wamelewa ,wamejisahau kabisa kua maisha yao yako rahani tu Mbele ya Allah.HaMimi nasema katika Wazanzibar watakapo kuja kufeli Mbele ya Allah na kupoteza dera kabisa ni kuipigia kura CCM ili endelee na mangamizi yake kwa Waislamu na vile vile itakua nikuwasaliti Masheikh wetu ndugu zetu ambao hivi sasa wanateseka wao na familia zao kiakili, kimawazo na hata kiwiliwili wanateseka vibaya sana chini ya utawala wa MACCM Madhalim wakubwa walio jivika vilemba vya uso ila ionekane kama hawaoni wanavyo watesa rai wema imaa kwa kuwatia jela au kwa umasikini wa kutafuta mlo moja usio patikana MACCM ndio ilowaweka Masheikh ndani jela huko nchini Tanganyika ambako hivi sasa wanateseka na kuadhirika kiakili na kuendelea kudhalilishwa.
Muislamu atakaye kuja kufanya hivyo basi hatokua na tafauti na hao watawala wa CCM ambao ndio chanzo chakuwaweka Masheikh ndani ,itakua na yeye kachangia kwa njia hii au nyingine kuendelezwa kwa ukandamizaji .
Yarrabbi jalia kwa rehma zako na nguvu zako tupitishie wepesi katika uchaguzi huu na uwaangamize wale wote wenye niambaya kwenye nafsi zao ambao wamekusudia mabaya yakuweza kuwadhuru wananchi na kutumia vyeo vyao na nguvu zao za madaraka ili kuwadhuru wananchi wa nchi hii ya Zanzibar.
Yarrabbi wadhuuru wao mwanzo kabla hata hayo walio yapanga katika nafsi zao ambayo wewe ni mjuzi wakuyajua yalomo ndani ya nafsi zao na nyoyo zao. Yarrabi walinde Masheikh wetu na uwafanyie uwepesi huko ndani waliko na uwanusuru na shari zote walizo kusudiwa na hao walio wakusudia.Ameen Ameen Ameen.
KILA MZANZIBARI ATAKAE IPIGIA KURA CCM ILI IBAKI MADARAKANI AJUWE NA YEYE ANACHANGIA KUFUNGWA KWA MASHEIKH NA KUTHALILISHWA KWAO NA KUENDELEZA DHULMA KATIKA NCHI YA ZANZIBAR UKAE UKIJUWA UTAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA,KUDHULUMIWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

No comments:

Post a Comment