Wednesday, October 7, 2015

NCHINI ZANZIBAR MGOMBEA URAIS KWA TIKETI YA CHAMA CHA CCM SHEIN AKIENDELEA NA KAMPENI NA KUHUTUBIA WANANCHI WA BUMBWINI MAKOBA WILAYA YA KASKAZINI B


Mama Fatma Karume akishuka jukwaani baada ya kuwahutubia Wananchi na Wana CCM katika viwanja vya mpira bumbwini makoba wakati wa mkutano wa Mgombea Urais wa nchi ya Zanzibar Shein, mkutano uliofanyika katika Jimbo la Bumbwini Unguja.


Mgombea wa Urais wa nchi ya Zanzibar Shein, akimpongeza Mama Fatma Karume baada ya kuwahutubia Wananchi na kumuombea Kura kwa Wananchi wakati wa Mkutano huo wa Kampeni katika Wilaya ya Kaskazini B uliofanyika viwanja vya mpira bumbwini makoba.


Mbunge wa Jimbo la Mpendae Mhe Salim Turky (Mr White) akiwa katika mkutano wa mgombea Urais wa nchi ya Zanzibar Shein, uliofanyika katika viwanja vya bumbwini makoba wakimsikiliza Mgombea.


Mwakilishi wa Jimbo la Tumbatu kwa kulazimisha kwa kutumia vikosi vya smz Mhe Haji Omar Kheri akiwahutubia Wananchi katika mkutano wa kampeni ya Mgombea wa CCM Shein, katika viwanja vya bumbwini makomba na kumuombea Kura Shein, ili kuendeleza atii amani na utilivu na Maendeleo ya Wazanzibar miaka 50 na ushaiya maendeleo yako wapi labda ya mdomo.



Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Balozi mdogo wa nchi ya Tanganyika kwa Masultani Weusi Tanganyika aliepo hapa nchini Zanzibar Balozi Iddi akiwahutubia Wananchi wa Mkoa wa Kaskazini na kueleza mafanikio yaliotekelezwa na Shein, katika kipindi chake cha miaka mitano inayomalizika na kuelezea Ilani ya CCM kwa miaka mitano ijayo.hahahahahahahaha bora nicheke.


Viongozi wa CCM na Mgombea Urais wa nchi ya Zanzibar Shein, wakiitikia dua iliokuwa ikisomwa na Mzee wa Kijiji cha Bumbwini Makoba baada ya kumalizika kwa mkutano wa Kampeni ya Urais wa nchi ya Zanzibar katika viwanja vya Mpira Bumbwini Makoba Wilaya ya Kaskazini B Unguja.
KILA MZANZIBARI ATAKAE IPIGIA KURA CCM ILI IBAKI MADARAKANI AJUWE NA YEYE ANACHANGIA KUFUNGWA KWA MASHEIKH NA KUTHALILISHWA KWAO NA KUENDELEZA DHULMA KATIKA NCHI YA ZANZIBAR UKAE UKIJUWA UTAULIZWA SIKU YA KIYAMA NA MWENYEZI MUNGU ULIPOSIKIA WAZANZIBARI WENZIO WANADHALILISHWA,KUDHULUMIWA NA KULAWITIWA NA HAWA JE ULIFANYA NINI TAFUTA JIBU LAKO MAPEMA KWA SIKU HIYO YA KIYAMA SIKU AMBAYO MALI NA WATOTO WAKO WALA CHEO CHAKO HAVITAKUFAA SIKU HIYO.

No comments:

Post a Comment