Thursday, June 30, 2011

ZIARA ZA MAALIM SEIF ZIMELETA TIJA

                                  WAZIRI FATMA ABDUL-HABIB FEREJ

WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi wameipitisha bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais ambayo iliwasilishwa juzi Barazani hapo na waziri wa Wizara hiyo Fatma Abdul-habib Ferej huku akitetea ziara ya Makamu wa Kwanza wa Rais nje ya nchi kwamba zilikuwa na maslahi na faida kubwa kwa maendeleo ya nchi.
Bajeti hiyo ilipitishwa baada ya wajumbe wote wa baraza hilo kuridhishwa na ufafanuzi wa hoja na masuali yao waliyouliza wakati wakijadili ambapo alitaja ziara za Makamu wa Kwanza faida zake ni nyingi ikiwemo ile ziara ya nchi za Mashariki ya Kati alipokutana na wafanyabishara na wawekezaji ambao baadhi yao wameonyesha nia ya kushirikiana na Zanzibar katika uwekezaji kufungua mahusiano kati ya Zanzibar na nchi hizo.
Katika ziara ya nchi za kiarabu ikiwemo Oman Waziri huyo alisema Makamu wa kwanza katika ziara yake hiyo imefungua milango kwa kurejesha mahusiano mema kwa kuwa Zanzibar na Oman ni marafiki na ndugu wa muda mrefu ambapo katika mazungumzo hayo yameweza kurejesha upya safari zake kati ya Oman na Zanzibar, mazungumzo ya kuanzisha shirika jipya la ndege la Zanzibar na msaada wa uchimbaji mafuta.
Wakati wakichangia hutuba ya bajeti ya ofisi ya makamu wa kwanza wa rais baadhi ya wawakilishi walitaka kujua mafanikio yaliopatikana katika ziara za makamu wa kwanza wa rais kwa kuwa kitabu cha hutuba hakijaeleza mafanikio yoyote yaliopatikana katika ziara hizo.
Aidha waziri huyo alisema mbali ya faida hizo, pia yalifanyika mazungumzo ya kuomba msaada wa ujenzi wa Bandari mpya na kudumisha uhusiano mwema baina ya Zanzibar na nchi za eneo hilo.
Akizungumzia suala la madawa ya kulevya ambalo limechukua muda mrefu kujadiliwa na wajumbe na kuitaka serikali kujikita katika suala hilo kwa kuweka mkazo mahsusi kwa lengo la kuwanusuru vijana Waziri huyo alisema anakubaliana na maoni ya wajumbe na kuahidi kwmaba serikali itaendelea na juhudi zake na kupambana na tatizo hilo kwa kushirikiana na vyombo husika na wananchi.
Kuhusu maambukizi ya vizuri ya ukimwi Ferej alisema Zanzibar kwa akiasi fulani imefanikiwa kudhibiti maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi na kueleza huku akijibu hoja za wajumbe ambao wamehji mfuko huo kutengewa fedha nyingi alisema ni kutokana na umuhimu wa kazi hiyo kubwa na kupambana na ukimwi.
Alisema Ofisi ya makamu wa kwanza wa rais ipo kwenye mikakati ya kuangalia mapungufu ya sheria ili kuweza kuzuia uingiaji wa dawa hizo nchini ambazo zimekuwa zikiathiri vijana wengi na hatimae kupata maambukizi ya vizuri vya ukimwi.
Kuhusu uharibifu wa maliasili zisizorekebishwa alilifahamisha baraza hilo kuwa Ofisi yake ipo hatua za mwisho kuweka kanunui ambazo zitasaidia kuzilinda na kuzififadhi kwa manufaa ya vizazi vilivypo na vijavyo.
Alisema Zanzibar inakabiliwa na changamoto ya tabia nchi, ikiwemo mashamba kuingia maji ya bahari, maji kuingia chumvi na hata baadhi ya maeneo kumengwa na bahari na kubainisha kuwa ofisi inaandaa mikakati ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Wakichangia bajeti ya Ofisi hiyo wajumbe hao wajumbe wa Baraza hilo waliomba nyumba za Sober House ambazo zimekuwa zikiwahifadhi vijana walioacha matumizi ya dawa za kulevya kujengwa mbali ya nyuma za makaazi ya watu.
Aidha alizungumzia suala zima la sekta ya utalii ambapo alisema zinapaswa kuwa na mikakati ya madhubuyi ya kupunguza kasi ya maambukizi ya ukimwi, pamoja na kuongeza kasi ya mapambano hasa ikizingatiwa kuwa Zanzibar imekuwa na uingiaji na utokaji mkubwa wa watu kutoka sehemu mbali mbali

No comments:

Post a Comment