Thursday, July 7, 2011

MAONI YA WATANGANYIKA THAIDI YA MUUNGANO-TANG-Z;BAR


Hizi kelele za Wazanzibari juu ya muungano zinaanza kututia kichefuchefu. Hivi wanadhani wao ni wazuri sie watu wa bara tunawataka sana, au? Kwa lipi hasa walilo nalo? Hivi Mtazania bara anasaidiwa nini na Mzanzibari leo hii? Huu Muungano unatusaidia nini Watanzania bara ambacho Wazanzibar wanaona tunafaidika sana?

Tunajua tatizo la Zanzibar ni kudhani watajiuza urababuni huko na kupata misaada mingi sana kiasi kila Mzanzibari awe tajiri. Zanzibar wana historia ya kutaka visiwa viungane na nchi fulani za uarabuni, tunajua hilo. Na sijui kama ni Wazanzibari wote wanataka hivyo au wale wenye asili ya kirabu tu. Si ajabu hoja ya kuuza uhuru wa Zanzibar kwa nchi fulani ya uarabuni kukaja kuwa hoja ya mauaji na mapinduzi mengine Zanzibar. Typical tabia za kimwinyi; wako tayari kuuza uhuru kwa ajili kupata tende mbili toka uarabuni. Huo ni Uzinzibari na sio Uzanzibari, na So be it!

Hata hivyo, tuko tayari kuuvunja muungano ikiwa yafuatayo yatafuatwa;

1. Watanganyika wote walio Zanzibar na Pemba warudi bara, na Wazanzibari na Wapemba wote walio bara warudi Zanzibar na Pemba, isipokuwa wale waliooana wakachanganyika na wabara na wazanzibar/wapemba.

2. Zanzibar mtaanza kulipia umeme na huduma yeyote toka bara kwa fedha ya kigeni

3. Biashara yeyote kati ya bara na visiwani itafanyika kwa fedha za kigeni na kulipiwa ushuru kamili.

4. Tutaweka mipaka bayana ya nchi kati ya Zanzibar na Tanzania bara, kwa kufuata kanuni za "central devide line" katika maji yanayotutengani sha, na itakuwa ni marufuku kwa upande wowote kuingilia maji ya nchi nyingine kwa lengo la kuvuna rasilimali za bahari

5. Utenganishwaji wa balozi zetu nje ya Tanzania utafanyika mara moja

6. Safari kati ya Tanzania bara na Zanzibar itakuwa ni kwa kutumia passport

7. Tanzania bara, kwa kuwa ndiyo iliyopoteza jina lake la Tanganyika baada ya Muungano, itakuwa na haki ya uamuzi wa kuendelea kutumia jina Tanzania au kurudia jina Tanganyika, au jina jingine itakaloona linafaa kuitambulisha nchi yake

8. Tutafanya referandum ya kuvunja muungano, na muungano utavunjwa iwapo tu zaidi ya asilimia 50 ya walioko bara na asilimia 50 ya walioko visiwani watakubali muungano uvunjwe, bila kuchanganya matokeo ya bara na visiwani.

Ikiwa upande mmoja hautaafiki kwa asilimia zaidi ya 50 muungano hautavunjwa milele na kelele zozote dhidi ya muungano zitachukuliwa kuwa ni uhaini dhidi ya serikali.
wabubge hao wanaotoa kejeli wafukuzwe na hawafai kuitwa viongozi, wananshindwa kuuelezea matatizo ya wananchi kila siku Muungano tuuuuu.hawana jipya bali ni wananfiki na wasaliti.

13 Rich 2011-07-02 14:43
Jamani jamani, dawa ya migogoro ya muungano ni kuwa na kura ya maoni Zanzibar na Tanganyika. Ukusikiliza michango ya wabunge kutoka ZNZ, zaidi hawapendi muungano sababu kubwa ni kuwa katiba ya CUF mwanzoni ilikuwa haitambui mapinduzi matukufu ya 1964 kwani serikali iliyopinduliwa ilikuwepo kihalali na muungano walikuwa hawakubaliani nao. Ndiyo maana mpaka leo hii wabunge na wawakilishi hao wanalalamika na hawataki muungano. Sisi tunashindwa kuelewa kwa nini Watanganyika hawataki kuwaachia Wa Zenji.Na kwa sababu ya dhambi hii, baada ya miaka mitano patatokea Jamhuri ya Pemba(CUF) na Jamhuri ya Zanzibar(Unguja CCM). Tanganyika itabaki Tanganyika kwa sababu wote ni watani hata kabla ya wakoloni kufika huku wazenj hawana utani. Ratiba ya kuandika katiba mpya na referundum ya muungano iwekwe wazi kabla ya 2013.
 MTANGANYIKA 2011-06-30 14:25
Muungano ukifa wapemba wote waliojazana kariakoo tutawatoa nduki, tutakata umeme tunaopeleka Unguja kutokea Dar na unaokwenda Pemba kutokea Tanga.
Mutatina Rwihura 2011-06-30 10:28
Ukweli unabaki pale pale kwamba wakati umefika wa kunagalia tena muungano gani unatakiwa na pande zote mbili. Mambo ya viongozi wawili kukutana na kusema muunganno bila ridhaa ya wananchi umepitwa na wakati ni lazima watu wasilikishwe. Hata hivyo muungano ulikuwa kati ya Tanganyika na Zanzibar kwanini Tanganyika ipotee na halafu kuzaa Tanzania ya muungano ambayo inakuwa kama kaka mkubwa na Zanzibar ambayo inakuwa kaka mdogo. Katika vipengele vya muungano kimoja kilisema "mojawapo ya nchi hizi ikijitoa basi muungano umekwisha" kwa sasa hiki kipengele hakina maana kwa sababu ni Zanzibar peke yake inayoweza kujitoa. Siyo ajabu muungano kufa angalia USSR muungano wa Russia umekwisha na nchi zimejitawala bila taabu hivyo hivyo Yugoslavia. Lazima tuwe tayari kuwa na mabadiliko.
Rwihura
Gabriel 2011-06-30 10:34
Tanzania haina demokrasia ya kweli. kwa nini viongozi wetu wanatetemeka kila wakati wananchi wanapopaliza sauti zao wakitaka kuhusishwa kwenye maamuzi ya mambo mazito yanayowahusu? Kura ya maoni ni kama maandamano. Nchi yenye katiba ya kidemokrasia inatakiwa kuwaruhusu wananchi watoe maoni yao kuhusu wanavyotaka kutawaliwa. Sasa ugumu uko wapi? Serikali ya muungano iandae kura za maoni bara na visiwani itakayosimamiwa na tume huru-siyo akina NEC wachakachuaji na matokeo yake yatumiwe kutangaza kwenye katiba mpya kama muungano ni hai au marehemu.
JI NCHI LOTE HILI HALIWATOSHI MPAKA VIJISIWA HIVI.....?

1 comment: