Maalim Seif Sharif Hamad akipokea zawadi kutoka kwamsaidizi wa Mfalme wa Ashanti, Otumfuo Osei Tutu, baada ya kumaliza mazungumzo yao,ofisini kwake Migombani.
Vile vile Maalim Seif alitumia fursa hiyo kumuomba Mfalme Tutu kuangalia uwezekano wa kuisaidia Zanzibar katika dhamira zake za kuimarisha huduma bora za afya, akielezea changamoto kadhaa zinazoikabili sekta hiyo, ikiwemo upungufu wa madaktari, vifaa na wataalamu mbali mbali.Maeneo mengine ambayo Maalim Seif aliomba kuendelezwa ushirikiano kati ya nchi mbili hizo ni pamoja na uimarishaji wa kilimo,hususan cha matunda na mbogamboga, akieleza azma ya wakulima wa Zanzibar kupata fursa ya kujifunza kutoka kwa ndugu zao wa Ghana.Pia Maalim Seif alimweleza Mfalme huyo dhamira ya Serikali ya Zanzibar katika kuimarisha zao la Karafuu ili kuleta ushindani na nchi kadhaa Duniani zinazozalisha zao hilo.
Alisema mbali na kuwepo uzalishaji mkubwa wa zao hilo kutoka nchi za Brazil, Indonesia,Syrilanka na Madagascar, Serikali imejipanga vyema kuirejeshea hadhi yake Zanzibar kama nchi inayoongoza kwa uzalishaji wa karafuu yenye ‘kiwango bora’ Duniani.Alisema ili kufikia azma hiyo kuna umuhimu kwa Ghana kusaidia katika utafiti.Katika hatua nyingine Maalim Seif ameiomba Ghana kusaidia utatuzi wa changamoto ya ugonjwa wa Ukimwi ili kupunguza/kuzuia maambukizo mapya sambamba na kukabiliana na uingiaji na matumizi ya madawa ya kulevya, ikizingatiwa mazingira ya Zanzibar kuwa ni ya kisiwa.Mapema Mfalme Tutu alisema Ghana na hususan Jimbo la Ashanti litaendeleza mashirikiano yake na Zanzibar kwa faida ya wananchi wake, na kuainisha kuwa taratibu za kubadilishana uzoefu zinasaidia katika kukuza maendeleo.
Aliipongeza mageuzi ya kisiasa yaliofanyika Zanzibar na kupelekea kuundwa kwa Serikali yenye mfumo wa umoja wa Kitaifa, na kusema hatua hiyo ni upanuzi wa Demokrasia.Aidha alitoa wito kwa Mataifa ya Afrika kukaa na kumaliza matataizo yao wenyewe bila ya ‘kuwaita watu weupe’ kuja kuwatatulia.
No comments:
Post a Comment