Friday, July 1, 2011

Z;BAR ID HAWAPEWI WANANYIMWA NA KUPEWA WATANGANYIKA ILIWAONEKANE NI WAZAWA WA Z;BAR


VITABULISHO NI VYA WAZENJI LAKINI HAWAPEWI WANAPEWA WATANGANYIKA ANASUBIRI FORM TU YA KUOMBA KITAMBULISHO NI ADHABU KUBWA NA NI HAKI YETU WAZENJI KUWA NA HIVYO VITAMBULISHO
WAJUMBE Baraza la Wawakilishi Zanzibar wamehoji fungu kubwa lililotengwa kwa ajili ya Idara ya Vitambulisho vya Mzanzibari Makaazi (Zan-ID) na utumiaji mbaya wa fedha za walipa kodi na urasimu unaofanywa na idara hiyo.
Wakichangia hutuba ya bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara ya nchi ofisi ya rais na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi ya mwaka wa fedha wa 2011-2012 wawakilishi hao wamesema utumiaji wa fedha katika idara hiyo umekuwa mkubwa mno.
Aidha wawakilishi hao walihoji fungu lililotengwa na serikali kwa ajili ya idara hiyo ambayo tokea kuanzishwa kwake imekuwa ikilalamikiwa na kushutumiwa kwa UBAGUZI MKUBW wa kutoa vitambulisho hivyo kwa misingi ya kichama ambapo Chama Cha Wananchi (CUF) kimesema idara hiyo Haijaweza kutenda haki katika baadhi ya wananchi wenye kutaka vitambulisho mbali ya UHASIMU MKUBWA uliopo katika upatikanaji wa vitambulisho hivyo.
Akichangia hotuba ya bajeti Mwakilishi wa Mji Mkongwe (CUF) Ismail Jussa Ladhu alisema anashangazwa kwamba fungu lililotengwa kwa ajili ya ofisi hiyo mwaka jana lilikuwa shilingi 910 millioni lakin mwaka huu limezidi na kufikia shilingi 1248 milioni.
Alisema kipindi cha mwaka jana kulikuwa na harakati nyingi zikiwemo zile za uchaguzi na utayarishaji wa ofisi hiyo lakini jambo la kushangaza wakati ofisi tayari imeshajipanga kuongezeka idadi hiyo ya fedha wakati sasa ni maendelezo ya shughuli zake.
“Inakuwaje fedha zilizotengwa zizidi kiasi hiki wakati mwaka jana tulikua na uchaguzi na mazonge mengi tu ya utoaji wa vitambulisho ambavyo ni vingi lakini kwa nini mwaka huu bajeti hiyo iongezeke kiasi hicho wakati haikupaswa kuzidi kiasi kama hicho” alihoji Jussa.
Jussa alisema katika ununuzi wa vifaa na matengenezo pia kuna fedha nyingi zimetengwa ambazo hazilingani na hali halisi ambapo katika bajeti iliyopita kulitengwa shilingi 15 millioni lakini katika bajeti ya mwaka huu imezidi na kufikia shilingi 50 millioni.
Aidha katika fungu la ushauri nasaha kwa maambukizi ya virusi vya ukimwi idara hiyo imetengewa shilingi 2 millioni katika bajeti iliyopita na bajeti ya mwaka huu zimeongezeka na kufikia shilingi 12 millioni kwa Unguja wakati upande wa Pemba bajeti yao ni hiyo hiyo kama ya mwaka jana 2 millioni.
“Kwa nini kwa upande wa Pemba ziwe shilingi 2 millioni kama mwaka jana lakini kwa upande wa Unguja ziwe zimezidi na kufikia shilingi 12 milioni ina maana maambukizi ya ukimwi yamezidi kiasi hicho kwa upande wa Unguja??? Alihoji Jussa ambaye tokea kuanza kwa bajeti amekuwa akihoji namna ya fedha zinavyotumika kwa kila kifungu.
Akichangia suala la urasimu Mwakilishi wa Jimbo la Mtambwe (CUF) Salim Abdalla Hamad alisema bado wananchi wananyimwa vitambulisho ambavyo ni haki yao ya kikatiba licha ya kelele nyingi zilizopigwa juu ya idara hiyo ambayo inayotowa vitambulisho kwa UBAGUZI.
Hamad ameitaka idara hiyo kuondosha urasimu na msururu wa vikwazo visivyo na msingi kwa ajili ya wananchi kupata vitambulisho vya mzanzibari mkaazi kwani hiyo ni haki yao kikatiba
“Mheshimiwa naibu spika vitambulisho vya ukaazi ndiyo utambulisho wa mzanzibari katika nchi yake ambavyo hivi ni muhimu sana lakini leo wananchi wananyimwa kwa makusudi tunaomba suala hili lishughulikiwe ili kila mwananchi apate haki yake…na urasimu uondolewe” alisisitiza Mwakilishi huyo.
Alisema licha ya katiba kutamka bayana kwamba kila mwananchi anayefikisha umri wa miaka 18 anastahiki kupatiwa kitambulisho hicho lakini idara inayohusika imekuwa kikwazo katika kuwapatia wananchi vitambulisho hivyo imekuwa ni shida kubwa kwa idara hiyo.
Salim alisema matokeo yake wananchi wengi walishindwa kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana kwa sababu hawana vitambulisho hivyo na kwa mujibu wa sheria kama huna kitambulisho huwezi kupiga kura katika uchaguzi mkuu.
“Kitendo cha kuwanyima wananchi vitambulisho vya ukaazi wa mzanzibari ni ukiukwaji wa katiba na haki za binaadamu kwa sababu wananchi wanashindwa kupiga kura katika nchi yao wakati kisheria wana haki ya kufanyaa hivyo …serikali tunaiomba ilishughulikie suala hili” alisema.
Hamad aliitaka serikali kuhakikisha kwamba wananchi wanapata vitambulisho hivyo na kuwawezesha kutumia haki yao ya kidemokrasia kupiga kura katika uchaguzi mkuu.
Mwakilishi huyo amesema Zanzibar imetoka mbali katika migogoro ambayo imesababishwa na matatizo kama hao ya kisiasa jambo ambalo serikali inatakiwa kujifunza ili kutorejea walipotoka kwani hali ilivyo sasa ni ya amani zaidi na inahitaji kuendelezwa.
Mwakilishi wa Jimbo la Micheweni (CUF) Subeit Khamis Faki alisema haoni sababu ya wananchi wa Zanzibar kukoseshwa vitambulisho vya ukaazi kwa kukosa cheti cha kuzaliwa kwa kuwa wazanzibari wengi hawakuwa na vyeti vya kuzaliwa kutokana na kuokuona umuhimu wa kuwa na vyeti na elimu juu ya suala hilo haikuwepo huko nyuma.
Alisema katika uchaguzi mkuu uliopita wapo wananchi wengi wakiwemo watu wazima walikosa kupiga kura kwa sababu hawana vyeti vya kuzaliwa jambo ambalo wamenyimwa haki yao ya msingi ya kuchagua kiongozi wanayemtaka.
“Mheshimiwa Spika kasoro hii tunatakiwa kuirekebisha mara moja…haiwezekani mtu kukosa cheti tu cha kuzaliwa na hivyo kumkosesha kupata kitambulisho cha mzanzibari mkaazi hali ambayo inamfanya kushindwa kupiga kura katika uchaguzi mkuu tunaomba sana hili litizamwe kwa umakini” alisema Faki.
Mwakilishi huyo alisema Serikali irekebishe kasoro hizo ambazo aliziita ni kubwa sana zinazotishia uhuru wa demokrasia katika mfumo wa vyama vingi ikiwemo wananchi kukosa haki zao za msingi ikiwemo kupiga kura na kupata haki nyengine kama pasi za kusafiria kwa kuwa usipokuwa na kitambulisho huwezi kupata pasi ya kusafiria na baadhi ya mambo mengine.
Katika hatua nyengine Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imewataka wananchi ambao hadi sasa hawana vitambulisho vya mzanzibari mkaazi na ambao hawajavichukuwa vitambulisho hivyo kwenda katika ofisi za idara hiyo na kuchukuwa.
Waziri wa nchi ofisi ya makamo wa pili wa rais Mohammed Aboud Mohammed aliwaambiya wajumbe wa baraza la wawakilishi wakati akijibu swali lililoulizwa na Mwakilishi wa viti maalumu, Kazija Khamis Kona wa (CUF) aliyetaka kujuwa suala la vitambulisho na Serikali imejipanga vipi katika uchaguzi mkuu ujao.
Aboud alisema yamekuwepo malalamiko ya wananchi kuhusu vitambulisho vya ukaazi wa mzanzibari mkaazi ambapo wananchi wengi wadai kwamba hawajapata vitambulisho hivyo lakini vitambulisho vipo vinasubiri wenyewe.
Alisema nia ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni kuona wananchi wote wanapata vitambulisho hivyo kwa mujibu wa sheria kwani hiyo ni haki yao ya kikatiba.
Alisema zipo jumla ya kadi za vitambulisho vya mzanzibari mkaazi vipatavyo 42,000 katika ofisi za idara hiyo ambavyo wananchi wameshindwa kwenda kuzichukuwa.
Aboud alisema wakati wananchi wanalalamika kukosa kadi za vitambulisho vya ukaazi wa mzanzibari lakini kumbe kadi hizo zipo katika ofisi za idara ya vitambulisho katika maeneo mbali mbali Unguja na Pemba.
Kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi,huwezi kupiga kura katika uchaguzi mkuu kama utakosa kadi ya usajili wa mzanzibari ambapo pia ni kosa kwa mujibu wa sheria mtu atakayefikisha umri wa miaka 18 kukosa kitambulisho hicho.

wanavibana kwa makusundi ili uchanguzi ujao watakuwa washawapa watanganyika ili wawapingiye kura watawambiya unataka kuwa mjanjibaliiiiiiii chukuwa kitambulisho ila utupigiye kura sasa jama katoka mkoani hata kitambulisho hajuwi ni nini leo kapewa bure unafikiri atafanya nini na wazanzibar halisi hawapewi na mimi ni moja wao hawataki kunipa na paspoti pia wameninyima na ndio usiseme utafikiri unachimba thahabu na nihaki yetu lakini hatupewi labda uwe na kibunda cha pesa hapo watakwenda mbio kusaini makaratasi haya na yale si mbio hizo utawaona jasho linawatoka kama majibwa ya usasini maana washaziona pesa haya ndio mambo ya ya serekali yetu ya ZANZIBAR RUSHWWWWWWWWWWWWWWAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA.

No comments:

Post a Comment